Rufiji: Vijiji 23 vimekumbwa na mafuriko makubwa kutoka Bwawa la Umeme la JNHPP. Je, Tathmini ya athari kwa mazingira ilipuuzwa kabla ya ujenzi?

Nchi hii ina mazingaombwe ya akili siku kadhaa nyuma kulikua na kauli za kusia samia, tumshukuru mama hayo mafuriko yameweza kuchukua kaya 1000 isingekuwa yeye yangechukua nchi nzima!
 
Na hii ndiyo imesababisha mtambo kuzimwa. Ccm huwa wanakurupuka sana.

Jiwe alikuwa hasmbiliki mshenzi yule. Yako wapi sasa? Legacy ziiiiii!!
 
Sidhani kusema wamesaidiwa ni sahihi, tukubaliane kuwa wameumizwa
 
Januari jr naona unakuja kwa style nyingine ya kujikosha!! Huku songwe hakuna Bwawa la Nyerere lakini vijiji vimezingirwa na maji.

Au kwa sababu huku Songwe tunakula Kitimoto?
 
Vijiji 23 si kidogo , hili ni janga kubwa mno ! Wazungu waliona haya mapema tukawapuuza na kuwaita mabeberu
Hamia huko Kwa wazungu, hao watu walishaambiwa kuhama hayo maeneo wakashupaza shingo, tatizo ni ucheleweshwaji wa kuwashwa Kwa turbines zote, turbines zote zingekuwa zinafanya kazi maji yangekuwa yakitoka kidogokidogo na bwawa lisingefurika hivyo kusingekuwa na haja ya kuyafungulia maji kama ilivyofanyika sasa.
 
Nchi hii ina mambo ya kijinga sana. Sasa maji yamefunika ardhi hiyo mbegu wataenda kuipanda wapi?
 
Umesha ambiwa hilo ni bonde bado unaenda kujenga, mtoa mada huna akili kama hao wanakijiji waliojenga bondeni.
Hivi umefanya tathmini kujua hao watu wapo hapo tokea lini? kuna mambo tusiyaangalie kiushabiki kama walikuja baada ya Bwawa kujengwa sawa wanamakosa ila kama Bwawa limejengwa wao walikuwa hapo toka zamani basi kuna swala la kijografia hapo ule mto kama unajua vyema huwa unapotea njia sana usiwalaumua bure.
 
Lissu alipondwa sana alipoliongelea hili kipindi kile.
 
Maji hayapandi mlima shehe, hao wamejenga bondeni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…