Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Jamani kumwachia huyu mwendawazimu kupigana hii vita wote tutaonekana wendawazimu tuu na mafisadi watashinda,kila akifungua mdomo ndio unagundua tunadeal na mwehu pale!
 
Aidha kwavile hata watoto wadogo mitaani wanalia naye nchi nzima kwamba ndiye fisadi anayeimaliza nchi yao, basi hata yeye atangulie mahakamani kama alivyoshitaki MwanaHALISI, kiyama kitamfuata tu. Saa ya ukombozi ni sasa!

Mbona wewe Mtikila umewashitaki mwanahalisi mahakamani tena ukapewa pesa za kufungulia kesi na Rostam ?

Unafiki wako utakumaliza mwaka huu, Mungu yupo upande wa haki hivyo jiandae na wewe kuitwa na kuzomewa kuwa ni fisadi tuu.
 
Mtikila,kuna kazi kubwa sana mbele yako ,zile nyingine uzirudishe pia na haswa zile ulikuwa unapewa ili kuhakikisha kuwa Gazeti la HOJA linaandika yatawekwa hapa hadharani.
 
Kuna point fulani na ujumbe nimeupata toka kwenye huu ujumbe, ila Mtikila ajaribu kutumia lugha nzuri, mataahira, sidhani kama ni sahihi hasa ukizingatia yeye ni mtumishi wa Mungu (japo sina uhakika), pili ameshapoteza imani kwa wananchi, na tena anazidi kutudhihirishia kuwa na yeye ni ama mmoja wao au alikuwa na lengo la kuwa pamoja nao ila mambo yamegeuka. Kwanini haya yote yaanze kuonekana leo hii, baada ya Sakarir kumuumbua?
Mtikila be honest, siasa imekushinda sasa, kilichobaki nondo hizo wape wengine waendeleze libeneke.
 
Mkuu ngwangwa karibu sana jamvini, hiyo hotuba inamakubwa, madogo yanauafadhali.
Hivi Mtikila amewahi kufanya kazi gani vile? usalama wa taifa au siyo?
 
Mtikila karusha mawe hapa. Sijui amekaa akaandika halafu akasoma? Huyu RA kweli ni rafiki yake maana naona anamjua vizuri. Sasa Mtikila tutafurahi kama utampeleka mahakamani kwa maswala uliomtuhumu.

Uraia wake nafikiri unaweza kuwa sababu ya kwanza pamoja na ufisadi. Tanzania mara nyingi wazawa wamelala usingizi, watu wengi wanaofanya mambo ya ajabu unakuta si watanzania halisi. Kuna haja ya kufuatilia madai ya mtikila kuhusu uraia halisi wa RA.
 
Mtikila anamwaga point nyingi sana hapa nafikiri Rostamu kama alifikiri kusema milioni tatu alikuwa amemaliza sasa inawezekana akawa amewasha moto ambao hataweza kuuzima.

Hawa watu inawezekana si raia wa tanzania nafikiri tufuatilie RA amesoma wapi? na hao ndugu zake wamesoma wapi anaweza kupatikana kirahisi sana.
 
Mtikila anamwaga point nyingi sana hapa nafikiri Rostamu kama alifikiri kusema milioni tatu alikuwa amemaliza sasa inawezekana akawa amewasha moto ambao hataweza kuuzima.

Hawa watu inawezekana si raia wa tanzania nafikiri tufuatilie RA amesoma wapi? na hao ndugu zake wamesoma wapi anaweza kupatikana kirahisi sana.

Je, serikali ya JK ina interest ya kutaka kufuatilia hayo? Documents zote ambazo zinaweza kumfunga RA ziko mikononi mwa serikali na wao sidhani kama wana nia ya kuchunguza hayo yote kwa kuwa ni mtu wao.

Hilo swala la uraia lina utata mkubwa sana na linahitaji umakini mkubwa kwenye kulifuatilia. Ila serikali ya Bongo kwa double standard siwawezi, ukienda kinyume nao ndiyo utawaona wanavyokuja kazi na madai ya uraia lakini kama uko nao swala la uraia halipo. Muulize Jenerali Twaha Ulimwengu na Marehemu Nabwa.
 
Adui wa Adui yako ni RAFIKI YAKO. Bila kujali kama Mtikila anaTUMBUKIAMO shimoni mwa UFISADI, maadamu anampatia RA habari zake, sisi kwetu poa. Acha wenyewe kwa wenyewe WAMALIZANE. Nasubiri Kikwete, Lowassa na RA wakianza kuzipiga hapo PATANOGA maana nafkiri Kikwete itabidi atumie Mashushu wake na UJESHI wake aanze kutembeza UIBILISI ili kulinda mfuko wake maana hawa akina Mama ndogo wako wengi na wao Vipodapoda na vimanukato wanavihitaji kwa wingi. Heee, MASIKIO yanawasha.
 
hivi kwanini Rostam alisema suala la watu wasioheshimu ndoa zao akijua mengi ya JK na ushemeji wao?
 
hivi kwanini Rostam alisema suala la watu wasioheshimu ndoa zao akijua mengi ya JK na ushemeji wao?

Mzee Mwanakijiji,

Samahani hebu fafanua kidogo hapa, una maana Rostam na JK mmoja wao anaenda na dad wa mwenzake? Ni JK au yeye Rostam?

Asante kwa ufafanuzi?

Njimba
 
Ujumbe mzuri. Naona umeingia kwa kasi sana humu kumtetea Mtikila. Kama unajua waliomtuma waambia nawaambie wamemfanya mwenzao ang'ate mkono uliokuwa ukimlisha lakini pia amejianika vile alivyo! mtupu kabisa. Mpe shukrani kwa kujifunga mabomu na kujilipua. Amesaidia kumshughulikia FISADI Rostam Aziz ila na yeye amekufa. Mwenzie bado anatapa tapa ila na yeye lazima amaliziwe. Mtikila is not a pastor, he is an impositor. Hoja zake kwenye huo waraka zina maana lakini yeye mwenyewe haya maana kabisa. Na hoja zake za ufisadi zina maana, lakini hoja zake za ubaguzi hazina maana kabisa! Tell him, shame on him!

Asha

Samahani sana wajumbe kwenye mjadala huu tunaokwenda kuujadili. Kuna kipindi kingi huwa najaribu kufuatilia maisha ya mafisadi na kukuta kwamba wale wanaoiba na kujenga ama makanisa au misikiti huwa wanatetewa na watu wa kwao. Sijui hili limekaaje.

Mimi nimefurahishwa sana na mwito wa kanisa la Lutheran la kumakana Rostam Aziz. Kwa kuwa haikuwa haki yake kulitumia jukwaa la dini kulelezea maswala yake ya kisiasa. Kama ilikuwa ni kuchangia tu, angechangia na akazungumza machache yanayomhusu yeye na imani na si yanayomhusu na yale ya bungeni ambayo alizuiliwa kuyatoa huko kwenye mjengo. Chonde chonde kama aliwajengea msikitiki isiwe sababu ya kumtetea. Huyo hatufai kabisa Tanzania.
 
Wezi hawa wanaipora nchi hii bila huruma, na ndio wanaowaambia watawala wa CCM cha kufanya ili wakombe mapesa yetu B.O.T na Hazina, na kutumia matrilioni yetu kuwatia viongozi wetu ndani ya mifuko ya makoti yao, ambamo wanalishwa masazo yao na kuchomoza vichwa kuchungulia nje kama vindege kuwasanifu wananchi, na kurudi mifukoni mwao wakidhani wanakula kumbe wanaliwa wao na Nchi yao! Hatutaki Rais wetu wala Wabunge wetu wawe vindege ndani ya mifuko ya makoti ya “Rostam” Aziz na Yusuf Manji!
[/B]

Mtikila kweli ni political entertainer namvulia kofia. Pamoja na yote ya kuvuta mshiko kwa Sakarir bado jamaa mi namkubali hasa pale ninapokuwa nahitaji kucheka du!!! jamaa sijui anatoa wapi maneno haya yaani hapa sina mbavu
 
Udhaifu wa Mtikila hauninyimi kuchukia ufisadi wa RA.
Matusi ya Mtikila hayanifanyi nisamehe uonevu ambao uafrika wangu umefanyiwa na waarabu RA akiwa mmoja wao.

Acheni tu mi ntalia bure!!!!!!!!!!!!!
 
Ile kauli ya SINCLAIR KUWA JK NDIYE MWENYE KAULI YA MWISHO INAJIDHIRISHA HAPO CHINI.

KWANI LABDA ALIYEMPA RIPOTI YA MADINI ALIMWAMBIA KUWA NI KWELI UAMUZI WA JK NI WA MWISHO.

NA KUTOKANA NA UKWELI KWAMBA KAMA MAHAKAMA KUU ISIPOTOWA UAMUZI WA KUHUSIANA NA KESI HIYO YA KINA MTIKILA...Basi ni kweli ile kauli ya SINCLAIR KWAMBA UAMUZI WAO YEYE NA JK NI WA MWISHO ITATIMIA!

SO NI MUHIMU KWAUNGA MKONO HAO PILCOM....

Kwa vile Rais Kikwete anahusika katika uporaji huu ambao ulimnufaisha hata katika hila za mtandao wake za kumwingiza Ikulu, na kutokana na udhaifu wake mkubwa wa kujali zaidi maslahi ya kibinafsi na maswahiba kuliko hatima ya nchi na walalahoi, tulifahamu kabla ya tamko lake kwamba atamtumia Mkurugenzi wa Mashitaka (Director of Public Prosecution) kuwalinda wote waliohusika katika uporaji wa Nchi pamoja na mtuhumiwa mkuu Benjamin William Mkapa.

Ndiyo maana Kamati hii ilianza kazi yake mwaka 2006 kwa kufungua kesi ya Katiba Nambari 86/2006 ili kumwondolea Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) mamlaka makubwa mno kupita matakwa ya Katiba ya Nchi, yaliyompa uwezo wa kuwalinda maharamia wote ambao Rais hatataka washitakiwe na kufungwa na kufilisiwa. Ndipo unaposimama ujasiri wa Kikwete wa kutamba kwamba atayalinda majizi ya mapesa yetu ya EPA, Richmond/Dowans yasifikishwe mahakamani! Tunataka haki ya wananchi ya kujiendeshea mashitaka wao wenyewe wasipokuwa na imani na DPP.

Swali zito ni Kwanini Mahakama Kuu haitoi hukumu ya kesi hii nyeti ya hatima ya Nchi yetu na uhuru wetu?

NB:Tusisahau kuwa hiyo PILCOM SI MTIKILA MWENYEWE!

Na kama sijakosea..Walisema kuwa kuna wabunge wengine wa ccm watakaojiunga nao!

Huu ndio muda wa kufanya yale yanayotakiwa kufanywa!

NI MUHIMU KUSIMAMIA UPANDE WA HAKI NA HIVYO BASI..PILCOM SI MTIKILA...NA HII NI KAMA ILIVYOELEZWA HAPO CHINI....

KAMATI YA KUPAMBANA NA UPORAJI WA NCHI
PUBLIC INTEREST LITIGATION COMMITTEE
(PILCOM)

Kamati hii ilianza kujiunda tangu mwaka 2006 na wahanga wa ukombozi wa nchi yetu, kutoka katika Vyama vya siasa, taasisi za kidini, makampuni ya wanasheria mahiri, Taasisi huru za wananchi, na mshikamano mtakatifu wa wazalendo ndani ya Bunge letu, ambalo katika Ibara ya Nane ya Katiba ya Nchi yetu ndilo linaloitwa “Wananchi”. Ni mbinu yetu ya vita kutowaweka wazi wahanga wetu kwa sasa.
 
Na hivyo basi...Hakuna mwananchi asiyewakilishwa kwenye PILCOM na hivyo tuache UMBEYA na kutowa sapoti kwa wazalendo!

Mbona mnamlaumu Mtikila na mmeiacha familia ya mwalimu iliyokataa kumkana Mkapa?

Mbona hamusimamii UPANDE WA HAKI?

KUNA WATU WANA WAZIMU HUMU NDANI AMA NI MAPEPO?

Hatutaki watu wa kutuvuruga na MIMI NIMESHASEMA SITOKUBALI!

Kwani tulijifunza mengi sana kwenye enzi za Mrema na NCCR MAGEUZI!

Na kama haya yanayotokea sasa hivi ambayo hayana tofauti kubwa sana na ya wakati ule yakiachiwa yaendelee...Basi TUMEKWISHA!

TULIFANYA MAKOSA MARA YA KWANZA NA TUKAINGIA UTUMWANI...SASA NI KIPI KINGINE MNATAKA NYIE MADHALIMU?
 
Unajua hapa Mtikila hakujipanga lakini ndo hivyo kaharibu kauli alizotoa zinasababisha RA ajipange zaidi kummaliza kabisa Mtikila.Cha kusikitisha alishindwa hata kwenda kukopa BANK?
Bank nazo si zimejaa ufisadi uleule? ukienda mweusi upati ukienda mweupe hata bila bond unapewa unazopenda sio unazohitaji. Upo hapo?
 
Hivi huyo mtikila anachunga nini????

Ni mchungaji au mtungaji???

Mi namuona ni dalali wa siasa tu!!!!
 
Mwanahalisi usiogope. Wengi tunakuunga mkono. Kama walitaka kukutoa roho pale walipokumwagia tindikali na bado hukuogopa kuendelea kuwaumbua, nini shs bilioni 3?. Kweli Mwanahalisi halina hizo bilioni 3 lakini sisi maskini wengi tunaotetewa na Mwanahalisi tutazichanga.
UJUMBE KWA ROSTAM: Fanya haraka uende mahakamani maana hata hilo ulilozuiwa kulisema bungeni, utaweza kulisema mahakamani!

Hili swala si jepesi sana kama mnavyoona , haihitaji ushabiki hapa.Kitakachoweza kumzuia Rostam kwenda mahakamani ni wenzake wakimshauri.Otherwise akienda mahakamani wengi wetu tunasema na vithibitisho hatuna,Japo walitakiwa na wanatakiwa wawe na vithibitisho.Sumaye ilikuwaje???.Swaala la kusema tutachanga haya magazeti tayari tunayachangia kwa kununua kila siku.kubenea asitake kuandika nakala ya kuonewa huruma hili ni yeye na Rostm.Akiwa na ushahidi aeleze umma ushahidi hupo kwa jinsi hii nitatoa mijihela mingi.Na unaonyesha wewe ni mmoja wa watanzania wachache ambao wako tayari kujitoa kupigania hali hii.Swali ni wko wangapi kama wewe?
 
Back
Top Bottom