Sababu zipi zilimfanya Mwl.Nyerere kuiingiza nchi katika ujamaa na chama kimoja?

Sababu zipi zilimfanya Mwl.Nyerere kuiingiza nchi katika ujamaa na chama kimoja?

Ujamaa wa Nyerere ni socialism derived from African communalism.
Mwenyewe alifafanua vizuri tofauti ya Communism na African Socialism.
Tena alisema wazi ujamaa (socialism) ulikuwepo kabla ya kuja wakoloni hapa Africa, na ulikuwa tofauti na Communism in some aspects.
Very Correct.

Ila kuna wimbi la watu wanaotaka kupotosha ukweli.
==========

Ukweli ni kwamba Tanzania haijawahi kuwa nchi ya Kikomunisti.

Ujamaa sio Ukomunisti kama watu wengi humu wanavyotaka kuaminisha

Itoshe, nyakati za the so called vita baridi(cold war) kati ya Ukomunisti wa Mashariki na Mebeberu wa magharibi, hususani wakati Urusi walivyoingia Cuba(bay of pigs saga) miaka ya 60-61 hivi, nchi nyingi zilikubaliana na kuridhia kwa kutokufungamana na upande wowote ule kati ya capitalist West na Communist East, wakihofia Vita kuu ya Tatu na Vita za kuangamizana kwa kutumia Nyuklia

Kumbuka, nchi nyingi zilikuwa kwenye nyakati na wakati mgumu kiuchumi kisiasa na kijamii baada ya vita vikuu vya pili vya Dunia na hivyo hawakutaka malumbano ya kati ya Nchi ya Urusi na Marekani kuwafikia.

Kwa kifupi, hawakutaka kuchagua upande wowote ule.

Ikaundwa N.A.M Non Aligned Movement.

Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi zilizounda movement hiyo.

Yaani, baadhi za nchi za Africa, Asia na America ya Kusini wakiwa ni miongoni mwa wanachama.

☝🏿Hiyo tunaweza kusema kuwa Tanzania hatukutaka Ukomunisti.

Na hivyo basi Mwl. Nyerere pia.

Wanaopotosha Tanzania ilikuwa ni nchi ya Kikomunisti, walaaniwe na waangazwe. Hawaitakii Tanzania mema. Ni waongo na ni wapuuzi.

Haya hivyo, Nyerere alitaka tufanane fanane kisera na kama Sweden Norway etc kwa sababu walikuwa ni wa Socialist.

Tofauti ya Ujamaa wa hizi nchi za Nordic ndio huo Mwl. Nyerere akauita African Socialism.
 
Sio Tanganyika tu baada ya kupata uhuru (late 1950s - 1970s) nchi nyingi za Afrika ziliadopt African socialism ideology but in different models

Hizi ni sababu kadhaa ziliwafanya waadopt socialism iliyopelekea mfumo wa chama kimoja:

●Waliamini wakiwa chini ya mfumo wa chama kimoja watakuwa na umoja na mshikamano kwa sababu taifa zima lingekuwa chini ya single ideology. Msemo kama Zidumu fikira za Mwalimu ulitumika sana


●Kuepusha upinzani kutoka vyama vingine vya kisiasa. Hapa waliamini kukiwa na upinzani maendeleo ya taifa yatakuwa hatarini na kucheleweshwa kwa sababu ya mitazamo tofauti


●Kuzuia vita vya wenyewe kwa wenyewe. Waliamini kuwa uwepo wa vyama vingi ingepelekea kila chama kupambana kiingie madarakani mwisho wa siku vita vya wenyewe kwa wenyewe


●Kuzuia ushawishi wa nchi za kibepari kwenye siasa za ndani. Walisema kwa kuwa multi party asili yake ni kutoka mataifa ya kibepari hivyo wanaweza kuweka vibaraka wao


●Uungwaji mkono kutoka nchi za ki-socialist kama USSR na China.

●Waliamini kuwa mfumo wa kibepari ni wa kinyonyaji


Ila mwishoni yakawashinda
Ndugu yangu umemaliza kabisa! Mengine ni kuataka tu kumdharirisha Mwalimu.

Hata hao Kenya Mzee Jomo Kenyatta kwani alifanyaje?

Watanzania tupate akili sasa, kumlaumu Nyerere badala ya kwenda mbele na hawa wanaotukwamisha sasa hivi ni ujinga uliokithiri.

Wenzetu wakenya hawamlaumu kabisa mwasisi wao japo aliwapora karibia ardhi yote akaifanya yake binafsi. Wao wanapambana na waliopo na wanafanikiwa.

Sisi huku hata kina Lissu!! Huwa nashangaa sana...wamekosa ushawishi wa kuwaunganisha watanzania wanaishia kumlaumu Mwalimu.

Hivi wakati wa kudai uhuru mwalimu angekuwa bize kuwaponda kina mtemi Mirambo, Kimmweri, Mkwawa n.k angefanikiwa kweli??!!!
 
Hakuwa na hoja ya msingi. Alidai anataka kuondoa tabaka la walionacho na wasio nacho,, Nyerere kwa kweli sio mfano wa kuigwa na nchi mpaka leo haiendelei sababu ya kuiga fikra zake zote, hata mambo ya kutekana yalianza huko

Hivo basi, hakuwa na hoja ya msingi. Yeye alidhani kwa kuadopt ujamaa basi masikini hawatokuepo na aliamini ujamaa ndio msingi mzuri wa kuwabana matajiri wasiwanyonye masikini

Lakini kama ambavyo ukienda Hotelini ukaagiza kuku basi inakuja na chips. Nyerere naye alikuwa na agenda yake ya kujihakikishia absolute power kwa kupitia ujamaa. He never liked to be challenged not even by his comrades within CCM
Alipenda sifa binafsi ndiyo maana akavuruga uandishi wa vitabu vya historia sahihi ya wapigania uhuru wa Tanganyika. Pia alivuruga uendeshaji wa vyama vya ushirika na mamlaka ya serikali za mitaa na kufuta vyama vya ushirika na mamlaka ya serikali za mitaa kwa maslahi yake binafsi.

Matokeo yake ni watawala kuendelea kufuata zile zilizoitwa fikra za mwenyekiti kama kasuku.
 
timing, wakati ule wote walikuwa communist I mean, waafrika na black people, communism ilijifanya kama ni mtetea wanyonge dhidi ya ukoloni kwa hivyo waliotawaliwa wote walikuwa attracted na communism,
☝🏿 Hayo juu hayana ukweli wowote ule. Msome Vernon McKay. Mmarekani alie andika kwa mapana kuhusu historia ya Afrika na hususani, kwanini Waafrika walikataa Ukomunisti.
nchi karibia zote za Afrika, carribean mpaka India na North Afrika walijiunga communism hivyo siyo Nyerere tu,
☝🏿Hiyo nayo sio kweli. Ni kinyume chake. Nchi za Africa, Asia, Carribean ama South Amerika waliunda kile kinachoitwa Non Aligned Movements. In essence by joining N.A.M Tanzania and many countries emphasized 'Independence and refusal to align with either Capitalist West and Communist East.'

Vernon McKay aliandika kati ya vitabu vyake na research zake kwamba "Hakuna nchi ya kiafrika itakayo kubali Ukomunisti".

Itoshe kusema hata Ethiopia, nchi moja wapo zilizo taka kukumbatia Ukomunisti, walikataa Ukomunisti.. Kama hiyo haitoshi, David Lamb katika maandiko yake "The Africans " observes, "No Doctrine, in fact, is more in conflict with the inherent character of Africa than Communism"

  • Africans are Capitalistic-kitu ambcho nimekuwa nikisema hapa mara nyingi.
  • Africans are Historically Democratic- Ukweli usiopingika mpaka pale wazungu walivyokuja kutuvuruga.
  • Africans are Individualistic
  • Africans simply do not work or produce when they are not rewarded with economic incentives-Je kuna mzungu asiyefanya hivyo? au binadamu yeyote yule?

uislamu wote au niseme nchi za kiislamu kuanzia irak, iran, syria mpaka palestina walifwata communism
☝🏿Hayo ni matango pori. Na ni propaganda za Wamarekani tu.
ndiyo maana kulikuwa na wimbi la black amerika converting to islam, kwa kifupi communism
😲😮😌
🤔 Umeyatoa wapi hayo?
iliwadanganya watu kwamba ni njia ya haki ya kujitawala.
Waafrika tulikuwa tukijitawala. Wazungu ndio walioharibu mifumo yetu. Niulize. Unarokota wapi hayo uliyoyaandika?
communism looks very good in paper lkn wengi hawajui kwamba communism ni satanic na wanaofund communism ndio hao hao wanaofund capitalism …
😮😅

Kwa kifupi ulitaka kupotosha na Propaganda.
 
Nyerere hakutaka ushauri na zile safari zake za awali kwenda china na nchi za communist ndio zilimpa nguvu kujiona yupo sahihi.

Miongoni mwa mambo mengi Nyerere alificha moja wapo ni kuunganisha zenji na Tanganyika , yeye alisema ni ishu ya kiusalama ila hoja hii ni dhaifu sana . jamaa kwa kweli alificha mengi mpaka akaona nchi inaenda kushoto akang'atuka .
Hadi leo sielewi kwann alituunganisha na zanzibar
 
Wakati tunapata uhuru nchi yetu ilikuwa nchi ya vyama vingi na uchumi wa soko huria kabla Nyerere hajabadilisha mfumo ni kutupeleka kwenye chama kimoja na ujamaa mwaka 1965 na 1967.

Ni hoja zipi Mwl Nyerere alizitumia alipofanya hayo mabadiliko makubwa hivyo ambayo yalitegemewa kuwa na hatimaye yamekuwa na matokeo mengi mchanganyiko kwa taifa hili?
Kama nilivyoandika juu huko, Nyerere alikuwa hajuwi alifanyalo, "socialism" ya Tanzania wakati wa Nyerere ni zao la Joan Wickens, Muingereza aliyekuwepo Ikulu kwa shinikizo la Uingereza, kuanzi kabla ya Uhuru mpaka kifo cha Nyerere.

Ukweli ni kuwa Nyerere alikuwa hajuwi alifanyalo, msione ile kujimwambafai mbele ya watu, alikuwa anaendeshwa na Waingereza na walikuwa na sababu zao, kumpa msishalisti ndiyo awe anamuongoza hapo Ikulu.
 
Back
Top Bottom