Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam hana ukingmaker wala nini ! zaidi ya ufisadi hana haliwezalo ndo maana hata press release aloitoa kempinsky aliandikiwa na lowassa. Upeo wake mdogo and most of the times he lacks original ideas ni mtu wa kukopakopa mawazo tu.
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza,rostam ana akili kuliko unavyoweza kudhania wewe....ata mtihani wa darasa la saba aliongoza mkoa wa tabora acha mbali first class ya degree yake.haya mambo ya kashfa ya ufisadi yameanza miaka ya 2005 wakati vodacom iko tangu mwaka 2002,hapo ulimpa wewe mtaji.radio uhuru alianzisha toka mwaka wa 1999 kabla ya kukipa chama.gazeti la mwananchi lilianzishwa toka mwaka wa 1996 kabla ya kulimerge na National.mashamba makubwa ya chai anayo toka mwaka 1994 na hapo alikuwa anapewa na nani...akili zake ni nyingi na mnuhitajika watu hamsini kama wewe ndio mtoe kichwa kimoja cha RA
 
Padri Karugendo,

Hili tulishalisemea toka zamani sana,ukiachilia mbali na hayo yote ya RA ila wewe kama mtu uliyesomea dini,naomba utuambie lego la kanisa kwa watu ambao waovu?Je tunawapokea na kuwakaribia au tunawatenga na kuwafukuza?

suala lingine ni hili la Mtikila,kila mtu yuko huru kuamua ajibizane na nani na sijibizane na nani,Mie nina uwezo wa kuamua tu kwamba sitaki kujibizana na Shalom kwa sababu zangu binafsi tu,au kubeza hoja za Mp,Naamua tu bila kuingiliwa na mtu mwingine.hilo alikuwa sahihi

Kuhusu suala la watu kutoridhika na nafasi zao,lina ukweli ndani yake na lilisababishwa na yeye kuwa karibu na Rais hivyo waliokosa walijua yeye ndiye alimshauri Raisi kuhsu hili.

Maendeleo ya Tanzania yanakuwa magumu kwa sababu ya kukosa sera zilizo bora na hayarudishwi nyuma na watu hata siku moja,ila ili uendelee unahitaji watu,siasa safi na utawala ulio bora.Tumekosa utawal ulio bora has akwa watendaji wengi wa serikali ambao wamaekuwa watumwa wa kukimbia 'workshop' na kuacha kubuni miradi ya maendeleo.

Mie nadhani kama tunaona RA ni mchafu,Yes i once said ni bora mwenye ushahidi aupeleke mahakamani


Maweee...!!! Kumbe kweli Gembe ni kibaraka mzuri wa Rostam?!
 
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza,rostam ana akili kuliko unavyoweza kudhania wewe....ata mtihani wa darasa la saba aliongoza mkoa wa tabora acha mbali first class ya degree yake.haya mambo ya kashfa ya ufisadi yameanza miaka ya 2005 wakati vodacom iko tangu mwaka 2002,hapo ulimpa wewe mtaji.radio uhuru alianzisha toka mwaka wa 1999 kabla ya kukipa chama.gazeti la mwananchi lilianzishwa toka mwaka wa 1996 kabla ya kulimerge na National.mashamba makubwa ya chai anayo toka mwaka 1994 na hapo alikuwa anapewa na nani...akili zake ni nyingi na mnuhitajika watu hamsini kama wewe ndio mtoe kichwa kimoja cha RA

Unamjua Rostam kama vile baba yako

...ndiyohiyo
 
Mada hapa ni Rostam Aziz..Tunaomba pia tuwekewe Aliases zake..Maana lazima ana majina mengine kama sikosei.

Mada haijatoka nje kabisa kwasababu huyo jamaa ana nguvu kuliko Rais mwenyewe na kwahiyo tukianza kumzungumzia ni lazima tu refresh memories...Na kwa kuanzia tunaangalia na timu yao ya wana mtandao ili kuweza kujuwa wana agenda gani.

Mara nyingi kamati ya uchaguzi ina reflect agenda za mgombeaji..Sasa wasome hao watu na ujiulize toka hiyo kamati ya uchaguzi ya kampeni ya JK iteuliwe hadi sasa ni mangapi yametokea na wajumbe wake akiwemo RA...wana husika vipi kwa mambo yote yaliyoigubika serikali ya JK na kwa jinsi mtu huyu alivyo na nguvu za kupindukia kwenye Taifa letu.

Kwanza bado tumeanzia juu juu tu.

Rostam ni eneo la huko Iran...Lina maana yake na ni la kihistoria...Hivyo huwezi kutenganisha Rostam na PRIDE YA MUIRAN...Huyo ni MUIRANI NA INTEREST ZAKE NI ZA IRAN NA SI TANZANIA.

Hilo liko wazi na HAKUNA KUMTETEA HAPA BILA YA KULETA MAELEZO YA KUTOSHA KUWA HUYU MTU NI NANI!

Huyu mtu aliyekuwa na biashara kwenye Taifa letu wakati babu yangu akimpiga mwarabu.

Tena labda alikuwa ni babu yake...Historia iwekwe wazi hapa...Na kama anataka kutawala Tanzania kwa misingi ya chuki za kidini na kikabila..Basi ajihadhari sana...Na nilishamwambia aachane na siasa.

Hata majina ya kampuni yake yana historia na Iran mfano (Ushahidi) Caspian ni kajisea ka huko. Kwa nguu zake ni kweli mfano alipata kazi kwenye mgodi fulani na mojawapo ya sababu ni kampuni hio kuwa karibu na serikali. Ushahid wa karatasi hapa hakuna lakini yalizungumzwa.
 
mshauri aende mahakamani ili umjibie hoja(ufisadi). With the help of dirty money he has amassed over the years through palm greasing and political patronage utajiri alionao si wa kujivunia wala hauvutii achilia mbali wewe kuuorodhesha kwa makeke na mbwembwe nyingi. Hautokani na jasho lake wala uwezo wake wa akili bali na dhuluma za wazi kwa wananchi wazalendo(kumbuka pamoja na ubunge wake wakununua hana chembe ya uzalendo na Tanzania yetu tukufu.
I regard your defence on his behalf as ultimate neurotic flight from reality and justice.
SHAME ON YOU.
 
ROSTAM AZIZ NI NANI?
Hoja hii kwa Watanzania makini ni nzito sana na mwandishi aliyejiuliza swali hili amezama kwenye mada kwa umakini mkubwa. Nataka tu kumsaidia kusema kuwa kwa sisi tunaomjua Rostam Aziz kwa karibu sana, usitake kujua kwa vipi, huyu bwana ni mtoto mdogo sana lakini fedha aliyoitwaa kwetu sisi wajinga imemlewesha na anatuona wote wapumbavu, watumwa ambao babu yake alikuwa akiwanunua na kuwauza huko Tabora kama alivyokiri mwenyewe.
Mimi nimeishi Mkoa wa Tabora kwa miaka mingi kidogo. Baba yake Rostam tulimjua kwa jina la Aziz Mchele, jina hilo la pili linatokana na kazi aliyokuwa anafanya baba yake. Alikuwa mchuuzi wa mchele, anasomba kwa gari yake kutoka Shinyanga kuja Dodoma hadi Dar es Salaam. Hakuwa tajiri, maana tajiri hakeshi usiku kucha akihangaika na malori akichuuza mchele.
Yeye mwenyewe Rostam na kaka zake alikuwa mchuuzi wa ngozi. Maisha magumu kwelikweli alikuwa nayo. Neema ameipata kipindi cha Mwinyi na Mkapa kwa kufunguliwa milango ya Hazina ya Taifa, kama ilivyofanyika kwa Manji.
Baba yake na mama yake Rostam Aziz wako nchini Iran. Ni raia wa huko. Ndugu zake karibu wote wako Iran, vilevile. Huyu ndo kada wa kuaminika wa CCM! Lazaros


Lazaros,
Hizi ni habari njema sana kuzisikia. Nilikuwa najiuliza tangu nimeanza kuzisoma thread kuhusu issue hii, hivi hakuna anayemfahamu Sakarir ambaye pengine amekua naye huko Igunga, kucheza naye na hata kusoma naye? Tunahitaji kupata more details zake wapi alikosoma, hata shule ya msingi, mwaka gani hadi mwaka gani, alikuwaje darasani, na mambo kama hayo. nadhani from there tunaweza kupata picha halisi alizaliwa mwaka gani maana kule kwenye web ya bunge ameficha, sijui kwa nini anaogopa? Leteni vitu jamani.
 
Fairplayer,

1852 kulikuwa na biashara mbili hapo maeneo ya Igunga ya sasa nayo ni Watumwa na Pembe za ndovu. Kama wasemavyo wenzetu, si vizuri kupenda kurusha mawe kama unaishi kwenye nyumba ya vioo.

Adili

Kwa kuwa utumwa ulikoma kitambo, sitaki kuamini kwamba huyu jamaa amechuma fedha hizi kwa kuuza pembe za ndovu. na kama ndivyo, yawezekana ni miongoni mwa wale 'wawindaji' haramu wanaoiba nyara za serikali. na kama ndivyo, basi ni hatari zaidi.
 
Eti magazeti ya African na Mtanzania ni ya nani?



NINASIKIA Jenerali Ulimwengu hana shea tena kwenye HCL? Je, ni kweli? Ninasikia mwenzao mmoja ambaye kashika pazuri kwenye ofisi fulani ya mkubwa ndiye aliyewauza wakati wao na waanzishli wanahisa wenzake hawana habari?

Tetesi ni kuwa mmiliki mpya kanunua magazeti hayo ili kuyatumia kama alivyotumia gazeti jingine maarufu nchini kumweka kipenzi chake Ikulu!

Na wale wale wakina Kingmaker wa Mkapa wenye asili ya Unyarwanda ndio viranja na wasuka mambo!!!!

Ikifika Juni 2009 Magazeti hayo yataanza kutumika full blast kumpromoti alternative president awe anayetakiwa au chaguo litakalowasaidia kazi wajanja wanaojua kuifagia Hazina na BOT!!!
 
Kama ni hivyo kuanzia kesho siwapi mafisadi shilingi yangu!
 
Kwa kuwa utumwa ulikoma kitambo, sitaki kuamini kwamba huyu jamaa amechuma fedha hizi kwa kuuza pembe za ndovu. na kama ndivyo, yawezekana ni miongoni mwa wale 'wawindaji' haramu wanaoiba nyara za serikali. na kama ndivyo, basi ni hatari zaidi.


Ni kuwa walikuwa na nguvu ya utajiri tangu enzi za utumwa kwani familia yake ilijihusisha na biashara ya utumwa i.e kizazi chake cha awali. Ni kama leo mramba atoweke kwenye ramani ya dunia, si watoto watabaki na utajiri hadi wajukuu?? Kibo Palace Hotel itaendelea kuwatunza na share za Precicion Air na nyinginezo. Ndiyo maana tunasema utajiri wao wa haramu kina RA umeanzia mbali huko. Uharamia wao uliendelea kukua zaidi pale walipoanza kujiingiza kwenye biashara ya nyara za serikali. Mtafuteni Barrati Godda ana data zote za biashara ya nyara za serikali za RA maana Barrati ndiye mwandani wake mkubwa japo hafaidiki na lolote pale. Yeye anaambuliwa kushika pembe wakamuaji ni wengine. Pia Mulla is a family member na anaendekeza libeneke la biashara ya nyara kama kawa!!!! Hivi zile nyara za Mullah zilikamatwa ikafichwafichwa imeishia wapi???

Utajiri wa RA= f(bu, ny,un,te,kg,epa ...n) where as
bu= biashara ya utumwa
ny= nyara za serikali
un=biashara ya unga
te=tax evasion (kujongo kodi)
kg=kugushi
epa=kagoda
n= you name all up to the nth variable i.e welcome to add yours!!!

Kwa mantiki hiyo, asijidai eti biashara zake ni clean and ni mtu safi. Hana adabu. Kwanza hiyo ni single equation. To him anatakiwa awe na multivariate equations ya mali zake za haramu.
 
Napenda kuuliza alipo RA, mara ya mwisho in public ameonekana TBC akiwa ktk kikao cha NEC pale Dom,

Kama wajua, au umemwona cku za karibuni tujulishe tujue, ni mtu mhimu sana huyu ...
 
Leo nje ya Marriot Hotel London nimemuona mtu kama Rostam .Je ni kweli ni yeye ama ni mawenge tu yamenishika ?Hebu wajuvi mlioko TZ nipeni habari kama huyu jamaa kesha rudi toka huku ama bado .
 
Leo nje ya Marriot Hotel London nimemuona mtu kama Rostam .Je ni kweli ni yeye ama ni mawenge tu yamenishika ?Hebu wajuvi mlioko TZ nipeni habari kama huyu jamaa kesha rudi toka huku ama bado .

Mkuu unakata viwanja tu... check ur PM
 
Leo nje ya Marriot Hotel London nimemuona mtu kama Rostam .Je ni kweli ni yeye ama ni mawenge tu yamenishika ?Hebu wajuvi mlioko TZ nipeni habari kama huyu jamaa kesha rudi toka huku ama bado .


acha uwongo

MARRIT LONDON ziko zaidi ya 10 ipi hiyo au ndio mikamba tuu?
 
Yupo mjini! Sasa sijui unataka kujua where he is at a given time? labda ufafanue zaidi kidogo swali lako...
 
Yupo mjini! Sasa sijui unataka kujua where he is at a given time? labda ufafanue zaidi kidogo swali lako...

yuko kimya na kwenye vijiwe vyake hatumwoni, nilitaka kujua kama kuna mtu kamtia jichoni for the past 10 days!
 
Mkuu unakata viwanja tu... check ur PM

Mkuu Masatu
Mie sijaona PM yako lakini yes niko viwanja huyo anayesema ni kamba sina muda wa kubishana naye .Swali langu lilikuwa dogo na majibu yake wachache wamenipa sasa huyo wa kulia na kamba kazi kwakko .
 
Siku zoote nimekuwa nikiamini RA is one of the smartest crooks we have in TZ lakini inaonekana si kiiivyo!!!!!!! With this one, jamaa ameplay so low!

Well mitambo ya dowans inauzwa na hii inaonekana imewekwa jana kwenye alibaba.com maana watu tumekuwa tukiitafuta details za DTL siku nyingi kwa kugugo na only this morning tunaiona hii ikiambatana na press release (Soma mwananchi hapo chini) iliyotolewa jana hiyo hiyo na Dowans. Soma mwenyewe uangalie hizo details za muuzaji halafu tell me kwamba je ni kweli hapa kuna uuzaji au changa la macho.


Mauzo (Bofya hapa mbele): On sale - Dowans Tanzania Ltd - Energy,

How do u sell stuff that is worth $100m (as quoted from Dowans)

1. Huna Address?

2. Mtu wa kumpigia anasema call me?

3. Simu yenyewe imekaa kimazabe mazabe au kimagumashi?

4. Company details hamna?

5. Hamna picha


KWA KIFUPI HUYU JAMAA SASA ANATAPATAPA. ETI HUU NI USHAHIDI KWAMBA WALIKUWA WANAUZA SI KWA TANESCO TU. But why ianze kuonekana kuanzia leo asubuhi????????


Dowans yaibuka na kitendawili
Mwananchi Tanzania News Paper



KAMPUNI ya Dowans Tanzania Limited (DTL) jana ilivunja ukimya wake katika sakata la ununuzi wa mitambo ya kuzalishia umeme wa dharura na kutoa taarifa ya ufafanuzi wa sakata hilo, huku ikiendeleza kuficha wahusika wake hapa nchini.


Serikali imekuwa ikihaha kutaka kununua mitambo hiyo ya Dowans, ambayo ilirithishwa mkataba wa uzalishaji wa umeme wa dharura kutoka kampuni Richmond Development Company iliyoshinda zabuni hiyo mwaka 2006, lakini wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na wadau wengine wamepinga vikali azma hiyo wakitaka Sheria ya Manunuzi ya Umma, inayopinga ununuzi wa mitambo ambayo ni mitumba, iheshimiwe.


Tangu kuanza kwa sakata hilo mwishoni mwa mwaka jana wakati Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini iliposhauri mitambo hiyo isinunuliwe, Dowans imekuwa kimya licha ya watu kadhaa kuhoji umiliki wake, huku watendaji wake wa hapa nchini wakikaa mbali na vyombo vya habari.


Lakini jana, Dowans ilitoa tangazo ambalo halikuwa na jina la aliyelitoa wala wadhifa wake, ikijielezea kuwa ni kampuni safi ambayo imefanya kazi sehemu mbalimbali duniani na kwamba mitambo yake ni bora, ambayo kama si Tanesco ingeshapata mnunuzi zamani.


Pia Dowans imetetea azma ya Tanesco ya kununua mitambo hiyo, lakini kuponda kitendo chake cha kusitisha mkataba uliokuwa uishe Septemba mwaka huu, ikisema kuwa kilifanywa bila ya kuwepo kwa malalamiko yoyote ya uzalishaji mbaya na kwamba kitendo hicho kimejibiwa kwa hatua muafaka, ambayo ni kuishtaki kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Biashara.


"Kwa kutilia maanani ukubwa wa uwekezaji wa DTL, madai na shutuma kwamba DTL siyo chochote na kuwa siyo mwekezaji makini na mwenye msimamo siyo za kweli, ni za kupotosha na kwa kweli ni za kupakana tope tu," inasema taarifa hiyo ya Dowans iliyotolewa na mtu ambaye hakutajwa jina wala wadhifa wake.


"Isitoshe, tofauti na ripoti kadhaa zisizokuwa za kweli, mitambo ya kuzalisha umeme ya Dowans haikurithiwa kutoka kwa “mtu mwingine".


DTL ni kampuni makini ambayo ilijiingiza kwa nia nzuri katika shughuli hiyo kwa misingi ya kibiashara.


"Mkataba wa DTL na Tanesco ulifikiwa kwa majadiliano ya wazi kabisa na DTL inaridhishwa na utendaji wake kwa muda wote wa mkataba kwa sababu tuliutekeleza mkataba huo kama ilivyostahili.


Na ili kuondosha shaka lolote, DTL haina uhusiano na haijapata kuwa na uhusiano na kampuni ya Richmond Development Company LLC, kampuni ya Texas, ambayo awali ilishinda mkataba wa kuzalisha umeme kwenye eneo la Ubungo.


"Yamekuwapo madai vile vile kuwa mitambo ya kisasa kabisa inayotumia gesi ya DTL ni “mizee na michakavu". Wakati wote wa muda wa mkataba kati ya Dowans na Tanesco, suala la utendaji na uwezo wa mitambo halikupata kutokea wala kutajwa na Tanesco, kwa sababu kila moja ya mitambo hiyo ni aina ya mitambo ya kuzalisha umeme inayoheshimika na kukubalika duniani, na kuwa mitambo hiyo ilinunuliwa moja kwa moja kiwandani kwa mtengenezaji/mwuzaji ikiwa mipya chini ya dhamana ya mwuzaji.


"Mitambo yote mitano inao uwezo wa miaka mingi wa kufanya kazi, na kama itatunzwa vizuri, inaweza kuendelea kuzalisha umeme kwa zaidi ya miaka 25."


Taarifa hiyo pia imezungumzia hatua ya mkurugenzi wa Tanesco, Dk Idris Rashid cha kusitisha mkataba huo kabla ya kipindi chake kumalizika, ikisema kuwa kilifanywa bila ya kuwepo na sababu yoyote iliyo dhahiri wala kuonyesha kutoridhishwa na utendaji wa Dowans.


Dk Rashid, ambaye amekuwa mstari wa mbele kushinikiza kununuliwa kwa mitambo hiyo, aliandika barua ya kuvunja mkataba na Dowans mwishoni mwa Julai, akisema urithishaji mkataba kutoka Richmond ulikuwa na matatizo ya kisheria na pia utata katika usajili wa Richmond, ambayo ilishindwa kuleta mitambo hiyo ya kuzalisha umeme wa dharura.


Hata hivyo taarifa hiyo ilifafanua kwamba, agizo la Tanesco la kuiamuru DTL kuacha kuzalisha umeme lilikuja ghafla, wakati DTL haikuwa na mipango bora zaidi ya kupata matumizi mengine ya mtambo wake katika eneo la Afrika Mashariki.


"Hatimaye, kwa kukiuka agizo lake la kutaka DTL iache kuzalisha umeme, Tanesco, kwa mara nyingine bila kuiarifu Dowans, ilifanikiwa kupata amri ya mahakama iliyotolewa bila DTL kuwasilisha maelezo yake, ya kuizuia DTL kuendelea na mchakato wa kujaribu kuuza mtambo wake. Hii, bila shaka, itaongeza gharama ambazo DTL tayari imeingia. Amri hiyo ya Mahakama... inapingwa kwa njia mwafaka," inaeleza taarifa hiyo ya Dowans.


Kuhusu hatua ya Tanesco kung'ang'ania kununua mitambo ya Dowans, taarifa hiyo inaeleza kuwa shirika hilo la umeme si mteja pekee kwa sababu tayari ilishaanza mchakato wa kuiuza katika soko la dunia, ambalo kampuni hiyo imedai lilivutia wateja wengi. Lakini imeeleza kuwa kitendo cha Tanesco kwenda mahakamani na kufanikiwa kupata amri ya kuzuia kuuzwa kwa mitambo hiyo ndio kumeifanya isitekeleze azma hiyo.


"Taarifa hiyo ilizidi kueleza kuwa, ingawa Tanesco ilijitahidi kutafuta kila njia ili kuikwamisha Dowans katika mipango yake, DTL ilikaribisha wanunuzi kwa njia ya uwazi na iliyo ya hadhara kutoka makampuni ya kimataifa yenye sifa ya kununua mitambo yake, inaeleza taarifa hiyo.


"Kwa hiyo hisia zozote kuwa TANESCO ilitaka kununua mtambo huo kinyemela na bila ushindani ni jambo lisilo la kweli. Kwa kutilia maanani mahitaji makubwa ya kimataifa kwa ajili ya mitambo ya kisasa kama hiyo na maombi yenye ushindani mkubwa ambayo yamepokelewa, ni dhahiri kuwa Mitambo hiyo ingekuwa imeanza kutumika kibiashara sehemu nyingine siku nyingi, kama isingekuwa kutokana na amri ya bahati mbaya kabisa ya mahakama iliyotolewa kwa Tanesco."


Dowans Tanzania Limited, ambayo inamilikiwa kwa pamoja na kampuni ya Dowans ya Costa Rica na Portek ya Singapore, imekuwa haipatikani kuzungumzia masuala mbalimbali yanayoihusu kutokana na watendaji wake kuelezwa kuwa wako nje kikazi kila wanapofuatwa kwenye ofisi zao zilizopo Ubungo.


Jana, Mwananchi ilifanikiwa kumpata mmoja wa maofisa wake ambaye nambari yake ya simu imewekwa kwenye tovuti yao, lakini hakutaka kutoa maelezo yoyote zaidi ya kuahidi kuwa wangetoa taarifa.


Mtu huyo, aliyekuwa akizungumza lugha ya Kiingereza, alikataa hata kutaja jina lake, akisema kuwa vyote vingekuwepo kwenye taarifa yao.


Lakini, taarifa hiyo (iko ukurasa wa 14 wa gazeti hili) haikutaja jina la mtendaji huyo wala muhusika mkuu hapa nchini. Hata mwandishi alipokwenda kwenye ofisi za kampuni hiyo jana, alijibiwa kuwa taarifa hizo zote zingetolewa kwenye tangazo hilo.


Ikizungumzia mitambo hiyo aina ya TM 2500 na LM 6000PD iliyotengenezwa Marekani na yenye uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 120, Dowans imeielezea kuwa ni ya bei nafuu, iliyonunuliwa ikiwa mipya, iliyotumika kwa muda mfupi na yenye uwezo wa kuendelea kufanya kazi kwa miaka 25 ijayo kama ikitunzwa vizuri.


"DTL ilifunga na kuzindua mtambo huo wa kisasa kabisa kwa gharama ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 100. Gharama hizo zinalingana, ama kuzidi, kabisa na gharama zinazokubalika kimataifa za kufunga mitambo ya umeme za kiasi cha Dola za Marekani milioni moja kwa megawati moja ya uwezo wa kuzalisha umeme (installed capacity)," inaeleza taarifa hiyo.


"Ni jambo lisilowezekana kufunga Mtambo unaofanana na huo kwa gharama ya dola za Marekani milioni 30."


Taarifa hiyo inalinganisha thamani ya mtambo wake na miradi mipya ya Kenya, ambako umefungwa mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 90 kwa gharama ya Dola 160 milioni za Kimarekani, Rwanda (mw 100 kwa Dola 325 milioni) na Ghana (mw 660 kwa Dola 900 milioni za Kimarekani) kuwa sehemu ya mifano ambayo inaonyesha gharama za mitambo hiyo kuwa kubwa.
 
Back
Top Bottom