Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Mchungaji mwongo... risiti imetaja church mzee wangu mwanakijiji!
 
mmhmhhmhmhmh.... hakuna kitu hapa Tanzania... Mtikila si wa-kuaminika kabisa
 
Bubu ataka kusema,

Hoja zako ni dhaifu sana! Maana ni kama hizo fedha zote... zimeenda kwa Rostam... kama huo ndio ushahidi kweli mnaongea upupu mtupu!!!>.. Poleni sana... kama ndio ushahidi wenu!

Wewe ndiye mwenye hoja nzito uliyeridhika kwa kuambiwa fisadi RA kafanya biashara tangu 1852 basi umeamini kwamba kama mtu alifanya biashara tangu 1852 anastahili kuwa tajiri wa kupindukia!!!!, bila hata kujua biashara hiyo ilikuwa ni biashara gani!!!! Kama alikuwa anauza ukwaju je? Eti mnasakama RA kwa sababu ya rangi yake!!! unasahau kwamba kuna wengine wenye rangi tofauti na fisadi RA na vyeo vikubwa kuliko yeye na wao pia wanasakamwa, halafu unajiita kuwa una hoja nzito!!!...LOL! Debe tupu......Jaribu kuchanganua mambo kwa marefu na mapana siyo mtu akisema kitu tu basi unakiamini kama kilivyo.

Inaelekea na wewe ilipata mshiko toka kwa fisadi RA ndiyo maana unamtetea kwa nguvu zako zote, mwambie yale aliyoyazungumza leo pale Kilimanjaro Hotel ni finyu mno hayajamridhisha yeyote, labda wewe mtetezi wa fisadi RA.
 
Mtikila na deni lake... hajasema alitakiwa arudishe lini? Jamaa ni msaniii
 
Mtikila na deni lake... hajasema alitakiwa arudishe lini? Jamaa ni msaniii

Lakini kama ni kukopa, hivi kweli tunakopa kwa wale wasafi tu? Nyerere na kuzilaani World bank na IMF bado alikuwa anaenda kukopa huko.

Pili nakubaliana na argument ya Mtikila kwamba yeye alikopa kwa shida yake, hakukuwa na masharti yoyote ya yeye kumsafisha Rostam. Pia wakati huo Rostam hakuwa kwenye matatizo makubwa ya ufisadi kama ilivyo sasa.

Kikubwa kukopa kwake hakukuwa na masharti ya kumsafisha RA ufisadi.

Kwa mazingira ya TZ, na ugumu wa kupata pesa, hata mtu safi anaweza kujikuta kwenye
hali hii ya Mtikila. Tofauti tu ni pale mtu mwema anapofanya kila jambo kiwazi wakati mwingine angechukua kama rushwa.
 
Rostam ni kweli familia yake imefanya biashara muda mrefu sana, lakini:-

1. Haibadili ukweli kuwa, wakati wa uchaguzi alikuwa akipewa hela za kampeni na Iran, kwa sababu yeye ni Mtanzania mwenye asili ya Iran, na ndiyo maana hata uwaziri aliukwepa kwa sababu wafadhili walimwambia Mkapa wazi kuwa akipewa uwaziri wa Fedha basi hakutakuwa na msada toka kwa wazungu.

2. Nilisema wazi kuwa Rostam anatoa hela Iran, haikupita muda gazeti maarufu huko London likarudia maneno yangu, Rostma na muungwana wakasema watalishitaki lile gazeti, je waliishia wapi?

Sasa mtu kwa aliyefanya biashara toka mwaka 1852, ilikuwaje kwenda Iran kuchukua hela za kmapeni? Ilikuwa ni kwa mtaji gani? Alipewa ngapi?

3. Ni kweli alianza biashara toka mwaka 1852, lakini Richimonduli na Dowans imekuwaje sasa amezihamishia kwa Manji, bila kufuata sheria zetu za Jamhuri za kuhamnisha mali au kampuni? Na kwa nini amezihamisha majuzi baada ya wabunge kuanza kuja juu? Kilichomshinda kwenda kwenye kamati ya Mwakyembe ni nini hasa mpaka sasa anaita waandishi aliowalipa tu na kusema taarabu?

Mbona kampuni zake zingine kama Vodacom hajahamishia kwa Manji? Halafu mbona zamani alikuwa haongei in public sasa hiii nguvu mpya ameipata wapi?
Au ana wasi wasi kuwa ameshikwa pabaya?

The next thing tutamuomba aseme majina ya viongozi wote waliwahi kupewa hela na yeye, hiyo ndiyo itakuwa siku ya kilio cha damu kwa taifa letu, maana ni kuanzia Upinzani mpaka CCM, aliowahi kuwapa hela, wa kwanza kabisa Mzee Ndejembi, alimpa shillingi millioni kumi kwa ajili ya kugombea uenyekiti wa CCM Dodoma na mpaka leo anamdai hajalipa
!

Rostam ni fisadi tu, lakini siku zinafikia ukingoni, maana ukiona wananza kuongea sana wakati zamani walikuwa kimyaa ujue chini kuna moto!
 
Baadhi ya Mahojiano ya Mtikila na Mwanakijiji.(Siyo direct quotation)

Mwanakijiji:Kuna taarifa kuwa umepewa shilingi milioni 3 na Rostam.
Mtikila:kaanza kueleza habari za Ufisadi, Richmond, Dowans, EPA ....

Mwanakijiji: Hayo tunajua tangu siku nyingi, je umepewa hela na Rostam
Mtikila: Ndiyo..kweli..nilikopa ,nilikuwa na shida ,.unajua Rostam rafiki yangu tangu siku nyingi..HIYO RISITI ROSTAM AMEFOJI

Mwanakijiji: Kwa nini uende kumuomba Rostam? huji kuwa umecompromise standard? watu hawatakuamini tena.hukuwaona watu wengine wa kwenda kuwakopa??

Mtikila:Hapana nikipewa napokea ila zisiwe kwa masharti ya kumsafisha, mara anaongelea mambo ya Manji,Milioni 3 nilimwomba aniazime na kuwa nitayarudisha.Kesho nitazungumza
kuwa kwa sababu nimesaini siyo rushwa.


Mwanakijiji:Unaonaje umrudishie fedha zake?

Mtikila:fedha nimemuazima kitambo sana kabla mambo hayajamfika shingoni.Sipawsi kuwa na maadui maana mimi ni mtu wa Rohoni.Mara kaenda kwenye mambo ya ushirikina bungeni.
.......................................................................

Mwanakijiji:TUNASUBIRI KESHO
Mtikila:Mwanakijiji umesahau... umesahaukuna kamati ya kupambana na wanaoporamali za nchi.Hata wakati Balali alipokufa Rostam alienda Marekani, kufanya nini? sijui.

END.

NIMECHOKA .......
 
Mtikila na deni lake... hajasema alitakiwa arudishe lini? Jamaa ni msaniii

Mtikila ameeleweka vya kutosha kabisa na Rostama hamwezi Mtikila hata kwa dawa.

Kwanza ushauri wangu ni kwamba naona RA aachiwe Mtikila kwenye siasa......Na kisheria pia kama utawala ukishindwa...Basi coalition yao nayo ipo...Na hawa watu wananweza kuchukuwa nchi.

Rostama mwenyewe kapewa muda wa kutosha na swahiba wake lakini nawasikitikia sana kwani hawajuwi Mtikila ni mtu mwenye Principle na ama kweli jamaa anaongea kwa makini na kila sentensi yake ni NONDO.

Mtikila kama ni kweli alikataa milioni mia nne basi huyu mtu anaona mbele.

Na pia tunajuwa alikuwa anafanya kazi kwenye mazingira magumu sana yeye kama mpinzani na kama kweli kashfa yake ni kukopa milioni tatu...Basi HUYU BADO NI SHUJAA!

Pia nilimwelewa vizuri sana pale aliposema kuwa urafiki wao haina maana kuwa asiseme mambo yanayomtia uchungu ambayo ni ya maslahi ya Kitaifa. Hapo alisema kuwa misimamo yake imepelekea kukosa marafiki ama kuwapoteza...HUYU NI KIONGOZI.

Tunaomba watanzania wamsikilize pia.

Tunaomba pia na yeye ashirikiane na wazalendo wenzake.

Tunataka pia sheria ya DPP ibadilishwe.

Pia alikumbushia yale ambayo kuna watu wengine humu ndani kama Kasheshe ambao kweli wame amua kuyafungia macho kwasababu zao binafsi.....Ama za kifisadi ama za kiitikadi...Ukweli kwamba kulikuwa na ushaidi wa kutosha kuwapiga pingu hawa watuhumiwa bila hata na haja ya kuunda kamati ya kina Mwema.

Utaratibu kwamba eti mtandao ni mkubwa na inabidi uchunguzi wa kamati uwe makini ni danganya toto ili kutaka kuimaliza issue.

Ushaidi wote wa kaguzi zote ulitosha na bado unatosha kuwafikisha mahakamani.

Kama alivyosema mchungaji Mtikila ni kuwa Rostam alifanya vibaya pale alipotoa Hotuba ya kujisafisha sambamba na utowaji wake wa sadaka.

Na ni kweli kuwa sasa hakuwa na mahali pengine pa kuendeleza vijembe vyake vya kisiasa na mbinu zake za kujisafisha zaidi ya kanisani kwani Bungeni ni mbaya na kesi inataka ifunguliwe so the noose is obviously tightening.

Ni wazi kuwa RA alikuwa na long term plans na ndio maana bila ya aibu anathubutu kutaja milioni tatu alizomkopa Mtikila.

Je kweli hata kama alimpa bure hizo milioni tatu...Hiyo je ndiyo pesa ya kumfanya Mtikila anyamaze?

Mtikila kweli angeamuwa kuwa kama kina Marando na Lamwai angeshindwa?

Na kwa maana hiyo basi...Mtikila anaona mbele na ni mtu wa Mungu pia.

Tunamuomba asigeuke wenzake tena...Aelewe pia kuwa TOGETHER WE CAN.
 
Baadhi ya Mahojiano ya Mtikila na Mwanakijiji.(Siyo direct quotation)

Mwanakijiji:Kuna taarifa kuwa umepewa shilingi milioni 3 na Rostam.
Mtikila:kaanza kueleza habari za Ufisadi, Richmond, Dowans, EPA ....

Mwanakijiji: Hayo tunajua tangu siku nyingi, je umepewa hela na Rostam
Mtikila: Ndiyo..kweli..nilikopa ,nilikuwa na shida ,.unajua Rostam rafiki yangu tangu siku nyingi..HIYO RISITI ROSTAM AMEFOJI

Mwanakijiji: Kwa nini uende kumuomba Rostam? huji kuwa umecompromise standard? watu hawatakuamini tena.hukuwaona watu wengine wa kwenda kuwakopa??

Mtikila:Hapana nikipewa napokea ila zisiwe kwa masharti ya kumsafisha, mara anaongelea mambo ya Manji,Milioni 3 nilimwomba aniazime na kuwa nitayarudisha.Kesho nitazungumza
kuwa kwa sababu nimesaini siyo rushwa.

Mwanakijiji:Unaonaje umrudishie fedha zake?

Mtikila:fedha nimemuazima kitambo sana kabla mambo hayajamfika shingoni.Sipawsi kuwa na maadui maana mimi ni mtu wa Rohoni.Mara kaenda kwenye mambo ya ushirikina bungeni.
.......................................................................

Mwanakijiji:TUNASUBIRI KESHO
Mtikila:Mwanakijiji umesahau... umesahaukuna kamati ya kupambana na wanaoporamali za nchi.Hata wakati Balali alipokufa Rostam alienda Marekani, kufanya nini? sijui.

END.

NIMECHOKA .......

Rostam ndiyo amechemsha!

Madai yake kuwa mbona alikuwa akitoa pesa na hazikurudishwa hayana msingi kwani hakuna aliyekuwa akijuwa kuhusu RICHMOND,DOWANS NA EPA wakati akitowa pesa hizo na sasa watu wana ushaidi kuhusiana na ufisadi wake wazi wazi na hakuna atakayekubali tena pesa zake!

Waulize wale waliokubali pesa zake kwa mgongo wa EPA watakwambia joto!

Kama Rostama mwenyewe aliweza kuwa Rafiki wa Kikwete na bado ni rafiki wa Kikwete...Je atashindwa kuwa rafiki wa nani kama akitaka?

Hivyo basi Mtikila kukopa Milioni tatu si UFISADI HATA KIDOGO!

Na kwahiyo basi...Kama alitegemea milioni tatu zake zitamfanya Mtikila afunge mdomo basi amekosea.

Kwani alikataa kufanya hivyo kwa milioni mia nne za Manji.

Kwani kama RA amweka JK mfukoni basi si kila mtu.

Kumbe kwa style aliyomtega JK ndiyo style hiyo hiyo anayotaka kuitumia sema tofauti alimpa JK more na kumtega kimafia zaidi ya mkopo wa milioni tatu alioenda kubadilisha hata saini za Mtikila.

Hivi nyie watu mkisikiliza mahojiano mnasikiliza vipi?
 
Mtikila na deni lake... hajasema alitakiwa arudishe lini? Jamaa ni msaniii

Na wewe mwenzetu mpaka sasa hivi umechukua mshiko kiasi gani katika juhudi zako za kumsafisha "mtu ambaye anaponzwa na rangi yake katika tuhuma dhidi ya ufisadi" na lini utaulipa mshiko huo?
 
Swali kwa fisadi Rostam je, ulimpa JK kiasi gani ili zimsaidie katika uchaguzi wa 2005 hasa katika kupata support kutoka wajumbe wa CCM ili aibuke kidedea kama mgombea wa CCM? Pesa hizo zilitoka mifukoni kwako, nchi za nje au kutoka kwa Watanzania wengine ndani na nje ya nchi? Unakumbuka kila mjumbe mlimnunua kwa kiasi gani ili ahamie kwenye kambi yenu ili amsupport JK? Unazo risiti za malipo kwa wajumbe hao maana inaelekea wewe ni mtunzaji mzuri wa risiti? Inasemekana wajumbe walikuwa wanalipwa kwa dollar au pound je hizo pesa mlizinunua toka duka lipi la kuuzia foreign currency? Maswali yanazidi kuongezeka
 
Just as i said here, this guy is a thug and he will choose the few waandishi he likes. So do it as waandishi wa ulaya, flock at the hotel, akishuka tu garini kabla hata ya kwenda ndani mbaneni maswali na mhakikishe kama hajibu basi mnaingia naye. Kama atalala hotelini basi mkae mlangoni wa chumbani kwake au mwa hilo chumba cha press!

Yale maswali niliyoyatoa hapa muulizeni huyo fisadi.

Asha

he is too big for them sidhani kama kuna mwandishi atakaekuwa jasiri ktk kumbana na maswali
 
Pamoja na kuliita Bunge "kijiwe", Rostam aliishatamka kuwa Bunge ni sawa na "Ze Comedy". Tatizo la huyu jamaa ni kuwa hakai Bungeni, yuko busy kutoa statements kwenye vyombo vya habari anavyomiliki kama vile RAI (kifupi cha Rostam Aziz wa Iran). It is disgusting kuwa Wasukuma wa Igunga wamempa hata "uchifu"! Ama kweli pesa inatesa!

bwana mtindi nimekuvulia kofia kwa jinsi ilivyotoa kirefu cha rai
 
Wanamaombi kutinga bungeni wiki ijayo

2008-07-13 22:26:42
Na Simon Mhina

Kamati ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo nchini, imemuandikia barua Spika wa Bunge, Bw. Samwel Sitta, ikimuomba awaruhusu waende Dodoma kulizunguka Bunge kwa ajili ya maombi na kusisitiza kwamba hawaamini taarifa iliyotolewa na Polisi kwamba unga uliopatikana ndani ya jengo hilo haukuwa na uchawi.

Kadhalika, Kamati hiyo imewashauri mawaziri na wabunge wenye hirizi kuzisalimisha kwao kabla ya kuanza maombi kwani wanaweza kuumbuka.

Pia Kamati hiyo imesema hatua ya Naibu Spika kufunga mjadala kuhusu `unga wa uchawi` haiwakatishi tamaa kufanya maombi hayo.

Kamati hiyo imesema taarifa ya polisi imewachanganya na sio sahihi kwa sababu dola haiamini mambo ya uchawi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamti hiyo, Askofu Isack Kalenge alisema uchunguzi huo wa Polisi, Mkemia Mkuu, Bunge na Usalama wa Taifa ni batili kwa kuwa vyombo hivyo ambavyo viko chini ya serikali, havina uwezo wa kutambua uchawi.

Askofu Kalenge, ambaye ni kiongozi wa Kanisa la Pentekoste International, alisema wanaamini kuwa bado uchawi upo bungeni na wabunge wengi wanateswa na nguvu hizo za giza.

``Uchawi ni jambo la kiroho, haliwezi kupimwa kwa kamera wala uchunguzi wa Mkemia Mkuu, tunaamini tatizo la uchawi bungeni halijapatiwa ufumbuzi, tunakwenda Dodoma kulimaliza tatizo hilo ili lisitokee tena,``alisema.

Akizungumza katika mkutano huo, Mchungaji Wilbert Ngowi alisema kamati hiyo haiwezi kufumbia macho taarifa hizo, kwa vile zimeliaibisha Taifa.

``Umefika wakati sasa kanisa liseme yale ambayo lilikuwa linayafumbia macho na lifanye mambo ambayo yalikuwa hayafanyiki, japokuwa hatua hii inaweza kutafsiriwa kwamba tunachanganya dini na siasa, lakini si vibaya.

Kuanzia sasa tumeamua kuchanganya dini na siasa kwa sababu maandiko matakatifu yanasema kufanya hivyo sio dhambi,``alisema.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mchungaji Christopher Mtikila alisema iwapo watapata ushirikiano wa Spika wataenda bungeni wiki ijayo.

Akifafanua, kiongozi huyo alisema wamemuomba Spika awape kibali cha kuingia bungeni kuwaombea wabunge na `kuharibu` nguvu za giza zilizojaa humo.

Mchungaji Mtikila alisema kabla hawajatia mguu Dodoma, wanawataka Wabunge, mawaziri na yoyote ambaye anatembea na hirizi aisalimishe kabla hawajaanza maombi.

``Ni matarajio ya Kamati kwamba wabunge wazalendo, hususan wale ambao hawatembei na hirizi vibindoni, watafurahia kazi hii njema ya watumishi wa Mungu yenye lengo la kuwaponya,``alisema.

Kiongozi huyo alisema iwapo watakataliwa kufanya mambo hayo, watalizunguka jengo la Bunge hilo na kurusha `makombora ya sala` na kuahidi kwamba hakuna mwanga wala hirizi itakayosalimika.

Aliahidi kuwa wabunge na mawaziri, ambao ni wapenda uchawi, wataumbuka vibaya kutokana na sala hizo.

Alisema tayari waumini mbalimbali wameshaanza kufunga kwa ajili ya kujiandaa na sala hiyo.

Alisema hawatarajii upinzani kutoka kwa Bw. Sitta kwa sababu hivi karibuni Spika huyo alinukuliwa akiwataka viongozi wa dini, kuliombea Bunge kutokana na kuwa katika wakati mgumu.

``Sisi tumeamua kwenda kuliombea Bunge kama alivyosema, ila sisi tutaenda na mamlaka makubwa, ambayo yatasambaratisha kila roho chafu.

Sisi wenye macho ya kiroho tumejua kwamba pale ndani pametundikwa kila aina ya uchawi, lakini hakuna hata mmoja ambao utasalimika,``alisema.

Akizungumza na Nipashe jana, Spika wa Bunge, Bw. Samweli Sitta, alisema bado hajapokea barua hiyo.

Hata hivyo, Spika alikataa kuzungumza iwapo atawaruhusu kutekeleza azama yao hiyo mara atakapopata barua yao.

``Hilo unalouliza ni jambo jipya, lakini siwezi kulisemea kwa vile sijapata barua yenyewe. Ni vema ukaandika zaidi maoni ya hiyo kamati,`` alisema.
 
Rostam ni kweli familia yake imefanya biashara muda mrefu sana, lakini:-

1. Haibadili ukweli kuwa, wakati wa uchaguzi alikuwa akipewa hela za kampeni na Iran, kwa sababu yeye ni Mtanzania mwenye asili ya Iran, na ndiyo maana hata uwaziri aliukwepa kwa sababu wafadhili walimwambia Mkapa wazi kuwa akipewa uwaziri wa Fedha basi hakutakuwa na msada toka kwa wazungu.

2. Nilisema wazi kuwa Rostam anatoa hela Iran, haikupita muda gazeti maarufu huko London likarudia maneno yangu, Rostma na muungwana wakasema watalishitaki lile gazeti, je waliishia wapi?

Sasa mtu kwa aliyefanya biashara toka mwaka 1852, ilikuwaje kwenda Iran kuchukua hela za kmapeni? Ilikuwa ni kwa mtaji gani? Alipewa ngapi?

3. Ni kweli alianza biashara toka mwaka 1852, lakini Richimonduli na Dowans imekuwaje sasa amezihamishia kwa Manji, bila kufuata sheria zetu za Jamhuri za kuhamnisha mali au kampuni? Na kwa nini amezihamisha majuzi baada ya wabunge kuanza kuja juu? Kilichomshinda kwenda kwenye kamati ya Mwakyembe ni nini hasa mpaka sasa anaita waandishi aliowalipa tu na kusema taarabu?

Mbona kampuni zake zingine kama Vodacom hajahamishia kwa Manji? Halafu mbona zamani alikuwa haongei in public sasa hiii nguvu mpya ameipata wapi?
Au ana wasi wasi kuwa ameshikwa pabaya?

The next thing tutamuomba aseme majina ya viongozi wote waliwahi kupewa hela na yeye, hiyo ndiyo itakuwa siku ya kilio cha damu kwa taifa letu, maana ni kuanzia Upinzani mpaka CCM, aliowahi kuwapa hela, wa kwanza kabisa Mzee Ndejembi, alimpa shillingi millioni kumi kwa ajili ya kugombea uenyekiti wa CCM Dodoma na mpaka leo anamdai hajalipa!

Rostam ni fisadi tu, lakini siku zinafikia ukingoni, maana ukiona wananza kuongea sana wakati zamani walikuwa kimyaa ujue chini kuna moto!

FMES...Kwenye highlights....

Kama umegunduwa...Wanataka wadai kuwa Vita ya Ufisadi ni vita kati ya MENGI NA MANJI...

Wewe hujui na THINK BIG Alikuwa akitoa misisitizo kuwa vita ya wafanyabiashara isiingiliwe na Rais...

Kwahiyo unaweza kuona kuwa huo ndio mpango wao na kina jk kuwa hawawezi kuingilia ugomvi kati ya Manji na Mengi.

Kuahamishiwa kwa makampuni ya Dowans na Richmond....Pamoja Na pesa na makampuni hayo feki anapewa Manji kwani yeye ndiye mwenye kusemekana kuwa ana mdhibiti Mengi.

Na hapo utakumbuka kuwa ADUI NAMBA MOJA WA MKAPA NA MAFISADI WENGINE NI MENGI PAMOJA NA WAZALENDO WENGINE!

Magazeti yake yamepambana kisawasawa na huyu mtu ni Mzalendo na kweli hata yeye amejitolea.

Hivyo sasa ni wakati wa kuondoa tofauti zetu zote na kusimamia maslahi ya BongTz.

Kuwa BongoTz NI YA WOTE.
 
Back
Top Bottom