I DIED TO SAVE MY PRESDENT
Sehemu 19
Nitakwenda nyumbani kwa
Pascal na kuitafuta hiyo pochi
mahala alipoificha Eliza na
nikiipata nitajua kilichomo ndani
yake”
“ Elvis !!...pauline akastuka
“ Please don’t do that.Leave
this matter as it is,Huyu Pascal
huwezi kujua ni kwa nini alitaka
kumuua Elizabeth kwa sababu tu
ya pochi.Naomba usijihusishe na
suala hili hata kidogo.Huyu
msichana tutamrejesha kwao
Iringa.” Akasema Patricia kwa
uoga
“ Usihofu kitu Patricia,nataka
tu kufahamu kilichomo ndani ya
hiyo pochi na baada ya hapo
sintakuwa na tatizo tena na Pascal
” akasema Elvis
“ Sawa Elvis lakini mimi moyo
wangu hauafiki kabisa suala hili lakinikwa kuwa umenihakikishia
kwamba hakutakuwa na tatizo
lolote basi nakuruhusu ufanye
hivyo unavyotaka k ufanya”
“ Ahsante kwa kukubaliana
nami.Lengo langu ni kutaka tu
kufahamu kwa nini Pascal alitaka
kumuua Elizabeth kwa sababu tu
ya pochi? Kuna kitu gani
kikubwa ndani ya hioyo pochi?
“ Utafanya nini ukigundua
kwambandaoi ya hiyo pochi kuna
jambo kubwa? Akauliza Patricia
“ Naomba nisikujibu kwa sasa
mke wangu hadi hapo
nitakapokuwa nimeipata hiyo
pochi na kujua kilichomo ndani
yake.” Kazi zetu sisi huwa
zimetawaliwa na usiri
mkubwa.Tunatembea na siri
nyingi za taifa kwa hiyoyawezekana katika pochi hiyo
kuna siri kubwa”
“ Umepanga kwenda lini
huko kwa Pascal?
“ Tonight.Ninapafahamu
nyumbani kwake,nimewahi
kwenda sikumoja na mkurugenzi
wangu wa zamani.Ninachohitaji ni
huyu msichana anielekeze mahala
alikoificha hiyo pochi ili
nikaichukue” akasema Elvis
*******************
Saa mbili na nusu za usiku
,Elvis akasimamisha gari nje ya
Akwinabe Bar halafu akashuka na
kuingia ndani ya baa ile maarufu
hasa kutokana na idadi kubwa ya
wasichana wanaouza miili
yao.Alikwenda kaunta akanunua
chupa kubwa ya maji ya kunywa halafu akatoka.Watu walikuwa
wengi kama kawaida ya mahala
hapa.
Akiwa na chupa yake ya maji
mkononi Elvis akaangaza angaza
pande zote kama kuna mtu
anayemfuatilia halafu akaanza
kupiga hatua akaondoka na
kuishika barabara iliyokuwa
ikielekea ilipo nyumba ya
Pascal.Ni nyumba ya nne toka
Akwinabe bar. Kwa mujibu wa
maelekezo aliyopewa na Elizabeth
ni kwamba njia rahisi ya kuingia
ndani ni kwa kupitia mlango
mdogo ulio nyuma ya nyumba
ambao hufungwa saa tano za
usiku.Saa nne usiku mbwa
hufunguliwa na kutolewa n je
kujisadia na saa tano za usiku
huingizwa tena ndani na mlango
huo hufungwa Elvis akapita katika
uchochoro mdogo uliolitenganisha
jumba la Pascal na nyumba ya
jirani akazunguka hadi nyuma ya
nyumba hakukuwa na mtu yeyote
kule nyuma,akatoa glovu nyeusi
akavaa halafu akachukua na kitu
mfano wa soksi kubwa akaivaa
kichwa na kubakisha eneo la
macho tu kisha akaambaa ambaa
na ukuta hadi katika mlango ule
mdogo akajaribu kuusukuma
ukafunguka.Taratibu na kwa
tahadhari ya aiana yake akaingia
ndani bastora yake ilikuwa
mkononi tayari kukabiliana na
chochote ambacho
kingejitokeza.Hakukuwa na mtu
yeyote kule nyuma ya nyumba.Taa
za ndani zilikuwa zinawaka
kuashiria kwamba kuna watu
walikuwemo ndani Moja kwa moja akaelekea
katika mti alioelekezwa na
Elizabeth ambako ndiko alikoificha
ile pochi ya Pascal.Mwangaza
haukuwa mkali sana eneo hilo
kutokana na matawi ya miti na
hakuweza kuonekana kiurahisi
kutokana na mavazi meusi
aliyoyavaa.Akavua begi alilokuwa
amevaa mgongoni akatoa kitu
Fulani kigumu chenye ncha kali
na kuanza kuchimba.Wakati
akiendelea na zoezi lile la kufukua
,ghafla mlango ule mdogo
ukafunguliwa na kijana mmoja
akaingia na bila kuhisi kitu
chochote akaelekea moja kwa
moja ndani.Elvis aliyekuwa
amejibanza pembeni ya mti
akaendelea na zoezi lake la
kuchimba .Baada ya muda
akakutana na kitu kama mfuko wa nailoni na ndaniyake kulikuwa
na pochi.Kwa haraka haraka
akaiweka pochi ile katika begi
lake halafu akaishika bastora
yake akatazama usalama wa
eneo lile kisha akaondoka kwa
tahadhari kubwa.Akaufungua
mlango mdogo lakini kabla
hajatoka mlango wa kuingilia
ndani ukafunguliwa na kwa
haraka akajirusha nje.Mara
akasikia msichana akipiga kelele
akiwaita watu waliokuwemo ndani
akawafahamisha kwamba ameona
mtu akitpoka pale mlangoni .Elvis
akavua ile kofia aliyokuwa
ameivaa kichwani halafu akatoka
mbio hadi barabarani na kuelekea
moja kwa moja katika baa mahala
alikoacha gari lake akaingia garini
na kuondoka kwa kasi ******************
Saa tano na dakika tatu za usiku
Elvis akawasili nyumbani
kwake.Patricia mke wake ndiye
aliyemfungulia geti.
“ Thank you lord you are
back” akasema Patricia na
kumkumbatia mumewe.Elvis
akambusu mkewe na kumshika
mkono wakaingia sebuleni.
“ Nilikuwa na wasi wasi sana
na ndiyo maana nimeshindwa
hata kupata usingizi”akasema
Patricia
“ Samahani kwa kukuweka
roho juu mpenzi wangu lakini
hakukuwa na sababu yoyote ya
kuwa na wasi wasi.Ilikuwa ni kazi
ndogo sana”
“ Usiseme hivyo Elvis.Ilikuwa
kazi ndogo kwako lakini ya hatari kubwa kwangu.Kazi yako naiogopa
sana.Kila siku namuomba Mungu
watume malaika zake
wakutangulie kokote
uendako.Sitaki upatwe na tatizo
lolote .I love you so much Elvis,you
are my everything.” Akasema
Patrician na kukilaza kichwa
chake katika kifua cha
mumewe.Elvis akainama
akambusu na kusema
“ I love you too Patricia.I love
you so much ” wakakumbatiana
.Baada ya muda kidogo Patricia
akauliza
“ Umeipata pochi hiyo
uliyokwenda kuitafuta?
“ Ndiyo nimeipata” akasema
Elvis halafu akainuka na
kulifungua begi lake akatoa pochi
ndogo akaifungua.Ndani ya pochi ile kulikuwa na kila kitu
alichokisema Elizabeth
“Kila kitu ni kama
alichokisema Elizabeth. Hizi fedha
sina haja nazo,tutampatia
Elizabeth zitamsaidia katika
matatizo yake.Vitu ambavyo
vilipelekea Pascal afikie maamuzi
ya kumuua Elizabeth ni hivi viwili
tu .Hii flash disc na h ii memory
card.” Akasema Elvis
“ Kuna nini ndani yake
mpaka afikie hatua ya kutaka
kuutoa uhai wa mtu kwa ajili ya
vitu hivi?” akauliza Patricia
“ I don’t know yet.I’ll find out”
akasema Elvis
“ Elizabeth anaendeleaje?
“ Anaendelea
vizuri.Ninaendelea kumpa
dawa.Hali yake inazidi kuboreka” Good.Hali yake ikisha
boreka itabidi tumsafirishe
kumrejesha kwao Iringa akaanze
maisha mapya.Hapa mjini
hatakiwi kuonekana kabisa.Ni
hatari kubwa kwake”
“ Hilo ni wazo la msingi
sana.Tutampatia mtaji wa
biashara akaanze maisha yake
huko kijijini.Hatupaswi kuendelea
kumuweka hapa kwa muda
mrefu” Elvis akamshika mkono
mkewe wakaelekea
chumbani.Elvis akamtazama
mkewe kwa makini bila
kumsemesha.
“ Vipi mbona unanitazama
hivyo Elvis?akauliza Patricia.Elvis
akamsogelea akambusu na
kusema
“ You are blessed my love.You
are so beautifull than all women in this world.I want to remind you
again of how much I love you and
how important you are in my life”
akasema Elvis
Patricia akamkumbatia kwa
nguvu kisha wakaanza kupeana
mabusu mazito na haukupita
muda wakahamia katika
ulimwengu wa huba
*************************
Saa sita za usiku Pascal
alirejea nyumbani kwake kama
kawaida yake.Mida hii ndiyo huwa
anarejea nyumbani kila siku.
Arejeapo nyumbani usiku huu
familia yote huwa imelala na hivyo
hufungua geti kwa kutumia
remote control.Aliingiza gari katika
gereji halafu akaingia sebuleni na
kushangaa kuwakuta Salvatory mdogo wake pamoja na mtumisi
wa ndani wakiwa sebuleni jambo
ambalo halikuwa la kawaida.
“Bado hamjalala mpaka mida
hii? Akauliza Pascal
“ Kaka tumeogopa kulala
kuna shida kidogo imetokea”
“ Shida gani imetokea?
“ Prisca anasema kwamba
alimuona mtu akiwa na mavazi
meusi akitoka ndani kwa kupitia
mlango wa nyuma”
“ Mtu ? !!..Pascal akashangaa
“ Ndiyo kaka” akajibu Prisca
mtumishi wa ndani
“ Ulimuona mtu huyo
alikuaje?
“ sikumuona usoni.Nilimuona
kwa nyuma wakati
akitoka.Alikuwa amevaa mavazi
meusi pamoja na begi mgongoni” Mmejaribu kuangalia kama
kuna sehemu yoyote kumevunjwa
au kuna kitu chochote kimeibiwa?
“ Tumeangalia lakini hakuna
sehemu yoyote iliyovunjwa au kitu
chochote kilichoibiwa.” Akasema
Salvatory.Pascal akafikiri kidogo
na kusema
“ Ok msiogope. Yawezekana
wakawa ni vibaka waliokuta
mlango uko wazi wakaingia ili
kutafuta cha kuiba
wakakosa.Msiache mlango wazi
tena ,muwe mkiufunga muda
wote” akasema Pasca na
kuzunguka nyumba yote
kuchunguza na kuhakikisha
hakuna sehemu iliyovunjwa
halafu akaingia katika chumba
chake ambacho hukitumia
kuhifadhia vitu vyake vya siri lazima atakuwa ni kibaka
aliyekuwa akitafuta nafasi ya
kuiba.Sina hakika kama ni mtu
aliyekuwa na nia yoyote mbaya na
mimi.Kama angekuwa ni mtu
mwenye kutafuta chochote toka
kwangu basi angeingia ndani.Hata
hivyo kuna ulazima wa kufunga
kamera za ulinzi hapa
nyumbani.Toka yule msichana
alipoipoteza ile pochi yangu yenye
vitu vyangu vya muhimu nimekosa
amani kabisa.Nashukuru niliwahi
kummaliza na nina hakika siku ile
ile hakutoka kabisa nje ya
nyumba hii kwa hiyo kama kuna
mtu alimtuma basi hakupata
nafasi ya kuonana naye
tena.Lakini sina hakika sana
kama kuna mtu yeyote anayeweza
kumtumia msichana kama yule
kuniibia vitu vyangu,najua shida yake ilikuwa ni fedha tu na vitu
vingine vyote akavitupa.Kama
angenieleza ukweli ningemsamehe
lakini aligoma kuwa mkweli na
kunilazimisha nimkate pumzi”
Akawaza Pascal
********************
Kumepambazuka siku ya
jumatatu,wiki mpya imeanza.Saa
kumi na mbili za asubuhi Elvis na
Patricia waliamka na kuelekea
katika chumba cha mazoezi na
kufanya mazoezi mepesi ya
viuongo .Kisha maliza maozezi
wakaingia bafuni wakaoga na
kujiandaa kwa ajili ya kuelekea
makazini.Kabla ya kutoka
wakapata kwanza kifungua
kinywa My love,sintoungana nawe
mchana wa leo kwa chakula
.Nitakuwa na kazi nyingi leo
kutokana na ujio wa rais wa
Marekani hapo kesho.Ugeni huu
ni mkubwa na idara zote za
usalama wa nchi zinahusika
kikamilifu” akasema Elvis wakiwa
mezani wakipata kifungua kinywa
“ Usihofu darling.I’ll miss you
a lot today”akasema Patricia
“I’ll miss you too my
angel.Kama kutakuwa na tatizo
lolote hospitali kuhusiana na
Elizabeth nitaarifu mara moja ili
tujue namna ya kufanya”
“ Usihofu Elvis.Sina hakika
kama kutakuwa na tatizo lolote.No
body cares for her.Kwa muda wote
aliokuwa hospitali hana fahamu
hakuna hata mtu mmoja
aliyejitokeza kumtafuta .Kila mtu pale hospitali anafahamu kwamba
ana matatizo ya akili kwa hiyo
hakuna anayejali kupotea
kwake.Kama kutakuwa na tatizo
lolote basi nitalimaliza mwenyewe
huko huko.” Akasema
Patricia.Baada ya kumaliza kupata
kifungua kinywa kila mmoja
akaingia katika gari lake na
kuondoka kuelekea kazini
Saa mbili kasorobo Elvis
akawasili ofisini na moja kwa moja
akaiwasha kompyuta yake.Kabla
hajaanza kufanya kazi yoyote
akatokea Sabina mmoja kati ya
wafanyakazi wapya wa idara
hii.Sabina alikuwa ni mtaalamu
wa kutegemewa wa masuala ya
kompyuta
“ Hello handsome” akasema
Sabina.Elvis akageuka huku
akitabasamu na kusema Hello queen of Africa”
Akasema Elvis huku akicheka
.Yeye na Sabina ni watu
waliozoeana sana na mara nyingi
wamekuwa wakitaniana.
“ How was your weekend?
Utanisamehe Elvis nilishindwa
kabisa kufika katika birthday
party ya mkeo,niliitwa mara moja
Morogoro anakosoma mdogo
wangu.Sherehe ilikwendaje?
“ Ilikuwa nzuri sana.We had
fun.Watu wengi
walihudhuria,tukala na
kunywa.Kwa ujumla ilikuwa nzuri”
akajibu Elvis
“ Nafurahi kusikia hivyo .Its
timefor work Elvis.Tal k to you
later “akasema Sabina na
kuelekea katika meza yake.
“Now its time to find the
truth. “ akawaza Elvis halafu akaichukua ile flash disc
akaichomeka katika kompyuta
yake na kuifungua.Kulikuwa na
mafaili matatu ndani yake
.Akafungua faili la kwanza na la
pili na la tatu yakamstua sana
.Zilikuwa ni nyaraka za kijeshi
zilizohusiana na silaha mbali
mbali za kivita.Kulikuwa na picha
mbali mbali za silaha nzito za
kivita na maelezo yake.Kulikuwa
na ndege vita tatu,vifaru tisa vya
kisasa ,na aina mbali mbali za
bunduki zenye nguvu na
mabomu.Mwanzoni mwa kila faili
kulikuwa jina la Pascal kwa
kalamu..
“Nyaraka za jeshi.Pascal
anahuska vipi na nyaraka hizi
nyeti za jeshi? Ninavyofahamu
mimi mambo ya silaha hasa silaha
nzito na kivita kama hizi huwa ni mambo ya siri ya kijeshi.Kwa nini
basi Pascal ambaye si mwanajeshi
awe na nyaraka kama hizi? Kuna
kitu anakichunguza ndani ya
jeshi? Hapana sina hakika kama
kuna kitu anachokifanyia
uchunguzi ndani ya
jeshi.Ninavyofahamu mimi kama
kuna tatizo lolote ndaniya jeshi
basi wana taratibu zao za kufanya
uchunguzi na si kwa kuwatumia
watu wasio wanajeshi kama Pascal
.Kama ni hivyo , Pascal amezipata
wapi nyaraka nyeti kama hizi za
kijeshi? akawaza Elvis
“ Sasa ninaanza kupata picha
ni kwa nini Pascalalitaka kumuua
Elizabeth kwa kuificha pochi
yake.Hakutaka nyaraka hizi
zionekane kwa watu wengine.Kwa
ninialiogopa? Ngoja kwanza
nifahamu Pascal ana daraja gani katika idara yake hadi kuwa na
nyaraka nyeti kama hizi ambazo
wahusika wake ni viongozi wakuu
wa nchi na wa jeshi ” Akawaza
Elvis na kuzitafuta namba Fulani
akapiga
“ Hallow Elvis” Habari za
siku?ikajibu sauti ya mwanadada
upande wa pili
“ Nzuri Imelda,unaendeleaje?
Umepotea sana siku hizi”akasema
Elvis
“ Nipo Elvis wewe tu ndiye
umepotea kabisa hata simu siku
hizi hutaki kunipigia”
“ Ni kweli Imelda sijawasiliana
nawe kwa kipindi kirefu kidogo
lakini ni kutokana na kubanwa
sana na kazi”
“ sawa Elvis,unahitaji nini leo
? Kwa sababu ukinipigia simu ni
lazima utakuwa na shida na unahitaji msaada.” Akasema
Imelda halafu wote wakacheka
“ Mbona unacheka Elvis? Ni
kweli hayo ninayoyasema? Huwa
hunikumbuki hadi upatwe na
tatizo”
“ Kweli Imelda nina shida
kidogo naomba unisaidie”
“ Una tatizo gani?
“ Imelda nahitaji kufahamu
Pascal Situmwa ana daraja gani
katika idara yenu ya usalama wa
taifa?
“ Daraja la PascalSitumwa?
Imelda akauliza
“ Ndiyo .Nahitaji kufahamu
daraja lake ndani ya idara yenu”
akasema Elvis
“ Elvis siwezi kujua kwa sasa
Pascal ni daraja gani hadi niingie
katika kompyuta ya mkurugenZi kwani haya huwa ni mambo ya siri
“
“ Ok do it for me Imelda”
akaomba Elvis
“ Ok naomba unipe dakika
tano nitakupigia” akasema Imelda
na kukata simu.Elvis akaendelea
kuziangalia silaha zile na baada ya
kama dakika nne Imelda akapiga
“ Elvis ,Pascal situmwa ni
mfanyakazi wa daraja la tatu yaani
daraja la kawaida sana na hana
cheo chochote ndani ya idara.”
“ Kama Pascal ni mtu wa
daraja la tatu na hana cheo
chochote ndani ya idara ya
usalama wa taifa,kwa ninibasi
awe na nyaraka nyeti kamahizi za
kijeshi? Akajiuliza Elvis
“ Elvis are you there ?
Akauliza Imelda baada ya kuona
kumekuwa kimya Nipo Imelda.Ahsante sana
kwa msaada wako lakini kuna
jambo lingine dogo nataka
unisaidie tena”
“ semaElvis ni jambo gani
unahitaji?
“ Naomba unisaidie namba ya
simu ya Pascal”
“ Elvis Pascal kafanya nini?
Kuna nini unataka kukifanya
kwake? Nakufahamu vizuri mpaka
umfanyie uchunguzi mtu lazima
kuna jambo” akauliza Imelda
“ usihofu kitu Imelda,hakuna
tatizo lolote.Kuna kitu kidogo
nilichohitaji kukifahamu
kuhusiana na Pascal”
Imelda akamtumia Elvis
namba za simu za pascal
“ Ninachotaka kukifahamu
mimi ,nyaraka hizi za kijeshi
zimefikaje mikononi mwa Pascal? Inaonekana nyaraka hizi zina
umuhimu mkubwa sana kwake na
ndiyo maana alikuwa tayari hata
kuutoa uhai wa mtu ili
kuhakikisha kwamba hazitui
katika mikono ya mtu
mwingine.Nahitaji kulifanyia
uchunguzi jambo hili.Nataka
kufahamu uhalali wa pascal kuwa
na nyaraka nyeti kama hizi.”
Akafikirikidogo halafu akainuka
na kuelekea katika ofisi ya Sabina
“ Sabina ninatoka kidogo
kuna mahala ninaelekea”
“Unaelekea wapi Elvis?
Mkurugenzi alisema kwamba
asubuhi ya leo tunatakiwa wote
katika kikao mumu cha kazi”
“ Please sweet baby,cover for
me.Ninakwenda sehemu Fulani
muhimu sana na sintakawia
kurudi ” akasema Elvis na kutoka akaingia garini .Kabla hajaondoka
akazitafuta namba za simu za
Doreen akampigia
“ hallo Elvis,habari za
asubuhi?” akasema Doreen baada
ya kupokea simu
“ habari nzuri sana
Doreen.Ukowapi mida hii?
“Niko ofisini .Kuna tatizo
lolote Elvis?
“ Ninahitaji kukuona
.Ninakuja huko ofisini kwako sasa
hivi”akasema Elvis na kumstua
sana Doreen
“ Kuna tatizo gani
Elvis?akauliza Doreen kwa wasi
wasi.Elvis akacheka kidogo na
kusema
“ Hakuna tatizo
Doreen.Nahitaji kukuona kuna
jambo nahitaji msaada wako”