Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA


SIMU; 0758573660


SEHEMU YA KUMI NA MOJA



Akiwa anajiuliza hayo akapigiwa honi na gari lililokuwa nyuma yake kuashiria atembeze gari foleni inasogea!!

Kichwani mwake maswali yalikuwa ni mengi kuliko majibu.

Ahsubuhi ile radio mbali mbali zilikuwa zinatangaza vichwa vya habari vya magazeti mbali mbali huku ikionekana habari kubwa ni ya mauaji ya ofisa wa jeshi la polisi.

Remi pia ambae hakuwa na usiku mzuri pia alikuwa ameamka na habari zake zilizoonekana kutikisa ahsubuhi ile.

Remi aliishiwa nguvu na kubaki akiwa anachuruzikwa na machozi sambamba na kamasi.

Remi alijuta kuijua Tanzania; na bado hakujua kiini cha yale yote na nini hatima ya mchezo ule na kwanini alilengwa yeye.

Hakika alitatizika!.

***

MOGADISHU

“Sijasikia ukifanya lolote Komredi” Aliuliza Sozi ambae alikuwa ameshikilia kisu kilichokuwa kimetapakaa damu.

Honda alibaki akimtizama bila kusema neno, kisha akaendelea na safari yake na Sozi akaingia ndani ya bafu alilokuwako Honda.

Alipiga mluzi mkubwa baada ya kuona binti yupo chini na nguo zake zimeraruliwa hivyo.

Alijua Honda p.a.k Ahmed atakuwa amemaliza kazi.

Sozi akatoka nje haraka na kukuta Honda amerejea kwenye gari akiwatizama wengine walichokuwa wanakifanya kwa raia wasiokuwa na hatia.

Sehemu nyingine ndani ya mji wa Mogadishu kulisikika mlio wa bip mara tatu mfululizo na hapo Haji aliekuwa anavaa suruali akaruka na kuiendea rununu iliotoa mlio ule na pia Zedi aliekuwa amejilaza kitandani nae akakurupuka na kumfuata Haji ambae wakati huo alikuwa ameshika rununu maalumu kwa ajili ya kuwasiliana na Honda ambae alikuwa kwenye kikundi cha Al-Islamiya kama double Agent.

“Hawa jamaa hawana muda wa kumpuzika aisee” Alisema Haji huku akibonyeza hapa na pale juu ya rununu ile ya kijanja.

“Inamaana wamempa kazi sio!” Alihoji Zedi.

“Bila shaka” Alijibu Haji.

Mlio ule ulikuwa ni taarifa maalumu kwao ya kuwa Honda atakuwa na ujumbe kwao mahali fulani hivyo ilibidi kwa kutumia kifaa maalumu wamfuatilie kujua ni wapi watakutana nae.

Haji ambae alikuwa ni mtaalamu wa tehama aliweka mambo sawa na kisha walianza kujiandaa kwa ajili ya kutoka na kufuatilia mienendo yake.

Wakati walipomaliza kujiandaa ni wakati huo ambao waliona kifaa kile kikitoka kijiji cha Saadan na kuelekea kusini mwa Mogadishu kwenye pwani ya bahari ya Hindi ambako kulitumika kushusha mizigo mbalimbali na meli kubwa zilikuwa zinatia nanga huko.

Honda alikuwa mtulivu ndani ya gari huku akiwa amepewa smg iliokuwa imejaa risasi.
Kamongo nae alikuwa amekaa pembeni yake huku akitupia macho huku na huko kuhakikisha safari yao inakuwa salama kabisa.

Nyuma ya magari yote kulikuwa kuna magari zaidi ya sita na yote yalikuwa yamejaa wapiganaji wa Al-Islamiya.

Njia nzima ilitawaliwa na ukimya huku kila mara Honda akiona watu wanakimbia kila walipoona msafara ule.

Hatimae magari yalisimama pembezoni kabisa mwa bandari kisha wapiganaji wote wakasambaratika kila mmoja kuchukua usawa wake na ndani ya gari alibaki Honda na Kamongo.

“Wewe teremka na utakaa pale kwenye kontena na ukiona msafara wa magari mawili unaelekea ndani ya lango la bandari piga mluzi mrefu mara moja kisha shuka na unisubiri” Kamongo alimwambia Honda huku akimpiga juu ya bega na Honda akashuka bila kuuliza zaidi.

Honda alitizama eneo lile jinsi lililovyokaa na upande wa mbele yake aliona jumba kubwa lenye muonekano wa majumba ya kale.

Alitamani kufanya kitu ndani ya jumba lile ila hakuona upenyo wa kufanya hivyo.

Akajipa muda!!

Alienda kukaa juu kabisa ya kontena moja lililoonekana kutotumika muda mrefu kidogo na ni kama lilisahaulika na mamlaka za bandari.

Akatulia tuli na mtutu wake.

Haikuwa hadi nusu saa alipona gari mbili zenye nembo na bendera ya Somalia zikiwa zimeongozana zikiingia upande wa mashariki mwa bandari ambako kulitumika kupakua mizigo iliokuwa inaletwa na meli kubwa.

Honda alipiga mluzi kama alivyoelekezwa na Kamongo kisha akashuka na kumsubiri.

Punde kamongo akatokea akiwa na kisu pekee huku mtutu wake akiwa ameuacha ndani ya gari, akaongoza kuelekea kwenye usawa wa lango linalotumiwa na makuli kuingia na kutoka katika bandari ile.

Honda nae akafuata!!

Safari yao ilikuwa ni kuelekea kwenye meli moja iliokuwa imetia nanga pembezoni kidogo mwa bandari na ilikuwa ipo tayari kwa kupakuliwa mzigo.

Waliingia hadi ndani ya meli ile na kushuka chini kisha wakapita korido mbili na kushuka tena na hatimae walijikuta wakiwa wametokea kwenye ukumbi mkubwa tu na ndani yake kulikuwa kuna watu watatu.

Wawili kati yao walikuwa ni wenye asili ya ufaransa yani wazungu na mmoja alikuwa ni mwenye asili ya kisomali na umri ulianza kumtupa mkono.

Honda alimtambua mtu yule na hapo akaguna kimoyomoyo!!

Mtu yule alikuwa na wadhifa mkubwa serikalini.

Isa; huyu ni nani?” Aliuliza mzee yule huku akiwa ametupa macho kwa Honda.

Honda nae akajua jina la kamongo ni Isa.

“Anaitwa Ahmed; tumemkomboa kwa wa Marekani.” Alijibu Isa.

Yule mzee alibaki akiwa anamkodolea macho Honda; p.a.k Ahmed.

“Back to bussnes” Alisema yule mzee na kumgeukia mzungu mmoja na kumpa ishara ya kugonganisha vidole kwa pamoja.

Mzungu mmoja aliondoka pale ndani na kuelekea kwenye vyumba vingine vilivyokuwa kushoto mwa ukumbi ule.

Hakukaa sana akarejea akiwa na begi kubwa akiburuta chini.
Alipofika akaliweka juu ya meza na kufungua!

Ilikuwa ni shehena kubwa ya risasi na silaha tatu kubwa za kivita na bastola mbili za kisasa.

“Hawa watu ni hatari sana” alijisemea Honda.

“Mzigo upo ndani hii ni sampo” Alisema yule mzee.

Kamongo alizishika zile risasi na kuzitekenyetekenya, kisha akachukua bunduki moja na kuikoki mara kadhaa na aliporidhika akachukua kiwambo cha kuzuia sauti na kuweka risasi kisha akalenga na kupiga chini risasi zote alizoweka.

Akachelelea Kamongo au Isa kwa jina lake kamili.

Alipenda nguvu ya silaha ile.

Alimgeukia Honda na kumpa ishara na Honda akachukua bastola moja na kuitia risasi saba kisha akaivesha kiwambo cha kuzuia sauti na kupiga chini pia.

Zilitoka risasi sita na ile ya saba haikutoka na ndio risasi aliyotarajia hasa baada ya kuiona ikiwa na kimo na kipenyo tofauti na risasi zingine.
Alijua ni ujumbe kutoka CIA kama walivyokuwa wamemwambia ya kuwa atakutana na ujumbe siku kukiwa na ununuzi wa silaha.

Kila mtu alimtizama Honda baada ya risasi ya saba kugoma kutoka.

Honda nae aliwatizama na hatimae macho yake yakagongana na ya mzungu mmoja.

Mzungu yule akapepesa macho kwa namna ya ajabu kabisa.

Honda alishindwa kuelewa ishara ile ilimaanisha nini japo alijua ina ujumbe fulani.

Honda akafungua kibeti cha risasi na kuichomoa risasi ile kisha akaitazama tena huku akijua macho yote yapo kwake!!

“Ipo vizuri ila imechanganywa humu kimakosa” Alisema Honda.

Wale wazungu walitabasamu na Honda akaichukua risasi ile na kuitupia kwenye mfuko wa shati lake.

“Tunamalizana vipi sasa!!” Aliuliza yule mzee.

“Msikiti wa Masjid nuur; Imamu Shafi’i” Alijibu Isa.

Yule mzee akampa karatasi Isa kisha akaongea kwa lugha ya kihabeshi ambayo bila shaka si Honda ama wale wazungu walielewa na hakuna aliejua ni kwanini aliamua kuongea kilugha sehemu kama ile.
Na laiti wangejua, hakika kila mtu angelitafuta jeneza lake!.


***


TUKUTANE JIONI
 
Shikamoo Honda,,, na wazungu ila naona hakuna Biashara hapo zaidi ya kutapeli watu na kuwauwa, ila Honda anaweza kuwa msaada mkubwa sana aisee shukrani sana mkuu,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA MBILI


Wale wazungu walitabasamu na Honda akaichukua risasi ile na kuitupia kwenye mfuko wa shati lake.

“Tunamalizana vipi sasa!!” Aliuliza yule mzee.

“Msikiti wa Masjid nuur; Imamu Shafi’i” Alijibu Isa.

Yule mzee akampa karatasi Isa kisha akaongea kwa lugha ya kihabeshi ambayo bila shaka si Honda ama wale wazungu walielewa na hakuna aliejua ni kwanini aliamua kuongea kilugha sehemu kama ile.
Na laiti wangejua, hakika kila mtu angelitafuta jeneza lake!.

***

Isa alimuita pembeni Honda baada ya kuwa amemsindikiza nje yule mzee.

Kulitokea mabishano kidogo kisha Honda akelekea kule ambako kulitolewa sihala za majaribio.

Huko alienda kukutana na shehena kubwa ya sihala nzuri na za kisasa huku kukiwa na mabomu ya kurusha kwa mkono na RPG za kutosha.

“Watu hawa wanajiandaa kufanya nini?” alijiuliza Honda huku mikono yake ikitalii kwenye vitako vya silaha zile.
Lakini tena alikumbuka mbinyo wa macho wa mzungu yule.

“Alitaka kunambia nini yule jamaa?” alijiuliza tena huku akitoka ndani ya chumba kile na kurejea ukumbini ambako bado wale wazungu wawili na Isa ama Kamongo kama ambvyo Honda alipenda kumuita.

“Kila kitu naona kipo sawa,ita vijana!!” Alisema Honda.

Isa hakumjibu, akageuka na kuchukua bastola moja iliokuwa imewekwa risasi nyingi na hazikuwa zimetumika.

Mzungu mmoja akaingiwa na mashaka!

“Nadhani tunemaliza na tuondoke sasa” yule mzungu aliepepesa kope zake wakati Honda anakagua silaha alizungumza.

Isa alicheka kwa dharau.

“Nani alisema ukioniona unapaswa kuishi?” alisema Isa huku akivuta kilimi cha kuondoa usalama.

Mara mzungu mmoja ambae alijua ni nini kitafuatia aliruka juu na kutua juu ya meza kisha kwa wepesi wa hali ya juu akapiga teke bastola iliokuwa mkononi mwa Isa na kusambaratika chini.

Isa hakutegemea kile kitendo na alipotaka kurudi nyuma alijikuta amechelewa akajikuta akienda chini mzimamzima baada ya kupigwa teke la sukuma katikati ya kifua.
Isa akataka kunyanyuka akajikuta akijaa mikononi mwa mzungu yule ambae alikuwa amegeuka mbogo ndani ya ukumbi ule.

Honda alibaki akiwatizama na huku kwa makini akifuatilia nyendo za mzungu aliekuwa amesimama huku akipeleka mkono wake nyuma ya kiuno.

Isa alipigwa kichwa cha paji la uso na kubaki akiona nyota nyota.

Mzungu yule akataka kutoa kisu na kupoteza umakini kwa Isa.
Isa nae hakutaka kupoteza hiyo bahati, kwa wepesi wa hali ya juu akamsukuma kwa nguvu yule mzungu kisha akaruka juu na kuachia teke safi lililoenda kutua kichwani kwa mzungu na kabla hajatulia akarusha tena teke zito lilitua mbavuni mwa mzungu na kumsambaratisha chini mzungu yule na ni wakati huo ambapo yalifanyika matukio mawili kwa wakati mmoja.

Isa alimuona vyema mzungu ambae alikuwa anajaribu kucheka na hisia za Honda kwa kuvuta silaha yake nyuma ya kiuno, hivyo haraka akachomoa kisu mbavuni mwake na kukirusha kistadi hadi kilipoenda kutua shingoni mwa mtu yule na ni wakati huo ambao mwili wake uliagana na nyonga kisha kupaa juu na kushuka huku akiwa amekunja goti moja na alipotua; alitua kwenye shingo ya mzungu aliekuwa anapambana nae na kuvunja shingo yake.
Isa akaruka na kutua pembeni huku akigonganisha viganja vyake kuashiria kazi imeisha.

Wazungu wote walienda chini kama mizigo.

Kazi kwisha!!

“nguruwe anamsumbuaje bwana wake!!” Alijitapa Isa; mtu mwenye kichwa kidogo na uso mwembamba huku akiwa na midomo kama samaki,alionesha umaridadi wake katika sanaa ya mapigano.

“U mjuvi sana wa kazi hizi komredi” Alisifia Honda.

“Ndio mana nilipewa kitengo na mrithi wangu ni Sozi.” Alizidi kujitapa Isa huku akichomoa kisu chake shingoni kwa mzungu ambae alikuwa anapigania pumzi zake za mwisho.

Isa alitoa simu ya upepo na kuwasiliana na vijana walioko nje kisha akamgeukia Honda.
“Mzee yule aliagiza tuwauwe hawa wazungu walioleta hizi silaha mana alihisi si wauzaji wa kawaida” Alifafanua ni kwa sababu gani aliwaua.

“Inapendeza!!” alijibu kiufupi tu bwana Honda.

Dakika sita baadae tayari silaha zilianza kusombwa kutoka ndani ya meli kuelekea nje ambako kulikuwa kuna ulinzi wa kutosha kuhakikisha usalama upo wa kutosha.

Honda nae alitaka kutumia mwanya ule kuelekea kule kwenye lile gofu aliloliona.

Taratibu akatoka akiwa ameongozana na vijana waliokuwa wanasomba silaha.

Hakuna alimtilia shaka!

Akatoka nje ya meli na huko alikutana na Sozi ambae alikuwa bize kabisa kuhakikisha usalama unakuwa wa asilimia zote.

Akaambaa na giza kama anaeenda kujisaidia kisha akapotea na kuelekea liliko gofu alilioona.

Safari yake ilikuwa ya umakini wa hali ya juu huku akihakisha hakuna anaemfuatilia.

Alijua anafanya jambo la hatari lakini hakujali kitu mana aliamua kujitoa muhanga kufanya operesheni ya hatari na watu hatari.

Alizidi kutokomea na hatimae akaingia kwenye jumba lile lililokuwa lina upweke wa kutisha.

Nyasi zilianza kutengeneza makazi ndani yake.
Akatoa kalamu ndogo iliokuwa maalumu kwa kumulika nyakati za usiku na kuanza kumulika ukutani.
Ulionekana kuwa ni ukuta wa rangi ilioanza kuchakaa.

Alisakanyasakanya jiwe ama kijiti na hatimae alipata kijiti ambacho kilimfaa sana.

Akaandika kitu ukutani kisha akatoweka ndani ya gofu lile na kuanza safari ya kurudi kule alikotoka.

Lakini alihisi kitu nyuma yake na kwa uzoefu wake alijua kabisa nyuma yake kuna mtu na ndivyo ilivyokuwa nae ilibidi atumie mbinu za kimedani kumtambua mtu yule.

Mara nyingi walifundishwa mbinu za kujificha kwa adui (camouflage).

**
Sozi alimaliza zoezi la kusimamia usalama na akampa taarifa Isa ambae alitoka na wakapanda wote ndani ya magari, ila Honda hakuonekana.

Wakajipa muda kidogo.

Dakika sita zilikatika bila Honda kutokea.

Isa akatoa amri ya kuanza msako wa kumtafuta Honda.

Vijana walizunguka kwa dakika tatu tu kila eneo bila kumuona Honda.

Isa alichanganyikiwa na hesabu zake zilimwaminisha ya kuwa Ahmed atakuwa ameamua kuwatoroka na kuendelea na maisha yake!

Akajua adhabu ambayo angelikutana nayo ni kubwa na ni kifo kwa uzembe alioufanya.

Vijana wakajipanga kungojea amri kutoka kwa Isa na muda ulizidi kwenda na eneo lile walihitajika kutoka kwa kuwa vikosi vya serikali vingepita pale kuweka doria.

“Mnadhani nini sasa!!” Honda aliwastua wote bila kufafanua kauli yake.

Wakamgeukia kwa pamoja.

Honda hakuwa peke yake,alikuwa amebeba mtu kwenye bega la kushoto na mkono wa kulia alishika mtutu wa bunduki.

Akajongea taratibu na kupita kati yao kisha akambwaga chini yule mtu ambae alikuwa amevaa koti refu jeusi na alikuwa na bastola kiunoni mwake, lakini pia shingoni kulikuwa kuna mkanda wa kamera ndogo yenye uwezo mkubwa wa kuchukua picha gizani.

Sozi akaiwahi kamera ile na kuanza kupitia picha zile zilizokuwa mle.

“Huyu bwege alitupiga picha tangu tuko kule kijijini” Alisema Sozi huku akimkabidhi Isa ile kamera.

Wote walizika hisia mbaya walizoanza kujenga kwa Honda na sasa walianza kumuona ni mtu mwenye akili nyingi sana.

“Umefanya kazi kubwa sana kujua uwepo wa huyu nyoka” Alisema Isa huku akimwinamia yule mtu ambae alionekana kupitia dhoruba nyingi kutoka kwenye mkono wa komando na gaidi aliekubuhu Ahmed Gailan p.a.k Honda.

“Huyu ni kutoka AL shabaab; nadhani wanajua uwepo wetu sasa” Alisema Isa kisha akatoa ishara fulani na vijana waliuchukua ule mwili na kuanza kuucharanga mapanga kisha kuutenganisha kiungo kimoja baada ya kingine.

Zoezi lilipokamilika msafara ukaondoka.

*****

Zedi na Haji walikuwa makini kabisa kufuatilia mwenendo wa ile alama nyekundu iliokuwa kwenye kifaa chao.

Nao walikuwa mitaa ile ya bandari, hata wakati alama ile inaelekea upande wa lile gofu, wao hawakuwa mbali na gofu lile na baada ya kuhisi kuwa ujumbe umeachwa alama ile ilizima na ilimanisha kazi imeishia pale.

Wakabaki na kazi moja tu kuhakikisha wanajua ilipozimia.
Haikuwachukua muda mrefu walijua ilizimikia kwenye jengo la mambo ya kale liliteketea kwa moto miaka kadhaa nyuma.

Waliingia hadi kwenye hilo gofu na kuanza kuangaza huku na huko kwa kutumia kurunzi ndogo kwa sababu hawakutaka kuvuta hisia za mtu ambae angelikuwa anakatisha mitaa ile.

“Kaa nyuma yangu na unitazame” Zedi alimwambia Haji Makame.

Zedi aliendelea kupitia kila sehemu na hatimae akaona mkwaruzo wa soli ngumu chini.

Nae akaenda hadi pale na alipotizama chini aliona aina ya mkwaruzo ule ni kama ulikusudiwa.

Akasimama huku akipiga hesabu za namna alivyokuwa amesimama mkwaruzaji.

“Aliposimama hapa, alitizama huku” Alisema Zedi huku macho yake yakielekea kule alikohisi msimamaji alisimama na kutazama.

Aliona!!

Macho yake yaliona mikwaruzo hafifu ukutani, akasogea na kuimulika kwa karibu zaidi.

“KEKERA” aliyanakili maneno yale kisha akaendelea kuchunguza ukutani pale na hatimae aliona tena maandishi mengine.

“Nü..Mďjust..fĺshai>”
Akayanakili tena maneno yale kisha akamstua Haji na wakapotea kwenye eneo lile na kurudi kwenye makazi yao ambayo yalikuwa katikati ya mji wa Mogadishu.

Saa moja badae iliwakuta wakiwa wametulia kwenye nyumba za viongozi wa serikali wakiwa ni kama walinzi wa viongozi wa ngazi za juu walioishi eneo lile ni hii ni baada ya kuhama kwenye hotel waliokuwa wakiishi tangu wafike Mogadishu. Makazi yao yalikuwa karibu na ubalozi wa Uturuki na hawakuwa mbali na Lido beach.

Waliweka mezani maneno walioyakuta kule kwenye gofu na yaliandikwa kwa code za kificho ili ambae atakutana nao na hahusiki basi asiweze kutambua kinachondelea.
Walianza na neno KEKERA.

Ndio ni kekera ila ila alimaanisha nini katika ujumbe huu” Alisema Haji huku akili yake ikizunguka kuhakikisha wanavunja code ile na kujua maana halisi ya ujumbe uliokusudiwa.

Zedi alikuna kichwa,hakujua ni nini sababu ila alijisikia tu kukuna kichwa.

Na kilichowachanganya ni kuwa ujumbe ulikuja kwa haraka sana tofauti na matarajio yao na hivyo kufanya kujua ya kuwa ujumbe ule ni wa muhimu sana.

Tatizo ni wa kuvunja fumbo.

Nywele ziliwasimama na ni lazima wafumbue ili wajue yaliomo.

Kazi ilikuwa ngumu hakika na muda ulizidi kusonga.

****

TUKUTANE KESHO JIONI
 
Akhsante kudo, hapa ntakuwa napita kuisoma mpaka nione imefika kama nusu hivi,
Ni strategy ya kupunguza alosto
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA TATU


Akasimama huku akipiga hesabu za namna alivyokuwa amesimama mkwaruzaji.

“Aliposimama hapa, alitizama huku” Alisema Zedi huku macho yake yakielekea kule alikohisi msimamaji alisimama na kutazama.

Aliona!!

Macho yake yaliona mikwaruzo hafifu ukutani, akasogea na kuimulika kwa karibu zaidi.

“KEKERA” aliyanakili maneno yale kisha akaendelea kuchunguza ukutani pale na hatimae aliona tena maandishi mengine.

“Nü..Mďjust..fĺshai>”
Akayanakili tena maneno yale kisha akamstua Haji na wakapotea kwenye eneo lile na kurudi kwenye makazi yao ambayo yalikuwa katikati ya mji wa Mogadishu.

Saa moja badae iliwakuta wakiwa wametulia kwenye nyumba za viongozi wa serikali wakiwa ni kama walinzi wa viongozi wa ngazi za juu walioishi eneo lile ni hii ni baada ya kuhama kwenye hotel waliokuwa wakiishi tangu wafike Mogadishu. Makazi yao yalikuwa karibu na ubalozi wa Uturuki na hawakuwa mbali na Lido beach.

Waliweka mezani maneno walioyakuta kule kwenye gofu na yaliandikwa kwa code za kificho ili ambae atakutana nao na hahusiki basi asiweze kutambua kinachondelea.
Walianza na neno KEKERA.

Ndio ni kekera ila ila alimaanisha nini katika ujumbe huu” Alisema Haji huku akili yake ikizunguka kuhakikisha wanavunja code ile na kujua maana halisi ya ujumbe uliokusudiwa.

Zedi alikuna kichwa,hakujua ni nini sababu ila alijisikia tu kukuna kichwa.

Na kilichowachanganya ni kuwa ujumbe ulikuja kwa haraka sana tofauti na matarajio yao na hivyo kufanya kujua ya kuwa ujumbe ule ni wa muhimu sana.

Tatizo ni wa kuvunja fumbo.

Nywele ziliwasimama na ni lazima wafumbue ili wajue yaliomo.

Kazi ilikuwa ngumu hakika na muda ulizidi kusonga.

Ilipita zaidi ya nusu saa,hakuna mtu Kati yao aliekuwa ametongoa lau maana ya maneno yale.

Tunafanya nini sasa!? Zedi alimuuliza Haji.

Hebu tujaribu kudadavua hili neno la pili.

“Nü..Mďjust..fĺshai>”

Waliyapitia tena maneno yale kisha kwa pamoja walianza kukubaliana kitu kimojakimoja kilichoonekana kuwaletea maana.

Walianza na neno “físhai”

Walianza kulipindua pindua ili kuleta maana katika lugha inayoeleweka.

Hatimae jibu waIilipata.

“Bila shaka ukiliweka liwe jina la mtu intapendeza sana!!” Alisema Haji.

“Ok jaribu kulisuka liwe jina” Alisema Zedi huku sasa akiwa anatazama mikono ya Haji iliokuwa bize kuandika.

“Ona hii” Haji alimwonesha Zedi karatasi.

“Shafi’i” Zedi alilitamka lile jina.

“Yesi ni Shafi’I” alisisitiza Haji.

“Aisee!! Inaleta mana hii” alisema Zedi huku akitabasamu.

“Na kama ni jina basi hilo ni la kiislam na kama ndivyo,basi alitaka tujue kitu kuhusu huyu jamaa” Alisema Zedi.

“Na nionavyo huyu atakuwa ni Imamu na kama ni Imamu basi haya maandishia yaliosalia ni jina la Msikiti.
“Nü..Mďjust..

“Yes,hebu igeuze hiyo u iwe a kisha tukiivunja tuseme hilo ..Mďjust. alimaanisha Masjid na hii “Nü..” inamaanisha nuur kwa sababu hapo juu ya u kuna doti mbili ikimaanisha hizo ni u mbili hivyo basi tunaweza kuusoma kama “Masjid nuur” Alisema Haji.

Zedi alitabasamu kiushindi.

“Kwa hiyo anamaanisha tumtafute Imamu Shafi’I kwenye msikiti wa Masjid nuur” Alisema Zedi.

“Lakini tunamtafuta kwa uzuri ama ubaya” Alihoji Haji.

“Haiwezi kuwa uzuri mana hapa Somali tupo sisi tu katika hii suicide mission na hakuna mwingine, hivyo huyo ni mbaya” Zedi alitanabaisha hisia zake.

Walikubaliana katika hilo.

Wakarudi tena kwa neno “KEKERA”

“kwani kesho ni siku gani?” Aliuliza Haji

“Alhamis” Alijibu Zed.

“Rais wa Kenya anahutubia si ndio” alihoji tena Haji na Zedi akaitikia.

“Basi tuliweke hili neno kama Kesho kenya Rais” Alifafanua Haji.

Zedi akaruka juu na kupiga mluzi wa nguvu kisha akaachia bonge la mtusi kuashiria kuwa anakubaliana na wa mawazo ya Haji.

“Sasa nimeelewa alichomaanisha bwana, yani mbali na kumtafuta Imamu Shafi’I; inatakiwa pia tujue kesho kuna tukio lingine kwenye hotuba ya Rais wa Kenya hapa Somalia” Alisema Zedi.

“sasa ana maana gani” Alihoji Haji huku akijikuna kichwa.

“He need to rescue the president” Alisema Zedi.

“Yah hilo linaweza kuwa ndilo wazo lake, lakini sasa hajasema litatokea tukio gani nyakati hizo” Alionesha mashaka Haji.

“Hawa ni magaidi na magaidi siku zote huwa wana njia mbili za kutekeleza mashambulio yao. Kwanza ni kwa kutumia collar bomb, hapa ni kujitoa muhanga na njia ya pili ni kwa kutumia wadunguaji” Alisema Zedi.

“Sasa hapa watatumia njia gani?” Aliuliza Haji.

“Ndo kazi yetu kujua ila nadhani wanaweza kutumia mdunguaji kwa sababu kujitoa muhanga mazingira yatakuwa hayawaruhusu.
Haji aliguna huku akikaa karibu na kompyuta lengo alitaka kujua ni wapi hasa mkutano wa Rais wa Kenya utafanyikia.

Aliwasha data na kuanza kuperuzi habari zinazohusu ziara hiyo.

“Watakuwa katikati ya mji kwenye ukumbi wa hoteli ya Lamada.” Alisema Haji huku akiendelea kuchezesha vidole vyake.

“Pale ni rahisi sana shambulio kufanyika kwa sababu ya majengo yaliozunguka hotel ile” Alisema Zedi.

“Hapa tukimtafuta mdunguaji tutachelewa, ila inabidi tuweke taharuki dakika chache baada ya hotuba kuanza” Alishauri Haji.

“Hatuwezi jua nafasi gani wanatumia ili kutekeleza tukio lao,hivyo inabidi tujue tunavuruga vipi mkutano huo kabla haujaanza” Alisema Zedi.

“So!” Alihoji Zedi.

“Tupange fake bomb, lile litazua taharuki na viongozi wataondolewa kabla ya kufanyika tukio”


“ooh sawa kamanda” Alisema Haji huku akiinuka na kuchukua chupa ya soda iliokuwa mezani kisha akachukua shati lake na kuiviringisha juu yake na alipomaliza alichukua kinyundo kidogo ambacho hutembea nacho kwenye begi akaanza kuiponda.

Dakika kumi baadae ule unga alikuwa anaujaza kwenye chupa nyingine na kisha alichukua njiti za kiberiti nazo pia alizisaga na kumchanganya ndani ya chupa iliokuwa na unga wa chupa iliosagwa kisha akachukua wine nyekundu iliokuwa kwenye jokofu na kuimimina mle na alichukua pia kiasi kidogo cha soda ya pepsi na kuweka kisha alianza kutikisa kwa nguvu na ilipoleta fukuto akafunika na kizibo kwa juu kisha akagongelea ili kuziba vizuri.

“ewaa,sasa huo mlio wake, bomu la nyukilia likasome kibada dadeki” Haji alijigamba.

“Hongera komredi mana naona unakamilisha taharuki” zedi alisema huku akicheka na kukaa kitandani.

“Zedi; hatuna muda wa kupoteza, ngoja tumsake huyu Imamu na msikiti wake” Alisema Haji huku akirudi tena kwenye kompyuta na kuendelea kutafuta jina la Masjid nuur.

Ukapita ukimya kidogo.

“Huu msikiti upo karibu na Casapoplare road na kilomita moja nyuma pia kuna shule ya msingi ya Imamu Shafi’I” Alisema Haji huku vidole vyake vikifanya kazi ya kusonta kwenye kioo cha kompyuta ambapo kulikuwa kuna ramani ya eneo lile.

“Jamaa inaonekana yupo vizuri mfukoni” Alisema Zedi.

“Tutajua mbivu na mbichi akijaa kwenye kumi na nane zetu” Alisema Haji.

Waliendelea kusoma ramani ile ili wajue mazingira ya kumtafuta Imamu Shafi’I.

Usiku nao ulizidi kuwa mkubwa!.

***

Honda na kundi la wapiganaji walipokewa katika misitu ya Ganigani kulikokuwa na kambi yao kubwa. Misitu ile ilikuwa juu ya vilima vya Ganigani na asilimia kubwa mji wa Mogadishu ulionekana vyema kuanzia pale.

Eneo lile lilikuwa ni la kimkakati kwao kwa sababu ya za kiusalama.

Mahema mengi na vidungu vilitamalaki eneo kubwa sana la kambi ile.

Wapiganaji wengi walikuwa ni watoto chini ya miaka kumi na saba lakini kwa mazoezi makali waliokuwa wanapitia walionekana kuwa ni wakubwa kuliko umri wao.

Sozi alimvuta mkono Honda na kuelekea nae kwenye hema moja lililokuwa pembeni kidogo ya kimlima.

“Hii ndo nyumba yako, maisha yetu unayajua hivyo vumilia, siku za furaha zinakaribia” Alisema Sozi.

Honda alitabasamu.

“Kwani kule Saadan kulikuwa ni kwa nani na kwanini kambi isiwe kule?” Alihoji Honda

“Hata mimi sijui ile nyumba ni ya nani, na sijawahi kuona mmiliki wake,lakini pia haiwezi kuishi mjini na hakuna usalama kabisa kule” Alisema Sozi na kisha akagongesha mikono na Honda na kuondoka kwenye hema lile.

Honda alibaki peke yake,alizunguka kila pahali kukagua na alipohakikisha kila kitu kiko sawa akaelekea kwenye godoro la sufi lililokuwa limewekwa juu ya kichanja.

Akajaribu kulala, alikutana na vumbi kubwa sana likitimka.

Akaguna.

Akalitoa godoro lile na kulipigapiga ili kupunguza vumbi.

Isa nae akaingia!!

“Inabidi uzoee na ndio maisha yetu yalivyo” Alisema Isa.

Honda hakujibu!

“Sasa hapa kuna jukumu kubwa la kufanya kesho na jukumu lenyewe ni kumwondoa mtu anaetusumbua hapa Somali ikiwa na yeye ana nchi yake, Kesho atakuwa hotel Lamada na vijana watu wameshafanya ukaguzi wa kutosha na hali ya ulinzi ni kubwa sana hivyo tumeona bora tutumie wadunguaji ambao watakaa jengo hili na hili” Alisema Isa huku akimwonesha Honda ramani aliokuwa ameshikilia mkononi.

“Vipi una uhakika una wadunguaji makini?” Alihoji Honda.

“Ninao vijana sita ni hodari sana kwa kazi hiyo” Isa alijibu.

“Good!!” Aliitikia Honda.

Isa aliondoka kwenye hema lile ili kumwacha Honda apumzike mana usiku ulikolea na mvua ilianza kunyesha.

Honda alipobaki peke yake, alitoa ile risasi alioikuta kwenye furushi la risasi zingine.
Akaifungua kichungi chake na ndani alikutana na kidude kidogo mithili ya kadi ya simu ila kilikuwa kinavibonyezeo kama viwili hivi na pia kulikuwa kuna kikaratasi chembamba kilichokuwa na maneno machache ya kiingereza.

“Press when you meet flamingo” Alijua ni kwanini alipewa kidubwasha kile kwa njia ile.

Alitafuna kikaratasi kile kisha akachukua kikasha cha risasi na kukifunga na kurudisha mfukoni huku kidubwasha kile akikipachika ndani ya nywele zake ndefu alizokuwa amezikata mtindo wa afro.

Kitu ambacho hakujua ni kuwa wakati analazimisha kikae sawia kwenye nywele alikibonyeza bahati mbaya na kilianza kusoma mawimbi.

Sozi alikuwa amelala na Isa pia alikuwa amelala.
Ila kuna mtu hema fulani hakuwa amelala na ni mwiko kwake kulala.
Mtu huyu alikuwa ni mtaalamu wa mawasiliano na kazi yake alihakikisha ananasa mawimbi ya radio yoyote ambayo ingelikuwa inasogelea kambi yao kwa sababu makomando ili wavamie ni lazima wawe na vifaa vya mawasiliano na pia alikuwa ndie anaeunganisha mawasiliano yote ya kambi nzima na watu waliokuwa nje ya kambi ambao ni viongozi wao.

Kifaa kimoja kilianza kukoroma kuashiria kuna muunganiko wa mawimbi rasimi na yasio rasimi.
Bwana yule akakifuatilia kifaa kile nacho kiliendelea kukoroma na kila alipojaribu kufuatilia mwelekeo wa mawimbi alipata ugumu kwa sababu ya mvua kubwa ya radi na miungurumo iliathiri utendaji wa kifaa kile.

Aligwaya!!

Ilimaanisha kufeli kwake ni kuangamiza kambi nzima.

Akavaa nguo za kuzuia mvua, akachukua kurunzi na kisu kisha akanyofoa kifaa kile na kutoka nje huku taratibu akiendelea kufuatilia mawimbi yale.

Honda alikuwa amelala chali huku mawazo lukuki yakipita kichwani kwake na utulivu wa mwili kwake ilikuwa ni afueni ili achanganue mambo.

Baada ya dakika nyingi za kuwaza hili na lile, taratibu usingizi ukaanza kujenga kibanda kichwani pake.

Mara muungurumo mkubwa wa radi ukarindima.

Usingizi ulikata.

Lakini akili yake ilimwambia kuna kitu cha ziada amekisikia wakati wa ngurumo ile.

Akatega sikio vyema.

Wakati wa mtiririko wa mvua “tatatatata……!” kuna sauti nyingine aliisikia katikati ya mtiririko ule.

Akatega tena!!

“tatatata.. ti..tatatata..ti..”

Ile ti,ilimwashia kengele ya tahadhari.

“hakuna mlinzi anaeweza kutembea katikati ya mvua kubwa hii” Alijisemea!!

Ndipo alipoamka na pia akahisi kitu kikiwaka na kuzima kichwani kwake.

Akakitoa kifaa kile na kukibonyeza kikaacha kumweka.

“tatatata…ti….tatatata..ti..”
Bado aliendelea kusikia sauti ile na sasa ilizidi kukaribia kwenye hema lake.

Roho ikamdunda!!

****

ITAENDELEA KESHO JIONI.
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA NNE




“hakuna mlinzi anaeweza kutembea katikati ya mvua kubwa hii” Alijisemea!!

Ndipo alipoamka na pia akahisi kitu kikiwaka na kuzima kichwani kwake.

Akakitoa kifaa kile na kukibonyeza kikaacha kumweka.

“tatatata…ti….tatatata..ti..”
Bado aliendelea kusikia sauti ile na sasa ilizidi kukaribia kwenye hema lake.

Roho ikamdunda!!

Kule nje yule bwana aliendelea kuhangaika kutafuta mwelekeo wa mawimbi na bado alijua mawimbi yale yalitokea kwenye moja ya mahema aliokuwa amesimama kati yake.

Akawa anapiga hatua moja mbele na hatua moja nyuma,yani bila kutoka pale alipokua lengo likiwa ni kujua mweleko sahihi wa mawimbi mageni.

Hatimae alijua ni upande gani mawimbi yale yalikuwa.

Honda nae kule ndani alikuwa amesimama karibu kabisa na mlango na kwa kusaidiwa na mwanga wa radi, aliweza kuona mtu akiwa hatua chache kutoka mlangoni kwake na alikuwa anahangaika huku na huko.

Honda akili ikamjia na haraka akawasha kidubwasha kile na kukirudisha ndani ya kikasha cha risasi kisha akaruka hatua kubwa na kuangukia kitandani na kulala.

“Aisee hawa watu wana mitambo yenye nguvu sana” Alijiwazia huku akimalizia kujifunika shuka.

Dakika moja badae, yule bwana aliingia mule ndani na bila kujali kama alikuta mtu au la, yeye aliendelea kukagua hapa na pale.
Hatimae kile kifaa kilianza kutoa mlio mkubwa mfululizo na Honda akaamka na kukutana na kisu kikiwa shingoni mwake.

“ulikuja kutupepeleza sio? Alihoji yule bwana huku akitumia mkono mwingine kuwasiliana kwa simu ya upepo.

Hazikupita dakika tatu wapiganaji zaidi ya sita wenye mitutu waliingia mle ndani na kumweka kati Honda.

Isa nae akaingia.

Yule bwana akampa maelekezo kwa lugha ya kienyeji na kisha akamwonesha kifaa kile chenye muundo wa risasi alichokikuta kwenye viatu vya Honda.

“Hii si ni ile ya kule melini?” Alihoji Isa huku akimtizama Honda.

“Ndo yenyewe! Kwani kuna nini mbona navamiwa usiku huu? Alihoji Honda.

“Aah ni usalama tu unazingatiwa ila usijali” Alisema Isa huku akiwapa ishara wapiganaji wake nao wakashusha silaha zao.

“Wale wazungu walikuwa ni mamluki na tulikuwa sahihi kuwapoteza, walituwekea mtego wa kujua tulipo aisee” Alisema Isa huku akimwangalia Honda ambae wakati huo alikuwa anafanya jitihada za kunyanyuka kitandani.

Isa aliongea na vijana wake kuwaelesha na kisha wakasambaratika mle hemani na kukiharibu kifaa kile.

Honda alipumua kwa afueni na kurudi kujilaza na hakulapua lau tone la usingizi hadi ilipotimu ahsubuhi.

***
Ahsubuhi ilikuwa na mengi ya kufanya kwa pande zaidi ya tatu.

Honda na wapiganaji wa AIAI waliamka wakiwa na lengo moja la kufanya mauaji katikati ya Mogadishu huku wadunguaji wakifanya zoezi kwa ajili ya kukamilisha kazi yao mida ya jioni ya siku hiyo.

Upande mwingine ulikuwa ni ule wa Zedi Wimba na Haji Makame ambao wao lengo lao lilikuwa ni kuvuruga mipango ya wauaji na kumuokoa Rais bila uwepo wao kujulikana popote.

Kundi lingine lilikuwa ni kundi la ulinzi na usalama wa viongozi wote watakao hudhuria mkutano huo na bila kujua lolote linalopangwa, wao waliendelea na taratibu zao kama kawaida kuhakikisha usalama upo kwa asilimia zote.

Hatimae wakati uliwadia!!

Maeneo yote yalikuwa na ulinzi wa kutosha kuhakikisha eneo la Lamada na viunga vyake lipo salama.

Misafara ya viongozi mbalimbali ilianza kuwasili kwenye hotel Lamada.

Aliingia Rais wa Somalia kisha akafuatia Rais wa Kenya na wajumbe wake.

Katika majengo matatu yaliokuwa yanatazamana na hotel ile, kulikuwa kuna makundi mawili yenye malengo tofauti.

Kundi la kwanza lilikuwa lile la wadunguaji ambao kila mmoja alikuwa amekaa sehemu yake kuhakikisha mlengwa wao hawamkosi na walitaka kufanikisha azima yao hiyo wakati rais huyo atakapokuwa akitoka ndani ya hotel.

Kundi lingine lilikuwa ni lile ambalo lilikuwa na watu wawili tu na wao walikuwa kwenye chumba cha hotel nyingine wakiwa na chupa yao iliokuwa na unga wa chupa nyingine na vitu vingine kadhaa ambavyo vingehakikisha sauti iliokusudiwa inatoka.

Walikaa wakihakikisha kabisa kila tukio linaloendelea kule chini linatazamwa na wao mubashara bila kukosa hata nukta.

Muda wa kuanza kikao ulianza na watu mbalimbali walikuwa wapo na radio zao wakisikiliza.

Waliongea viongozi kadhaa na hatimae wakati rais wa Kenya anataka kuzungumza; Zedi na Haji walikonyezana.

Na hatua iliofuata ilikuwa ni kufungua dirisha kisha wakapachika chupa ya bia kwenye mdomo wa bunduki aina ya gobole kisha wakafyatua kuelekea kule ilipokuwa Lamada hotel na kilichofuata ni sauti kubwa ilioambatana na moshi mzito.

Ilikuwa ni taharuki iliozuka,walinzi wa viongozi hawakujua kimetokea nini na harakati zao zilikuwa ni kuhakikisha hakuna madhara yanayotokea kwa viongozi hao.

Wadunguaji nao walibaki wakiwa wamebutwaika wasijue kilichotokea.

Isa ambae alikuwa karibu ya eneo la tukio na Honda; walishuhudia mtafaruku usiosemekana.
“Shukeni wote, na msiache alama” Isa alitahadharisha vijana wake kisha akaondoa gari na wakarejea porini huku wakiwa wameshindwa kuekeleza mpango wao.

Zedi na Haji nao walikuwa wako mbali na eneo lile huku wakiwa wanashingilia ushindi wao kwa kuvuruga mpango ule ambao hawakuwa na hakika kama walikuwa sahihi,ila walijua wamefanya kile walichopaswa kufanya.

Na kazi ikabaki ni kumtafuta Imamu Shafi’I wa msikiti wa Masjid nuur.


***

- TANZANIA-

Ahsubuhi ile ilikuwa ni ahsubuhi mbaya kabisa kwa Remi.

Alilia peke yake na kulikuwa hakuna wa kumsaidia wala kumuonea huruma.

Alilia na Mungu wake.

Nchi nzima kulitapakaa taarifa zake na picha zake, mitandao ya kijamii ilikuwa ndio taarifa kuu.

Alikuwa amesahau kuzima simu yake na mara ikaita.

Namba zilikuwa ni za Kagoshima.

“Nadhani kuna haja ya wewe kujisalimisha kituoni”
Alisema Kagoshima.

“Muda ukifika nitafanya hivyo ila sio sasa” Alijibu kinyonge Remi.

“Ila tambua serikali ina mkono mrefu itakufikia tu” Alisema Kagoshima.

“Haina shida” Alijibu Remi na kukata simu.

Alishusha pumzi na kuzishusha, alihitaji kuhama pale mana si pahali salama tena kwake.

Walikuwa na nyumba nyingine mwananyamala kisiwani.

Wakati anatoka kwenye ile nyumba alihisi hayuko peke yake,licha ya kujifunika kanga juu hadi chini.
Licha ya kuhisi huko lakini kamwe hakuona mtu mwenyewe yupo umbali gani nae mana watu walikuwa ni wengi nyuma yake.

Alichukua bodaboda na kwenda kushukia komakoma na kuanza kutupa tena miguu yake kwa hatua za mashaka tele.

Hakufika hata mbali, alihisi kitu kidogo kikipenya kwenye shingo yake na kilichofuata hakujua licha ya kuhisi akiangukia mikononi mwa mtu.

Remi mbio zake ziliishia ukingoni.

***

Tukutane wakati mwingine
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660


SEHEMU YA KUMI NA TANO



***

- TANZANIA-

Ahsubuhi ile ilikuwa ni ahsubuhi mbaya kabisa kwa Remi.

Alilia peke yake na kulikuwa hakuna wa kumsaidia wala kumuonea huruma.

Alilia na Mungu wake.

Nchi nzima kulitapakaa taarifa zake na picha zake, mitandao ya kijamii ilikuwa ndio taarifa kuu.

Alikuwa amesahau kuzima simu yake na mara ikaita.

Namba zilikuwa ni za Kagoshima.

“Nadhani kuna haja ya wewe kujisalimisha kituoni”
Alisema Kagoshima.

“Muda ukifika nitafanya hivyo ila sio sasa” Alijibu kinyonge Remi.

“Ila tambua serikali ina mkono mrefu itakufikia tu” Alisema Kagoshima.

“Haina shida” Alijibu Remi na kukata simu.

Alishusha pumzi na kuzishusha, alihitaji kuhama pale mana si pahali salama tena kwake.

Walikuwa na nyumba nyingine mwananyamala kisiwani.

Wakati anatoka kwenye ile nyumba alihisi hayuko peke yake,licha ya kujifunika kanga juu hadi chini.
Licha ya kuhisi huko lakini kamwe hakuona mtu mwenyewe yupo umbali gani nae mana watu walikuwa ni wengi nyuma yake.

Alichukua bodaboda na kwenda kushukia komakoma na kuanza kutupa tena miguu yake kwa hatua za mashaka tele.

Hakufika hata mbali, alihisi kitu kidogo kikipenya kwenye shingo yake na kilichofuata hakujua licha ya kuhisi akiangukia mikononi mwa mtu.

Remi mbio zake ziliishia ukingoni.

***

Sajenti Kobelo; aliegesha gari kwenye uwanja wa ccm mwinjuma kisha akatembea kwa miguu kuelekea kilipokuwa kituo cha polisi.

Baada ya kufanya taratibu zote za kujitambulisha na kueleza nia yake pale kituoni, hatimae alielekezwa ilipokuwa ofisi ya marehemu Vengu ambayo ilikuwa inakaimiwa na mtu mwingine wakati huo.

Aliingia na kumkuta mtu yule ambae alikuwa na cheo sawa na chake.

Itifaki ilizingatiwa kisha akasema kilichompeleka pale.

Alipewa faili ambalo alikuwa akilitumia Sajini Vengu.

Alianza kuyakagua kwa umakini wa hali ya juu sana.

Alikutana na maelezo yaliokuwa yameandikwa na Remi. Pia alisoma namna tukio la kutekwa kwa mwandishi lilivyomhusanisha na ofisi za uchunguzi wa mambo kale na pia ni kwanini mtuhumiwa alitakiwa kuwa Remi.

Alitoa kitabu chake kidogi a kuanza kuandika yale alioona ni muhimu kwake na pia alikutana na namba za simu za Remi.

Alizinakili pia kisha akawa ametoka na picha mbili tofauti.

Remi anahusika na pia Remi hahusiki.

Kwanini?

Kwa sababu Remi aliwasiliana na Davis Minja na kumwelekeza jambo hivyo anahusika kwa asilimia kadhaa kujua alipo mwandishi yule.

Lakini pia Remi anaweza kuwa hahusiki kwa sababu asingeweza kufanya tukio akiwa ofisini kwake.
Hoja ya mwisho ilikuwa na mashiko kidogo.

Lakini kuna kitu kingine kilimpa maswali…
Kwa nini Davis afuatiliwe na kisha atekwe kwenye ofisi za Remi?

Remi Haji Makame!!
Aliliandika jina lile kwenye kitabu chake kisha akaaga na kuondoka.

Lakini kabla hajatoka mle ofisini akamgeukia ofisa aliemkuta mle ndani.

“Kama kuna mtu atakuja kujitambulisha kwako kwa jina la Kenge; basi mwambie lolote ila sio hizo kablasha nilizokagua” Alisema sajenti Kobelo.

Ofisa yule alikubali.

Sajenti alitoka na kuelekea alikokuwa amepaki gari lake, akapanda na kuondoka lengo likiwa ni kuelekea nyumbani kwa Sajini Vengu ambae msiba ulikuwa umewekwa kwao kimara na yeye alikuwa anaishi mwananyamala kwa Bibi titi.

Njiani yalipita maswali kadhaa kichwani kwake.

Alihitaji kumjua kwanza Remi.
Haji Makame ni jina la watu wa Pemba na kiasili ni waislam na Remi ni jina ambalo halijasidifu imani yoyote ila si jina lenye asili ya huko Pemba; sasa vije tena Remi iungane na Makame?

Hata!!

Kuna walakini katika jina hilo.

Lakini kulikuwa kuna haja gani ya kumuua Sajini Vengu?

Kuna jambo si bure.

Alipiga ngeta baada ya mwili wake kumsisimka.

Moja ya vitu alivyokuwa amejaliwa Sajenti kobelo; ni hisia.
Kila anapokuwa katikati ya jambo zito, mwili wake huamsha msisimko usiokifani na hapo hujiandaa kukabiliana na hatari.

Kwa maelekezo ya ananuani alioikuta ndani ya kituo cha mwinjuma ni kuwa Vengu aliishi nyumba namba kumi na tano.

Njia haikuruhusu gari kupita, alitafuta sehemu alioona inafaa akapaki gari kisha akaanza kutafuta namba ya nyumba hiyo.

Hakukawia kuiona!

Kulikuwa kuna geti jekundu na nyumba ilionekana kuwa pweke.

Akasukuma geti na kuingia ndani kisha akageuka na kulitazama lile geti.

Inamaana hakuwa amelifunga hili geti?

Hakukuwa na wa kumjibu.

Akapiga hatua zake ndogo ndogo huku akijaribu kutazama mazingira ya nje ya nyumba ile ambayo haikuwa kubwa licha ya kuwa na geti.

Kulia kwake kulikuwa kuna kibanda ambacho kwa ndani kulikuwa kuna pikipiki kubwa ya Baja.

Akarudisha macho kutazama mlangoni mwa nyumba.

Mmmh!!

Aliguna baada ya kuhisi kuchunguliwa na mtu kutokea ndani upande ambao alihisi kuna chumba kulingana na dirisha lilivyokuwa limekaa.

Alihisi kabisa kuna mtu alikuwa amesogeza pazia na kumtazama.

Ni nan na anafanya nini?

Akaongeza tahadhari!!

Akasukuma mlango.

Nao ulikuwa wazi.

Ala!!

Akaingia kwa tahadhari kubwa huku akiwa makini kuliko makini yenyewe.

Mezani alikuta kuna kompyuta mpakato iliokuwa imefungwa nusu yani kama vile mfungaji alikuwa na haraka sana.

Akaikunja kompyuta ile kisha akaiacha pale mezani na kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye chumba alichohisi kuona mtu akimtizama.

Alipokaribia mlangoni tu akajikuta akirushwa sebuleni kwa teke zito lilitua sawia kifuani mwake na kwenda kumsambaratisha chini kama mzigo.

Akakataka kusimama ila alijikuta akijaa kwenye mikono ya mvamizi na kupigwa double hit kifuani kwa lengo la kumvunja mifupa ya kifua ila akawahi kujua hila hiyo hivyo kwa tabu akajitahidi kurudi nyuma kwa mtindo wa aina yake na kujikuta akipamia kabati ambalo alisambaratika nalo chini.

Bado mvamizi hakumwacha, akamzoa chini kwa mikono miwili kisha akamtwisha kichwa katikati ya paji la uso na Kobelo akabweka kama mbwa dume aliepokonywa mwanamke wake.

Maumivu yakamsambaa mwili mzima.

Kobelo akaona akizubaa nae ataitwa maiti.

Kwa nguvu zilizosalia akajiachia na kufyatuka kichwa kikali kilichoenda kutua kifuani mwa mvamizi na kisha kumrusha nyuma kwa kasi na kumbwaga chini akasambaratika kama gunia la nyanya mbichi huku akilia kama mbwa jike aliezidiwa na mkuyenge.

Sajenti kobelo aligundua kitu wakati akijipanga kumkabili adui.
Alihisi kichwa chake kimekutana na nyama laini hivi lakini kilio kilichotoka kilikuwa cha kike.

Ebana e!

Mvamizi alisimama,alikuwa ni mwanamke.

Kila mmoja alijipanga kumkabili mwenzie.

Mvamizi akanesa kidogo na kuachia ngumi za harakaharaka lakini zote zilienda kupiga hewa na alijikuta akipokea makonde mawili ya nguvu mbavuni mwake.

Akabweka kama bwege.

Akajaribu tena kurusha mateke, lakini yalipanguliwa kistadi na sajenti kisha akamwachia konde zito kwenye mbavu za kulia.

Mvamizi alimanusura atapike dagaa aliokula.

Alipojaribu kuhema akashindwa na alipotaka kusimama pia alishindwa.

“Mwanamke waacha kuoelewa unakuja kupambana na waume zako pumbavu wewe” Alisema Sajenti Kobelo huku akiwa anamtazama mvamizi akijaribu kujiinua bila mafanikio.

Mara likatokea tukio ambalo Kobelo hakulitarajia.

Mvamizi kwa kasi ya ajabu alitoa kitu mifukoni kwake na kupiga chini na kuzuka moshi mzito ambao ulimchanganya Kobelo na alichosikia ni sauti ya mgongano wa mtu na mlango na alioojaribu kufuata nyuma hakuna alichoambulia zaidi ya sauti za mgongano wa milango ya geti.

“ooh shit” alimaka Sajenti huku akirudi ndani na kuikwapua kompyuta kisha akatoka haraka eneo lile.

Kitu ambacho hakujua ni kuwa kompyuta ile ilienda kuzua utata.

Utata ambao ulizidi kuwa utata!!

***

Nb: hakuna kitu kinachokatisha tamaa Kama kuona uposti zaidi ya vipande sita kwa siku tatu afu unakutana na komenti nne tu na pale unapokuwa na majukumu mengine usipoposit siku mbili kuna watu wanatokea na kukuvurumishia majina ya kila aina mara unalinga mara hivi mara vile,wakati ukipost huwaoni.

Ni wambie kitu!!

Hakuna kitu ambacho mwandishi anapenda na kupata moyo kuendelea na kazi yake kama kuona anapata sapoti na ushauri wa watu kuhusu kazi anayoipost kwa sababu unapoandika huwa upo peke yako na unapopost unabaki kuwa peke yako dah lazima ukate tamaa au hata ule mzuka wa kutupia kila siku unaweza kuisha na usijali.

Sapoti yako ni muhimu kuliko matusi yako!!

Tukutane kesho
 
Back
Top Bottom