Riwaya ya kipelelezi: Wakala wa Siri

Riwaya ya kipelelezi: Wakala wa Siri

WAKALA WA SIRI 18
Mtunzi; Robert Hereil
0693322300

ILIPOISHIA
Sajenti Warioba alimtazama yule Dereva wa Uber kumdadisi kama alikuwa amegundua jambo lolote. Lakini Dereva hakuwa na hili wala lile, alikuwa kashika usukani akiwa kaangalia mbele akiendesha gari lake. Hali hiyo ilimfanya Sajenti aumbe tabasamu dogo usoni mwake. Sajenti aligeuka nyuma kuangalia kama kuna gari iliyokuwa inawafuatilia lakini hakuona hatari yoyote.
“Boss nikushushie Posta ipi?” Dereva aliuliza na kumfanya Sajenti ashtuke na kugeuka mbele upesi kwani alikuwa amegeukia nyuma ya gari kutazama usalama wa safari yake.
“anhaa! Nipeleke mpaka ulipo Mtaa wa Madaraka” Sajenti akaongea huku akiangalia mbele mahali alipokuwa akimuelekeza Dereva wa Uber.

ENDELEA
“Nikushushe wapi Boss?” Dereva wa Uber akauliza baada ya kuingia mtaa wa Madaraka.

“ Nishushe hapo karibu na hiyo shule”

“ Sawa Boss” Dereva akajibu, kisha baada ya nusu dakika akasimamisha gari, Sajenti akashuka; wakaagana.

Baada ya Uber kuondoka, Sajenti akaangaza macho yake huku na huku, mtaa ule haukuwa na msongamano mkubwa wa watu, isipokuwa magari machache yaliyokuwa yakipita, eneo lile kulikuwa na ofisi nyingi na magari kadhaa yaliyokuwa yameegeshwa. Sajenti pasipo kupoteza muda alichukua uelekeo kuifuata barabara ya kivukoni, ndani ya dakika chache alikuwa amesimama lilipo jengo la wizara ya mambo ya nje. Akasimama kwa sekunde kadhaa huku akiangalia nyuma kuona kama kuna mtu aliyekuwa akimfuatilia, hakuona hatari yeyote, mambo yalikuwa shwari, akatazama lango kuu la kuingilia wizara ya mambo ya nje, akaona walinzi walioshikilia silaha, walikuwa walinzi wanne wenye sare kichwani wakiwa wamevaa vikofia vya rangi nyekundu. Sajenti bila ya kupoteza muda akasonga kulifuata lango kuu la kuingilia wizara ya mambo ya nje.

“ Habari yako, unahitaji kuonana na nani humu?”

“ Habari yangu ni nzuri, Samahani nilikuwa nataka kuonana na Dr. Jimmy Nicholas” Sajenti akajibu huku akimtazama Yule mlinzi ambaye uso wake ulikuwa mkavu usio na dalili ya mzaha.

“ Dr. Jimmy Nicholas?” Yule Mlinzi akauliza, macho yake yakijaribu kumtambua mtu huyo aliyetajwa na Sajenti.

“ Yes, Dr. Jimmy Nicholas, haumfahamu?”

“ Mimi simfahamu kwakweli, unauhakika anafanya kazi hapa?” Yule Mlinza akauliza, Sajenti akashtuka kuona Dr. Jimmy hafahamiki pale.

“ Nina uhakika anafanya kazi hapa, yeye ni katibu wizara ya mambo ya nje” Sajenti akajibu.

“ Dr. Kalunde?”

“Ewaah! Huyo huyo, Dr. Kalunde. Mimi napenda kumuita Dr.Jimmy. Kumbe ninyi mnamfahamu kwa jina la Ukoo.” Sajenti akasema huku wote wakicheka.

“sisi tunamfahamu kama Dr. Kalunde Rafiki, je unamiadi naye?”

“Hapana, ila ukimuambia tuu kuwa nataka kuonana naye nafikiri haitakuwa shida” Sajenti akasema huku akijaribu kuumba uso wa ushawishi. Macho yake yaliendelea kuangaza huku na huku kuhakikisha usalama wake haupotei. Alijua fika kuwa bado kuna watu wanamfuatilia usiku na mchana.

“ Sasa ndugu yangu, kama huna miadi naye unafikiri ni rahisi kama unavyoongea hapo? Sisi haturuhusiwi kumruhusu mtu yeyote kuingia humu pasipo kupewa maelekezo na Maboss zetu” Yule mlinzi akasema huku akimtazama Sajenti kwa uso wa kutokukubaliana naye.

“ Ndugu yangu, naomba unisaidie, nahitaji kuonana na Dr. Kalunde, naomba unisadie, kuna jambo la muhimu sana napaswa nizungumze na…” kabla hajamaliza kuongea akakatishwa na Mlinzi mwingine aliyekuwa amefika.

“ Hemed huyu anashida gani, naona mmezungumza kwa kirefu”

“ Anahitaji kuonana na Dr. Kalunde, lakini hana miadi naye, najaribu kumueleza hapa anakuwa mbishi” Mlinzi aitwaye Hemed akasema.

“ Ati ndugu, unamhitaji Dr. Kalunde kwa shida ipi, sema huenda naweza kukusaidia”

Yule mlinzi aliyekuja akamuuliza Sajenti huku akimtazama.

“ Ni kweli namuhitaji Dr. Kalunde ndugu yangu, lakini siwezi eleza shida yangu kwenu” Sajenti akasema.

“ Wewe ni nani kwakwe, na unaitwa nani kutokea wapi?”

“ Mimi ni rafiki yake niliyesoma naye tangu shule ya sekondari, naitwa Mr. Warioba, kwa sasa naishi mkoani Kilimanjaro” Sajenti akasema huku akiwa ameshaanza kukasirishwa na hali ile. Hakutaka tena maswali.

“ Hawa walinzi nao wanamaswali ya kitoto sana, yaani wangejua wanavyoniudhi kwa kweli wasingeendelea kuniuliza, kama sio eneo hili kuwa na ulinzi mkali, hakika ningewafunza adabu” Sajenti akawaza.

“Kwani hupajui kwake mpaka uje huku ofisini ndugu, huku hakuna mambo ya urafiki, huku ni mambo ya kikazi, tulijua umekuja kwa shida za kikazi kumbe wewe unaleta mambo ya urafiki, sijui kusoma wote. Tafadhali naomba uondoke hapa. Mtafute Dr, Kalunde nyumbani kwake au mahali pengine isipokuwa hapa. Sawa?” Yule mlinzi aliyekuja akasema kwa sauti kali ya amri, Sajenti akamuelewa alikuwa akimaanisha.

“ Ndugu zangu, mnaweza wasiliana naye nikiwa hapa hapa, mkamuuliza..” Sajenti akaongea lakini akakatishwa.

“ Ndugu embu ondoka hapa, usijiletee matatizo, kwanza Dr. Kalunde hayupo hapa, wameondoka tangu saa mbili asubuhi, wanakikao na Mhe. Rais…” Akameza fumba la mate kisha akaendelea;

“Ondoka, akirudi tutampa taarifa ulikuja, kisha tutampa namba zako, haya taja mawasiliano yako” Yule mlinzi akasema kisha akatoa simu akiwa tayari kumsikiliza Sajenti.

Baada ya Sajenti kutaja namba zake akaaga pale akaondoka.

“ Sasa muda wote siwangesema tuu kwamba hayupo, yaani kuna watu wanaroho ya korosho, sijui kwa nini watu kama hawa walipewa namba za kuja huku duniani, wanakera sana. Hata hivyo wana bahati, kama sio eneo lile hakika ningewafunza adabu” Sajenti akawaza huku akikatiza mtaa wa pili akiukaribia mtaa wa mirambo. Punde ikapita bajaji akaisimamisha,

“ Habari kijana, nipeleke Mnazi mmoja..” Sajenti akasema.

“ Sawa kiongozi haina shida. Elfu tano tuu”

“ Hatutashindwana, twende tuu” Sajenti akasema na safari ikaanza.

Njiani Sajenti mawazo yalibisha hodi na kuingia katika kichwa chake.

“Hivi aliyeiba Cadaver ni nani? Na aliyechukua zile sampo za uchunguzi ni nani? Tayari chipu ya darubini nimeshaitia mikononi. Hii kwangu inanipa matumaini ya kurejea katika uhuru wangu, nimechoka kukimbia kimbia kama digidigi, uhuru wangu ulikuwa upo matatani kutowehswa na wahuni. Lazima walipie! Lazima…! Watalipia, hawezi kunifanyia hivi. Anyone involved in this will pay for it” Sajenti akawaza bado bajaji ilikuwa ikichanja barabara, kama sio foleni za hapa na pale basi wangekuwa wameshafika mnazi mmoja lakini, jiji la Dar linachangamoto ya foleni, kero ambayo wengi wanailalamikia.

“ Dr, Binamungu! Tayari nimeshamjua msaliti mmoja, huyu anaweza kujua mambo mengi maovu yanayoendelea, yeye ni sehemu ya haya yanayonipata, nikianza naye nafikiri naweza pata mwanga wa kufika kwa wabaya wangu. Wapi anapokaa Dr. Binamungu?” Akawa Sajenti Warioba.

“ Nimekumbuka, lazima nionane na Dr, Beatus, yeye ndiye atanielekeza anapoishi Dr. Binamungu. Nikishampata huyu nitajua uelekeo wa haya. Ule mwili ulioibiwa ulikuwa mwili wa nani, maana niliitwa tuu na kupewa kazi ya kuitafuta chipu, sampo, na mwili ulioibiwa maabara ya boreti, lakini sikuambiwa mwili ule ulikuwa wa nani. Walioiiba ni kina nani na kwa nini wauibe, yaani maswali ni mengi alafu ni magumu kupata majibu yake” mawazo ya sajenti yalikatishwa na sauti ya dereva bajaji.

“ Boss tumeshafika”

ITAENDELEA.....

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
zodo.jpg

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
  • Thanks
Reactions: ADK
siri.jpg


WAKALA WA SIRI 19
Mtunzi: Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA
“ Nimekumbuka, lazima nionane na Dr, Beatus, yeye ndiye atanielekeza anapoishi Dr. Binamungu. Nikishampata huyu nitajua uelekeo wa haya. Ule mwili ulioibiwa ulikuwa mwili wa nani, maana niliitwa tuu na kupewa kazi ya kuitafuta chipu, sampo, na mwili ulioibiwa maabara ya boreti, lakini sikuambiwa mwili ule ulikuwa wa nani. Walioiiba ni kina nani na kwa nini wauibe, yaani maswali ni mengi alafu ni magumu kupata majibu yake” mawazo ya sajenti yalikatishwa na sauti ya dereva bajaji.

“ Boss tumeshafika”

ENDELEA

“ Nipeleke kwenye jengo la SHDC” Sajenti Warioba akasema huku akitazama mbele kulitafuta jengo hilo ambalo anakumbuka lilikuwa mitaa hiyo hiyo.

“Jengo la SHDC liko wapi, mimi silifahamu Boss” Dereva Bajaji akauliza.

“ Nakumbuka lipo mitaa hii, endelea kuendesha nikiendelea kutazama kulitafuta. Juu kabisa limeandikwa kwa herufi kubwa SHDC ” Sajenti akasema huku dereva bajaji akiendesha polepole huku naye akiangaza macho yake huku na huku kusoma majina ya majengo marefu yaliyopo mitaa ile.

“ Lile! Nimeliona Boss” Dereva bajaji akasema. Sajenti naye alipoliona akamwambia ndilo hilohilo, Walipofika akampa Dereva pesa yake, kisha akashuka na dereva bajaji akaondoka.

Sajenti akatembea kidogo kufuata ngazi za jengo lile, kisha akaifuata moja ya nguzo kubwa ya jengo lile akasimama kwa sekunde kusoma nyendo za weatu wa eneo lile, akajiridhisha kuwa hakuna anayemfuatilia, kila mtu alikuwa na mihangaiko yake. Alipojihakikishia kuna usalama akapiga hatua kufuata mlango wa kioo ambapo alipoukaribia ulitawanyika kushoto na kulia kumpisha apite katikati, ilikuwa ni ile milango yenye detector ambayo hufunguka pale mtu anaposimama mbele yake. Milango hii hutumia optical sensors or motion detectors. Sajenti akaingia ndani moja kwa moja na kupanda lifti mpaka ilipoghorofa ya kumi. Akaifuata korido ndefu iliyokuwa mkono wa kushoto, akatembea mpaka alipokuta kibao kilichoandikwa “SHDC” ambacho kilimuelekeza afuate mkono wa kulia, alipokatisha akakutana na mlango wa aluminiamu na kioo ambao juu yake yaliandikwa maneno “welcome SHDC” akasimama mbele ya ule mlango, kwa pembeni mkono wa kulia ambapo hukaaga kitasa cha mlango akaona sehemu ya kuweka dole gumba, akaweka dole gumba lake la mkono wa kulia. Baada ya kuweka kikatokea kioo kidogo kama kioo kilichopo kwenye ATM MASHINE, kisha yakatokea maandishi “please wait!”Sajenti akasimama kusubiri, kitambo kidogo Sajenti akashtushwa na kile kioo baada ya kuandika “You are not registered, you are not recognized, Contact the office” Kisha chini yake ziliandikwa namba za ofisi. Sajenti akapaniki, iweje mashine ile imuambie hajasajiliwa na hatambuliki ilhali yeye ni mwanachama, na analipa kwa wakati ada ya uanachama. Akili ya Sajenti ikapoteza utulivu akaitoa simu mfukoni akaanza kuiandika ile namba ya simu ili awapigie, akiwa karibu kuipiga akakumbuka jambo ambalo likamfanya atabasamu na kusonya papo hapo.

“nimekumbuka, kijanja cha mkono wangu wa kulia kilivalishwa ngozi ya kiganja cha mtu aitwaye Peter Mirambo kule Brazil nilipopelekwa na Fernanda kwa mzee Da silva. Hakika teknoljia inakua, inamaana mkono wangu wa kulia unaalama za vidole vya mtu mwingine aitwaye Peter Mirambo” Sajenti akawaza huku akiweka dole gumba la mkono wa kushoto kwenye ile mashine, Alipoweka akaambiwa asubiri, kisha baada ya muda ujumbe mfupi ukatokea kwenye kioo cha ile mashine, welcome Mr. Jacob Warioba. Kisha mlango ukafunguka akaingia ndani. Macho yake yalipokelewa na vijiofisi vingi vilivyodizainiwa kwa vioo na aluminium na kila kijiofisi kulikuwa na mtu akiwa anachezea kompyuta. Sajenti akasonga moja kwa moja mpaka ilipokijiofisi kilichoandikwa SHDC21. Akamkuta Dada mmoja aliyekuwa makini na kompyuta.

“ Habari yako Dada” Sajenti akasalimia

“ Nzuri sana, karibu”

“Ahsante. Nimekuja kuna kitu nataka kukichukua” Akasema Sajenti.

Yule Dada akampa Sajenti kidude Fulani kisha akamuambia aweke dole gumba lake, Sajenti akataka kuweka dole gumba la mkono wa kulia, lakini ghafla akaacha baada ya kukumbuka kuwa dole gumba lile halina taarifa zake isipokuwa taarifa za Peter Mirambo. Upesi akabadilisha mkono na kuweka dole gumba la mkono wa kushoto, mshtuko aliouonyesha ulimshtua mpaka Yule dada.

“ Mbona umebadilisha mkono? Alafu umeonyesha kushtuka mpaka nimeogopa, kuna shida yoyote kaka?” Yule dada akauliza.

“ Hapana! Hakuna shida yoyote, nilisajilia na dole gumba la mkono wa kushoto, sasa nilipotaka kuweka mkono wa kulia ndio nikakumbuka, ndio maana ukaona nimeshtuka” Sajenti akasema huku akitabasamu.

“ Hahaha! Wewe kaka! Hivi hujui alama za dole gumba za mkono wa kulia na kushoto zipo sawa?” Yule dada akasema macho yake yakimshangaa na kumuona Sajenti kama mtu mshamba asiyejua lolote. Kumbe alikuwa amedanganywa, Sajenti alitumia mbinu ya kujifanya mjinga na mshamba kumdanganyadada Yule.

“Karibu sana Mr. Jacob Warioba”Yule dada akasema baada ya jina la Sajenti wa Warioba kutokeza kwenye Kompyuta.

“ Nifuate” Akasema Yule Dada, kisha sajenti akaongozana na Yule dada kumfuata alipokuwa akielekea. Walitembea wakizipita ofisi zilizokuwa mule kwenye ule ukumbi, mpaka waliposimama mbele ya mlango ambao mara waliposimama sauti kutoka katika spika zilizochomekwa kwenye ule mlango ikasikika “Please specify a code” hapo hapo Yule dada akataja “SHDC216” alipotaja msimbo huo, ikaja mishale miwili kwenye kioo cha mlango, mshale mmoja wa kijani na mwingine mwekundu. Akabonyeza mshale wa kijani, kisha ikasikika sauti kama ile ya mwanzo ikisema “Code SHDC 216 Given 10 minutes” Kisha mlango ukafunguka.

“ Mr. Warioba tumepewa dakika kumi tuu. Nafikiri unafahamu taratibu” Yule Dada akasema, sajenti akaitikia kwa kutumia kichwa.

“ Unaweza kuingia, mimi narudi kuendelea na kazi, kukiwa na shida yoyote utawasiliana na mimi” Yule Dada akasema kisha akamtajia Sajenti namba yake ya simu, akaondoka na kumuacha Sajenti akiwa ameingia ndani katika ukumbi ule uitwao SHDC400.

Mazingira ya SHDC400 hayakuwa na mabadiliko makubwa tangu alipoyaacha Sajenti, kulikuwa na makabati mengi sana ambayo kila moja lilikuwa na visanduku vilivyoandikwa namba Fulani kama msimbo. Juu ya paa zilikuwepo taa nyingi kubwa zilizofanya eneo la ukumbu kuwa na nuru ya kutosha, ubaridi uliotokana na uwepo wa AC ulifanya ukumbi ule uwe na hali nzuri ya hewa. Ukumbi wa SHDC400 ulikuwa kimya sana, Sajenti hakuona mtu yeyote mule ndani, akasonga akiwa katikati ya shelfu ndefu za makabati, akakatisha kulia, akatembea kidogo kama kisha akakata kulia tena, akasonga kwa nusu dakika akakata kushoto. Hapo akatembea kidogo lakini kabla hafika alipokusudia alishtushwa na macho yake yalipomuona Mzee mmoja mwenye upaa katikati ya kichwa lakini pembeni zikiwepo nywele zenye mvi nyeupe na kijivu, kidevuni akiwa na ndevu nyingi, Kilichomshtua Sajenti ni kuwa, hakujua kuwa mule ndani kulikuwa na mtu, hivyo kitendo cha kumuona Yule mzee kilimfanya akose utulivu. Yule mzee hakuwa amemuona Sajenti Warioba, alikuwa akiendelea kubonyeza vitufe vilivyokuwa katika lile kabati.

Sajenti akaachana naye, akasonga mpaka lilipokuwepo kabati lenye shelfu la rangi ya dhahabu, akafika kwenye kisanduku kilichoandikwa JW16. Akabonyeza kitufe Fulani, taa ya kijani ikawaka kisha kioo cha kile kisanduku kikawaka na kumuamuru aweke dole dumba, akaweka. Akaambiwa asubiri wakati ombi lake linashughulikiwa, baada ya dakika moja unusu, yakatoke maandishi “ Welcome Jacob Warioba” “Kuthibitisha kuwa ndiye, weka msimbo wako” Sajenti akaweka msimbo wa siri. Kwenye kioo pakaandika “ Welcome” kisha sanduku likafunguka. Sajenti akatoa ndani ya lile sanduku bahasha ya kaki, kisha akaifungua ile bahasha akaangalia ndani yake, akajiridhisha, akachukua bahasha nyingine, akaitoa kisha akaingiza mkono mfukoni na kuitoa ile chipu alafu akaiweka ndani ya ile bahasha. Akairudisha ndani ya sanduku. Akiwa anaendelea na hayo punde sauti katika lile kabati ikasikika ikisema “Jacob Warioba has two minutes left, hurry up to avoid inconvenience” Sajenti kwa upesi akazikagua zile nyaraka zingine na alipojiridhisha akiwa amebakiwa na dakika moja akarudisha vizuri akiwa kaiweka ile chipu kwenye bahasha.Akafungu sanduku, kisha yakatokea maandishi yakimtaka aweke msimbo mpya wa siri, akaweka, akaamriwa aweke dole gumba akaweka, akaondoka.

Zikiwa zimebaki sekunde akaondoka akiwa amebeba bahasha moja ya kaki ile aliyokuwa ameishika mwanzoni, akasonga mpaka alipofika mahali alipomuona Yule mzee mwenye mvi, hakumuona, mzee alikuwa ameshaondoka. Akaenda mpaka kwenye lile kabati alilokuwa Yule mzee, akakuta kabati lile limeandikwa BL21. Sajenti akatoka, akafika mpaka zilipoofisi ya Yule Dada SHDC21.

“ Umeshakamilisha ulichokuwa unakihitaji?” Yule akauliza akimtazama Sajenti.

“ Bilashaka! Nimekamilisha. Nashukuru sana Dada” Sajenti akasema. Yule Dada akampa karatasi Fulani, Sajenti akaijaza, alipomaliza akamrudishia. Wakaagana, wakati Sajanti anaondoka akakumbuka jambo. Akarudi kwa Yule Dada.

“ Samahani Dada kama nitakuwa msumbufu, umenihudumia vizuri kabis, nimefurahi sana. Sitakuwa na muungwana endapo sitauliza jina lako, tafadhali naomba nikufahamu unaitwa nani?” Sajenti akasema huku uso wake akiweka sura ya urafiki.

“ Naitwa Belinda, mbona nimekuhudumia kawaida, Mr. Jacob” Belinda akasema huku akitabasamu na kufanya uzuri wake uliokuwa umejificha udhihirike.

“ Niite Mr. Warioba, sipendi kutumia Jacob, niite jina hilo nitashukuru sana Belinda” Sajenti akasema kwa utani na kumfanya Belinda azidi kucheka.

“ Hahah! Nimekuelewa Mr. Warioba, nitakuita kama ulivyosema” Belinda akasema akimtazama Sajenti kwa hamu ya mazungumzo yaendelee. Lakini jambo Fulani la kushtusha akaliona Sajenti, alishangaa kuona kusoma jina “Agricola Kihohozi” katika beji aliyokuwa ameivaa Belinda. Macho yake yasimama kwa sekunde katika beji aliyokuwa ameivaa Belinda jambo hilo likampa wasiwasi Belinda na kumfanya ajitazame kifuani, Belinda akashusha pumzi baada ya kugundua alichokuwa akikiangalia Sajentim kisha akasema;

ITAENDELEA
OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
ZUDU.jpg

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
siri.jpg


WAKALA WA SIRI 20
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA
“ Hahah! Nimekuelewa Mr. Warioba, nitakuita kama ulivyosema” Belinda akasema akimtazama Sajenti kwa hamu ya mazungumzo yaendelee. Lakini jambo Fulani la kushtusha akaliona Sajenti, alishangaa kuona kusoma jina “Agricola Kihohozi” katika beji aliyokuwa ameivaa Belinda. Macho yake yasimama kwa sekunde katika beji aliyokuwa ameivaa Belinda jambo hilo likampa wasiwasi Belinda na kumfanya ajitazame kifuani, Belinda akashusha pumzi baada ya kugundua alichokuwa akikiangalia Sajentim kisha akasema;

ENDELEA;

“ Umenishtua sana. Kumbe ni hii beji. Jina langu la ofisini na Agricola kikohozi. Ila jina la ubatizo naitwa Belinda. Nalipenda Belinda na ndilo ninalolitumia kwa marafiki zangu, hata hapa ofisini nalitumia pia. Ulidhani nimekuongopea?” Belinda aliongea akiwa ametabasamu.

“ Hapana, ila sijui kilichonifanya nishtuke ni nini. Huenda nilidhani umenidanganya. Hahah” Sajenti akasema akiwa anacheka. Kisha akaendelea;

“ Nimefurahi kukufahamu Belinda, naomba nikuache, si ulinipa namba zako. Nimezihifadhi, nikifika nyumbani tutawasiliana kwa mengi zaidi” Sajenti akasema kisha akamuuacha Belinda pale ofisini.

Baada ya kuondoka katika jengo la SHDC Ambalo kirefu chake ni Storage and Handling of Documents Collection; ambalo ni shirika lisilo la kiserikali ambalo makao yake makuu yapo uingereza. Ambapo kazi yake ni kuhifadhi na kutunza nyaraka za wazi na za siri za watu binafsi, makampuni, mashirika ya kiserikali, miongoni mwa nyaraka zingine, SHDC huhifadhi nyaraka kwa mfumo wa nakala ngumu na nakala za kieletroniki ambazo zipo kwenye mfumo wa softcopy. Kutokana na kukua kwa teknolojia na uibaji wa nyaraka za watu binafsi, mashirika, na makampuni, shirika hili limejipa kazi ya kuhifadhi nyaraka hizo mahali salama na tangu kuanzishwa kwake mwaka 1940 huko nchini uingereza haijawahi kutokea kuibiwa au kupotea kwa nyaraka zilizowasilishwa katika shirika hili. Hii ndio sababu watu wenye nyadhifa kubwa serikali, wamiliki wa makampuni na mashirika hulitumia shirika hili kuzihifadhi nyaraka zao hasa nyaraka zilizo za siri. Katika shirika hili Sajenti Warioba alihifadhi nyaraka zake na vitu vyake vikiwemo Kadi za siri za benki pamoja na funguo za nyumba ya siri aliyokuwa ameijenga ambayo watu wengi walikuwa hawaijui.

Sajenti alivyotoka aliingia moja kwa moja Benki akiwa na kadi yake aliyoitoa kwenye ile bahasha aliyoichukua kule SHDC. Kadi ile ya Benki ilikuwa imesajiliwa kwa majina mengine ambayo Sajenti alikuwa akiyatumia. Katika kazi za kijasusi ni kawaida kwa jambo hili. Majasusi huwa utambulisho wa majina mbalimbali, na hata katika masuala ya kifedha husajili akaunti zenye majina tofauti tofauti kwa usalama wa baadaye. Sajenti baada kutoa milioni ishirini benki akatoka, na moja kwa moja akaelekea kwenye Yard za kuuzia magari. Tayari aliona usumbufu wa kupanda magari ya kukodisha, lakini pia aliona hatari ya kufahamika kwa urahisi Kupitia kupanda usafiri tofauti tofauti.

Akafika katika Yard moja yenye magari mazuri iliyopo maeneo ya Mnazi mmoja iliyopo pembeni ya barabara iendayo kariakoo.

“ Sasa hapa nitakuwa huru kufanya kazi zangu, haya masuala ya kupanda usafiri wa umma yatanihatarishia usalama wangu” Sajenti akawaza.

“ Niwekeeni tinted kwenye vioo, si mnafanya na huduma hiyo?” Sajenti akawauliza wale wauzaji wa magari baada ya kukamilisha malipo ya ununuzi wa gari.

“ Ngoja tukuwekee Boss, haichukua muda mrefu” Moja wa wauzaji magari akasema. Baaada ya muda kitambo tayari shughuli ya kuweka tinted kwenye vioo ikawa imekamilia,. Sajenti akamalizana nao, kisha akaondoka pale akiwa na gari lake jipya.

“ Fernanda masikini, sijui yupo wapi, miezi kadhaa imepita tangu ni nimkimbie pale hotelini. Sijui atakuwa salama, atakuwa amenitafuta mpaka amechoka, I’m sorry for this Fernanda. Haikuwa lengo langu kukukimbia, sitaki uingie katika shida, hawa watu sio wazuri kabisa. Lakini Fernanda atakuwa wapi” Sajenti alikuwa akiwaza huku akiendesha gari yake akiwa tayari keshafika maeneo ya fire, sasa alikuwa akiitafuta magomeni.

Mawazo yake yakampeleka mpaka kwenye ile meli ya ambagon, siku alipokutana na Fernanda, alikumbuka siku ile akiwa kwenye Casino lililomo ndani ya Meli ya Ambagon. Fernanda akiwa katika mavazi ya kikahaba akamfuata,

“ Fernanda was sweet, cute with the power of love” Sajenti akasema kwa sauti ndogo huku uso wake ukichanua kwa tabasamu. Akakumbuka walivyofika kisiwa cha Montenegro kule Brazil kisha wakaenda kwenye nyumba ya Fernanda iliyopo Juques.

“Lazima nitarudi Copacabana, raundi hii sitaenda kwa kazi bali nitaenda kustarehe na kipenzi change Fernanda. Fukwe za Copacabana na Ipanema ni kama fukwe za peponi kwa uzuri. Sikuwahi kuhisi kuna upepo wenye ladha tamu kama upepo wa fukwe za Copacabana, Fernanda uko wapi mpenzi wangu, nimekumbuka raha ulizonipa kule Copacabana” Sajenti akawaza bado akiwa ndani ya gari. Kumbukumbu akiwa Brazil jijini Rio de jeneiro zilikuwa ziliranda randa katika kichwa chake. Zilikuwa kumbukumbu zilizorejesha furaha yake moyoni, licha ya kuwa zilikuwa zimepita lakini zilikuwa zimeacha alama ubongo isiyofutika. Mawazo ya Sajenti yalikatika baada ya kufika mbele ya geti jeusi, alikuwa ameshafika, akasimamisha gari kisha akachukua ile bahasha ya kaki aliyoichukulia kule SHDC kisha akatoa funguo na kifaa Fulani chenye vitufe viwili. Ilikuwa rimoti ya geti, akabonyeza geti likafunguka, Sajenti akapokelewa na jumba kubwa ambalo mbele yake kulikuwa na majani yaliyoota hovyo hovyo kutokana na kutokutunzwa. Sajenti akaingiza gari kisha akabonyeza rimoti geti likajifunga.

“ Oooh! Nimerejea tena, ni mieiz kadhaa tangu niondoke hapa, bado hapajaharibika sana, majani haya yameota hovyo hovyo kutokana na kutokuwepo mtu wa kuyatunza, Sajenti baada ya kuegesha gari lake akashuka, akaanza kuzunguka kwenye nyumba yake kuikagua. Maua ya bustani yaliota hovyo hovyo, alizunguka upande wa pili lilipo bwawa la kuogelea, hapo akakuka maji yakiwa na majani majani yaliyopeperushwa na upepo, akazunguka kwa nyuma kabisa, moja kwa moja akaliendea bwawa la samaki wa mapambo aliokuwa akiwafuga, alisikitika kuona samaki wote walikuwa wamekufa siku nyingi kutokana na kukosa chakula. Sajenti akachukua fungua na kuingia ndani. Ndani kulikuwa na vumbi licha ya kuwa jumba lilikuwa limefungwa kwa vioo. Harufu ya uvundo kwa mbali ilizichezea pua yake, upesi akaenda kufungua mapazia na madirisha kuruhusu hewa iingie. Akaingia ndani kabisa kulipo na maktaba ya ile nyumba, akachukua kijarida kimoja chenye picha ya mtu aliyeshika ndoo ya maji pamoja na brashi. Akatoa simu akabinya binya kisha akaweka namba sikioni.

“ Hallo! Mr. Zaburi hapa, naomba mje hapa Mbezi Magari Saba kunifanyia usafi, msichelewe. Nashukuru” Sajenti akaongea na simu kisha akakata. Baada ya dakika thelasini, kampuni ya usafi ya TCS Iliwasili ikiwa na vijana wawili na mabinti wawili.Sajneti aliwapa maelekezo kisha akatoka kwenda kula kwani tayari ilikuwa imefika saa sita mchana, njaa ilikuwa imembana kwani tangu jana alikuwa hajatia kitu mdomoni..

ITAENDELEA.

Kitabu hiki kinamahusiano makubwa na Kitabu cha " MLIO WA RISASI HARUSINI" ambacho tayari kipo sokoni.

Jipatie Hardcopy kwa bei ya Ofa Tsh 10,000/= Ikatayodumu mpaka tar 14/10/2021

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
ZUDU.jpg

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
siri.jpg


WAKALA WA SIRI SEASONAL 2.
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA

Ndani kulikuwa na vumbi licha ya kuwa jumba lilikuwa limefungwa kwa vioo. Harufu ya uvundo kwa mbali ilizichezea pua yake, upesi akaenda kufungua mapazia na madirisha kuruhusu hewa iingie. Akaingia ndani kabisa kulipo na maktaba ya ile nyumba, akachukua kijarida kimoja chenye picha ya mtu aliyeshika ndoo ya maji pamoja na brashi. Akatoa simu akabinya binya kisha akaweka namba sikioni.
“ Hallo! Mr. Zaburi hapa, naomba mje hapa Mbezi Magari Saba kunifanyia usafi, msichelewe. Nashukuru” Sajenti akaongea na simu kisha akakata. Baada ya dakika thelasini, kampuni ya usafi ya TCS Iliwasili ikiwa na vijana wawili na mabinti wawili.Sajneti aliwapa maelekezo kisha akatoka kwenda kula kwani tayari ilikuwa imefika saa sita mchana, njaa ilikuwa imembana kwani tangu jana alikuwa hajatia kitu mdomoni..

SEASON 2 >>> EPISODE 01

“Hii simu ya Meja Venance Kagoda lazima iwe na mambo makubwa ya siri, inaweza ikawa msaada mkubwa kwangu. Lakini kwa nini Meja Venance auawe, kama hiyo haitoshi familia yake mpaka sasa haijulikani mahali ilipo, hakuna anayejua wako hai au wamekufa. Waliomuua ni kina nani; Baada ya mwili wake kuchukuliwa kwa ajili ya uchunguzi na kupelekwa katika maabara ya Boreti ukaibiwa, Who did this?” Fernanda akawaza huku akitoka katika nyumba za Meja Venance akiwa ameibeba ile simu janja aliyoikuta sirini, chumbani kwa Meja Venance. Akapanda ukutani kama mjusi, akatoa kichwa akachungulia nje kukagua usalama wa eneo la nje. Hali ilikuwa ni tulivu, giza na mwanga hafifu wa taa za nyumba za eneo lile zilimfanya Fernanda awe macho, hakuyaamini kabisa mazingira yale. Upande wa kulia aliliona gari lake alilokuwa ameliegesha, akatazama kwa kitambo akiwa bado amening’inia juu ya ukuta; akaona hali ni shwari. Akaruka kwa nje. Akasonga kulifuata gari akiwa mkononi kaishika bastola vizuri. Kila alipopiga hatua tano aligeuka huku na huku kuangalia usalama mpaka alipolikaribia gari lake. Akasimama, akaangalia alipotoka kisha akaangalia saa yake ya mkononi iliyomuonyesha ilikuwa saa saba za usiku. Fernanda hakutaka kupoteza muda akabonyeza rimoti ya gari, mlango ukafunguka akatoma ndani. Akaitoa ile simu janja, kisha akajaribu kuiwasha lakini ikagoma kuwaka,

“ Itakuwa haina chaji, nikifika nyumbani, nitaichaji kisha niikague, mbona akili yangu inanituma kuwa ndani ya simu hii kuna mambo mazito ya siri. Nafikiri itakuwa hivyo, maana hata ilipofichwa lazima itakuwa na jambo zito la siri.” Fernanda akajiwazia huku akiirudisha simu mfukoni. Alafu akawasha gari lakini kabla hajaweka gia alishtushwa na kitu kigumu kikigusa kisogo chake, na kabla akili yake haijampa cha kufanya, sauti nzito isiyomzaha ikasema;

“ Tulia hivyo hivyo, usijitingishe wala kufanya jambo lolote, nisije nikapasua bichwa lako” Yule mtu akaongea kisha akameza mate alafu akaendelea;

“Weka mikono yako juu…..”

“ Wewe ni nani, unashida gani na mimi??” Fernanda akamkatisha huku akiweka mikono yake juu.

“ Kaa kimya! Ukithubutu kufungua mdomo wako nitakichangua kichwa chako. Fuata maelekezo” Yule mtu akasema, sauti yake ilikuwa ikitokea nyuma ya kisogo cha Fernanda, ilikuwa sauti iliyomfanya Fernanda achore picha ya mwanaume jeuri mwenye sura ya kikatili, ilikuwa sauti nzito na mbaya. Fernanda akakaa kimya akisubiri maelekezo, kitambo kidogo kilipita pakiwa kimya hali iliyomfanya Fernanda atake kugeuka nyuma ili amuangalie mtu Yule. Alipogeuka bahati haikuwa yake, akakutana na kitu kizito kilichompiga usoni, Fernanda akaanguka na kupoteza Fahamu.

****************************************************************



Taa zilikuwa zikiwaka katika ghorofa ya nane katika jengo hili. Lilikuwa jengo refu la ghorofa zisizopungua kumi na tano. Pamoja na kuwa ilikuwa usiku wa manane lakini ndani ya jengo hili kulikuwa na kikao kizito kilichokuwa kinaendelea. Watu kumi walikuwa wamekaa kwenye meza yenye muundo wa Herufi U “U-Shape Style” Wote walikuwa wamevaa suti maridadi zilizokuwa zimewakaa vyema. Kiongozi wa kikao hiki cha siri alikuwa amekaa amevaa suti ya kijani uso wake ukiwa nyumba ya miwani ya macho.

“ Mipango yetu imesimama, kila mmoja wetu anafahamu sababu ya kusimama kwake, inaweza kuwa ni uzembe wa baadhi yetu humu, kama sivyo, leo hii tungekuwa tumeshafika mbali. Inashangaza kuona mpaka muda huu tumedorora, tupo katika mdororo, tangu kiungo wetu muhimu auawe na hasimu wetu mambo yetu yamesimama kama sio kurudi nyuma, tulifanikiwa kuiba mwili wake katika maabara ile, najaribu kufikiria kama tusingemuwekea IN-BODY GPS iliyotusaidia kutoa taarifa ya mwili wa Meja Venance Kagoda ulipo, tungepata kazi ngumu na yaziada kujua ulipo mwili wa ndugu yetu. Kazi hii aliifanya Adele kwa weledi mkubwa kabisa” Yule mtu akasema kisha akameza funda la mate, akamgeukia mwanadada mmoja aliyevalia suti ya kijibu iliyomkaa vyema.

“ Adele! Nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kazi nzuri uliyoifanya kwa weledi wa hali ya juu. Hakika tunajivunia kuwa na wewe, nafikiri wote tuliiona video iliyoletwa na Dr. Binamungu iliyoonyesha kazi kubwa aliyoifanya Adele, ilikuwa ni kazi nzuri sana. Dr. Binamungu kama mtakumbuka siku ile alituambia kuwa siku waliyokaa kikao kujadili tukio la kuibiwa mwili wa Meja Venance, karibu watu wote waliokuwa kwenye hicho kikao walisema kuwa aliyefanya tukio hili alikuwa mwanaume….” Yule mtu alikatishwa na vicheko vya wanakikao wengine, naye akaungana nao kucheka. Kisha akaendelea.

“These people are so stupid, I can't understand their ignorance is endless or what it is, kumuita Adele ni mwanaume wakati ni mwanamke mrembo kuna maana mbili ambazo ni; mosi, hawana elimu ya ujasusi katika utambuzi wa miondoko na utendaji wa wahusika katika matukio ya uhalifu; pili, walikuwa wamejawa na hofu au kuchanganyikiwa kwa kile kilichotokea” Yule mtu akameza mateka kisha akaendelea;

“ Natoa zawadi ya Milioni hamsini kwa Adele, kisha kila mtu humu atapatiwa milioni ishirini kama sehemu ya kujipongeza kwa kuuokoa mwili wa kiungo wetu, Meja Venance” Yule mtu akasema kisha sauti za makofi yakikijaza chumba kile.

“Naomba tutulia tafadhali, hatuna muda wa kutosha” Yule mtu akasema akijaribu kuwatuliza wanakikao.

“ Nimewaiteni hapa kuwajulisha kuwa kikao chetu kilikuwa na agenda kuu mbili ambayo ya kwanza nimeshawaeleza, kuhusu mdororo unaoendelea katika mpango wetu, lakini jambo la pili ni kueleza kuhusu hali inavyoendelea katika utafutaji wa chipu ambayo kwa taarifa za kiungo wetu anasema chipu hiyo ipo mikononi mwa kijana mmoja aitwaye Sajenti Jacob Warioba…..” Yule Mtu akasema lakini akakatishwa na Adele.

“ Sajenti Warioba?” Adele akabwatuka kwa sauti jambo lililowafanya wanakikao wamtazame kwa mshangao.​

“ Unamfahamu?” Yule mtu akauliza.​

“ Sajenti….! Kama ni yeye basi tuna kazi ya kufanya” Adele akasema wenzake wakimtazama. Kisha akaendelea.​

“ Sajenti ndiye alinifanya nifungwe kwa miaka miwili kabla hamjaja kunitoa, kijana huyu ni hatari, nimeshtuka kusikia jina lake mahali hapa” Adele akasema akiwa amehamanika.

“ Unataka kuniambia ndiye Yule aliyefanya uchunguzi wa kifo cha Ramla na walioharibu harusi ya Ismaiya na Robert?” Yule Mtu akauliza.

“ Sina uhakika kama ndiye, lakini majina yake ni hayohayo”

“ Huyu si ndiye aliyepambana na kundi letu la Ambagon kule Mogadishu, Somalia? Si ndiye huyuhuyu aliyeleta fujo katika meli yetu ya ambagoni na kuua watu wetu? Kama ndiye naapa he must pay, he will regret getting into the crocodile's mouth” Yule mtu akasema huku sauti yake ikiwa imebadilika kwa kiasi kikubwa, ilikuwa sio ile sauti ya mwanzo, aliongea kwa hasira midomo ikitetemeka.

“ Huyu mbwa wakati huu hatanikimbia, alinikatili katika mipango yangu ya kumuua Ismaiya wakati ule, akasababisha nikafungwa na kusota jela nikila maharage na kuishi maisha kama panya buku. Sajenti I swear by the name of the world, I will teach you. Nitakapokukamata nitakuua kifo kibaya ambacho tangu dunia iwepo hakuna aliyeonja uchungu wake” Adele alikuwa akiwaza.

“ Taarifa tulizonazo ni kuwa, Sajenti kwa sasa hana makazi maalumu na haifahamiki anaishi wapi, hiyo haitatuzuia kumtia mikononi mwetu. Tunakila nyenzo zitakazotusaidia kumkamata mtu huyu. Hana uwezo wa kutukimbia, wengi waliofanya kama yeye walijileta wenyewe pasipo kujua” Yule mtu akasema kisha akamtazama Adele;

“ Adele tupo pamoja? Maana naona upo mbali kimawazo”

“ Ndio Mkuu tupo Pamoja” Adele akasema wakati huu akiwa makini kumsikiliza Yule Mtu.

“ Tutamkamata Sajenti kwa sababu kuu mbili; yakwanza ni kuhusu suala la chipu, hili ndilo la muhimu kwa sasa, alafu lapili ni kulipa kisasi cha aliyotufanyia, kwa kweli hatuwezi kumsamehe kwa aliyotufanyia huyu Panya. Niwaombe jambo moja, hakikisheni Sajenti anakamatwa mzima mzima akiwa hai, sitaki aletwe hapa akiwa amekufa, kwani kwa akiwa hai ndio itakuwa nafasi yetu ya muhimu kutimiza mipango yetu” Yule Mtu akiwa anaongea mara simu yake iliyokuwa mezani ikaita, jambo lililowafanya wote waitazame na kimya kidogo kitawale. Yule mtu akaichukua simu yake akapokea na kuiweka sikioni.

“ Hallo! Kweli! Upo wapi! Sawa nakuja sasa hivi” Yule mtu akasema akiongea na mtu wa upande wa pili simuni, kisha simu ikakatika.

“ Samahani nimepata dharura hapa, simu hii imetoka kwa moja ya viungo wetu waliopo maeneo mbalimbali hapa jijini, mambo yanazidi kunyooka, nafikiri niwaache muendelee na kikao mimi nikakutane na kiungo wetu huyu ili mambo haya yasilale. Mr. Gombe utaendelea kuendesha kikao hiki alafu utanipa maazimio” Yule mtu akasema kisha akatoka akiwaacha wenzake wakitamani kujua anaenda wapi.

ITAENDELEA.

Kitabu hiki kinamahusiano makubwa na Kitabu cha " MLIO WA RISASI HARUSINI" ambacho tayari kipo sokoni.

Jipatie Hardcopy kwa bei ya Ofa Tsh 10,000/= Ikatayodumu mpaka tar 14/10/2021

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
Back
Top Bottom