Roma Mkatoliki amwibua Mwakyembe, adai hana elimu ya kumshauri yeye mwenye digrii 4. Kama anapenda siasa aanzishe chama cha siasa

Roma Mkatoliki amwibua Mwakyembe, adai hana elimu ya kumshauri yeye mwenye digrii 4. Kama anapenda siasa aanzishe chama cha siasa

Digriii nne amewai kuvumbua nini kipya??

Ama digiriii za kukariri kwenye vitabu?Unaweza ukawa na uwezo mkubwa wa kukariri lakini usiweze kuchanganua mambo!!
Ni haki ya Roma kikatiba kukosoa ile hali avunji sheria.
 
Baada ya Waziri fulani kujitumumua na kujimwambafai mbele ya waandishi wa habari kuwa msanii fulani hawezi kumkosoa kwa kuwa yeye ana degree 4, hizo insults nahisi zina-hold for all na tumedharauliwa wote wenye tuelimu tudogo kwamba eti tulioishia darasa la 7 kamwe hatuwezi kuwaonya na kuwakosoa wenye degree 4.

Wale wote tulioishia la saba tuungane tuone ni jinsi gani tunaweza ku-rise nguvu ya kuweza kuwakosoa wale waliopotoka kwa kuwa wana madrigrii mengi mengi zinazokaribia zile za thermometer.
 
Sasa ni awamu ya wenye madigrii mengi kutamba!

Clip ya Dr Harrison Mwakyembe inatamba sasa hivi akitambia usomi wake.

Dr. Mwakyembe anasema hawezi kushauriwa na mtu asiyesoma, wa darasa la saba.

Na hao wasiosoma ndio wako wengi nchi hii, watu wenye uwezo wa kukuondoa madarakani kwa kura yao isiyosoma.

Kusoma si vibaya , hata ukiwa na madigrii kumi. Swala la kujiuliza ulizipataje?

Ulizilipia kwa hela yako au wazazi wako wa cacao ya Kyela?

Au ni hela ya walipa kodi masikini wa darasa la saba?

Mnatunyonya tuwasomeshe kwa kodi zetu ili mje kututukana sisi walipa kodi walala hoi?

Dr. Mwakyembe omba radhi fasta kabla hujapata kiitikio stahili toka kwa walala hoi.
 
Huyo Kembekembe, sijawahi kumkubali hata siku moja, anajikuta sana hyo dingi..
Nape zilimfaa sana zile ofisi, ila Magu na Bashite wake ndo wametuleta huku
 
Mwambieni hekima, busara na utashi havipimwi na wingi wa degree ulizonazo....

Mwambieni wazee wetu walipambana na wakoloni na hawakuwa na hayo madegree ila walishinda , wao na madegree yao panya road tu wanawatoa jasho.

Mwambieni kipimo cha akili si madegree, itokee siku anyang'anywe madaraka yote, na pesa zote na Mali zote alafu aletwe huku mtaani aone kati ya yeye mwenye madegree na alieshia lasaba nani atalala njaa...

Mwambieni anakula analala, anaenda msalani kwa kodi zetu tusio na degree...


Kwakifupi mwambieni awe na heshima ......Njaa isimfanye awaze kwa .....Mwambieni nimesema


Baba Mtakatifu
 
Kama kweli elimu ni ufunguo wa maisha, aliyeanzisha elimu funguo alitoa wapi? Basi alikuwa na akili iliyomwezesha kuanzisha elimu.
 
Na haka ka phd kangu bibi yangu aliuza sana ng'ombe zake kunilipia ada ya sekondari, sababu hajaenda shule hawezi kusoma wala kuandika na anaongea kilugha. hii phd imenifanya mtu wa kuongea sana kizungu na kiswahili kidogo hadi napata shida kuwasiliana na bibi yangu kwa kilugha, kwani kimepotea sana kichwani
 
Ndio sasa naelewa kwanini mfalme Suleiman hakuomba Mungu amepe utajiri ila aliomba apewe hekima tuuu.... wazee wetu wengi walikuwa wasomi sana ila babu na bibi zetu waliowasomesha wengi wao hawakuwa na elimu kabisa ila walijaliwa hekima na maarifa hivyo hata uwe profesa walikuwa wanakukalisha chini na kukuonya wanapoona huendi sawa katika maisha
 
Back
Top Bottom