Kenya 2022 Ruto Ameshinda, Je, ni kweli Rais Uhuru Kenyatta Ameshindwa? Au Odinga kachezewa Mchezo?

Kenya 2022 Ruto Ameshinda, Je, ni kweli Rais Uhuru Kenyatta Ameshindwa? Au Odinga kachezewa Mchezo?

Kenya 2022 General Election
Mnaofikilia kuwa RUTO na UHURU ati walikuwa na ugomvi basi mlikuwa mbali sana na uhalisia.Wale ni marafiki wakubwa na urafiki wao haukuwahi kuteteleka.Walichokuwa wanakifanya ni kumlaghai RAILA ODINGA tuuu.
Kwenye siasa watu hupenda ku-create conspiracy theories na mara nyingi huwa zinapata ma-believer na mashabiki wengi sana. Hii ni mojawapo. Uhuru katu asingeweza kucheza kamari mbaya namna hiyo kwani hakuwa anajua outcome itakuwaje hasa jinsi uchaguzi na uhesabu wa kura ulivyokuwa wa uwazi. Na zaidi ukichukuwa margin Ruto aliyoshinda nayo utajua kabisa kuwa yeyote kati yao angeweza kushinda. Niambieni kilichofanya Raila kushindwa ni watu wengi kutojitokeza kupiga kura nitaelewa.
 
Huu ni mchezo umechezwa. Akili kubwa sana imetumika. Raila kauzwa.

Hili igizo la ugomvi ilikuwa ni muhimu kwa sababu zifuatazo;

1. Serikali inayomaliza muda wake huwa haipendwi hivyo Ruto angegombea toka serikali inayomaliza muda wake asingeuzika. Hivyo ilibidi wajifanye wanagombana ili chuki dhidi ya serikali inayomaliza muda wake isimuhusu Ruto.

2. Rais kumaliza muda wake na kumuachia makamu wake ingeleta dhana ya Ufalme na wananchi wangemkataa Ruto.

3. Hata angeuzika na akashinda kiuhalali au kwa kuiba kura, kutangazwa kwake Ruto kungeleta fujo kubwa hivyo ilibidi serikali ijifanye inamuunga mkono Odinga ili akitangazwa kushindwa ionekane hapakuwa na namna.

4. Serikali inayoondoka madarakani mara nyingi inachukiwa, hivyo Kenyata kumuunga mkono Raila ni kumuhamishia lawama zake hivyo wasiompenda Kenyata na serikali yake lazima wamchukie na mgombea wake / anayemuunga mkono. A friend of my enemy is my enemy.

5. Kujifanya Uhuru na Ruto wanagombana ni kumtafutia kura za huruma kwa Ruto kwamba kasalitiwa na ananyanyaswa.

6. Uhuru kumuunga mkono Raila ni kumvuta karibu ili kumshauri vibaya na kuchota siri za kambi yake wakati wa uchaguzi.

7. Uhuru kumuunga mkono Raila ni kuonesha kuwa watoto wa viongozi wanataka kupeana madaraka so Ruto anajitokeza kama Hustler, son of no body ili kuwavuta watu wengi wa hali ya chini.

Hapa Uhuru kafaulu kumuachia jamaa yake kama walivyoahidiana.
Great
 
Back
Top Bottom