Marilyn Monroe
Member
- Apr 2, 2020
- 80
- 167
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 35
“Siku moja nilitembelewa na watu nisiowafahamu ofisini kwangu, ambao walinitaka nifanye mambo kama yale niliyokuwa nikikufanyia wewe kule kwenye ile nyumba kwa mashinikizo ya Wagga Maingo...ila wao walinitaka nimfanyie rais....”
“Whaaat?” Nilishitushwa na taarifa ile na kumgeukia yule Dokta kwa mshangao.
“Mmmnh! Ndivyo walivyonitaka na nadhani unaweza kukisia ni jinsi gani nivyoshituka juu ya ombi lao hilo. Niliwakatalia katakata na kutishia kuwaripoti serikalini.”
“Lakini...kwa nini walitaka kitu kama hicho...”
“Walitaka kunitumia kumtia rais wazimu...kisha asiwe tena na uwezo wa kuongoza nchi... wenyewe walidai kuwa hiyo ilikuwa ni njia pekee ya amani ya kumtoa rais madarakani bila kumwaga damu...( alicheka kwa dharau na kutikisa kichwa kwa masikitiko) Yaani lilikuwa ni jambo la kipumbavu nililowahi kulisikia maishani mwangu”
Eh...jamani! Haya mapya kuliko!
Pale jirani na kile chuo cha ubaharia kulikuwa na geti dogo ambalo lilitokea kwenye ngazi ndefu za mbao na chuma zilizokuwa zikiteremka pwani, eneo ambalo zamani ilikuwa inaegeshwa boti kubwa ya kwenda Zanzibar iliyoitwa MS SEPIDEH. Dokta Kashushu alijitambulisha kwa mlinzi wa pale getini ambaye alionekana kumtambua vizuri na kumuambia kuwa tulikuwa tunaelekea kwenye boti lake huko chini, na kwamba mkewe atafika muda mfupi ujao. Tuliteremka zile ngazi huku nikimuuliza kuwa alikuwa anamiliki boti. Aliafiki kwa kichwa bila kuonesha kujali juu ya swala lile.
“Baada ya wale watu ambao baadaye nilikuja kuelewa kuwa walikuwa ni wawakilishi wa kundi moja la upinzani lililokuwa likiendesha vita vya msituni dhini ya majeshi ya serikali kuona kuwa nimezidi kuwa mkaidi katika kutekeleza matakwa yao, walianza vitisho kuwa nikithubutu tu kutoa taarifa serikalini, wataiteketeza familia yangu yote! Nilikuwa kwenye wakati mgumu sana Tigga, na nilipoendelea na msimamo wangu, waliwateka mke na watoto wangu. Wakinishinikiza nimfanyie rais vile wao walivyotaka, kwani ni mimi pekee ndiye niliyeidhinisha dawa aina yoyote anayopewa rais iwapo atakuwa mgonjwa, na jambo ambalo ulimwengu haukulijua ni kwamba kwa wakati ule rais alikuwa akisumbulia na ugonjwa wa kisukari ambao ulimlazimu awe anameza vidonge maalum kila mara. Nilichotakiwa kufanya ni kumchanganyia dawa zangu za kumharibu akili pamoja na zile dawa za kisukari.”
“Dokta Kashushu haya mambo unayonieleza ni mazito sana! Inawezekana vipi mambo kama haya?” Nilimuuliza kwa msahangao. Yule Dokta alitikisa kichwa kwa masikitiko.
“Ninachokueleza Tigga ni kweli kimetokea. Hatimaye nilimweleza rais ukweli wa jambo lote, na kujiuzulu nafasi yangu ya utabibu wa rais. Rais alianzisha msako mkali wa kuwasaka mke na watoto wangu waliotekwa na wale watu ambao niliwajua kwa sura lakini sikuyajua majina yao. Kitendo hicho kiliwaudhi sana wale watu na siku moja baada ya kujiuzulu nafasi yangu, miili ya mke na watoto wangu ilikutwa kando ya msitu mmoja wakiwa wameuawa...” Aliniambia kwa huzuni nami nikahuzunika pamoja naye.
“Siku ile ile wale watu walinitumia wauaji nyumbani kwangu kuja kuniangamiza. Lakini jambo walilosahau ni kwamba mimi nilisomea shahada yangu ya udaktari huko Urusi, ambapo pamoja na shahada hiyo nilisomea pia mbinu za kijasusi na mapambano, kwani wakati huo urusi ndio ilikuwa inaendekeza zile siasa zake za ujamaa na ilikuwa ikisomesha waafrika wengi bure na kuwatumia katika propaganda zake za kijamaa. Niliwateketeza wale wauaji wawili na kuiacha nyumba yangu ikiteketea kwa moto, nami nikakimbia ile nchi Tigga. Nchi yangu niliyozaliwa na kukulia. Nilikuwa nimeficha pesa nyingi nje ya nchi, hivyo haikuwa taabu kwangu kutoroka nchini. Na kuanzia hapo nikawa mkimbizi Tigga. Huku nyuma nikasikia ndege iliyokuwa imembeba rais wetu na yule wa Rwanda ilianguka na kuwaua wote, lakini nilijua kuwa ni lile kundi lililokuwa likinitaka nimharibu akili rais ndilo lilihusika na kuanguka kwa ndege ile.” Dokta Kashushu alimalizia maelezo yake taratibu. Tuliingia kwenye ile boti yake ambayo kwa kweli ilikuwa kubwa na ghali sana. Aliniambia kuwa alikuwa ameiandaa ile boti kwa ajili ya tukio kama hili, ingawa huwa anakuja na mkewe mara kwa mara na kuiendesha hadi katikati ya bahari, siku nyingine wakiishi kwenye ile boti kwa siku mbili au tatu kabla ya kurudi tena nyumbani kwao Mbezi bichi.
Dokta Kashushu aliniambia kuwa alikimbilia Senegal. Baadaye alimtambua mmoja wa wale watu waliomfuta na kumshurutisha kumharibu akili rais akiwa miongoni mwa mawaziri wapya wa Rwanda, nchi ambayo ilikuwa ikishirikiana na waasi waliokuwa wakiipinga serikali ya Burundi. Kisha uchunguzi wa kifo cha rais wa Burundi na yule wa Rwanda ulianza, kwamba ile ndege haikuanguka kwa hitilafu za kawaida, bali huenda ikawa ilitunguliwa. Hapo wale watu wakaanza kumsaka tena ili kummaliza, kwani walijua ni yeye tu ndiye anayeweza kuwatambua wale watu waliomfuata na kumshurutisha kumharibu akili rais. Walimuibukia Senegal. Akafanikiwa kuwatoroka na kwenda Botswana. Huko nako akaondoka baada ya miaka miwili na miaka sita iliyopita akaingia Tanzania kwa pasipoti ya bandia aliyomtambulisha kuwa yeye ni Mtanzania aliyejulikana kwa Jina la Dokta Mohammed Kashushu. Hapa alianza maisha mapya na alioa mwanamke aliyekuwa yatima, kwani alijua kuwa wale watu bado walikuwa wakimsaka na hakupenda kabisa kujihusisha na mwanamke mwenye familia. Akiwa Tanzania, yule mtu aliyemtambua kuwa ni mmoja wa wale waliokwenda kumshurutisha kufanya mambo ya ajabu kwa marehemu rais wa Burundi, ambaye baadaye alikuwa miongoni mwa mawaziri wapya wa Rwanda baada ya mauaji ya halaiki, alionekana kwenye Televisheni akiwa ni mmoja kati ya watu waliokamatwa na kuletwa kwenye mahakama ya kimataifa dhidi ya mauaji ya halaiki ya Rwanda na Burundi iliyopo Arusha, Tanzania. Kufikia hapo alianza kuona mashaka juu ya usalama na amani yake nchini Tanzania, hivyo alimweleza ukweli mkewe mtanzania. Mkewe huyo aliamua kuwa pamoja naye popote atakapoenda, na ndio maana tukawa pale tukimsubiri mkewe ili atoroke naye.
Haya maelezo yalikuwa mapya sana kwangu na nikaanza kufikiria upya mkasa wote ule. Nilikumbuka kusoma habari za mahakama ya kimataifa dhidi ya mauaji ya halaiki ya Rwanda na Burundi. Nilikumbuka kusoma habari juu ya mtanzania kuteuliwa kuwa jaji wa mahakama hiyo...
“Lakini Dokta Kashushu, ilikuwaje ukapata nafasi ya kufanya kazi hapa nchini kwani vyeti vyako vya shule, hizo digrii zako, zilikuwa zinakuonesha wewe kama Dokta Kashushu? Kwani hilo ndilo jina ulilokuwa ukilitumia wakati unasoma?” Nilimuuliza.
“Hapana Tigga. Ukumbuke kuwa nilikuwa na pesa nyingi. Nilipata digrii zangu Urusi. Lakini pia nilitengeneza vyeti vya digrii hiyo hiyo kutoka vyuo vingine viwili vya nchi za magharibi, kimoja Finland na kingine kutoka chuo kidogo sana kisichojulikana kabisa kilichokuwa nchini Austria. Hiki cheti cha Austria kilinitambulisha kwa jina la Mohammed Kashushu kutoka Tanzania. Na hiki ndicho cheti ninachokitumia hapa Tanzania. Kwa hiyo ingawa fani niliyosomea ni ya kweli kabisa kama inavyoonekana kwenye cheti, jina lililo kwenye cheti na chuo ambacho kinaonekana kwenye cheti kuwa nimesomea si vya kweli. Chuo cha kweli nilichosomea kiko Urusi na katika cheti cha chuo kile kuna jina langu halisi, ambalo siwezi kukutajia kwa sababu ambazo nadhani unazielewa kufikia sasa.” Dokta Kashushu alinifafanulia. Haya mambo kwangu yalizidi kuwa mazito.
“Sasa ina maana kuwa wale watu waliokuwa wakikusakama tangu Burundi, Senegal na Botswana ndio hawa akina Wagga Maingo?” Nilimuuliza Dokta Kashushu kwa mshangao, huku nikianza kupata hofu kubwa juu ya huu mkasa mzima ulioniangukia.
“Hapana...huenda hawa wakawa na uhusiano na wale, lakini sio wale walionifuata kule Burundi. Kilichotokea hapa Tanzania, ambapo kama ulivyoelewa, nilikuwa nikiishi kwa amani sana, lakini kama Burundi, siku nne tu zilizopita yule mtu niliyekuja kumtambua kama Wagga Maingo aliniijia ofisini kwangu na kuniambia kuwa anajua kuwa mimi si mtanzania na ninaishi kwa hati bandia, na nimepewa nafasi nzuri sana katika nchi hii iliyoniwezesha kuishi kwa raha. Na akanitaka nimfanyie kazi yake, ambayo nikiifanya bila matatizo, wataendelea kunitunzia siri yangu na kuniacha niendelee kuishi kwa amani hapa nchini...kinyume na hapo, wao wangepiga simu idara ya uhamiaji na maisha yangu yangesambaratika.”
“Oh, Mungu wangu...!”
“Ndio Tigga. Nilikuwa na wakati mgumu. Na wakati huu umri wangu umesogea, sikuwa tena na uwezo wa kujiingiza kwenye mikiki-mikiki kama hapo mwanzo. Kwa hiyo sikuwa na la kufanya, nikakubaliana na sharti lao, ingawa sikuwa na uhakika kuwa huu ndio ungekuwa mwisho...nadhani sasa unaelewa ni kwa nini nililazimika kufanya vile Tigga, na nataraji utapata nafasi katika moyo wako kunisamehe kwa hili....” Dokta Kashushu alimalizia huku akinitazama kwa huzuni. Sikuwa na la kusema. Nilibaki nikiwa nimeduwaa.
“Kwa hiyo hujui hawa watu...akina Wagga Maingo walikuwa wanataka nini hasa?” Nilimuuliza.
“Hapana. Ila nakuhakikishia kuwa hawa watu ni wabaya sana. Sasa kama wana uhusiano na lile kundi lililofanya mambo ya kule Burundi miaka ile, basi nchi yenu sasa iko hatarini, na kwa kuwa wewe unaonekana kuwa na kitu wanachokitaka, nakushauri na wewe ukimbie mdogo wangu. Hapa hapakufai tena. Ukiwapa wanachokitaka, sina shaka kuwa wataiangamiza nchi yenu...wataitia kwenye balaa fulani tu! Hawa ni watu wanaopenda kuvuruga amani ndani ya nchi Tigga...kwa namna fulani ili wao wawe na maisha mazuri, ni wajibu kusiwe na amani.Kama kuna amani si mahala pao...ndio maana nakushauri kuwa ukimbie Tigga...ukipenda tunaweza kukuchukua pamoja nasi...nitakupatia pasipoti ya nchi yoyote uitakayo ukakae huko...”
“Hapana! Hapana Dokta Kashushu...mimi hapa ndio kwetu! Nina ndugu na jamaa zangu hapa, siwezi kuwaacha...” Nilimjibu kwa hamasa. Na hapo mkewe akafika. Walikumbatiana kwa upendo huku yule dada, ambaye alikuwa kijana zaidi ya Dokta Kashushu, akibubujikwa na machozi. Alimtazama mumewe kwa upendo na huruma, kisha macho yake yakaangukia kwenye pingu iliyokuwa ikining’inia kwenye mkono wake wa kushoto na kumuuliza kwa woga kulikoni.
“Ni hadithi ndefu...nitakuelezea baadaye...” Dokta Kashushu alimjibu. Mkewe akaanza kumchunguza ule mkono uliojeruhiwa kwa risasi lakini Dokta Kashushu alimtoa wasi wasi kuwa halikuwa tatizo kubwa. Yule dada alikuwa amehamanika vibaya sana. Walikuwa na mtoto wa kike aliyapata miaka minne ambaye naye alikuwa akilia kwa kumuona tu mama yake akilia. Dokta Kashushu alinitazama huku akiwa amemkumbatia mkewe.
“Sisi hatuna muda wa kupoteza Tigga...inatupasa tuanze safari mara moja. Una hakika hutaki kuambatana nasi?” Aliniuliza. Nillimtazama yule Dokta mtu mzima kwa muda huku nikimhurumia kwa mikasa iliyompata. Nilitamani kuwa pamoja naye, lakini akilini mwangu nilikuwa na mambo mengi niliyotaka kuyafanyia kazi nikiwa hapa hapa nchini. Nilitaka kujua sababu ya yule mtu kuuawa kule msituni, nilitaka kumjua ni nani yule mtu kigulu aliyekuwa na akina Wagga Maingo kule msituni, nilitaka kujua nini hatma ya yule dada askari aliyekuwa akishirikiana na akina Wagga Maingo...nilitaka kujua juu ya yule mwanamke mwenye hijab, aliyetuvurumishia risasi na ambaye nadhani ndiye aliyehusika na kifo cha Dick Bwasha...na hatma ya John Vata.Masikini John...iliniwia vigumu sana kuamini kuwa amefariki.
“Mimi nitabaki hapa hapa Dokta Kashushu...hata kama nitauawa, ni bora nifie nchini kwangu.” Nilimjibu taratibu. Yule Dokta alinitazama kwa muda, kisha akafungua begi alilokuja nalo mkewe na kutoa funguo zipatazo tatu zilizokuwa zimefungwa pamoja na kunikabidhi.
“Basi nakuomba uchukue hizi funguo za nyumba yangu nyingine Tigga. Hakuna mtu yeyote anayeijua nyumba hii, na nimeaindikisha kwa jina la huyu binti yangu.Unaweza ukahitaji maficho...nadhani huko kutakufaa kwani nina imani ukiwa kule hutagundulika kirahisi...na vitu vyote utakavyovikuta humo ni mali yako kuanzia leo...hiyo ni namna yangu ya kukusaidia katika mtihani huu Tigga...”
“Ah! Dokta Kashushu...siwezi kukubali jambo kama hilo...mkeo....?” Nilimwambia yule Dokta huku nikimtazama mkewe. Yule mwanamke mwenye sura ya kuvutia na mwili uliojigawa vizuri aliniambia kuwa nisikatae amana ile. Kwani hata yeye hatarudi tena hapa nchini. Nilipokea kwa mikono iliyojaa kitetemeshi.
“Sa...sasa ni wapi huko, yaani nitapajuaje....?” Niliwauliza. Dokta Kashushu alimwambia mkewe anichoree ramani ya eneo ilipo ile nyumba na akanitajia maeneo ya kuulizia ili nifike hapo, halafu akatoa picha ya ile nyumba na kunikabidhi. Ilikuwa ni nyumba ndogo ambayo ilikuwa bado haijamaliziwa sawasawa kujengwa kwa maana kuwa haikuwa imepigwa plasta kwa nje, ingawa ilikuwa imeezekwa kwa vigae na ilikuwa imewekwa madirisha na milango na ilikuwa imewekewa “grill” madirishani na milangoni.
“Ahsante sana Dokta...na Mrs. Kashushu... Mungu awajaalie huko mwendako.” Niliwashukuru, na Dokta Kashushu alimwambia mkewe aandike barua ya kunitambulisha kwa mlinzi wao, akiniambia kuwa mkewe ndiye aliyekuwa akijulikana sana na yule mlinzi kuliko hata yeye. Yule dada aliandika na kusaini ile barua kisha akanikabidhi. Kisha yeye alinitoa nje ya ile boti nami nikateremka na kusimama kwenye ukingo wa bahari juu ya baraza. Dokta Kashushu alinitazama na kuniuliza.
“Yule mwanamke aliyekuwa akitutupia risasi...unamfahamu? Ulionekana kuwa uliwahi kukutana naye hapo mwanzo...”
“Aaah! Yule...hapana, ila kuna mtu aliuawa, na ikasemekana kuwa mtu wa mwisho kuonana naye alikuwa ni mwanamke aliyevaa baibui...hivyo nikahisi labda ni yeye. Kwani vipi?”
“Umeshawahi kumsikia mtu aitwaye ‘The Virus’?” Aliniuliza. Nikamjibu hapana, na kumuuliza huyo ni nani.
“Ni muuaji wa kukodiwa...kama Carlos the Jackal, kama uliwahi kumsikia, lakini yeye anajiita The Virus...yaani Kirusi...huwa anafanya kazi zake Afrika. Nadhani ndiye yule aliyekuwa akitushambulia pale...”
“Ah, lakini yule alikuwa mwanamke...!” Nilimjibu kwa hamasa.
“Ndio maana nakwambia hivyo...kwa sababu inasemekana kuwa huyo The Virus, ni mwanamke!” Dokta Kashushu alinijibu. Nilibaki mdomo wazi.
Muuaji wa kukodiwa! Tanzania hii? Hapana hii sasa imekuwa kazi kubwa!
“Kila la kheri Tigga, we have to go now (yatupasa twende sasa)” Aliniambia nami nikampungia mkono. Dokta Kashushu aliingia kwenye boti lake, na muda ule ile boti ikaanza kuondoka kwa mwendo mdogo.
Nilisimama pale nikilitazama lile boti likiondoka mpaka likapotea kwenye upeo wa macho yangu.
Goodbye Dokta Mohammed Kashushu....Mwenyezi Mungu akulinde huko uendako...
***Heh, huyu muuaji The Virus ni nani? Dokta Kashushu ndio huyo ameenda zake na kumuacha Tigga katikati ya mashaka bila ya msaada wa Kamishna Vata...atawamudu vipi akina Martin Lundi muongo wakisaidiwa na huyu muuaji hatari, The Virus?
“Siku moja nilitembelewa na watu nisiowafahamu ofisini kwangu, ambao walinitaka nifanye mambo kama yale niliyokuwa nikikufanyia wewe kule kwenye ile nyumba kwa mashinikizo ya Wagga Maingo...ila wao walinitaka nimfanyie rais....”
“Whaaat?” Nilishitushwa na taarifa ile na kumgeukia yule Dokta kwa mshangao.
“Mmmnh! Ndivyo walivyonitaka na nadhani unaweza kukisia ni jinsi gani nivyoshituka juu ya ombi lao hilo. Niliwakatalia katakata na kutishia kuwaripoti serikalini.”
“Lakini...kwa nini walitaka kitu kama hicho...”
“Walitaka kunitumia kumtia rais wazimu...kisha asiwe tena na uwezo wa kuongoza nchi... wenyewe walidai kuwa hiyo ilikuwa ni njia pekee ya amani ya kumtoa rais madarakani bila kumwaga damu...( alicheka kwa dharau na kutikisa kichwa kwa masikitiko) Yaani lilikuwa ni jambo la kipumbavu nililowahi kulisikia maishani mwangu”
Eh...jamani! Haya mapya kuliko!
Pale jirani na kile chuo cha ubaharia kulikuwa na geti dogo ambalo lilitokea kwenye ngazi ndefu za mbao na chuma zilizokuwa zikiteremka pwani, eneo ambalo zamani ilikuwa inaegeshwa boti kubwa ya kwenda Zanzibar iliyoitwa MS SEPIDEH. Dokta Kashushu alijitambulisha kwa mlinzi wa pale getini ambaye alionekana kumtambua vizuri na kumuambia kuwa tulikuwa tunaelekea kwenye boti lake huko chini, na kwamba mkewe atafika muda mfupi ujao. Tuliteremka zile ngazi huku nikimuuliza kuwa alikuwa anamiliki boti. Aliafiki kwa kichwa bila kuonesha kujali juu ya swala lile.
“Baada ya wale watu ambao baadaye nilikuja kuelewa kuwa walikuwa ni wawakilishi wa kundi moja la upinzani lililokuwa likiendesha vita vya msituni dhini ya majeshi ya serikali kuona kuwa nimezidi kuwa mkaidi katika kutekeleza matakwa yao, walianza vitisho kuwa nikithubutu tu kutoa taarifa serikalini, wataiteketeza familia yangu yote! Nilikuwa kwenye wakati mgumu sana Tigga, na nilipoendelea na msimamo wangu, waliwateka mke na watoto wangu. Wakinishinikiza nimfanyie rais vile wao walivyotaka, kwani ni mimi pekee ndiye niliyeidhinisha dawa aina yoyote anayopewa rais iwapo atakuwa mgonjwa, na jambo ambalo ulimwengu haukulijua ni kwamba kwa wakati ule rais alikuwa akisumbulia na ugonjwa wa kisukari ambao ulimlazimu awe anameza vidonge maalum kila mara. Nilichotakiwa kufanya ni kumchanganyia dawa zangu za kumharibu akili pamoja na zile dawa za kisukari.”
“Dokta Kashushu haya mambo unayonieleza ni mazito sana! Inawezekana vipi mambo kama haya?” Nilimuuliza kwa msahangao. Yule Dokta alitikisa kichwa kwa masikitiko.
“Ninachokueleza Tigga ni kweli kimetokea. Hatimaye nilimweleza rais ukweli wa jambo lote, na kujiuzulu nafasi yangu ya utabibu wa rais. Rais alianzisha msako mkali wa kuwasaka mke na watoto wangu waliotekwa na wale watu ambao niliwajua kwa sura lakini sikuyajua majina yao. Kitendo hicho kiliwaudhi sana wale watu na siku moja baada ya kujiuzulu nafasi yangu, miili ya mke na watoto wangu ilikutwa kando ya msitu mmoja wakiwa wameuawa...” Aliniambia kwa huzuni nami nikahuzunika pamoja naye.
“Siku ile ile wale watu walinitumia wauaji nyumbani kwangu kuja kuniangamiza. Lakini jambo walilosahau ni kwamba mimi nilisomea shahada yangu ya udaktari huko Urusi, ambapo pamoja na shahada hiyo nilisomea pia mbinu za kijasusi na mapambano, kwani wakati huo urusi ndio ilikuwa inaendekeza zile siasa zake za ujamaa na ilikuwa ikisomesha waafrika wengi bure na kuwatumia katika propaganda zake za kijamaa. Niliwateketeza wale wauaji wawili na kuiacha nyumba yangu ikiteketea kwa moto, nami nikakimbia ile nchi Tigga. Nchi yangu niliyozaliwa na kukulia. Nilikuwa nimeficha pesa nyingi nje ya nchi, hivyo haikuwa taabu kwangu kutoroka nchini. Na kuanzia hapo nikawa mkimbizi Tigga. Huku nyuma nikasikia ndege iliyokuwa imembeba rais wetu na yule wa Rwanda ilianguka na kuwaua wote, lakini nilijua kuwa ni lile kundi lililokuwa likinitaka nimharibu akili rais ndilo lilihusika na kuanguka kwa ndege ile.” Dokta Kashushu alimalizia maelezo yake taratibu. Tuliingia kwenye ile boti yake ambayo kwa kweli ilikuwa kubwa na ghali sana. Aliniambia kuwa alikuwa ameiandaa ile boti kwa ajili ya tukio kama hili, ingawa huwa anakuja na mkewe mara kwa mara na kuiendesha hadi katikati ya bahari, siku nyingine wakiishi kwenye ile boti kwa siku mbili au tatu kabla ya kurudi tena nyumbani kwao Mbezi bichi.
Dokta Kashushu aliniambia kuwa alikimbilia Senegal. Baadaye alimtambua mmoja wa wale watu waliomfuta na kumshurutisha kumharibu akili rais akiwa miongoni mwa mawaziri wapya wa Rwanda, nchi ambayo ilikuwa ikishirikiana na waasi waliokuwa wakiipinga serikali ya Burundi. Kisha uchunguzi wa kifo cha rais wa Burundi na yule wa Rwanda ulianza, kwamba ile ndege haikuanguka kwa hitilafu za kawaida, bali huenda ikawa ilitunguliwa. Hapo wale watu wakaanza kumsaka tena ili kummaliza, kwani walijua ni yeye tu ndiye anayeweza kuwatambua wale watu waliomfuata na kumshurutisha kumharibu akili rais. Walimuibukia Senegal. Akafanikiwa kuwatoroka na kwenda Botswana. Huko nako akaondoka baada ya miaka miwili na miaka sita iliyopita akaingia Tanzania kwa pasipoti ya bandia aliyomtambulisha kuwa yeye ni Mtanzania aliyejulikana kwa Jina la Dokta Mohammed Kashushu. Hapa alianza maisha mapya na alioa mwanamke aliyekuwa yatima, kwani alijua kuwa wale watu bado walikuwa wakimsaka na hakupenda kabisa kujihusisha na mwanamke mwenye familia. Akiwa Tanzania, yule mtu aliyemtambua kuwa ni mmoja wa wale waliokwenda kumshurutisha kufanya mambo ya ajabu kwa marehemu rais wa Burundi, ambaye baadaye alikuwa miongoni mwa mawaziri wapya wa Rwanda baada ya mauaji ya halaiki, alionekana kwenye Televisheni akiwa ni mmoja kati ya watu waliokamatwa na kuletwa kwenye mahakama ya kimataifa dhidi ya mauaji ya halaiki ya Rwanda na Burundi iliyopo Arusha, Tanzania. Kufikia hapo alianza kuona mashaka juu ya usalama na amani yake nchini Tanzania, hivyo alimweleza ukweli mkewe mtanzania. Mkewe huyo aliamua kuwa pamoja naye popote atakapoenda, na ndio maana tukawa pale tukimsubiri mkewe ili atoroke naye.
Haya maelezo yalikuwa mapya sana kwangu na nikaanza kufikiria upya mkasa wote ule. Nilikumbuka kusoma habari za mahakama ya kimataifa dhidi ya mauaji ya halaiki ya Rwanda na Burundi. Nilikumbuka kusoma habari juu ya mtanzania kuteuliwa kuwa jaji wa mahakama hiyo...
“Lakini Dokta Kashushu, ilikuwaje ukapata nafasi ya kufanya kazi hapa nchini kwani vyeti vyako vya shule, hizo digrii zako, zilikuwa zinakuonesha wewe kama Dokta Kashushu? Kwani hilo ndilo jina ulilokuwa ukilitumia wakati unasoma?” Nilimuuliza.
“Hapana Tigga. Ukumbuke kuwa nilikuwa na pesa nyingi. Nilipata digrii zangu Urusi. Lakini pia nilitengeneza vyeti vya digrii hiyo hiyo kutoka vyuo vingine viwili vya nchi za magharibi, kimoja Finland na kingine kutoka chuo kidogo sana kisichojulikana kabisa kilichokuwa nchini Austria. Hiki cheti cha Austria kilinitambulisha kwa jina la Mohammed Kashushu kutoka Tanzania. Na hiki ndicho cheti ninachokitumia hapa Tanzania. Kwa hiyo ingawa fani niliyosomea ni ya kweli kabisa kama inavyoonekana kwenye cheti, jina lililo kwenye cheti na chuo ambacho kinaonekana kwenye cheti kuwa nimesomea si vya kweli. Chuo cha kweli nilichosomea kiko Urusi na katika cheti cha chuo kile kuna jina langu halisi, ambalo siwezi kukutajia kwa sababu ambazo nadhani unazielewa kufikia sasa.” Dokta Kashushu alinifafanulia. Haya mambo kwangu yalizidi kuwa mazito.
“Sasa ina maana kuwa wale watu waliokuwa wakikusakama tangu Burundi, Senegal na Botswana ndio hawa akina Wagga Maingo?” Nilimuuliza Dokta Kashushu kwa mshangao, huku nikianza kupata hofu kubwa juu ya huu mkasa mzima ulioniangukia.
“Hapana...huenda hawa wakawa na uhusiano na wale, lakini sio wale walionifuata kule Burundi. Kilichotokea hapa Tanzania, ambapo kama ulivyoelewa, nilikuwa nikiishi kwa amani sana, lakini kama Burundi, siku nne tu zilizopita yule mtu niliyekuja kumtambua kama Wagga Maingo aliniijia ofisini kwangu na kuniambia kuwa anajua kuwa mimi si mtanzania na ninaishi kwa hati bandia, na nimepewa nafasi nzuri sana katika nchi hii iliyoniwezesha kuishi kwa raha. Na akanitaka nimfanyie kazi yake, ambayo nikiifanya bila matatizo, wataendelea kunitunzia siri yangu na kuniacha niendelee kuishi kwa amani hapa nchini...kinyume na hapo, wao wangepiga simu idara ya uhamiaji na maisha yangu yangesambaratika.”
“Oh, Mungu wangu...!”
“Ndio Tigga. Nilikuwa na wakati mgumu. Na wakati huu umri wangu umesogea, sikuwa tena na uwezo wa kujiingiza kwenye mikiki-mikiki kama hapo mwanzo. Kwa hiyo sikuwa na la kufanya, nikakubaliana na sharti lao, ingawa sikuwa na uhakika kuwa huu ndio ungekuwa mwisho...nadhani sasa unaelewa ni kwa nini nililazimika kufanya vile Tigga, na nataraji utapata nafasi katika moyo wako kunisamehe kwa hili....” Dokta Kashushu alimalizia huku akinitazama kwa huzuni. Sikuwa na la kusema. Nilibaki nikiwa nimeduwaa.
“Kwa hiyo hujui hawa watu...akina Wagga Maingo walikuwa wanataka nini hasa?” Nilimuuliza.
“Hapana. Ila nakuhakikishia kuwa hawa watu ni wabaya sana. Sasa kama wana uhusiano na lile kundi lililofanya mambo ya kule Burundi miaka ile, basi nchi yenu sasa iko hatarini, na kwa kuwa wewe unaonekana kuwa na kitu wanachokitaka, nakushauri na wewe ukimbie mdogo wangu. Hapa hapakufai tena. Ukiwapa wanachokitaka, sina shaka kuwa wataiangamiza nchi yenu...wataitia kwenye balaa fulani tu! Hawa ni watu wanaopenda kuvuruga amani ndani ya nchi Tigga...kwa namna fulani ili wao wawe na maisha mazuri, ni wajibu kusiwe na amani.Kama kuna amani si mahala pao...ndio maana nakushauri kuwa ukimbie Tigga...ukipenda tunaweza kukuchukua pamoja nasi...nitakupatia pasipoti ya nchi yoyote uitakayo ukakae huko...”
“Hapana! Hapana Dokta Kashushu...mimi hapa ndio kwetu! Nina ndugu na jamaa zangu hapa, siwezi kuwaacha...” Nilimjibu kwa hamasa. Na hapo mkewe akafika. Walikumbatiana kwa upendo huku yule dada, ambaye alikuwa kijana zaidi ya Dokta Kashushu, akibubujikwa na machozi. Alimtazama mumewe kwa upendo na huruma, kisha macho yake yakaangukia kwenye pingu iliyokuwa ikining’inia kwenye mkono wake wa kushoto na kumuuliza kwa woga kulikoni.
“Ni hadithi ndefu...nitakuelezea baadaye...” Dokta Kashushu alimjibu. Mkewe akaanza kumchunguza ule mkono uliojeruhiwa kwa risasi lakini Dokta Kashushu alimtoa wasi wasi kuwa halikuwa tatizo kubwa. Yule dada alikuwa amehamanika vibaya sana. Walikuwa na mtoto wa kike aliyapata miaka minne ambaye naye alikuwa akilia kwa kumuona tu mama yake akilia. Dokta Kashushu alinitazama huku akiwa amemkumbatia mkewe.
“Sisi hatuna muda wa kupoteza Tigga...inatupasa tuanze safari mara moja. Una hakika hutaki kuambatana nasi?” Aliniuliza. Nillimtazama yule Dokta mtu mzima kwa muda huku nikimhurumia kwa mikasa iliyompata. Nilitamani kuwa pamoja naye, lakini akilini mwangu nilikuwa na mambo mengi niliyotaka kuyafanyia kazi nikiwa hapa hapa nchini. Nilitaka kujua sababu ya yule mtu kuuawa kule msituni, nilitaka kumjua ni nani yule mtu kigulu aliyekuwa na akina Wagga Maingo kule msituni, nilitaka kujua nini hatma ya yule dada askari aliyekuwa akishirikiana na akina Wagga Maingo...nilitaka kujua juu ya yule mwanamke mwenye hijab, aliyetuvurumishia risasi na ambaye nadhani ndiye aliyehusika na kifo cha Dick Bwasha...na hatma ya John Vata.Masikini John...iliniwia vigumu sana kuamini kuwa amefariki.
“Mimi nitabaki hapa hapa Dokta Kashushu...hata kama nitauawa, ni bora nifie nchini kwangu.” Nilimjibu taratibu. Yule Dokta alinitazama kwa muda, kisha akafungua begi alilokuja nalo mkewe na kutoa funguo zipatazo tatu zilizokuwa zimefungwa pamoja na kunikabidhi.
“Basi nakuomba uchukue hizi funguo za nyumba yangu nyingine Tigga. Hakuna mtu yeyote anayeijua nyumba hii, na nimeaindikisha kwa jina la huyu binti yangu.Unaweza ukahitaji maficho...nadhani huko kutakufaa kwani nina imani ukiwa kule hutagundulika kirahisi...na vitu vyote utakavyovikuta humo ni mali yako kuanzia leo...hiyo ni namna yangu ya kukusaidia katika mtihani huu Tigga...”
“Ah! Dokta Kashushu...siwezi kukubali jambo kama hilo...mkeo....?” Nilimwambia yule Dokta huku nikimtazama mkewe. Yule mwanamke mwenye sura ya kuvutia na mwili uliojigawa vizuri aliniambia kuwa nisikatae amana ile. Kwani hata yeye hatarudi tena hapa nchini. Nilipokea kwa mikono iliyojaa kitetemeshi.
“Sa...sasa ni wapi huko, yaani nitapajuaje....?” Niliwauliza. Dokta Kashushu alimwambia mkewe anichoree ramani ya eneo ilipo ile nyumba na akanitajia maeneo ya kuulizia ili nifike hapo, halafu akatoa picha ya ile nyumba na kunikabidhi. Ilikuwa ni nyumba ndogo ambayo ilikuwa bado haijamaliziwa sawasawa kujengwa kwa maana kuwa haikuwa imepigwa plasta kwa nje, ingawa ilikuwa imeezekwa kwa vigae na ilikuwa imewekwa madirisha na milango na ilikuwa imewekewa “grill” madirishani na milangoni.
“Ahsante sana Dokta...na Mrs. Kashushu... Mungu awajaalie huko mwendako.” Niliwashukuru, na Dokta Kashushu alimwambia mkewe aandike barua ya kunitambulisha kwa mlinzi wao, akiniambia kuwa mkewe ndiye aliyekuwa akijulikana sana na yule mlinzi kuliko hata yeye. Yule dada aliandika na kusaini ile barua kisha akanikabidhi. Kisha yeye alinitoa nje ya ile boti nami nikateremka na kusimama kwenye ukingo wa bahari juu ya baraza. Dokta Kashushu alinitazama na kuniuliza.
“Yule mwanamke aliyekuwa akitutupia risasi...unamfahamu? Ulionekana kuwa uliwahi kukutana naye hapo mwanzo...”
“Aaah! Yule...hapana, ila kuna mtu aliuawa, na ikasemekana kuwa mtu wa mwisho kuonana naye alikuwa ni mwanamke aliyevaa baibui...hivyo nikahisi labda ni yeye. Kwani vipi?”
“Umeshawahi kumsikia mtu aitwaye ‘The Virus’?” Aliniuliza. Nikamjibu hapana, na kumuuliza huyo ni nani.
“Ni muuaji wa kukodiwa...kama Carlos the Jackal, kama uliwahi kumsikia, lakini yeye anajiita The Virus...yaani Kirusi...huwa anafanya kazi zake Afrika. Nadhani ndiye yule aliyekuwa akitushambulia pale...”
“Ah, lakini yule alikuwa mwanamke...!” Nilimjibu kwa hamasa.
“Ndio maana nakwambia hivyo...kwa sababu inasemekana kuwa huyo The Virus, ni mwanamke!” Dokta Kashushu alinijibu. Nilibaki mdomo wazi.
Muuaji wa kukodiwa! Tanzania hii? Hapana hii sasa imekuwa kazi kubwa!
“Kila la kheri Tigga, we have to go now (yatupasa twende sasa)” Aliniambia nami nikampungia mkono. Dokta Kashushu aliingia kwenye boti lake, na muda ule ile boti ikaanza kuondoka kwa mwendo mdogo.
Nilisimama pale nikilitazama lile boti likiondoka mpaka likapotea kwenye upeo wa macho yangu.
Goodbye Dokta Mohammed Kashushu....Mwenyezi Mungu akulinde huko uendako...
***Heh, huyu muuaji The Virus ni nani? Dokta Kashushu ndio huyo ameenda zake na kumuacha Tigga katikati ya mashaka bila ya msaada wa Kamishna Vata...atawamudu vipi akina Martin Lundi muongo wakisaidiwa na huyu muuaji hatari, The Virus?