Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Si Nasikia Kuna Wahariri Wengine Wako Kwenye Paycheck Ya Mafisadi!? Sasa Ni Kweli Wahariri Wa Bongo Wanaweza Kuungana? Kwa Sababu Pesa Ya Mafisadi Inaweza Kuwanunua Baadhi Yao. Cha Muhimu Ni Kumtatutia Hata Kumsaidia Kulipa Lawyer Mzuri, Ingawa Kwa System Zetu Za Afrika Mtu Aliye Kwenye Power Anaweza Kuwa-influence Majaji. Labda Kama Kungekuwa Na Jury System Na Hao Ma-jury Wenyewe Wasinunuliwe. Ila Namtakia Kila La Heri Jamaa Na Ni Kweli Wahariri Inabidi Ku-stand Up Kwa Mwenzao. Goodluck Wahariri All I Can Do Is Pray 4 U
 
Licha ya wahariri kuwa kwenye paycheque za wanaodhaniwa kuwa mafisadi (Mh. Aziz)lakini magazeti yenyewe yanamilikiwa na hao, kwa hiyo iether wahariri are in or out.
As we all know talk is cheap,
we can talk all we want,
We can click all we want, but truth is truth, and it is thre to be uncovered for those who are IN OF need it.
Kama tunataka kuosha vinywa kwa kuongea tu, its okay as ni anasa mojawapo.
Lakini nina matumaini kuwa kuna mtu anasoma, hizi hoja za humu, anachambua na anazifanyia KAZI.
 
Naomba kuuliza hivi kuna ubaya gani mtu kushtaki kama anaona ameandikwa vibaya? Na kama hakuna ubaya kwa nini wahariri wamvae huyu jamaa? Au waandishi na wenyewe wanataka kuwachagulia walaji wa habari nani aongee na aongee nini. Kama hawamtaki basi hawampi nafasi ya kuongea na akiongea anashambuliwa. Naomba wachangiaji mnisaidie kujibu hayo maswali mawili.
 
Katika toleo lake la wiki hii lililotoka leo, ukurasa wa mbele wa gazeti la RAIA MWEMA wamemuomba radhi Rostam Aziz kwa makala ambayo ilichapishwa katika ukurasa wa 15 wa gazeti hilo la Aprili 9, 2008. Naomba tujadili, je, alikua na haki ya kuombwa radhi? Je, kwanini hiyo radhi itoke ukurasa wa mbele wakati makala ilikua ukurasa wa 15? Kwanini itoke siku ambayo Mwanahalisi wametishiwa kushitakiwa?

Naanza kuchangia kwa kusema wazi kwamba BINAFSI sijafurahishwa kabisa na uamuzi huo wa Raia Mwema, kwani sisi wasomaji hatujashirikishwa kikamilifu katika uamuzi huo ambao unaashiria mambo mengi mabaya ikiwa ni pamoja na woga ama kuingia makubaliano, mambo ambayo WASOMAJI WA RAIA MWEME tunaamini kwamba si MSIMAMO wa Timu nzuri ya RAIA MWEMA ikiongozwa na mkongwe katika fani, Jenerali Ulimwengu.

MAKALA YA MIHANGWA AMBAYO RA AMEDAI KWAMBA AMEKASHIFIWA HII HAPA.

http://www.raiamwema.co.tz/08/04/09/mihangwa.php


 
kaombwa radhi katika aya ipi? hebu tuwekee nimesoma sijaona au nami nimechoka?
 
kaombwa radhi katika aya ipi? hebu tuwekee nimesoma sijaona au nami nimechoka?

Habari iliyomuomba radhi haijawekwa katika mtandao, tumeisoma tulioko Tanzania, kama uko Tanzania nunua Raia Mwema utaona... Ila makala ambayo ilimkera RA mpaka akawatisha Raia Mwema ni hiyo hapo juu, tujadili
 
Mimi sioni ubaya wacha tu wamuombe radhi!
Tumeshasoma na tumejua kilichojiri kwenye sakata la EPA kwenye hiyo makala ya Mihangwa madhambi ya RA.....Anatapatapa tu...
 
Halisi tunaomba uiscan then uirushe...

Pia mbona kuna makala zimemtetea Rostam-http://raiamwema.co.tz/08/04/23/23.php hapa napo vipi?
 
makucha ya vijisenti vimeanza kunyamazisha sasa... tusikate tamaa mwendo uwe huu huu
 
Mtu wa Pwani: Nafikiri aya zilizoleta shida kwa RA kwenye makala ya Raia Mwema ni hizi nilizozi-quote hapa chini. Baada ya kuisome hii makala ndio sasa naelewa kwa nini JK aliyamka kwamba urais wake hauna ubia kumbe tayari alikuwa amebanwa mbavu. Hii ni kubwa kwa sababu, pamoja na kwamba inasomeka vizuri sana na watu wengi wanaweza kukubaliana nayo, unawezaje kuthibitisha kwamba kulikuwa/kuna serikali mbili Tanzania ya JK na ya wafanyabiashara. Kwa hapa nawatetea Rai Mwema kuomba radhi. Hata hivyo kuomba kwao radhi sioni kama ni issue kwa sababu message yenyewe imeshakuwa sent. Sasa ni juu ya JK kuamua kuendelea kuilea hiyo serikali ya pili au aizime.

Labda ni muhimu watu wanaofikiria kugombea urais huko mbele wajifunze kwa yanayompata JK kwamba ukikubali pesa chafu zikuingize madarakani itakuwa ngumu sana kujinyofoa kutoka kwenye huo uchafu baada ya kuingia madarakani. By the way, Halisi, ile ahadi ya JK ya kuleta sheria ya kudhibiti upatikanaji wa hela za kampeni iliishia wapi au anaogopa kwamba itamrudi?

 
Halisi,

Poleni sana. Ndio mapambano hayo na muda wote kutakuwa na kupanda milima na kutelemka.

Muhimu ni kutokukata tamaa na kwa hili kama gazeti walikosea basi ni bora walivyofanya. Muhimu ni kuwa makini na kuhakikisha waandishi hawaandiki majina halisi ya wahusika mpaka pale wanapokuwa na uhakika mkubwa na habari husika.
 
You know, I do put people into two groups as far as decision concernd. A helcopter grp and a plan grp a helcopter does not take time to takeoff but a plan takes time to takeoff, so there people who used to rush to the decision without thinking or reasoning like wise RA (Huu ni ukurupukaji)if he would be in the grp of a plan wala asingefikia uamuzi wa kwenda mahakamani. People who are in a grp of a plan allways they take time to decide and find themselfs in the right way
 
Kwa sasa sina comments zozote naangalia na nitasema muda muafaka. Nataka kuwa kama Mkapa kidogo na baadaye niibuke .Kwa kuweka kijineno kuomba msamaa hakuleti nafuu yeyote kwa ukweli wa mambo ya Rostam na wana CCM wengine .Yeye ataendelea kunyamwa tu .
 
Cha msingi ninanachokiona hapa ni kwamba wote wanaweza kuwa sawa kwa mtizamo wa kisheria kwa vile bado ni tuhuma. Na kwa vile sheria inatafuta ukweli basi mahakama inaweza kuwa ndio kiwanja kizuri cha kwenda kuonyeshana mbivu na mbichi. Labda linalosumbua hapa ni suala la je ni kwa nini wahariri walishupalie. Mimi nalitazama katika jicho la utawala bora na uhuru wa vyombo vya habari... Na kwa vile wenye taaluma hivyo wanafikiri wanaweza kutetea haki ya mwanahalisi na mhariri wake mkuu kwa umoja, basi hatuna budi kukubaliana na hoja yao. Nadhani kwa mtazamo wa umoja wa wenye taaluma fulani ndio huo utasaidia kuleta mapinduzi stahiki na kutafuta kwa anayestahili haki hiyo, kwa vile haki kama hakustahili si haki yako.
Kumbe hapa tunaweza kujifunza jambo moja kwamba masuala yote yanyohusu taaluma fulani mathalan ualimu, uandishi wa habari, uhandis, na kada nyingine za kitaalam, ni vyema yakawa yatatuliwa kwa ushirikiano wa wadau wenyewe. Mie naunga mkono kwa wanahabari kutafuta namna ya kuupata ukweli kwa kutumia ushirika wa taaluma zao. Kwa vile wanazo kanuni za kiuandishi na kiuhariri zinazo waongoza katika shughuli zao, wanaweza kuona waanzie wapi katika kumsaidia mwanahabari mwenzao.
 

I said earlier kwamba jamaa yaani Rostam kakurupuka .Ama walio mpa ushahuri wamemkchoka wanataka akanyage mawaya arushwe ama kuna mtego wame mweka .Kaeni macho mtaona wenyewe soon. Hii kesi italeta weingi .

Juu ya wahariri wana haki kama tunavyi suggest hapa kila mara kwenda mahakamani kudai katiba .Mike alipo kamatwa JF tulikuja juu nakufanya jitihada .Leo hawa wahariri kusema ni sawa mana Kubenea wako naye .Sasa whether wako kweye payroll ama hapana tuanzie pale ambapo watamaliza kukutana tuanze kuona mwelekeo wao .
 
I absolutely agree with you Mwanangurumo for what you just said, but on the other side of the coin it's better to let that big guy RA to exercise his constitutional right... Once the truth will be revealed then we will be able to measure his ability to analyse things before making what we call final decisions in his career and personal life as well. I'll be thankful to see what will happen in the court of law. Money worth nothing but sauti za wanyonge....
 
Raia Mwema, kwa "kumwomba radhi" Rostam Aziz, wamedhihirisha ukweli kwamba wao ni wale wale wa Rai ya Rostam Aziz. Hakuna kipya. Usanii ndani ya usanii! Ndio maana sikulipenda hili gazeti!

Kaeni mkao wa kula, kitu kipya kikali zaidi ya MwanaHALISI kiko jikoni, karibu kitatoka. Utakuwa wimbo mtamu sana... yaani albam itauza kopi zote na chenji hairudi!

./Mwana wa Haki!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…