Riwaya ya kipelelezi: Wakala wa Siri

Mwandishi bado hujajirekebisha tu. Hili tukio la treni na watu wenye bunduki halikufaa kuwa hapa. Linaharibu mtiririko wa riwaya. Hapa huyu mtu atajiokoaje sasa kama matukio yamepandiliana namna hii. Hayampi nafasi.
Unaharibu riwaya kwa kuandika matukio impossible.
 
Chief usitake ije kama unavyotaka tulia fuata mtunzi alichokuandalia
Nchi hii bado sana. Unatutungia vitu mtu akisoma anaona kavisa siyo halisia. Akikosolewa mnakasirika? Kukosoa ni sehemu ya fasihi. Huwezi kututungia vitu vinavyokiuka misingi ya fasihi halafu tuchekelee tu. Tatizo wasomi wa siku hizi wametumia google kwenye kusoma. Upeo wa kufikiri ni mdogo.
Ndio maana mnatunga vitu visivyowezekana kwa akili ya kawaida.
 
Chief usitake ije kama unavyotaka tulia fuata mtunzi alichokuandalia
Unakosea sana.
Mtunzi ameleta riwaya humu siyo watu wasahihishe bali waburudike,waondoe stress na kujifunza.
Kama wiki mbili hivi zimepita watu walidai mwendelezo,wewe unaleta upinzani.
Lete riwaya yako tuone kama ukweli wewe ni mahili kwenye mpangilio.
Ungekuwa na busara hata kidogo ungemshauri nje ya hapa.

Mleta riwaya mpuuze hiyo twende kazi

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Hebu leta ile yako uliyotunga ambalo lina mtiririko vizuri tuone .
 
Sidhani kama umelezimishwa kusoma
 


Mkuu naomba nisikujibu Kwa heshima ya wasomaji wengine.

Sanaa ya uandishi wa FASIHI ni Pana mno,

Kuna Fiction Novels ambazo kazi yake ni Kueleza mambo yasiyowezekana, yasiyokuwepo, yakufikirika,

Wasanii wote wakubwa Duniani Kwa upande wa RIWAYA wameandika Fiction Novels mathalani Shaaban Robert, Kezilahabi, E. Semzaba, Ngugi, Ole seyinka, n.k.

Nakushauri uwe msomaji wa RIWAYA nyingi ili uzidi kuijua Fasihi Kwa undani,

RIWAYA niliyoandika ni RIWAYA ya kipelelezi ambayo Asilimia kubwa nimetumia uhalisia.

Je ungesoma RIWAYA yangu ya "SIKU YANGU YA KUFA ILIPITA" si ndio ungetoa povu mpaka basi

πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„

Relax hii ni KAZI ya Sanaa
 


πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„

Hayampi nafasi Nani Mkuu?

Relax Mkuu, fuatilia Simulizi
 
Sawa Mkuu. Mimi sijui.

Muhimu usome
Mdogo wangu sisi wengine si watunzi ila ni wasomaji wazuri wa riwaya ni kweli anachosema/anachoshauli huyo msomaji matukio yanafulilizana mno kiasi inafikia kupunguza radha

Hao wengine wanachotaka wewe utoe hii hadithi na wao waisome hawana habari ya ubora
Mimi kwa ushauri tu fuata ushauri unaopewa punguza kuunganisha matukio mengi kwa wakati mmoja ili kuleta uhalisia na radha
Mwisho nikupongeze wewe ni mtunzi mzuri jaribu kuzingatia ushauri utafika mbali katika tasnia hii
 


Nashukuru sana
 
Sasa si uhame nchi mkuu
 
Mkuu tupia muendelezo please.
Achana na wakosoaji!
 
Nimeshasoma zaidi ya vitabu mia tatu. Hivyo havitoshi?
 
Na kama utunzi wako ndio wa aina hii na kila unapokosolewa unakuwa mkali au kuejdelea kug'ang'ania aina ya huo uandishi wako. Hutofika mbali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…