TANZIA Ruge Mutahaba afariki Dunia! Azikwa kishujaa kwao Kabale, Bukoba

TANZIA Ruge Mutahaba afariki Dunia! Azikwa kishujaa kwao Kabale, Bukoba

Lakini siyo mpasha habari. Anatakiwa asubili habari rasimi ndiyo atoe neno.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna taratibu za kutangaza misiba, hasa ya watu muhimu japo hata ya kawaida, ni dhahiri mfano taarifa za kifo cha mzazi wako, mwenza, mtoto wako hautangaziwi kienyeji enyeji.

Kwa watu wazito pia upo utaratibu wa kutangaza vifo vyao, CMG pamoja na utitiri wa media outlets walizonazo usifikiri walishindwa kutangaza wa kwanza na kuacha Rais atangaze then ITV kisha baadae sana wao.

Mataifa mengine wana mpaka sheria kwenye katiba ya namna ya kutangaza msiba wa kiongozi wao ambapo huanza na mlolongo wa viashiria kwanza kabla ya kutolewa official obituary.
 
Usipende kujumuisha Watu penda kujjitetea wewe kama wewe, Ruge alifarikia mida ya Saa 11:30-45 za Tanzania kwa Afrika Kusini ni Saa 10:30-45 jioni , Watu walifahamu na wengine walitoa taarifa ila sio rahisi kushadadia Taarifa ambayo huna Uhakika nayo ndio maana wengi walishituka baada ya Rais kutwiti!
 
Mrembo kama alikuwa anamkubali kwanini hakuacha sheria ifuate mkondo wake baada ya Bashite VYETI FAKE kuvamia ofisi za Clouds ili waweke kipindi cha Shilawadu ambacho kichaa alikuwa anasubiri akiangalie?

Hii ndo point...na alichangia mil 50, na Rais alikuwa anamkubali sana Ruge

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mrembo kama alikuwa anamkubali kwanini hakuacha sheria ifuate mkondo wake baada ya Bashite VYETI FAKE kuvamia ofisi za Clouds ili waweke kipindi cha Shilawadu ambacho kichaa alikuwa anasubiri akiangalie?
Best usijitoe ufahamu....toka lini stone akawa over bashiiite?...tuseme ukweli[emoji44]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
In some very rare situations almost exclusive ones... The majesty should be notified first.... BAE (if you can use this) it might be a coicedence OR deliberately planned... Or just common errors in human pre-planned missions

Jr[emoji769]
Coincidence,Andika tu kiswahili acha kulazimisha usivyovijua.
 
Mimi binafsi hua nina questioning mind, hua sikubaliani na kila ninachoambiwa bila kujiuliza.

Kwa maelezo ya mwana familia, Ruge alifariki majira ya sa kumi jioni siku ya juzi tarehe 26.2.2019 huko kwa Mzee Mandela.

Katika hali ya kawaida najua watu wa kwanza kujua habari ya kifo ni wanafamilia pamoja na ndugu na marafiki wa karbu mapema kabisa baada ya mpendwa wao kuwatoka. Hili la Ruge limekua tofauti, baada ya kupita takribani masaa 4 baada ya kifo, taarifa ya kifo imekuja kutolewa kwa hadhara na Mheshimiwa Rais.

Najiuliza tu, ilikuaje rais ndio akawa mtu wa kwanza kuujulisha umma kifo cha Ruge. Hakuna asiejua kua Ruge ni mtu maarufu ila hakua kiongozi wa kisiasa.

Najiuliza tu.

Rais aliwatangazia wapi? Tupe taarifa ya Ikulu ya kutangaza kifo cha ruge

Sema ww umepata taarifa kupitia personal page ya Rais Magufuli
 
Back
Top Bottom