Roho inaniuma sana, mabati niliyoezekea nyumba yangu yamepauka sana

Roho inaniuma sana, mabati niliyoezekea nyumba yangu yamepauka sana

TUSAIDIE KUJUA FAKE NA ORIGINAL TAFADHAL
Zinakuwa zimeandikwa ALAF hapo
Unaiona kwa nyuma na kwa mbele
Halafu zinakuwa na code nyuma ya bati sema sikupiga picha nilivyonunua
Ila kiuhakika zaidi bora ukachukue kiwandani au store kubwa ambayo haiuzi vitu fakeView attachment 2324970
IMG_20220529_114803.jpg
 
Umepigwa. Sio zenyewe.

Nashindwa elewa inakuwaje za jirani ziko vile vile zangu ndo zipauke wakati aina na geji na rangi na kampuni ni hizo hizo na alikonunua namie ndio nilenda chukulia hapo hapo
 
Mkuu bati ambazo hazipauki hazijawahi kuwepo relax usiishii kwa mashindano na kujifananisha kila kitu, iliyopauka ni rangi siyo bati ..

Rangi za bati zako kupauka kusipoteze Furaha ya Nyumba yako. Tusiumie kwa tulivyopoteza na kusahau tulivyobaki navyoo.

Zipp bhana mbona tunaziona kwa majirani kila siku zinaonekana mpya?
 
Piga rangi maisha yaendelee.

Bidhaa huwa zinazalishwa kwa batch. So unaweza kukuta batch moja iko vizuri ila nyingine ikazingua.

So za jirani ni za kampuni Sawa na yako ila ni batch tofauti. Kwa hiyo inawezekana yake iko vizuri ila wewe ulibahatika kununua batch zisizo nzuri.

Hujawahi kuona nyumba moja na bati alinunua za kampuni moja lakini unakuta baadhi zimeshaanza kupauka na zingine bado rangi iko vizuri?

Au unakuta kofia bado zinang'aa lakini bati imepoteza mng'ao wake. Au bati iko poa ila kofia zimepauka!

Kweli kabisa hili ndio limenitokea sana hadi kofia nazo zimepauka
 

Inaniuma sana tena kama nikiangalia hizo bati walizofanya kama uzio sehemu ujenzi unafanyika ni kama zangu walah zinang'a utadhani kila siku wanapaka rangi wakati zinafanana na zangu rangi hiyo hiyo yaani daaa!!!
 
Kuna siku nilinunua Bati- baada yakufika site Fundi alipokuja alinipigia Simu kuwa zile bati sio za ALAF ni fake. Bahati nna Jamaa angu anafanya kazi ALAF nilipompigia akanielekeza namna ya kutambuwa ALAF original na Fake!

Niliporudi Dukani Mmoja ya alieniuzia (walikuwa wawili) akaanza maneno ya shombo. Mimi nikawaambia wanibadilishie zile Bati wanipe Original au wanipe pesa yangu! Vinginevyo Kesi nawausisha ALAF Ili wawasaidie kuwaonyesha Walipozipata hizo fake ALAF mwenzake aliposikia hivyo akanipa tena Bati 50 zingine.

Akalipia usafiri wa kupeleka original Bati site na kusomba zile fake kurudisha dukani. Ni Zaidi ya Mwaka Bati zote zipo na same color.Pole sana ila kama una risiti ya Hizo Bati washirikishe ALAF mwende Dukani mkakomae nao

Sijanunua alaf mkuu mi niliaminishwa nikanunua pale tazara kuna kampuni moja kubwa sana inachuana na alaf
 
Ukiwa na ujenzi kama unaweza kwenda kiwandani alaf nenda, kama huwezi hakikisha huyo wakala anakupa guarantee kuepika kununua bati fake.

Kabisa mkuu najilaumu sana
 
Asikwambie mtu Hamna kitu inauma kama bati inapauka hata bado kuamia hujahamia[emoji38]

Hapa sina hamu hata ya kuhumia na jilijitutumua paa la style style ili nifunike mtaa na bati langu la blue paa limenyanyuka senta ya 400sentimita yaani daaa[emoji24][emoji24][emoji24]
 
Mkuu paka rangi,tena piga PVA chapa kiboko,utanishukuru baadae

Kuna mtu kanishauri hivyo hivyo ila yeye kaniambia ya plascon eti nipake kwa ufagio (softbroom)kama hizi wanzofagia nazo ndani eti ndio rangi itakolea vizuri na akakazia nisutumie mashine eti nikitumia mashine zitajapauka tena baadae
 
Zinakuwa zimeandikwa ALAF hapo
Unaiona kwa nyuma na kwa mbele
Halafu zinakuwa na code nyuma ya bati sema sikupiga picha nilivyonunua
Ila kiuhakika zaidi bora ukachukue kiwandani au store kubwa ambayo haiuzi vitu fakeView attachment 2324970View attachment 2324971

Inawezekana ukweli maana juzi hapa jamaa tangu kaenda nunua hapa nineona maandishi hayo hayo unavyosema nje na ndani!
 
Back
Top Bottom