Roma afungiwa miezi sita kujihusisha na sanaa

Lini hebu jazia jazia
BREAKING NEWS: Roma Apigwa Kitanzi cha Miezi Sita

MUUNGWANA BLOG / 1 hour ago



Msanii wa Bongo Fleva, Roma Mkatoliki amefungiwa miezi sita kutojihusisha na Muziki ikiwa ni kutekeleza azma ya Serikali kwa kile kinachodaiwa kukiuka maadili ya jamii za kitanzania kwenye wimbo wake wa "KIBAMIA".

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, amesema kuwa Roma amedharau wito wa serikali ambapo leo aliitwa ili ahojiwe kutokana na wimbo wake huo ikiwa ni hatua ya pili mara baada ya Baraza la Sanaa Nchini Basata kumuita na kumtaka arekebishe baadhi ya sehemu katika wimbo huo.

"Tumempigia simu mara kadhaa hajapokea, tumemtumia meseji anasoma lakini hajibu chochote hivyo hiyo ni dharau na hatuendelei kudili na mtu mmoja wasanii ni wengi ambao wanahitaji msaada kutoka kwetu" alisema Shonza.
 
Mmmh utafika muda kila jiwe litatoa Saut ata sauti za aina ile wanazoitaga weird noise
 
Msanii wa kizazi kipya kwa miondoko ya hip hop amefungiwa kwa miezi 6 na naibu wazur wa habari sanaa na michezo.

Hebu ngoja nijaribu Kuunganisha haya matukio tafadhali ambapo la Kwanza lilikuwa ni la Kutekwa na kuokotwa Ununio mkabala na Mahaba Beach, la pili ni hili la BASATA kupitia Wizara husika ambacho ni chombo cha Serikali kumfungia kwa miezi Sita ( 6 ) na tukio la tatu Kwake sijui litakuwa nini labda kama Members mtanisaidia.
 
Sasa wanasubiri nn kujiunga na maandamabo
 
Ofisi inaendeshwa kwa simu? Huo wito wangempa kwa barua...akija sema hakua na simu ila alikua amejifungia stdio watabisha??
 
Sijaelewa apa Mbona nyimbo zenyewe zakitambo Sana na zmehiti sana
 
hiyo hakunaga ushemaji imehit weeh sasa hivi imepotea ndio wanakumbuka kuifungia....basata bwana
Hii sio point. Kwani hakuna wanaozaliwa! Hakuna throwback? Hakunaga zilipendwa!
 
Wameufungia na Bongo bahati mbaya?!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…