Roho inaniuma sana, mabati niliyoezekea nyumba yangu yamepauka sana

Roho inaniuma sana, mabati niliyoezekea nyumba yangu yamepauka sana

Sio kila kitu chenye bei kubwa ni kizuri au kila kitu chenye bei ndogo ni hafifu.
Kuna watu wametumia Alaf Original kutoka kiwandani bati zimepauka.
Mnatuchanganya sasa,tununue bati gani sasa
 
Screenshot_2022-08-26-20-31-24-91_965bbf4d18d205f782c6b8409c5773a4.jpg

Screenshot_2022-08-26-20-30-15-33_965bbf4d18d205f782c6b8409c5773a4.jpg



Miaka mitatu kuelekea minne na Bado linawaka. Nilipata wakala wa kueleweka. Ila haya mambo ni kubahatisha tu. Kuna ujanja ujanja mwingi sana.

Hapo mkuu paka rangi tu. Usiingie gharama za kupaua upya.
 
Mtaani kwetu wote waliopaua na bati ya alaf na dragon hakuna iliyopauka, binafsi nimepaua na dragon.

Jambo la msingi nenda kiwandani bati ikatwe unaiona upewe na warranty, usichukue za bando.

Pia mtoa mada alichokosea ni kuchukua rangi ya blue, ikipauka inaonekana sana.
 
Nunua Bati nyeupe za alafu simba dumu zile og kabisa
Paua nyumba yako baada ya miaka mitani paka rangi

Note;
simba dumu og inamaandishi meusi yameandikwa alafu na namba namba ....pia zinakua na nembo ya simba ya kupigwa na Moto.


Feki zinakuwa hazina maandishi meusi ya alafu pia nembo ya simba inakua ya ndala kama Mpira flani hivi.
 
Yaani nimefanikiwa kujenga nyumba tena kubwa ila sijahamia bado vitu vichache nihamie, lakini kinachoniuma kipindi napaua (kupiga bati)niliaminishwa kuwa bati za kampuni fulani (hapa siitaji jina) ni nzuri na nikaonyeshwa nyumba ya jirani yenye hizo bati kuwa hazipauki.

Nilikubali baada ya kukagua na nikajiridhisha kila kitu, nikaenda nunua hizo bati pale Tazara nikapaua nyumba vizuri tu, sasa ni miaka 4 tangu nipaue sijahamia lakini zile bati kwa kweli zinatia kinyaa zimepauka hadi sina hamu ya kuhamia tena huko.

Hapa kinachoniuma zaidi nyumba ya jirani zake rangi iko vile vile na ni yeye aliniagizia alikonunua hadi bei ni hiyo hiyo, na hata jirani na ofisini kuna bati kama hizo hizo zimezungushiwa kama fensi sehemu wanakojenga hazijapauka kila siku naona ni mpya na nashindwa elewa hapa kuna siri gani kwenye hiyo kampuni nyingine zipauke nyingine zisipauke!

Hapa nawaza je! Ninunue bati zingine au ninunue rangi ya bati nikapake upya kwa mkono?

Ushauri wenu naombeni.
mwanzoni makampuni ya kuuza mabati walikuwa makini kupiga rangi, mabati yalikuwa hayapauki. Siku hizi bora ukanunua mabati yasiyo na rangi za viwandani ukapiga rangi wewe mwenyewe.
 
mwanzoni makampuni ya kuuza mabati walikuwa makini kupiga rangi, mabati yalikuwa hayapauki. Siku hizi bora ukanunua mabati yasiyo na rangi za viwandani ukapiga rangi wewe mwenyewe.
Alaf, hua wananunua 'coils' zikiwa colored kabisa toka SA, wao ni kuweka iyo mikunjo na hayo mawimbi ( roll forming )

sishangai izo kampuni zinapaka wenyewe hapahapa, bati baada ya miezi 6 hupauka
 
Alaf, hua wananunua 'coils' zikiwa colored kabisa toka SA, wao ni kuweka iyo mikunjo na hayo mawimbi ( roll forming )

sishangai izo kampuni zinapaka wenyewe hapahapa, bati baada ya miezi 6 hupauka
sidhani kama wananunua ikiwa zimeshapakwa. ingekuwa hivyo, wakisha press bati kuform migogo bati zingechubuka. MImi nilinunua Alaf mwaka 2006 mpaka leo ziko safi. 2015 nikampeleka jamaa yangu akanunua, ni aibu hata kusema ni za alafu. zimepauka vibaya
 
Alaf, hua wananunua 'coils' zikiwa colored kabisa toka SA, wao ni kuweka iyo mikunjo na hayo mawimbi ( roll forming )

sishangai izo kampuni zinapaka wenyewe hapahapa, bati baada ya miezi 6 hupauka
Nao hununua china ila ubora wake ndo tatizo
 
Inaniuma sana tena kama nikiangalia hizo bati walizofanya kama uzio sehemu ujenzi unafanyika ni kama zangu walah zinang'a utadhani kila siku wanapaka rangi wakati zinafanana na zangu rangi hiyo hiyo yaani daaa!!!
Hii kitu hujagundua? Slope ya paa huchangia na kupauka haraka kwa bati, kwa hiyo usitegemee bati iliyosimama ya fensi kupauka haraka.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Ila kuna fundi rangi kaniambia kupaka inatumika fagio laini ndio inakole na akakazia kuwa nikitumia mashine eti zitajapauka tena.au ananipanga hivyo maana mashine hana ili alambe kazi
Ni sahihi kabisa, Tena tumia ule ufagio wa kudekia wenye muundo wa kama tambi za kuweka kwenye vibatari
 
sidhani kama wananunua ikiwa zimeshapakwa. ingekuwa hivyo, wakisha press bati kuform migogo bati zingechubuka. MImi nilinunua Alaf mwaka 2006 mpaka leo ziko safi. 2015 nikampeleka jamaa yangu akanunua, ni aibu hata kusema ni za alafu. zimepauka vibaya
Coils zote huwa zinakuja zikiwa zina rangi kabisa ila kinachotofautisha ni Ile thickness ya coating. Kuna baadhi ya makampuni Yao hata ukichubua kwa mkono tu rangi inatoka.
 
Mkuu bati ambazo hazipauki hazijawahi kuwepo relax usiishii kwa mashindano na kujifananisha kila kitu, iliyopauka ni rangi siyo bati ..

Rangi za bati zako kupauka kusipoteze Furaha ya Nyumba yako. Tusiumie kwa tulivyopoteza na kusahau tulivyobaki navyoo.
AlAF hazipauki mkuu
 
sidhani kama wananunua ikiwa zimeshapakwa. ingekuwa hivyo, wakisha press bati kuform migogo bati zingechubuka. MImi nilinunua Alaf mwaka 2006 mpaka leo ziko safi. 2015 nikampeleka jamaa yangu akanunua, ni aibu hata kusema ni za alafu. zimepauka vibaya

Wao Tanzania humiliki zile mashine za kuweka migongo kwa design mbalimbali lakini yale macoil wanaagiza china au South Africa kilichofanyika zamani macoil yalitengenezwa kwa ufanisi kuanzia nje lakini siku hizi hata wao wanalipua tu na vile tunapiga tu mabati bila kujua hali ya hewa ya eneo husika na ushauri wa kitaalamu hatupati ndio hivo mfano wa coils hizo ni [emoji1541][emoji1541]
IMG_0769.jpg

IMG_0768.jpg
 
Back
Top Bottom