Duh!mleta uzi kafariki?kifupi hadithi imefika mwisho baada ya kufika kembo alimwambia kassim wageni wako hawa na kassim akawauliza shida yao ndipo denny akamuuliza kama anamjua asha rajabu?kassim akasema hamkumbuki ndipo denny akamkumbusha kisa cha miaka 25 ilopita akamwambia ulimpa mimba.Kassim akajibu lakini nilimsaidia denny akajibu kwa kumchoma visu na kimoja kilinipata hapa akararua shati lake kufumba na kufumbua yule bepari akachomoa bastola na kurusha risasi denny akafanya kembo kama kinga na risasi zikampata kembo na kumrusha.
Dakika hiyo hiyo kassim akaruka kimanga na kukimbilia nje denny akamfuata na kukuta kaliwasha benz denny nae akawasha Bentley na kuanza kufukuzana betty akalia ili asubiriwe haikuwepo nafasi hiyo,watu wakaweka pembeni magari yao ilikuwa kama mashindano kwani madereva wote wawili walikuwa hodari yaani ikawa kama mashindano ya mjerumani na mmarekani mpaka wakafika katika mlima hatari wa kata hewa uliosifika kwa kona nyingi na madaraja membamba.