Sababu za ndege kumwaga mafuta angani

Sababu za ndege kumwaga mafuta angani

Du
Ndege kumwaga mafuta angani kitaalamu #FuelDump au #Jetsoning ni utaratibu wa dharura unaofanywa na rubani kutoa mafuta nje ya tanki za ndege ikiwa angani.

Mara nyingi ndege kubwa na za kati zina uwezo wa kumwaga mafuta angani kupitia tundu maalumu '#Nozel' zilizopo nyuma ya mbawa endapo itapatwa na dharura inayohitaji kutua haraka hasa pale muda mfupi baada ya kupaa.

Kwanini muda mfupi baada ya kupaa? Kwasababu mafuta yanakuwa bado ni mengi hivyo ndege kuwa na uzito mkubwa unaopitiliza mipaka ya usalama wake kwenye kutua...
Duh!! Yaan miaka yote najuaga Ni Rocket zinatoa Moshi. Asante kwa knowledge mkuu!! Kumbe Sasa Kuna umuhimu wa kufatilia vitu kitaalamu.
 
Naomba nitoke nje ya mada kidogo. Mfano ndege kutoka Dares salaam mpka china inaweza tumia lita ngapi kwa makadirio?
Tank la ndege kubwa zinzweza kujaa lita ngapi (full tank).

Kipimo cha ulaji wa mafuta kwenye ndege upoje.. Eg lita kadhaa sawa na km kadhaa!

Shukran kwa elimu
 
Khaaaaa asante mkuu Hahaha
Kumbuka usifananishe kwani umwagaji mafuta huu pia unaacha mistari ya mvuke isiyodumu nyuma inayotaka kufanana kidogo na ile hali michirizi ya wingu inayoganda na baridi (#condensation) pale ndege inakuwa kimo cha juu sana ambayo wengi huita roketi kimakosa.

Ulikuwa sahihi utotoni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo rocket ikinyenyuka mwendo wa wima haiendi haibadirishi kwenda ulalo
Nimelisema hili pia. Rocket nia yake kwenda juu, kwanini lisafiri horizontally kuja uku then ndo lipande wakati hata lilikofyatuliwa kuna anga.
Huwa linalazwa nyuzi kidogo tu hili likiripuka lisidondoke kwenye launch pad.
 
aiseee!since nimezaliwa leo ndo najua hili jambo 😂salaaalee! watu tulishazoea kusema ni rockets kumbe ni mafuta yanayo mwagwa kutoka kwenye ndege...😂😂 Shukran mkuu kwa taarifa...
Elewa wewe! Mafuta yananwagwa shortly after take off
 
I am today years old ndiyo nimejua wakati wa utotoni zile ndege tulizokua tunaita ndege za Urusi actually ni ndege zinakua zinamwaga mafuta.

This just made me hungry.
Hapana. Hizo ni condensation trails zilizoongelewa
 
Nimelisema hili pia. Rocket nia yake kwenda juu, kwanini lisafiri horizontally kuja uku then ndo lipande wakati hata lilikofyatuliwa kuna anga.
Huwa linalazwa nyuzi kidogo tu hili likiripuka lisidondoke kwenye launch pad.
Alafu kaanza kwa mbwembwe na hiyo aliyooita physics Yani kashindwa kujua rockets zinakuwa launched vertically na kudeviate degree chache tu kwa sababu ambazo Kama umezielezea aisee..
 
Hizo condensation trails tulikua tunaziona na ndege iliyokua ikifanya hivyo tulikua tunaiita ndege ya Urusi. As tulikua tunaziona zikiwa juu sana mpaka zinaonekana ndogo huku hizo trails zikionekana
Tumetoka mbali
 
Naamini kwa Sasa naweza kurusha ndege
 
Acha kutudanganya mkuu. Nimesoma topic ya physics ya advance ya rocket propulsion

Embu google hapo rocket propulsion utaelewa kitu kingine tofauti na cha mtoa mada. Hiyo topic nimeisoma advance naielewa kuliko mtoa mada. Rocket huwa zinatoa moshi mwingi nyuma kwenye mawingu ya juu yale sio mafuta.

Force of rocket = (dm/dt) X velocity
dm/dt inaendana sanjali na mafuta yanayo unguzwa na moshi unaotolewa nyuma ya rocket hivyo ndivyo speed yake huongezeka.
Ka mtoa mada make generalize kitu ambacho sio kweli.
..lakini Roketi haina mabawa mkuu! Na kama hizi tunazoona ni roketi, zingepaswa kuwa na mchirizi mmoja tu wa moshi unaotoka kwa nyuma!
Ukiona michirizi minne fahamu kuwa ni ndege ya masafu marefu yenye injini Nne, mbili kila Bawa!
Na mara nyingi moshi ule hautokani na kumwaga mafuta kwa dharura, maana ingekuwa hivyo basi usafiri wa ndege ni dharura maana kumbuka wewe mwenyewe kwenye siku moja tu ya kawaida utaona ndege ngapi zinazoacha moshi zikikata anga! Dharura?

Nimependa maelezo ya Mkuu mmoja ambayo ametoa hapo kuhusu ule moshi ambao sio moshi kwa maana halisi bali ni aina ya mvuke tu unaotokana na baridi kali iliyopo hukoo juu inayotokana na joto kali linaloachwa nyuma na injini za ndege hizo...na ametoa mfano mzuri wa wewe mwenyewe kutoka nje siku ya baridi kali na kupumua kwa kutumia mdomo, uone mvuke mweupe unaotoka mdomoni mwako!!!
 
..lakini Roketi haina mabawa mkuu! Na kama hizi tunazoona ni roketi, zingepaswa kuwa na mchirizi mmoja tu wa moshi unaotoka kwa nyuma!
Ukiona michirizi minne fahamu kuwa ni ndege ya masafu marefu yenye injini Nne, mbili kila Bawa!
Na mara nyingi moshi ule hautokani na kumwaga mafuta kwa dharura, maana ingekuwa hivyo basi usafiri wa ndege ni dharura maana kumbuka wewe mwenyewe kwenye siku moja tu ya kawaida utaona ndege ngapi zinazoacha moshi zikikata anga! Dharura?

Nimependa maelezo ya Mkuu mmoja ambayo ametoa hapo kuhusu ule moshi ambao sio moshi kwa maana halisi bali ni aina ya mvuke tu unaotokana na baridi kali iliyopo hukoo juu inayotokana na joto kali linaloachwa nyuma na injini za ndege hizo...na ametoa mfano mzuri wa wewe mwenyewe kutoka nje siku ya baridi kali na kupumua kwa kutumia mdomo, uone mvuke mweupe unaotoka mdomoni mwako!!!
Sikila Rocket ina mchirizi mmoja...Rockets za SpaceX zinaitwa Falcon zinakuwa na Booster mbili pemeni hivyo zinakuwa na michirizi mitatau.
 
Mtoa Mada Upo sahihi kabisa [emoji28]
Wale tunaoita zile Rockets ni iko hivi

Ni Reaction Kati ya HOT HUMID AIR From JET ENGINE na AIR MOLUCULES then inatengeza VAPOUR, ile VAPOUR ina condesnce ina'turn' into GAS kama Mawingu hivi na Ndio kile kinacho,onekana pale zinaitwa CONTRAILS
Na sio Rockets(Rocket Anga la Africa??)
WeWe ndio hajaeleweka kabisaa mmk

Sent from my VFD 200 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom