RIWAYA: Wivu-Beka Mfaume

RIWAYA: Wivu-Beka Mfaume

Casuist

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2014
Posts
1,189
Reaction score
2,970
Habari wanajukwaa, kuna softcopy kadhaa nnazo za hadithi tofauti nkaona si vibaya ku-share ikizingatia watunzi wake wameziweka public hivyo kutohesabika kama wizi wa kazi za watu au kuharibu mapato.. Kila siku nitaweka sehemu moja, watakuwepo ambao wameshazisoma lakini pia kutakua na wengi ambao hawajahi kuzisoma,




MWANDISHI: BEKA MFAUME

SEHEMU YA KWANZA

JUDI alimalizia kujifunga mkufu shingoni baada ya kukamilisha kujikwatua kwa vipodozi tofauti vya gharama huku akiwa amevaa vazi lililompendeza mwilini. Alikuwa ameamkia nyumbani kwa Richard ambako alikuja usiku uliopita na kulala hadi asubuhi hiyo. Yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kumaliza kuoga na alikuwa akimsubiri Richardamalize kuoga kisha watoke pamoja kwenye gari la Richard. Kituo chao cha kwanza kingekuwa kwenye mgahawa wa Monde uliopo katikati yajiji kwa ajili ya kifungua kinywa, kisha baada ya hapo, Richard angempeleka kazini kwake.

Akiwa amekaa kitandani baada ya kutoka kujiangalia kwenye kioo kilichopo kwenye kabati la kuvalia, Judi alianza kujiuliza kama ulikuwa ni wakati mwafaka wa kumuuliza Richard kuhusu matumaini yake ya kuolewa naye. Walikuwa ndani ya uhusiano wa mapenzi kwa muda mrefu na alikuwa akijisikia fahari mbele ya wanawake wenzake kuwa na uhusiano huo na Richard ambaye ni mtoto wa mfanyabiashara tajiri na maarufu jijini Dar es Salaam. Pamoja nakuwepo na uhusiano huo wa muda mrefu, lakini haikuwahi kutokea hatasiku moja kujikuta wakizungumzia suala la kuoana. Haikuwa ni marayake ya kwanza kulala nyumbani kwa Richard.

Alishakuwa mwenyeji wanyumba hiyo tokea uhusiano wao ulivyoanza na kumfikisha hadi sikuhiyo. Mara nyingi, husan siku za mwishoni mwa wiki kuanzia Ijumaahadi Jumatatu alikuwa na mazoea ya kuhamia nyumbani kwa Richard nakuumiliki umama wa mwenye nyumba kuanzia usafi hadi mapishi namengineyo, kiasi kwamba hata nguo zake zikawa zimegawanyika sehemumbili; baadhi zikiwa nyumbani kwao ambako aliishi na wazazi wake nanyingine zikiwa nyumbani kwa Richard.

Uhusiano wao ulifahamikahadi kwa wazazi wao na kila mmoja alikuwa amejenga uhusiano mzuri kwaupande wa wazazi wa mwenzake. Richard alikuwa na uwezo wa kwendanyumbani kwa akina Judi na kuomba kuondoka naye kwa muda wowote. Halikadhalika, Judi aliweza kwenda nyumbani kwa Richard kwa muda wowotealioamua. Ingawa wote walikuwa huru kuyafanya mambo hayo, lakiniwalikuwa wakitofautiana kimawazo. Kwa upande wa Judi, yeye alikuwahajiamini kama alikuwa peke yake kwenye penzi la Richard. Hakujua nikwa nini alikuwa akipatwa na hisia hizo mara kwa mara, kuna wakatialikiri huenda ni kwa vile Richard alikuwa ni mtoto aliyezungukwa nautajiri wa baba yake na mwonekano wake kumvutia msichana mwingineyeyote kutaka awe naye!
Wivu! Hilo ndilo lililokuwa likimsumbua nakumwingiza kwenye wasiwasi huo. Alikiri dhana hiyo ya wivu ndioiliyokuwa ikiisumbua
nafsi yake na kumjengea woga kuwa, Robertalikuwa na wanawake wa nje! Pamoja na kuwa na hisia za aina hizo,lakini hakuwahi kumfumania na mwanamke mwingine japo mara moja!

Kwaupande wa Richard, yeye mawazo yake yalikuwa yakikinzana kimkabalana mawazo ya Judi. Yeye alikuwa akiamini Judi alikuwa hanamwanamume mwingine zaidi yake kutokana na uaminifu aliokuwa nao Judi.Pamoja na kuwa na mitazamo tofauti kati yao, ajabu ni kwamba, hakunahata mmoja aliyediriki kuzizungumza hisia hizo kwamwenzake.

Mahusiano yao ya muda mrefu yaliwawezesha kuwajengeamazoea ya kuzoeana, wakawa na uhuru kwa kila mmoja kwenda kwamwenzake kwa muda wowote na wakati mwingine bila hata yakutaarifiana. Uhuru huo ulimfanya Judi na wazazi wa pande zote mbilikuamini kuwa, suala la ufungaji wa ndoa kati yao lilikuwa lipo njianina lingetangazwa wakati wowote. Lakini kama ilivyo ada kwa tamaduniza Kiafrika, mwanamume ndiye aliyepewa jukumu la kutamka dhamirahiyo, Judi akaamini, ipo siku Richard angekuja kulitamka jambo hilokwake. Richard hakufanya hivyo! Na Judi naye akashindwakuvumilia! Ndipo asubuhi hiyo, Judi alipoamua iwe siku ya kuuvunjaukimya huo!

* * * * *

Richard alitoka kuoga nakuingia chumbani. Kitendo cha kufunguliwa kwa mlango wa maliwatoniambayo ilikuwa imo humo humo chumbani, ile hali ya kutoka kuogaaliyokuwa nayo Richard na kufunguliwa kwa mlango huo kulisababishaharufu ya sabuni ya kuogea iingie chumbani humo, lakini ilichukuasekunde chache harufu hiyo kumezwa na manukato yenye harufu ya nuniyaliyokuwa yamepulizwa mwilini na kwenye nguo alizovaa Judi.

Judiakaanza kumpigia mahesabu Richard aliyekuwa ameanza kuvaa nguo yandani na kisha akamwona akivaa suruali aliyoitoa kwenye kining'inizocha kuwekea nguo kwa kutumbukiza mguu mmoja baada ya mwingine kwenyesuruali hiyo. Judi akashusha pumzi kwa nguvu bila ya kutarajia. Halihiyo ilimjia baada ya kugundua jambo alilokuwa anataka kulizungumzakwa Richard lilikuwa na uzito mkubwa kwenye mustakabali wa maishayake ya baadaye.

Hali ya utambuzi wa mustakabali huo ilimuwekakwenye unyonge, hata kule kujiamini kuwa yeye ndiye mwenye nafasi yakuolewa na Richard, ghafla kukaanza kumuweka kwenye njia panda. Hofuhiyo ikamuweka kwenye mizani kwa kuzivuta kumbukumbu za matukio kwakipindi chote alichokuwa na Richard, ikawa kama vile anajifanyiausaili utakaomwezesha kumpa moyo wa kuendelea na dhamira yakealiyoidhamiria; dhamira ya kulizungumza suala la ndoa kwaRichard!

Aliyakumbuka matukio mengi mazuri yaliyoonyesha upenzikati yao; kama vile kununuliwa vito na nguo za thamani kwenye madukayanaouza bidhaa hizo kwa bei ghali; kutoka pamoja kwa ajili ya kulachakula cha usiku kwenye hoteli za kifahari au migahawa ya Kimataifa;kuhudhuria kwa pamoja mialiko tofauti ya sherehe walizokuwawakialikwa au wakati mwingine kufurahisha nyoyo zao kwa kwenda kwenyemahoteli yaliyopo nje ya jiji la Dar es Salaam au kwenye majumbatofauti ya starehe.

Ujumla wa kuyakumbuka matukio hayo ulimfanyaajione ni nembo maalumu ya Richard na kuamini kuwa, ni yeye ndiyealiyechaguliwa! Lakini pia, pamoja na kuyakumbuka mazuri yoteyaliyofanyika kati yao, pia aliikumbuka mizozo waliyokuwa wakizozanakwa mambo madogo. Kama vile kukasirikiana kutokana na maudhiyaliyokuwa yakisababishwa na vijijambo vya kipuuzi, wakati mwinginekuwafikisha kununiana kwa saa kadhaa au zaidi ya hivyo.

Baadhi yamatukio waliyoudhiana waliweza kuombana misamaha, lakini pia kunabaadhi yaliyowafanya wasiombane misamaha kwa sababu kila mmojaalijiona ana haki ya kuvuta kamba upande wake. Mizozo ambayohakuwakuombana misamaha iliweza kumalizika kimya kimya na kuwa kamavile hakukuwepo na mtafaruku uliotokea kati yao. Alipoyawekakwenye mizani matukio hayo, mengi yakawa ni mazuri na zile kasorochache zilizokuwa zikijitokeza, akazichukulia ni sehemu ya kawaidakwa binadamu wanaoishi kwa karibu. Ukweli huo ukamuweka Judi kwenyeimani aliyoikubali kuwa, walikuwa wakipendana kwa dhati.

Akajionayupo kwenye nafasi kubwa ya kuolewa na Richard! Hali hiyoikamrejeshea nguvu ya kuitupa karata yake juu ya meza! "Richie,"Judi aliita. Alikuwa amezoea kumwita Richard kwa jina hilo. Richardaliyekuwa amesimama mkabala na kioo kilichopo kwenye kabati lakuvalia akiwa anazichana nywele zake, aligeuka na kuitikia hukuakimwangalia Judi aliyekuwa bado amekaa kitandani. "Kuna jambonataka nikuulize," Judi alisema huku akijaribu kuyatuliza machoyake kumwangalia Richard usoni na wakati mwinginekuyakwepesha. Richard alishitushwa na kauli hiyo baada ya kugunduaJudi alikuwa amekosa utulivu usoni mwake wakati akiitamka. Akahisikulikuwa na tatizo! "Jambo gani?" Richard aliuliza huku akiwaameganda na kitana chake mkononi.
"Una mpango wowote wakunioa?"

Richard alionekana kama aliyesukumiwa ngumi ya ghaflailiyotua usoni mwake! Akiwa ameishiwa nguvu ghafla baada yakupigwa swali hilo, alijikokota kwa kujisogeza taratibu hadi kwenyekabati la kuvalia, akaliegemea. Uso wake ulikuwa umepigwa na tahayari iliyomwonyesha kuwa, alikuwa akihaha kulitafuta jibu. Macho yakeyalishindwa kuyakabili macho ya Judi yaliyokuwa yakimwangalia.Akaiangalia sakafu iliyojengwa kwa marumaru kama vile eneo hilo ndilolingetoa majibu ya swali alilokuwa ameulizwa. Ukimya uliofanywa naRichard ukaanza kumchanganya Judi. Akili yake ilianza kukataakuamini kile anachokishuhudia kutoka kwa Richard.
Richard alikuwaakionekana kupata kigugumizi kulijibu swali ambalo lingehitimishandoto ya Judi; ndoto ya kuolewa! "Mbona hunijibu?" Judialiuliza huku sauti yake ikionyesha ukakamavu wa kutaka ajibiwe,lakini moyo wake ukisambaratika kwa maumivu yaliyoanza kumkatishatamaa. Woga na hofu ya kupewa jibu litakalomwumiza vikawa vinaitafunanafsi yake, hali hiyo ikauweka moyo wake kwenye mapigo ya kasiyaliyotishia uhai wake!

Richard alianza kwa kupiga kite nakushusha pumzi huku uso wake ukiwa bado unaangaliasakafuni."Hapana Judi!" Richard alijibu kama vile alikuwaakiongea na sakafu aliyokuwa akiitazama. Kisha akauinua uso wakekumwangalia Judi. "Sina mpango wowote wa kukuoa!"alimalizia. "Yesu wangu!" Judi alinong'ona peke yake nakuishiwa nguvu huku
akiwa amefumba macho. "Najua haitokuwarahisi…" Richard alianza kuutetea uamuzi wake.

Judi akawahikumnyooshea mkono Richard kumzuia asiendelee kuzungumza. Kimyakikapita kati yao. Judi akashusha pumzi kwa nguvu akiwa badoamefumba macho. "Uko serious na jibu lako?" aliuliza. Richardakaonekana kuwa kwenye wakati mgumu, lakini pamoja na kuwa kwenyehali hiyo, bado alikusudia kuwa kwenye msitari wa ukweli. "Ndiyo!Niko serious!" Richard alisema.
Judi akanywea, kila kiungo chakecha mwili kikaonekana kama kimekataa kufanya kazi! Akatulia palekitandani alipokuwa. Ghafla
akalikumbuka tukio la kufanya mapenzina Richard saa chache zilizopita baada ya kurudi kutoka disko kablahawajalala na kuamka asubuhi hiyo.

Halikuwa tukio geni kwao,lakini tukio hilo la saa chache zilizopita likawa kama tukio pekeekatika maisha yake na Richard lililompa picha halisi jinsi Richardalivyokuwa akimchezea katika maisha ya ngono walizokuwa wakizifanyahuku yeye akiamini kwa imani zote kuwa, ilikuwa ni njia ya kuelekeakwenye kufunga ndoa!

Lilikuwa pigo kwenye maisha yake! Aliusikiamoyo wake ukikatika pande mbili kwa maumivu makali aliyokuwahajawahi kukumbana
nayo. Alihisi kama anayeelekea kuzirai,akajaribu kupambana na hali hiyo isimtokee akiwa ndani ya nyumba hiyoambayo sasa ilishakuwa ni nyumba asiyotaka aendelee kuwemo tena.Akamudu kuizuia hali hiyo, lakini akashitukizwa na tukio jingineambalo laiti angepatwa na hisia za mapema kuwa lilikuwa njianikumtokea, kamwe asingeweza kuliruhusu limtokee mbele ya Richard;Richard alishakuwa Shetani mbele yake! Yalikuwa machozialiyoshindwa kuyazuia! Kitu kikaja kumbana kooni na kumwanzishiakilio chenye kwikwi iliyomuweka kwenye kilele cha majuto! Richardakamsogelea na kumshika maungoni ili ambembeleze, Judi akaupangua kwanguvu mkono wa Richard usimshike! "Tafadhali usinishike!" Judialisema kwa sauti yenye chuki iliyotawaliwa na hasira zilizokuwakatikati ya kilio. Kuanzia siku hiyo uhusiano wao ukawa umeingiadoa!

*****

JOHN Sailas akiwa varandani mwa nyumbaanayoishi yenye chumba kimoja cha kulalia, varanda moja, jiko na chooambayo alipanga, alitengeneza tabasamu dogo mdomoni mwake wakatiakiisoma barua iliyoletwa na mshenga wake iliyokuwa imejibu baruayake ya uchumba aliomchumbia rafiki yake wa kike anayeitwa Dina sikukadhaa zilizopita. Barua aliyokuwa akiisoma ilikuwa ikielezeajinsi alivyokubaliwa uchumba wake na tabasamu alilokuwa amelijengalilikuja baada ya kusoma masharti yaliyokuwa yanahitaji yatimizwesiku itakayopelekwa mahari. Baadhi ya masharti aliyaona kama aina yamzaha unaochekesha.

Kukubaliwa kwake kumuoa Dina alikutarajia kwasababu alikwisha kuizungumza nia yake hiyo kwa mwenyewe Dina,wakakubaliana na ndipo alipomtuma mshenga kuipeleka posa hiyo. Lakinipia, hata kabla ya kulizungumza hilo, uhusiano wao wa mapenziuliokwishadumu kwa zaidi ya mwaka mmoja, nao ulikuwa ukifahamika nawazazi wa Dina, hali kadhalika na wazazi wake mwenyewe. Pamoja yakuwa mila za Kiafrika huwa zinawaweka mbali mtu na mkwewe, lakiniuhusiano wake na Dina
uliweza kumuweka karibu na mama mkwe wakekiasi kwamba kukawa na urafiki fulani ulioongezea aina ya utani wahapa na pale.
Ukaribu huo na mama mkwe wake ndio uliompa Johnuelewa kuwa, posa yake hiyo isingekumbana na vikwazo vyovyote.Alikuwa akijua mama yake Dina ndiye aliyekuwa na sauti ndani yanyumba huku baba yake Dina ambaye ni mstaafu akiwa hana kauli yakumpinga mama huyo. Mama yake Dina ambaye bado ni mwajiriwa, ndiyealiyekuwa mwendeshaji wa nyumba kwa karibu kila kitu.

Johnaliikunja barua aliyokuwa akiisoma na kuirudisha kwenye bahasha,kisha akaiweka juu ya meza na yeye mwenyewe kujilaza kivivu kwenyesofa aliyoikalia. Uso wake aliuelekeza juu na kuliangalia pangaboilililokuwa likizunguka kwa kasi ndogo. Uzungukaji wa pangaboialiokuwa akiuangalia ilikuwa ni kama vile alikuwa akizirudisha nyumatafakuri zake kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja uliopita kwakuikumbuka siku ambayo yeye na Dina walionana kwa mara ya kwanza.Ilikuwa siku ya Jumamosi!

Aliikumbuka vizuri siku hiyo. Siku hiyoalikwenda eneo la Ndege Beach akiwa na pikipiki yake. Hakuwa mgeni naeneo hilo, alikuwa na mazoea ya kwenda mara kwa mara kwa ajili yakuogelea kutokana na fukwe ya eneo hilo kuwa ya kupendezaukilinganisha na fukwe nyingine zilizopo Dar es Salaam kamaukiziondoa zile za eneo la Kigamboni.
Akiwa na begi lakelililobeba nguo yake ya kuogelea baada ya kufika kwenye fukwe hiyo,alilitua begi juu ya mchanga mweupe hatua chache kutoka baharini.Aliwaangalia kwa sekunde chache watu waliokuwa wakiogelea kwenyebahari ambayo haikuwa na mawimbi makubwa kwa siku hiyo. Kishaaliinama tena, akalifungua begi lake na kutoa bukta aliyoiandaakuogelea nayo. Kabla ya kuivaa bukta hiyo, alijifunga taulo kubwailiyoziba maungo yake ya kati hadi miguuni, akaivua suruali yake yajeans kwa kuiunganishia na chupi aliyokuwa ameivaa na kuzikunjavizuri nguo hizo kisha akaivaa bukta ya kuogelea. Baada ya kuwakamilifu kwenye hali ya kwenda kuogelea, alizichukua nguo zakealizozivua na kuzitia kwenye begi pamoja na ile taulo. Badalaya kwenda kuogelea, John alikaa kwenye mchanga kando na lilipo begilake na kuanza kuwatizama waliokuwa wakiogelea baharini.

Akavutiwana kundi dogo la wasichana watatu, wawili wakionekana angalauwanaweza kujaribu kuogelea na yule watatu akiwa hajui kabisakuogelea. Msichana huyo wa tatu ndiye aliyemvutia; na si kwamba kwavile alikuwa hajui kuogela, lakini pia alikuwa na mvuto kulikowenzake aliokuwa nao. Msichana huyo mwenye umbo la kupendeza lenyeurefu wa wastani, alipendezwa na nguo za kuogelea aina ya bikiniambayo ilimfanya John apate ushawishi wa kumkaribia msichana huyo iliamwone vizuri!

Aliendelea kumwangalia msichana huyo alivyokuwaakijilaza kwenye maji kama anayetaka kuogelea, lakini kwa kukosaustadi wa kujua kuogelea, akawa anaishia kwenye mwelekeo wa kuzamakila alipokuwa akijaribu kuogelea. Wakati wote alipokuwa akijaribualijikuta akiishia kupiga magoti na sura yake kuangukia majini.Kitendo hicho kilimfanya ajiinue kwa haraka kila tukio hilolilivyofanyika na kuonyesha woga wa kuogopa kuzama huku akijifutamaji ya usoni na kuhema kwa kuacha mdomo wazi na kuzitafuta pumzikwa kuruka ruka kwenye maji huku akipenua macho yake. Hali hiyoilimfanya John atabasamu peke yake. John aliondoka alipokuwaamekaa na kuelekea kwenye maji, akaenda upande walipokuwepo wasichanahao na kumfuata yule aliyekuwa hajui kuogelea. "Samahani,"John alimwambia yule msichana. "Una nia ya kujua kuogelea?" Usowa msichana yule ukajengwa na aibu kwa kugundulika kuwa hajuikuogelea, hata hivyo aibu hiyo akaiziba kwa tabasamu lenye haya. "Kwajinsi unavyojaribu kuogelea, katu hutojua kuogelea,"John aliendelea bila ya kusubiri jibu la msichana huyo. "Kwanzani mwoga. Pili, maji hayawezi yakakuinua kwa sababu tu, unatakakuelea. Kuna mbinu za uogeleaji ambazo lazima ufundishwe ndipoutakapoweza kuogelea," John alisema. Akakumbuka kujitambulisha."Jina langu ni John, John Sailas. Unaitwa..?" Moja kwa mojamacho ya msichana yule yakawaangalia wenzake walioacha kuogelea,nao wakawa wanakuja pale aliposimama na John. "Vipi?" mmoja wawale wenzake wawili alimwuliza huku akijaribu kumwangalia John kwakutaka kujua kinachoendelea. "Nataka kumfundisha mwenzenu namnaya kuogelea," John alijibu ingawa swali lililoulizwa lilikuwahalikulenga kwake.

Nyuso za mshangao zikajengwa na wasichana haowawili na kuonyesha dhahiri hawakulitarajia jibu hilo. Wakajikutawakimwangalia mwenzao kama kutaka kujua ameliafiki vipi wazo hilo.Mwenzao hakujibu chochote, ukimya wake ukawajumuisha wote watatu kupigwa na ganzi ya kutojua wajibu nini kwa mtu huyo au wawili haowamshauri vipi mwenzao. "Nitarudi baadaye nijue mmeamuaje!"John alisema kisha alijilaza kwenye uso wa maji na kuanza kuogeleakwa ustadi wa kukusudia kuwaonyesha wasichana hao namna gani jinsianavyojua kuyakata maji. John aliogelea kwa umbali mrefu kama njiaya ushawishi kumfanya msichana huyo endapo atakubali kufundishwanaye basi ajione atakuwa salama mikononi mwake.

John aliporuditena kwa wale wasichana, wakakubali amfundishe mwenzao, lakini kwasharti kuwa hata nao walihitaji kufundishwa.
"Basi nitaanza nahuyu ambaye hajui kabisa," John alisema. Wazo la Johnlikakubaliwa.
Wakiwa wawili peke yao kabla ya kuanza kufundishanakuogelea, John akakumbuka kujitambulisha tena, "Jina langu ni John Sailas…" Macho ya John na yule msichana yakaangaliana. Johnakauhisi moyo wake ukipiga kwa kasi. Akakijua kilichopo moyoni mwakedhidi ya msichana huyo. "Naitwa Dina," msichana alisema hukuakionyesha tabasamu dogo lililojificha kwa dhamira. Ni sikuambayo John hakuisahau kamwe!

ITAENDELEA KESHO..
 


mtunzi: Beka mfaume.

Sehemu ya pili


wazo la john likakubaliwa. Wakiwa wawili peke yao kabla ya kuanza kufundishana kuogelea, john akakumbuka kujitambulisha tena, "jinalangu ni john sailas…" macho ya john na yule msichana yakaangaliana. John akauhisi moyo wake ukipiga kwa kasi. Akakijua kilichopo moyoni mwake dhidi ya msichana huyo. "naitwa dina,"msichana alisema huku akionyesha tabasamu dogo lililojificha kwadhamira.
Ni siku ambayo john hakuisahau kamwe!

* * * **

aliacha kuliangalia pangaboi lililokuwa likizunguka nakukiangalia kiambaza cha varandani mwake. Akiwa hajaondoka kimawazokuzikumbuka siku za mwanzo alivyoonana na dina, john alizikumbukasiku hizo jinsi walivyokuwa wakipanga na wasichana hao siku zakuendelea kuwafundisha. Akiwa ameanza kwa kumfundisha dina kamamakubaliano yao yalivyo, john alijikuta akipata wakati mgumu wakutoonyesha hisia zake jinsi alivyokuwa akiteketea kimapenzi kwamsichana huyo hasa pale alipokuwa akiuzuia mwili wa dina kwa mikonoyake ambayo ilikuwa ikilaliwa na dina aliyekuwa akijilaza juu iliasizame wakati akimfundisha mbinu za kutumia mikono na miguu wakatiwa kuogelea. Kitendo hicho ambacho kilifanya mgusano wa mara kwa marakwenye matiti ya dina na ulaini wa tumbo la msichana huyo kukawakunampelekea john kwenye hisia za matamanio zaidi, isitoshe wakatimwingine dina alikuwa akionyesha woga wa kuzama na kujikutaakimkumbatia john. Kitendo cha mgusano wa miili yao kwa kukumbatiwana


dinakilimfanya john awe anajihisi kama anayepigwa na shoti ya umeme!kadri walivyokuwa wakizoeana, macho yao yakaanza kuonyesha ukweli wamambo kila walipokuwa wakitazamana. Ujumbe wa kuonyeshana kuwa wotewawili wanahitajiana ukawa dhahiri kati yao!
Siku moja johnakauvunja ukimya! "dina," john aliita wakati wakiwa ndani ya majiyaliyowafika kwenye vifua vyao wakiangaliana ana kwa ana. "natakauwe girl friend wangu!" ajabu ni kwamba, dina hakuonyesha mshitukona kauli hiyo, ikiwa ni kinyume na john alivyotarajia kuwa ingeletaubishano kati yao.


"nilijuaipo siku ungeniambia hivi," dina alisema na kuikunja miguu yakendani ya maji na kuanza kuelea na kichwa chake kuwa juu na hapo hapoakayapuliza nje maji yaliyoingia kinywani mwake. "nataka upajueninapoishi," john aliendelea. "tutapanga!" dina alisemakirahisi kama vile jambo hilo halikuwa na umuhimu kwake, kashaalianza kuogelea na kumuacha john akiwa amesimama palepalealipokuwa.


Hawakupanga!john alisita kulikumbushia, alihofia angeonekana anaharakisha mambo.dina naye akawa anaonyesha kama vile hakukuzungumzwa jambo la mapenzikati yao! John akaendelea kuwafundisha kuogelea wasichana hao hukudina akiwa kwenye hatua kubwa ya kujua kuogelea.
John akaonasubira yake inaweza ikamwangamiza. Akamvaa tena dina! "dina natakajumapili uje nyumbani kwangu!" john alimwambia dina kwenye simu,safari hii likawa sio ombi tena, bali ni mwendelezo wa kilealichokianza! "si tutaonana jumapili beach? Tutakapoonanatutalizungumza hilo," dina alijibu kwa utulivu. John akatambua yupokwenye kuyeyushwa na dina. Akakaza buti!
"jumapili sitokwendabeach," alisema. "nitaitumia siku hiyo kwa ajili ya kukusubiriwewe uje nyumbani."
"huoni kama utakapokuja beach utawezakunielekeza vizuri nyumbani kwako na tutakapoipanga siku itakuwa nisuala la mimi kuja moja kwa moja?"
"naishi kimara baruti,niambie ni saa ngapi utakuja hiyo jumapili ili nikusubiri kituoni?"john aliingiza karata ya ubishani. "john mbona hivyo?" dinaalilalamika. "nimekwambia tutakapoonana beach tutayazungumza yotehayo. Kwani una wasiwasi gani?" "kwa hiyo unanikatalia?" kimyakikajiunda kwenye simu.
"dina," john aliita.
"bee,"dina aliitika.
"kwa hiyo nijue hutaki?" john aliuliza.
Johnakamsikia dina kwenye simu akishusha pumzi.
"basi nitakuja saanne," hatimaye dina alikubali.
"nisubiri kituoni."
saanne! John aliwaza. Akaufikiria muda huo jinsi unavyotumiwa kwa sikuza jumapili kwa watu mbali mbali kupeana ahadi. Hakujua ni kwa niniulionekana ni muda bora kuliko muda mwingine! "utanikutanikikusubiri," john alisema.


Baadaya kukata mawasiliano, john akatambua zilikuwa zimebaki siku mbilikuiwezesha jumapili ifike! Akaomba ahadi ya dina iwe ya kweli naakamwomba mungu siku hiyo kusitokee tatizo lolote litakaloingiza doaahadi hiyo.


Jumapiliikafika, john akawa kituoni kabla ya saa nne. Akatarajia kumwona dinaakiwasili kwa daladala, akashangaa alipomwona akiteremka kutokakwenye teksi!
Ukawa mwanzo wa penzi lao, sasa wanataka kuoana!


** * * *

johnaliinuka kutoka pale varandani alipokuwa amekaa, akaichukua baruayake ya majibu na kuingia nayo chumbani kwake. Aliyafikiria maharialiyotajiwa, kidogo yalikuwa juu lakini hayakumwumiza kichwa.akafikiria namna ya kuzipeleka habari hizo kwa wazazi wake. Alijuaangelaumiwa kwa kiasi fulani kwa kuyafanya mambo kipeke yake hadikufikia hatua hiyo bila ya kuwahusisha wao. Hilo nalo halikumsumbuakichwa, wazazi wake hawakuwa wakiendekeza lawama zisizokuwa na tija.walikuwa waelewa na wenye ufahamu wa kuyajua mazingira tofauti. Simuyake ikaita. Alikuwa muddy, rafiki yake wa karibu sana.
"semamuddy," john alisema baada ya kuipokea simu.
"nakuja kwako,upo nyumbani?"
"wewe uko wapi?" john aliuliza.
"ninakama dakika tatu au mbili nitakuwa nimeshatia timuhapo
kwako."
"utanikuta," john alisema.
Muddyalimkuta john akilifunga jokofu lake baada ya kujimiminia maji yakunywa kwenye glasi na kuirudisha chupa.
"na mimi nahitaji hayomaji," muddy alisema na kwenda kuchukua glasi iliyokuwa ndani yakabati la vyombo la kisasa.
John aliyekuwa ameitoa tena nje yajokofu chupa ya maji aliyoitumia awali, alimmininia kwenye glasi majialiyokuwa akiyahitaji muddy. Muddy akayanywa maji akiwaamesimama.
"posa imejibu," john alisema.
"usiniambie!"muddy alisema huku akijifuta mdomo kwa kiganja chake na kuiweka glasijuu ya meza.
"subiri nikuletee barua yenyewe," john alisemaakiwa na furaha huku akielekea chumbani kwake.
Muddy aliisomabarua hiyo na kadri alivyokuwa akiendelea kuisoma, uso wakeulizidisha tabasamu hadi alipoimaliza.
"mwanangu unaoa!"alisema huku akiirudisha barua hiyo kwa john.
"ndiomanaake!"
"lakini mahari wamegonga!"
"kitu chenyewekile ghali."
"kweli mwanangu, dina mgogoro!"
wotewakacheka na kugongesheana mikono.
"umeshamwambia mwenyewe?"muddy aliuliza.
"nani, dina?"
"yeah."
"sijamwambia,lakini si atakuwa anajua?"
"hata kama anajua, kumwambia nakokuna raha yake."
"jioni atakuja, nitamwambia. Isitoshe ninampango wa kumnunulia na kumvisha pete ya uchumba, lakini hatutafanyasherehe yoyote."
"ahh, hebu mtwangie umpe news."
"unajuahata wazee bado sijawaambia!" john alisema.
"eti?" muddyaliuliza huku uso wake ukionyesha kutoamini kilealichokisikia.
"sijawaambia!"
"lakini si wanajua kuwaumechumbia?"
"hilo nalo sijawaambia!"
"hayo masiharajohn?"
"kweli sikuwaambia!"
muddy akaonekana kuchokaghafla, akakaa kwenye sofa. "yaani wewe siku zote hizi za mchakatowa kutaka kumchumbia dina, ina maana wazazi walikuwa hawajui?"aliuliza.
John akionekana kama aliyekosa amani, naye alijikutaakikaa kwenye sofa.
"leo nitakwenda kuwafahamisha,"alisema.
"duu!" muddy aliguna, kisha hakuendelea.
"lakiniwazazi ni waelewa, watanielewa tu." john alisema na sauti yakeilionyesha wazi alikuwa akijitetea.
"hivyo ulivyofanya kamadharau ya kiaina mwanangu," muddy alilalamika.
"wao ndiowatakaokuwa kila kitu kwenye harusi yako, halafu hawajui kamaumechumbia na wakati wanamjua dina. Hiyo noma nahaipendezi!"
"nitakwenda kuyaweka sawa, usiwe napresha."
"tatizo lako john unajiamini sana. Shauriyako!"
john akaamua kuyabadilishamazungumzo.

*****


mzee ken richard korogwe, tajirimaarufu jijini dar es salaam mwenye kumiliki meli mbili ndogo zamizigo zinazoitwa vidigidigi zinazosafirisha mizigo kwenye mwambao waafrika ya mashariki kama vile mombasa, zanzibar na comoro na ambayepia ni mmiliki wa malori ya mafuta na vituo vya mafuta kwenye maeneotofauti jijini na vingine vikiwa mikoani, ndiye baba mzazi warichard, mtoto pekee aliyezaa na mkewe kwa miaka thelathini na mitanowanayoishi ndani ya ndoa yao. Baada ya kuzaliwa richard, miakamichache baadaye mkewe aligundulika kuwa na matatizo
ya tumbo nakufanyiwa operesheni ya kuondolewa kizazi, hali iliyowafanya wabakina mtoto mmoja tu. Kubaki kuwa na mtoto mmoja kukawafanya yeye namkewe wamwone richard kama jicho lao, nembo na tunda la ndoayao.
Mzee ken na mkewe walihakikisha wanampa richard elimu iliyobora na kumfanya richard afanikiwe kupata shahada yake nchiniuingereza.
Mzee ken kitaaluma ni mhasibu, awali aliwahi kuajiriwakuwa mhasibu mkuu kwenye kampuni ya mafuta kwa miaka kadhaa kabla yakuteuliwakuwa mkurugenzi wa fedha na utawala kabla ya kuacha kazi nakufungua biashara zake.
Mafanikio ya richard kupata shahadayalitokana na umahiri wake
kwenye somo la hisabati nakulidhihirisha kurithi kipaji cha baba yake. Richard baada ya kupatashahada yake alirudi nchini na kujiunga na biashara za baba yake nakuwa mmoja wa viongozi kwenye kampuni inayomilikiwa na babayake.
Malezi yalimfanya richard awe na jeuri na kiburi chakudharau watu.
Ujio wa richard kwenye kampuni hiyo ya baba yakekukazua malalamiko ya kuwanyanyasa wafanyakazi na malalamiko hayoyakamfikia mzee ken. Lakini mzee huyo kutokana na shinikizo kutokakwa mkewe ambaye ni
mama yake richard, akawa anashindwakumchukulia hatua kali mwanae, badala yake akawa anamsihi asiweanawanyanyasa wafanyakazi hasa wa ngazi ya chini. Usia wake ukasaidiakupunguza kwa kiasi fulani manyanyaso hayo, lakini haukumaliza dharauza kijana huyo aliyekuwa akiringia utajiri wa baba yake na elimualiyokuwa nayo. Baadhi ya wafanyakazi walilazimika kuacha kazi kwaajili yake, ikawa inamlazimu mzee ken apate kazi ya kuziba nafasizinazoachwa kwa kuajiri wafanyakazi wengine
kila matukio hayoyalipojileta!
Richard alikuwa haiishi na wazazi wake, alikuwaakiishi kwenye moja ya nyumba nzuri zilizokuwa zikimilikiwa na babayake iliyopo eneo la mlalakuwa. Huko ndiko alikokuwa akiutumia mudawake na rafiki yake wa kike judi, hadi walipokorofishana kuhusiana namasuala ya ndoa!

* * * * *

kitendo cha richard kukataakumuoa kilimdhihirishia judi kuwa alikuwa ahitajiki tena na richard!jambo hilo lilimpa wakati mgumu, likakatisha tamaa mustakabali wahatima ya maisha yake ya ndoa kuishi na richard.
Alimpendarichard, alimpenda si kwa sababu ni mtoto wa tajiri, lakini piaalimpenda kwa sababu ni kweli alikuwa akimpenda! Alimheshimu kwa kilahali. Alimfanya aikatae mialiko ya kumtaka kimapenzi aliyokuwaakipewa na wanaume tofauti wenye uwezo wa juu wa kimaisha. Kamwehakutarajia kama ingetokea siku richard angemtamkia kauli kamahiyo!
Lilikuwa pigo kwake!
Ingawa richard alijaribukumbembeleza waendelee kuwa wapenzi, lakini kwa kutoa sharti lakutofunga ndoa wakati alipokuwa akijaribu kumfafanulia uamuzi wakehuo wa kutomuoa, hata hivyo judi hakuliridhia ombi hilo ingawa alijuakama angelikubali lingetoa nafasi nyingine ya kuendelea kufaidikakupata huduma za richard. Judi alikiri kama angekubaliana na ombihilo angekuwa sawa na kukubali kutumika kingono huku akijua haolewi!ingawa alikiri, endapo angekubaliana na ombi hilo la richard ingekuwani nafasi yake ya kuweza kuificha siri ya kukataliwa kwake kuolewa,lakini pia, kungewezesha kuendelea kuwakomoa kwa kuwaumiza wanawakewenzake waliokuwa wakimwonea wivu. Hata hivyo aliuona uamuzi wakukubali kuendelea kuwa hawara wa richard usingemsaidia.
Hakuwatayari kuchezewa kisa tu, aonekane na wanawake wenzake kuwaamemdhibiti richard! Alichokihitaji ni ndoa na sio kuchezewa!
Uamuzihuo wa richard wa kukataa kumuoa ulimwumiza kila
alipoikumbukakauli hiyo iliyokana kumuoa na wakati mwingine ilifanya aina yamwangi uliomtesa kichwani mwake. Aliiona ni aina ya dharaualiyofanyiwa na alikuwa hakujiandaa na tukio la aina hiyo kutokana nakujiamini kwa asilimia zote kuwa, alikuwa ni chaguo la richard! Judialijijua kuwa ni mmoja kati ya wanawake wenye sifa za uzuri na mwenyemvuto kiasi cha kujiona alikuwa ni chaguo maridhawa kwa mtu aina yarichard. Alikumbuka jinsi alivyokuwa hakusita kuonyesha dalili zakumkubalia wakati richard alipokuwa akimzengea siku za nyuma kablahawajafikia kuwa na mahusiano ya kimapenzi. Na baada ya kuwa wapenzi,urafiki wao ukawa wa wazi, popote walipokwenda walikuwa pamoja.uhusiano wao ukawa sehemu ya mazungumzo kwa vijana wenye
umri waohususan wasichana ambao wengine hawakuzificha hisia zao za kumwoneawivu.
Viongozi wenye vyeo tofauti, serikalini, mashirika binafsina taasisi
nyinginezo walikuwa wakimjua richard kuwa ni mtoto wamzee ken, mfanyabiashara tajiri. Na kila walipokuwa wakikutana nayewakati akiwa na judi, richard hakusita kutoa ujulisho kuwa, judi nirafiki yake wa kike!
Ujulisho huo ukampa judi umaarufu wakujulikana kama mchumba wa richard. Ukamzidishia kupata marafikiwaliojikomba kwake na wakaibuka vile vile waliokuwa wakimwoneadonge!
Umaarufu wa kujulikana kwake ulimfanya apewe kipaumbelekwa
kuletewa kadi kadhaa za mialiko kutoka kwa watu mbalimbaliwenye daraja la juu kimaisha, zilizokuwa zikimtaka ahudhurie vikaovya harusi, michango ya sherehe na harambee nyingine tofauti. Namahudhurio yake katika shughuli kama hizo yalikuwa yakitukuzwa kwakupokewa kama mtu maalumu. Judi alikiri heshima zote alizokuwaakizipata zilitokana na uhusiano wake wa kuwa na richard ubavunimwake! Akajiuliza, kwa nini richard alitumia nguvu zote zakumtambulisha kwa watu mbalimbali
kisha aje kumtosa kirahisihivyo?
Ilimuuma!
Ilimuuma kwa sababu hakuijua sababuiliyomfanya richard akatae
kumuoa. Moyo wake ulipata tabu yakuamini labda kuna mwanamke mwingine ambaye richard alipanga kumuoa.alishindwa kuliamini hilo kutokana na ukweli wa mzunguko wa maishaaliyoishi akiwa na richard.
Richard alikuwa akimtimizia kilaalichokuwa akikihitaji, lakini pia,
aliweza hata kumfungulia benkiakaunti yenye kiwango kizuri cha pesa huku akaunti yake ya zamaniikiendelea kuwepo.
Judi alizidi kutatizwa na tukio la kukataliwakuolewa na richard ilhali richard tokea awali alikuwa akimwonyeshadalili zote kuwa alikuwa akimpenda na hakuwahi kumfanyia visa vyaaina yoyote pamoja na kuzungukwa na hisia za kumhisi kuwa anawanawake wengine.
Kwa nini richard amekataa kunioa? Swali hilolikabaki kuwa mwiba
uliomwumiza moyoni kila alipojiuliza!
Judihakuwa mtoto wa maskini, lakini pia hakuwa mtoto wa tajiri. Wazaziwake wote wawili walikuwa wasomi na wenye uwezo wa pesa wa kawaidauliotokana na ajira zao wakiwa ni watawala makazini wanakofanyiakazi.
Maisha hayo ya wazazi wake ambao anaishi nao kwenye nyumbanzuri waliyoijenga eneo la makongo na yeye mwenyewe kupewa elimu yakutosha iliyompatia kazi nzuri, aliamini yangeweza kumsaidia kumuwekakwenye uamuzi wa kuachana na richard, kisha angejenga subira kwakutoa nafasi kwa mwanamume mwingine msomi mwenye kazi nzuri na maishamazuri
kujitokeza ambaye atakuwa na mapenzi ya dhati na hatimayekufunga naye ndoa.
Kwa kuupitisha uamuzi huo, judi akajiandaakupambana na wakati
mgumu wakati uhusiano wake na richardutakapojulikana kuwa
umevunjika. Alijua wapo watu ambaowangemkabili bila ya aibu na
kumwuliza ukweli wa jambo hilo. Nawengine wangetaka kuijua hata sababu ya uhusiano wao kuvunjika, wengiwao wakiwa ni wanawake!
Wanawake! Judi aliwaza. Kweli tunamatatizo!


* * * * *

ofisi za kampuni ya mzee kenzipo kwenye jengo moja maarufu jijini dar es salaam lililokuwa namaofisi mengine ya makampuni tofauti lililoko katikati ya jiji. Ofisiza kampuni yake zilikuwa kwenye ghorofa ya nne ndani ya jengo hilolenye ghorofa zaidi ya kumi na mbili. Mzee ken mwenyewe alishikiliavyeo vya mkurugenzi mtendaji na mhasibu mkuu huku mwanae richardakiwa ni mkaguzi wa ndani wa mahesabu.
Asubuhi ya siku hiyorichard aliingia ofisini na kumkuta karani wake wa kike akiwashughulini na kompyuta.
"niitie rama!" richard alimwambiakarani wake bila ya kutanguliza salamu yoyote, alionyesha kisiraniasubuhi hiyo na sauti yake ilifanya amri.
Karani huyo aliyeitwarehema alimwangalia richard na kugundua bosi wake yupo kwenyekisirani asubuhi hiyo. Alikuwa akizijua vizuri tabia za richard naalikwishazizoea na kumzoea richard mwenyewe. Aliubinua mdomo wake kwaaina ya dharau wakati richard akiingia ofisini kwake.
Rama ambayeni dereva anayetumiwa mara kwa mara kuliendesha gari la richard paleanapohitajika dereva wa kuliendesha, umri wake ulikuwa wa mtu mzimaaliyevuka miaka hamsini. Wafanyakazi wote kasoro richard, walikuwawakimuita kwa jina la ‘mzee rama.' mara zote alikuwa akivaa kofiaya baragashea na suti ya kaunda yenye rangi ya ugoro ambayo ni sareyake ya kazini. Alifika ofisini kwa rehema kuitikia mwito, akasimamambele ya meza aliyokuwepo rehema.
"umesema bosi ananiita?"mzee rama aliuliza.
"yuko ndani!" rehema alisema kwa sautiiliyoonyesha kumchukia richard.
"na leo uangalie, naona jamaahakuamka vizuri!"
macho yaliyoonyesha woga yakajitokeza usonikwa mzee rama, akajikuta akiuangalia mlango wa ofisi ya richard kamavile richard angejitokeza muda huo huo. Akaurudisha uso wake kwarehema kasha akaiinamia meza na kujizuia kwa mhimili wa mikonoyake.
"kwani anasemaje?" alinong'ona huku akiwa ametengenezakibyongo mgongoni
mwake. Sauti yake haikufanya mzaha, alionyeshadhahiri alikuwa akimwogopa richard.
"mi, ntajuaje?" rehemaalimshushua mzee rama kwa kumpa jibu la mkato. Kisha akaendelea, "nawewe mzee acha woga! Unamwogopa huyo richard utadhani ni munguwako!"
mzee rama akajaribu kutengeneza tabasamu lililokataausoni kwake.
"huyu kijana ni mkorofi sana!" alisema.
"hee!unaanza kuogopa kabla hujajua anachotaka kukwambia? Huyu si kamamwanao tu! Naona siku atakayokwambia kibarua kimeisha, utarudishwanyumbani ukiwa maiti!"
mzee rama akajichekesha. "wewe mtotoacha maneno ya uchuro!" alisema huku akiendeleakujichekesha.
Mlango wa ofisi ya richard ukafunguliwa, richardakatokeza! Mzee rama akashituka, akaganda pale alipokuwa, akabadilikakama siye yeye aliyekuwa akizungumza. Kujichekesha kukayeyuka,akauchuna uso kama samaki aliyekaushwa! Rehema akawa anaumia mbavunikwa kujizuia kucheka huku akijitahidi kuendelea na kazi kwenyekompyuta kama vile hajui kinachoendelea.
Richard alikuwa amekamatafunguo za gari mkononi, akamwangalia mzee rama, kisha bila yakusimama akamtupia funguo hizo, zikampiga mzee rama maungoni nakuangukia miguuni mwake huku akihangaika kutaka kuzidaka.
"kalikoshegari langu!" richard alisema bila ya kugeuka nyuma, akatokahukuakimuacha mzee rama ameinama akiziokota funguo alizotupiwa.
Baadaya richard kutoka nje ya ofisi, rehema alisikitika peke yake nakulalamika kwa hasira, "huyu baba huyu!" kisha asiendelee.
Usowa mzee rama ulikuwa bado umejengwa na hofu ya nidhamu ya woga,akamwangalia rehema na kusema, "wacha nitoke, asije akarudi nakunikuta!"
rehema alimwangalia mzee rama alivyokuwa akitokakisha akaendelea tena kusikitika peke yake. Akajisemea moyoni: Laitiningetupiwa mimi funguo zile, nami ningeziokota na kumrudishia kwakumtupia nazo na kazi leo hii ningeacha!


* * * * *

mzeeken alimaliza kifungua kinywa akiwa na mkewe kwenye meza ya chakula,wote wawili wakiwa wamejiandaa kutoka, kila mmoja na safari yake nausafiri wake.
"unakumbuka leo kuna kikao kingine cha harusi?"mkewe alisema.
"nakumbuka lakini sitokwenda!" mzee kenalijibu.
"kikao kilichopita hukwenda na hiki pia huendi?"
"leomchana nitakuwa kwenye mkutano utakaokutanisha
wafanyabiashara wahapa nchini na ujumbe maalumu wa kibiashara kutoka uturukiunaoongozwa na waziri wao wa biashara aliyewasili hapa nchini jana.ukienda wewe inatosha, sio lazima wote tufike."
"sawa, basinitamfahamisha adam kuwa na leo hutofika."
"na mimi baadayenitampigia simu kumjulisha kuwa sitofika," mzee
ken alisema hukuakionyesha kutaka kuondoka.
Mkewe akamwangalia kwa sura yenyejambo. "una haraka sana?"
aliuliza.
"kwani vipi?"
"kunakitu nataka kuzungumza na wewe!"
kauli hiyo ikamfanya mzee kenatulie na kumwangalia mkewe kwa
utulivu. "kinahusiana na hichokikao cha harusi?" aliuliza.
"hapana. Kinamhusu richard!"
"ananini?"
"hivi richard anataka mpaka mmoja wetu afe ndioaoe?"
swali hilo kidogo lilionyesha kama kumchanganya mzeeken,
akaonyesha uso wenye mshangao. "kwa nini unasema hivyo?"aliuliza.
"ulishawahi kumshauri lolote kuhusu suala la kuoa?"mkewe aliuliza swali badala ya kujibu swali.
"mbona sijakuelewaunachotaka kukizungumza?"
"nataka kujua ni lini richardatapata wazo la kuoa?"
"nadhani hilo ni suala lake binafsi.kwa nini usimwulize?"
"najua ni suala lake binafsi, lakinisisi wazazi wake ni jukumu letu
kumshauri au kujua mawazo yakekuhusu jambo hilo. Unadhani yeye na judi wataishi maisha ya uhawarampaka lini? Wamekwishakaa hivyo kwa muda mrefu, nadhani sasa umefikawakati wa kumshauri afunge ndoa na mwenzake."
mzee ken hakufanyaharaka ya kujibu. Alionekana kutafakari huku
akivigonga vidolevyake juu ya meza.
"ni vyema tukamshauri hivyo," mkewe akawahikusema kabla ya
mzee ken hajajibu na kuichukua nafasi hiyokulieleza alilotaka kulieleza.
"ukaaji wao wa uhawara kwa mudamrefu unaweza ukawafikisha
kwenye vishawishi vingine vinavyowezakuwaingiza kwenye migogoro itakayowafikisha kuachana. Matokeo yake,richard anaweza akadakwa na shangingi. Akapungwa vilivyo na hatimayekudai kumuoa. Si unawajua wanawake wa mijini walivyo werevu hasawakishanusa harufu ya fedha.
Wakijua richard ni mwanao unadhaniwatamwachia? Watahakikisha wanamdhibiti hata kama ikibidi kwenda kwawaganga ili mradi wamuinamishe, kama wenyewe wanayosema kulishwalimbwata. Usije ukashangaa ukamwona mwanao akatuletea mwanamke ambayesiye na akadai kutaka kumuoa!"
"unayoongea ni kweli, lakinipia tunatakiwa tuangalie na upande wa pili. Inawezekana wenyewewakawa hawajapanga hivyo."
"kuna ubaya gani tukiwashaurihivyo? Utajuaje ikiwa hujakaa na
mwanao na kuzungumza naye?"
"kwahiyo, unachokitaka nikae na richard ili nimwulize kama ana
mpangowowote wa kuoana na judi? Au nimwulize kama ana mpango wowote wakuoa?"
"sasa ni yupi mwingine wa kumuoa zaidi ya judi? Judindiye
tunayemfahamu na hata wewe mwenyewe umekwisha kumsifiakuhusu tabia zake. Kwanza ana elimu nzuri, kazi nzuri na tabia yakeni nzuri. Ni yupi mwingine zaidi yake? Richard atakaponiletea kirukanjia unafikiri nitakubaliana naye?"
"sawa," mzee ken alisemakwa sauti ndogo.
"usiitikie kama vile nakulazimisha!" mkewealisema huku akionyesha kuugundua unyonge ulioonyeshwa kwenye sautiya mumewe. "we huoni fahari endapo richard ataoa sisi tukiwa hai?au hujisikii vibaya kila baada ya muda tunaletewa kadi za kuhudhuriavikao vya harusi za wenzetu wanaotaka kuozesha watoto wao? Sisi kaziyetu itakuwa ni kuwachangia hadi lini? Na sisi tutachangiwa lini? Auunataka tuchangiwe michango ya sanda badala ya harusi? Aaa bwana,lazima ifikie mahali na sisi tuchangiwe, na sisi tusikie faharikumwona mtoto wetu anaoa. Nimeshachoka kuwapigia watoto wa wenzanguvigelegele, nataka na mimi mtoto wangu apigiwe vigelegele!"
"sasalawama za nini tena mke wangu? Umeongeanimekukubalia!
Nimekwishakwambia nitakwenda kuzungumza na richardasubuhi hii ili tumsikilize na yeye ana maoni gani!"

richardhataki kumuoa judi, mama rich anaulizia mwanae anaoa lini?? Mzeerichard ameahidi kuzungumza na mwanae juu ya hilo.
Kwanini richardhataki kumuoa judy??
Nini hatma ya ndoa ya john na dina???
 
Mtunzi: Beka mfaume.

Sehemu ya tatu

Richard baada ya kumtupia funguo mzee rama na kutoka ofisini, alielekea mojakwa moja hadi ilipo ofisi ya baba yake. Aliingia na kumkuta katibumuhtasi wa baba yake ambaye ni mama wa makamo, akamsalimia kwakiingereza kwa dhamira ya kukwepa kutoa shikamoo.
"baba yupo?"richard aliuliza baada ya kusalimia, wakati huo huo akauangaliamlango wa ofisi ya mzee ken. "bado hajafika," mama huyo alijibuhuku akimwangalia richard usoni.


Richardakashukuru na kutoka. Akaelekea kwenye korido inayoelekea kwenyelifti, akaisikia kengele ya lifti inayoashiria kuwasili kwa liftikwenye ghorofa hiyo na kuusikia mlango wake ukijifungua. Wakatokawatu wawili, mzee ken na dereva wake aliyekuwa amebeba mkoba waofisini. Richard akasimama.
"nimetokea kukuulizia sasa hivi,"richard alisema na kumsalimia baba yake baada ya kukaribiana hukudereva wa baba yake akisalimiana naye bila ya kusimama.
"vipiuna tatizo?" mzee ken aliuliza.
"nilikuja kuhusu masuala yaleya tra."
"bado sijayamaliza, nitakujulisha yakiwatayari."
"halafu pia, nilitaka kutoka na huenda nikachelewakidogo kurudi,"


richardalisema kwa kujiamini, akauparaza mkono wake kwenye mgongo wa taiiliyompendeza.
"kabla hujatoka, kwanza nataka tuzungumze,"mzee ken alisema na kuondoka. Kauli hiyo ikamlazimisha richardamfuate baba yake. Wakati wakianza kuingia kwenye ofisi yakatibu muhtasi, wakapishana na dereva wa mzee ken aliyekuwa akitoka.richard akatangulia kuingia ofisini kwa baba yake wakati mzee kenakiwa amesimama akisalimiana na katibu muhtasi wake. Wakiwa ofisini,mzee ken akiwa amekaa nyuma ya meza yake ya thamani na richard akiwaamekaa mbele kwenye sofa ya wageni, mzee ken alianza kwa kusema,"mama yako..," akasita ghafla. Akabadilisha kauli, "kuna jambotumelijadili mimi na mama yako, na tumeona ni wajibu wetu kukushauri,hata kama jambo hilo litakuwa linaingiliana na maisha yako binafsi,"hapa alinyamaza na kumwangalia kwa utulivu richard. Kisha akasema,"richard, mna mpango wowote wa kuoana, wewe na judi?"


Swali hilo likaonekana ni la ghafla kwa richard aliyeonyesha dhahirikutolitarajia. Kwa sekunde kadhaa alionekana akiwa kwenye wakatimgumu wa kuweza kulijibu. Akakumbuka kuulizwa swali kama hilo na judisiku chache zilizopita.
"hatuna mpango wowote," hatimayerichard alijibu.
"kwa hiyo mtaishi kwenye uhawara mpaka lini? Auhamna mpango hata wa kutangaziana kuwa ni wachumba?"
richardakajenga ukimya mwingine. Kisha aliinua kichwa chake kumwangalia babayake. "nitakapokuwa tayari kuhusu suala hilo nitawaelezeni,"alisema. "sipingani na kauli yako, lakini napata shida kuamini kamakwa kipindi chote mlivyoishi pamoja mkiwa marafiki mtakuwa hamjawahikujadiliana jambo hilo?" swali hilo likaonyesha kumpa tena wakatimgumu richard. Akakitengeneza kimya kingine.
"tulishawahikulijadili," hatimaye richard alisema.
Safari hii mzee kenhakuingiza neno. Akamwonyesha richard kuwa anasubiri maelezo zaidi yajambo alilolizungumza.
"lakini hatukuelewana!" richard alisemahuku akiiangalia sakafu ya vigae ing'aayo.
"kwanini?"
"nilimkatalia!"
"nadhani sijakuelewa vizuri!ulimkatalia…?" mzee ken alisema huku akionyesha kutokiaminialichokisikia.
"nilimwambia sina mpango wa kumuoa!"
kaulihiyo ikakamilisha mshituko wa mzee ken, hata hivyo utulivu wakealiouonyesha uliweza kuuficha mshituko wake.
"judi alisemajebaada ya kumtamkia hivyo?" mzee ken aliuliza na alijaribu kujiwekakwenye utulivu zaidi.

Safari hii richard aliuinua uso wake nakumwangalia baba yake, kisha aliinama tena kuiangalia sakafu."hatukuwa na maelewano tena!" alisema na kunyamaza. Ghaflaakaendelea, "sasa hivi hatuko pamoja!"
bila ya kutarajia, mzeeken alijikuta akishusha pumzi kwa nguvu. Akaikumbuka kauli ya mkeweiliyoonya hatari ya richard kuangukia kwenye mikono ya shangingi."kama ulijiona huna mpango wa kumuoa karibuni, kwa niniusingemweleza ukweli kuwa, kwa sasa hivi huna mpango huo, lakiniungempa matumaini ya baadaye!" mzee ken alisema huku akionyeshawazi kutoridhika na maamuzi hayo ya mwanae na hata sauti yakeilifanya mkwaruzo. "kwa nini umweleze kuwa huna mpango wakumuoa?"
"nilimweleza hivyo kwa sababu sio chaguolangu!"
"jesus!" mzee ken alihamanika na kushindwa kuaminikuisikia kauli hiyo ikitoka kwa mwanae. "kwa hiyo chaguo lako ninani?"
"dina!" richard alisema bila ya kutafunamaneno.
"dina?" mzee ken aliuliza huku akiwa amepigwa nabutwaa na hofu ya kuwa analetewa shangingi aliyetabiriwa na mkeweikiwa imekwisha kumvaa. "ni nani huyo dina?" safari hii sautiyake aliipandisha kidogo.
"sisi tunamjua?" aliuliza kwa lughaya kiingereza.
"dina nzasa. Mama anamjua!"


* * * **

usiku baada ya mkewe kurudi kutoka kwenye kikao cha harusina yeye kurudi kutoka kwenye mkutano, wakiwa tena kwenye meza yachakula, baada ya kumaliza kula ndipo mzee ken alipomwelezea mkeweyaliyojiri kwenye mazungumzo kati yake na richard.
"na anasemaunamjua huyo dina!" mzee ken alimalizia.
"dina nzasa…dinanzasa…" mkewe alijaribu kuvuta kumbukumbu.
"ah,nimekwishamfahamu!" alisema na uso wake kujaa nuru. "si yulebinti wa bwana nzasa anayeishi karibu na duka la vinywaji hapa mtaawa nyuma yetu?"
"nzasa yupi?" mzee ken aliuliza hukuakionyesha bado hajamtambua mtu anayefahamishwa.
"nzasa huyualiyekuwa mwenyekiti wa bodi ya utalii, sasa hivi amestaafu. Ana kamamiaka miwili tokea astaafu. Mkewe ni huyu dada anayefanya kazi ardhiambaye alitusaidia kupata hati ya umiliki wa kiwanja chetu kilichopoboko. Mara hii umekwisha kumsahau?"
"nimekwisha kumkumbuka!"mzee ken alisema. "si huyu aliyekuwa
akimtuma binti yake hapanyumbani kutuletea zile nyaraka…"
"haswaa!" mkewealidakia. "basi ndiye huyo anayeitwa dina!" kisha sauti yakeikatulia na kuendelea, "dina anavyoonekana ni msichana aliyetuliana miye nilikuwa sijui kama wana uhusiano wowote na richard. Aurichard alikwambia kama nilikuwa naujua uhusiano wao?"
"yeyealisema, wewe unamjua dina."
"ni kweli namjua! Richardjamani!" mkewe mzee ken akapiga kite cha kuhamanika. Kisha akasemakwa sauti ya kuhuzunisha, "hili la richard kusema eti judi siochaguo lake, kwa kweli limeniumiza mno. Unajua nashindwa kumwelewamwanao! Alimtongozaje kama sio chaguo lake? Inahuzunisha kumwonamwanangu amempotezea muda wake yule msichana, kwa kweli siamini!maskini judi, nilikuwa nampenda huyu binti wa watu na yeye mwenyewealikuwa anampenda sana richard. Hivi nitamwangaliaje sikututakapokutana?" mke wa mzee ken akaonyesha kukata tamaa. "ndiohivyo, hatuwezi tukayaingilia maamuzi ya richard. Yeye ndiyeanayemjua vizuri judi kuliko tunavyomjua sisi na hatujui kwa niniamemchagua dina, labda ndiye aliyemwona anamfaa. Pengine amependezwana tabia zake!"
"lakini kuna tatizo jingine linaloumiza kichwakuliko hilo," mzee ken alisema, kisha kabla ya kuendeleaaliinamisha kichwa na kusikitika.
"ni mtafaruku juu yamtafaruku," alisema. Mkewe mzee ken akaingiwa na mshangao,akasubiri kusikia mumewe atasema nini.
"dina hamtaki richard!"mzee ken alisema kwa msisitizo.
Mkewe mzee ken akaishiwa nguvu!"amekwambia richard mwenyewe?" aliuliza kama asiyeaminialichokisikia.
"yeye mwenyewe richard ameniambia, tena bila yawasiwasi wowote!
Anasema amejitahidi sana kumbembeleza dina kwakutumia mbinu tofauti lakini anadai dina alikataa katakata kukubalikuolewa naye. Cha ajabu mwanao bado anasisitiza kuwa, dina ndiyechaguo lake!"
"huyu mtoto ana wazimu?" mke wa mzee kenaling'aka. "mwanamke amemkataa si basi!"
"labda ana sababuya kumng'ang'ania."
"hawa watoto wetu wa siku hiziwatatuua kwa presha. Kama mwanamke amekukataa si unatafuta mchumbamwingine wa kuja kumuoa?"
"naona unayazungumza mamboyaliyopitwa na wakati mke wangu. Hayo unayoyazungumza ni ya enzizetu, enzi zetu unatafutiwa mchumba halafu unaonyeshwa, baadayeunaulizwa kama umemkubali au umemkataa. Ukisema humtaki, basiunatafutiwa mchumba mwingine. Leo hakuna hilo. Wenyewe kwa wenyewewanatafutana huko huko wanapoonana na wakishakubaliana kuoana ndipowanapokuja kwetu na kutufahamisha na mara nyingine hata kama wazaziwakikataa, wao wanalazimisha kuoana.
Lakini hili la mwanaolimekuja kiaina yake, mwanao hatakiwi, yeye analazimisha!utaliingiliaje jambo kama hilo?"
"tena umenikumbusha babarichard!" mkewe mzee ken alisema.
"nakumbuka mama yake huyumsichana aliwahi kuniambia yuko mbioni kutaka kumwozesha bintiyake…ndio nakumbuka! Aliniambia angeniletea na kadi yamchango!"
"binti yake yupi?"
"nadhani atakuwa ni huyuhuyu dina."
"anataka kuolewa na nani?"
"sijui."
usowa mzee ken ukaangukia kwenye mshangao. "ina maana richard
hajuikama huyo anayetaka kumuoa kuwa anaolewa na mtu mwingine?"aliuliza.
"sijui. Naona huyu mtoto anatakakutuchanganya!"
"wacha niongee naye sasa hivi!" mzee kenalisema na kuichukua simu yake ya mkononi iliyokuwa mezani. Akampigiarichard.
Kimya kilipita kati yao wakati mzee ken akisubirikujibiwa kwenye simu aliyoipiga. Hatimaye mzee ken alijitikisa mwilina kusema, "richard! Mbona huyu msichana uliyemzungumza kumbe nayeanataka kuolewa?"
"najua!" richard alijibu kutoka upande wapili wa simu.
"lakini ni yeye ndiye niliyempenda na moyo wanguunaniuma kuona anaolewa na
mtu mwingine!" richardalisema.
"nitakupigia baadaye!" mzee ken alisema na papohapoalikata simu. Akamwangalia mkewe, "unajua huyu mtoto hovyo sana!"aling'aka.
"kwani anasemaje?"
"anasema analijua jambohilo!"
"jambo gani?"
"la dina kuolewa!"
"ebo!"mkewe mzee ken alisema kwa mshangao.
"ndivyo anavyodai! Halafuanaendelea kusema, eti huyo ndiye aliyempenda na moyo wake unamuumasana kuona anaolewa na mtu mwingine! Huyu mtoto ana wazimu?"
"amakweli moyo ukipenda..!" mkewe alisema bila yakumalizia.
Akasikitika peke yake.
"sasa ana maana gani kusemahivi?" mzee ken aling'aka tena.
Mkewe akafikiri, kishaakasema, "hawa watoto wetu wa siku hizi si ajabu ukasikia amefanyajambo la ajabu kwa vitu vya kipuuzi kama hivi!"
mzee kenakamwangalia mkewe kwa kushituka. "una maana gani?"aliuliza.
"lakini sidhani kwa richard kama anaweza akafanyaupuuzi wa aina hiyo," mkewe alisema huku akijaribu kuituliza sautiyake.
"upuuzi gani?" mzee ken aliuliza huku akionyesha kamavile alikuwa akikijua kinachotaka kutamkwa na mkewe.
"anawezaakajiua!"
"ohoo, sasa mke wangu unaongea nini!" mzee kenalihamanika.
"khee! Unashangaa hilo? Kwa nini asiweze? Hawawatoto wetu wa leo wana akili? Au unafikiri huko kusoma nje ndiokutamfanya asiweze kufanya upuuzi wa aina hiyo?"
"sasa kwamfano akiung'ang'ania huo upuuzi wa kutakakumuoa
tutafanyaje?"
"itabidi tukaingize fitna ili dinaasiolewe na huyo anayetaka kumuoa!"
"halafu?"
"aolewena richard!"
"wakati huyo dina kishamwambia wazi mwanao kuwahamtaki?"
"yeye dina ni nani hadi awe na jeuri hiyo?" mke wamzee ken alisema kwa sauti ya dharau.
"sasautafanyaje?"
"sijajua, lakini naweza nikaivuruga ndoa yakeasiolewe na huyo anayetaka kumuoa, kisha nikakigeuza kibao mwanangurichard akageuka kuwa mume wa kuja kumuoa dina. Babu, mwanamkemwenzake ni
mwanamke, asikwambie mtu!"
"utakwenda kumwambianini huyo dina ili akuelewe unachokizungumza?"
"sina muda wakuongea naye!" mke wa mzee ken alisema kijeuri na kubenua mdomowake.
"kumbe utakwenda kuongea na nani?" mzee ken aliuliza kwakauli iliyoonekana kama kitu anachokizungumzia ni kigumukufanyika.
"mama yake!"
"tutakuwa tumefanya dhambi!"mzee ken alisema bila ya kumwangalia mkewe machoni.
"kwa hiyoupo tayari mwanao ajiue?"

mzee ken akaduwaa na kumwangaliamkewe. "lakini hajasema kama atajiua!" alisema.
"anayetakakujiua anasema? Naomba hili jambo uniachie mimi!"
mzee kenalishusha pumzi, akakosa la kusema.
"hivi, kama richard anatakakumuoa dina, kwa nini ishindikane kumuoa?" mkewe mzee ken alisemakwa sauti ya kiburi. "marafiki zetu watatuelewaje wakisikia kuwatumeshindwa kutumia uwezo wetu wa utajiri kuishawishi familiatuliyoizidi kipato kukubali binti yao aolewe na mtoto wetu? Mumeweyule mama sasa hivi hana kitu! Mafao yake ya kustaafu alikwendakuyanunulia shamba, shamba limewashinda na nasikia wameliuza auwanataka kuliuza. Sasa hivi yule mama ndiye mlishaji wa nyumba kwakutegemea hicho kibarua chake cha huko ardhi, sijui ana kicheo gani!we si umeona baada ya kutufanikishia kuipata hati ya kiwanja chaboko, mbona zile laki tatu tulizompa kama ahsantehakuzikataa?
Azikatae ana jeuri hiyo?"
mzee ken akabaki kuwabubu.
"na sitaki umwambie richard lolote!" mkewe alionya."niwachie mimi mambo yote nitayaweka sawa."

******

ilikuwausiku muda mfupi baada ya taarifa habari kutoka kwenye runingakumalizika, mama yake dina aliusikia mngurumo wa gari inayosimama njeya nyumba yao, kisha akasikia mlio wa mlango wa gari uliofungwa.akajua ni mgeni wa hapo nyumbani.
"nadhani kuna mgeni," mzeenzasa alisema akiwa amekaa sebuleni kwenye sofa akiangaliaruninga.
Mama yake dina aliinuka kutoka kwenye sofa akaendamlangoni.
"hodi!" sauti ya mwanamke ilisikika kutoka nje akiwaamekwishaingia ndani ya uzio wa nyumba hiyo kupitia kwenye geti dogolililokuwa wazi.
"karibu," mama yake dina aliitikia akiwandani, akaufungua mlango wa mbele. "oh, karibu mama richard,"alisema.
"ahsante mama dina," mke wa mzee ken alisema nakuingia ndani.
"karibu mama, karibu!" mzee nzasa alisemaalipomwona mke wa mzee ken.
"ahsante shemeji," mama richardalisema na kumpa mkono mzee nzasa na kusalimiana naye kabla ya kukaakwenye sofa.
"gari umeiacha na mtu nje?" mama dinaaliuliza.
"hapana."
"hakuna haja ya kutia wasiwasi,vibaka hawapitipiti kwenye mtaa huu," mzee nzasa alisema. "wachaniwapisheni."
"ah, hapana shemeji, mbona nimekuja kwamazungumzo ya kawaida
tu," mama richard alisema.
"lakini siumekuja kwa ajili ya kumwona mwenzako?"
"ni kweli, lakini siofaragha."
"usijali, nitaangalia tv ya chumbani, nyieendeleeni," mzee nzasa alisema na kuondoka.
"ehee, za sikumbili, tatu mama richard?" mama dina aliuliza baada ya mzee nzasakuondoka.
"nzuri tu, za kwenu?"
"sisi hatujambo,karibu."
"dina yupo?" mama richard aliuliza na kuangaliaupande wenye korido ambako kuna vyumba.
"yupo chumbani kwakeanaangalia tv."
"kilichonileta kwako mama dina," mamarichard alisema.
"nakumbuka uliwahi kuniambia unataka kumwozeshabinti yako na ungeniletea kadi ya mchango. Nimeifuata hiyokadi."
"kadi za mchango bado sijaanza kutoa mama richard,nikitoa nitakupitishia. Wala usitie shaka."
"ukweli ni kwambanilianza kutia shaka, nikasema mhh, huyu mama dina si aliniambiaanataka kumwozesha binti yake na angenipitishia kadi ya mchango?mbona kimya? Ndio nimeamua kuja mwenzangu, pengineumenisahau."
"sijakusahau mama richard, nasubiri tu mamboyaive ndio nikufuate."
"basi kumbe wasiwasi wangu ulikuwa wabure."
"sijui nisemeje mama richard, nakushukuru kwakuyafuatilia haya mambo, si unajua yanavyochanganya kichwa?"
"hayoni ya kuyasema? Mhh, we haya mambo yaangalie kwa mwenzako tu, lakiniyakija kwako lazima yakuchanganye!" mama richard alisema, akanyamzana kujenga ukimya mfupi. Kisha akajiweka vizuri kuuliza swalilililomleta kwenye nyumba hiyo. "kwani ni binti yako yupianayeolewa?" aliuliza.
"anayeolewa ni dina!" mama dinaakajinasisha.
Mama richard akamudu kuutengeneza mshangao wa bandiausoni kwake. "haa! Dina ndiye anayeolewa?" alisema huku sautiyake ikionyesha kufanikiwa kushangaa.
"dina mwenzangu!" mamadina akazidi kujiingiza kichwa kichwa.
"anaye rafiki yake,wenyewe wamekubaliana waoane, basi ndio ameleta
barua yakumchumbia."
"kwa hiyo tayari mmemjibu?"
"tumemjibu,sasa tunasubiri alete hayo mahari kisha nasi tuanze vikao."
mamarichard akaitumbukiza karata aliyoipanga kuanza kuicheza.
"nakumbukadina aliwahi kuniambia kitu kama vile alikuwa akisubiri majibu yakeya kidato cha sita? Na majibu si tayari yametoka? Kwani hakuchaguliwakwenda chuo kikuu?"
"hakubahatika mwenzangu!" mama dinaalisema na kuguna.
"imeniuma sana kutochaguliwa kwake!"
hapondipo mama richard alipoukamata usukani wa kumwongoza mamadina!
"sasa kwa nini mnakimbilia kumwozesha? Simngemtafutia kwanza chuo cha kusoma? Au hata awe na ajira yake kishandio aolewe?"
"kuna mipango ya kazi tunayomfanyia."
"sasakwa nini msisubiri kwanza aanze kazi kisha aolewe?"
"hatawajomba zake walilizungumza hilo, na sisi tulimshauri hilo nahajakataa, lakini anauliza hiyo kazi itapatikana lini? Ili kamakuiahirisha harusi basi ijulikane itaahirishwa kwa muda gani."
mamarichard akajiona yupo karibu ya kumuua tembo kwa ubua.
"akipatakazi sehemu nyingine yoyote si anaweza akafanya? Au lazima apate hukomnakomtafutia?" alisema.
"mwenzangu kokote kule! Je, hukotunakotegemea ikikosekana?"
mama richard akaitumbukiza karatayake ya mwisho.
"basi mimi nitazungumza na baba richard iliampatie kazi kwenye kampuni yake. Nadhani sio vyema mkafanya harakaya kumwozesha, bora aende kwa mumewe akiwa na kazi yake, maishayenyewe haya ni ya kusaidiana. Tena nitamwambia baba richard ampemshahara mzuri."
kitanzi kikawa kimening'inizwa usoni kwa mamadina, naye bila ya kusita akakitumbukiza kichwa chake. "mbonanitakushukuru mama richard kama ukiweza kunifanyia hilo!"alisema.
"kama mimi mwenyewe nimekuahidi, basi hilo usilitieshaka nalo. Nitahakikisha baba richard anampatia dina kazi yenyemshahara mzuri!"
hali ikabadilika ghafla. Mama dina alijikutaakiwa ananyenyekea kama kijakazi mbele ya nokoa na hata pale mamarichard alipoaga, ilibidi mama dina kutaka kwenda kumuita dina iliaje kumsalimia.
"hapana usimsumbue mtoto, mwache apumzike.lakini kitu kimoja mama dina," mama richard alisema kwa utulivu."habari hizi za kazi usimgusie kabisa dina, usimwambie kama kunakazi ninayomtafutia. Na
sitaki ajue kama ni mimi ndiyeninayemtafutia. Na endapo kama atajua, ama kwa kumwambia wewemwenyewe au kuambiwa na mtu mwingine yeyote, mama dina itabidiunisamehe, ujue sitohangaika kumtafutia kazi mwanao! Naomba hiloulizingatie. Please usimwambie!"
"kwa jina la yesu kristomsalabani, sitamwambia!"
"nitafurahi ukilizingatiahilo!"
"sitomwambia, hilo nakuahidi!"

kabla ya mamarichard hajatoka nje, aliombwa asubiri kidogo ili aitwe mzee nzasaambaye alitoka na kumsindikiza pamoja hadi nje. Huko nje mama yakedina alionyesha unyenyekevu uliopitiliza kwa mama richard nakumwombea kwa kumtaja yesu kila baada ya muda kabla ya mama
richardhajaingia kwenye gari.
Mama richard alipokuwa akiondoka na garilake, mama dina aliipunga mikono yake yote miwili kwa furaha yenyeunyenyekevu.

* * * * *
 
MTUNZI:BEKA MFAUME

SEHEMU YA NNE

Hali ikabadilika ghafla. MamaDina alijikuta akiwa ananyenyekea kama kijakazi mbele ya nokoa nahata pale mama Richard alipoaga, ilibidi mama Dina kutaka kwendakumuita Dina ili aje kumsalimia.

"Hapana usimsumbue mtoto,mwache apumzike. Lakini kitu kimoja mama Dina," mama Richardalisema kwa utulivu. "Habari hizi za kazi usimgusie kabisa Dina,usimwambie kama kuna kazi ninayomtafutia. Na sitaki ajue kama ni mimindiye ninayemtafutia. Na endapo kama atajua, ama kwa kumwambia wewemwenyewe au kuambiwa na mtu mwingine yeyote, mama Dina itabidiunisamehe, ujue sitohangaika kumtafutia kazi mwanao! Naomba hiloulizingatie. Please usimwambie!"

"Kwa jina la Yesu KristoMsalabani, sitamwambia!" "Nitafurahi ukilizingatiahilo!"

"Sitomwambia, hilo nakuahidi!"

Kabla yamama Richard hajatoka nje, aliombwa asubiri kidogo ili aitwe mzeeNzasa ambaye alitoka na kumsindikiza pamoja hadi nje. Huko nje mamayake Dina alionyesha unyenyekevu uliopitiliza kwa mama Richard nakumwombea kwa kumtaja Yesu kila baada ya muda kabla ya mama Richardhajaingia kwenye gari.

Mama Richard alipokuwa akiondoka nagari lake, mama Dina aliipunga mikono yake yote miwili kwa furahayenye unyenyekevu.

* * * * *

"Nimekwishakummaliza!" mama Richard alimwambia mzee Ken wakati alipokuwaakimwelezea kuhusu mazungumzo yake na mama Dina yalivyokwenda. "Kwahiyo, kinachotakiwa ni kumwajiri na kumpa kazi itakayomuweka karibuna Richard na Richard ataitumia nafasi hiyo kumshawishi Dina asiolewena badala yake amuoe yeye!"

"Usitegemee jambo hilolitafanyika kwa haraka kama unavyozungumza!" mzee Ken alionya hukuakiwa ndani ya vazi la pajama akiwa amelala kitandani kama ilivyokuwakwa mkewe.

"Lipi? La kumwajiri? Au la kumshawishi?" mamaRichard aliuliza kwa sauti iliyoonyesha kushituliwa na kauli ya mzeeKen.

"La kumshawishi Dina hadi akubali," mzee Ken alijibuakiwa amelala chali. "Lazima litachukua muda hadi kufanikiwa. Naendapo itakuwa hivyo, ujue uwezekano wa Dina kuolewa na huyo mchumbawake mara tu baada ya kupata kazi utakuwepo. Utakuwepo kwa sababukikwazo kilichokuwa kimeisimamisha ndoa yao kitakuwa hakipo tena! Kwahiyo, ipo hatari ya ndoa hiyo kufanyika wakati Richard akiwa badohajafanikiwa kumshawishi Dina kuizuia ndoa hiyo!"
"Ken, lazimaitumike mbinu kumzuia Dina asiolewe na huyo mchumba wake!" mamaRichard alisema kwa sauti kavu.
"Kivipi?" mzee Ken aliulizakwa sauti ya upole.
"Mbinu ni hii Ken; utakapomwajiri Dina, umpebarua itakayomuweka chini ya uangalizi wa miezi mitatu hadi ajirayake itakapothibitishwa," mama Richard alisema. "Barua hiyoitatoa masharti atakayoyasaini, na moja ya masharti hayo ni kuwa, kwakipindi hicho cha miezi mitatu atakachokuwa anaangaliwa utendajiwake, hakutakuwa na ruhusa ya dharura atakayopewa itakayozidi sikumoja labda itokee kuwe na msiba wa kifo cha mmoja wa wazazi wake,kaka au dada wa kuzaliwa naye! Sharti hilo litambana ashindwe kuombaruhusa kwa ajili ya kwenda kufunga ndoa!"

"Usisahau kuwa,umekwisha kujenga ukaribu na mama yake na anaweza akautumia ukaribuhuo kuja kumwombea mwanae apatiwe ruhusa ya kwenda kuolewa!"

"Hapondipo atakapokosea! Nitaitumia nafasi hiyo kumweleza umuhimu wa kaziya mwanae kimaisha, na nitamshawishi na lazima atashawishika kukubalikuliahirisha suala la ndoa hadi baada ya miezi mitatu aliyopewamwanae imalizike. Nina hakika kwa mshahara utakaokuwa unampa Dina,kamwe hatokubali kuilaani bahati hiyo."

"Kuna umuhimu waRichard kuambiwa kusudio hilo?"

"Hapana, kwa sasaasiambiwe! Ataambiwa baada ya Dina kuajiriwa." "Na ikimalizikamiezi hiyo mitatu huku Dina akiendelea na msimamo wake wa kukataakuolewa na Richard, hapo itakuwaje?" "Ikatishe ajira yake!"

** * * *

Mawasiliano kati ya mama Richard na mama Dinayakaendelea bila ya watoto wao kufahamu, huku mmoja akiijua njamaanayoifanya dhidi ya mwenzake, mwingine akiwa haijui njamaanayofanyiwa na mwenzake!

Baada ya wiki moja, zengwe la mamaRichard likawa limekamilika, na ulipofika usiku akampigia simu mamaDina!
"Mwambie Dina, kesho asubuhi saa nne awe ofisini kwa mzeeKen," mama Richard alimwambia mama Dina kwenye simu na kumwelekezailipo ofisi yenyewe. "Aende na vyeti vyake vya shule. Akifikamapokezi aseme ameitwa na mzee Ken."
"Nitamwambia usiku huuaanze kuvitafuta vyeti vyake!" mama Dina alisema kwa sautiiliyonyenyekea.
"Yeye akifika mwambie ajitambulishe kwa mzee Kenkuwa ni mtoto wa mzee Nzasa."
"Nitamwambia dada, kwa kwelinakushukuru sana." "Haina tabu. Haya usiku mwema."
"Nawepia. Yesu akubariki mama Richard!"
"Amen."

****

RICHARDalikuwa amesimama, mgongo wake ukiwa umeelekezwa mlangoni wakatialipokuwa akizungumza na msichana mfanyakazi anayefanya kazi idara yamapokezi kwenye kampuni ya mzee Ken. Richard aliyekuwa amemsindikizamgeni wake aliyemtoa hadi hapo mapokezi na kuagana naye sekundechache zilizopita, lakini kabla hajarudi tena ofisini kwake,akakumbuka kuwa, asubuhi hiyo magazeti aliyokuwa ameletewa ofisinikwake yalikuwa pungufu.

"Leo sijaliona gazeti la Flameslikiletwa ofisini kwangu, wewe unalo hapo kwako?" Richardalimwuliza msichana huyo wa mapokezi.
"Mtu wa magazeti leokaleta hilo moja tu la Flames, na limepelekwa kwa Mkurugenzi,"msichana wa mapokezi alijibu.
Wakati msichana yule alipokuwaakijibu, mlango wa kuingilia hapo mapokezi uliotengenezwa kwa kiooukasikika ukifunguliwa. Macho ya yule msichana yakavutika kuuangaliamlango huo, kitendo hicho nacho kikamvuta Richard aangaliemlangoni.

Wakamwona Dina akiingia!

Kitendo cha kuonanakati ya Dina na Richard kikawa kimewaletea mshituko wote wawili nakuonyesha dhahiri hakuna yeyote aliyetarajia kukutana na mwenzakeeneo hilo huku Dina akionyesha wazi kabla ya hapo alikuwa hajui kamaRichard alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni hiyo!

Tukio lakumwona Dina akiingia kulimfanya Richard agande kwa sekunde chachehuku akiwa hayaamini macho yake kama aliyekuwa akimwangalia alikuwakweli ni Dina. Akili yake kwa sekunde hizo chache ilikuwa kamailiyokuwa imepooza, ikashindwa kuwaza kwa haraka. Akabaki akiwaameduwaa huku akimwangalia Dina ambaye naye alikuwa akimwangalia.Ndipo Richard akakumbuka tukio lililoufanya moyo wake uzidi kupatapigo…

Aliikumbuka kauli aliyoambiwa na Dina mara ya mwishowalipokutana nje ya duka linalouzwa simu, kauli iliyomtaarifu kuwa,Dina na John Sailas wanatarajia kufunga ndoa wakati wowote!

** * * *

Richard alikuwa akimfahamu John Sailas, wote waliwahikusoma shule moja ya Azania, walikutana wakiwa kidato cha kwanza nawakawa darasa moja. Hawakuwa na ukaribu wa kuitwa marafiki, lakiniwalikuwa na ukaribu wa kuwa wanafunzi waliosoma darasa moja. Walisomawakiwa pamoja kwa muhula mmoja pekee. Muhula wa pili, Richardalihamishiwa shule nyingine nchini Kenya.

Kwa upande mwingineujuano wa kujuana kati ya Richard na Dina ulikuwa ni wa muda mrefu.Walijuana tokea wakiwa wadogo kutokana na kuishi eneo moja na mitaayao ilikuwa jirani. Wakati Richard alipokuwa kidato cha kwanza, Dinaalikuwa darasa la sita. Mwanzo wa Richard kuanza kumtongoza Dinakilikuwa ni kipindi Richard alichokuwa amerudi likizo kutoka nchiniKenya wakati huo akiwa kidato cha tatu na Dina akiwa ameingia kidatocha kwanza.

Kupoteana kwao kulikosababishwa na Richard kusomanchini Kenya, kulimfanya Richard ayashangae mabadiliko ya ghafla yakimwili yaliyomtokea Dina baada ya yeye Richard kurudi nchini kwaajili ya likizo. Richard alimwona Dina kama aliyekua harakakimaumbile. Umbile zuri la kike lililokuwa limejichomoza kwa kuvigawaviungo vya Dina kwenye hesabu sahihi, kulimfanya Richard aingiwe nahisia za matamanio ya mapenzi dhidi ya jirani yake huyo.

Uzuriwa Dina na umbile lake hilo lililoanza kutatanisha wanaume wenginelilimfanya Richard awe na wakati mgumu wa kushindwa kuzificha hisiazake na kujikuta kama mtu anayepigwa na shambulizi la ghafla kilaalipokuwa akikutana na Dina njiani. Akashindwa kujizuia, akaamuakumkabili Dina na kumpa yake kauli.

Dina akamkataa!

Richardhakukata tamaa. Akabuni mbinu mpya ambayo kwa upande mwingine ilikuwakama ya kitoto; mbinu ya kulitumia jina la baba yake. Akawa anamwombaDina aende naye nyumbani kwao na kumwambia kuwa, baba yake angefurahisana kama angemwona naye. Richard alikuwa akiamini kama Dinaangeukubali mwito huo wa kwenda nyumbani kwao, ule ufahari wakimaisha ulioenea kila sehemu ya nyumba yao ungekuwa ni chachu kuu yakumfanya Dina amkubali kirahisi. Hata hivyo, Dina hakulikubalikaribisho hilo!

Si kwamba Dina alikuwa hamjui baba yakeRichard, alikuwa akimjua vizuri sana mzee Ken kuwa ndiye baba yakeRichard, na utajiri wa mzee huyo ulikuwa ukijulikana na kila mtukwenye kila kona ya maeneo hayo wanayoishi. Hata hivyo, sababuiliyomfanya Dina kumkataa Richard ilitokana na Dina kujiona ndiokwanza ameanza masomo ya Sekondari na alikuwa amepania afike mbalikimasomo, hivyo hakuwa tayari kujiingiza katika mapenzi na mwanamumeyeyote.

Hatimaye Richard aliondoka na kwenda masomoniUingereza baada ya kufanikiwa kupata chuo, lakini aliondoka akijijuaana deni la kuja kuhitimisha dhamira yake aliyoiwekea nadhiri kuwalazima aje kumpata Dina kimapenzi wakati atakaporudi likizo.

Likizoyake ya kwanza ilipowadia, Richard alirudi nchini akiwa na matumainitele ya kumpata Dina. Alirudi akiwa amebadilika tabia. Akawa mtu wakunata na kujisikia huku akionyesha kuuhusudu Uzungu kupitiliza.Katika siku za mwanzoni mwa likizo yake alidhani kule kusoma kwakenchini Uingereza kungemfanya Dina ampapatikie na angeweza kumpatakirahisi. Lakini Dina hakuwa hivyo! Dina aliendeleza msimamo wakeuleule wa kuhakikisha Richard hampati!

Kengele ya hadhariikalia kichwani mwa Richard, akagundua kumbe ujivuni ungemharibiamambo. Akajibadili kutoka kwenye tabia ya ujivuni na kuingia kwenyetabia ya kuwa mpole, akawa mnyenyekevu mbele ya Dina. Akaepukakuzungumza stori za mapenzi kila alivyokuwa akikutana naye. Akaanzakuzungumza stori za matukio ya kusisimua yaliyopo na yaliyotokeanchini Uingereza. Stori hizo zenye mchanganyiko wa kutoka kwenyematukio halisi na historia nyingine za kuvutia alizokuwa akiziangaliakutoka kwenye dokumentari tofauti za vipindi vya kwenye runinga hukuakimudu kuvielezea kwa ufasaha, vikaonekana kumwingia na kumvutaDina.

Hali ikabadilika ghafla, Dina akaanza kuyafurahiamazungumzo hayo kila alipoonana na Richard. Ukaribu wao ukazidi, naRichard akajaribu kuitumia tena nafasi hiyo kumtaka Dina afikenyumbani kwao, lakini Dina hakuwa tayari kwa hilo. Hata hivyo, mkaapamoja na waridi hunukia waridi. Ukaribu huo ukaanza kuletamabadiliko, mwelekeo wa kuelekea kwenye mapenzi ukaanza kimya kimya.Ikafikia mahali ikawa halahala mti na macho! Richard akakaribiakidogo afanikiwe kumpata Dina kimapenzi.

Tukio hilo lilianziausiku wakiwa pamoja nje ya nyumba ya akina Dina, walikuwa peke yaokwenye eneo hilo walilokuwa wakipenda kuonana na kuzungumza storizao. Richard akazungumza neno lililomfurahisha Dina, Dina akajikutaakicheka na kukiegemeza kichwa chake kwenye bega la Richard. GhaflaRichard akapata akili ya kujaribu bahati yake, akauzungusha mkonowake kwenye shingo ya Dina na kumkumbatia. Akaunamia uso wa Dina nakuonyesha dhahiri alikuwa na lengo la kuubusu mdomo wa Dina. Mungu siAdam, akaishikia siku ya Richard kwa Richard kujikuta akinyonyanandimi na Dina bila ya bishano la aina yoyote.

Siku hiyoRichard hakuiamini bahati hiyo! Hata alivyokwenda kulala, usingiziulikataa kuja mapema, muda mrefu alijikuta akilifikiria tendo hilo nakuwa kama gurudumu la santuri ya video iliyokuwa ikijirudia wakatiwote!

Lakini bahati hiyo ikaja kuharibiwa na marafiki zakeambao ni watoto wa matajiri kama alivyo yeye. Badala ya kuendelea namkakati wa kutulia uliomletea matunda kwa Dina, Richard akaanzakukosa utulivu. Marafiki zake wakaanza kumyumbisha kwa kumfuatanyumbani kwao na kwenda naye kwenye madisko. Ikawa leo huko, keshokule. Mara kwenye fukwe za bahari, mara wako na wasichana hawa, keshowale. Dina akazishitukia tabia za Richard za kubadilisha wasichana,hata hivyo akaamua asimlalamikie Richard jambo hilo.

Aliamuaasimlalamikie kwa sababu hakuuona ulazima huo! Ukaribu wao haukuwamzito hivyo, hata kile kitendo cha faragha kilichofanyika kati yaocha kunyonyana ndimi zao hakikuwa kimemwumiza kutokana na kuwa,kilifanyika mara moja!

Dina hakukubali tena kukirudia kitendohicho kila walipokuwa pamoja. Akawa amembadilikia ghafla Richard!Akaanza kumkwepa Richard kila Richard alivyokuwa akiomba kuonana nayena hata wakati walivyokuwa wakionana, Dina hakuwa tayari tenakukubali kusimama eneo lolote la faragha. Akawa anampa picha ya waziRichard kumwonyesha kuwa, sasa ule ukaribu uliokuwa ukihitajiwa katiyao haukuwa na umuhimu tena! Richard akaanza kumlalamikia Dina kuwaamebadilika ghafla, hata hivyo Dina aliamua kutompa sababu ya kwanini alikuwa akifanya hivyo!

Kugundua kuwa alikuwa hatakiwi naDina kulianza kumchanganya Richard, lakini kilichomchanganya zaidi nikule kutoijua sababu iliyomfanya Dina auchukue uamuzi huo wa ghaflawa kumkataa pasipo kumtamkia. Matumaini ya uhusiano wao baada yatukio la kuzikutanisha ndimi zao akayaona yakiteleza mikononi mwakehuku juhudi za kuzuia zikipoteza dalili zote.Hapo ukawa mwanzo waRichard kugundua kile alichokuwa hakijui mwanzoni kuwa, kitendo chakukataliwa na Dina kilikuwa ni jambo lisilokubalika kwake!

Mapenziya kumpenda Dina yalikwisha kumuingiza kichwa kichwa kiasi chakujiona hawezi akajitoa! Ukawa ni mshituko ambao hakuutarajia, likawani pigo kwake kukataliwa baada ya kupenda! Akajaribu kuomba aina yoteya misamaha, lakini Dina hakuonyesha dalili ya kurudi nyuma kwenyeuamuzi wake!

Wakati akiwa kwenye jitihada zote za kutakakulirudisha tena penzi kwa Dina, likizo nayo iliyokuwa ikimuwekanchini ikaisha. Richard akarudi Uingereza bila ya mafanikio yakuurudisha tena uhusiano wake na Dina!

* * * **

****DINA ndani ya ofisi moja na RICHARD..mpenzi wakewa utotoni…nini kitaendelea??

****Je? Ile mbinu ya MamaRichard itazaa matunda.
***Ndoa ya John na Dina…na vipi hatma yaJudy???
**NI VITA KATI YA PESA, MAPENZI NA WIVU!!!
 
mtunzi: Beka mfaume

sehemu ya tano


Mapenzi yakumpenda dina yalikwisha kumuingiza kichwa kichwa kiasi cha kujionahawezi akajitoa! Ukawa ni mshituko ambao hakuutarajia, likawa ni pigokwake kukataliwa baada ya kupenda! Akajaribu kuomba aina yote yamisamaha, lakini dina hakuonyesha dalili ya kurudi nyuma kwenyeuamuzi wake!

Wakati akiwa kwenye jitihada zote za kutakakulirudisha tena penzi kwa dina, likizo nayo iliyokuwa ikimuwekanchini ikaisha. Richard akarudi uingereza bila ya mafanikio yakuurudisha tena uhusiano wake na dina!


* * * * *

kurudikwake uingereza kukaonyesha ni namna gani alivyokuwa amechanganyikiwana penzi lililovurugika. Tukio la kunyonyana ndimi na dinalikaendelea kuleta jinamizi lisiloisha kwake. Richard akaanza kupigasimu za mara kwa mara hasa usiku kutoka uingereza kumpigia dina.alibembeleza na kulalamika huku akimsihi dina amweleze sababu yakumgeuzia kibao.

Dina hakuonyesha hasira wala kinyongo wakatiwote alipokuwa akizipokea simu za richard, alimsikiliza richardalivyokuwa akihangaika na maneno, na mwisho wa mazungumzo yao dinaaling'ang'ania msimamo wake wa kutomwambia richard sababu yakumkataa, zaidi ya kumwambia, "niliamua tu iwe basi!"

ikawani kauli iliyomtesa richard wakati wote. Umbali uliokuwepo kati yakena dina ukawa ni kikwazo kingine, akawa anatamani arudi nchiniangalau kungemuwezesha kuonana na dina na kuyaweka mambo sawa napengine fursa hiyo ingempa nafasi ya kukijua kile kilichomfanya dinaamkatae ghafla. Hata hivyo mawazo yake hayo yakabaki kuwa ni jambolisilowezekana kutekelezeka kwa ukweli kuwa, asingeweza kuruditanzania na kuacha masomo.
Baada ya kukiri asingeweza kurudinchini, ndipo richard alipojaribu kuicheza karata yake ya mwisho kwakumuahidi dina pindi atakapomaliza masomo yake nchini uingereza nakurudi nyumbani, jambo la kwanza ambalo angelifanya ni kumuoa!
Karatahiyo nayo, dina akaitolea nje!

Richard akanyoosha mikonokusalimu amri akiwa london!

* * * * *

baada yakukaa uingereza na kumaliza masomo yake, richard alirudi nchini akiwana shahada yake. Ujio wake wa kurudi nchini, haukumshitua dina.richard akalielewa hilo, likamwumiza moyoni. Hata hivyo, akajaributena bahati yake kwa kuonana na dina na kumlia kiapo kuwa ahadi yakumuoa aliyoiahidi ilikuwa ni ya dhati na angekuwa tayari hata kwendakujieleza kwa wazazi wake dina kuhusu kusudio lake hilo.
Dinaakapangua tena!

Ndipo richard alipoamua kuanzisha urafiki najudi!

Aliuanzisha uhusiano na judi kwa sababu alikuwa akijuajudi na dina walikuwa wakifahamiana! Wasichana hao wawili walikuwa nahistoria iliyokuwa ikifanana kidogo na ile ya richard na john. Haonao waliwahi kusoma shule moja kama ilivyokuwa kwa john na richard.tofauti iliyokuwepo kati yao ni kuwa judi na dina wao walisoma pamojakuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne kabla ya kuachana huku kilammoja akienda kumalizia masomo ya kidato cha tano na cha sita kwenyeshule tofauti. Kwa fikra za richard alizokuwanazo, alifikiri urafikialiouanzisha na judi ungeweza kumwumiza dina na aliamini ingekuwa nisehemu ya kulipiza kisasi chake kwa yale ambayo dina alimfanyia!
Kwaupande wa judi, pamoja na kukubali kuwa rafiki wa kike wa richard,lakini yeye alikuwa haijui nasaba yoyote iliyokuwepo kati ya richardna dina. Hata hivyo, dina alikuja kujua baadaye kuwa richardameanzisha uhusiano wa mapenzi na judi. Ingawa taarifa hizohazikumwumiza lakini kwa kiasi fulani zilimkera.

Kwa kuwalengo lilikuwa ni kumwumiza dina, richard alipokuja kujua kuwa dinaalikuwa akiufahamu uhusiano uliopo kati yake na judi, kinadhariaakajiona tayari ni mshindi! Jambo hilo likamfanya richard kuuimarishauhusiano wake na judi kwa kwenda naye kila mahali na kumtambulishakwa kila mtu aliyekuwa akimfahamu huku akiamini uhusiano wao huoungeleta gumzo jijini dar na wangekuwa mfano wa watu wapendanao.akawa na hakika sifa hizo zingemfikia dina, na aliamini zingemchomana kumwumiza kama alivyoumizwa yeye na dina! Uamuzi wake huo wakujenga uhusiano na judi akategemea ingekuwa ni fimbo pekee yakumwadhibu nayo dina ili ajutie nafasi aliyoichezea!

Richardakaanza kuamini ushindi ulikuwa ukienda upande wake baada ya kubainihabari za uhusiano wake na judi zilikuwa zipo kwenye kilele chakuzungumzwa na watu tofauti na hasa wale wa daraja lao. Isitoshe,wengine wakawa wanazizidisha kwa kutia chumvi kwa kutangaza kuwa,wawili hao wangeoana!

Richard akaridhika kuwa amemkomoa dina,lakini pia, akafanikiwa kumuondoa dina kwenye fikra zake huku nafsiyake ikiridhika kuwa ameweza kulipiza kisasi. Pamoja na kuamini kuwaameweza kuitimiza nadhiri ya kumwumiza dina na yeye mwenyewe kuanzakuusahau ule ulazima wa kumwona dina ni sehemu muhimu ya maisha yake,lakini bado alikiri kwenye moyo wake kuwa, adhabu aliyoipata nakuitumikia kutoka kwa msichana huyo ilikuwa kubwa na iliyomwumizamno. Akajionya kuwa, mara nyingine asifikie kumpenda mwanamkemwingine kama alivyompenda dina ambaye amemuachia kovu kwenye moyowake lililosababishwa na jeraha la kupenda!

Lakini akiwa ndaniya imani hiyo ya kuwa ameweza kuitekeleza nadhiri yake, ghafla pasipomategemeo richard akajikuta akiingia kwenye mshituko mwingineasioutarajia pale alipobaini kuwa, kovu hilo lililoachwa na dinamoyoni mwake, kumbe kidonda chake kilikuwa bado kibichi na kilikuwambali na unafuu wa kupona.

Utambuzi huo ulikuja kama sikumbaya kwake, siku ya mwishoni mwa wiki aliyokuwa akiifurahia akiwa najudi. Ilikuwa siku ya jumapili!
Siku hiyo alikuwa akiisheherekeamapumziko ya juma la mwisho akiwa na judi wakiwa kwenye hoteli ya bbhiliyopo nje ya jiji kandoni mwa fukwe ya bahari. Ilianzia wakatirichard akiwa anatoka chooni akimrudia judi aliyekuwa amemuachaufukoni akipunga upepo. Choo alichokuwa ametoka kukitumia kilikuwakaribu na bwawa la kuogelea, na alipokuwa akirudi aliamua kuitumianjia nyingine tofauti na ile aliyoitumia awali kuendea chooni. Njiahii aliyoamua kurudi nayo ilipita karibu na hilo bwawa, tofauti naile ya mwanzo ambayo ilipita mbali na bwawa na pia ilikuwa yamzunguko hadi kufika chooni.

Ghafla wakati alipokuwa akirudikutoka chooni, richard akamwona john sailas! John alikuwa amevaabukta pekee mwilini iliyolowa maji kuonyesha muda mfupi uliopitaalikuwa akiogelea, alikuwa akitokea kwenye baa akiwa amezibeba glasimbili za vinywaji vya aina moja vyenye rangi ya kijani ambavyoalihisi ni kinywaji aina ya crème de menthe vilivyotumbukizwa barafuiliyosagwa. Kitendo cha kumwona john kikamfanya kutaka kumuita, nasababu ya kutaka kumuita ni kwamba walikuwa hawajaonana kwa kipindikirefu kidogo. Akasita kuitekeleza dhamira yake hiyo ya kumuita baadaya kumwona msichana aliyekuwa hatua kadhaa mbele huku mgongo wamsichana huyo ukiwa umeelekea kwake akiwa amekaa kwenye kingo zabwawa la kuogelea na nywele zake zikiwa zimelowa huku miguu yakeameitumbukiza kwenye maji. Msichana huyo alikuwa amevaa bikini yakuogelea ambayo ni chupi na sidiria akiwa amegeuka kuangalia nyuma nakutabasamu baada ya kumwona john.

Richard alisimama ghaflabaada ya kugundua msichana aliyekuwa akimwangalia alikuwa ni dina!bila ya kukusudia kuufanya uamuzi huo, richard alijikuta akirudikinyume nyume kama aliyekuwa ameona jambo la hatari. Akabadili njiahuku akiendelea kumwangalia dina alivyokuwa akimpokea john glasiyenye kinywaji, kisha john akajiunga kukaa pembeni mwa alipokaa dina,naye miguu yake akaitumbukiza majini kuwakabili kuwaangalia watuwaliokuwa wakiogelea. Kitendo cha john kukaa karibu na dinakukayafanya mabega yao yagusane, dina akatumia bega lake kuligongabega la john kiushikaji. Kitendo hicho hakikuwa na nguvu iliyotumika,lakini john akafanya igizo kama aliyekuwa amesukumwa kwa nguvu.akayumba kidogo kuonyesha ameyumbishwa na msukumo wa bega la dina,kisha akamwangalia dina aliyekuwa akimwangalia kwa ncha za macho yakehuku akitabasamu. John naye akatabasamu, kisha wote wawiliwakazikutanisha papi za midomo yao na kubusana kwa mara moja.
Tukiohilo likamuacha richard kwenye maumivu yaliyomchanganya kichwa.ilikuwa ni vigumu kwake kusadikisha yanayotokea ni sehemu yamkanganyiko wa mawazo yanayomjengea taswira zisizokuwepo kutokana najinamizi la kuachwa na dina, au yupo ndotoni akiiota ndoto hiyo!
Yotealiyoyaona aliyapinga kwa kuamini hayakuwa kwenye ithibati ya matukioya kweli. Hakukubali kukiri kama aliyemwona ni john sailas na yulealiyekuwa naye ni dina. Pili, hakukiamini kile kilichokuwakinamdhihirishia kichwani mwake kuwa, endapo ni kweli hao aliowaonani john sailas na dina, basi kinachomdhihirishia hapo ni kwamba watuhao ni wapenzi, tena ni wapenzi wa muda mrefu!

Akakubalikujiondoa kwenye uhayawani wa kuukataa ukweli unaotokea mbele yake,akakiri hayuko ndotoni na anayoyaona ni ya kweli! Lakini pia hakujuakilichokuwa kikimwumiza. Ni kule kumwona dina akiwa na bwanamwingine? Au ni kumwona dina akiwa na john sailas? Akagunduakilichokuwa kikimwumiza ni kugundua john sailas ni bwana wake dina!awali alitarajia kitendo chake cha kumchukua judi na kumfanya rafikiyake wa kike kingemfanya dina alipize kisasi kwa kumtafuta bwana wauhakika na mwenye uwezo kama aliokuwa nao yeye. Kamwe hakutarajiadina na uzuri aliokuwa nao angeweza kumkubali mtu kama john sailasmwenye maisha ya kawaida yanayoendeshwa kwa kutegemea ajira yenyekipato cha wastani! Richard aliishiwa nguvu, akashusha pumzi nakusikitika
peke yake. Akarudi alipokuwa amemuacha judi.

Kerola aina ya maisha aliyonayo john bado liliendelea kumsulubu richard.alimshangaa dina kumkubali mtu mwenye kumiliki usafiri wa pikipiki.akailinganisha tofauti iliyokuwepo kati yake na john. Yeye alikuwa nimtoto wa tajiri mwenye kuuchezea utajiri wa baba yake unaompa umilikiwa kubadilisha magari ya kifahari muda wowote anaotaka. Isitoshe pia,ni mrithi mtarajiwa wa mali za baba yake pindi akifariki. Alikwishakuonana na john sailas barabarani zaidi ya mara tatu wakati yeyeakiwa anaendesha gari lake la kifahari na john akiwa na pikipiki yakeakiwa amekifunika kichwa chake kwa kofia ngumu ya helmeti. Utofautihuo wa kimaisha, richard aliuona ungempa moja kwa moja turufu yaushindi kwenye vita hiyo ya mapenzi, lakini haikuwa hivyo! Ni johnsailas ndiye aliyeonekana ni mshindi!

Lilikuwa pigo kwarichard, pigo lililomuanzishia kumchukia john na kumwona ni adui yakenamba moja. Hakuamini mtu mwenye maisha aina ya john sailas anawezaakamshinda. Fikra hizo zikamuweka kwenye ubishi wa kutokubalikushindwa. Akaamini, endapo safari hii kama ataianzisha tena vita yakumrudisha dina mikononi mwake angeweza akafanikiwa nayo. Alihisikulikuwa na dosari ndogo aliyokuwa ameifanya kwenye kumwongoza dinawakati mtafaruku wao ulipotokea. Hakuijua dosari hiyo, lakinialiamini ilikuwa ni ndogo ambayo anaweza akaisawazisha. Vinginevyo,dina asingeweza amuache yeye aliyezungukwa na utajiri, kishaakamfuata mtu kama john sailas ambaye alimwona kama mbabaishaji wamaisha!

Tukio hilo la kumwona john sailas akiwa na dina,richard alilichukulia kama tusi na fedheha kwake, lakini piaakalifanya ni changamoto kwake. Hakutaka kuamini mtu kama johnanaweza akawa na ubavu wa kumnyang'anya msichana kama dina!akajiapiza lazima arudi kwenye vita ya kumrudisha dina mikononimwake! Tukio hilo likaendelea kumtesa, akakosa amani. Kwa mara yakwanza alijikuta akikiri kuwa, uamuzi wake wa kumchukua judi kamanjia ya kumkomoa dina ilikuwa sawa na hakuna alichokifanya!

Richardakaapa, piga ua lazima amrudishe tena dina mikononi mwake kwa gharamayoyote!

Siku chache baada ya tukio hilo kutokea, ndipo judialipomwuliza richard kuhusu kufunga ndoa kwao. Likawa ombilililokwishachelewa kutolewa! Akili ya richard ilikuwa imetekwa upyana penzi la dina huku akijitangazia vita dhidi ya john sailas!


** * * *

richard akaingia rasmi vitani kumsaka dina,lakini haikuwa rahisi kwa kumvizia barabarani. Kwa mara ya kwanzaalijikuta akijilaumu kwa uamuzi wake wa awali wa kuifuta namba yasimu ya dina siku chache baada ya kuanzisha urafiki na judi.kukosekana kwa namba ya simu ya dina kukawa ni tatizo jipya kwake.richard akawa hana mtu wa karibu ambaye angemwezesha kuipata nambahiyo kwa urahisi.

Uwezekano pekee ambao ungemwezesha kuonanana dina kirahisi ni kwenda nyumbani kwao dina. Wazo hilo alilipingamoja kwa moja, aliuona ni uamuzi wa kujirahisisha na ungetoa nafasikwa dina kujiweka kwenye ujivuni usio na lazima pale ambapo angemwonaamekuja nyumbani kwao kwa ajili ya kubembeleza penzi. Kikwazo hichokikamuweka richard kwenye wakati mgumu wa kuweza kuonana na dina.siku zikaanza kupotea huku kila siku richard akihaha kutafuta njia yakuonana na dina.

Mara nyingi ukiomba kwa dhati huwa unapewa.mungu akampa richard bahati hiyo ya kuonana na dina. Walionana bilaya kutarajiana. Ilikuwa wakati richard akikatiza kwa nje kwenye dukalinalouzwa simu lililopo katikati ya jiji. Akiwa anaukaribia mlangowa duka hilo kwa nia ya kuupita ili aendelee na safari yake, ndipodina akawa anatoka kutoka kwenye duka hilo. Wote wawiliwakashituka.

"dina!" richard aliita kwa uchangamfuuliokuwa hauna nguvu sana. Aliogopa kujiamini moja kwa moja.
Dinaalitabasamu na kusema, "hai, richard!"
"za sikunyingi?"
"poa. Zako?"
"zangu mbaya."
"kwanini?"
"sikutarajia kunikataa kwako kukufanye unichukie hividina. Umekuwa sio mtu wa kunitafuta kwa simu japo kwa kusemaheloh?"

"unanilaumu mimi wakati wewe mwenyewe unafanyakitu hicho hicho?"

"mimi nataka sana kukupigia dina,lakini naogopa kutonesha jeraha uliloniachia moyoni. Ukweli ni kwambabado nakupenda dina."

"sio vizuri judi akikusikia ukisemakauli kama hiyo kwangu."
"judi siko naye tena!"

"etiunasemaje richard?"
"tumeachana!"
"kwa nini?
"ukwelini kwamba bado hajapatikana mtu wa kuiziba nafasi yako. Badonakupenda dina!"
kauli hiyo ikamfanya dina atoe kicheko cha kamaaliyeguna.
"ina maana huna habari?" alisema.

Richardakaonyesha kushangaa kidogo.
"habari ipi?" aliuliza.

Ndipo Dina alipomweleza Richard kuwa, anatarajiwa kuolewa na john sailassiku chache zijazo! Taarifa hizo zikawa zimemmaliza richard!
Akiwabado hajayaponya majeraha yaliyotoneshwa upya, wiki mbili baadayerichard anashangaa kumwona dina akiwasili kwenye ofisi za kampuni yababa yake!.......


**Richard amegundua kuwa kulipiza kisasikatika mapenzi hakusaidii bali kunaumiza zaidi…ameaamua kupiganiamoyo wake unapomuelekeza….moyo unamtaka dina!!!

***Dina yupokatika hatua za mwisho za kutolewa mahali na john sailas….je mpangohuu utafanikiwa???


**Richard kijana wa kitajiri ametangazarasmi vita ya mapenzi dhidi ya john sailas.
 
MTUNZI: BEKA MFAUME

SEHEMU YA SITA


Akiwa bado hajayaponya majeraha yaliyotoneshwa upya, wiki mbili baadaye Richard anashangaa kumwona Dina akiwasili kwenye ofisi za kampuni ya babayake!

LILIKUWA kama shambulizi la ghafla walilofanyiana. Wote wawili, Dina na Richard walitumia takriban sekunde mbili au tatukushangaana huku wakitazamana bila yeyote kati yao kutamkaneno.

"Dada karibu," msichana wa mapokezi alisema hukuakimwangalia Dina na wakati huo huo akiiba kumwangalia Richardaliyekuwa bado ameduwaa akimwangalia Dina.

"Ahsante," Dinaalisema na kuonyesha kuondoka kwenye mshangao uliompata.
"Nadhanini mgeni wangu!" Richard alimwambia msichana wa mapokezi kabla yamsichana huyo hajaanza kumhoji Dina.
"Karibu Dina."
"Nimekuja kumwona mzee Ken," Dina alisema huku akimwangalia Richard.
Richard akaonyesha kidogo kupigwa na butwaaa.
"Karibu yupo," alisema kabla hajatekwa na butwaa lake.
"Anajua kama utakuja?"
"Anajua,"Dina alijibu.

"Twende nikupeleke ofisini kwake," Richard alisema na kuuweka mkono wake mgongoni mwa Dina na kuondokanaye.
Walifika ofisini kwa Katibu Muhtasi na Richard alimtambulisha Dina kuwa ni mgeni wa Mzee Ken, kisha akamwongoza Dina hadi mlangoni mwa ofisi ya mzee Ken. Aliugonga mlango na kuufungua,akamwingiza Dina na kusema huku akimwangalia mzee Ken, "Mgeniwako!" kisha baada ya kusema hivyo alitoka na kuufungamlango.
Mazungumzo kati ya mzee Ken na Dina yalichukua takribanidakika kumi na tano hadi ishirini. Dina akafahamishwa kazi ambayoangeajiriwa, akaikubali.

"Nitakulipa mshahara wa shilingilaki nane na nusu ukiwa chini ya uangalizi wa miezi mitatu, naikifika miezi sita, nitakupandishia mshahara wako na kufikia shilingimilioni moja na elfu sabini na tano," mzee Ken alisema.
Dinahakuamini alichokuwa akiambiwa, alihisi kulikuwa na makosa kwenyematamshi ya mzee Ken. Akatamani amwambie mzee huyo arudie kauli yake,lakini hakuweza.

"Upo tayari kwa mshahara huo?" mzee Kenaliuliza huku akili yake
ikicheza na akili ya Dina na kugunduabinti huyo alikuwa tayari amekimeza chambo.
"Nipo tayari,"Dina alisema kwa sauti hafifu ambayo ilibaki kidogo ikatae kutokakutokana na kutoamini bahati iliyomwangukia ya kuajiriwa kwa kulipwamshahara mkubwa.

"Subiri hapo nje," mzee Kenalisema.
"Ukitoka niitie huyo mama." Dina alisimama kwanidhamu kabla hajaondoka, na hatua zake
alivyoanza kutoka alikuwaakitembea kwa woga na miguu yake alihisi kama iliyokuwa ikitetemekana kutembea kwa tahadhari kama vile alionywa sakafu ya humo ofisiniingevunjika kama angeikanyaga kwa nguvu. Alitoka na kuyapelekamaagizo aliyotumwa kumpelekea Katibu Muhtasi.

Baada ya KatibuMuhtasi kuingia ofisini kwa mzee Ken alikokuwa ameitwa, ikamchukuamuda mfupi akatoka. Alipotoka alimchukua Dina hadi kwenye ofisiiliyokuwa jirani na ilipo ofisi ya Richard. Huko walimkuta kijanaaliyeonekana kuwa na umri wa takribani miaka thelathini anayeitwaMohamed Hussein, lakini alikuwa akiitwa kwa jina la mkato,Mohsein.

"Mohsein," Katibu Muhtasi alimuita kijanahuyo.
"Huyu binti ni mfanyakazi wetu mpya, anaitwa Dina.Utamfundisha kazi unazozifanya ili akusaidie na muwe pamoja," baadaya kusema hivyo, akamgeukia Dina na kusema, "Dina, huyu anaitwaMohamed Hussein, wengi tunamuita Mohsein. Utakuwa naye pamoja naatakufundisha kazi zote unazotakiwa kuzijua," baada ya kusema hivyoakamgeukia tena Mohsein.
"Mohsein, utamwonyesha Dina bosi wenuni nani."

Baada ya kumtambulisha Dina, Katibu Muhtasialitoka, akaenda ofisini kwa Richard ambako alimhabarisha Richardkuhusu ujio wa Dina.
Siku hiyo hiyo Dina akaanza kazi rasmi!

** * * *

"Eti nini?" John Sailasi aling'aka akiwa nabutwaa usoni mwake kuonyesha kutokiamini kile alichokisikia kutokakwa Dina. Akazunguka chumbani mwake kama mnyama mkali aliyejeruhiwa.Akiwa amejikamata kiuno, John alimwangalia Dina huku uso wakeukionekana kama anayetatizwa na kitu. Akacheka kicheko kilichoonyeshakumwumiza. "Usiniambie barua uliipeleka leo, na kazi ukaianza leohii!" alisema.
"Isitoshe, umeahidiwa kulipwa shilingi lakinane na nusu kama mshahara wako na baada ya miezi sita utaongezewahadi kufikia milioni na ushee!

Huoni kama kuna sintofahamukatikati yake? Hujiulizi inakuwaje huna ujuzi wowote, lakini badoutalipwa shilingi laki nane na nusu kama mshahara wako wa kuanzia? Zanini zote hizo wakati hauna umaalumu wowote kwenye kazi hiyo? Halafukitu cha ajabu ni kuwa umetakiwa uripoti kazi zako kwa Richard, huuni mzaha, Dina!"

"Mzaha ki-vipi?" Dina aliuliza kwautulivu.

"Wakati ulivyoambiwa uandike barua, ulijua ni kazigani unayokwenda kuifanya?"

"Sikuijua!" Dina alisema nakuinua juu mabega yake kama mtu asiye na hatia. "Nilichotakiwaniandike ni barua ya kuomba kazi na niambatanishe na vyeti vyangu vyashule."

"Uliwahi kumwambia mama yako akutafutie kazikwenye kampuni ya baba yake Richard?"

"Sikuwahi kuongeanaye. Lakini hiyo sio sababu ya kutonitafutia kazi."

"Ninavyoshangaahivi, sina maana sitaki ufanye kazi! Lakini huwa najiuliza, imekuwajeukapata kazi ghafla na kirahisi hivyo? Hiyo barua uliyoiandika,ulikuwa umeomba nafasi kazi gani? Au walikuwa wakimuhitaji mtu kwaharaka sana kwenye nafasi hiyo waliyokupa?"

"Niliandikakazi yoyote, nadhani elimu yangu ya kidato cha sita labda ndioiliyonifanya wakubali kunipa mshahara huo."
John akachekakicheko cha dhihaka na kusikitika.
"Mshahara huo waliokuahidikukupa haupishani sana na wa mhitimu wa Chuo Kikuu aliyeondoka nashahada yake! Sembuse kidato chako cha sita ukiwa umekosa hata alamaza kukupeleka chuoni? Tuachane na hilo, lakini pia bado huna ujuziwowote wa kazi unayoijua zaidi ya kuhitimu na kupata cheti cha kidatocha sita, halafu ulipwe mshahara huo? Huo ni mzaha Dina, lazima hapakuna namna!"

Uso wa Dina ukiwa kama uliogwaya, alimwangaliaJohn na kusema kwa sauti ya utetezi, "Labda ni kwa vile mama yanguna mke wa mzee Ken ni marafiki."

"Nina muda gani tokeanianze na wewe Dina?" John aliuliza kwa aina ya kusuta. "Kipindichote hicho hujawahi kuniambia kama mama yako na mama yakeRichard..," hapa alisita, kisha akasema kwa mkazo, "Mimi simuitimke wa mzee Ken…namuita mama yake Richard! Sioni sababu yakuzunguka! Hujawahi hata siku moja kunitamkia kama wao ni marafiki!Nakumbuka uliwahi kuniambia kuna wakati mama yako aliwasaidia waokupata hati ya kiwanja kutoka Wizara ya Ardhi, basi! Leo unaniambiawao ni marafiki? Dina! Au kwa sababu ya kupata hiyo kazi?"

"Kwahiyo unafikiri hii kazi nimeipata kwa sababu ya Richard?" "Kunasababu nyingine?"

Dina akacheka kicheko cha karaha, kifupina kilichoudhi.
"Yaani John unamaanisha nini?" Dina alisemakwa sauti iliyokereka.
"Yaani mimi kukubali kufanya kazi kwenyekampuni ya mzee Ken maana yake kazi hiyo kanifanyia mipango Richard?Au kufanya kazi chini yake ndio nitakuwa demu wake?"

"Nakijuaunachokiwaza wewe! Unahisi mimi nalia wivu, lakini wacha ionekanehivyo..!" John akasita, akacheka kicheko kidogo kilichoonyeshakumwumiza ndani kwa ndani.
"Sitaki kusema zaidi, lakininakwambia kitu kimoja, mimi siridhiki wewe ufanye kazi pale!"

"Kwahiyo ina maana huniamini? Umekwishaniona kuwa nakusaliti?" Dinaalisema kwa sauti ya kulalamika na iliyoonyesha lawama ndaniyake.

"Wewe umepelekwa pale kama chambo, nakwambiaDina!"
"Kwa hiyo mama yangu ameshiriki kwenye njama zakuniuza?"
"Sina maana hiyo!"

"Sasa una maanagani ukisema nimepelekwa pale kama chambo wakati ni mama yangu ndiyealiyenifanyia mipango hii ya kazi?"
"Tuyaache hayo Dina,"John alisema na kuonyesha kukata tamaa. "Fanya nikusindikizenyumbani!"
Dina alishusha pumzi kwa nguvu, kisha akaunamishachini uso wake na kuubana mdomo wake. Akazama kwenye fikra.
Ilikuwani siku ya kwanza Dina akiwa ameanza kazi, lakini pia ikawa siku yakwanza kazi hiyo kumwingiza kwenye mgogoro na John!


* * ** *

Ajira hiyo ya Dina ilimkosesha amani John Sailas. Taarifaalizopewa na Dina kuwa ameanza kazi kwenye kampuni ya mzee Ken nakazi hiyo akiwa anaifanya chini ya usimamizi wa Richard, halikadhalika na kiwango cha mshahara alichoahidiwa kupewa,ulimkamilishia jawabu kuwa, kuna zengwe lililosukwa dhidi yaDina!

John alikuwa akijua Richard na Dina waliwahi kuwa namahusiano
kabla ya kufarakana, na pia alikuwa akizijuajuhudi alizozifanya Richard kumwomba Dina waurudishe uhusiano huo naDina alikataa. Taarifa hizo, John alikuwa ameambiwa na Dina mwenyewekwenye mazungumzo yao ya kawaida huku Dina akiapa kuwa hajawahikutembea na Richard, lakini alikiri uhusiano wao ulikuwa ni wa ainaya mapenzi. Tukio la kuambiwa taarifa hizo lilitokea siku za mwanzoniza urafiki wao baada ya John kujua pahali ilipo nyumba ya akina Dinani jirani na anapoishi Richard. John akamwambia Dina kuwa, yeye naRichard waliwahi kusoma shule moja na darasa moja walipokuwa kidatocha kwanza kabla ya Richard kuhamia nchini Kenya kwa masomo, ndipoDina naye alipomweleza John uhusiano uliokuwepo kati yake na Richardkabla hawajafarakana.

Kwa kipindi chote hicho, ingawa Johnbaadhi ya wakati alikuwa akionana na Richard hususan baada ya Richardkurudi kutoka Uingereza, lakini John hakudiriki kumtamkia Richardkuwa ana mahusiano na Dina. Na sababu iliyomfanya John asimwambieRichard ni kutokana na kutokuwa watu wa karibu kiurafiki zaidi yakule kujuana kuwa waliwahi kusoma shule moja, kidato kimoja, na kwamwaka mmoja! Pamoja na kutomwambia kutokana na sababu hiyo, lakinisababu nyingine iliyomfanya asimgusie lolote linalohusu uhusiano wakena Dina, ni kwamba John hakutaka Richard aujue uhusiano huo kati yakena Dina kwa kuhofia endapo Richard angejua, angeweza kuianzisha vitaya kumgombea Dina na yeye John alihisi angeshindwa vita hiyo kutokanana kuwa Richard ni mtoto wa tajiri mwenye uwezo wa vishawishi vyoteambavyo vingemfanya Dina arudi tena kwake!

Tokea wakati huo,John alipokuwa akimsikia Dina akilalamika kuwa Richard alikuwa badoakimsumbua kwa kumfuata fuata, alijikuta akiingiwa na homa yawasiwasi huenda siku moja Richard angeweza kufanikiwa kumgeuza mawazoDina na Dina angeurudisha tena uhusiano wake na Richard na yeyeakitoswa!

Mawazo hayo yalikuwa yakimtesa na kumkosesha amani.Faraja pekee aliyokuwa akiipata ambayo hakuiwekea asilimia mia mojani kule kupewa moyo na Dina kuwa aondoe wasiwasi, huku Dinaakimhakikishia kuwa kamwe asingeweza kurudisha uhusiano wake naRichard hata ingetokea wakiachana yeye na John! Huo ulikuwa upandemmoja wa faraja.

Lakini upande wa pili wa faraja aliyokuwaakiipata John ni kule kusoma kwa Richard Uingereza. Akawa anajaribukuitumia nafasi ya kutokuwepo kwa Richard nchini kuuimarisha uhusianowake na Dina.
Akahisi amefanikiwa kulitimiza hilo! Lakini wakatiakifikiri hivyo, siku chache baadaye akapata habari kuwa Richardamerudi nchini, tena moja kwa moja!
Habari hizo zilimsumbua kwasababu ya kumpenda sana Dina. Usumbufu huo ukamfanya ajikute akifanyamambo ya kibwege yaliyotawaliwa na wivu, akaanza kuzifuatilia nyendoza Dina kwa siri kuchunguza kama angeziona dalili za watu hao wawilikuurudisha uhusiano. Lakini kabla ya matokeo ya upelelezi wakehayajampa picha yoyote, ndipo alipojikuta akipata faraja baada yakusikia Richard ameanzisha mahusiano na Judi!

Unjema wa habarihizo ulikuja pale Dina alipomhabarisha kuwa, msichana aliyeingiakwenye mahusiano na Richard ni msichana aliyesoma naye pamojasekondari na walikuwa wakifahamiana vizuri ingawa hawakuwa na urafikiwa karibu sana, lakini walikuwa na aina ya urafiki. Tukio hilolikampa John imani kuwa, isingekuwa rahisi kwa Dina kumkubali tenaRichard wakati akijua ana mahusiano na Judi ambaye alisoma naye shulemoja kwa miaka minne huku wakiwa na urafiki fulani.

HatimayeJohn akaja kuzisikia habari zilizokuwa zimeanza kuenea kuwa, Richardna Judi wanataka kuoana! Taarifa hizo zikamchanganya akili kutokanana furaha aliyoipata na iliyomhakikishia kuwa, ndoa hiyo kati yaRichard na Judi itasababisha kutokuwepo tena na uwezekano wa Richardna Dina kurudiana! Furaha yake hiyo ikamlazimisha na yeye ajibumapigo kwa haraka kama jibu la kumfurahisha Dina; akaamua kupelekaposa kwa wazazi wake Dina! Aliamini hilo lilikuwa jibu kwa Dina asijeakajisikia unyonge atakapomwona mwenzake anaolewa!

Lakini sikuchache baada ya kujibiwa posa yake kuwa imekubaliwa, John akaambiwana Dina kuwa, mahusiano kati ya Richard na Judi yamefikia tamati! Nitaarifa ambazo kidogo zilimshitua, lakini hazikumuweka roho juu hasakutokana na kule kukubaliwa posa yake, akaamini ndoa atakayoifunga naDina itamfanya ammiliki msichana huyo anayempenda kuliko kitu kinginechochote kile, kwa haki zote. Hata hivyo faraja hiyo haikudumu, kablaya ndoa yake kufanyika mashaka mapya yakapandikizwa moyoni mwake,baada ya Dina kumfahamisha kuwa amepata ajira kwenye kampuni ya babayake Richard!

Akiwa ametoka kumsindikiza Dina na kumfikishanyumbani kwao huku kiza kikiwa kimeishaingia, alipokuwa anarudinyumbani kwake akiwa ndani ya daladala na akiwa ameiacha pikipikiyake nyumbani kutokana na Dina kuapa kuwa hapandi pikipiki, Johnalikuwa amejawa na hofu ya wazi iliyomkosesha amani kufuatia kitendocha Dina kukubali kuajiriwa kwenye kampuni ya baba yake Richard!Zilikuwa ni habari zilizomjia kama shambulizi la ghafla ambalohakujiandaa nalo, na laiti angekuwa anazifahamu kabla, angewezakuweka pingamizi kwa kumshawishi Dina asikubali.

AliaminiRichard alikuwa amepania kutaka kumrudisha Dina kwenye himaya yake yamapenzi baada ya harusi yake na Judi kuvunjika, na akawa na dhanakuwa Richard ameamua kufanya hivyo kama eneo la kumlipizia kisasiJudi. John akakiri kuwa, endapo Richard atafanikiwa kuurudishauhusiano wake na Dina ni wazi kitendo hicho kitakuwa kinaitishia ndoayake isifanyike! Hakuwa na uhakika ni mbinu za aina gani zilizotumiwana Richard hadi kufanikisha Dina aajiriwe kwenye kampuni ya babayake, lakini aliamini, ama Richard alimtumia mama yake kwendakumwambia mama yake Dina kumwambia kuna nafasi ya kazi inayomfaaDina, au Richard mwenyewe alimkabili mama yake Dina na kumwambia kunakazi anayotaka kumwajiri Dina huku akijua mama yake Dina asingewezakuilaani bahati hiyo kutokana na binti yake kutokuwa naajira.

Mzunguko wa ajira hiyo ulivyopatikana bado uliendeleakumtia mashaka baada ya kukifikiria kiwango cha mshaharaatakacholipwa Dina, ni kiwango kilichoonyesha mazingira aliyoyaaminiyana ushawishi wa kumshawishi Dina aikubali ajira hiyo na kisha pia,aione familia hiyo ya mzee Ken kuwa ni wakarimu. Alizikumbuka tuhumaalizowahi kuzisikia kuwa, Richard hudekezwa sana na wazazi wake.Alijikuta akizipa nguvu tuhuma hizo kwa kuihusisha familia hiyokujiingiza kikamilifu kwenye kuitengeneza njama ya kumsaidia Richardili afanikiwe kumpata Dina! John alihisi Richard atakuwa amewaambiawazazi wake jinsi anavyomuhitaji Dina na huenda baba yake alimpahakikisho la kumsaidia kuliondoa tatizo hilo kwa kukubali kumpa ajiraDina kwenye kampuni hiyo, vinginevyo, mzee huyo asingekuwa tayarikumwajiri Dina kwa kupoteza pesa nyingi kumlipa mshahara mkubwa waaina hiyo!

John hakuona mantiki nyingine yoyote iliyotumikakumfanya Dina alipwe mshahara mkubwa kama huo wakati ni mbumbumbuasiyekuwa na ujuzi wowote wa kazi anayoijua. Aliamini hakuna mwajiriyeyote duniani anayeweza kumwaga pesa kwa ajili kulipa mshaharamkubwa bila ya kuwepo faida. Aliamini Dina hakuwa na faida yoyote kwamzee huyo kibiashara na wala hakuwa na thamani ya kulipwa mshaharakama huo, isipokuwa amelifanya hilo kwa ajili ya kumsaidiamwanae!

Kumfanya Dina awe chini ya uongozi wa Richard kikazi,John aliamini ni sehemu ya mkakati utakaoimarisha kuurudisha uhusianouliopotea kati ya Richard na Dina. Hali hiyo ikamfanya John ajiulizekama taarifa za kuolewa kwa Dina zilikuwa zikifahamika na familia yamzee Ken? Na kama zitakuwa zinafahamika, inakuwaje wafanye maamuzi yakuhatarisha kuivunja ndoa ya Dina? Na kama watakuwa hawana habarihizo je, urafiki wa mama Dina na mama Richard unaodaiwa na Dina,inakuwaje mama yake asimfahamishe mama Richard kuwa Dina anatarajiwakuolewa hivi karibuni?

John akaanza kuingiwa na wasiwasi kuwahuenda Dina alimdanganya alipodai kuwa, hakuwa aliijua mipango hiyoya kazi tokea mapema! Lakini hata kama ni kweli alikuwa haijui, Johnaliwaza, ina maana ajira ile ya kuwekwa karibu na Richardhaikumshitua? Akaifikiria kauli ya Dina ya kujiamini aliposema,asingeweza kukubali kuwa demu wa Richard hata kama wangeshirikiana naRichard ofisi moja! John alishindwa kujipanga auegemee upande upikati ya kuiamini kauli ya Dina au Dina alisema vile kumwondoanjiani?

Katika kufikiri huko, John alikiri kitu kimoja kuwa,yeye na Richard wapo kwenye mpambano wa kumgombea Dina! Ingawaaliingiwa tena na ile hofu ya kuwa anapambana na mtu mwenye uwezo wakipesa, lakini kulijua hilo hakukumkatisha tamaa, aliamini Dinaangekuwa upande wake kwenye vita hivyo. John akaiona njia pekee yakupambana na Richard ni kuhakikisha anaharakisha ulipaji wa maharialiyotakiwa atoe na kisha afanye haraka ya kutangaza siku ya kufungandoa.

John akajikuta akiwa na ari mpya iliyompatia nguvu mpyaya kuhakikisha anafanikiwa kuikamilisha mahari hiyo ndani ya wikimbili zijazo!



***DINA ameanza kazi rasmi, John SAILASkwa roho upande anakubaliana na hali huku akiamini kuwa DINA amewekwapale kama chambo.
LAITI kama John angekuwa na pesa huendaangemzuia DINA asifanye kazi lakini JOHN ni maskini.
***JE?Richard atafanikiwa kumrejesha DINA katika himaya yake????
 
[FONT=Helvetica, Arial, lucida grande, tahoma, verdana, arial, sans-serif][/FONT]MTUNZI:BEKA MFAUME

SEHEMU YA NANE
[FONT=Helvetica, Arial, lucida grande, tahoma, verdana, arial, sans-serif]
[/FONT]
[FONT=Helvetica, Arial, lucida grande, tahoma, verdana, arial, sans-serif]
"Nimekupa uisome ili ujuehaitawezekana kufunga ndoa, hadi miezi mitatu ipite! Hukuyaonamasharti niliyoandikiwa? Si umeona siruhusiwi kuchukua ruhusa zaidiya siku moja? Ndoa inahitaji uwe huru, ikibidi uwe na ruhusa yazaidi ya wiki moja, wengine huchukua hadi likizo. Kwa hiyo tareheuliyoitaja haitowezekana. Itabidi tusubiri hadi baada ya miezi mitatundio tufunge ndoa!"

Kauli hiyo ikamnyong'onyesha John,ikamchanganya kwa muda huku akiuona mpango wake ukielekeakushindwa.

Hakukubali!

"Tunaweza tukaoana bilasherehe!" John alisema kama aliyekurupuka huku akionekana kukosaumakini.

"Usinichekeshe John! Tuoane bila ya sherehe kisanini?" Dina aliuliza katika hali inayomshushua John.

Johnakaanza kuueleza uwongo wake, Dina akausikiliza mwanzo hadimwisho.

"Muda wa wewe kwenda kusoma na muda niliopewa kazinihautatofautiana sana," Dina alisema kwa utulivu baada yakumsikiliza John.
"Mimi nitakuwa tayari kukusubiri hadi urudi!Kwani kuna haraka gani mpaka tufunge ndoa kwenye mazingira kama hayoyasiyo na sherehe? Nitasubiri hadi utakaporudi ili tuweze kufanyakitu cha uhakika. Hata hivyo, unadhani upande wetu utalikubali wazolako? Eti tuoane kwanza halafu sherehe baadaye? Najua nao watakujibukama hivi ninavyojibu. Mimi nakuomba usisumbuke kuwapa ushauri huoupande wa kwetu. Nakushauri kitu kimoja," Dina akanyamaza nakumwangalia John aliyekuwa amesimama kama aliyeumbuliwa hukuakionekana kukosa hoja.
"Fanya hiyo mahari iletwe kamaulivyopanga. Itakuwa vizuri ukiilipa kabla hujaondoka nchini iliuonekane kweli una dhamira ya kunioa!"

Pigano la kwanzadhidi ya Richard, John akakiri amekwishalipoteza!

***

RICHARDakiwa amekiegesha kidevu juu ya vidole alivyovifumbata pamoja hukumikono yake ikiwa imeegemea juu ya meza ya ofisini kwake, alikuwaametulia katika hali hiyo kwa muda mrefu na kuonekana kutekwa mawazona kitu alichokuwa akikifikiri. Ilikuwa kama fumbo mfumbie mjinga!Alikuwa akikifikiria kitendo cha kuajiriwa Dina hapo ofisinikilivyokuwa kimemshitua, kilimshitua kutokana na kitendo hichokufanyika siku chache baada ya kutoka kuzungumza na baba yake kuhusumsichana huyo huyo ambaye alikiri anampenda na yupo tayarikumuoa.

Kuajiriwa kwa Dina katika mazingira aliyoyachukuliakuwa ni ya kumshitukizia ambayo yalifanyika kimya kimya kishaakakabidhiwa awe chini ya uongozi wake, Richard aliwaza jinsi babayake alivyokuwa hakufanya tena rejea ya mazungumzo yaliyomhusumsichana huyo tokea pale mara ya mwisho walivyolizungumzia suala lakena matokeo yake ni kumleta hapo akiwa amekwisha ajiriwa.

Richardalidhani kuajiriwa kwa Dina hapo ofisini kungekuwa ni sababu tosha yakumfanya baba yake alirejeshe tena suala la msichana huyo kwenyemjadala wao uliokuwa haujamalizika kuhusu kumuoa, lakini alishangaakumwona baba yake hakufanya hivyo! Ukimya huo wa baba yakeulimshangaza, lakini pia, alishangaa na kujiuliza kwa nini baba yakehakutaka kumshauri au kumdokeza kama alikuwa na mipango ya kumwajiriDina?

Awali katika siku za mwanzoni, ajira hiyo ya Dinailimsumbua kichwa kutokana na kumchukulia Dina kuwa ni adui yakebaada ya kumkataa na kisha kukubali kuposwa na John. Tukio hilo laDina kuajiriwa na kisha kuletwa kwenye idara yake kufanya kazi; tenabila ya barua ya ujulisho, lilimfanya apigwe na butwaa na kutomwelewababa yake kwa uamuzi huo. Akawa anajiuliza mara kwa mara, ni ninikilichomfanya baba yake amwajiri msichana huyo wakatialikwishamfahamisha kuwa, alikataa kuolewa naye?

Lakini wingula uteguzi wa kitendawili hicho kilichokuwa kimemuweka kwa sikukadhaa kwenye sintofahamu iliyokuwepo kati yake na baba yake kuhusuajira hiyo ya Dina, Richard alianza kukitegua kitendawili hicho baadaya baba yake kumwandikia barua ya kiofisi zikiwa zimepita takribanisiku tano tokea Dina kuajiriwa. Aliikumbuka barua hiyo iliyomjulishakuwa, Dina atakuwa chini ya uongozi wake na ikamjulisha kiwango chamshahara ambacho angelipwa.

Kiwango cha mshahara ndichokilichokuwa chachu ya kumzindua akili! Mara ya kwanza alipokuwaakikisoma kiwango hicho alijikuta akiamini kuna makosa ya kisarufiyaliyofanyika kwenye barua hiyo, lakini baada ya kuona kiwango hichokilikuwa kimeenda sambamba kwa kurudiwa kimaandishi, akawa amepigwana butwaa baada ya kuona hakukuwa na maantiki yoyote iliyostahilishaDina alipwe mshahara mkubwa kama huo wakati hana ujuzi wowote wakazi!

Richard alikumbuka jinsi alivyoingiwa na ushawishi wakwenda kumkabili baba yake mara baada ya kuletewa barua hiyo iliamwulize ni kwa nini alimwajiri Dina bila ya kushauriana na yeye haliakijua kuwa yeye na Dina hawaelewani? Isitoshe, pia alikusudiakumwuliza ni kwa nini ameamua kumlipa mshahara mkubwa kama huo wakatiwapo wafanyakazi walioajiriwa wakiwa na ujuzi wao ambao hawapatimshahara kama huo? Akakumbuka kabla ya kuuchukua uamuzi huo wakumkabili baba yake, alijiwa na wazo lililomfanya asite kuuchukuauamuzi huo baada ya kujiuliza kuwa, huenda kuna sababuiliyomlazimisha baba yake kumwajiri Dina na kuamua kumlipa mshaharawa aina hiyo. Wazo hilo ndilo lililompa nafasi ya kuufikiria uamuzihuo wa baba yake na kabla hajaenda mbali kifikra ndipo alipowezakukitegua kitendawili hicho alichotegwa na baba yake!

Chachuya kukitegua kitendawili hicho ilimjia Richard baada ya kuuwaziamshahara ambao angepewa Dina na kuyawekea mashaka maamuzi hayo.Akahisi lazima kungekuwa na sababu nyuma ya maamuzi hayoyaliyolazimisha Dina aanze kazi na mshahara kama huo. Ndipoalipogundua kuwa kiwango hicho cha mshahara kilikuwa ni aina yachambo kilichovikwa kwenye ndoana alichotegeshewa Dina ilikumlainisha na aione familia ya mzee Ken ipo karibu naye. Ulikuwamtego! Richard aliwaza. Mtego ambao ulikusudiwa kwa Dina ili aulegezemsimamo wake wa kukataa kuolewa na familia hiyo! Richard alitabasamupeke yake baada ya kugundua kuwa, Dina amechezwa shere kwakutengenezewa wigo asioweza kuutoka; wigo utakaomfanya amkubali iliasiupoteze mshahara huo!

Richard akakiri kwa mtaji huo,isingekuwa ajabu kumwona Dina akiurudisha uhusiano uliokuwa umetowekakati yao!

Ghafla akamkumbuka John! Akakumbuka kuwa, Dina yupokaribu kuolewa na John! Badala ya wazo hilo kumwingiza kwenye unyongekama ilivyokuwa awali kila alipokuwa akikumbuka jambo hilo, safarihii Richard alijikuta akiliwazia jambo hilo kwa mtazamo tofauti.Kilichomfanya awe na mtazamo huo tofauti ni kule kuajiriwa kwa Dinahapo ofisini. Aliamini kuletwa kwa Dina na kuwekwa karibu yakekungemwezesha kuua Tembo kwa ubua. Richard alitengeneza tabasamu laushari baada ya kujiona safari hii ana nafasi kubwa ya kumpata Dinahata kama ataolewa na John! Aliamini bado angekuwa na nafasi yakumchukua na kutembea naye kwa siri akiwa ameolewa!

Wazo hilola kuja kutembea na Dina akiwa ameolewa na John lilimfariji mno nakujisikia burudiko kwenye moyo wake. Aliuona huo ndio ungekuwa wakatimwafaka wa kulipiza kisasi kwa John! Na kwake ingekuwa ni furahailioje kama angefanikiwa kukifanya kitendo hicho katika mazingirahayo Dina akiwa ameolewa! Kitendo hicho kingemfurahisha zaidi moyowake kwani angejiona angekuwa analipiza kisasi katika njiainayostahili, na ingekuwa ni nafasi yake ya kumdhihirishia John kuwaalifanya makosa kumpora Dina akiwa mikononi mwake! Alitaka liwefundisho kwa John ili mara nyingine asivamie maeneo yanayomilikiwa nawatu wenye pesa kama yeye!

Kisasi chake alitaka kisiishie kwakumchukulia John mke wake halafu iwe basi; lakini pia, alitaka Johnaje atambue kuwa yeye anatembea na mke wake! Na sio tu John ajue kuwamkewe anatembea na yeye, lakini pia, aliapa kuitumia nafasi hiyokuhakikisha anamdhibiti Dina kimapenzi hadi awe chizi kwa ajili yakena John alifahamu hilo! Alipenda amwone John akitesekea penzi kamaalivyoteseka yeye wakati alipokuwa akimbembeleza Dina warudiane.Alitaka kusiwepo maelewano kati ya John na Dina kwenye ndoa yao.Alipania kuisambaratisha ndoa hiyo, alitaka amshuhudie Johnakihangaika kwenda kuomba msaada kwa Padri ili kuiokoa ndoa yake bilaya mafanikio! Alitaka Kanisa lifikie mahali likubali kuvunjwa kwandoa hiyo, kisha yeye ndiye aje kumuoa Dina!

Lakini wakatiakiifikiria mikakati hiyo ya kumsulubisha John na kumrudisha Dinakwenye himaya yake ya mapenzi, Richard alikiri bado kulikuwa natatizo mbele yake ambalo alikiri kuwa ni kubwa na linalohitaji ainanyingine ya maamuzi! Tatizo hilo aliliangalia kama vile Mwanasayansianavyokiangalia kirusi cha hatari kinachotaka kujipenyeza kwenyemfumo mzima wa mawasiliano ya chombo muhimu.
AlikuwaMohsein!

Alimwona Mohsein kama mtu aliyekuwa akihatarishaharakati zake ziingie kwenye ugumu usio wa lazima. Na tatizo halikuwakwa Mohsein mwenyewe, bali lilikuwa ni Dina! Aligundua Dina alikuwaakimpenda Mohsein. Kulikuwa na dalili za wazi zilizokuwa zikionyeshwana Dina kuwa amekwisha kimahaba kwa Mohsein na akalikumbuka tukio lakuwafumania wakiwa wamevigusisha pamoja vichwa vyao kwa aina fulaniya mahaba wakati alipokuwa amewaingilia ghafla ofisini.

Tukiohilo lilikuwa likimtafuna Richard, wivu na chuki ya kumchukia Mohseinikawa imejijenga, na hakutaka kujidanganya; kwa sababu dalili zotezilikuwa ziko wazi zikionyesha kuwa, kama kuna mtu anayeweza kumpataDina kirahisi bila ya kujali kikwazo cha uchumba uliopo kwa John basiMohsein ndiye mwenye nafasi hiyo! Richard akajionya endapo hatochukuahatua za haraka, uwezekano wa Mohsein kumchukua Dina mbele ya machoyake usingezuilika!

Richard alikiri hilo ni tatizo na akalionani kubwa na la hatari! Asingekubali litokee huku akiliona! Afanyenini? alijiuliza. Amfanyie fitna Mohsein afukuzwe kazi? Aliiona hiyondio njia pekee itakayomuweka kwenye amani, lakini pia, aliogopakitendo hicho kingeweza kigandulika na Mohsein kuwa, amefukuzwa kazikwa ajili ya kuonewa wivu dhidi ya Dina! Hilo lingeweza kumchocheaMohsein kufanya juhudi za ziada kuhakikisha anatembea na Dina kamasehemu ya kulipiza kisasi! Richard alipolifikiria hilo, mchomo wawivu ukapenya moyoni mwake! Akajionya kuwa, maamuzi yoyote yakumfukuza kazi Mohsein yangeleta janga badala yasuluhisho.

Akajaribu kujituliza na kufikiri kwa kutumia uwezowa akili badala ya akili za nguvu. Akajiuliza, ni njia ipi yakuitumia ili Mohsein aachane na fikra za kumtaka Dina kimapenzi? Njiapekee aliyoiona kuwa inaweza ikamsaidia, ni kufanya kila njia iliMohsein ajue kuwa, yeye ndiye aliyemwajiri Dina na Dina yuko hapo kwaajili yake. Alikuwa na uhakika endapo Mohsein atalifahamu hilo, basiangeogopa kujihusisha kimapenzi na Dina kwani angeelewa, Dina ni maliza bosi wake!

Kwa kuwa alikuwa na safari ya kikazi ya kwendaMorogoro, Richard akapanga mara atakaporudi kutoka Morogoro ndipoangeyaonyesha makucha yake kuwa yeye ndiye bosi na mmoja wa wamilikiwa kampuni hiyo. Akaamini, mwelekeo wa uelewa huo ungemtishaMohsein!

Laiti angelijua kosa analolifanya, kamwe Richardasingeenda safari hiyo ya Morogoro!



* * * **

Ilikuwa siku ya pili tokea Richard alivyokuwaamekwenda Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa ndani wamahesabu kwenye kituo chao cha mafuta ambacho ni kikubwa kulikovingine vyote mkoani humo. Mohsein akawa amekaimu nafasi yakekiofisi.

Ilikuwa ni kawaida kwa kila inapokuwa Richard hayupoofisini kikazi, Mohsein ndiye anayekaimu madaraka yake, labda itokeewote wasafiri safari moja ya kikazi. Siku ambayo Richard aliondokakwenda Morogoro aliacha maagizo kwa Mohsein kuwa, kukahesabiwe vifaaalivyokuwa ameviorodhesha kwenye nyaraka aliyomkabidhi Mohsein ilivikahesabiwe upya baada ya kutokea utata wa orodha kamili ya mahesabukuhusu vifaa hivyo vilivyokuwa vimehifadhiwa stoo na alitaka shughulihiyo ifanyike siku hiyo hiyo aliyokuwa akisafiri ili akirudi akutemajibu.

Lakini baada ya Richard kuondoka, Mohsein akazembeakuianza kazi siku hiyo kama alivyokuwa ameagizwa, akasubiri hadi sikuya pili asubuhi ndipo alipoikabidhi kazi hiyo kwa kumpa Dinaakaifanye badala ya kuifanya yeye.

Ilikuwa ni kazi ya sikumoja, lakini Dina akaingia nayo siku ya pili akiwa badohajaimaliza!

Ikiwa ndani ya siku ya pili kazi hiyohaijamalizwa, na ikiwa ni siku ya tatu tokea Richard alivyoondokakwenda Morogoro, ilipofika saa tano asubuhi, Mohsein akaanza kuingiwana mashaka kuwa, huenda Richard angerudi siku hiyo na kuikuta kaziikiwa haijamalizika. Kwa kumhofia Richard asije akaja kumbwatukiaatakapoikuta kazi hiyo haijamalizika na wakati jukumu hilo alipewayeye, Mohsein aliamua kumfuatilia Dina ili ajue amefikia wapi naendapo ikibidi amsaidie.

Alimfuata Dina aliyekuwa peke yakekwenye hiyo stoo ambayo haikuwa kubwa ya kutosha na iliyozungukwa namakabati ya chuma yaliyokuwa wazi ambayo yalibeba vifaa mbalimbalivya kampuni, akamkuta yupo katikati ya kuhesabu.

"Badohujamaliza?" Mohsein alimwuliza Dina.

"Ungenikutanimekwishamaliza," Dina alijitetea.
"Lakini kulikuwa nabaadhi ya maboksi ilibidi niyapangue kwanza kisha ndio nikaendeleakuhesabu."
"Kwani bado sana?"

"Kama utanisaidia,tutamaliza mapema."
"Umebakiza upande upi?"

Dinaakamwonyesha Mohsein upande wa makabati yaliyokuwa na vifaa hivyo.Mohsein akaenda kuhesabu. Iliwachukua dakika arobaini na tano hadikuimaliza kazi hiyo.

"Chukua hesabu nilizozipata ili uingizekwenye mahesabu yako," Mohsein alisema huku akimpa Dina karatasialiyokuwa akiingizia nukuu za hesabu zake alizozipata.

Dinaaliichukua karatasi hiyo na kusogea kwenye mwanga zaidi ambakoalikwenda kuegemea kwenye kabati lililokuwa na uwazi na kuutumiauwazi huo kama meza ya kurekebishia hesabu zake huku akiwa amesimama.Mohsein akajiunga naye. Wakasaidiana kuzifanya pamoja hesabuhizo.

Wakati walipokuwa wakiendelea kuzifanya hesabu hizo,mabega yao yalikuwa yakigusana mara kwa mara na hali hiyo kuonekanani ya kawaida kwao hadi walipomaliza na kupata uhakika wa hesabuwalizozirekebisha.

"Nakushukuru kwa msaada wako," Dinaalisema, akiwa amegeuka kumwangalia Mohsein.

Mohseinakamwangalia Dina. "Usijali," alisema.

"Lazima nijalibwana…" Dina alisema na kutabasamu huku akiendelea kumwangaliaMohsein.
"Ningekuwa sijaimaliza hii kazi kama sio wewe kuja nakunisaidia!"

Mohsein naye akatengeneza tabasamu na kusema,"Poa."

Ghafla kukajenga ukimya kati yao ulioleta faraghahumo ndani huku kila mmoja akishindwa kujisogeza alipokuwa amesimama.Wakatekwa na ukimya, kisaikolojia wakajiona wapo kwenye faraghailiyojitokeza huku kila mmoja akikiri nafsini mwake kuwa ilikuwa najambo mbele yao linalohitaji kufanywa kati yao. Wakaangaliana, wakawamabubu kwenye vinywa vyao, lakini macho yao yakawa yanazungumza lughaya ukimya ambayo kila mmoja aliielewa maana yake. Mapigo ya mioyo yaoikaanza kwenda kasi. Mohsein akawa wa kwanza kuonyesha kusudio lakekwa kuuangalia mdomo wa Dina, akauinamisha uso wake na kuusogezausoni kwa Dina na mdomo wake kuulengasha mdomoni mwa Dina!

Mohseinakasita kuupeleka moja kwa moja mdomo wake kinywani kwa Dina,akasikilizia marejesho ya Dina yatakuwaje. Dina akawa ameganda kamaaliyepigwa na shoti ya umeme, naye akajikuta akiuangalia mdomo waMohsein kwa macho yaliyoonyesha haiba ya kukubali kitendokinachofuatia, kisha akafumba macho. Mohsein akaupeleka mdomo wakekinywani kwa Dina na papi zao za midomo kugusana. Mohsein akaupitishaulimi wake..!

Dina akaupokea!

Kila mmoja alilihisi jotola ulimi wa mwenzake wakati ndimi zao zikinyonyana. Dina akauhisimkono wa Mohsein ukianza kumpapasa kwenye paja lake ukiwaumeipandisha juu nguo yake, akawahi kuuzuia alipouhisi ukitakakuingia ndani zaidi. Akaendelea kukaza msuli wake wa mkono kuuzuiamkono wa Mohsein uliokuwa ukitaka uende zaidi ya hapo.

Vita yakuzuiana mikono iliendelea huku ndimi zao zikiendeleakunyonyana!

*****

HAIKUWA wiki njema kwa John tokeaalivyojibiwa na Dina kuwa hakukuwa na uwezekano wa wao kuoana mapemakama alivyokuwa amekusudia. Sababu iliyokuwa imetolewa na Dina, Johnaliiafiki kuwa ni ya msingi, lakini alilaani kipengele kilichotumikakwenye barua ile kilichomnyima Dina kupata ruhusa ya kupumzika kikazihadi miezi mitatu ikatike! Kipengele hicho alikiona kama vilekilikusudiwa kuingia kwenye dhamira yake ya kumuoa Dinaisifanikiwe.

Hofu dhidi ya Richard iliendelea kujikita kilaalipoifikiria miezi hiyo mitatu ipite bure bila ya kufunga ndoa naDina, lakini wakati huo huo miezi hiyo ikitumika akimwona Dina akiwakaribu na Richard! Kihoro hicho ndicho kilichokuwa kikimtesa kwawivu! Hakuamini kama Dina angekuwa na ubavu wa kuendelea kuhimilivishawishi vitakavyofanywa na Richard kwa wakati wote huo, hali hiyoilimfanya awe na wingi wa hisia kuwa, Dina atamsaliti!

Hofuilikuwa ikimtawala na kumuweka kwenye hali ngumu kila alivyokumbukakuwashuhudia wanawake wengi wakiwaacha wanaume waliokuwa wakiwapendana kuwafuata wanaume wenye pesa! John alizidi kuumia moyoni jinsiwanawake hao walivyokuwa hawajali maumivu yaliyowakuta wanaumewaliokuwa nao baada ya kuwaacha, na wakati mwingine walidiriki hatakuwatolea maneno ya kebehi wakati wanaume hao walipokuwawakiwabembeleza warudiane.

Fedha! John alinyong'onyea baadaya kuikiri nguvu ya chombo hicho. Awali kabla ya Dina kuajiriwa nakampuni ya mzee Ken, John aliwahi kujisifia kuwa ni mwenye bahati yakumpata msichana aliyeumbika kama Dina aliyekuwa tayari kumkataamwanamume mwenye pesa kwa ajili yake na kukichukulia kitendo cha Dinakumkataa Richard kama kigezo chake cha kupendwa. Alikuwa akijiona nishujaa na kuhisi burudiko moyoni mwake kila alipokuwa akionana naRichard na kumcheka moyoni. Na wakati Richard alipokuwa akijaribukumbembeleza Dina ili warudiane, John alifikia hali ya kumshangaa nakumwona kama aliyepungukiwa na akili!
Hakutaka kuamini Dinaangeweza kumsaliti kupitia kwa mtu aliyekwisha kumkataa tokea awali.Lakini kwa upande wa pili hisia zilikuwa zikiendelea kumuonya marakwa mara kuwa, ukaribu wa kikazi kati ya Dina na Richardungewalazimisha watu hao wawili wajenge maelewano kati yao ambayoRichard angeyatumia kurejesha tena uhusiano wa mapenzi uliotoweka!John aliuhisi moyo wake ukienda mbio na dalili za kupandwa nashinikizo la damu zilikuwa zikimwashiria kutokana na wivu ulioitawalaakili yake. Akakiri moyoni kuwa, kitendo cha kurudiana kwa Dina naRichard kama kitafanyika kingemwumiza mno!

Akaingiwa na akiliya kutaka kumshawishi Dina aache kazi, lakini alijikuta akijijibumwenyewe kuwa hilo lisingewezekana! Aliamini hilo lisingewezekanakutokana na ukweli alioukiri mwenyewe kuwa, nyota yake ya mapenziilikuwa imefunikwa na nyota ya Dina! Dina alikuwa na sauti dhidiyake, alilolitaka ndilo litakalofanyika na aliamini Dina angelikataawazo lake hilo na asingekuwa na ubavu wa kumlazimisha!

Ndaniya nafsi yake alikuwa akiandamwa na hatia iliyokuwa ikimsuta kutokanana ukweli kuwa alikuwa akimpenda mno Dina. Hatia hiyo ikawainamuingiza kwenye hofu ya kuachwa na hata kudiriki kutawaliwa namawazo ya kijinga kuwa kusingekuwa na mbadala wa maisha mengine bilaya Dina! Akauhisi ule unyonge wa kutokuwa na ushawishi wa kumuwekaDina chini ya himaya ya amri yake ukimzomea.

Mawazo yakeyakarudi kule kule kwenye kuwahi kumuoa Dina mapema kabla ya Richardhajafanikiwa kurudisha uhusiano na Dina, aliamini hatua hiyo angalauingemuweka kwenye haki ya kummiliki Dina kuwa mkewe, haki ambayoangeitumia kukabiliana na Richard kama angediriki au hata kujihusishana Dina kimapenzi. Lakini ukweli huo ulikuwa mbali!

Alijuaasingeweza kumshawishi Dina aache kazi kwa sababu Dinaasingemsikiliza. Lakini pia asingeweza kumkabili Richard na kumuonyadhidi ya Dina kwa sababu Dina bado hajawa mkewe, na asingeweza kumvaaRichard kwa mkwara wowote kwa sababu mwenzake ana pesa inayowezakutumika kwenye vyombo vya sheria na vyombo hivyo kumgeukia yeye naakajikuta akiswekwa mahabusu au pengine hata gerezani!

Akiliyake ikajiwa na wazo la kimbilio la wanyonge; kwenda kwa waganga kwaajili ya ushirikina! Angalau kwa kiasi fulani wazo hilo lilianzakumfariji baada ya kuifikiria hatua hiyo. Hakuwa ni mtu aliyependakujihusisha na vitendo vya ushirikina, lakini aliamini ushirikinaupo. Alishawahi kuzisikia sifa za mara kwa mara walizokuwa wakisifiwawaganga waliopo kijijini kwao, sifa ambazo zilikuwa zikitolewa nawatu wa mkoa wao. Hatua ya kuwafuata waganga kama hao aliamini kamaataichukua ingemsaidia kupambana na Richard. Fikra za kujipamatumaini kuwa dawa ya mtu mwenye pesa ni kupambana naye kwa kutumianjia za kishirikina ikaanza kumtawala kichwani.

Kwa upande huoaliamini angemwendea fundi wa shughuli hizo na kumtaka afanye uchawiwake ili Dina anapomwona Richard aingiwe na hisia kama vile ameonakinyesi! Pili, angemtaka fundi huyo afanye utaalamu wake wa kuifanyanyota yake iitawale nyota ya Dina ili aweze kumdhibiti kimapenzi.Aliamini kitendo hicho kingemfanya awe na sauti mbele ya Dina na Dinaangegeuzwa kuwa kama Kondoo kwa kutii kila ambalo angelizungumza.Fikra hizo zikamrudisha John kwenye Ukamanda wa kujiona yupo tayarikurudi tena kwenye uwanja wa vita kupambana na Richard! Kwa mtazamohuo, John akaisifia akili yake kupata wazo la kishirikina!

Akaipangasiku maalumu ya kwenda kumwona mganga kijijini kwao!

* * * **
[/FONT]
 
MTUNZI:BEKA MFAUME

SEHEMU YA TISA

Kwa upande huo aliamini angemwendea fundi wa shughuli hizo na kumtaka afanye uchawi wake ili Dina anapomwona Richard aingiwe na hisia kama vile ameona kinyesi!Pili, angemtaka fundi huyo afanye utaalamu wake wa kuifanya nyotayake iitawale nyota ya Dina ili aweze kumdhibiti kimapenzi. Aliaminikitendo hicho kingemfanya awe na sauti mbele ya Dina na Dinaangegeuzwa kuwa kama Kondoo kwa kutii kila ambalo angelizungumza.Fikra hizo zikamrudisha John kwenye Ukamanda wa kujiona yupo tayarikurudi tena kwenye uwanja wa vita kupambana na Richard! Kwa mtazamohuo, John akaisifia akili yake kupata wazo la kishirikina!

Akaipanga siku maalumu ya kwenda kumwona mganga kijijini kwao!


* * ** *

Usiku, Dina alichelewa kupata usingizi kutokana nafikra zilizokuwa zimemtawala karibu kutwa nzima ya siku hiyo; fikraza kumfikiria Mohsein na tukio lilitokea siku hiyo kati yao kwenyestoo ya kazini kwao! Ni tukio lililomlazimisha awafikirie watu wawilikwa wakati mmoja, Mohsein na John! Alikiri tukio la kufanya mapenzina Mohsein siku hiyo lilikuwa limedhihirisha jinsi lilivyoishinda iledhamira yake aliyojipa awali ya kuchukua hadhari na maamuzi yakepindi anapokuwa na Mohsein. Alikuwa ameshindwa kuitekeleza! Alikirikushindwa huko kulitokana na ukweli kuwa, akiwa mbele ya Mohseinalikuwa akijisikia raha wakati wote kama vile alirogwanaye!

Kumruhusu Mohsein afanya naye mapenzi kulimdhirishia ninamna gani moyo wake ulivyotekwa na jamaa huyo. Hakutaka kuamini kamaametokea kumpenda, kwa sababu aliamini ni John pekee ndiye aliyetokeakumpenda. Alikubali kuwepo kwa hisia fulani zilizokuwa zikimfanyaafarijike kila anapokuwa yuko na Mohsein, lakini alipingana na nafsiyake kuwa amempenda Mohsein. Aliamini mapenzi yake yapo kwa John nakukiri John ndiye kila kitu kwake. Lakini hata hivyo, nafsi yakeiliendelea kumsuta kwa kukataa kuungama kuwa, kitendo cha kufanyamapenzi na Mohsein kilishatia ufa kwenye msimamo wake huo wa kuwa,John ni kila kitu kwake!

Ufa huo ulioutikisa msimamo wakeulimfanya akiri kwa mara ya kwanza kuwa, binadamu ana udhaifu ndaniya nafsi yake. Ni udhaifu wenye msukumo mkubwa wa ushawishi paleunapojikuta umezungukwa kwa ukaribu na ushawishi huo. Alikiri njiapekee ya kuepusha kuingia kwenye majaribu ni kukaa mbali na ushawishiwa aina hiyo; vinginevyo ni kushawishika kama alivyojikutaakishawishika kwa Mohsein! Yeye na Mohsein walikuwa na ukaribu,ukaribu uliokuja baada ya nafsi yake kukiri mapema kuwa Mohsein nimwenye haiba ya kupendeza, jamali wa sura na umbile! Kukiri hukokukawa kama aliyeiruhusu sumu imwingie kwenye mishipa yake ya damu!Huo ndio ukawa udhaifu wa kwanza uliomwingiza kwenye ushawishi ambaoulikuja kuchochewa na ukaribu wao wa kila siku. Sumu ikaanzakumtafuna!

Akamruhusu Mohsein afanye naye mapenzi katikamazingira ambayo mwenyewe alikiri kuwa, alikubali mwenyewe kwa hiariyake. Kukubali kuwa alikifanya kitendo hicho kwa hiari yake kunakipindi akawa anakijutia kiaina, lakini pia majuto hayo yakawahayamwumizi sana kichwa kwa sababu alichokifanya ulikuwa ni uamuziwake mwenyewe! Kuyumba huko kimawazo kukamdhihirishia jinsialivyomkubali Mohsein kwenye nafsi yake na hakutaka kujidanganya kwahilo, kwa kuwa alishakiri alikuwa akiufurahia ukaribu uliopo katiyake na Mohsein!

Kukiri huko kulimfanya kila alipokuwaakimfikiria Mohsein na kile kitendo kilichofanyika stoo kulimleteamsisimko fulani, lakini pamoja na kuwaza hivyo, fikra za kumfikiriaJohn nazo zikawa zinajipenyeza muda huo huo. Alimfikiria John kwasababu aliamini ndiye anayempenda na aliamini pia, hata ndoa yao nayoingefanyika kama walivyopanga. Lakini pia akakiri moyoni kuwa, badoangeendelea kumruhusu Mohsein kuwa mtu wake wa karibu kuiba kufanyanaye ngono!

Katika hali ya kujipanga kisaikolojia, Dinaalikiri upo uwezekano wa kuiratibu mihimili yenye uzito tofauti yakupenda watu wawili kwa wakati mmoja. Alijua mambo hayo huwayanafanyika na huendelea kufanyika kila kukicha kwa wanandoa kufanyamapenzi nje ya ndoa. Dina aliamini matendo hayo huwa yanajulikanandani ya jamii na wakati mwingine huchukuliwa kama ni matukio yakawaida, lakini hugeuka kutokuwa ya kawaida, pale fumanizilinapotokea.

Ni matukio yanaohusisha kada tofauti, wake nawaume. Wapo waheshimiwa wenye heshima zao, wapo wenye elimu zao, wapowenye madaraka makubwa na wakati mwingine hata kwa viongozi wakidini, wote hao hujihusisha na vitendo hivyo. Udhaifu wa mwanadamu!Dina aliwaza. Lakini kwa upande mwingine hisia za kupingana na mawazohayo zilimjia. Akazitazama katika mtazamo wa Kishetani, lakiniakakiri ni mtazamo uliokaa kifalsafa zaidi kuliko Kibaolojia.Akakubali kuwa, inapotokea binadamu akatawaliwa na udhaifu huo huwani vigumu kuuondoa kirahisi kama mahubiri ya dini yalivyo. Akakirikuwa, hata yaliyomtokea kati yake na Mohsein yalitokana na udhaifu wakibinadamu na sio Ushetani!

Jambo pekee ambalo alilionalingemuweka kwenye utulivu na amani katika kukabiliana na hali hiyoni kujipanga kuitunza siri hiyo isijulikane na John! Siri ndioingetumika kuliendesha zoezi hilo la kumtumikia John na Mohsein, kwasababu kwa upande wa John ni kuwa alimpenda, na kwa upande wa Mohseinni kwamba nafsi yake ilitaka awe naye. Hata hivyo, ili kuitunza sirihiyo alikiri mmoja alipaswa amjue mwingine na sio wote kutojuana!Alimwona Mohsein ndiye mwenye haki ya kutakiwa kumjua John, ili ajueni mchumba wake na anahitaji kuheshimiwa.

Hisia za Shetani!alijiambia wakati akiyawaza hayo. Lakini akazipuuza kwa kujiwekakibaolojia zaidi kuwa yeye ni binadamu wakati mwingine huendeshwa nanafsi yake inavyomshawishi! Akauona huo ndio ukweli wenyewe naanapaswa akabiliane nao!

Richard! Tukio la kumkumbuka lilikujakama onyo asilolitarajia, onyo lililomkumbusha kuwa kuna mtu muhimualiyekuwa amesahauliwa. Dina aliiona hatari iliyopo mbele yake endapoRichard atagundua mahusiano ya mapenzi yaliyopo kati yake na Mohsein!Alijua ugunduzi huo ungemletea Richard wivu wa mapenzi ambao aliaminiungeweza kuleta kizaaza cha kumpotezea kazi mmoja wao, ama yeye auMohsein! Au wote kwa pamoja! Dina alikuwa na uhakika Richard alikuwabado hajaachana na nia yake ya kutaka kumuoa, na alijua lazimaangekuja kumwomba ili warudiane. Dalili zilikuwa za wazi zilizokuwazikimuashiria kuwa Richard alikuwa bado akimuhitaji, kuanziauangaliaji wake hadi uzungumzaji. Kila kitu kilijidhihirisha kwa Dinakuwa, Richard alikuwa bado akiendelea kuteseka na penzi lake!

Tokeaawali, baada ya kuajiriwa na kufahamu kumbe Richard naye anafanyakazi kampuni hiyo hiyo, Dina alijipanga mapema kuwa, endapo Richardatamwomba waurudishe uhusiano wao, asingemkubalia! Na alijiandaakuitumia sababu ya kuchumbiwa na John kuwa ni kigezo cha kumkatalia.Alijua uamuzi huo ungeendeleza uadui kati yao, lakini aliaminiRichard asingeweza kumfukuza kazi kwa sababu sio yeye aliyemwajiri,bali ni baba yake!

Lakini ni hili tatizo jipya lililojitokezandilo lililokuwa likiichachafya akili yake. Mahusiano yake naMohsein! Hakutaka kujidanganya na tatizo hilo. Alijua ni tatizo kubwana lingeleta balaa endapo Richard atagundua kuwa yeye na Mohsein wanauhusiano wa mapenzi. Alikuwa na uhakika tatizo hilo litawasha moto wakutisha hapo ofisini kati ya watu hao wawili; Richard na Mohsein!Pengine hata kufikia kupigana au kufanyiana visa vya kuudhi. Hofuikaanza kumuumiza Dina na kichwa kikamuuma, mashaka yakamwingia kuwaanaweza akasababisha mtafaruku utakaoivuruga ofisi nzima na kusambaahadi kwa mzee Ken na mzee Ken angemwambia mama Richard na mamaRichard angemwambia mama Dina, na mama Dina angemwambia baba Dina nabaadaye taarifa hizo zingemfikia John!

Wote hao wangemwonayeye ndiye chanzo cha matatizo na mzigo wote wa lawama ungemwangukia.Uamuzi wa kufukuzwa kazi alikuwa na uhakika ungefanyika, na aliaminikusingetokea mtu yeyote kati ya hao ambaye angemwonea huruma,isitoshe hata wazazi wake wasingesita kumlaani kwa kupoteza kaziiliyokuwa ikimpatia kipato kizuri ambacho kingekuwa msaada mkubwa kwawazazi wake hao.

Akiwa amechanganyikiwa na kuzinduka kwakehuko, Dina alikurupuka kitandani na kuichukua simu iliyokuwa pembeniyake, akampigia Mohsein.

"Sema Dina," sauti ya Mohseinilisikika baada ya kuipokea simu. Ilikuwa nzito yenye kujiamini nailiyotulia, ikionekana kama aliyekuwa ametoka usingizini.

"Ulikuwaumelala?" Dina aliuliza kwa tahadhari, hakutaka kuingia moja kwamoja kwenye hoja.

"Siwezi nikasema hivyo, lakini nilikuwanimepitiwa na usingizi nikiwa kwenye kochi."

"Ulikuwaukifanya nini hapo kwenye kochi?"

"Nilikuwa naangaliaruninga nikapitiwa na usingizi. Vipi?" "Mohsein, kuna jambomuhimu nataka nikwambie," Dina alisema kwa sauti iliyokuwa naumakini.

"Niambie mpenzi," Mohsein alisema kwa kujiaminina kiburi cha ujivuni kikawepo ndani yake huku sauti yake ikiendeleakujenga kujiamini.
"Nakuomba uhusiano wetu asiujue mtu yeyotepale ofisini!"

Kimya kidogo kikapita, kisha Mohsein akasema,"Kwa nini unasema hivyo? Au unadhani mimi ni mropokaji?"
"Sinamaana hiyo, lakini sitaki watu wajue!"

"Ni hilo tu?"Mohsein aliuliza kiwepesi.
"Hofu ondoa, labda uje utamke wewemwenyewe kwa watu!"

Dina akagundua jinsi Mohsein alivyoijibuhoja hiyo kiwepesi. Akaingiwa na wasiwasi.
"Mohseinplease, niko serious!" alisema kwa sauti yenye kusisitiza.

"Mbonaunaonekana kama una hofu fulani?"

"Ni kweli nina hofuMohsein…stori yake ni ndefu, lakini nataka ujue kuwa, yeyoteatakayeufahamu uhusiano wetu na habari hizo zikamfikia Richard, ujueama sote kwa pamoja au mmoja wetu, kibarua kitaota nyasi!"

"Mbonasikuelewi Dina?" Mohsein aliuliza na safari hii sauti yakeiliondoka kwenye kujiamini na kutwaliwa na wasiwasi.

"Nistori ndefu kama nilivyokwambia, kesho asubuhi tutakapokutana ofisininitakuelezea."

Siku ya pili walipokutana, Dina alimpa ukweliwote Mohsein!

Ikawa ni mara ya kwanza Mohsein kutambua kuwa,Dina ana mchumba na harusi ingefanyika baada ya miezi mitatu ijayo.Akatajiwa jina la mchumbiaji na kukiri alikuwa hamjui. Lakini kibayazaidi ni pale alipoupata mshituko uliomwogopesha, aliposikia kuwa,hata Richard ni mmoja kati ya watu wanaowania kumuoa Dina!

* ** * *

Richard alirudi kutoka Morogoro baada ya siku tatuakaenda ofisini moja kwa moja. Alifika ofisini saa sita mchana,akawasalimu baadhi ya wafanyakazi aliojisikia kusalimiana nao.Aliwakuta Mohsein na Dina wakijiandaa kutaka kwenda kula chakula chamchana. Tukio hilo la kuwaona Mohsein na Dina wakitaka kutoka pamojalikapenyeza mchomo mkali wa wivu moyoni mwake.

"Dinanisubiri!" Richard alimwambia Dina kwa sauti iliyoonyesha ana jambomuhimu analotaka kulizungumza kwake. Kisha akatoka ofisini humo bilaya kusubiri jibu.

Dina na Mohsein wakaangaliana kwa machoyaliyoingiwa na wasiwasi, hofu ikaingia kwenye mioyo yao na kilammoja akaingiwa na sintofahamu ya agizo hilo.

"Kwani vipi?"Mohsein aliuliza kwa sauti ya chini kama vile alikuwa akiogopaRichard asisikie huko alipo.

Dina akayainua na kuyashushamabega yake. "Sijui!" alijibu. Mohsein akauangalia mlango waofisi yao kama vile alitarajia Richar angerudi tena. Kila mmoja akawaameingiwa na hofu kuwa, Richard amekwishapata habari ya mahusianoyao, lakini kila mmoja akashindwa kumwuliza mwenzake swalihilo.

"Kwa hiyo nikusubiri?" Mohsein aliuliza huku sautiyake ikionyesha kujiamini kwake kulishaondoka.

"Sio vizuriakituona tukiondoka pamoja!" Dina alisema kwa sauti yakuonya.
"Wewe nenda kale!"

Mohsein akawa kamaaliyepigwa butwaa na jibu la Dina.
"Kwa hiyo hutokuja?"aliuliza huku akionyesha kutoridhishwa na uamuzi wa Dina.

Dinaakaonekana kidogo kama amechanganyikiwa.
"Agh, Mohsein wenenda!" alisema huku sauti yake ikiwa na hasira. Hakutaka Richardawakute wakiwa bado wako pamoja humo ofisini ingawa ni ofisi yaokikazi. Hatia ilikuwa imemjenga. Kwa mara ya kwanza alijitambua kuwa,alianza kumwogopa Richard!

Mohsein akamwangalia Dina kwa usouliohamanika, akasema kwa unyonge, "Poa." Kisha akatoka na haliile ile ya unyonge.

Kila mmoja alikiri moyoni kuwa, ujio waRichard umekuja kutibua fungate yao ya siku mbili iliyokuwa imewapauhuru humo ofisini kwa kuonyeshana kuwa ni wapenzi wapendanao hukuwakifanyiana dalili zote za kimahaba na wakati mwingine walifikiahadi kujiamini kwa kuitumia nafasi ya kuwepo kwao wawili ofisinikunyonyana ndimi zao.

Ilikuwa kama vile Paka akiondoka…Ndivyo ilivyokuwa kwao!

Dina akiwa amebaki peke yake humoofisini baada ya Mohsein kutoka, alijikuta akishindwa kuendelea nakazi. Akili ilikuwa imekwama kuwaza jambo lolote, agizo alilopewa naRichard lilikuwa kama lililoitia akili yake ugonjwa wakiharusi.

Laiti isingekuwa mahusiano ya mapenzi aliyoyaanzishana Mohsein, kamwe agizo hilo lisingemshitua! alijiambia moyoni.Angejiamini kama alivyokuwa akijiamini siku za nyuma wakatialivyokuwa akiitwa na Richard ofisini na alikuwa hamwogopi hata palewalivyokuwa wakizungumza ana kwa ana. Lakini tukio hilo la kuanzishamahusiano ya mapenzi na Mohsein, ghafla kukawa kumeibadilisha halihiyo. Sasa alianza kumwogopa Richard tena kwa kasi kubwa kulikoalivyotarajia. Ikawa kama vile alikuwa amejitengenezea mwenyeweShetani wa kuja kumtisha!

Maswali yaliyotawaliwa na hofu kuwahuenda taarifa za mahusiano yake na Mohsein zimekwisha kumfikiaRichard yalikuwa yakirindima kichwani mwake na kuhisi hicho ndichoalichokuwa akiitiwa. Akajiuliza, ni kipi hasa alichokuwa akikihofia?Ni ile hofu ya kugundulika mahusiano yake na Mohsein? Au ni kufukuzwakazi baada ya kugundulika mahusiano hayo? Dina akakosa utulivu waakili wa kuchanganua mchanganuo huo!

Richard akaufungua mlangowa humo ofisini bila kupiga hodi. Hakuingia moja kwa moja, alisimamamlangoni na kuuzuia mlango usijifunge. Kitendo hicho kikamshituaDina, lakini kibaya zaidi ni pale alipoonyesha dalili zote zakumwogopa Richard! Bahati iliyoje, Richard akawa hakuuona wogauliokuwepo usoni mwa Dina.

"Njoo ofisini!" Richard alisemakwa sauti kavu, kisha bila ya kupoteza muda wala kuhangaikakumchanganya machoni Dina, akatoka.

Dina akashusha pumzi,akajizoa kitini na kusimama, kisha akatoka ofisini. Alimkuta Richardamekaa nyuma ya meza akiandika, Dina akaenda kukaa kwenye kitikilichopo mbele ya meza ya Richard kwa nidhamu ambayo hajawahikuifanya tokea siku aliyoanza kuingia kwenye ofisi hiyo.

Uingiajiwa Dina humo ofisini haukumfanya Richard auinue uso wake kumwangaliaingawa alijua kuwa ni Dina ndiye aliyeingia. Aliendelea kuandika kamavile hakuna mtu aliyeingia. Dina akaenda kukaa kwenye kiti cha wagenikilichopo mbele ya meza ya Richard. Kitendo hicho nacho hakikumshituaRichard kuinua macho yake kumwangalia mtu aliyekaa. Dakika kadhaazilipita huku akiendelea kuandika na bila ya kumsemesha Dina. Halihiyo ikawa inamtesa Dina Kisaikolojia na kujikuta akihofia hatakujikohoza. Ilikuwa ni kama vile ni zamu ya Richard kumtesaDina!

Hatimaye Richard aliacha kuandika, akauegemea mgongo wakiti kwa aina fulani ya ujivuni na kumtazama Dina kwa mara ya kwanzatokea alivyokuwa ameingia.

"Dina," Richard aliita kwasauti ya kuonyesha yeye ni bosi. Dina aliitikia kwa sauti iliyokwamakusikika vizuri.

Kabla ya kuendelea kuzungumza, Richardakaonekana kama vile ameigundua hali aliyokuwa nayo Dina, akaonyeshadalili ya kutaka kumwuliza kama alikuwa anaumwa.

"Jumatatutunakwenda Arusha kikazi!" Richard alisema ghafla. Ule mwonekanoaliouonyesha kutaka kuiulizia afya ya Dina ukawa umetoweka usonimwake. "Tunakwenda kufanya ukaguzi wa ndani wa mahesabu. Huendaikatuchukua wiki moja au zaidi," akanyamaza na kumwangalia Dinamachoni.

Dina akayakwepesha macho yake. Kauli ya Richardilikuwa shambulio alilokuwa hakujiandaa nalo.

"Ni moja yautaratibu wa kazi zetu ulivyo," Richard akaendelea bila ya kusubirijibu la Dina. "Huwa ni kawaida kwenda mikoani kufanya ukaguzi wandani wa mahesabu kila baada ya muda fulani, hutegemea na mkoawenyewe. Juzi na jana nilikuwa Mororgoro kwa shughuli kama hiyo. Kwahiyo mkoa unaofuata ni Arusha. Jiandae kwa safari hiyo!"
"Tunakwendawangapi?" Dina aliuliza.

"Wawili, mimi na wewe!" Richardalijibu kisha akamwangalia Dina kwa macho ya kuuliza kama ana swalijingine.

Dina akabaki kimya.

"Sawa?" Richardaliuliza na kumwangalia Dina kwa mtazamo wa kumsanifu.

Dinaalionyesha kusita, kisha akajibu kwa sauti ndogo yenye unyonge kwakusema, "Sawa."

* * * * *

Mohsein alirudiofisini baada ya kuutumia muda wa kula mchana kwa kunywa soda nakeki, hamu ya kula ilikuwa imemtoka! Alimkuta Dina akiwa amejiinamiaofisini. Kumwona Dina akiwa kwenye hali hiyo, moja kwa moja akajuaDina amepata tatizo na bila ya kujiuliza, akahisi tatizo hilolitakuwa limesababishwa na Richard!

"Vipi?" Mohseinaliuliza akiwa ameinama huku akijaribu kukiinua kichwa cha Dinaaliyekuwa amekilalisha juu ya meza.

Dina akakitikisa kichwachake kumtaka Mohsein amuachie. Mohsein akahisi kuna tatizo kubwakuliko alivyolichukulia awali.

"Dina!" Mohsein aliitaakiwa ameuondoa mkono wake kichwani kwa Dina na kuufanya mhimili wakewa kuegemea kwa kuukita juu ya meza.
"Mhh," Dina aliitikiabila ya kuuinua uso wake.

Mohsein akahisi Dina alikuwa akilia.Hali hiyo ikamchanganya! Akapatwa na kihere, "Kwani vipi?"aliuliza.
Badala ya kujibu, Dina akashusha pumzi kwa nguvu hukuakijiinua na kukaa vizuri. Hakuwa alikuwa akilia, lakini alionekanakuikaribia hali hiyo. Akaangalia juu ya meza kisha asisemelolote.

"Richard amekwambiaje?" Mohsein aliuliza hukuakiwa na uhakika ni Richard ndiye aliyemfikisha Dina kwenye halihiyo.

"Amenitaka niende naye Arusha kikazi!" Dina alisemabila kuondoa macho yake mezani. Sauti yake ilikuwa imenyongea na usowake kuonekana kuzidiwa na mawazo.

"Ahh!" Mohsein aligunakwa sauti iliyotaharuki.
"Lini?"aliuliza.
"Jumatatu!"

"Amekwambia mnaendawangapi?" Mohsein aliuliza kwa kihoro cha kuogopa jibuatakalopewa.

"Mimi na yeye!"

Mohsein akatoa tusi lakumtukana mzazi wa Richard!

Mchomo wa wivu ulikuwa umepenyamoyoni mwa Mohsein, akaonekana kuchoka kama aliyeibuliwa kutokakwenye msukule, akaongoza taratibu hadi kwenye meza yake na kukaa.Nguvu zilikuwa zimemuishia!

"Jamaa amepania!" Mohseinalisema kwa sauti ndogo na kuonekana kama aliyekuwa akiongea pekeyake.
"Umemjibu nini?" safari hii aliipandisha juu sauti yakekutaka Dina asikie.

Dina akamwangalia Mohsein kwa mara yakwanza tokea alivyokuwa ameingia.
"Ulitaka nimwambieje?"naye aliuliza kwa sauti ya taratibu huku akionekana hana chakujitetea.

"Mwambie unaumwa huwezi ukaenda!" Mohseinalibwata na kuonyesha wivu ulikuwa ukichukua nafasi yakekumchanganya.

Dina hakujibu. Kimya kikapita kati yao.

Kwamara ya kwanza, Mohsein akagundua ni kwa kiasi gani alikuwa akimpendaDina na kwa wigo gani aliokuwa akimhitaji awe naye karibu. Wivuulikuwa ukirindima na kumtafuna. Alihofu safari hiyo Richardaliipanga kwa kuikusudia kwa lengo la kupata faragha atakayoitumiakumbembeleza Dina ili atembee naye kimwili.

"Kwa hiyo?"Mohsein aliuliza kama -------- aliyechanganyikiwa huku akimwangaliaDina.

"Kwa hiyo?" Dina alirudishia swali kwa sauti ile ileya taratibu huku akionyesha kushangaa kwa kutomwelewaMohsein.

"Nenda kamfahamishe kuwa unaumwa na hutoweza kwendasafari hiyo!" Mohsein alisema kwa msisitizo.

"Wacha tu,niende!" Dina alisema kwa mkato.

"Uende naye Arusha?"Mohsein aliuliza kama vile hakuamini alichokisia.

"Ghaflanimwambie kuwa naumwa?" Dina alisema.
"Atanishangaakumlalamikia hivyo baada ya kutajiwa safari!"

"Yeye sialikuwa Morogoro! Utamwambia una karibu siku mbili ulikuwaunaumwa!"

"Atataka kujua kwa nini sikumwambia palepale? Naatataka kujua kama kazini nilikuwa nakuja siku zote. Akijua kamanilikuwa nakuja siku zote, atajua siumwi bali nasingizia ugonjwa kwakuikataa safari!"

Mohsein akanywea! Akaonekana kushindwakuendelea kumshawishi Dina aikatae safari hiyo.

"Kwanza wewekazi yenyewe hujaijua vizuri, kwa nini asinichukue mimi?" Mohseinalilalamika na kuuonyesha dhahiri kuumizwa na wivu aliokuwa nao."Kwani wewe Arusha huna ndugu?"

Uso wa Dina ukaonyeshamshangao kutokana na swali aliloulizwa. Akatingisha kichwakukataa.
"Sina!" alisema.
"Kwa nini unaniulizahivyo?"

"Kama ungekuwa na ndugu yeyote ningekushauriukalale kwake baada ya kufika Arusha."

Dina akatingisha tenakichwa na kusema, "Sina!"

"Mimi ninaye dada yangu,anaishi Kaloleni. Unaonaje nikiongea naye?"

"Ili nifikiekwake?" Dina aliuliza, akaonekana kumshangaa Mohsein. "Bila yakufanya hivyo huyu mshamba atakusumbua mkifika Arusha!

Atatakamfikie hoteli moja na pengine hata kukodi chumba kimoja!"
"Hilohalitawezekana!" Dina alisema na sauti yake ilijenga ubishi. "Etinini, achukue chumba kimoja? Hawezi akaniburuza kirahisi hivyo! Sibora niache hiyo kazi yenyewe!"

Kauli hiyo ikamfanya Mohseinkutaka kuiteka nyara hoja hiyo ili amshawishi Dina bora aache kazikuliko kwenda Arusha! Mtazamo wa wivu ndio uliokuwa ukimtesa, kwasababu alihofu endapo Dina atakubali kwenda Arusha, ni wazi kuwaRichard atakuwa na nafasi kubwa ya kumpata Dina! Lakini moyo wakehaukumpa ushujaa wa kuyatamka hayo. Alijua ungekuwa ni ushauri wakijinga uliotokana na wivu, alihofu Dina angemdharau. Badala yakeakaongea kwa kujitetea huku sauti yake ikinyongea. "Nina hakikamkifika Arusha atakuletea upuuzi wa kukutaka kimapenzi, ukimchekeashauri yako!"

Dina akafanya tabasamu dogo kumwonyeshaMohsein kuwa amemuelewa. "Mimi sio mtoto mdogo, haweziakanilazimisha!"

"Hata hivyo, bado ukifika unayo haki yakukataa kukaa naye hoteli moja! Hakuna sheria itakayokulazimishakukaa naye hoteli moja!"

"Mohsein," Dina aliita kwautulivu, kisha akaendelea, "Pamoja na kwamba mimi na Richard tunauadui wetu, lakini bado ni bosi wangu. Kuna mambo ambayo nawezakumkatalia, lakini sio ya kikazi! Safari tunayokwenda ni ya kikazi nahata kama tutakaa hoteli moja bado litakuwa ni suala la kikazi.Lakini pale atakapotaka kunilazimisha kukaa chumba kimoja na yeye,hilo litakuwa sio suala la kikazi tena na nitakuwa na haki yakumkatalia!"

***RICHARD ameamua kuvunja ukimya katika vita hii anataka kusafiri na DINA kikazi…je? Kitatokea nini hukombeleni……MOHSEIN ana wasiwasi mkubwa sana juu ya jambohili…..WIVU umemtawala bila kutarajia…….
***VIPI harakati zaJohn na waganga wa jadi!!
 
Back
Top Bottom