TANZIA Ruge Mutahaba afariki Dunia! Azikwa kishujaa kwao Kabale, Bukoba

In some very rare situations almost exclusive ones... The majesty should be notified first.... BAE (if you can use this) it might be a coicedence OR deliberately planned... Or just common errors in human pre-planned missions

Jr[emoji769]
Am just saying; I mean, am just highlighting my take on this
 
Cha ajabu ITV Walikuwa wa kwanza kutangaza taarifa ya msiba kabla ya clouds kulikuwa na nini
Hapo kweli kuna cha ajabu,mimi nilivyoona tweeter ya Rais nikaweka cloud plus waliweka tangazo lao la changia matibabu.nikajiuliza hii clouds plus ni yao au kuna nini.
 

Vitu vingine wala havihitaji nguvu nyingi kuanza Kuvihoji au kuviwekea hisia fulani na ambazo pengine zimechanganyika na Chuki zetu kwa Rais Dkt. Magufuli au Utawala wake huu au Chama chake cha CCM. Kama leo unahoji ni kwanini Mheshimiwa Rais alikuwa wa Kwanza Kututangazia Kifo cha Ruge mbona haujahoji au huhoji ni kwanini Rais huyo huyo ndiyo alikuwa wa Kwanza Kujitolea Pesa za Kumsaidia Ruge kwa matibabu yake huko Umauti ulikomkutia?

Hakuna asiyejua kuwa Marehemu Ruge alikuwa na ' influence ' kubwa sana si tu nchini bali hata Serikalini na katika Chama chake cha CCM kutokana na umuhimu wake hasa wa Kifikra, Kiuwajibikaji na Ubunifu ambao uliweza kumfanya akubalike na aaminiwe na hata kufanywa Waziri Kivuli asiye na Wizara ' Maalum ' kwa Imani kwani kuna Mambo mengine / Vitu vingine Ruge alikuwa akivifanya ambavyo hata hao wenye Dhamana Wakuu wa Mikoa au Mawaziri hawakuweza kufanya au kuthubutu vile vile.

' Protocally ' Kitendo tu cha Mheshimiwa Rais ' Kujitolea ' vile katika matibabu ya Ruge tayari ilikuwa ni taa ya Kijani kwamba ' State House ' ilikuwa kwa 75% inasimamia kila Kitu chake na huenda hata taarifa za Maendeleo yake ya Ugonjwa zilikuwa zinaanza Kwanza kumfikia Yeye kisha ndipo zinaenda kwa Familia yake. Kwa mantiki hiyo its so obvious kwamba hata Kifo chake kilipotokea ilkuwa ni rahisi Kwake Kuutangazia Umma na nina uhakika hata Familia ya Ruge nayo ilimkabidhi Mtoto wao kwa ' State ' hali ambayo ndiyo maana hata Tangazo la Kifo chake Kilipotokea tu Mwenye Hisa mkubwa ' Tajiri ' Joseph Kusaga alianza Kwanza Kumshukuru Mheshimiwa Rais na Serikali yake ndipo akamalizia Kutushukuru na Kutupa pole akina ' Kajamba Nani ' siye.

Ni Mpumbavu / Popoma tu pekee ndiyo mpaka hivi leo hawezi kujua au hajajua kuwa ' Influence ' ya Ruge nchini ilikuwa ni Kubwa kuliko hata Watendaji wengine na ndiyo maana hata taarifa ambazo niligusiwa na Mtu mwaka jana ni kwamba kama isingekuwa huu Ugonjwa wake basi Marehemu Ruge ilikuwa ama ateuliwe Ubunge ili apewe Wizara au Kuundwe Taasisi moja muhimu nchini yenye Kujihusisha na Maendeleo ya Vijana na Ujasirimali ili aisimamie. Mheshimiwa Rais alimpenda sana Marehemu Ruge.

Mwisho kabisa kwa Kukusaidia tu ni kwamba ni desturi sehemu nyingi kwa Marais ambao huwa wanastaafu hupenda Kuwaacha ' Warithi ' Wao na taarifa muhimu za Watu wa Kufanya nao Kazi ili Uongozi wao uende vyema. Hakuna asiyejua kuwa Marehemu Ruge alikuwa ni Kipenzi cha Rais Mstaafu Kikwete na hata Mafanikio mengi ya Marehemu Ruge na Taasisi yake ya CMG yalikuja kuwa mazuri na kufanikiwa sana wakati wa Uongozi wa Awamu ya Nne hivyo ilikuwa ni rahisi mno kwa Mzee Kikwete ' Kumuambukiza ' Upendo wake kwa Ruge Rais Dkt. Magufuli ambaye kwa bahati nzuri nae pia aliona Uchapakazi wa Kutukuka wa Marehemu Ruge ndipo nae akaongeza Mapenzi yake maradufu Kwake.

Kikubwa kwa sasa tuache Kumjadili Marehemu Ruge kama tabia zetu za Kiswahili Kiswahili zilivyo bali tumuombee tu Makazi mema huko atakapohifadhiwa katika Nyumba yake ya Milele, Mwenyezi Mungu amsamehe, Sisi pia tumsamehe pale alipotukosea na tumuenzi zaidi kwa yale yote mema aliyoyafanya kwani siyo Siri alikuwa na Kipaji cha Kipekee kabisa na ameacha ' Legacy ' ya Kutukuka kabisa ambayo nina uhakika itatuchukua muda mrefu kuisahau na pengo lake kuja Kuzibika ni Kazi pevu / ngumu.

Rest In Peace ' Genius ' wa Entertainment and Creative Industry nchini Tanzania ' Mtani ' wangu wa Kihaya Ruge Mutahaba. Tutakukumbuka sana na mno Kaka. Nenda Kaka umeumaliza mwendo wako vyema na tuliobaki tutajitahidi kupita mule mule ulikokuwa Wewe japo najua Viatu vyako vitakuwa ni Vikubwa Kwetu na vitatupwaya kama siyo kutupwelepweta tu.
 
Mbona hajatoa pesa ya matibabu kwa lissu au lissu influence yake ndogo sana na tukio lake la kawaida sana ndiyo maana amelikataza na bunge kutoa pesa?. Vipi MO na Ruge nani influential katika uchumi uchumi na ajila kwa tz?. Kuwa mkweri rais anatumia baadhi ya matukio kisiasa na diyo maana anajadiliwa kisiasa kwa kila jambo lake. GENTAMYCINE,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wenzetu wana mind za kufanya discovery na innovation....sisi za kwetu ndo hizi
sawa sawa mkuu naona unataka kufumbua jambo
 
Lissu aliwahi kusema "tuna. ...... wa ajabu haijawahi kutokea!"
 
Wakiruhusu uzi wake spesho wa msiba naomba uniite

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya ndo nayozungumzia sasa ingekuwa na uzi wake, lkn humu kwenye taarifa ya kifo!!

Mods huu ni ukatili wa kihisia mnaotufanyia

Mnajua kabisa wengine hatuna channel ya clouds na mitandao mingineyo hatumo

Kimbilio ni humu lakini mnavyodengua sasa.......mfyuuuuuu
Watoto wa proffesor Mutahaba katika picha ya pamojaView attachment 1034003

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maandalizi ya kumzika marehemu Ruge Mutahaba katika kijiji cha Kiziru Wilaya ya Bukoba yamepamba moto na ujenzi wa kaburi umeanza leo.

Akizungumzia maandalizi hayo Siperatus Mbeikya, mmoja wa wanafamilia amesema taratibu zinaendelea ikiwa ni pamoja na kupokea wageni kutokana maeneo mbalimbali.

Pia, amesema maandalizi hayo yamekwenda sambamba na kukubaliana na kikosi cha usalama barabarani sehemu utakapopita msafara wenye mwili wa marehemu Ruge.

Pilikapilika zimeongezeka katika eneo la msiba ikiwa ni pamoja na kumwaga vifusi kwenye maeneo korofi.

Uchimbaji wa kaburi ulianza jana tangu kamati ya maandalizi ilipotangaza kuwa Ruge atazikwa kijijini na umeendelea leo asubuhi hatua itakayofuatiwa na ujenzi wake.

Ndani ya nyumba baadhi ya ndugu wa karibu walikuwa wakiendelea na kikao cha maandalizi ya msiba.
 
What if
asipoumia kama unavyotaka we we? What if kama ruge ndo alikuwa tatizo after heartbrake Dada wa watu akaamua Ku move on? What if hiyo kiduku ndio moyo wake ulipo?
 
GENTAMYCINE,
Dada, mambo ya chuki kwa rais yametokea wapi mamaangu?

Rais alikua wa kwanza kumchangia Ruge, ni kweli ila ni baada ya umma kutangaziwa kua Ruge anaumwa ndio rais akatoa mchango wake.
 
What if

asipoumia kama unavyotaka we we? What if kama ruge ndo alikuwa tatizo after heartbrake Dada wa watu akaamua Ku move on? What if hiyo kiduku ndio moyo wake ulipo?

😊😊😊..leo unasema hvyo tukimove on siku nyinhine mtasema wanawake huwa waharidhiki..alikua malaya tu..kha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…