Riwaya ya kipelelezi: Wakala wa Siri

Riwaya ya kipelelezi: Wakala wa Siri

ZUDU.jpg

ITAENDELEA.

Kitabu hiki kinamahusiano makubwa na Kitabu cha " MLIO WA RISASI HARUSINI" ambacho tayari kipo sokoni.

Jipatie Hardcopy kwa bei ya Ofa Tsh 10,000/= Ikatayodumu mpaka tar 14/10/2021

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
siri.jpg


WAKALA WA SIRI S2 EP 02
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA
Yule Mtu akiwa anaongea mara simu yake iliyokuwa mezani ikaita, jambo lililowafanya wote waitazame na kimya kidogo kitawale. Yule mtu akaichukua simu yake akapokea na kuiweka sikioni.

“ Hallo! Kweli! Upo wapi! Sawa nakuja sasa hivi” Yule mtu akasema akiongea na mtu wa upande wa pili simuni, kisha simu ikakatika.

“ Samahani nimepata dharura hapa, simu hii imetoka kwa moja ya viungo wetu waliopo maeneo mbalimbali hapa jijini, mambo yanazidi kunyooka, nafikiri niwaache muendelee na kikao mimi nikakutane na kiungo wetu huyu ili mambo haya yasilale. Mr. Gombe utaendelea kuendesha kikao hiki alafu utanipa maazimio” Yule mtu akasema kisha akatoka akiwaacha wenzake wakitamani kujua anaenda wapi.

ENDELEA

Ni katika chumba ambacho kulikuwepo na kitanda cha futi 3*6, pembeni lilikuwepo dirisha lenye pazi jeusi, kuta za chumba kile zilikuwa za rangi ya maziwa, sakafu ilikuwa ya vigae. Pembeni ya kitanda kulikuwa na stuli ambayo juu yake ilkuwepo taa ya sola iliyokuwa ikiwaka na kutoa mwanga uliotosha watu kuonana ingawaje haukuwa mwanga mkali. Juu ya kile kitanda alikuwa amelazwa Fernanda aliyekuwa hajitambui kwani alikuwa amepotza fahamu. Hapakuwa na mtu mwingine.

Muda kidogo ulipita, Fernanda akarejewa na fahamu, alijikuta akiwa amelala kwenye kitanda kisicho na godoro akiwa amefungwa mikono na miguuni huku mdomoni akiwa kawekwa kitu ili asiweze kupiga kelele.

“ Sasa hapa nitakuwa nipo wapi, yule mtu aliyeniteka kaenda wapi? Simu! Simu! Ile simu ndio ya muhimu. Kama wameichukua watakuwa wamenirudisha nyuma maili kadhaa” Fernanda akawaza huku akigeuza shingo yake upande huu na upande huu kukagua chumba kile. Kwenye kona kabisa akaona kimeza chenye droo, lakini hakuona vilivyopo juu yake kwani mwanga haukuwa na nuru ya kutosha kumfanya aone

“ Yule mtu aliyeniteka atakuwa ni nani? Anashida gani na mimi? Au ni hawa wanaomtafuta Sajenti, kwa kweli mambo haya yamenichosha, kila siku kusumbuliwa, nashindwa kufanya kazi zangu kisa kuwafahamisha alipokimbilia Sajenti. Hata kama ningekuwa nafahamu naapa nisingewaambia ng’oo” Fernanda akawaza lakini mawazo yake yalikatishwa baada ya mlango wa kile chumba kufungulia/ Akatangulia mwanaume mmoja aliyevaa tisheti iliyombana iliyochora kifua chake, akiwa kavalia na suruali ya kadeti, kisha akafuatia mtu aliyevalia suti ya kijani iliyomkaa vyema uso wake ukiwa nyuma ya miwani ya macho. Ndiye yule aliyekuwa akiongoza kikao cha siri.

“ Umefanya kazi nzuri sana. Alafu kumbe ni binti mrembo kabisa. Sasa inakuwaje binti mrembo kama huyu kujiingiza katika kazi za hatari namna hii?” Mtu yule akasema huku akisogea karibu na kitanda alichokuwa amelazwa Fernanda.

“ Embu washa taa nimuone vizuri” Yule mtu akasema na jambo hilo likafanyia, nuru ya taa ya umeme ikakijaza chumba chote na kuimeza nuru ya taa ya sola.

“ Waooh! She is an angel. Yuko na uzuri wa ajabu. Naweza muona vizuri sasa” Yule mtu asiye na jina akasema huku akitazamana na Fernanda.

“ Huyu Baba vipi, maneno yake ni dhihaka yananitia kichefuchefu” Fernanda akawaza huku akimtazama mtu yule mwenye asili ya kiarabu.

“Habari msichana mzuri, jina langu naitwa Abidin Wahid, ningependa kukufahamu. Sijui jina lako nani?” Abidin akasema akimtazama Fernanda kwa macho ya mtu mwenye kufurahia kuona kitu kizuri. Fernanda hakumjibu kitu, alikaa kimya huku akimtazama kwa hasira.

“ Msichana mzuri! Nimekuuliza unaitwa nani? Mbona hujibu, je wewe ni Bubu huwezi kusema?” Abidin akasema huku akimshika Fernanda kwenye kingo cha nywele zake usoni.

“ Hivi hawa wanaakili kweli? Kama machizi, Wameniwekea kitu mdomoni mimi nitaongeaje” Fernanda akawaza huku akiwa kaukunja uso wake.

“ Embu mfungue hiyo kamba mdomoni” Abidin akasema, yule mtu aliyejazia akamfungua Fernanda ile kamba mdomoni. Fernanda akavuta pumzi na kuiachia kama mtu aliyekuwa amebeba mzigo mzito.

“ Haya sasa tunaweza kuzungumza. Wewe ni nani, ulifuata nini kwenye nyumba ya Meja Venance, usiku wa manane kama huu?” Abidin akasema akimtazama Fernanda kwa macho ya upole kana kwamba ni mtu mwema. Fernanda bado alikuwa kimya zaidi ya yote akageukia upande wa pili kuwakwepa wasimtazame, Jambo hilo halikumfurahisha Abidin na yule Mwanaume mwenye mwili wa mazoezi.

“ Usitulazimishe kuwa watu wabaya, sisi ni watu wema, unapogeukia upande huo ni dalili ya dharau na kutupuuza, kamwe hilo siwezi kulivumilia na wote waliowahi kunionyeshea dharau walijutia maamuzi yao” Abidin akasema mara hii sauti yake ilikuwa mbali na sauti ya mwanzo aliyokuwa akizungumza, alizungumza kwa mitetemo ya hasira.

“ Haya msichana mzuri naomba unieleze, wewe ni nani na pale nyumbani kwa Marehemu Venance usiku huu ulikuwa unaraka nini?” Abidin akasema wakati huu akiwa amekishika kichwa cha Fernanda na kukigeuza kwa nguvu ili watazamane.

“ Mkuu huyu atatupotezea muda, kama hataki kwa hiyari tunaweza tumia nguvu” Yule mwanaume akasema.

“ Hapana Morris, Msichana huyu ni mzuri, tunapaswa tumuhoji kwa njia nzuri kama uzuri wake ulivyo, si ndivyo msichana?” Abidin akasema akimgeukia tena Fernanda pale kitandani.

“ Mnafiki Mkubwa wewe..” Fernanda akamtemea mate Abidin kisha akaendelea kusema;

“ Kama ningekuwa mzuri usingenifunga hivi, tangu lini Malaika akafungwa na pingu namna hii. Kama wewe usivyovumilia dharau ndivyo na mimi nisivyoweza kuvumilia kejeli na dhihaka” Fernanda akasema huku uso wake ukiwa umekasirika ungedhani jinni pori. Abidin alitoa kitambaa cha kujifutia mfukoni akajifuta, kisha kwa upesi kama umeme akamzaba kofi la uso Fernanda, lilikuwa kofi maridadi kabisa lililomfanya Fernanda aone Nyota na mwezi kwa wakati mmoja.

“ Unafanya makosa ambayo yataweza kukugharimu, ninaweza kukufanya uonekane kinyago watu wanaokufahamu wakakushangaa, nitakurarua..!” Abidin akafoka huku akimtolea maneno makali Fernanda huku akimkazia macho yake ambayo Fernanda aligundua ni yakidhalimu baada ya Abidin kutoa miwani usoni.

“ Mfungue hizo pingu” Abidin akasema,

“ Hapana Mkuu, huyu ni mateka hatari..”

“ Hatari? Kwa hiyo unamuogopa. Sivyo?” Abidin akasema akiwa kamkatisha Morris.

“Hapa sio kama namuogopa..”

“ Nimesema Mfungue hizo pingu” Abidini akasema kwa sauti ya juu yenye amri. Morris hakuwa na jinsi akamfungua Fernanda.

“ Mkuu, usidanganywe na uzuri wa huyu dada, huyu dada ni hatari kubwa, kama ungemuona mtu aliyemuua kule kwenye nyumba ya Meja Vennace nakuhakikisha wala tusingemfungua hizi pingu” Morris akasema akiwa tayari kamfungua Fernanda pingu za miguuni na mikononi. Fernanda alijisikia kaunafuu, mwili wake ulikuwa huru ingawaje alikaa kinyonge.

“ Hapa lazima nicheze na akili za hawa mbuzi, nijiweke kinyonge, nijilegeze na kulendea lendea ili wasiwe na hofu juu yangu, alafu baadaye niwashtukize. Mbona wataonja joto la jiwe” Fernanda akawaza huku akiwa bado kajilaza akiwa kafunguliwa pingu.

“ Unaweza kukaa ewe msichana mzuri” Abidin akasema huku akimtazama Fernanda na kumuashiria kwa macho akae. Fernanda akakaa akiwa kajinyong’onyesha”

“ Ni kweli tulifanya makosa kumfunga pingu Malaika, We made a mistake, please forgive us. Haya Bilashaka sasa tunaweza kuzungumza” Abidin akasema akiwa kairejesha sauti yake mfukoni kama awali akiongea kama mtu mwema anayepaswa kutumainiwa. Kisha akatoa Sigara Mfukoni akampa Fernanda, akaingiza tena mfukoni akatoa sigara nyingine na kiberiti cha gesi. Wakati huo Fernanda alikuwa keshaweka sigara mdomoni, Abidin akawasha kiberiti na kuiwasha sigara ya Fernanda aliyokuwa kaiweka mdomoni, kisha Abidin naye akaiweka sigara mdomoni mwake, akakiwasha kiberiti na kuiwasha sigara yake. Kimya kidogo kilipita wakati wawili hao wakiwa wanavuta sigara, Morris akiwa makini kuzichunga nyendo za Fernanda asijeleta hila yoyote.

“ Naomba nijitambulishe tena, Niite Abidin Wahid, huyu ni kijana wangu anaitwa Morris. Nafurahishwa kuwa nawe usiku huu mnene, nilipokuwa mdogo nilisomaga kitabu kilichokuwa kinajina “Angels descend during the great night” kilikuwa kitabu kizuri sana. Kilieleza kuwa Malaika wazuri hushuka nyakati wa usiku mkuu kama huu. Miaka kadhaa imepita leo nimethibitisha maneno ya kitabu kile. Naamini hata malaika wanamajina, tena majina mazuri. Haya embu nambie jina lako waitwa nani?” Abidin akasema kwa sauti iliyotulia, hakika maneno yake kwa mwanamke dhaifu huweza kuuchota moyo wake, lakini haikuwa kwa Fernanda.

“ Ninaitwa Fernanda, malaika jike mtoa roho” Fernanda akasema huku akiangaza macho yake huku na huku. Maneno hayo yakamfanya Abidin atabasamu,

“ Mwanamke huyu ni mzuri kama nini, lakini pia anasauti zuri mithili ya ndege waimbao asubuhi” Abidin akawaza.

“ Malaika mzuri mtoa roho, nini ulichokuwa unakitafuta katika nyumba ya Meja Venance?”

“Labda ningetangulia kwanza kuwauliza ninyi, jambo gani limewafanya mnikamate nikiwa katika nyumba ya Marehemu Meja Venance? Ninyi ni kina nani? Mkinijibu hayo basi nitawaambia kilichonipeleka kwa Meja” Fernanda akasema, kisha wote wakapeleka sigara mdomoni wakavuta pafu ndefu kisha wakaachia na kutoa moshi mzito mdomoni na puani ulioziba nyuso zao kwa kitambo.

“Ninyi ndio mlimtuma yule mwenzenu niliyemuua kule kwa Meja Venance?” Fernanda akauliza baada ya kuutupa moshi nje yam domo na pua zake.

“ Umeua! Hivi kumbe ni kweli..” Abidin akakatishwa na Morris

“ Mkuu nilikuambia nilipofika kule kwa Meja Venance, baada ya kumzimisha huyu, niliingia kwenye nyumba ya Meja, nikakuta mwanaume wa miraba minne ameuawa muda mfupi tuu. Nikajua aliyemuua ni huyu mwanamke hapa..” Kabla Morris hajamaliza kuongea Fernanda alimpulizia Morris moshi mwingi usoni uliompata sawia, na kwa upesi akamrukia Abidin na kumpiga ngumi mbili mfululizo zilizomfanya Abidin aanguke chini, lilikuwa shambulizi la kushtukza ambalo kamwe yeyote kati yao hakuwa amelitarajia. Bila kupoteza nafasi huku akijua kuwa anacheza na mdomo wa mamba, Fernanda akamrukia yule mwanaume mgongoni na kumpiga visukusuku vya kichwa kama vitatu, yule mtu akaanguka chini. Abidin akiwa pale chini akawaa anahangaika kuitoa bastola yake ili ampige Fernanda lakini kabla hajaikoki aachie risasi bado akiwa amemnyooshea bastola Fernanda, masikini alikuwa kachelewa, Fernanda alimrukia Free Kick na kuupiga mkono bastola ikaruka juu na kabla haijafika chini Fernanda akaiwahi kuidaka, wakati huo Morris alikuwa akija nyuma kwa kasi ili ampige Fernanda, kama paka akajibetua ili amkwepe Morris, ndio alifanikiwa kumkwepa lakini aliparazwa kidogo na mkono wa morris jambo lililomfanya apepesuke na kupoetaza muelekeo akaangusha bastola. Morris akaenda kumuangukia Abidin pale chini. Kama mtu mmoja wakaamka kwa pamoja Morris na Fernanda wakawa wanatazamana kwa hasira na uchungu wa kuuana, macho yao yakaenda pamoja mpaka ilipoandukia Bastola. Bahati mbaya bastola ilikuwa karibu zaidi ya Morris kuliko aliposimama Fernanda. Morris alivyoona hivyo akatabasamu huku macho yake bado yakiwa makini kutazamana na Fernanda.

Morris akafyatuka kama mshale kuiwahi ile bastola lakini akiwa kainama kabla hajaiokota, Fernanda akainyanyua stuli ambayo juu yake ilikuwepo taa ya sola. Akampiga nayo ya kichwa, Morris akaanguka na damu zikamtoka mdomoni, wakati huo Abidin alikuwa akinyanyuka kwa upesi kuifuata ile Bastola lakin naye alikuwa kachelewa, Fernanda alimrukia akampiga teke la uso Abidin akaangukia upande ilipomeza akaigonga ile meza na mara vitu vilivyokuwa juu ya meza vikaanguka. Macho ya Fernanda yalihamanika alipoiona ile simu ya Meja Venance aliyoichukua kule nyumbani kwake. Kwa upesi Fernanda akachukua bastola akamuelekezea Abidin aliyekuwa pale chini akimtazama Fernanda kwa macho ya kuomba msaada. Kabla Fernanda hajataka kumpiga risasi akasikia kuna sauti ya mtu akija, kwa upesi akaiokota ile simu. Kisha akamnyanyua Abidin na kumkaba akiwa kamuwekea risasi shingoni. Mlango ukafungulia akatokea mwanaume aliyevalia suti nzuri iliyosimama. Yule mwanaume alikuwa hajajiandaa vyema kwani hakujua kuna hatari yoyote, hivyo alikuwa amekuja mzima mzima kama kifurushi kinachopelekwa na maji. Fernanda hakutaka kupoteza muda akampiga risasi ya kichwa yule kijana akadondoka chini.

Jambo hilo likazidi kumuogopesha Abidin, lakini pia likampa wasiwasi Fernanda kwani bastola haikuwa na kiwambo cha kuzuia sauti, hima hima Fernanda akatoka akiwa kamuweka Abidin kama ngao yake. Akafungua mlango na kuchungulia upande huu na upande huu, hapakuwa na mtu isipokuwa korido ndefu sana.

“ Njia ya kutoka humu ni ipi?” Fernanda akauliza.

“ Hautafanikiwa kutoka humu ndani. Upo gorofa ya chini kabisa katika jengo hili. Umejiingiza katika matatizo makubwa sana Fernanda” Abidin akasema. Fernanda akampiga na kitako cha bastola,

“ Nimekuuliza njia ya kutoka humu ni ipi? Sitaki maelezo mengine” Fernnda akasema akiwa amekasirika. Kabla hajajibu sauti za watu wanaokimbia zikasikika zikija mkukumkuku upande walipo wakina Fernanda. Hapo Fernanda akajua sauti ya risasi waliisikia.

“ Nimekuambia hautafanikiwa kutoka hapa, ni bora ujisalimishe huenda ukaonewa huruma lakini kwa kitendo ulichokifanya cha kuua vijana wangu sina uhakika kama hilo litawezekana” Abidin akasema huku akitabasamu, sauti yake sasa ilijawa na nguvu baada ya kusikia wenzake wakija kumuokoa. Fernanda bila kupoteza muda akamkokota Abidin upande mwingine wa korido ambao hakusikia watu wakija.

“ Huku unaenda wapi msichana mzuri? Huku hakuna njia” Abidin akasema lakini Fernanda hakuwa akimsikiliza alimkokota wakatokea sehemu yenye mgawanyiko wa njia mbili zenye korido ndefu pia.

“ Nambie njia ya kutokea ni ipi, nitakuua usiniletee upuuzi. Sema njia ni ipi?” Fernanda akampiga Abidin risasi ya paja, abiding akapiga ukulele wa maumivu.

“ Unaniua! Unaniua wewe shetani! Nakuhakikishia utalipia” Wakati Abidin akisema hayo mara wale watu waliokuwa wakija wakatokea wakiwa na silaha za moto, Fernanda akawarudisha kwa kupiga risasi jambo lililowafanya wajibanze. Fernanda akazidi kumkokota Abidin akisonga kuwakimbia watu wale, punde jengo zima likaanza kulia alamu ya kuashiria kuna hatari,

“Kumekucha! Kazi ndio imeanza hapa, hawa mbuzi wanaitana humu. Lazima niharakishe kuondoka, nikileta mchezo inaweza kuwa hatari kwangu, hii ndio nafasi ya pekee ya kujiokoa ambayo naamini haiwezi jirudie tena” Fernanda akawaza huku akimkokota Abidin kama mzigo, Hata hivyo akaona Abidin anamuelemea.

“ Chagua nikuue au unasema njia ilipo?” Fernanda akamsukuma Abidin akaanguka chini alafu akamuwekea bastola kichwani.

“ Subiri Fernanda, usiniue. Pita njia hii itakutoa” Abidin akasema kwa maana macho aliyoyaona kwa Fernanda hayakuwa macho ya kibinadamu, yalimuambia kuwa akileta mchezo yatafyonza roho yake. Fernanda akampiga Abidin kitako cha bastola, Abidin akapoteza fahamu. Fernanda akampekua Abidin mifukoni lakini kabla hajafika mbali sauti kali ya amri ikitokea mita kama hamsini ikasikika ikisema;

“ Tulia hivyo hivyo”

ITAENDELEA.

Kitabu hiki kinamahusiano makubwa na Kitabu cha " MLIO WA RISASI HARUSINI" ambacho tayari kipo sokoni.

Jipatie Hardcopy kwa bei ya Ofa Tsh 10,000/= Ikatayodumu mpaka tar 14/10/2021

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
ZUDU.jpg

ITAENDELEA.

Kitabu hiki kinamahusiano makubwa na Kitabu cha " MLIO WA RISASI HARUSINI" ambacho tayari kipo sokoni.

Jipatie Hardcopy kwa bei ya Ofa Tsh 10,000/= Ikatayodumu mpaka tar 14/10/2021

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
Riwaya inakosa mvuto. Matukio yanapandiliana sana. Hayatoi nafasi. Tukio moja likiisha inatakiwa kupatikane mpenyo wa jambo lingine siyo kupandiliana.
Mfano Fernanda anatafuta upenyo wa kutoroka lakini hatuuoni maana kuna mtu yuko mita hamsini anamweka mtu kati.
Sasa riwaya ya namna hii inachosha. Haileti uhalisia. Inatakiwa mtunzi atuoneshe Fernanda ametoroka kwenye jengo lile ili kama kuna tukio lingine la kuwekwa mtu kati litokee baadaye baada ya kisa cha kutoka kwenye jengo kimeeleweka.
Niliisoma riwaya ya Mlio wa Risasi Harusini.
Ukweli ni riwaya nzuri lakini matukio yanapandiliana. Hayapumziki kuleta uhalisia.
Watunzi wa kizazi cha leo someni riwaya za zamani muone mtiririko wa matukio.
Yalikuwa yanavutia kuliko ilvyo kwenye hizi riwaya za kileo.
 
Riwaya inakosa mvuto. Matukio yanapandiliana sana. Hayatoi nafasi. Tukio moja likiisha inatakiwa kupatikane mpenyo wa jambo lingine siyo kupandiliana.
Mfano Fernanda anatafuta upenyo wa kutoroka lakini hatuuoni maana kuna mtu yuko mita hamsini anamweka mtu kati.
Sasa riwaya ya namna hii inachosha. Haileti uhalisia. Inatakiwa mtunzi atuoneshe Fernanda ametoroka kwenye jengo lile ili kama kuna tukio lingine la kuwekwa mtu kati litokee baadaye baada ya kisa cha kutoka kwenye jengo kimeeleweka.
Niliisoma riwaya ya Mlio wa Risasi Harusini.
Ukweli ni riwaya nzuri lakini matukio yanapandiliana. Hayapumziki kuleta uhalisia.
Watunzi wa kizazi cha leo someni riwaya za zamani muone mtiririko wa matukio.
Yalikuwa yanavutia kuliko ilvyo kwenye hizi riwaya za kileo.


Tupo pamoja
 
siri.jpg



WAKALA WA SIRI EP 03
Mtunzi; Robert Hereil
0693322300

ILIPOISHIA

Kumekucha! Kazi ndio imeanza hapa, hawa mbuzi wanaitana humu. Lazima niharakishe kuondoka, nikileta mchezo inaweza kuwa hatari kwangu, hii ndio nafasi ya pekee ya kujiokoa ambayo naamini haiwezi jirudie tena” Fernanda akawaza huku akimkokota Abidin kama mzigo, Hata hivyo akaona Abidin anamuelemea.

“ Chagua nikuue au unasema njia ilipo?” Fernanda akamsukuma Abidin akaanguka chini alafu akamuwekea bastola kichwani.

“ Subiri Fernanda, usiniue. Pita njia hii itakutoa” Abidin akasema kwa maana macho aliyoyaona kwa Fernanda hayakuwa macho ya kibinadamu, yalimuambia kuwa akileta mchezo yatafyonza roho yake. Fernanda akampiga Abidin kitako cha bastola, Abidin akapoteza fahamu. Fernanda akampekua Abidin mifukoni lakini kabla hajafika mbali sauti kali ya amri ikitokea mita kama hamsini ikasikika ikisema;

“ Tulia hivyo hivyo”

ENDELEA..
“ Tulia hivyo hivyo”

Fernanda akageuka nyuma ilipotokea sauti hiyo akaona watu wawili waliomuelekezea bunduki wakiwa wamevaa suti nyeusi na miwani nyeusi usoni.

“Sipaswi kuchelewa kufikiri, lazima nifanye upesi kujinasua hapa wasije kuninasa” Fernanda akawaza akiwa kasimama akiwatazama. Kwa upesi wa kustaajabisha akajirusha chini akajiviringa kama jongoo, akaanza kuviringa kama gunzi la muhindi wakati huo risasi zikimfuata kwa uchu, kila alipoondoa mwili wake risasi za moto zikichimba eneo hilo, ilikuwa ni mchezo hatari aliokuwa akiucheza Fernanda ambao unafanana kabisa na kuchezea kifo. Wale wavaa suti wakaendelea kumrushia Fernanda risasi wakijaribu kuipata shabaha lakini kila walipojaribu walimpunyua punyua; Punde kiza kikatawala baada ya Fernanda kuipiga taa ya umeme iliyokuwa inawaka kwenye korido ile. Watu wale walishikwa na mduwao kwa sekunde, giza liliwapumbaza lakini ghafla akili zao zilirejea mchezoni baada ya Fernanda kuachia risasi, wakaanza kupiga hovyo hovyo risasi kwani walikuwa hawamuoni kutokana na giza, Risasi za moto walizokuwa wakiziachia zilifanya eneo walilosimama kuwa na mwanga, moja ya wale wavaa suti akamshika mwenzake bega;

“ Stop! Acha! Nimesema Acha! Kupiga hivi tunaweza kumpiga mwenzetu Abidin,” Mmoja wa wale wavaa suti akasema, kisha kimya kizito kilichopambwa na giza kikatawala katika korido ile. Wale wavaa suti wakagawana ukuta katika korido ile wakaanza kutembea kuelekea kule alipokuwa Fernanda,

“ Kuko kimya sana, atakuwa keshakimbia” sauti ya moja ya wale wanaume ikasema. Fernanda alikuwa keshakimbia kwenye ile korido. Sauti ya watu wanaokimbia zilikuwa zikisikia zikija upande wa ile korido, haikuchukua dakika walifika wakiwa na silaha nzito; wakawakuta wale wavaa suti wakiwa kwenye kiza totoro.

“ Hakuna mwenye tochi” Sauti ikasikika kutoka kwa wale wanaume, sekunde chache tochi ikawaka na korido yote ikajazwa na nuru. Wale wavaa suti wakamulika upande alikokuwa Fernanda, hawakumuona, alikuwa keshawakimbia, wakamuona Abidin akiwa kalala pale chini wasijue kama ni mzima au amekufa. Wakamkilimbia bado bunduki zao zikiwa makini mikononi tayari kwa kukabiliana na hatari yoyote endapo ingejitokeza.

“ Mapigo yake yapo chini sana, wawili wambebe wampeleke kwenye chumba cha matibabu. Sisi wengine tuliobaki tutaendelea kumfukuzia huyu mdudu mdogo aliyefanya haya, lazima tumkamate, nina hakika hawezi kutoka ndani ya jengo hili kwani upande alioelekea hakuna njia rahisi ya kutokea, Alafu ni mtoto wa kike, hawezi akatushinda wanaume,” Mwanaume mmoja mwenye ndevu nyingi na uso mrefu akasema, akameza mate kisha akaendelea.

“ Tupo saba hapa, wawili wakimpelekea Abidin tutabaki watano, tunatosha kabisa kuifanya kazi hii. Haya kazi ianze” Yule mwanaume akasema, bila kujadiliana wanaume wawili wakambeba Abidin kumpeleka chumba cha matibabu, kisha wale watano wakasonga mbele kuufuata uelekeo aliokimbilia Fernanda, walitembea kwa kasi huku miendoko yao ikiwa yakibabe yenye tahadhari zote za kivita. Wakatembea kwa dakika moja wakafika mahali ambapo kuna njia mbili, njia ya kwanza ilikuwa ni korido ya upande wa kuchoto; njia ya pili ilikuwa upande wa kulia lakini ni ngazi zinazoshuka chini. Hapo wakasimama, yule mwanaume mwenye ndevu na uso mrefu akaonyesha ishara wawili wataenda upande wa kulia, alafu watatu wataambatana naye kuifuatanjia iendayo chini yenye ngazi. Muda wote kulikuwa na giza, walikuwa wakisaidiwa na taa ya kurunzi pamoja na taa za simu walizokuwa nazo.

“ Mkuu hili giza kwetu linaweza kuwa ni mtego wa kifo, huyu mwanamke mshenzi inaonekana kila alivyopita alipasua taa kwa risasi ili kutupa sisi changamoto ya kutokuona vizuri. Napendekeza tuagize kurunzi ziletwe zitakazotusaidia, hasa ninyi mnaoelekea upande wa chini kabisa wa jengo hili” Mwanaume mmoja akasema, jambo ambalo likaonekana kukubaliwa na wengi.

“ Kwa muono wangu, hakuna haja ya kwenda kuchukua kurunzi, naamini huyu mwanamke mshenzi atakuwa katumia njii hii ishukayo chini, giza la upande wa korido ya kushoto naamini limekomea pale kwenye ile kona, si unaona pale kuna mwanga hafifu?” Yule mwanaume mwenye uso mrefu na midevu akasema, wenzake wakageuka kutazama korido ya upande wa kushoto, walipoona kwa mbali mwanga hafifu wakakubaliana na yule mwanaume ambaye bila shaka ndiye mkuu wao.

“ Sisi tutakaoenda upande wa chini ndio tutakaoenda na kurunzi, ninyi wawili mtaenda hivyo hviyo. Sawa? Haya tutawanyike. Hakikisheni mkimuona mnamtia nguvuni iwe akiwa hai au akiwa amekufa. Sawa?” Mwanaume yule akasema kwa sauti yenye amri na wote wakatawanyika. Wakasonga wakishuka ngazi kwenda chini kwa kitambo wakizunguka ngazi zile zilizokuwa zikienda chini, kila walipopita kulikuwa kiza. Fernanda alikuwa amezipasua taa zile kwa risasi.

*****************

Fernanda akaokea upande wa chini kabisa, huku hakukuta taa yoyote, kulikuwa na giza totoro ambalo lilimfanya asione hata hatua moja kwenda mbele. Akayafumba macho yake na kuyaminya kwa nguvu kama sekunde thelasini alafu akayafumbua, mbinu hiyo hutumika kuyafanya macho yalizoee giza, hasa giza totoro, angala kidogo sana akaweza kuona mbele kama hatua moja. Akasonga hatua mojamoja za tahadhari kuifuata ile korido ambayo hakujua ingemfikisha upande gani. Mkononi akiwa bado ameishikilia bastola yake akasonga mpaka alipofika ukingo wa ile korido ambapo mbele yake alipata kizuizi, hapakuwa na njia. Moyo wa Fernanda ukakosa utulivu, mapigo ya moyo yakawa kama yametelekezwa, yakawa yanadunda bila mpangilio, tayari alinusa hatari iliyokuwa inamkabili, akapapasa ukute ule uliokuwa kizuizi kwake, punde akashtuka kugusa chuma, akagusa zaidi , ilikuwa ni geti dogo la chuma lililokuwa limefungwa, Kwa jinsi alivyokuwa akilishika, akili yake ikamuambia kuwa geti lile lilikuwa limeshika kutu, na lilikuwa na mchanganyiko wa vumbi na utando wa buibui.

Fernanda akapapasa zaidi akagusa kitu kama kufuli, “Mlango huu unaonekana haujafunguliwa muda mrefu, mpaka kufuli linashika kutu” Fernanda akawaza akiwa anaendelea kulishika lile kufuli. Akajaribu kulivuta kwa chini kuona kama litafunguka lakini wapi, halikufunguka, akapata wazo kuwa atumie bastola kuivunja ile kufuli, wazo hilo akakubaliana nalo. Akaikoki bastola, akasimama alafu akalenga shabaha kwenye lile kufuli. “PAAAH” Kufuli ikavunjika na kufunguka,

“ Mlio huu wa risasi utawapa uelekeo wale majitu na kujua mahali nilipo. Yanipasa niharakishe” Fernanda akawaza. Kisha akauvuta ule mlango kwa nguvu lakini bado mlango ukagoma kufungua. Fernanda akapandwa na hasira. Akauvuta tena lakini haukufunguka, akaona ausukume lakini juhudi zote zilikuwa sawa na bure. “ Nini kinazuia huu mlango usifunguke, mambo haya yananichosha sasa” Fernanda akawaza, ghafla nuru hafifu kutokea upande wa nyuma ikazuka. Fernanda akageuka nyuma, hakuona mtu lakini akaona mwale wa kurunzi ulioangza ile korido umbali wa mita thelasini.

“ Ohh Come on! Haya mashetani yanakuja, Mlango funguka tafadhali” Fernanda akasema kwa sauti ya chini akijaribu kuuvuta na kusukuma lile geti. Ule mwanga ukawa unazidi kuongezeka, kadiri ulivyokuwa ukiongezeka kwa kasi ndivyo hofu ilivyozidi kuziharibu hisia za Fernanda, jambo asilolitegemea likatokea, macho yake yakajawa na mshtuko, Fernanda akaona mnyororo kwa juu kabisa uliozunguka kulifunga geti lile, kama sio mwanga ule kuongezeka basi Fernanda asingeweza kuuona ule mnyonyoro. Kwa upesi akainyanyua bastola yake akaupiga ule mnyororo Paah! Lakini mnyororo haukukatika, mlio wa risasi ukafanya mwanga uzidi kuongezeka kwa upesi, hii ilimaanisha kuwa wale watu wabaya waliokuwa wakimfukuza walikuwa wakikimbia kumfuata, Fernanda akapiga risasi ya pili, mnyororo ukakatika. “ Vizuri sana. Umefanya kazi nzuri, siku zote nakuaminia” Fernanda akasema kwa sauti ndogo akiiambia bastola yake na kuibusu. Kisha akaanza kuvuta lile geti, akaona halifunguki, akatazama nyuma kwa wasiwasi kuangalia kule mwanga unapotokea, akaona asukume kwa nguvu lile geti badala ya kulivuta, “ Vizuri” Geti likafunguka Fernanda akiwa hoi hofu ya kifo ikimsakama. Fernanda hakutaka kupoteza muda. Akasonga kufuata njia ile, lilikuwa ni handaki kubwa la mviringo ambalo lilimfanya atembee kwa uhuru pasipo kichwa chake kugusa dari. Mwanga ule hafifu ulimsaidia kidogo kuona mbele yake lakini kadiri alivyokuwa akitembea ndivyo giza nene la lile handaki lilivyokuwa likimlaki. Nusu dakika wale wanaume waliovalia suti wakatokea wakiwa wanakuja mbiombio wakilifuata geti lililovunjwa na Fernanda. Hatua zao zilidhamiria, sura zao zilizingirwa na hasira kali zenye kiu ya kumwaga damu. Kadiri walivyokuwa wakimfukuza ndivyo hamu ya kuinyonya damu yake ilivyoongezeka. Fernanda akageuka nyuma akiwa anakimbia katika handaki lile, aliona wanaume watatu wakiwa wamelikaribia lile geti alilolivunja. Fernanda akaongeza kasi lakini kwa woga kwani alikuwa haoni vizuri mbele, Akasonga na kusonga nyuma yake wale watu wabaya wakimuandama pasipo kuchoka, ingawaje watu wale bado walikuwa hawajamuona ila waliamini kuwa Fernanda hakuwa mbali na eneo lile kutokana na mlio ule wa risasi waliousikia.

Fernanda akakimbia lakini macho na akili yake vikashikwa na machale kuwa mbele yake kunatatizo, akapunguza mwendo, akatembea kwa tahadhari, kitambo kidogo macho yake yakashtuka kuona kizuizi kilichozuia njia, Fernanda akasogelea kile kizuizi, akashusha pumzi nzito na matumaini ya kuwatoroka wale watu wabaya yakayeyuka. Njia ilikuwa imezibwa na kizuizi mfano wa Pangaboya kubwa lenye kutu, Fernanda akaenda kulishika lile pangaboya kubwa lenye kutu; akalizungusha kwa nguvu zake zote lakini hakuwa na nguvu hata kidogo ya kuweza kulizungusha, akajaribu tena kwa nguvu zake zote lakini ilikuwa kazi bure, halikuzunguka, Fernanda akaona ajaribu kupitisha kichwa kwenye nafasi ndogo iliyokuwepo kwenye lile pangaboya ili apite upenda wa pili, kichwa chake kikafanikiwa kupita akapokelewa na harufu mbaya ya uvundo iliyokuwa upande wa pili na giza nene kushinda alipokuwa anatoka. Lakini ingekuwa bora harufu hiyo kuliko kukamatwa na wale watu wabaya wenye roho za kikatili. Fernanda akajaribu kupitisha mabega yake lakini hilo likashindika, akajaribu zaidi na zaidi lakini hakuweza, akarudisha kichwa chake akawa anapumua kwa kasi, akageuka nyuma akaona kwa mbali mwanga wa kurunzi ukisogea kwa kasi kuja kule aliko,

ITAENDELEA.

Kitabu hiki kinamahusiano makubwa na Kitabu cha " MLIO WA RISASI HARUSINI" ambacho tayari kipo sokoni.

Jipatie Hardcopy kwa bei ya Ofa Tsh 10,000/= Ikatayodumu mpaka tar 14/10/2021

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
ZUDU.jpg

ITAENDELEA.

Kitabu hiki kinamahusiano makubwa na Kitabu cha " MLIO WA RISASI HARUSINI" ambacho tayari kipo sokoni.

Jipatie Hardcopy kwa bei ya Ofa Tsh 10,000/= Ikatayodumu mpaka tar 14/10/2021

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
siri.jpg


WAKALA WA SIRI EP 04
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA

Fernanda akakimbia lakini macho na akili yake vikashikwa na machale kuwa mbele yake kunatatizo, akapunguza mwendo, akatembea kwa tahadhari, kitambo kidogo macho yake yakashtuka kuona kizuizi kilichozuia njia, Fernanda akasogelea kile kizuizi, akashusha pumzi nzito na matumaini ya kuwatoroka wale watu wabaya yakayeyuka. Njia ilikuwa imezibwa na kizuizi mfano wa Pangaboya kubwa lenye kutu, Fernanda akaenda kulishika lile pangaboya kubwa lenye kutu; akalizungusha kwa nguvu zake zote lakini hakuwa na nguvu hata kidogo ya kuweza kulizungusha, akajaribu tena kwa nguvu zake zote lakini ilikuwa kazi bure, halikuzunguka, Fernanda akaona ajaribu kupitisha kichwa kwenye nafasi ndogo iliyokuwepo kwenye lile pangaboya ili apite upenda wa pili, kichwa chake kikafanikiwa kupita akapokelewa na harufu mbaya ya uvundo iliyokuwa upande wa pili na giza nene kushinda alipokuwa anatoka. Lakini ingekuwa bora harufu hiyo kuliko kukamatwa na wale watu wabaya wenye roho za kikatili. Fernanda akajaribu kupitisha mabega yake lakini hilo likashindika, akajaribu zaidi na zaidi lakini hakuweza, akarudisha kichwa chake akawa anapumua kwa kasi, akageuka nyuma akaona kwa mbali mwanga wa kurunzi ukisogea kwa kasi kuja kule aliko,

ENDELEA..

“ Sasa hapa nitafanya nini? Mbona nimekamatika kirahisi hivi, sitakubali kukamatwa mzima mzima kama kuku wa sikukuu” Fernanda akawaza huku akiuangalia ule mwanga wa kurunzi unaokuja upande wake. Akili yake ilikuwa kama ngeredere anayerukia tawi hili na hili kumkimbia mkulima aliyeiba mahindi yake. Fernanda akageuka tena upande wenye kizuizi mfano wa pangaboya kubwa ya chuma iliyoshika kutu, mara hii mwanga ulikuwa umeongezeka kutokana na miale ya kurunzi ya wale watu wabaya, Fernanda akalikagua lile pangaboya kwa juu akaona kitu mfano wa Mkasi kilichozuia lile pangaboya lisizunguke, kwa upesi huku akijua hana muda mwema uliobaki, akarukia ule mkasi na kuuvuta kwa chini, lile pangaboya likaanza kuzunguka, “Vizuri” akasema kimoyomoyo. Akageuka nyuma wakati huu wale watu wabaya walikuwa washamuona na kuanza kumrushia risasi ambazo zilikuwa zilimpunyua na kulipiga lile pangaboya. Fernanda hakuwa na muda wa kupoteza, akasubiria upande wa pangaboya wenye nafasi kubwa ya yeye kupenya, hata hivyo kumbe lile pangaboya lilikuwa likizunguka polepole lakini kadiri linavyoendelea kuzunguka ndivyo linavyoongezeka kasi yake. Fernanda kwa kuona hivyo akarukia ile nafasi na kuzamia upande wa pili, kisha akalishika lile pangaboya na kulizungusha kwa kasi kuliongezea kasi yake ili wale wavaa suti za mauti wasimfikie. Kitendo cha kufanya kulizungusha lile pangaboya kulifanya kasi yake iongezeke maradufu asiwepo mtu awezaye kupita katikati yake. Fernanda akashusha pumzi kwa nguvu baada ya kukamilisha kazi hiyo nzito.

“ Nimeweza kuwaponyoka, lakini sasa huku ninakoenda ni wapi, nitatokea wapi. Giza la humu ndani linanitia hofu, harufu ya mahali hapa ni mbaya kama nini, sijui huku wanatupaga nini?” Fernanda akawaza huku akitembea polepole akiliacha lile panga boya likizunguka kwa kasi na kutengeneza upepo wenye harufu mbaya ya uvundo wa lile handaki. Fernanda akasonga mpaka alipofika sehemu ambayo akakanyaga kitu mfano wa matope, “ Sijui ni chemba ya maji take?” Fernanda akawaza. Akasonga akizidi kukanyaga majimaji na matope ya maji taka huku harufu mbaya ikishambulia pua yake, giza nene lililomfanya asione hata hatua moja lilizidi kumfunika, wala hapakuwa na tofauti yoyote kama angetembea kwa kufumba macho au akiwa ameyafumbua. Lilikuwa ni giza kuu,

“ Sikuwahi kufikiri kama kuna giza kama hili tangu nimezaliwa” Fernanda akawaza huku akizidi kusonga. Harufu ilizidi kuongezeka lakini hakuwa na chaguo, ilikuwa ni kheri harufu mbaya na giza kama lile kuliko kukamatwa na wale watu aliowaona kama mashetani wa makaburini. Akiwa anatembea mawazo yake yakaanza kuchora taswira katika ubongo wake;



“ Naitwa Stanslaus Mahige, naingia popote, hakuna mlango ambao utafungwa nisiufungue. Hata hivyo sijaja hapa kueleza habari hizo. Kilichonileta ni jambo moja tuu. Tafadhali nambie, Sajenti Warioba Yupo wapi?”

“ Tokea lini Sajenti Warioba anaishi hapa? Au kuna mtu kakuambia Sajenti yupo hapa? Mmeenda kwake hamjamkuta?”
Fernanda alisema.

“ Sikiliza wewe Mwanamke, sijaja hapa kujibishana na wewe, nambie Sajenti yupo wapi?”

“ Sijui Sajenti yupo wapi? Mwenyewe namtafuta, nani kakutuma umtafute Sajenti, na unamtafuta kwa nini?”

“ Hakuna asiyejua kuwa Sajenti ni adui wa nchi, yeye ndiye aliyeiba chipu ya Darubini ya maabara, yeye ndiye kaiba Cadava, yeye ndiye kaiba sampo za uchunguzi, tena akamtorosha Mateka wa ushahidi, sasa kaamua kutoroka. Huyajui mambo haya au upo pamoja naye kwenye uovu wake? Embu niambie Sajenti yupo wapi hiyo ndio salama yako, usiponiambia utajiingiza kwenye matatizo makubwa”
Fernanda ubongo wake ulikumbuka tukio lake la Stanslaus Mahige, kijana huyu ndiye alikuwa wakwanza kumvamia nyumbani kwake akimuamuru amwambia mahali alipo Sajenti Warioba.

“ Itakuwa Stanslaus Mahige alitumwa na hawa watu, lakini watu hawa ni kina nani? Inaonekana ni watu hatari sana, wakatili wenye roho za kishetani, lakini ikawaje Meja Venance Kagoda akawa na ushirika nao, mambo haya yananichanganya sana, lakini naamini majibu yote yatakuwa katika simu niliyonayo niliyoichukua chumbani kwa Meja Venance” Fernanda akawaza wakati akiwa anatembea katika matope yanayonuka giza likiwa limemfunika asiweze kuona anakanyaga nini.

Kitambo kidogo akavuka eneo lenye matope akawa anakanyaga mchanga wa changarawe, “ angalau hapa” akajisemea mwenyewe huku mkononi akiwa bado anabastola yake ambayo aliamini haikuwa na risasi zaidi ya mbili, hata hivyo bado aliiona itamsaidia kwa namna moja ama nyingine. Harufu na eneo lile ikawa imebadilika kutoka katika kuwa harufu mbaya kama ya maji taka na sasa akawa anasikia harufu mbaya ya kemikali kama ya madawa hivi. Akasonga lakini kadiri alivyokuwa akisonga akaanza kuhisi kuzunguzungu, bila shaka ni ile harufu mbaya ya kemikali ndio ilikuwa inamuathiri,

“ Harufu hii inaweza kuwa ni sumu, au pengine inaweza kuwa kemikali inayoathiri mfumo wa ufahamu. Nahisi kichwa kizito” Fernanada akawaza wakati anaongeza mwendo haraka haraka kuondoka eneo lile akitarajia mwendo mfupi ujao atakuwa ameepa harufu ile ambayo tayari imeanza kumdhuru. Akasonga kwa kitambo cha dakika mbili kwa mbali macho yake yakaona mwanga, moyo wake ukalipuka kwa tumaini, akazidisha mwendo lakini muda huu akaanza kuuona mwili wake unazidi kuwa mzito na macho yake yakiona mawenge,

“Fernanda don't die in this place, do your best! Move forward. There is hope, the Light is waiting for you. Come on Fernanda! Jikaze! Usikubali Fernanda” Mawazo ya Fernanda yalimsemesha akiwa anatembea akiyumba yumba kama mlevi kutokana na kizunguzungu, akishika ukuta huku akijikokota kuufuata mwanga aliouona mbele yake. Tayari alikuwa keshazidiwa, hali yake ilikuwa tete, asingejiongopea kuwa hana uwezo tena wakusonga mbele, ingawaje moyo wake ulikuwa radhi lakini mwili ulikuwa dhaifu. Fernanda akasimama akiwa kalegea kama mlenga, akakaa chini, akiwa pale chini, taswira nyingi kama filamu iliyorekodiwa zilipita katika kichwa chake. Akamuona Sajenti akiwa amepanda Farasi wa rangi ya udongo mwenye doa jeupe kichwani, Sajenti alikuwa kava kofia kubwa kama cowboy wa mexico, alikuwa amevaa shati jeupe ambalo hajalifunga vishikizo na pensi, akawa anakuja kwa kasi na farasi akiwa anatabasamu huku shati lake likipepea kwa upepo wa kasi ya Farasi, Fernanda nate akatabasamu. Sajenti akasema ; Don’t die in this place” kisha akaanza kumeguka na yule farasi kama vile kichuguu cha mchwa kinavyomeguka. Fernanda akashtuka, kumbe yalikuwa ni mawazo yaliyovurugwa na zile kemikali.

Fernanda akaanza kutambaa kama mtoto mdogo akiwa amebakiza hatua kadhaa aufikie mwanga hafifu uliokuwa mbele yake. Alipoukaribia ule mwanga akashangaa kukuta reli ya treni iliyokuwa ikitoka upande wake wa kushoto ikielekea kulia na hivyo kutengenaza makutano kama alama ya jumlisha. Eneo hili halikuwa na ile harufu ya kemikali, ingawaje bado Fernanda mwili ulikuwa mzito na kizunguzungu kilimzingua. Fernanda akaona apumzike pale, akakaa kwenye ile reli. Akiwa kapumzika usingizi ukimmendea huku mawazo mengi yakiweka foleni ndefu ubongoni mwake, mara akashtuliwa na sauti ya gari moshi iliyokuwa inatokea upande wa kushoto. Akageuka upande wa kushoto lakini hakuona kitu kutokana na giza lakini bado sauti ya gari moshi inayokuja alikuwa anaisikia. Fernanda muda huu akiwa amepata nguvu kidogo baada ya kupumzika akaona muda wa kuondoka mahali pale umewadia, Fernanda akawaza kuwa ataitumia Treni hiyo inayokuja kujikomboa kutoka mahali pale. Dakika moja iliyofuata Fernanda alikunja uso wake na kuyafinya macho yake baada ya mwanga mkali kutoka kwenye gari moshi uliokuwa ukimmulika usoni akiwa katikati ya reli. Gari moshi lilikuwa umbali wa mita hamsini lakini mwanga wake uliweza kuangaza umbali mrefu, Fernanda akaweka mkono wake usoni kuziba mwanga usimpige machoni huku akijitahidi kuangalia ile Treni kwa umakini. Looh! Macho yake hayakuweza kukubali, akiwa bado kasimama alishtuka kuona mdomo wa bunduki na mlengaji akiwa juu ya kichwa cha Treni vikiwa vinamtazama, upesi akajirusha pembeni huku akifukuzwa na milio ya risasi, Fernanda akaamka upesi na kuanza kukimbia akiiacha Reli, akanyooka moja kwa moja kule mwanga ulipokuwa unatokea, Treni ilipofika mahali alipokuwa amesimama akasikia watu wakishuka huku wengine wakimshambulia kwa risasi, Fernanda alikimbia kwa nguvu zake zote huku mwanga hafifu ukimsaidia. Nyuma yake wale watu hawakutaka kumpa nafasi ya kutoroka, walimuandama kama kivuli cha kifo. Ghafla bin vuu jambo baya likatokea, mbele ya Fernanda kama hatua kumi lilikuwepo shimo refu lakini juu yake kulikuwepo na tundu kubwa linaloingiza mwanga kutokea juu. Nyuma yake wale watu wabaya walikuwa hawapo mbali, walikuwa wakija kwa uhakika wa kumpata Fernanda; Akasimama, akageuka nyuma kuwatazama watu wale, kisha akageuka kulitazama lile shimo ambalo ndani yake mwanga ulikuwa ukiingia, chini kabisa ya lile shimo kwa mbali akaona kuna kamba mbili, wakati bado hata hajatambua rangi ya kamba zile, akahisi maumivu yakipenya katika bega lake la kulia, na punde akaanguka chini ya lile shimo refu lenye giza kwa chini licha ya kuwa kulikuwa na mwanga ukitokea juu yake.

***************************

ITAENDELEA.

Kitabu hiki kinamahusiano makubwa na Kitabu cha " MLIO WA RISASI HARUSINI" ambacho tayari kipo sokoni.

Jipatie Hardcopy kwa bei ya Ofa Tsh 10,000/= Ikatayodumu mpaka tar 14/10/2021

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
ZUDU.jpg


ZIMEBAKI SIKU MBILI TUU

OFA HII ISIKUPITE!

ZISIKUACHE SIKU!

PAta nakala yako ya Kitabu cha MLIO WA RISASI HARUSINI
Bei ya Ofa Tsh 10,000/= badala ya bei yake halisi Tsh 15,000/=

OFA HII ITADUMU MPAKA 14th october 2021

TUMA PESA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel

0758216209
M-PESA
Robert Heriel

Bila shaka utaburudika
 
Riwaya inakosa mvuto. Matukio yanapandiliana sana. Hayatoi nafasi. Tukio moja likiisha inatakiwa kupatikane mpenyo wa jambo lingine siyo kupandiliana.
Mfano Fernanda anatafuta upenyo wa kutoroka lakini hatuuoni maana kuna mtu yuko mita hamsini anamweka mtu kati.
Sasa riwaya ya namna hii inachosha. Haileti uhalisia. Inatakiwa mtunzi atuoneshe Fernanda ametoroka kwenye jengo lile ili kama kuna tukio lingine la kuwekwa mtu kati litokee baadaye baada ya kisa cha kutoka kwenye jengo kimeeleweka.
Niliisoma riwaya ya Mlio wa Risasi Harusini.
Ukweli ni riwaya nzuri lakini matukio yanapandiliana. Hayapumziki kuleta uhalisia.
Watunzi wa kizazi cha leo someni riwaya za zamani muone mtiririko wa matukio.
Yalikuwa yanavutia kuliko ilvyo kwenye hizi riwaya za kileo.
Chief usitake ije kama unavyotaka tulia fuata mtunzi alichokuandalia
 
Back
Top Bottom