Rostam Azizi ahoji wawekezaji uchwara

VERY SENSEFUL ANAKUJA MTU ANAJIITA MWEKEZAJI ANAJAZA NCHINI MASHINE ZA KAMARI BADALA YA MWEKEZAJI KUWA MKULIMA MKUBWA, FOOD PROCESOR, AU MMILIKI WA VIWANDA VIKUBWA VIKUBWA VYA NGUO NA N. K, THE GUYS IS SO SMART.
BY 100%.
Wawekezaji uchwara wa Kichina watimuliwe mara moja.
 
One size never fits all. Huo mfano wa mabati hauwezi kuwakilisha bidhaa zote zisizo na ubora. Bidhaa ziko nyingi sana. Hata spare parts za magari makubwa kwa madogo.

Ongelea bidhaa kwa ujumla wake. Sasa unawatetetea masikini kuhusu bidhaa kama Tvs.
 
One size never fits all. Huo mfano wa mabati hauwezi kuwakilisha bidhaa zote zisizo na ubora. Bidhaa ziko nyingi sana. Hata spare parts za magari makubwa kwa madogo.

Ongelea bidhaa kwa ujumla wake. Sasa unawatetetea masikini kuhusu bidhaa kama Tvs.
kwa maisha yetu ya kimaskini,ubora sio muhimu sanaaa,na ndio maana kwa soko la Afrika mchina amelishika vizuri,kulinganisha na mataifa mengine.Huo mfano wa bati ni mmoja tu lakini bidhaa ni nyingi sana,Mfano kwa maisha yetu haya ni wangapi wanaweza kununua pikipiki ya mjapani?!!
 
Kama kawaida yako, hujaelewa. Hoja yake ni ukweli lakini yeye mwenyewe ametokea huko huko. Rostam ni mwekezaji uchwara aliye-take advantage ya uongozi mbovu wa CCM kifikia hapo alipo. Inakuwaje leo ndiyo analiona hili wakati ndilo lililombeba? Jibu ni moja tu. Ni wivu. Hatuonei huruma wazawa kama wajinga wachache wanavyodanganyika. Analisema hili kwa sababu anaona himaya zake ziko kwenye tishio.
 
Ukweli ni kwamba Rostam haonei huruma wazawa, watanzania. Rostam anajua kabisa jinsi viongozi wetu na mifumo yetu ilivyo dhaifu, hivyo anaona ni tishio kuruhusu wawekezaji uchwara waje kwani mfumu na viongozi wetu utawabeba na baada ya muda watakuwa tishio kwake. Yeye anajua kabisa sisi wazawa bado tumelala hivyo siyo tishio kwake. Usinielewe vibaya: hoja yake ni ukweli mtupu. Ila sababu ya kutoa hoja ndiyo ina walakini. Ni kama simba anavyowashambilia wanyama wengine walao nyama kama chui. Siyo kwamba anawaonea kina nyumbu na swala huruma, la hasha. Anaona himaya yake inaingiliwa.
 
Mkuu kwa ujumla bidhaa fake zipo sana kitaa. Tena nyingi tu ambazo haziwahusu masikini. Kwa upande wa pikipiki hakuna shida. Hizo zinarudisha pesa kwa vijana waliojiajiri.

Lakini soko likishakuwa saturated na bidhaa zisizo na ubora, halafu tukashabikia kwasbabu kuna ambazo masikini ananufaika kama wewe unavyodhani, basi we are a nation doomed for failure.
 
Nimeipata hoja yako. Lakini nadhani someone, somewhere has to say something.

Mfano huo ukweli kuhusu hayo madubwasha ya betting yanavyomaliza vijana ambao ndo nguvu kazi ya Taifa.

Taifa kwasasa lina vijana wengi sana Lakini bure kabisa. Kijana analala na kuamka akiwazia kupata chochote kitu aende ku bet kwa mchina.
 
Huyu hapa. Akemea wawekezaji uchwara

View attachment 2396908
Arudishe kwanza mgao wa Richmond ndipo tutamuamini. Vinginevyo huu ni wivu wa kike. Wachina wanafanya shughuli zao kihalali na wanalipa kodi serikalini yeye anataka wafukuzwe halafu nchi ikose kodi? Kamari sio dhambi na serikali inaruhusu kuchezesha kamari ilmradi tu huyo mchina analipa kodi. Yeye kinachomuuma ni nini? Akae chini atulize tako ama vipi naye arudi kwao Iran atuachie nchi yetu asichonganishe na wawekezaji. Mfyuuu zake!
 
Unadhani chanzo cha tatizo ni nini mkuu? What exactly is the root cause of the problem? Wachezesha kamari wapo kihalali na wanalipa kodi serikalini. Jambo la msingi ni kushauri nini kifanyike ili serikali iachane na kodi za kamari. So long as serikali haina vyanzo vingine vya mapato, kamari itaendelea kuwepo na vijana wasiokuwa na ajira watazidi kutopea kwenye uraibu wa kamari.
 
Anguko la ngozi nyeusi toka enzi na dahali ni kuamini, kusujudu, na kuhisani mgeni.

Rostam sio mweusi ndio maana anaona athari za kuji compromise na kuji expose kwa mgeni.

Rostam alisema mbele ya Samia Suluhu na Uhuru Kenyatta kwamba Tanzania hatuwezi kuwa mateja wa wageni siku zote. Ni baada ya Samia kutoa ki flimsy and thoughtless speech eti acha waja waje kwa sababu wao wana mtaji sisi hatuna mtaji. Wiki moja baada ya kifo cha aliyekuwa anatuambia tembeeni kifua mbele.

Mhindi anakuwa mzalendo kwa Tanzania kuliko mbantu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…