the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,611
- 7,063
- Thread starter
-
- #81
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO..
SEHEMU YA KUMI NA TISA.
mama kayoza akaendelea,
"baba
yako aliponiona aliniangalia kisha
akawa kama anataka kusema kitu, ila
nguvu hakuwa nazo, akaishia
kukunyooshea kidole, kisha akakata
roho, Alafu wewe ukapoteza fahamu,
nilijisikia uchungu sana, nilianza
kulia kwa kwikwi pale mlangoni, nililia sana kiasi kwamba nikapoteza fahamu, nilizinduka nikaendelea kulia ila
cha kushangaza bibi yako
akuonyesha wasiwasi kabisa na wala hakutoa chozi la uchungu kuonesha kuwa amempoteza mwanae, badala
yake aliniambia kuwa yule mzimu wa
ukoo ameingia mwilini kwako wewe Kayoza
kwa ruhusa yake, yaani ruhusa ya bibi yako.
akaniambia kuwa kuanzia
hapo hakutakuwa tena na shida, na
kama shida itatokea ni kwa ajili ya
kukulinda wewe (Kayoza), na sharti
kubwa ambalo mzimu alitaka
uzingatie ni kwamba, usifanye
mapenzi mpaka uoe na pia ukae mbali na harufu ya damu ya aina yoyote na uepuke kuwa mtu wa hasira hasira. Shangazi yako hajawahi kumwambia hivyo?" Mama Kayoza akamuuliza mwanae,
"Uwa ananisisitizia sana hayo mambo na kiukweli niliyamudu sana, hakuwahi kuniambia sababu ya mimi kutofanya hivyo" Kayoza alimjibu mama yake,
"Kwanini hajakwambia?" Mama kayoza akamuuliza mwanae,
"Mimi sijui" Kayoza akajibu,
"Labda alikuwa na sababu zake" Mamá Kayoza aliongea huku akiinuka kitini,
"Sasa mbona tena unaondoka?" Kayoza alimuuliza mamá yake,
"Naenda jikoni kuangalia maharage, yasije yakaungua bure" Mamá kayoza aliongea huku akifuata uelekeo wa jikoni.
******************
Sajenti Minja alirudi mpaka nyumbani kwake na kupanga nguo zake katika mabegi kwa ajili ya kujiandaa na safari, kwa maana alishajua kuwa kesho kukikucha ni lazima aitwe ofisini ili akakabidhi vitu muhimu vya kiaskari.
Alipomaliza kupanga vizuri nguo zake, aliingia bafuni kuoga na kisha alipotoka tu alipotoka tu bafuni, akaona njia nzuri ya kupumzisha kichwa ni kulala. Akaingia chumbani kwake na kulala.
_____________________
SIKU ILIYOFUATA..
_____________________
Kama alivyotegemea kuwa ni lazima siku hii aitwe ofisini na ndivyo ilivyokuwa.
Sajenti Minja baada ya kuamka na kupata kifungua kinywa, alipokea simu kuhitajika kufika ofisini kutoka kwa mkuu wa kituo chake cha polisi.
Alijitayarisha haraka haraka na kuondoka mpaka kituoni na moja kwa moja akaenda kwenye ofisi ya mkuu wake,
"Kaa hapo" Mkuu wake alimwambia huku akimuoneshea kiti kilichopo pembeni. Sajenti Minja akakaa.
"Barua yako nimeipata na kuipokea asubuhi hii, nimeipitia na kwa upande wangu sina tatizo" Mkuu wake alimwambia huku akiwa anaandika andika vitu katika karatasi,
"Asante sana mkuu kwa kunielewa" Sajenti Minja aliongea huku akimshukuru Mungu kwa kuitikia maombi yake,
"Sasa cha muhimu ni kunikabidhi bastola uliyopewa na ofisi na namba zako za kazi na kitambulisho pia" Mkuu wake aliongea na kisha Sajenti Minja akavitoa vitu vyote alivyotakiwa akabidhi,
"Hivi hapa mkuu" Sajenti Minja aliongea huku akiviweka vile vitu juu ya meza,
"Mpaka hapa mimi na wewe tumemalizana" Mkuu aliongea huku akimuangalia Sajenti Minja,
"Nashukuru mkuu, kwa hiyo naweza kuondoka?" Sajenti Minja aliuliza,
"Kumbuka kuwa hapa ulikuja kufanya kazi tu, ila muajiri wako ni jeshi la wananchi, kwa hiyo ni lazima uende uko ndio watakupa majibu yao kama wamekubaliana na wewe au lah" Mkuu alimpa maelezo Sajenti Minja,
"Hakuna shida, nitaenda pia uko" Sajenti Minja aliongea huku akitabasamu,
"Wapo nje wanakusubiri" Mkuu aliongea na kumfanya Sajenti Minja ashtuke,
"Wananisubiri?" Sajenti Minja akauliza,
"Ndio" Mkuu aliongea huku akinyanyua mkonga wa simu na kubonyeza namba fulani, akawa anasubiri upande wa pili upokee simu,
"Mimi nimeshamalizana nae, nawasubiri nyinyi mkuu" Mkuu wa polisi aliongea kwenye simu na kisha akairudisha simu mezani,
"Sasa Kwanini wamenifuata?" Sajenti Minja aliuliza baada ya mkuu wake kukata simu,
"Mimi sijui, labda Ndio utaratibu wenu wanajeshi" Mkuu alijibu kabla hawajasikia mtu akigonga hodi,
"Pita ndani" Mkuu alijibu kisha wakaingia ndani wanajeshi wawili waliovaa gwanda zilizoandikwa MP begani, wakampigia saluti mkuu wa polisi,
"Nyoosha mikono mbele" MP mmoja aliongea huku akiitoa pingu na kuishika mkononi,
"Mambo gani tena ya kufungana pingu" Sajenti Minja aliongea huku akipingana na wale MP, alishangaa anapigwa makofi mengi sana yasiyokuwa na idadi,
"Minja acha ukorofi, sikiliza unachoambiwa na kumbuka ndani ya jeshi hakuna maombi, kuna amri tu" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja ambaye alionekana kukubaliana nae na akakubali kufungwa pingu na kisha wale MP wakatoka nae nje na kumuingiza ndani ya gari nyeusi iliyokuwa na namba ya jeshi.
Kisha ile gari iliondoka.
****************
Baada ya kutoka jikoni, mama Kayoza alirudi sebuleni na kwenda kwenye jokofu na kuchukua maziwa fresh na kujimiminia kwenye glass,
"Na sisi tunataka" Kayoza akamwambia mama yake,
"Mimi Ndio nimeongea sana, kwa hiyo ni muhimu kulainisha koo" Mama Kayoza aliongea huku akitabasamu,
"Sawa, endelea na story" Kayoza akamwambia mama yake,
Ngoja niendelee, Baada ya miaka
miwili tangu baba yako afariki,
nilitaka kuondoka ili niende sehemu
nyingine nikaanze kuishi maisha ya
kujitegemea, kipindi hicho ulikuwa
una umri wa miaka mitatu, Ilo wazo langu
lilipingwa na shangazi zako na baba
zako, mimi kuona hivyo nikawa naenda
sana kanisani kufanyiwa maombi,
kumbe yale maombezi yalikuwa
yanaleta madhara katika mzimu wao,
ila kwa kuwa mzimu ulishanipa
ahadi ya kutonidhuru ukawa
unavumilia tu, Siku moja wakati
nimelala na wewe usiku, nakumbuka
nilikuwa nasoma biblia, bila kutarajia nilikuona ukiinuka na
ukakaa kitandani, mimi nikajua labda
unataka kukojoa, nikakuvua nguo
kisha nikakushusha chini ukojoe
kwenye kopo, ila cha ajabu macho
yako yakawa meupe ya kung'aa na
meno yakakutoka yakawa marefu, mimi kuona hivyo nikahisi hatari nikataka kukimbia, ila ulinishika mkono na kunivuta na nikaangukia kitandani, hili nalo lilinishangaza, yaani mtoto wa miaka mitatu uwe na nguvu ya kunivuta na nikaanguka?
Baada ya mimi kuanguka, ukaniangalia kwa sekunde kadhaa
kisha ukasema kuwa umenivumilia
kwa muda mrefu sana, hapo ndio
nikagundua kuwa aliekua anaongea
ni mzimu na wala sio wewe, kwa sababu
ya muonekano wako, na maneno
ulivyokuwa unayatamka kwa ufasaha,
wakati katika hali yako ya kawaida
ulikuwa huwezi kutamka maneno
vizuri.
Nakumbuka uliniambia ikifika
kesho niondoke, maana nimeshindwa
kulipa fadhira, ulidai ulinipenda sana ila maombi ninayofanyiwa uko kanisani ninapoendaga uwa yanamfanya anakosa raha, kwa hiyo basi, hana sababu ya kuniadhibu kwa kuwa aliniahidi kuwa kamwe hawezi kuniadhibu, ila cha kufanya ni mimi kuondoka hiyo kesho asubuhi.
Kesho yake ilipofika,
nikamwambia bibi yako kilichotokea,
ikabidi awaite wanaukoo wote ambao walikuwa jirani na pale tunapoishi na kuwaelezea yote niliyoambiwa na mzimu.
wakakubaliana niondoke,
ila wewe nikuache, na kuhusu malezi
yako, atakaehusika nayo ni shangazi yako
mkubwa, ambae alikuwa anakaa
kigoma, nikakubali kwa roho safi, kwa
makubaliano ya kila baada ya miezi
miwili ningeenda kwa shangazi yako kukuangalia......
******ITAENDELEA******
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO..
SEHEMU YA KUMI NA TISA.
mama kayoza akaendelea,
"baba
yako aliponiona aliniangalia kisha
akawa kama anataka kusema kitu, ila
nguvu hakuwa nazo, akaishia
kukunyooshea kidole, kisha akakata
roho, Alafu wewe ukapoteza fahamu,
nilijisikia uchungu sana, nilianza
kulia kwa kwikwi pale mlangoni, nililia sana kiasi kwamba nikapoteza fahamu, nilizinduka nikaendelea kulia ila
cha kushangaza bibi yako
akuonyesha wasiwasi kabisa na wala hakutoa chozi la uchungu kuonesha kuwa amempoteza mwanae, badala
yake aliniambia kuwa yule mzimu wa
ukoo ameingia mwilini kwako wewe Kayoza
kwa ruhusa yake, yaani ruhusa ya bibi yako.
akaniambia kuwa kuanzia
hapo hakutakuwa tena na shida, na
kama shida itatokea ni kwa ajili ya
kukulinda wewe (Kayoza), na sharti
kubwa ambalo mzimu alitaka
uzingatie ni kwamba, usifanye
mapenzi mpaka uoe na pia ukae mbali na harufu ya damu ya aina yoyote na uepuke kuwa mtu wa hasira hasira. Shangazi yako hajawahi kumwambia hivyo?" Mama Kayoza akamuuliza mwanae,
"Uwa ananisisitizia sana hayo mambo na kiukweli niliyamudu sana, hakuwahi kuniambia sababu ya mimi kutofanya hivyo" Kayoza alimjibu mama yake,
"Kwanini hajakwambia?" Mama kayoza akamuuliza mwanae,
"Mimi sijui" Kayoza akajibu,
"Labda alikuwa na sababu zake" Mamá Kayoza aliongea huku akiinuka kitini,
"Sasa mbona tena unaondoka?" Kayoza alimuuliza mamá yake,
"Naenda jikoni kuangalia maharage, yasije yakaungua bure" Mamá kayoza aliongea huku akifuata uelekeo wa jikoni.
******************
Sajenti Minja alirudi mpaka nyumbani kwake na kupanga nguo zake katika mabegi kwa ajili ya kujiandaa na safari, kwa maana alishajua kuwa kesho kukikucha ni lazima aitwe ofisini ili akakabidhi vitu muhimu vya kiaskari.
Alipomaliza kupanga vizuri nguo zake, aliingia bafuni kuoga na kisha alipotoka tu alipotoka tu bafuni, akaona njia nzuri ya kupumzisha kichwa ni kulala. Akaingia chumbani kwake na kulala.
_____________________
SIKU ILIYOFUATA..
_____________________
Kama alivyotegemea kuwa ni lazima siku hii aitwe ofisini na ndivyo ilivyokuwa.
Sajenti Minja baada ya kuamka na kupata kifungua kinywa, alipokea simu kuhitajika kufika ofisini kutoka kwa mkuu wa kituo chake cha polisi.
Alijitayarisha haraka haraka na kuondoka mpaka kituoni na moja kwa moja akaenda kwenye ofisi ya mkuu wake,
"Kaa hapo" Mkuu wake alimwambia huku akimuoneshea kiti kilichopo pembeni. Sajenti Minja akakaa.
"Barua yako nimeipata na kuipokea asubuhi hii, nimeipitia na kwa upande wangu sina tatizo" Mkuu wake alimwambia huku akiwa anaandika andika vitu katika karatasi,
"Asante sana mkuu kwa kunielewa" Sajenti Minja aliongea huku akimshukuru Mungu kwa kuitikia maombi yake,
"Sasa cha muhimu ni kunikabidhi bastola uliyopewa na ofisi na namba zako za kazi na kitambulisho pia" Mkuu wake aliongea na kisha Sajenti Minja akavitoa vitu vyote alivyotakiwa akabidhi,
"Hivi hapa mkuu" Sajenti Minja aliongea huku akiviweka vile vitu juu ya meza,
"Mpaka hapa mimi na wewe tumemalizana" Mkuu aliongea huku akimuangalia Sajenti Minja,
"Nashukuru mkuu, kwa hiyo naweza kuondoka?" Sajenti Minja aliuliza,
"Kumbuka kuwa hapa ulikuja kufanya kazi tu, ila muajiri wako ni jeshi la wananchi, kwa hiyo ni lazima uende uko ndio watakupa majibu yao kama wamekubaliana na wewe au lah" Mkuu alimpa maelezo Sajenti Minja,
"Hakuna shida, nitaenda pia uko" Sajenti Minja aliongea huku akitabasamu,
"Wapo nje wanakusubiri" Mkuu aliongea na kumfanya Sajenti Minja ashtuke,
"Wananisubiri?" Sajenti Minja akauliza,
"Ndio" Mkuu aliongea huku akinyanyua mkonga wa simu na kubonyeza namba fulani, akawa anasubiri upande wa pili upokee simu,
"Mimi nimeshamalizana nae, nawasubiri nyinyi mkuu" Mkuu wa polisi aliongea kwenye simu na kisha akairudisha simu mezani,
"Sasa Kwanini wamenifuata?" Sajenti Minja aliuliza baada ya mkuu wake kukata simu,
"Mimi sijui, labda Ndio utaratibu wenu wanajeshi" Mkuu alijibu kabla hawajasikia mtu akigonga hodi,
"Pita ndani" Mkuu alijibu kisha wakaingia ndani wanajeshi wawili waliovaa gwanda zilizoandikwa MP begani, wakampigia saluti mkuu wa polisi,
"Nyoosha mikono mbele" MP mmoja aliongea huku akiitoa pingu na kuishika mkononi,
"Mambo gani tena ya kufungana pingu" Sajenti Minja aliongea huku akipingana na wale MP, alishangaa anapigwa makofi mengi sana yasiyokuwa na idadi,
"Minja acha ukorofi, sikiliza unachoambiwa na kumbuka ndani ya jeshi hakuna maombi, kuna amri tu" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja ambaye alionekana kukubaliana nae na akakubali kufungwa pingu na kisha wale MP wakatoka nae nje na kumuingiza ndani ya gari nyeusi iliyokuwa na namba ya jeshi.
Kisha ile gari iliondoka.
****************
Baada ya kutoka jikoni, mama Kayoza alirudi sebuleni na kwenda kwenye jokofu na kuchukua maziwa fresh na kujimiminia kwenye glass,
"Na sisi tunataka" Kayoza akamwambia mama yake,
"Mimi Ndio nimeongea sana, kwa hiyo ni muhimu kulainisha koo" Mama Kayoza aliongea huku akitabasamu,
"Sawa, endelea na story" Kayoza akamwambia mama yake,
Ngoja niendelee, Baada ya miaka
miwili tangu baba yako afariki,
nilitaka kuondoka ili niende sehemu
nyingine nikaanze kuishi maisha ya
kujitegemea, kipindi hicho ulikuwa
una umri wa miaka mitatu, Ilo wazo langu
lilipingwa na shangazi zako na baba
zako, mimi kuona hivyo nikawa naenda
sana kanisani kufanyiwa maombi,
kumbe yale maombezi yalikuwa
yanaleta madhara katika mzimu wao,
ila kwa kuwa mzimu ulishanipa
ahadi ya kutonidhuru ukawa
unavumilia tu, Siku moja wakati
nimelala na wewe usiku, nakumbuka
nilikuwa nasoma biblia, bila kutarajia nilikuona ukiinuka na
ukakaa kitandani, mimi nikajua labda
unataka kukojoa, nikakuvua nguo
kisha nikakushusha chini ukojoe
kwenye kopo, ila cha ajabu macho
yako yakawa meupe ya kung'aa na
meno yakakutoka yakawa marefu, mimi kuona hivyo nikahisi hatari nikataka kukimbia, ila ulinishika mkono na kunivuta na nikaangukia kitandani, hili nalo lilinishangaza, yaani mtoto wa miaka mitatu uwe na nguvu ya kunivuta na nikaanguka?
Baada ya mimi kuanguka, ukaniangalia kwa sekunde kadhaa
kisha ukasema kuwa umenivumilia
kwa muda mrefu sana, hapo ndio
nikagundua kuwa aliekua anaongea
ni mzimu na wala sio wewe, kwa sababu
ya muonekano wako, na maneno
ulivyokuwa unayatamka kwa ufasaha,
wakati katika hali yako ya kawaida
ulikuwa huwezi kutamka maneno
vizuri.
Nakumbuka uliniambia ikifika
kesho niondoke, maana nimeshindwa
kulipa fadhira, ulidai ulinipenda sana ila maombi ninayofanyiwa uko kanisani ninapoendaga uwa yanamfanya anakosa raha, kwa hiyo basi, hana sababu ya kuniadhibu kwa kuwa aliniahidi kuwa kamwe hawezi kuniadhibu, ila cha kufanya ni mimi kuondoka hiyo kesho asubuhi.
Kesho yake ilipofika,
nikamwambia bibi yako kilichotokea,
ikabidi awaite wanaukoo wote ambao walikuwa jirani na pale tunapoishi na kuwaelezea yote niliyoambiwa na mzimu.
wakakubaliana niondoke,
ila wewe nikuache, na kuhusu malezi
yako, atakaehusika nayo ni shangazi yako
mkubwa, ambae alikuwa anakaa
kigoma, nikakubali kwa roho safi, kwa
makubaliano ya kila baada ya miezi
miwili ningeenda kwa shangazi yako kukuangalia......
******ITAENDELEA******
the Legend☆