Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

Riwaya: Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia

RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA


***
Akiwa njiani; Sajenti Kobelo aliamua kupita kwenye vibanda vya kutengeneza simu, na alipofika aliomba wamtolee mfumo wa kudai neno la siri kwenye kioo kabla hujaendelea kufanya mengine kwenye simu.

Alilipa na kuahidiwa dakika chache kila kitu kitakuwa sawa.

Haikupita hata dakika ishirini, tayari fundi alimkabidhi simu janja aliopora mfukoni mwa marehemu J Malao.

Akaondoka huku akiwa na lengo la kuelekea kituoni kwake kuripoti mchana ule kama zamu yake ilivyohitaji kwa siku hiyo.

Njiani mawazo lukuki yalikuwa yanampitia hasa alipokumbuka kauli ya baunsa kwenda kwa Kenge.
Aliirejea "Fanya yanayokuhusu"

Aliguna!

Inamaana Kenge kuna kitu anajua kuhusu sakata hili sasa vije tena aonekane kushupalia suala hili, na kama baunsa aliamua kumuonya tu ili ujumbe umfikie kwa nini sasa alitaka kumlipua?

Yalikuwa ni maswali bila majibu na kulikuwa hakuna wa kumjibu zaidi ya yeye mwenyewe kulitafuta jibu.

Kenge kuna kitu anajua bwana" Kobelo alijisemea peke yake.

Kobelo aliingia kwenye maegesho ya utawala na kupaki gari lake kisha akashuka na kuelekea kituoni.


"Sajenti; kuna ujumbe wako hapa" Aliseme WP Mengi ambae alikuwa anatoa huduma mapokezi.

Kobelo alisogea karibu yake.

"Unahitajika kwa OCD tafadhali" Alisema WP Mengi.


"Nashukuru" Alisema Kobelo na kupiga hatua kuelekea mlango wa ofisi za mkuu wa kituo kile kidogo.

Alisukuma mlango na kuingia ndani baada ya kuruhusiwa kuingia.
Ndani alikuatana na Mzee wa makamo ambae umri wake ulikuwa bado unaruhusu kuendelea kufanya kazi kwa miaka kadhaa badae.


"Sajenti; unaweza kunambia ni kitu gani kimekuweka bize siku mbili hizi" alisema OCD huku akiwa amefumbata mikono pamoja na kuegemea juu ya meza iliokuwa karibu yake.


"Afande nipo tu nashuguli zangu za kila siku hasa baada ya kutoka kazini" Kobelo alijibu.
.
Mzee alitabasamu.

"Umri unanienda ila bado sijafikia kudanganywa namna hiyo bwana mdogo" OCD alisema huku macho yake yakiwa usoni mwa Kobelo.

Kobelo alitizama pembeni kwa aibu ya kugundulika.

"Umefikia wapi na kesi unayofuatilia?" OCD alihoji.

Kobelo alishituka licha ya kutoonesha mshituko wake hadharani.

"Najua umejipa kesi ambayo hutakiwi kuifuatilia na ipo mikononi mwa askari mwingine, huko ni kukosa nidhamu na pia ni viashiria vya rushwa kwa sababu hadi sasa umesababisha mauaji ya mhariri J Malao" Alieleza mzee.

Ohoo!!

Ilikuwa ni ngumu kumeza; Kobelo alitumbua macho mithili ya jogoo aliekosa kitoweo. Amesababisha vipi mauaji wakati hajui hata namna alivyokufa huyo mtu na ni nani mhusika kati ya Kenge na yule baunsa.

Ebenaee!

Kobelo aligwaya kwa muda na alijua msala umemwangukia jumla jumla.

"Ni kweli ila sijahusika na mauaji yake afande" Alijitetea Kobelo.

"Hata kama hujahusika na vipi unahusika katika kesi isiokuhusu? Au hujui huko ni kuharibu upelelezi? Na kwanini waenda kinyume na maadili ya kazi yako?" OCD aling'aka.

Kobelo alipiga kimya.

OCD alibinua droo na kutoa bahasha na kumkabidhi Kobelo.

"Unasimamishwa kazi kwa muda usiojulikana hadi uchunguzi juu yako utakapokamilika na wakati wote huu usijaribu kufanya jambo lolote la kijinga, hatutakuwa na huruma na wewe tena zaidi tutakusekweka ndani" Aliunguruma Mzee huku akiwa amemtolea jicho Kobelo.

Kobelo alinywea gafla na kushindwa kuamini, hakupata kauli japo ya kujitetea na hatimae alibeba barua ile na kusaluti kisha akatoka nje akiwa mnyonge kupitiliza.

Kobelo alitupwa nje ya kazi kwa muda usiojulikana.


***

Upande mwingine alikuwepo Kenge akiwa amefungwa bandeji karibu uso mzima na kubakiza sehemu ndogo tu ya uso wake.

Licha ya kupachikwa bandeji hizo ila bado alionekana uso umemvimba na pia majeraha mengine yalikuwa yamejitokeza kwenye mikono yake..

Vioo vya kabati vilimuumiza sana ila uso uliumizwa na kofi alilopigwa na baunsa.

Licha ya kuwa na bandeji usoni bado miwani yake haikumtoka usoni ila wakati huu aliivaa juu ya bandeji na kufunika macho kwa juu juu tu.

Alikuwa ameshika kalamu na karatasi, ambazo alikuwa anazisoma kwa kuzinyayua juu mana kutazama mezani asingeweza kwa kuwa bandeji ilifungwa kuanzia shingoni.

Alizungusha shingo yake na kumtazama afande mwenye cheo cha koplo aliekuwa amesimama peke kando yake ndani ya ofisi ile.


"Nenda uniletee yule mwanamke" Aliagiza kibabe.

Koplo alitoka kutekeleza amri na dakika chache badae alirudi akiwa ameongozana na Remi ambae kimuonekano alionekana kudhoofu sana.



Kenge alipomuona alinyanyuka kwa hasira ila alirudi gafla kwenye kiti huku akigugumia kwa maumivu, alijisahau ya kuwa mbavu zake na mguu mmoja navyo vilikuwa vimefungwa kwa bandeji kuzungushia pande zote baada ya kuonekana mbavu zilipata athari kidogo wakati wa makabiliano.

Ingelikuwa ni mtu mwingine basi wakati ule angekuwa nyumbani ama hospitali kama alivyoshauriwa na matabibu, ila sio Kenge ambae bado alisisitiziwa kupewa pesa endapo angefanikiwa kumsainisha karatasi zenye maelezo ya kukiri kuua na kuhusika kwa sakata lile msichana Remi.

Angelala vipi wakati ameahidiwa donge nono!


Hata!!

Lazima Remi asaini.

Kwa hasira alimsukumia karatasi na kumuamuru asaini.

Remi akazichukua na kuzisoma kisha akacheka.

"Hata kama ningekuwa nimeua kweli, bado nisingekubali kusaini maelezo ya mtu mwingine; Polisi ni sehemu ya kupata haki vije tena ionekane mwataka kukandamiza haki ya mtu asiehusika."
Remi akanyamaza kidogo na kuendelea.

"Sikia nikwambie wewe askari mabandeji, nifungeni mtakavyo ila sisaini, nipigeni muwezavyo ila sisaini." Akanyamaza tena na kumtazama Kenge.

"Afu aliekufanya hivyo, angeongeza kidogo hakika hata nguo ningemvulia, mbona kakupiga kidogo afande" Alimalizia kwa tabasamu.

Kenge huwa hapendi dharau, ila afanye nini sasa wakati anamaumivu kila sehemu, kuinuka tu ni tabu vipi kurusha mkono.

Kenge alijikuta akivimba tu bila kumfanya lolote mtuhumiwa wake.

"Afu ulisema unaitwa Kenge; wewe kweli ni askari Kenge; yani unashindwa kutafuta ukweli unakuja na maelezo feki na kwanini nipo humu muda wote bila kupewa karatasi niandike mwenyewe? Askari Kenge" Remi aliongea kwa uchungu na maneno yake yakazidi kumuumiza Inspekta Kenge..

Kenge chozi likamtoka.

Kwanini?.


Kwa sababu alilia hana uwezo wa kumwadabisha Remi na alishaonywa na wakubwa zake kuhusu kuruhusu mtu mwingine kumwadhibu mtuhumiwa aliemikononi mwake hadi viongozi wajiridhishe na uhitaji huo, lakini pia alilia kuona Remi katia ngumu kusaini ili yeye apate pesa na kukabidhi kesi mahakamani.

Ilitia uchungu hakika.

"Wewe mwanamke nikipona utalipa maneno yako yote ya leo fisi wewe" Alijitutumua Kenge..

"Ukiona askari anaependa kutukana watuhumiwa, basi huyo kichwa chake kinawalakini. Mimi ni mtuhumiwa tu wala sio muuaji na nipo kwenye mikono salama hivi sasa, sasa kwanini mnataka nionekane nipo jehanamu" Remi alisema kwa uchungu.

"Najua uonaongea hayo kwa kuwa waniona nipo hivi afu..." Kenge hakumalizia kauli yake, akaingia mtu mwingine ndani ya ofisi zile.

Kenge alishituka kuona mtu mwenye cheo kikubwa na anaefanya kazi makao makuu akiingia mle ofisini kwake.

Kenge akapaparika kutoka saluti ila kajikuta hawezi na kuishia kupiga mweleka huku akitoa mguno wa maumivu.

Ofisa alieingia akatabasamu kwa tukio lile kisha kwa madaha alikaa kwenye kiti alichokuwa amekalia Kenge.

"Inspekta Kibe nadhani unahitaji kupumzika lau siku mbili hivi, nitaongea na mkubwa wako akuache upumzike na hongera kwa kuipenda kazi yako" Ofisa alisema.

Kenge akajichekesha huku akifanya juhudi za kusimama na kisha kutoka mle ndani baada ya kupewa ishara atoke.

Alikuwa ni Naibu Kamishina P. Kagoshima.

"Najua hupendi kuwa humu Remi; ila hakuna namna ni lazima uwepo humu kwa usalama wako" Alisema Kagoshima.

Remi hakumjibu.

"Nimekuja hapa kukusalimia na pia kuweka mambo fulani sawa" Kagoshima alisema tena.

Remi kimywa.

"Uwezo wa kujisaidia unao, ila hutaki tu Remi"

"Vipi unataka nijisaidie kwa kukiri kuuwa? Au najisaidia vipi sasa ikiwa nipo selo?" Remi alisema..

Kagoshima alitabasamu.

"Remi sio kukiri, ila ombi langu tu linaweza kukutoa humu" Kagoshima alisema.

"Lionee haya vazi tukufu ulilovaa, mbona walidhalilisha namna hiyo? Unawezaje Ofisa mkubwa kutega kwa kutumia matatizo yangu?" Alijitutumua Remi.

Kagoshima alikunja uso.

"U jeuri sana, ila jeuri yako si lolote, kumbuka upo mikononi mwa dola na unatuhumiwa kuua, mumeo anatuhumiwa ugaidi, vipi kuhusu mwanao Pius?" Kagoshima alitupa karata makini sana.

Remi alistuka kukumbushwa mwanae ambae alikuwa shule wakati huo na hajui maendeleo yake. Ni vipi kama ataendelea kushikiliwa na mwanae afunge shule nani atampokea ama nani atampa pesa aende kwa ndugu zake Zanzibar alikozaliwa baba yake?

Ebana eeh!!

Ubaridi ulimtambaa mwili mzima. Alimtizama Kagoshima kwa huruma na Kagoshima akainua mabega juu bila kusema neno.

Ilimaanisha maamuzi yapo kwa Remi mwenyewe,abaki selo mwanae ahangaike ama akubali kuwa mpango wa kando kwa Kagoshima ili ajue namna ya kumweka sawa mwanae.

Utata!!..



NB; KUNA WATU HAWAPENDI ALOSTO, HIVYO BASI ILI UWATANGULIE WENGINE, UNAPASWA KUNUNUA KWA TSH 2000/=
UNATUMIWA KWA NJIA YA WHATSAPP NA EMAIL.

NAMBA ZA MALIPO NI 0758573660 NA 0658564341 NA 0624155629.

Namba zote jina ni Bahati Mwamba.
 
mwenzenu niko icu sababu ya arosto🙄🙄 maana ametupa kimoja tu kama dawa jomon😱🤪😁😁
 
Baunsa likasimama kwa gadhabu ya kutekenywa likaachia kwenzi mujarabu ilioenda kutua utosini mwa Kenge na kumzubaisha kwa sekunde kadhaa.
 
Kudo buana!!! Umenijengea mazoea mabaya sana ya kukimbilia mwisho wa kila episode...kuna mikwara mizito sana unaitupia pale inaleta hamasa ya kutaka kujua kifuatacho. LAITI WANGEJUA, WANGETAFUTA MAJENEZA YAO WENYEWE[emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI


***

---MOGADISHU---


ilikuwa ni siku ya pili tangu Haji aanze kufuatilia nyendo za Imamu Shafi'I. Na kutoka msikiti wa Masjid nuur; kuna kitu Haji alibaini.

Kila inapokuwa alfajiri huwa kuna gari mbili zinafika kwa wakati mmoja na gari moja humshusha Imamu na gari la pili humshusha mtu alievaa mavazi ya kike na kujitanda juu hadi chini.

Mwanzo alidhani anaweza kuwa ni mke wa Imamu ila siku ya pili alihisi kitu kikubwa zaidi.
Mtu yule hakuwa akielekea mlango wa kuingilia upande wa wanawake ila aliingia mlango wanaposwali wanaume na kutokea hapo hapo wakati wa kutoka.


Haji nae ni muumini wa dhehebu la suni; akaingia siku ya pili yake.

Ajabu hakumuona yule mwanamke na pia hakuona kama kuna pahali unaweza kupita na kuelekea upande wa pili ambako wanaswali wanawake ni kama kulikuwa kuna ukuta ambao haukuruhusu pande zile kukutana endapo mtu angetaka kuingia huko baada ya ibada.

Lakini pia hakuona tena mtu alievaa nguo zile za kike.

Aah!

Sasa aliemuona anaingia yupo upande gani na kama hajavaa mavazi hayo amekaa wapi!

Haji aliendelea na utaratibu alfajiri ile huku macho yake akiyazungusha kama kinyonga na kutazama watu wote ambao aliamua wawe mbele yake.

Hakuona kabisa alipo mtu yule.

Ila alihisi mtu yule anafanya sala nyuma ya mimbari kulikokuwa kuna radio iliokuwa inatumika kurusha matangazo ya ibada ile ya ahsubuhi.

Akapanga tena kwenda kukaa pale anapokuwaga kila siku na kutazama yanayoendelea kule msikitini.

Siku hiyo aliwahi kutoka kabla ya wengine na kwenda mbali kidogo na eneo lile kisha akachukua kiona mbali na kukaa vyema kusubiri kuona kama mtu yule atatoka tena..

Karibu watu wote walikuwa wameshaondoka msikitini baada ya swala ya ahsubuhi ndipo alipoona tena Imamu anatoka akiwa ameongozana na mwanamke yule na kisha wakazungumza kidogo na kila mmoja kupanda kwenye gari lake na kuondoka.

Haji Makame aliguna.

Sasa kama ni mwanamke kwa nini asisali kunakomhusu? Na kwanini mule ndani hakuonekana wakati wa ibada?


Kuna nini?.


Hakukuwa na wa kumjibu Haji.

Haji alijikuta anaanza kumhusisha Imamu na Shafi'I na kile wanachokitafuta Mogadishu na hapo ndipo alipojikuta anaanza kumchukia Imamu yule.

Kwanini!

Kwa sababu wanatumia vibaya mwamvuli wa dini kufanya mambo yao ya hovyo. Wakati wengine wakipigana kusambaza uislamu Dunia nzima, wao wanautumia kufanya hujuma kwa masilahi yao.

Haji alijiapiza kula nae sahani moja, hawezi kuchafua dini yake ya haki kwa mabaya wanayoyafanya.

Alitoka alipokuwa amejibanza, akapanda gari na kurudi wanakoishi ili kujadili kile alichokiona msikitini kwa Imamu Shafi'I.

***

Majira ya saa nne tayari Haji alikuwa mezani na Komando Zedi wakijadili kazi yao.

"Hapa kwenye mtandao naona wasifu wake ni kuwa ni mwanazuoni wa shahada mbili za uzamivu na pia amehitimu katika chuo cha dini ya kiislamu huko Saudia. Na tofauti na hapo wamemtaja tu kama mwanzilishi wa shule na...." Haji hakumalizia kauli yake; Zedi akadakia.

"Hapo shuleni napo kuna kitu nimeona hizi siku mbili"

Haji alikaa kitako tayari kwa kusikiliza .

"Kuna wanafunzi wengi huletwa na magari kila siku na kufuatwa, ila kuna mwanafunzi mmoja huletwa na gari la kifahari na mbali ya ufahari huo ila pia huletwa akiwa ameongozana na walinzi watatu wakiwa na silaha na hukaa pale hadi wakati wa kuondoka huondoka nae" Alisema Zedi.

Haji alipiga kimya.

"Kuna namna hapa, kwanini ulinzi? Na vipi ulifanikiwa kujua anakoishi?" Alihoji Haji.

"Yah! Nilifuatilia hadi gari lao lilipoingia kwenye mtaa wa Ibiru kando ya ubalozi wa China na kuingia kwenye nyumba kubwa na ya kisasa na bada ya hapo sijapata kuona mtu akitoka wala kuingia ndani ya jumba lile" Alisema Zedi.

Haji alitikisa kichwa.

"Honda yupo sahihi na taarifa zake" Alisema Haji huku akiparaza kwenye kompyuta.

"Inabidi tumtumie Imamu Shafi'I kumfikia Mohamed Farrah Aidid." Alisema Zedi.

"Tunamfikiaje sasa, mana wanaoekana wapo makini sana watu hawa" Aliuliza Haji.

"Wapo makini ila hawakosi kuwa na kosa litakalotufikisha kwao" Alisema Zedi huku akionekana kuzama mawazoni kutafuta ufumbuzi.

"Nadhani nirudi tena kujua zile gari zinazokuja ahsubuhi msikitini zinaelekea wapi na baada ya hapo tutajua cha kufanya kamanda" Alisema Haji.

Zedi alitikisa kichwa kukubaliana nae.

"Kwani mchana haziambatani pamoja?" Alihoji Zedi..

"Hapana,Mchana huonekana Imamu peke yake, labda tujaribu jioni" Alisema Haji huku akijilaza kitandani.

**

Jioni ilifika na Haji kama kawaida alikuwa ni miongoni mwa waumini wa msikiti wa Masjid nuur.

Alikuwa amevaa kanzu yake safi na balagashia safi.

Aliingia akiwa amechelewa dakika chache tu tangu wengine walipoanza ibada.

Kama kawaida alijiweka nyuma ya wengine na kuanza kusujudu kisha akawa anazungusha macho yake kila pande kwa umakini sana na kuna kitu alikiona nyuma ya mgongo wa Imamu Shafi'I ambae alikuwa anaongoza ibada.

Aliona pazia likitikisika na kuna mtu alichungulia kupitia tundu ilikopita waya ya maiki.

Aliona mawazo yake yalikuwa sahihi kuwaza kuwa kuna mtu huwa anakaa nyuma ya mimbari wakati wa Ibada.

Kwanini?

Hakika hakujua sababu za mtu yule kufanya vile.

Ibada iliisha ilifuata hotuba nayo iliisha na waumini waaanza kutoka na kila mmoja kuelekea zake.

Haji alirejea kwenye gari yake na kuanza safari kisha hakufika mbali alisimamisha na kuelekea dukani na kununua vocha kisha akajichelewesha pale kwa kujifanya anakwangua na kuweka.

Punde magari mawili yalipita kwa mwendo wa wastani tu.

Lilikuwa ni gari la Imamu na lile la mwanamke mvaa hijabu.

Akaacha tofauti ya dakika tatu na kuingia ndani ya gari lake na kisha kuendelea na safari yake.

Haikumchukua muda murefu akawa nyuma ya magari yale mawili huku akiacha magari matatu yawe mbele yake ili kutokuwastua walioko gari la mbele ambazo anazifuata.

Waliifuata barabara ya corso Somalia kisha wakakunja na kuelekea kwenye makutano ya mnara wa askari, na hapo ndipo magari yaliokuwa mbele ya gari la Haji yalitawanyika kila gari kuchukua uelekeo wake na wao wakazidi kuelekea ulipo mtaa wa Ibaru.

Mwendo ulikuwa wa taratibu na hapo ndipo Haji alijistukia akaamua kuyapita magari yale na kunyoosha hadi barabara ya kwenda ubalozi wa China kisha akasimama.

Hazikuzidi dakika saba magari yale nayo yakatokea na kuelekea kwenye nyumba za jirani na ubalozi.

Haji nae akajipitisha pale na kuona gari la Imamu likiingia huku lile lingine likiwa limesimama tu bila kuonesha dalili za kuingia.

Gari lile liliokuwa linaendeshwa na mwanamke yule alievaa hijabu likaondoka.

Haji akalifuata.


Safari ilikuwa ndefu kidogo na halikuonekana kufika karibuni.

Na gafla gari lile likakunja kwa kasi na kuelekea mtaa watu masikini, mtaa mpweke wa Kanisaab.

Haji alijua ule ni mtego tu na ili kuukwepa akaendelea kwenda taratibu na alipoufikia mtaa ule aliona majengo yakiwa na muonekano wa ajabu na kulionekana kuishi watu wa hali duni sana.

Kila alipokuwa akisonga, mwili wake ulianza kukataa kumpa ushirikiano.

Akasimamisha gari na kutulia kidogo.

Mara akaona watu waliovaa hovyohovyo wakijitokeza barabarani.

Alipowatizama kwa makini aliona bunduki mikononi mwao na alipotupia macho kwenye majengo marefu aliona watu wakijitokeza na mawe mikononi mwao.

Alijua kaingia cha kike.

Akataka kugeuza mara gari yake ikapatwa na dhoruba ya kunyanyuliwa kidogo na kubwagwa chini.
Ilikuwa imekoswa na bomu la RPG
.

Bahati ikawa kwake, akafanikiwa kuigeuza gari ila mawe yakaanza kushuswa kama mvua na risasi zikaanza kumwandama akakoleza moto wa gari ila mbele yake pia kulikuwa kuna kundi kubwa la watu wenye silaha.

Jasho likamtoka Haji.
 
RIWAYA; URITHI WA GAIDI

NA; BAHATI MWAMBA

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU



***

Haji Makame aliona akizubaa umauti utamkuta, hivyo kwa kujitoa aliamua kuendesha gari katikati ya umati wa watu wale ambao walikuwa tayari kuiwinda roho yake kwa udi na uvumba.

Risasi zilidi kurindima kwa fujo.

Hakujali!

Aliongeza kasi ya gari lake ambalo bado lilikuwa linapatwa na risasi huku akikoswa na mabomu ya hapa na pale.

Hakuna anaependa kifo jama!!

Baada ya wale watu kuwa wameziba njia, walishangaa ujasiri wa mtu wao kuendelea kuendesha bila kuogopa milio ya risasi.

Ilikuwa ni patashika kwenye mitaa ile.

Watu wale waliona wakiendelea kukaa barabarani si ajabu watagongwa na lile gari ambalo licha ya kudhurika pakubwa bado liliweza kuendelea na Safari na sasa ilikuwa inawalenga wao.

Walijikuta wanahama barabara bila kupenda.

Na Haji alipita kwa kasi ya kimbunga huku bado mawe na risasi vikizidi kumuandama.

Bahati ilikuwa kwa Haji na hatimae alifanikiwa kutoka kwenye mitaa ile, ila nyuma alisikia magari yakija kwa kasi.

Hakutaka wajue anakoelekea.
Haraka alishuka ndani ya gari na kutoa bastola yake kisha akalenga upande wa hifadhi ya mafuta na kuachia risasi kisha hakasubiri,akatimua mbio na kuacha gari lake likiteketea kwa moto.

Alitokomea vichochoroni na kurejea kwenye makazi yao.

**

"Pole sana kamanda" Alisema Zedi huku akijitahidi kumsafisha majeraha alioyapata.


"Dah! yule mwanamke ni hatari sana aisee,yani mitaa yote ile wamejaa vibaraka wake" Alisema Haji.

"Na hapo ndipo inabidi tupitie kuufikia ukweli" Alisema zedi huku akiinuka na kuelekea kwenye droo kutoa dawa zaidi.

"Ok tumeshajua tatizo yule mtoto na Imamu wanaishia nyumba moja kifuatacho sasa!" Alisema Haji.

"Nadhani kuna haja ya kuingia ndani ya nyumba ile" Alisema Zedi.

"Inawezekana vipi kuingia wakati inaonekana inalindwa sana" Haji alionesha mashaka yake.

"Itabidi tumpe ugonjwa yule binti" Alisema Zedi kifupi huku akifungua kibegi chake na kutoka na kichupa kidogo na kukitikisa.


"Hiyo nini Komredi," Aliuliza Haji.


"Hiki ni kirusi Maria na tulikitengeneza Pakistani kwa kazi kama hii" Alisema Zedi huku akitoa huyu kichupa kingine chenye ukubwa kama ule ule wa kichupa cha kwanza.


"Hii ni tiba yake" Alisema Zedi.

"kinafanyaje kazi sasa" Aliuliza Haji.

"Hii kitu akiambukizwa, anakuwa na tatizo la kustukastuka kila mara na mwilini hukosa nguvu" Alisema Zedi.

Haji aliguna.

"Usiwe na shaka, hakuna daktari atakaeweza kuponyesha hii kitu zaidi ya hii dawa" Alisema Zedi.


"Ok!! Mpango ukoje sasa" Aliuliza Haji.

"Inabidi tutege barabarani na kisha, tutengeneze ajali bandia ili kuwavuta wale walinzi na baada ya hapo tutajua cha kufanya mana inatakiwa ivutwe hewa yake ili iweze kufanya kazi" Alisema Zedi.

Haji alitikisa kichwa kwa kukubaliana na mpango huo.

Mara ujumbe wa kengele ya tahadhari ulilia kutokea kwenye kompyuta iliounganishwa na Honda kwa mawasiliano ya dharura.

Haji aliruka kwa kasi na kuifikia huku akimsikia Zedi akiguna kwa fadhaa.


"He's in trouble" Alisema Haji huku akiwa ameshindwa kuelewa afanye nini ili kuondoa hali iliomkumba gafla.

Zedi alibaki akizunguka asijue la kufanya.

"Imekuwa haraka sana aisee" Alilalama Zedi.

Haji aliishia kushusha pumzi tu.

****

Honda alikuwa amebebwa kwenye gari akiwa chini ya ulinzi mkali wa wapiganaji wa AIAI.

Kwa mtazamo tu alijua kutakuwa kuna tatizo limejitokeza.

Akaamua kuwa na subira huku mawazo lukuki yakipita kichwani mwake.

Woga nao haukuwa mbali.

Safari yao ilikuwa ni ya kimya kimya hadi waliporejea tena kwenye lile jumba kubwa lililokuwa Sadan.

Aliamriwa kushushwa na kuingizwa ndani ya nyumba ile kisha wakamfungia kwenye chumba chenye giza.

Honda alishindwa kuelewa ni kitu gani kilikuwa kinaendelea.

Akiwa bado anawaza hili na lile mara mlango ulifunguliwa na alirejeshwa tena sebuleni na mara hii alikutana na wapiganaji wengine tofauti na waliokuwa wamemleta pale.

Hawa walikuwa ni wapiganaji ambao kwa mtazamo tu alijua inaweza kuwa ni makomando waliofuzu hatua zote kwa jinsi walivyokuwa wanaonekana.

Walikuwa sita jumla yao.

Bila maelezo walimuomba aongozane nao kuelekea nje ambako walipanda gari lingine na kuelekea katikati ya mji.
.

Walipofika Old Mogadishu walisimamisha gari na kumfunga kitambaa usoni na kisha safari ikaendelea hadi walipoingia ndani ya geti la nyumba ambayo hakufahamu ukubwa wake.


Mawazoni mwake alijua labda walistukia nyendo zake wakati anaenda kutoa taarifa ya kuhusu njama za mauaji ya Rais wa Kenya ambayo yalivurugwa dakika za mwisho.

Alijua hawezi kupona kwa kuwa msaliti huwa haponi Zaidi ya kuchinjwa.

Mwili ulimzizima.

Alihofia kwa kuwa suala lile tayari ilikuwa limeshaleta mzozo baina yao, na tayari kikosi chao cha upepelezi kilikuwa kimeshaingia mjini kujua kilitokea nini hadi jaribio lao lilishindwa dakika za mwishoni.

Honda aligwaya ila alijipa ujasiri bandia.

Aliketishwa kwenye kiti kisha akavuliwa kitambaa usoni na hakuwa peke yake pale alipokalishwa.

Mbele yake kulikuwa kuna kijana mmoja mwenye asili ya watu wa Saudia na mzee ambae alikuwa na asili ya kisomali.


Mzee yule alimtambua.

Na ndie alikuwa lengo la operesheni yao.

Huyu ndie alikuwa FLAMINGO kwa lugha yao ya kazi ile.

Alikuwa ni Mohamed Farrah Aidid kiongozi wa kikundi cha Al-Islamiya.

Alitetemeka ndani ya mwili wake bila kuonekana nje.

Wapiganaji waliomleta waliopewa ishara fulani na ndani ya dakika moja alishangaa akiwa amepigwa pingu mikononi na miguuni kwa kasi ya ajabu.

Wapiganaji wale walikuwa si mchezo.


Kijana yule wa kisaudia alitoa picha mbili.

Moja akamuonesha Honda.


Honda alitamani kuona akiota na akiamka aambiwe ni masihara tu yale.

Ila haikuwezekana.

Alikuwa amepewa picha ya Haji Makame.

Picha ile iliambatanishwa na kipande cha gazeti, kilichokuwa na picha tatu, picha yake akitambuliwa kama Ahmed Twalib na picha nyingine ikiwa ni ya Zedi akitambulishwa kama ni Aahmed Boka Ghailan na nyingine ikiwa ni ya Haji ambae haikuwa na maelezo mengi zaidi ya kumhusisha na kutoroka kwa Ahmed gerezani.


"Ahmed; mtu huyu yupo hapa Mogadishu na kama walivyondika wamarekani ndivyo yupo hapa kukutafuta" Alisema Mohamed Farrah.

Honda alitikisa kichwa kukataa.

"Huyu jamaa simfahamu kabisa" Alijitetea Honda.

Mohamed alicheka kisha akampa ishara tena yule kijana wa kisaudia na kijana yule akatoa picha nyingine mbili na kumpa Honda.

Honda alizidi kuchanganyikiwa zaidi.

Picha moja ilikuwa ni ya kwake akiwa na mavazi ya kijeshi na picha nyingine ilikuwa ni ya Haji akiwa na mavazi ya kipolisi huku cheo chake kikijionesha mabegani.


"Hizi ni taarifa kutoka kwenu Tanzania; na mara ya mwisho ulikuwa kazini mwaka juzi ila sisi Ahmed tunaemtafuta alitoweka tangu mwaka 1998 baada ya shambulio la ubalozi wa marekani jijini Nairobi." Alisema tena Mohamed Farrah.

Ebana ee!

Kitumbua kimeingia mchanga mapema.


"Ila umekuwa ukitumika kutuhujumu, na hata mauaji ya Osama inasadikika ulitengenezwa tena na ulifanikiwa kumhujumu Osama hadi mauti yake" Aliendelea Kuongea Mohamed Farrah Aidid.


Kitu kimoja alichogundua Honda ni kuwa watu wale licha ya kuzipata taarifa zake ila hawakuwa wakimjua Ahmed halisi na hilo likampa afueni kidogo japo hakujua hatima yake.
.

Honda alikana kuzijua picha zile na akasingizia ya kuwa labda zimechongeshwa tu ila si yeye.

Watu wote waliangua kicheko cha dhihaka mule ndani.

"Ok! Mengine tutaongea badae, ila kwa sasa tunahitaji jambo moja tu" Mohamed Farrah alisema na kuweka kituo na kumtazama Honda.


Mlinzi mmoja akaweka kitabu kikubwa chenye ukubwa kama msahafu kwenye meza karibu na Honda.

Honda akaoneshwa ishara ya kukifunua, nae akafunua.

Alikutana na maandishi ya kiarabu.

Lugha ile aliilewa!..

Kwa haraka alijua kile ni kitabu cha wosia kilichokuwa na mambo mengi ikiwemo Fatwa'a nyingi kuhusu maonyo Osama kwa wamarekani na namna ya kupambana na wabaguzi wa nchi za kiarabu.

Kifunikwa kitabu na kuondolewa.

"Kitabu hiki kimeondolewa kurasa sita za katikati na ndizo kurasa muhimu katika kitabu hiki, na inasemekana ulihusika katika kuzinyofoa kurasa zile" Alisema Mohamed Farrah.

Ebana eeh lilikuwa ni jambo jipya kwa Honda.

Hakujua kabisa kitabu kile na kurasa hizo zinazoongelewa.

Akabaki njia panda na mateso yalinukia.
 

Pitieni hapa,hakika hutajutia muda wako
 
Back
Top Bottom