Safari za Rais Samia nje ya nchi

Safari za Rais Samia nje ya nchi

Gharama kiasi gani? Je hizo gharama zina impact gani kwenye hili ongezeko la pato la Taifa?

View attachment 2912570
Mfano Toka Magu aingie Madarakani hakuna mwaka ambao pato la Taifa limeongezeka zaidi ya 5B usd, ila miaka 3 tu ya mama ongezeko la zaidi ya 7B kila mwaka, je hizo Extra income compare na Gharama za usafiri ni worth it?
duuuu em toa uchizi umesomea ujinga shule, kwa magu atujawahi kuwa na mfumuko kama huu wala fedha kukosa thamani unashika ten kama buku sokoni, uo uchumi unaosema ni role ya watu wachache sio watanzania, wezii samia na watu wake wana tudhulumu haki zetu
 
Tangia lini balozi akachukua nafsi ya Rais? Balozi atasaini na kujadili kila mkataba? Atakaa mezani na kufanya maamuzi kama ambayo yangefanywa na mkuu wa nchi? Basi kama ndio kusingekuwa na maana ya wakuu wa nchi kukutana sehemu yoyote ile maana kazi hiyo ingefanywa na mabalozi tu.
Hakuna maana yoyote ya wakuu wa nchi kukutana mara kwa mara.
 
Namibia si some random country, kuna uhusiano mkubwa kati ya Tanzania na Namibia, wa Namibia wamekaa sana Tanzania wakipigania uhuru.

Rais Museveni wa Uganda alihadithia jinsi alivyokaa Upanga wapigania uhuru wa SWAPO.

Samia ana kazi ya ku repair some of the damage done by Magufuli during his isolationist era.

Rais wa nchi ana kazi yenye sura ya ndani ya nchi na nje ya nchi.

Na hata kama anatakiwa apunguze safari, si busara kukata safari za mazishi kwenye nchi yenye uhusiano mzuri nasi kama Namibia.

Aliyefariki Namibia ni head of state, ni rais, si VP. Ki itifaki rais anatakiwa kuzikwa na ma rais wenzake, ukimpeleka VP ni kama umem slight.
Namibia sio nchi muhimu sana kwa Tanzania kiuchumi au kisiasa. Kama sisi tuliwasaidia kupigania uhuru Rais wao ndio anatakiwa aonekane mara kwa mara Dar es Salaam na sio kinyume chake.
 
Namibia sio nchi muhimu sana kwa Tanzania kiuchumi au kisiasa. Kama sisi tuliwasaidia kupigania uhuru Rais wao ndio anatakiwa aonekane mara kwa mara Dar es Salaam na sio kinyume chake.
Kiutamaduni na kidiplomasia kwenye kuzikana hatuendi hivyo.

Hutakiwi kusema "Msiba wa mdogo wangu si muhimu sana kwangu. Kama mimi nilisaidia kumlea, yeye ndiye anatakiwa kuja kwangu sana na si kinyume chake".

Hata kama yeye anatakiwa kuja sana kwako, hata kwenye msiba nako ushindwe kwenda?

Yani mnaweka nongwa rais kwenda kwenye msiba kweli?

How unTanzanian is that?
 
Kwenye msiba mimi sina lawama.

Na hata hizo safari nyingine zinazoweza kuwa na tija, zikifanywa vizuri, siwezi kumlaumu.

Rais hatakiwi kutapanya fedha kwa safari zisizo na tija.

Lakini pia, rais si mwali ajifungie nyumbani tu.

Unaweza kulalamika rais kafanya safari ya kutumia dola milioni moja, ukasema hizo ni pesa nyingi sana. Lakini, kama hiyo safari imeleta faida ya dola bilioni moja, then it is justified.

Kuna namna ya ku balance kusafiri na kukaa ndani.

1. Safari ziwe na cost benefit analysis nzuri. Tujue rais anaenda kufanya nini, anaenda ku represent intetests gani za kiuchumi, kisiasa, kidiplomasia.

2. Safari ziwe na uwazi. Tujue gharama, tujue sababu, tuweze kupima.

3. Safari ziwe na jumbe ndogo zinazolipiwa na serikali, zikiruhusu wajumbe wengine watakaoandamana na rais, kama wafanyabiashara walioidhinishwa, kuwa katika msafara wa rais, kwa kujilipia wenyewe gharama zote.

Mimi huwa namsema sana Magufuli, vibaya. Lakini, katika hili la tatu, Magufuli aliweza kudhibiti vizuri sana ukubwa wa jumbe za Tanzania hususan kwenye mikutano ya UN New York City.

Jumbe za Tanzania nje kabla ya Magufuli zilikuwa zinafanya kufuru.

Nakumbuka niliona ripoti moja ya TV ya New York City (local news), walifanya expose ya mabalozi wa nchi/ UN delegations za kiafrika walivyokuwa wanatanua kwenye hoteli za bei mbaya za New York City, na kufanya shoppings za kufa mtu.

Lakini, walitoa mfano mmoja mzuri wa ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri Augustine Mahiga ulivyokuwa mdogo na ulivyokaa kwenye hoteli za bei nafuu sana.

Tunaweza kufanya hizi safari kwa tija tukakataa rais kutokuwa na safari kabisa kwa upande mmoja na kusafiri sana kwa upande mwingine.

Tatizo moja naliona Tanzania tunakuwa sana watu wa "all or nothing at all".

Mtu kama Magufuli aliona tatizo la rais kusafiri sana, akatuletea tatizo lingine la rais ambaye hasafiri kabisa.
Rais kutosafiri kabisa nje ya nchi hakuna tatizo, mmojawapo wa Marais waliokuwa hawasafiri sana ni Ian Khama na Botswana iliendelea vizuri tu chini ya Utawala wake.
 
Kiutamaduni na kidiplomasia kwenye kuzikana hatuendi hivyo.

Hutakiwi kusema "Msiba wa mdogo wangu si muhimu sana kwangu. Kama mimi nilisaidia kumlea, yeye ndiye anatakiwa kuja kwangu sana na si kinyume chake".

Hata kama yeye anatakiwa kuja sana kwako, hata kwenye msiba nako ushindwe kwenda?

Yani mnaweka nongwa rais kwenda kwenye msiba kweli?

How unTanzanian is that?
Mkuu kama nchi kwa sasa inatakiwa kuangalia sana mambo yetu kwa jicho la Uchumi, kama nchi tumeshawasaidia wengi sana kwa muda mrefu, pia hata kama ni mahusiano mazuri ya diplomasia kwa gharama na faida zipi. Niliona kuna wakati watu walipiga sana kelele kuhusu Magufuli kuimarisha Mahusiano na Morocco akipuuza mgogoro wa Sahrawi!
 
Rais kutosafiri kabisa nje ya nchi hakuna tatizo, mmojawapo wa Marais waliokuwa hawasafiri sana ni Ian Khama na Botswana iliendelea vizuri tu chini ya Utawala wake.
Kwanza kabisa, kila nchi iko tofauti hivyo kufananisha Botswana na Tanzania unaweza kuwa unafanya makosa.

Pili, kitu kikifanyika Botswana haimaanishi kitu hicho ni sawa. Inawezekana walikisea na wewe unataka kugeza makosa.

Tatu, kazi ya urais ina sura ya kitaifa na kimataifa. Rais kutosafiri anaipunja nchi yake kidiplomasia. Wakuu wa nchi wenzake watakaa wajadiki mustakabali wa dunia, yeye atakuwa kajitenga kama mkoma, kajifungia kama mwali. Hiyo nchi itakuwa kichekesho.

Nne, nchi yenye umasikini ndiyo kabisa haiwezi ku afford rais kujifungia kwao. Rais ni mtangazaji wa nchi namba moja, mwana diplomasia wa kwanza wa nchi. Akijifungia kwao anaipunja n hi nafasi ya kutangazwa kwenye sehemu kubwa kabisa za dunia watu wanapofanya ma deal makubwa, nchi itakosa fursa za biashara, misaada,ushawishi katika kiweka ajenda kwenye mikutano ya kimataifa.

Tano, rais mwenyeee anatakiwa ajifunze mambo mengi sana kutika kwa wenzake wa nje, kwa kuona moja kwa moja mwenyewe akiwa huko, bika kutegemea watu wengine wanaoweza kumdanganya. Akutane na watu kuanzia raia wa kigeni, mpaka Watanzania walio nje.

Rais kujifungia nchini kwake ni ushamba wa hali ya juu, ni kuji shortchange mwenyewe.
 
Mkuu kama nchi kwa sasa inatakiwa kuangalia sana mambo yetu kwa jicho la Uchumi, kama nchi tumeshawasaidia wengi sana kwa muda mrefu, pia hata kama ni mahusiano mazuri ya diplomasia kwa gharama na faida zipi. Niliona kuna wakati watu walipiga sana kelele kuhusu Magufuli kuimarisha Mahusiano na Morocco akipuuza mgogoro wa Sahrawi!

Sasa hivi inawezekana Samia anasafiri safari zake, halafu analipizia safari alizozembea Magufuli, kufanya repair.

Namibia kuna fursa za kufanya biashara na kazi nyingi. Namibia wanatuelewa na kutuheshimu sana.

Kuna Watanzania wanapiga kazi huko. Namibia haina watu wengi hata serikali yao kusimama ilitegemea watu waende kutoka nje. Wabongo kibao wameenda huko.

Namibia ni bonge la chimbo, basi wabongo hawajalistukia tu.

Tumepita nao kwenye bonde la uvuli wa mauti la utawala wa makaburu, keo wako huru ndiyo tuutupe uhusiano huu mkubwa?

Tanzania tukipuuza mahusiano na Namibia sasa hivi tutakuwa watu wajinga sana.

Tutakuwa kama baba aliyemsomesha mtoto wake kwa shida sana, baadaye huyo mtoto alivyomaliza chuo na kupata kazi, kuweza kujitegemea, sasa Baba ndiyo aanze kumkana mtoto na kusema kuwa na huyu mtoto ni mzigo tu.

Yani Namibia tumehangaika nao wamekaa hapa Tanzania wakimbizi wanatafuta uhuru miaka kibao, leo wamepata uhuru wana uchumi tunaoweza kushirikiana nao kuujenga na kufanya biashara ndiyo tudharau mahusiano nao?

Backasswards.
 
duuuu em toa uchizi umesomea ujinga shule, kwa magu atujawahi kuwa na mfumuko kama huu wala fedha kukosa thamani unashika ten kama buku sokoni, uo uchumi unaosema ni role ya watu wachache sio watanzania, wezii samia na watu wake wana tudhulumu haki zetu
Ongea kwa data mkuu, Kikwete Alituachia sukari 1800 tu, Alivyoingia Magu cha kwanza tu Sukari ikapanda hadi 3000, na hapo Hakukuwa na chochote, tofauti na sasa ambapo mfumuko WA Bei Unaikumba dunia nzima.
 
kariakoo kwa wakimbia kodii? apo sokoni kila nikidai risiti naambiwa sio lazima kununua apa nafukuzwa maduka karibu kumi toka mwaka juzi December till leo
Na still record za Mapato zinavunjwa hapo hapo kkoo, Mapato yanakusanywa Makubwa kuliko kipindi chochote toka upate uhuru, so kama hio dalili sijui utapata dalili gani.
 
Sidhani kama Rais anajipangia safari. Ana timu ya wataalamu wabobezi; mabingwa wa nyanja zote ambao hupanga safari zake. All options, possibilities, pros and cons; advantages and disadvantages zinakuwa zimezingatiwa by the time Rais anapokuwa anaelekea airport. Take that!
Tatizo ni uadilifu wa hao wanaopanga hizo safari.
 
Mjinga mimi nina swali. Ni swali kumhusu Rais Samia [baadhi yenu ni mama yenu].

Sina takwimu wala taarifa zingine zozote za kuufuta huu ujinga wangu.

Na hata sijui niende wapi ili kuzipata takwimu na taarifa hizo.

Hivyo basi, JamiiForums ndiyo kimbilio langu nitakapo kupata baadhi ya taarifa.

Kwa namna fulani, JF imekuwa ni injini ya utafutaji wa baadhi ya taarifa.

Sasa ni hivi; huyu Rais wetu tokea achukue madaraka, ameshakaa nchini kwa hata mwezi mzima [mmoja] bila kusafiri kwenda nje ya nchi?

Nauliza hivyo kwa sababu naona kama vile kila baada ya wiki mbili hivi huwa ni lazima asafiri kwenda nje ya nchi, jambo ambalo sidhani kama lina tija sana kitaifa.

Wajuzi nijuzeni, tafadhalini sana.
Mambo ni mengi muda ni mdogo mwacheni mama afungue nchi.
 
Mjinga mimi nina swali. Ni swali kumhusu Rais Samia [baadhi yenu ni mama yenu].

Sina takwimu wala taarifa zingine zozote za kuufuta huu ujinga wangu.

Na hata sijui niende wapi ili kuzipata takwimu na taarifa hizo.

Hivyo basi, JamiiForums ndiyo kimbilio langu nitakapo kupata baadhi ya taarifa.

Kwa namna fulani, JF imekuwa ni injini ya utafutaji wa baadhi ya taarifa.

Sasa ni hivi; huyu Rais wetu tokea achukue madaraka, ameshakaa nchini kwa hata mwezi mzima [mmoja] bila kusafiri kwenda nje ya nchi?

Nauliza hivyo kwa sababu naona kama vile kila baada ya wiki mbili hivi huwa ni lazima asafiri kwenda nje ya nchi, jambo ambalo sidhani kama lina tija sana kitaifa.

Wajuzi nijuzeni, tafadhalini sana.
Huenda hadi 2025 akavunja rekodi ya Vasco da Gama wetu Jk?. Wote hawa ni waswahili wa pwani🇹🇿😭😭
 
Usiangalie gharama linapokuja suala la kukutana na viongozi wenzako bali angalia tija ya vikao na ziara hizo itakayopatikana kwa Taifa lako. Ziara za Mh Rais zimeleta matokeo chanya sana kwa Taifa letu.imeifungua nchi yetu na sasa fursa za kiuchumi zinatiririka nchini kama maji ya mafuriko.
Tunaomba orodha ya hizo furusa za kiuchumi zilizotililika kama Maji....ili tutambe Nazo Mtaani.
 
Inasemekana Rais Samia bado yupo nje ya nchi….

Akirudi kutoka huko aliko, nitashangaa sana endapo atakaa Tanzania hata kwa wiki mbili tu kabla ya kusafiri tena kwenda nje….
 
Wanajamvi salaam, samahani kuwa chkulia muda wenu,natafuta mtu binafsi,shirika, kampuni,kunidhamini/ fadhili ticketi ya ndege kwenda TOGO na kurudi Dar, mazungumzo kwa maslahi ya pande zote karibu WhatsApp +255755846814
 
Back
Top Bottom