Sababu zipi zilimfanya Mwl.Nyerere kuiingiza nchi katika ujamaa na chama kimoja?

Sababu zipi zilimfanya Mwl.Nyerere kuiingiza nchi katika ujamaa na chama kimoja?

kaongela ujamaa, ujamaa ni commumism …
Ujamaa wa Nyerere ni socialism derived from African communalism.
Mwenyewe alifafanua vizuri tofauti ya Communism na African Socialism.
Tena alisema wazi ujamaa (socialism) ulikuwepo kabla ya kuja wakoloni hapa Africa, na ulikuwa tofauti na Communism in some aspects.
 
Ubepari ni ushenzi na matatizo mengi ya dunia hivi sasa ni matokeo ya ubepari. Laiti kama tusingefata ujamaa kipindi hicho leo hii tungeongea mengine kabisa hapa tanganyika tunaambiwa dunia imeadvance technologically lakini kuna watu wengi wanakufa na njaa why? Ni wazembe sana au?
 
Wakati tunapata uhuru nchi yetu ilikuwa nchi ya vyama vingi na uchumi wa soko huria kabla Nyerere hajabadilisha mfumo ni kutupeleka kwenye chama kimoja na ujamaa mwaka 1965 na 1967.

Ni hoja zipi Mwl Nyerere alizitumia alipofanya hayo mabadiliko makubwa hivyo ambayo yalitegemewa kuwa na hatimaye yamekuwa na matokeo mengi mchanganyiko kwa taifa hili?
Uchu wa madaraka na kujiona anaakili kuliko watu wote.
 
Ujamaa wa Nyerere ni socialism derived from African communalism.
Mwenyewe alifafanua vizuri tofauti ya Communism na African Socialism.
Tena alisema wazi ujamaa (socialism) ulikuwepo kabla ya kuja wakoloni hapa Africa, na ulikuwa tofauti na Communism in some aspects.
Communism is the highest stage of socialism
 
Kwa kweli yanahitaji maelezo ya kina.

Tukisema kutawaliwa kuna mataifa kadha wa kadha yalitawaliwa na wala hayakuona kabisa umuhimu wa kufagilia siasa za kikomunisti.

Mbaya ni kwamba licha ukomunisti kuanguka na kuvurugika duniani na yeye kung'atuka kwa nchi kumshinda bado aliendelea kuamini kuwa mawazo yake yalikuwa sahihi.

Can you imagine mfadhili wake mkubwa mchina alianza mabadiliko toka miaka ya 70 ya kujiengua zaidi huko katika uchumi akaja yule mzee Deng akazidi kufanya mabadiliko zaidi na zaidi ya kuweka mambo sawa na hawa ni wakomunisti pure kabisa waliofuata mtiririko wote wa kuusimika ukomunisti katika nchi lakini walibadilika ili kuondoa taifa katika shida kubwa lakini yeye Nyerere bado aliendelea kushikilia msimamo wake kuwa yupo sawa.

Hata alipo mteua mwinyi alimuona wa ajabu kwa kutotilia maanani misimamo yake.
Lakini hujajibu hoja hata moja iliyowasilishwa kwenye mada. Wewe unajipigia tu kivyako, pamoja na kwamba mleta mada kakusoma na 'kupenda' ulicho andika.
Hiyo China ya miaka ya 70 uliiona wapi kama siyo kuijenga kwenye mawazo yako kukidhi uliyo nayo dhidi ya Mwalimu Nyerere?
Kifupi ni kwamba uelewa ni mdogo juu ya mambo haya, lakini msukumo wa kuhoji aliyo fanya Nyerere unakusumbua na kujiachia kuonyesha ufinyu wa uelewa.
 
Mkuu katika mfumo wowote ule wa utawala lazima kuna watu watanafuaika tu na huo mfumo,
Sina uhakika kama haya masuala ya ardhi yalikuwa sababu alizozitoa Nyerere katika kuwapeleka watu kwenye ujamaa, lakini pia sheria ya ardhi ya Tanzania haijuzuia matatizo na madhila huko Ngorongoro na Loliondo kwa Wamasai na sehemu nyingine nyingi tu za utalii.
Lakini pia Tanzania inaweza kuwa ni mojawapo ya mataifa yenye kesi na migogoro mingi sana ya ardhi.
1. Ukweli kwamba katika mfumo wowote ule wa utawala kuna watu lazima watanufaika tu na huo mfumo hauzuii ukweli kwamba uongozi una wajibu wa kuweka level playing field, kusiwe na kunufaika zaidi kwa watu fulani. Hii kanuni hata mabepari wanaodogosha habari za usawa wa watu wanaielewa, ndiyo maana hata nchi za kibepari kama Marekani serikali bado ina regulate biashara na kuweka fairness.

So hii point haina mashiko.

Yani ukweli kwamba wizi upo na watu wataiba popote pale si sababu ya kukufanya ulale mlango wazi.

In fact, ukweli kwamba wizi upo popote pale ndio unatakiwa ukufanye ufunge milango zaidi kupunguza uwezekano wa kuibiwa.

2. Kanuni moja kubwa kabisa ya Ujamaa ni kuweka control ya means of productions kwa wananchi. Means of production kubwa kabisa ni ardhi. Kama huelewi hiki hujamuelewa Nyerere, hujalisoma Azimio la Arusha. Hujaelewa Ujamaa.

3. Matatizo ya ardhi ya Loliondo na Wamasai kwa kiasi kikubwa sana yamekuja baada ya Tanzania kutupilia mbali habari za Ujamaa na Azimio la Arusha. Haya ni matqtizo yqliyoanzia utawala wa Mwinyi.
 
Alikuwa hajuwi alifanyalo.
You are absolutely right. Mwalimu alisoma ujamaa bahati mbaya sana yeye na kundi lake wote na makomredi wengine bado wako hai na tunawapa heshima kubwa ila wote hawakuuelewa ujamaa kabisa hadi leo!!

Ukisoma modes of production, utaona ujamaa ni ideology inayotanguliwa na ubepari sasa logically nchi haiwezi kuwa na ujamaa bila kuwa tajiri and capitalist kwanza na kuwa na mapebari wakubwa wachache wanaomiliki viwanda, ardhi kubwa na biashara kubwa na wanaoamua mambo ya nchi nzima na kuwanyonya sana mamilioni ya watu, hivyo ujamaa huja kuwakomboa wanyonge kupitia kuwakamua matajiri kodi kubwa na kuhakikisha mishahara iko juu na wasio na ajira kupewa na serikali (manispaa) pesa ya kujikimu kila mwezi.

Ujamaa hutakiwa kuja kwenye capitalist society yenye matabaka mawili makubwa, capitalists and proletariat au workers sasa bongo kuna matabaka kibao capitalists, proletariat, peasants, machinga, small business owners, mtu kaajiriwa nayeye kaajiri shamba boy na housegirl yaani vurugu mechi, sijui huyu mzee alisoma wapi aliyoyafanya!!

Ila pia kiasili ubepari huendana na human nature of selfishness na kujilimbikizia mali na huchochea tech , entrepreneurship na uanzishwaji wa viwanda ambavyo hukua haraka kwa mtu binafsi au kampuni kupata maximum profit kupitia unyonyaji wa kutoa low wages, tofauti na ujamaa ambapo employee wengi hufanya kazi kwa mazoea tu kama wale watumishi wetu, uende kazini usiende mshahara unaingia!!

Ujamaa ni mfumo unaohitaji usawa na kuwe na tofauti ndogo ya kipato kati ya raia kitu kinachopingana na human nature kwakuwa binadamu wako tofauti wengine wavivu, wengine wachapa kazi, kuna wafanyabiashara wadogo na wakubwa , wasanii, wakulima wadogo, wachimba madini, wafanyakazi, wanaume, wanawake, wasomi, mbumbumbu, vilaza na vipanga, madada na makaka poa, wauza unga nk haiwezekani kamwe binadamu wakafanana kipato!!

Ujamaa ni ideology ya kufikirika (utopian) , isiyotekelezeka na iliojaa ubabe wa viongozi na mauaji ya wale pingapinga fc, hivyo viongozi wengi weusi huupenda ujamaa kwa kuwa wana roho za kimaskini , wengi wana roho mbaya, wote ni wababe, kuna wale malimbukeni na washamba ambao wamezaliwa bush na wote kamwe hawataki na hawapendi kabisa kukosolewa wala kuachia madaraka ambayo ni matamu mno!! Mtu akiwakosoa hadharani lazima wammalize!! Utasikia tu katekwa kaokotwa mabwepande!!

Ni wakati muafaka sasa mashuleni ujamaa ufutwe kwa kuendeleza ujinga na umaskini na akili ya kuajiriwa na badala yake kufundishwe ubepari ambao huchochea self determination, entrepreneurship, investments, tech and industrialization.


Huwezi kuwa na uzalendo huku wewe ni maskini, kwasababu kiasili binadamu ni selfish animal, lazima utaiba tu mali ya umma, ila huwezi kujiibia kwenye mali binafsi, natamani sana mitaala ifute ujamaa ni ujinga mtupu and waste of resources, wazungu wanatudharau sana kufundishana ujinga huu.

Ni ajabu sana ya mtu mweusi baba kaenda ila bado wanaogopa hadi kivuli chake badala ya kufutilia mbali mawazo yake yasiyo na faida katika dunia iliyopo sasa!!
 
Sio Tanganyika tu baada ya kupata uhuru (late 1950s - 1970s) nchi nyingi za Afrika ziliadopt African socialism ideology but in different models

Hizi ni sababu kadhaa ziliwafanya waadopt socialism iliyopelekea mfumo wa chama kimoja:

●Waliamini wakiwa chini ya mfumo wa chama kimoja watakuwa na umoja na mshikamano kwa sababu taifa zima lingekuwa chini ya single ideology. Msemo kama Zidumu fikira za Mwalimu ulitumika sana


●Kuepusha upinzani kutoka vyama vingine vya kisiasa. Hapa waliamini kukiwa na upinzani maendeleo ya taifa yatakuwa hatarini na kucheleweshwa kwa sababu ya mitazamo tofauti


●Kuzuia vita vya wenyewe kwa wenyewe. Waliamini kuwa uwepo wa vyama vingi ingepelekea kila chama kupambana kiingie madarakani mwisho wa siku vita vya wenyewe kwa wenyewe


●Kuzuia ushawishi wa nchi za kibepari kwenye siasa za ndani. Walisema kwa kuwa multi party asili yake ni kutoka mataifa ya kibepari hivyo wanaweza kuweka vibaraka wao


●Uungwaji mkono kutoka nchi za ki-socialist kama USSR na China.

●Waliamini kuwa mfumo wa kibepari ni wa kinyonyaji


Ila mwishoni yakawashinda
Kongole mkuu. Tukitaka kukosoa Nyerere kuingiza nchi kwenye mfumo wa kijamaa lazima turudi kwenye mazingira ya wakati ule na sio kukosoa kwa kuangalia hali ya sasa. Ujamaa ulikua na faida na hasara kwa nchi yetu.
 
Baada ya Vita kuu ya pili ya Dunia kuisha Cold War ikaanza kukawa na Kambi mbili na sisi kama Tanzania tulipata UHURU kipindi hicho cha Cold War.
 
Wakati tunapata uhuru nchi yetu ilikuwa nchi ya vyama vingi na uchumi wa soko huria kabla Nyerere hajabadilisha mfumo ni kutupeleka kwenye chama kimoja na ujamaa mwaka 1965 na 1967.

Ni hoja zipi Mwl Nyerere alizitumia alipofanya hayo mabadiliko makubwa hivyo ambayo yalitegemewa kuwa na hatimaye yamekuwa na matokeo mengi mchanganyiko kwa taifa hili?
Ni mada inayojadilika, ingawaje imewekwa kama chambo tu.

TANU wakati ule wa uhuru ilipata uungwaji mkono mkubwa sana toka kwa wananchi kuliko chama kingine chochote, hata vile vyama vilivyokuwa vikiungwa mkono na wakoloni.
Baada ya uhuru, uungwaji mkono wa TANU ulizidi kuimarika zaidi, hasa pale Mwalimu Nyerere alipo achia u-waziri mkuu na kwenda kukijenga chama.
Kwa hiyo TANU wakati ule haikuwa imeji-'impose' kwa wananchi. Chama kilipendwa na wananchi. Hili ni muhimu kuanza nalo kuondoa upotoshaji unaofanywa kwa maksudi kwa sababu zisizokuwa na maana.
Kuhusu kufutwa kwa vyama vingine vya upinzani; hili swali tunaweza kumuuliza karibu kilakiongozi wa Afrika wa wakati huo, siyo kazi aliyoibuni Mwalimu Nyerere. Ninayo maelezo ya hili, lakini nitaliachaa lilivyo.

"Uchumi wa soko huria", ulikuwa ni uchumi wa nani; nina maana ya nani aliyekuwa akifaidika zaidi na uchumi huo?

Huu uchumi huria unaozungumziwa, hasa maana yake ni nini? Pamba ikilimwa na mkulima Tanzania akauza kwa wakala katika eneo lake na kuendelea katika mnyororo wote hadi huko kwenye soko la wakubwa, "uhuria" wake upo wapi kwa huyo mkulima? Tunaposoma nadharia hizi katika vitabu, na tukaimbishwa nyimbo zake na hao hao wanaoendeleza ukandamizaji wetu; kwa nini tukose akili hta za kudadisi?

Tulikuwa tukitegemea sana mazao ya aina ile ile, kama pamba, mkonge, kahawa, 'pyrethrum, , na nini tena?Huko duniani kwenye "soko huria" ambako sisi hatukuwa na sauti yoyote ile, tungefanya nini ili tuendelee kupata manufaa ya kazi zetu hapa? Mkonge, mJapan kagundua nylon, zao bei ikabuma. Hivyo hivyo na pamba. Kahawa Brazil kateka soko,n.k., n.k,; leo hii tunakuja tunarudia nyimbo zile zile za ujamaa kuvunja "soko huria"!

Sasa leo tunapokuja hapa na kuhoji "Ni hoja zipi Mwalimu Nyerere alizitumia kuleta mabadiliko haya...", ni kana kwamba hali yetu ilikuwa inakwenda vizuri sana, hadi hapo Mwalimu alipoleta hoja zake!
Ni nchi zipi Afrika, (actually siyo Afrika pekee), ambazo zilibadili mifumo ya kiuchumi, hata kama siyo kama huo "Ujamaa" wa Nyerere tunaouongelea leo. Ni nchi zipi hazikuunda Mashirika ya Umma?
Sasa hata huko kwa wakubwa, wote walishikilia huo "uchumi huria" kwa sura ile ile iliyotumika katika kila nchi. Kulikuwa na "mwongozo (Blue Print) ya kwamba uchumi huria ni lazima ufanyike katika njia moja hii?

Ndiyo: hata katika yaliyofanyika hapa kwetu katika huo ujamaa hayakuwa 'perfect', na hapakuwa na shinikizo kwamba hakuna kinachoweza kubadilishwa kufuatana na hali iliyopo ili kupata ufanisi mkubwa kwa manufaa ya waTanzania (wote); na hakuna popote palipokatazwa kwa mtu kufanya bidii za ziada kwa manufa zaidi kwake.

Huo mfano wa China sasa watu wanauvungavunga tu kukidhi matakwa yao. China hadi leo ni nchi ya kikomunist. Kuwa na "soko huria" haina maana ya kuondoa lengo la watu kunufaika na uchumi wa nchi yao.
 
Ni mada inayojadilika, ingawaje imewekwa kama chambo tu.

TANU wakati ule wa uhuru ilipata uungwaji mkono mkubwa sana toka kwa wananchi kuliko chama kingine chochote, hata vile vyama vilivyokuwa vikiungwa mkono na wakoloni.
Baada ya uhuru, uungwaji mkono wa TANU ulizidi kuimarika zaidi, hasa pale Mwalimu Nyerere alipo achia u-waziri mkuu na kwenda kukijenga chama.
Kwa hiyo TANU wakati ule haikuwa imeji-'impose' kwa wananchi. Chama kilipendwa na wananchi. Hili ni muhimu kuanza nalo kuondoa upotoshaji unaofanywa kwa maksudi kwa sababu zisizokuwa na maana.
Kuhusu kufutwa kwa vyama vingine vya upinzani; hili swali tunaweza kumuuliza karibu kilakiongozi wa Afrika wa wakati huo, siyo kazi aliyoibuni Mwalimu Nyerere. Ninayo maelezo ya hili, lakini nitaliachaa lilivyo.

"Uchumi wa soko huria", ulikuwa ni uchumi wa nani; nina maana ya nani aliyekuwa akifaidika zaidi na uchumi huo?

Huu uchumi huria unaozungumziwa, hasa maana yake ni nini? Pamba ikilimwa na mkulima Tanzania akauza kwa wakala katika eneo lake na kuendelea katika mnyororo wote hadi huko kwenye soko la wakubwa, "uhuria" wake upo wapi kwa huyo mkulima? Tunaposoma nadharia hizi katika vitabu, na tukaimbishwa nyimbo zake na hao hao wanaoendeleza ukandamizaji wetu; kwa nini tukose akili hta za kudadisi?

Tulikuwa tukitegemea sana mazao ya aina ile ile, kama pamba, mkonge, kahawa, 'pyrethrum, , na nini tena?Huko duniani kwenye "soko huria" ambako sisi hatukuwa na sauti yoyote ile, tungefanya nini ili tuendelee kupata manufaa ya kazi zetu hapa? Mkonge, mJapan kagundua nylon, zao bei ikabuma. Hivyo hivyo na pamba. Kahawa Brazil kateka soko,n.k., n.k,; leo hii tunakuja tunarudia nyimbo zile zile za ujamaa kuvunja "soko huria"!

Sasa leo tunapokuja hapa na kuhoji "Ni hoja zipi Mwalimu Nyerere alizitumia kuleta mabadiliko haya...", ni kana kwamba hali yetu ilikuwa inakwenda vizuri sana, hadi hapo Mwalimu alipoleta hoja zake!
Ni nchi zipi Afrika, (actually siyo Afrika pekee), ambazo zilibadili mifumo ya kiuchumi, hata kama siyo kama huo "Ujamaa" wa Nyerere tunaouongelea leo. Ni nchi zipi hazikuunda Mashirika ya Umma?
Sasa hata huko kwa wakubwa, wote walishikilia huo "uchumi huria" kwa sura ile ile iliyotumika katika kila nchi. Kulikuwa na "mwongozo (Blue Print) ya kwamba uchumi huria ni lazima ufanyike katika njia moja hii?

Ndiyo: hata katika yaliyofanyika hapa kwetu katika huo ujamaa hayakuwa 'perfect', na hapakuwa na shinikizo kwamba hakuna kinachoweza kubadilishwa kufuatana na hali iliyopo ili kupata ufanisi mkubwa kwa manufaa ya waTanzania (wote); na hakuna popote palipokatazwa kwa mtu kufanya bidii za ziada kwa manufa zaidi kwake.

Huo mfano wa China sasa watu wanauvungavunga tu kukidhi matakwa yao. China hadi leo ni nchi ya kikomunist. Kuwa na "soko huria" haina maana ya kuondoa lengo la watu kunufaika na uchumi wa nchi yao.
Mkuu umeuliza mengi sana kuhusu soko huria lakini huu ni mfumo rahisi sana kuuelewa na kufanya kazi tofauti na ujamaa. Uelewa wa uchumi wa soko huria umefafanuliwa vizuri sana na Adam Smith kupitia dhana ya "invisible hand"
 
2. Kanuni moja kubwa kabisa ya Ujamaa ni kuweka control ya means of productions kwa wananchi.
Na hapa ndipo tatizo kubwa linapoanzia katika ujamaa. Hii huwa inasababisha ubunifu kuwa mdogo, bidii ndogo na matumizi mabaya ya rasilimali za raia/nchi.
 
Mkuu umeuliza mengi sana kuhusu soko huria lakini huu ni mfumo rahisi sana kuuelewa na kufanya kazi tofauti na ujamaa. Uelewa wa uchumi wa soko huria umefafanuliwa vizuri sana na Adam Smith kupitia dhana ya "invisible hand"
Kitabu kilicholeta utajiri wa Ulaya na Marekani kinachoelezea capitalism kinaitwa The Wealth of Nations by Adam Smith (1776). Ni bahati mbaya sana viongozi wetu hawasomi kitabu hiki, au labda wanasoma na hawaelewi.

Kitabu kingine muhimu kusoma na kuponda ujamaa ni Stages of Economic growth by Walt Rostow, 1960.

Ukimsoma Karl Marx utagundua japo alikuwa genius, ila alitoka tabaka la watu maskini akipingana kwa hoja na matajiri (capitalists) na waafrika wakaruka na ideas zake zinazoakisi maisha ya uzunguni bila kuzielewa mf baba yetu alietujaza umaskini wa fikra na mali hadi leo!!

Nyerere aliandika vitabu vingi mf "Arusha Declaration Ten Years After" akiamini anaelezea how to implement socialism kitaalam , ila wazungu waligundua hakuelewa kabisa meaning of "socialism" na wakaamua theories zake zilizoshindwa kuleta development ziitwe "ujamaa" na wala sio "socialism" waliyoelezea wao!! This means ujamaa is not the true meaning or reflection of socialism!!
 
Na hapa ndipo tatizo kubwa linapoanzia katika ujamaa. Hii huwa inasababisha ubunifu kuwa mdogo, bidii ndogo na matumizi mabaya ya rasilimali za raia/nchi.
Hilo si tatizo la ujamaa.

Hilo ni tatizo la jamii yenye elimu ndogo na ubunifu mdogo.

Jamii ikiwa na elimu kubwa na ubunifu mkubwa, tatizo hilo halitakuwepo,
 
Mkuu umeuliza mengi sana kuhusu soko huria lakini huu ni mfumo rahisi sana kuuelewa na kufanya kazi tofauti na ujamaa. Uelewa wa uchumi wa soko huria umefafanuliwa vizuri sana na Adam Smith kupitia dhana ya "invisible hand"
HeeeeeHEEEE!
"Hizo "Invisible Hands" mbona zimejazana kila mahali mkuu 'Yoda'?
Invisible hands wakati wa Vita Baridi ulikuwa huzioni kama ulikuwa na umri wa kutosha kuzielewa?

Haya maswala tusiwe tunayachukulia kirahisi rahisi hivi.

Leo hii hata bila ya hiyo "Invisible Hand" mZimbabwe anahangaika, hata baada ya miaka kadhaa baada ya Mugabe. Akina Kaguta hapo Uganda, wamekaa na mafuta toka 2006 hadi leo, hata tone moja halijasafirishwa kuingiza pesa mGanda naye apate nafuu ya maisha!
 
Wakati tunapata uhuru nchi yetu ilikuwa nchi ya vyama vingi na uchumi wa soko huria kabla Nyerere hajabadilisha mfumo ni kutupeleka kwenye chama kimoja na ujamaa mwaka 1965 na 1967.

Ni hoja zipi Mwl Nyerere alizitumia alipofanya hayo mabadiliko makubwa hivyo ambayo yalitegemewa kuwa na hatimaye yamekuwa na matokeo mengi mchanganyiko kwa taifa hili?
Majibu yapo ukisoma THE RISE OF SOCIALISM

Pia humo ndani utajifunza the lesson learnt from Russia revolution of 1917

Utamsoma Mao ze dong na chama chake CCP

Kuna Utopia socialism na Kuna scientific socialism..

Kwenye Utopia socialism ilikua Ni ngumu Sana mkuu kufikia Marengo yao ya kusadikika 😊
 
Hiki ulicho andika hakina tofauti na hiki "Democratic People's Republic Of Korea".
Huu mfano uliutoa tokea jana au juzi, lakini nikakueleza ni mfano'superficial' kabisa unaoonyesha mtu asiyekuwa na upeo wa maswala kama haya.
Bado umo kwenye mapambano ya mifumo ya Vita Baridi, wakati dunia ilishakwenda mbele.
Usisome sana vipeperushi viavyotokea Korea Kusini kuhusu Korea Kaskazini; hivyo hivyo usichukulie Maputo ya uchafu toka Korea Kaskazini kwenda kusini ukadhanihapo ndipo dunia inapoishia.
Bado upo kwenye kasumba kubwa sana.
 
Back
Top Bottom