Safari ya kuusafirisha mwili wa Mtanzania Nemes Tarimo kutoka Urusi hadi Tanzania inaanza 24 Januari, 2023

Safari ya kuusafirisha mwili wa Mtanzania Nemes Tarimo kutoka Urusi hadi Tanzania inaanza 24 Januari, 2023

Hizo ni akili zako za kufikirika lakini uhalisia ni kwamba huwa wanapelekwa front line bila mafunzo yeyote mfano mzuri na wale mobilizations
Huyu kijana si nafikiri km nlivuosoma mahali alikutwa na kesi ya ngada, ilipokuja suala la vita wakamwambia ajoin jeshi Lao watamsaidia kupunguza kifungo chake gerezani
 
Mwili wako sahv uko transit, uturuki

Safari yake ya kuja bongo....

Ukifika utaenda kuzikwa tukuyu,mbeya

Ova
 
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Familia ya Mtanzania Nemes Raymond Tarimo (34) ambaye alifariki wakati akipigana upande wa Jeshi binafsi la Urusi la Wagner Group dhidi ya Ukraine, zinaeleza kuwa safari ya kuurejesha mwili wake Nchini Tanzania inatarajiwa kuanza kesho Jumanne Januari 24, 2023.

Muda wa kuwasili Tanzania bado haujawekwa wazi lakini taratibu za kuupokea zimeshafanyika ambapo ndugu, jamaa na marafiki wanasubiri ratiba kamili juu ya muda wa kuwasili kutoka Urusi.


Pia soma: Tarimo Nemes, anayedaiwa alifariki akiwa vitani Ukraine, aligombea Ubunge

Mtanzania Tarimo Nemes Raymond, afariki akiwapigania Wagner wa Urusi, kule Ukraine
Rest in peace
 
Alikuwa well trained na kupitia mafunzo ya vyuo mbalimbali vya kijeshi hata south africa so usimchukulie poa
Acha kudanganya wewe hakuwa na mafunzo yoyote labda aliyopewa na Wagner!!
 
Kuna wengine tupo huku mboni hawatuoni au mpaka tuwafuate uko uko kwenda kuwapigania si waje watuchukue huku tunaotaka kufa twende tukafe uko, Wagner mje mtuchukue na huku
Kama unataka wakuchukue ukawe Chambo wewe nenda urusi kafanye kosa wakufunge gerezani hapo sasa utawaona Wagner wanakuja kuchukua mzigo wao!!
 
Kama unataka wakuchukue ukawe Chambo wewe nenda urusi kafanye kosa wakufunge gerezani hapo sasa utawaona Wagner wanakuja kuchukua mzigo wao!!
Waweke tawi na huku basi km ni hivyo maana huku si ubalozi wao au?!
 
Hakuna cha kutengua ukweli ndio huo!! Vitani huwezi kwenda tu kwa sababu umejisikia.

Huyo alikuwa mateka vikozi vya wiki mbili au miezi 6 sio kamili bado kuna siraha za aina mbali mbali kupata kufunzwa na majaribio yake unategemea atachomoka kwa mwanajeshi mwenye zaidi ya mwaka ktk uwanja wa vita?
 
Huyo ni mpambanaji na historia imeandikwa, hapa wanaoponda wengi wetu tunapata viazi nyumbani kwetu
Mpambanaji aliyeipigania nchi nyingine iliyomfunga!! Bora hata angeifia nchi yake Tanzania!!
 
Jamaa ana spirit kama ya wa West Africa. Alijua akifanikiwa akitoboa ndo basi mpunga wake angeish vizuri siku zake zilizobaki duniani sema ndo hvyo imekuwa bahati mbya. Alikufa kijeshi Na ndo maana wamemuaga kijeshi.
Hajafa kizembe....
Watanzania waoga sana.
Kiukweli amekufa kizembe kabisa huna mafunzo unapelekwa kupigana na wanaume hayo ndiyo matokeo yake!!
 
Back
Top Bottom