Safari ya Mwisho ya Mwanahabari Nguli wa Siasa, Marin Hassan Marine, Alianzisha Jambo TZ na Ameacha Alama ya TBC Aridhio

Safari ya Mwisho ya Mwanahabari Nguli wa Siasa, Marin Hassan Marine, Alianzisha Jambo TZ na Ameacha Alama ya TBC Aridhio

Baada ya msiba, TBC imetumiwa salaam mbalimbali za rambirambi zikiwemo kutoka kwa Rais wa JMT, Dr. John Pombe Magufuli ambaye ametoa ndege yake kuupeleka mwili wa Marin Zanzibar.

Kwa mujibu wa Yusuf Omar Chunda, Marin alianzia uandishi wa habari, katika gazeti la Al Noor, ndipo akaonyesha kupenda zaidi utangazaji, hivyo Chunda akamuombea ajira TVZ, akakubaliwa ndipo akajiunga na TVZ.
P
 
I remember his voice was exceptional, but ningependa tuwe na tabia ya kumsifia mtu akiwa hai, treatment of whichever kind apewe akishuhudia, I dont know why huwa tunawasubiri mpaka wafe ndio tuwape heshima wanazostahili.

O.T.. Nasubiri siku uende CCM nitakuheshimu zaidi, lile bandiko lako la jana ulikuwa mkweli kupitiliza, hasa kile kipengele cha tano, nilipenda ulivyofunguka, japo kuna sehemu ulituchanganyia zile zilipendwa za kuunga mkono juhudi.

Kwa mwendo huu, unaenda kuchukua nafasi ya Shonza kirahisi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Poleni sana TBC, poleni sana wanahabari.
Marine Hassan Marine was simply the best kwenye kila kazi aliyoifanya nyuma ya Camera na pengine kuja na wazo na kipindi kama ardhio.

Nimekuwa mfuatiliaji wa karibu kwenye tasnia ya habari, sio rahisi sana kupata mtu creative na mwenye upekee kama aliokuwa nao Marine Hassan Marine
 
Wanabodi,
Wale wenye nafasi, unganeni nami kupitia TBC Live kuangazia Safari ya Mwisho ya Mwanahabari Nguli wa Siasa nchini Tanzania, Mtangazaji wa TBC, Marin Hassan Marine, aliyefariki jana asubuhi kwenye hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Marin Hassan Marine ndiye aliyeanzisha kipindi cha Jambo TZ, Safari ya Dodoma, Nyumba ya Jirani na ameacha alama kubwa kabisa ya kipindi kipya cha TBC Aridhio.

Kwa hapa Dar es Salaam, Mwili wa Marin uliswaliwa Msikiti Maamur hapo jana, na kusafirishwa kwa ndege ya rais kupelekwa Zanzibar, Leo asubuhi mwili wa Marin umemaliza kuswaliwa katika msikiti wa Amaan na sasa ni safari ya kuelekea makaburi ya Mwanakwerekwe Uguja ambako ndiko kutafanyika maziko.

Andamana nami.

Paskali
dah..... jamaa katumika na chama chetu kama big G halafu hakupewa hata kanafasi ka u DAS tu, huku Gondwe ambaye hakusaidia chama kwa lolote akigewa u DC.

hii waione wanahabari wachumia tumbo (mkuu Pascal Mayalla haumo kwenye kundi hili I swear!)
 
Nikiwa TVT nilipostiwa Zanzibar hivyo nilifanya kazi na Marin akiwa TVZ na baadaye alipokuja kujoin TBC 2005 mimi tayari nilikuwa nimeisha ondoka, ila tukafanya nae mahojiano mbalimbali ndani ya Jambo Tanzania.
Maziko yamemalizika sasa ni dua ya mwisho.
P
 
Back
Top Bottom