Safari za Rais Samia nje ya nchi

duuuu em toa uchizi umesomea ujinga shule, kwa magu atujawahi kuwa na mfumuko kama huu wala fedha kukosa thamani unashika ten kama buku sokoni, uo uchumi unaosema ni role ya watu wachache sio watanzania, wezii samia na watu wake wana tudhulumu haki zetu
 
Hakuna maana yoyote ya wakuu wa nchi kukutana mara kwa mara.
 
Namibia sio nchi muhimu sana kwa Tanzania kiuchumi au kisiasa. Kama sisi tuliwasaidia kupigania uhuru Rais wao ndio anatakiwa aonekane mara kwa mara Dar es Salaam na sio kinyume chake.
 
Namibia sio nchi muhimu sana kwa Tanzania kiuchumi au kisiasa. Kama sisi tuliwasaidia kupigania uhuru Rais wao ndio anatakiwa aonekane mara kwa mara Dar es Salaam na sio kinyume chake.
Kiutamaduni na kidiplomasia kwenye kuzikana hatuendi hivyo.

Hutakiwi kusema "Msiba wa mdogo wangu si muhimu sana kwangu. Kama mimi nilisaidia kumlea, yeye ndiye anatakiwa kuja kwangu sana na si kinyume chake".

Hata kama yeye anatakiwa kuja sana kwako, hata kwenye msiba nako ushindwe kwenda?

Yani mnaweka nongwa rais kwenda kwenye msiba kweli?

How unTanzanian is that?
 
Rais kutosafiri kabisa nje ya nchi hakuna tatizo, mmojawapo wa Marais waliokuwa hawasafiri sana ni Ian Khama na Botswana iliendelea vizuri tu chini ya Utawala wake.
 
Mkuu kama nchi kwa sasa inatakiwa kuangalia sana mambo yetu kwa jicho la Uchumi, kama nchi tumeshawasaidia wengi sana kwa muda mrefu, pia hata kama ni mahusiano mazuri ya diplomasia kwa gharama na faida zipi. Niliona kuna wakati watu walipiga sana kelele kuhusu Magufuli kuimarisha Mahusiano na Morocco akipuuza mgogoro wa Sahrawi!
 
Rais kutosafiri kabisa nje ya nchi hakuna tatizo, mmojawapo wa Marais waliokuwa hawasafiri sana ni Ian Khama na Botswana iliendelea vizuri tu chini ya Utawala wake.
Kwanza kabisa, kila nchi iko tofauti hivyo kufananisha Botswana na Tanzania unaweza kuwa unafanya makosa.

Pili, kitu kikifanyika Botswana haimaanishi kitu hicho ni sawa. Inawezekana walikisea na wewe unataka kugeza makosa.

Tatu, kazi ya urais ina sura ya kitaifa na kimataifa. Rais kutosafiri anaipunja nchi yake kidiplomasia. Wakuu wa nchi wenzake watakaa wajadiki mustakabali wa dunia, yeye atakuwa kajitenga kama mkoma, kajifungia kama mwali. Hiyo nchi itakuwa kichekesho.

Nne, nchi yenye umasikini ndiyo kabisa haiwezi ku afford rais kujifungia kwao. Rais ni mtangazaji wa nchi namba moja, mwana diplomasia wa kwanza wa nchi. Akijifungia kwao anaipunja n hi nafasi ya kutangazwa kwenye sehemu kubwa kabisa za dunia watu wanapofanya ma deal makubwa, nchi itakosa fursa za biashara, misaada,ushawishi katika kiweka ajenda kwenye mikutano ya kimataifa.

Tano, rais mwenyeee anatakiwa ajifunze mambo mengi sana kutika kwa wenzake wa nje, kwa kuona moja kwa moja mwenyewe akiwa huko, bika kutegemea watu wengine wanaoweza kumdanganya. Akutane na watu kuanzia raia wa kigeni, mpaka Watanzania walio nje.

Rais kujifungia nchini kwake ni ushamba wa hali ya juu, ni kuji shortchange mwenyewe.
 

Sasa hivi inawezekana Samia anasafiri safari zake, halafu analipizia safari alizozembea Magufuli, kufanya repair.

Namibia kuna fursa za kufanya biashara na kazi nyingi. Namibia wanatuelewa na kutuheshimu sana.

Kuna Watanzania wanapiga kazi huko. Namibia haina watu wengi hata serikali yao kusimama ilitegemea watu waende kutoka nje. Wabongo kibao wameenda huko.

Namibia ni bonge la chimbo, basi wabongo hawajalistukia tu.

Tumepita nao kwenye bonde la uvuli wa mauti la utawala wa makaburu, keo wako huru ndiyo tuutupe uhusiano huu mkubwa?

Tanzania tukipuuza mahusiano na Namibia sasa hivi tutakuwa watu wajinga sana.

Tutakuwa kama baba aliyemsomesha mtoto wake kwa shida sana, baadaye huyo mtoto alivyomaliza chuo na kupata kazi, kuweza kujitegemea, sasa Baba ndiyo aanze kumkana mtoto na kusema kuwa na huyu mtoto ni mzigo tu.

Yani Namibia tumehangaika nao wamekaa hapa Tanzania wakimbizi wanatafuta uhuru miaka kibao, leo wamepata uhuru wana uchumi tunaoweza kushirikiana nao kuujenga na kufanya biashara ndiyo tudharau mahusiano nao?

Backasswards.
 
Ongea kwa data mkuu, Kikwete Alituachia sukari 1800 tu, Alivyoingia Magu cha kwanza tu Sukari ikapanda hadi 3000, na hapo Hakukuwa na chochote, tofauti na sasa ambapo mfumuko WA Bei Unaikumba dunia nzima.
 
kariakoo kwa wakimbia kodii? apo sokoni kila nikidai risiti naambiwa sio lazima kununua apa nafukuzwa maduka karibu kumi toka mwaka juzi December till leo
Na still record za Mapato zinavunjwa hapo hapo kkoo, Mapato yanakusanywa Makubwa kuliko kipindi chochote toka upate uhuru, so kama hio dalili sijui utapata dalili gani.
 
Tatizo ni uadilifu wa hao wanaopanga hizo safari.
 
Mambo ni mengi muda ni mdogo mwacheni mama afungue nchi.
 
Huenda hadi 2025 akavunja rekodi ya Vasco da Gama wetu Jk?. Wote hawa ni waswahili wa pwani🇹🇿😭😭
 
Tunaomba orodha ya hizo furusa za kiuchumi zilizotililika kama Maji....ili tutambe Nazo Mtaani.
 
Inasemekana Rais Samia bado yupo nje ya nchi….

Akirudi kutoka huko aliko, nitashangaa sana endapo atakaa Tanzania hata kwa wiki mbili tu kabla ya kusafiri tena kwenda nje….
 
Wanajamvi salaam, samahani kuwa chkulia muda wenu,natafuta mtu binafsi,shirika, kampuni,kunidhamini/ fadhili ticketi ya ndege kwenda TOGO na kurudi Dar, mazungumzo kwa maslahi ya pande zote karibu WhatsApp +255755846814
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…