Mkushi w jani
JF-Expert Member
- Oct 2, 2021
- 1,798
- 1,570
Eeeeeehsi huyo boya alivyo na kichwa kigumu kuelewa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Eeeeeehsi huyo boya alivyo na kichwa kigumu kuelewa
Kashusha kitu kizitoAisee asante sana mkuu umejua kutukata kiu leo
Sanaaaa,napata hofu tutamuona tena hapa mwakaniKashusha kitu kizito
Ha haaaaaaaaaaaaaaaaaaaaSanaaaa,napata hofu tutamuona tena hapa mwakani
Usimuache mkuu.RIWAYA: MWANAMKE KAMA MAMA YANGU
MTUNZI: KELVIN KAGAMBO
TEMBELEA KWA RIWAYA ZAIDI: http://riwayatakatifu.weebly.com/
SEHEMU YA KUMI NA NNE (14)
ILIPOISHIA….
Alipomaliza aliirejesha kwangu na kutuaga na safari yetu ikaanza. Katikati ya safari nilijaribu kupanga na Mke kwamba ni siku gani ingekuwa nzuri ya sisi kukutana na mwalimu na tuzungumze naye.
"Naona ni Jumapili" akanambia
"Sawa, basi nitampigia simu kesho nimwambie" nilimaliza na safari ikaendelea ambapo tulifika nyumbani na kufanya tafrija ndogo ya kifamilia kwa ajili ya kumpongeza mwanangu
SHUKA NAYOOOOO…..
Jumapili ya kukutana na Mwalimu Makoronjo ililfika, lakini kwa bahati mbaya siku hiyo nilihitajika kazini. Hata hivyo nilihitajika kwa muda mfupi tu kwahiyo ulikuwepo uwezekano wa kukutana na Mwalimu.
Nilifika kazini na kujaribu kukimbizana na muda ili kabla ya muda wa mihadi haujafika niwe nimekwisha kamilisha kazi. Lakini nilishindwa, Kazi zilinibana na kusabisha hata nikakosa nafasi ya kuchomoka na muda huo Mwalimu alianza kunitafuta katika simu.
"Haloo Mr. Jamal, niko karibu na nyumbani kwako, unielekeze" alinambia aliponipigia.
"Sawa, lakini mimi nimetoka mara moja ila ngoja nimpe Mke wangu namba yako, yeye atakusaidia kufika nyumbani. Mimi nitarudi hivi punde" nikamwambia.
Ikawa hivyo, nikampigia Mke wangu simu na kumueleza hali halisi kisha nikamtumia na namba ya Mwalimu ili afanye mawasiliano naye.
Robo saa baadae Ashura alinipigia simu na kunipa taarifa kwamba tayari Mwalimu ameshafika nyumbani na muda huo pia nilikuwa nimeshamaliza kazi na niko huru kuondoka.
Nikatoka mbio mbio kukimbia kwenye gari yangu ili niwahi nyumbani na kulinda heshima yangu kwa Mwalimu kwani ningeonekana mswahili kwa kushindwa kwenda na muda.
Mungu naye alinitazama kwa jicho la karibu sana kwani sikupata mushkheri wowote hadi nafika nyumbani.
Niliwasili na kukuta Mwalimu yupo sebuleni akizungumza na Khadija wakati Mke wangu akitayarisha chakula cha mchana.
Nilisalimiana na Mwalimu punde baada ya kufika nyumbani na pia nikajumuika naye hapo sebuleni na kupiga soga za hapa na pale wakati tukisubiri chakula.
Tuliongea mengi mengi sana na nilichogundua ni kwamba tulikuwa tukifafana kwa mambo tunayoyapenda na hiyo ilipelekea tusikose cha kuongea.
Nusu saa baadae chakula kilikuwa tayari, Mke wangu akaandaa mezani na kutukaribisha na kwa pamoja tukajumuika na kupata pilau ya Kuku safi iliyoandaliwa na Ashura. Alikuwa ni fundi wa kupika kwahiyo kula vitu vya namna hiyo toka kwangu haikuwa mara yangu ya kwanza ingawa kwa sasa nimevimiss.
Nime-miss mapochopocho hayo kwasababu siku hizi ameacha kupika na si kwamba ndiyo utaratibu tuliowekeana bali ameamua tu, kule kubadilika kwa tabia zake ndiyo kumezaa hayo, siku hizi mimi ndiyi nimekuwa kama mpishi.
Nashindwa hata nikamshitaki wapi kwani wazazi wangu yaani Baba yangu, Mzee Shomari na Mama yangu Bi Khadija wote ni marehemu kwa sasa; walifariki tangu mwanangu Khadija akiwa na umri wa miaka minne.
Kesi kama hizo labda ningezipeleka kwa Baba yangu Mkubwa lakini nako huko nilihofia, Baba yangu mkubwa ni mropokaji na angeweza hata kusababisha Mimi na Mke wangu tukaachana jambo ambalo sikuwa nikitaka kuona linatokea kwani naamini kuachana na Mke wangu kungepelekea wanangu kuteseka kweli kweli.
Niliwahi kupeleka kesi hizo kwa wazazi wake lakini kama hawakuwa wakizitilia maanani na pengine ni kwasababu Baba mkwe hakuwa na hali nzuri kiafya. Alikuwa akiandamwa na maradhi ya mara kwa mara na hivyo kupelekea nikakosa msaada wake.
Mama asingeweza kuchukua hatua yoyote zaidi ya kumuelekeza mwanaye jinsi ya kuishi vyema na mume wake lakini hiyo nayo haikuwa dawa ya ugonjwa wa tabia chafu anaoumwa Mke wangu.
Chakula kiliwekwa mezani nasi tukaanza kukifakamia. Tulikula kwa furaha kutokana na wingi wa walaji huku hatima ya mlo huo ikiwa ni mazungumzo ya sisi na Mwalimu Makoronjo.
Tuliketi nje, eneo ambalo nilipanda maua chini ya mti wenye kivuli na hiyo ilikuwa sehemu sahihi kwa aina ya mazungumzo aliyokuwa nayo.
Tulizungumza kwa muda mrefu, takribani dakika ishirini lakini mzizi au kiini cha mazungumzo yote hayo ni Mwalimu Makoronjo kutaka tumuendeleze Khadija kielimu kwani ni mtoto mwenye uwezo mkubwa sana.
Mwalimu alitushauri kwamba tumuhamishe shule anayosoma sasa na tumpeleke kwenye shule iliyo bora zaidi.
Hakuishia hapo, alikwenda mbali zaidi na kutueleza kwamba ingekuwa vyema zaidi kama angehama nje ya Tanzania na kwenda kusoma Kenya ambapo kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba kenya inatoa elimu ya kiwango cha zaidi ya Tanzania.
Unajua Mwalimu Makoronjo ni raia wa Kenya, amezaliwa huko Nairobi lakini alikulia Mombasa ambapo alimfuata Mama yake mara baada ya wazazi wake kutengana.
Kwahiyo akasomea huko na sasa anafanya kazi Tanzania hivyo ni rahisi kwa yeye kugundua kwamba ni nchi inatoa elimu bora kati ya hizi mbili.
Binafsi sikutaka kuona hilo likitokea, eti mwanangu nimuamishe nchi? Nisingeweza labda na mimi ningekwenda kuishi huko.
Kama ni elimu angeipata hapa Tanzania. Elimu ya kwetu ni bora na inamtosha sana cha msingi ni mimi Baba yake kumuunga mkono kwa kumpeleka shule za uhakika; za kulipia gharama kubwa.
Ukubali ukatae elimu ni ghali kwahiyo lazima iwe hivyo, kama Mzazi ama mlezi ujipinde kuhakikisha mwanao anatajarika kielimu.
"Wazo zuri mwalimu lakini ingependeza kama ungetupa muda mimi na Mke wangu tulijadili" nikamwambia lakini akili yangu tayari ikiwa imebeba jibu la hapana.
Nilitaka atupe muda ili nipate jinsi nzuri ya kumkatalia, papo kwa papo isingependeza.
Aliondoka na kutuacha na Mke wangu ambapo usiku tukiwa kitandani nilijaribu kuzungumza suala hilo na Mke wangu ili kujua naye ana mtazamo gani.
"Kwahiyo Mke wangu unashauri nini kuhusu hili la Khadija kwenda Kenya?" nilimuuliza hivyo tu, tena kwa ukarimu na utaratibu lakini jibu alilonipa lilinichosha na kunifanya hata nijute kumuuliza.
"Bwana vyovyote itakavyokuwa ni sawa tu kwanza mimi nataka kulala" akanambia maneno hayo huku akigeuka upande wa pili akinipa mgongo, akavuta shuka na kujifunika gubigubi kama ishara ya kwamba hataki stori na mimi.
Nikashindwa kumuelewa na hadi sasa simuelewi na sitamuelewa ni mwanamke wa aina gani, mwanamke asiyetaka kuzungumzia mambo muhimu ya familia yake. Mwanamke mwenye nguvu ya kumjibu mume wake vile atakavyo, hakika huyu si Ashura ninayemfahamu mimi,
Ashura niliyemuona na kuishi naye kwa upendo kipindi kile, nikampenda, akanipenda, tukapendana na kunifinya nijihisi huru kusema Ashura ni Mke wangu hata mbele ya kadamnasi.
Lakini huyu wa sasa siwezi, sina umwamba wa kusimama na kusema huyu ndiye Mke wangu kwani hana tabia za kupendeza za kuitwa Mke.
Lazima kuna kitu kitakuwa kimembadilisha.
Basi nikamuacha alale kama alivyotaka, nigaeukia upande mwingine tukawa tumepeana migongo na hadi pakakucha hivyo hivyo.
*******************
Siku ya tatu tangu Mwalimu Makoronjo alete lile pendekezo kwetu alinipigia simu. Alifanya hivyo ili kufahamu kwa tumefikia wapi ili naye aanze kufanya mipango.
Binafsi sikuridhia na nilichoona bora kumjibu ni kumwambia kwamba amuache Khadija amalizie elimu ya msingi hapa hapa Tanzania na nitampeleka huku pindi atakapofika sekondari.
Mwalimu hakuwa na jinsi na asingeweza kulazimisha ikiwa mimi ndiye mzazi wa mtoto.
*************************
Bas niliendelea kumtazama Mke wangu jinsi anavyolia kwa uchungu wa kupoteza watu muhimu kwenye maish; watoto na Mama.Lakini nadhani atalia sana pindi atakapogundua kuwa yeye ndiye msababishi kwani bila kuondokaq kwake mwanangu Ally asingepata tabu ya kwenda kumtafuta na hatimaye kupigwa na radi, pia kama Ally asingepigwa radi basi ni wazi kwamba mwanangu Khadija asingekufa kwa mshituko wa kuona maiti ya mdogo wake imeungua vile. Na pia Mama yake asingekufa kama asingesikia yale maneno ya muasherati mwenzake na Mke wangu (Mwanaume aliyekuwa naye huko)
Aliketi chini huku kilio kikipungua muda huu, pengine alichoka kwani alilia kwa muda mrefu sana huku wsisi sisi tukimtazama tu.
Mara Baba Mkwe akasimama, akatutazama sote tulioketi kwenye kochi na kusema "Kwaherini, nakwenda nyumbani" akaweka koma hapo, akavuta pumzi kwa sekunde mbili na kuongeza.
"Jamal huyu ni mke wako, una mamlaka ya kumfanya chochote upendacho. Kama utaamua kumuacha ni wewe; umpe talaka nami nitampokea kwasababu ni mwanangu wa kumzaa na hana Baba mwingine" akanambia hivyo kisha akaanza kutembea kuelekea mlangoni ambapo ndipo alipokuwa ameketi mwanaye. Akasimama pemsbeni yake akimtazama kwa huruma.
"Ashura... Nakutakia maisha mema kama mume wako ataamua kuendelea kuishi nawe, lakini nakukaribisha nyumbani kama ataamua kukuacha. Kwaheri" akamwambia sentesi fupi namna hiyo kisha akaondoka na kutuacha pale.
Na ndugu zangu nao wakasimama wote kwa pamoja.
"Kwaheri Jamal" wakaniaga na kuondoka na hatimaye ndani nikabaki mimi na Ashura tu.
Sikufahamu kwanini waliamua kufanya vile lakini yawezekana walinipa nafasi ya kufanya maamuzi. Bila shaka waliogopa hata kunishauri kwamba niendelee kuishi naye au nimeuache kwani kile kilichotokea kilikuwa ni kizito kwao hata kunipa ushauri.
Basi nikawa mwenyewe pale tena nikimtazama kwa hasira mke wangu kwani namhesabia kama ni mtu aliyeniharibia maisha yangu. Nilitamani nimuue pia ili aone uchungu ambao wameupata wanangu.
Yeye hakuthubutu hata kunyanyua uso wake kunitazama. Nikajikuta nimesimama huku nikiendelea kumtazama kana kwamba kuna jambo nataka kumueleza.
******************************
LEO SISEMI KITU ZAIDI YA KUKUSIKILIZA WEWE, NAOMBA UNISHAURI CHA KUMFANYA HUYU MWANAMKE, NIMUACHE AU NIENDELEE NAYE?
WAWEZA WASILIANA NA MWANDISHI KWA NAMBA TAJWA HAPO JUU KUPATA RIWAYA HII NA NYINGINE NYINGI KWA HALAKA ZAIDI.