Sababu za kiroho kwanini Tanzania ya Mama Samia itakuwa yenye neema kubwa sana kwa Watanzania

Sababu za kiroho kwanini Tanzania ya Mama Samia itakuwa yenye neema kubwa sana kwa Watanzania

hupendi kufikiria.

Angekuwa vipi Rais kama Mungu asinge mchukua Magu? Hapo ndio kwenye content.
Magu si alichaguliwa na Watanzania kwa 84% ya kura kwenye uchaguzi wa mwezi October 2020.....Mungu yupi aliyemchagua......?
 
Maisha yanabadilika haraka Sana ndugu, Mungu Ni mkali kwa kweli, nmewaza kwamba mzee baba alikuwa ni njia tu ya bi mkubwa kufika hapa
 
Mama Samia alichaguliwa na Hayati JPM kuwa Mgombea Mwenza, na kisha amechaguliwa na vifungu vya sheria kuwa rais. Tusimsingizie Mungu
Unahitaji dua au maombi ww,acha kwenda kwa waganga
 
Unahitaji dua au maombi ww, acha kwenda kwa waganga
Nasadiki kwa Mungu mmoja, Muumba wa mbingu na nchi, na vitu vyote, vinavyoonekana na visivyoonekana.
Huu msemo wa kusema eti fulani amechaguliwa na Mungu, umekaa kisiasa zaidi kuliko kiimani
 
Mama Samia Hajachaguliwa na Mungu ni Takwa la Katiba...isome katiba inasemaje kuhusu Rais aliye madarakani akifa nani anashika uongozi wa nchi na kwa namna gani....
hujapenda kufikiria mkuu. Mungu asingemuita Magufuli then Mama Samia asingeweza kuwa Rais leo hii. so nasisitiza Mama Samia ni chaguo la Mungu
 
Maisha yanabadilika haraka Sana ndugu,Mungu Ni mkali kwa kweli,nmewaza kwamba mzee baba alikuwa Ni njia tu ya bi mkubwa kufika hapa
very possible
 
Aboreshe maisha ya mtanzania kwa kuboresha maslahi ya wafanyakazi, aajiri, awezeshe wakulima kupata mikopo yenye masharti nafuu, wafugaji watengewe maeneo ya malisho, aimarishe ulinzi na usalama wa wananchi, ajenge usawa wa kisiasa. Mengine mbwembwe tu!
sema insha allah
 
Acha unafiki, Afrika nzima inamlilia Magufuli saivi. Mwaache yetu amalizie kazi ya Musa. Mimi naamini Magufuli ni Musa, mama Samia ndio Yoshua.
Africa nzima wanamlilia? Hebu otea je Mimi ni mzungu, Mhindi, mwarabu au nani?
 
Nikubaliane na wewe mleta mada ya kwamba Kuna kilicho juu ya kila kitu ambacho huamua yote.
Na haya yalio tutokea sio kwa nasibu.
Hivyo Basi aina hii ya uongozi ilioingia leo haita tuacha Kama ilivyotukuta.

Mungu amjalie pumziko la milele ndugu magufuli.

Mama Samia japo sio imani yako lakini naamini Mama Maria mama wa Kristo aliewekwa kua mwombezi wa taifa hili na Alie mwombezi wetu sore atakuombea kwake Bwana wetu Kristo nawe hautatindikiwa na kitu katika utawala wako.
ameeeen
 
SABABU NAMBA MOJA: Mama Samia Suluhu Hassan ni CHAGUO LA MUNGU moja kwa moja. Kwa lugha nyingine Mama Samia amechaguliwa na Mungu moja kwa moja kuwa Rais wa nchi hii. Namaanisha hivi urais wa Mama Samia is a result of a Divine/ Heavenly Decree. Mungu mwenyewe ndio ameamua kumuita Magufuli na in his stead akamsimika Mama Samia Suluhu Hassan kuongoza Taifa hili la Tanzania.

URAIS WA MAMA SAMIA SULUHU HASSAN IS A PURELY ACT OF GOD. ( VIS MAJOR ) Hajachaguliwa na mtu wala timu wala hajaiba kura wala hajafanya chochote isipokuwa Mungu mwenyewe kwa sababu anazozijua mwenyewe ( ambazo obviously lazima ziwe sababu sahihi na bora to the interest of all the people of Tanzania bila kujali dini zao vyamavyao makabila yao au rangi zao ) ameamua kumchagua Mama Samia Suluhu Hassan.

Hakika tangu tupate uhuru Mama Samia ndio Rais wa kwanza ambae amechaguliwa kuongoza taifa hili na Mungu mwenyewe moja kwa moja. Nyerere aliteuliwa na chama chake,Mzee Mwinyi aliteuliwa na chama chake, Mzee Mkapaalichaguliwa kwa kupigiwa kura na watanzania kama ilivyo kuwa kwa Kikwtete na Magufuli lakini Mama Samia amechaguliwa na Mungu mwenyewe kwa hiyo Watanzania tutarajie neema kubwa sana chini ya uongozi wa mama Samia kwa sababu Mama Samia amechaguliwa na Mungu moja kwa moja kwa moja na kazi ya Mungu haina makosa.

Kwa wale watanzania ambao walipo teza haki zao katika kipindi cha miaka mitano nawaambia FURAHINI KATIKA BWANA NASEMA TENA FURAHINI SANA ( WAFILIPI 4: 4-7 ) kwa sababu HII NI SIKU AMBAYO BWANA AMEIFANYA ( ZABURI 118: 24 ) Mungu anakwenda kuirudisha miaka hiyo mitano ambayo imeliwa na nzige ( YOELI 2:25-27)

kwa wasio amini katika Mungu kama Kiranga bila shaka mnaamini katika "nature" sasa itoshe kusema kwamba MAMA SAMIA SULUHU HASSAN HAS BEEN NATURALLY SELECTED TO BE THE PRESIDENT OF THIS BELOVED NATION BY MOTHER NATURE HERSELF. Nature ndio imeamua Magufuli arejee katika kwayo na nafasi yake iwe replaced by Mama Samia SULUHU HASSAN.

SABABU NAMBA MBILI : IN THE REALM OF THE SPIRIT " WOMEN ARE A PORTAL WHICH CONNECT THE HEAVEN TO THE EARTH ". Katika ulimwengu wa rohoni MWANAMKE NI LANGO LINALO TUMIKA KUUNGANISHA KATI YA MBINGU NA DUNIA. Mfano wake ni huu wewe binadamu roho yako imetoka kwa Mungu mbinguni, ili uje hapa duniani lazima upitie kwenye tumbo la mwanamke.

Hapo mwanamke ametumika kama lango.

Hata wakristo wanao amini katika Uungu wa Kristo wanajua kwamba KRISTO ( AMBAE NI NAFSI YA PILI YA MUNGU ILIYO ISHI MBINGUNI ) alikuja duniani kupitia mwanamke.( MAMA MARIA ) Mama MARIA alitumika kama lango la kuinganisha mbingu (KRISTO ) na dunia.

Mungu akitaKA kuleta mbingu duniani hufanya hivyo kupitia mwanamke. Believe my words Mungu anaenda kuileta MBINGU (NEEMA) nchini Tanzania kupitia MAMA SAMIA SULUHU HASSAN. MUNGU MWENYEWE ANAENDA KULIONGOZA TAIFA LA TANZANIA KUPITIA MAMA SAMIA. MAMA SAMIA AMETUMIKA KAMA LANGO AMBALO MUNGU MWENYEWE ANALITUMIA KUDHIHIRISHA MAPENZI NA MIPANGO YAKE JUU YA TAIFA LA TANZANIA

MUNGU IBARIKI TANZANIA

MUNGU MBARIKI RAIS WETU MAMA SAMIA SULUHU HASSAN AMBAE WEWE MWENYEWE UME MCHAGUA KULIONGOZA TAIFA LAKO HILI LILILO BARIKIWA KULIKO MATAIFA YOTE DUNIANI
naandika nafuta,naandika nafuta ....nitarudi baadae.
 
Acha unafiki, Afrika nzima inamlilia Magufuli saivi. Mwaache yetu amalizie kazi ya Musa. Mimi naamini Magufuli ni Musa, mama Samia ndio Yoshua.
Mussa? Usitake tuandike kiusahihi mseme tunadharau msiba wenu.
 
hujapenda kufikiria mkuu. Mungu asingemuita Magufuli then Mama Samia asingeweza kuwa Rais leo hii. so nasisitiza Mama Samia ni chaguo la Mungu
.....Nafikiria tu ...kama katiba pia isingetoa "option" ya Makamu wa Rais kuapishwa kuwa Rais kumalizia kipindi cha Rais aliyekuwa madarakani kufariki...Basi Mama Samia asingekuwa Rais leo hii.....Nasisitiza Mama Samia ni kuwa Rais ni Takwa la Katiba...
 
.....Nafikiria tu ...kama katiba pia isingetoa "option" ya Makamu wa Rais kuapishwa kuwa Rais kumalizia kipindi cha Rais aliyekuwa madarakani kufariki...Basi Mama Samia asingekuwa Rais leo hii.....Nasisitiza Mama Samia ni kuwa Rais ni Takwa la Katiba...
ok
 
S

Si kweli.
Amepigiwa Kura, nae Kampeni akapiga mara zote mbili 2015 na juzi 2020.
Au yu-mwingine si yule wa kwenye Karatasi ya Kura?

Kura ilikuwa ya kuwa makamo wa Rais... lakini sasa ni Rais kamili baada ya kutokea yaliyotokea.
 
Kweli ni Mungu. sikuwahi kufikiria kingetokea kitu kama hiki, maombi yangu yenyewe yalikuwa Mungu ampe busara na hekima aliyekuwa Rais, ghafka anachukuliwa.
Mungu anafanya mambo yaliyo juu ya fahamu na fikra zetu.
hukuwah kufikiria au hukuwahi kusoma Katiba juu ya kiti Cha urais?
 
Back
Top Bottom