Roma: Boss Ruge amehangaika na sisi kuanzia asubuhi mpaka sasa tupo pamoja naye

Roma: Boss Ruge amehangaika na sisi kuanzia asubuhi mpaka sasa tupo pamoja naye

Yaani mkuu ile utekaji hata mtoto wa std7 anaweza akawazidi akili....
Unakwenda kuwa chukua watu usiowajua??
Unakwenda na Noah yenye siti7, afu mpo watano?? So una siti2 tu tupu.
Unachukua watu wanne, unamchukua na houseboy unawaacha wasanii wengine hapo nje??
Unachukua tv....... What was your mission....
Mission kama ile ya kuteka kituo cha radio na tv mbele ya cctv camera.Inaonekana ni akili ileile na watu ni walewale.Same shit different day.Joyce Wowowo na baba yake watakuwa wanajua.
 
Baada kupatikana kwa msanii Roma na Moni pamoja na producer wao Bin laden nini kimeendelea sasa....... [emoji51][emoji51][emoji51][emoji51]
 
Kesho kuna tukio gani jingine linaloingiliana na la ROMA kuongea ?
 
Nadhani hii nayoo ni movie kama zingine tuu...!!
 
My take,

Roma anaweza akawa amepigwa biti asiseme alikuwa amefichwa wapi, lakini naamini Ruge ndiye mtu sahihi wa kumuhoji hawa madogo walikuwa wapi??

Kama alihangaika nao kuanzia asubuhi ya Jana mpaka usiku ni wazi kuwa anajua aliwahangaikia wapi na kwa Muda gani. Ruge kwenye hili wewe ndo utasema ukweli.

Ombi:
Ruge Kama utafanya lolote kumuokoa yeyote kwenye hili Tope, Muda ndo utakaoamua mustakabali wa biashara yako.
[HASHTAG]#kumbukauvamizi[/HASHTAG]
Ikiwa Roma alikuwa ametekwa alijuaje Ruge alikuwa ana muhangaikia? walikuwa pamoja?
Huu ni ushahidi kuwa ROMA hakutekwa bali ni michezo ya watu hahaha
 
Kila mtu mpenda haki na demokrasia katika nchi yetu anapenda kusikia ni nini kiliwapata kina Roma pamoja wenzake...

- Ni nani aliyewateka?
- Walipelekwa wapi?
- Walifanywa nini?
- Aliyewateka alikuwa na lengo gani?

Sasa sisi kama watanzania tumekuwa tukisisitiza waseme ukweli bila woga hata kama maisha yao yatakuwa hatarini kiasi gani ila tunawataka waseme ukweli, Sasa hoja yangu ni hii, kwa unafiki wa tulio wengi ni nini tutakifanya kama watanzania endapo watatutajia aliyewateka?

Nini tutakifanya endapo kama utekaji huo utakuwa ulifanywa na kiongozi wa serikali/ raia wa kawaida?

Je, tutaendeleza unafiki wakusema tunaishauri serikali/rais achukue hatua wakati alishasema tusimpangie cha kufanya?

Nini tunaenda kufanya kama tukiujua ukweli na muhusika wa huu unyama!?

Tuweke itikadi zetu kando, tujadili kama watanzania. UNAFIKI NI DHAMBI MBELE ZA MUNGU.
 
Back
Top Bottom