Kenya 2022 Ruto Ameshinda, Je, ni kweli Rais Uhuru Kenyatta Ameshindwa? Au Odinga kachezewa Mchezo?

Kenya 2022 Ruto Ameshinda, Je, ni kweli Rais Uhuru Kenyatta Ameshindwa? Au Odinga kachezewa Mchezo?

Kenya 2022 General Election

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC), jana ilimtangaza Ndugu, William Samoei Arap Ruto kuwa Rais Mteule wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Kenya. Ruto ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kenya, na amehudumu chini ya Rais Uhuru Kenyatta kwa takribani miaka 10 sasa.

Pamoja na urafiki wa muda mrefu wa wawili hawa lakini mara kadhaa walikuwa wakipishana kauli na mwaka jana walikwaruzana kiasi cha Rais Kenyatta, kuamua kumuunga mkono mgombea urais kupitia Azimio la Umoja, Raila Odinga "Baba" akimtosa makamu wake Ruto aliyesimama kwa tiketi ya Kenya Kwanza.

Baada ya kutangazwa ushindi wa Ruto kuwa Rais Mteule wa Rais ya Kenya, maswali yamekuwa mengi vichwani mwa watu wengi.

Je Rais Uhuru Kenyatta ni kweli ameshindwa? Ni kweli kabisa Rais Kenyatta alichagua upande ambao hakua na uhakika wa kushinda?

Mwanafalsafa Muitaliano, Niccolò di Bernardo dei Machiavelli aliwahi kusema ni mpumbavu pekee anayeweza kupoteza uchaguzi akiwa madarakani, je tumuweke Uhuru katika hili kundi la Machiavelli au tuanze kuwa kwamba kuna namna Baba amechezewa mchezo?

Huyuhuyu Uhuru aliwahi kuwaambia Wakenya yeyey akitoka madarakani ataiacha nchi kwa kijana zaidi yake na sio kwa mzee, Je ndio tuseme amelihakikisha hilo?
Je, kugombana kwake na Ruto ilikuwa ni sehemu ya kumsafishia njia na kumuondoa kwenye kivuli cha madhila ya Serikali aliyohudumu kwa miaka 10?

Wakati bado unatafakari nakuacha na mfano huu:

"UHUU na RUU walikuwa marafiki. RUU akamwomba UHUU amuamchie kibanda chake cha mihogo kwa kuwa juma amemaliza muda wake…..........UHUU akamwambia RUU kuwa akimwachia kibanda ghafla atatengeneza uadui na wengine kwani kila mtu anataka kibanda hicho, lakini pia itaonekana kama wanapokezana kijiti …....... UHUU na RUU wakapanga kuwa wagombane kwa muda mrefu …..ugomvi wao ulidumu kwa mwaka mmoja hivi na watu wote mtaani waliamini hivyo........uchaguzi ukaja, HADHARANI, UHUU akamuunga mkono BABA, ila kwa kifupi ni kwamba jana UHUU kampa RUU kibanda."

Tafakari, Tujadili.

Uhuru-Kenyatta-Raila-Odinga-and-William-Ruto.jpeg
 
Ukomavu wake nini? Kuhamisha kura 10k
Ruto ni familia ya ikulu
Kenyatta ya ikulu
Odinga ana nani?
Nazungumzia umafia unaofanyika chini kwa chini mpaka kumpata Rais!
Yaani ukiwa mweupe kichwani huwezi gundua kuwa Uhuru, JK na toru ni marafiki wa kuzikana kabisa!
Hii ndiyo maana naiona siasa ni sayansi.
 
Je Rais Uhuru Kenyatta ni kweli ameshindwa? Ni kweli kabisa Rais Kenyatta alichagua upande ambao hakua na uhakika wa kushinda?
Ndiyo. Uhuru ni kilaza wa siasa, alibebwa na dynasty tu.

Ruto ndiye aliyemuingiza Uhuru kwenye ubunge kwa mara ya kwanza baada ya kuombwa kumfanyia kampeni na mzee Moi.

Ruto ndiyo aliyemuingiza Uhuru kwenye urais 2013 baada ya wote kuchomoka toka the Hague.

Lakini pia kumbuka kuna bifu la kiasili kati ya Luos na Kikuyus. Handshake na support ya Uhuru kwa Odinga (Mluo) ni Kama matusi kwa wakikuyu.

Ruto ndiye injini ya siasa kwa Sasa pale Kenya. Kipaji chake kiligunduliwa na mzee Moi mwanzoni mwa miaka ya 90.
 
Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC), jana ilimtangaza Ndugu, William Samoei Arap Ruto kuwa Rais Mteule wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Kenya. Ruto ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kenya, na amehudumu chini ya Rais Uhuru Kenyatta kwa takribani miaka 10 sasa...

Huu ni mchezo umechezwa. Akili kubwa sana imetumika. Raila kauzwa.

Hili igizo la ugomvi ilikuwa ni muhimu kwa sababu zifuatazo;

1. Serikali inayomaliza muda wake huwa haipendwi hivyo Ruto angegombea toka serikali inayomaliza muda wake asingeuzika. Hivyo ilibidi wajifanye wanagombana ili chuki dhidi ya serikali inayomaliza muda wake isimuhusu Ruto.

2. Rais kumaliza muda wake na kumuachia makamu wake ingeleta dhana ya Ufalme na wananchi wangemkataa Ruto.

3. Hata angeuzika na akashinda kiuhalali au kwa kuiba kura, kutangazwa kwake Ruto kungeleta fujo kubwa hivyo ilibidi serikali ijifanye inamuunga mkono Odinga ili akitangazwa kushindwa ionekane hapakuwa na namna.

4. Serikali inayoondoka madarakani mara nyingi inachukiwa, hivyo Kenyata kumuunga mkono Raila ni kumuhamishia lawama zake hivyo wasiompenda Kenyata na serikali yake lazima wamchukie na mgombea wake / anayemuunga mkono. A friend of my enemy is my enemy.

5. Kujifanya Uhuru na Ruto wanagombana ni kumtafutia kura za huruma kwa Ruto kwamba kasalitiwa na ananyanyaswa.

6. Uhuru kumuunga mkono Raila ni kumvuta karibu ili kumshauri vibaya na kuchota siri za kambi yake wakati wa uchaguzi.

7. Uhuru kumuunga mkono Raila ni kuonesha kuwa watoto wa viongozi wanataka kupeana madaraka so Ruto anajitokeza kama Hustler, son of no body ili kuwavuta watu wengi wa hali ya chini.

Hapa Uhuru kafaulu kumuachia jamaa yake kama walivyoahidiana.
 
Kwanza nilianza kushangaa, pamoja na Ruto kuchomolewa kura zake elfu kumi na IEBC but still jamaa alikuwa relaxed, very composed, hakulalamikia chochote.

Raila anaenda makanisani kusema yeye ndie mshindi, still Ruto yupo kimya very relaxed, anasema watu hupiga kura ila Mungu ndie huchagua mshindi.

Kwenye kutangaza matokeo, Raila haonekani.. anajitokeza Ruto na tabasamu lake kubwa kama kawaida yake.

Niliona Ruto alishaanza kujitenga na yaliyofanyika kwenye serikali ya Uhuru, kwenye kampeni zake alikuwa anamponda Uhuru mpaka kusema hakuwa jasiri, hasa Uhuru alipotaka ku step down baada ya yale machafuko ya 2007.

Lakini kama kweli kuna mchezo ulichezwa kati ya Uhuru na Ruto basi wale jamaa wawili kwangu watakuwa ni super genious, kumzunguka Raila kwa akili kubwa kiasi hicho ya kutengeneza ugomvi wa uongo kati yao to me its not an easy task.

Binafsi nachoona, Ruto ameshinda kihalali, wale vijana tuliowaona wakijitokeza kwenda kupiga kura wakiwa na mataulo viunoni, na miswaki mdomoni, ndio wameamua Ruto awe Rais wao ili awape ajira wanazotaka wakiamini Ruto ni mwenzao, aliyetokea chini kama wao - hustler.
 
Back
Top Bottom