Said Lugumi avunja ukimya kuhusu tuhuma za ufisadi zinazoikabili kampuni yake

Said Lugumi avunja ukimya kuhusu tuhuma za ufisadi zinazoikabili kampuni yake

Kipengele kimoja kwenye hii taarifa ya Lugumi kinasema: "Kwa mujibu wa mkataba kama kuna mgogoro katika utekelezaji wa mkataba, upande usioridhika na utekelezaji wake utatangaza mgogoro kwa Mwanasheria mkuu. Si jeshi la polisi kwa upande mmoja, wala sisi kwa upande mwingine aliyetangaza mgogoro wo wote dhidi ya mwingine, kwa mujibu wa matakwa ya mkataba". mwisho wa kunukuu.

Sasa, la kujiuliza, kama watu wawili mmeshirikiana kufanya ufisadi, nani kati yao atatangaza mgogoro kuwa utekelezaji wa mkataba ulikiukwa wakati lengo lao ni moja??!!

Cha maana wangetuambia kama walitekeleza matakwa yote ya mkataba kwa ku-supply vifaa vyote vilivyokuwa vinatakiwa, katika muda na ubora uliotakiwa.
 
Sawa Bwana Moshi SABURI, Umetoa maelezo mazuri ila mambo mengi ya msingi umekwepa kuyatolea maelezo.
 
Duhh hii ni kali ya mwaka! Kwa mujibu wa hii barua Lugumi hana mgogoro wa utekelezaji wa mkataba na Jeshi la Polisi!
 



Lugumi alisema mwenyewe kasafiri usiku kupitia airport ambayo inalindwa na wala hakukuwa na tatizo, msemaji wa kampuni anasema ni uzushi.

Kusafiri kwa mkurungezi ni maisha yake binafsi na kazi yake na wala siyo hoja inayoshindaniwa hapa.

Msemaji anataka watu wanyamaze kwa sababu eti mkataba wake ulitaka kama kuna dissatisfaction yeye ama jeshi la polisi ndio tu wana nafasi ya kuraise concern. Anasahau kwamba Jeshi la polisi na yeye walikuwa wanaogelea kwenye fedha za walipa kodi wa TAnzanai ambao ni zaidi ya polisi na lugumi. Anasahau kwamba fedha yoyote ya umma katika mikataba haiishiii kwa hao wabia tu bali ina mkono wa tatu unaowakilisha umma. Yeys Lugumi hataki!. Tanzania!!!!!!!!!!!

Anasema uzushi mtupu na uwongo wa kupuuzwa. Ni upi uzushi? Kama msemaji wa Lugumi angelikuwa hatetemiki, asingetufokea tunyamaze na kutuambia tupuuze habar zinazoashiria kuwa chanzo cha mateso na maumivu vikiwemo vifo vya ndugu zetu wengi Watanzania. Tumepoteza ndugu zetu kwa kukos ahuduma za afya, misongo ya mawazo na maisha magumu kwa ajili ya mfumo fisadi ambao lugumi anataka tuupuze.

Katika hali ya kawaida, nilitgemea Lugumi angekathibitisha kwamba hakpata tenda kwa favoritism kwa sababu ni mkwe wa aliyekuw IGP na kwamba kazi ilitangazwa kweny eTender board, alitenda na kuwashinda wenzake kihalali.

Alitakiwa athbithishe kwamba fedha alizopewa ndiyo thamani halisi ya mradi huo na kwamba billion 5 za training ya viongozi watano ama ni gharama halisi ya mafunzo hayo; au haikuw abillioni tano bali ilikuw akadhaa, ama waliokwenda mafunzo hawakuwa watano bali walikuwa atu kadhaa.

Nilitegemea msemaji wa lugumi aseme kwamba kazi hiyo ilifanyika kama mkaaba ulivyotaka na kumalizika ndani ya muda sahihi kwa gharama na kiwango sahihi na kwamba mashine hizo zilikaguliwa na kuwa ziko katika ubora unaotakiwa kabla hajalipwa fedha zote.

Kusema tu "Tulishirikiana na wabia wetu wote kama ilivyo katika kutekeleza mkataba ili utekelezeke bla bla ..... hakuna kati yetu aliyelalamika....", ni mzaha kwa Watanzania wanaoteseka sana kwa sabbu ya ufisadi. ananikumbusha na msemo wake kwamba "siyo kia jipu linatumbuliwa".

Ninaomba tu Watanzania kwa ajli y ahii scenario, tuingalie kwa mtazamo wa kupima thamani ya elimu ya Tanzania dhidi ya elimu sahihi. Awamu ya nne ilipoua elimu and kuojiondolea kabisa ufahamu juu ya maana wala faida ya kuwa na elimu bora, sijui ilikuwa inalenga kuwa na taifa la aina gani.

Lakini hii ya Lugumi ndiyo taswara sahihi na halisi ya :BRN, na taifa lililokuwa likitengenezwa na awamu yanne ambayo haijaelewa hata kukubali kwamba muda wake sasa umekwisha na hautakaa urudi tena. Good bye BRN.
 
Sijaona utetezi wa kijinga kama huu maana hawajajibu hoja. Hapa watuhumiwa ni wawili, Lugumi na Polisi. Halafu Lugumi anatuambia kuwa tulikuabaliana na mtuhumiwa mwenzangu, yeyote asiporidhika na chochote aende kwa Mwanasheria Mkuu! Upuuzi kabisa!

1) Lugumi anatakiwa ajibu tuhuma kuwa hakuwa na sifa wala uwezo wa contract aliyopewa. Athibitishe kama alikuwa na uwezo au hapana. Na kama hakuwa na uwezo, kwa nini alipewa? Ni rushwa au upendeleo wa kifamilia ndiyo uliosaidia?

2) Kazi hakuifanya, lakini kalipwa karibia hela yote kinyume cha utaratibu, kwa nini? Alitoa rushwa au watoa tenda nao walikuwa ni sehemu ya Lugumi?

Hizi ni tuhuma za wizi uliofanywa na Polisi/Mambo ya Ndani na Lugumi, halafu Lugumi anajitetea kuwa walikubaliana na mtuhumiwa mwenzake, halafu anasema amefanya ufafanuzi.

Huu ni ufafanuzi wa kueleza kuwa watuhumiwa hawa walikuwa na makubaliano fulani kwa nia ovu wakiamini wamejiwekea kinga. Hii ni sawa una mtoto umempa hela akateleze jukumu fulani, njiani anaamua kushirikiana na tapeli, wanaposhtakiwa wote, tapeli anasema tulikuwa tumefanya makubaliano na mwenzangu tukutapeli namna gani, halafu kwa kusema hivyo anaamini amejisafisha!
 
Tuhuma nzito kama izi mnazijibu kirahisi ivyo no facts wala figures.
Acheni dharau ivi mnajua mlicholipwa ni sehemu ya kodi yetu tuna wajibu wa kuhoji either moja kwa moja au kupitia bunge.
 
  • Thanks
Reactions: 911
Ni mzuri kwanza tukajua mashine hizo zilinunuliwa toka company ipi na baada ya hapo tutumie Tume kujua kama bei haijawa inlated kama Radar ya bwana vijisenti a.k.a Nyoka wa makengeza, then turudi na kutrace nani alipokea, nani alivunja utaratibu wa manunuzi, nani alisaini mkataba wa kishetani
 
Ela waliolipwa LUGUMI ni ya walipa kodi wa Tanzania nikiwemo mimi.
Habari ya kua POLISI haijalalamika haiwaondolei waTZ na wadau wengine kuufuatilia mkataba huo kama haki imetendeka au hapana.
Kwa kua ela ni ya kwetu tumewalipa lugumi wafanye kazi, basi kazi ionekane imefanyika.
Kila mtanzania anayo haki ya kuufuatilia huo mkataba.
Ela walizolipwa lugumi sio za Jeshi la Polisi ni za wananchi walipa kodi.
 
Nilitegemea kama huo ni uzushi basi watueleze
ukweli maana wao wanaujua..... hii iko so cheap kumeza...... sijui hata kama kweli imetoka Lugumi maana kwa mambo yao niliyo some na kwa ukubwa wa kampuni ya kupewa tenda kubwa kiasi hiki, nilitegemea wawe na mtaalamu wa propaganda na mwandishi makini....
 
Kuifuatilia sana Tz na mambo yanavyo endeshwa baada ya miaka 4 ukienda India kwenda kufanya check up unaweza ukangundulika una ugonjwa usiotibika! Haya mambo mim naona ni bora wamiliki wa media social network kuachana na kuandika mambo yote ya ujinga yanayohusu hii serikali!!
 
Ela waliolipwa LUGUMI ni ya walipa kodi wa Tanzania nikiwemo mimi.
Habari ya kua POLISI haijalalamika haiwaondolei waTZ na wadau wengine kuufuatilia mkataba huo kama haki imetendeka au hapana.
Kwa kua ela ni ya kwetu tumewalipa lugumi wafanye kazi, basi kazi ionekane imefanyika.
Kila mTZ anayo haki ya kuufuatilia huo mkataba.
Ela walizolipwa lugumi sio za Jeshi la Polisi ni za wananchi walipa kodi.
Mkuu jeshi linalalamikaje kama IGP aliye kuwepo
wakati wanapata kazi anaitwa Said kama Lugumi, alibadili dini baada ya kumpa mimba mtoto wa Saidi IGP na inawezekana aliitwa Saidi kufuata jina la baba mkwe (joke).... shikamoo Tz.....
 
Hivi vituo vyote vya polisi hizo AFIS zipo?
 
Kwanini nilizaliwa mtanzania?
Na hauna pa kukimbilia, si India, South Afrika, Panama au hata Marekani au Canada. Ukifanya kitu kizuri tuta ku honour hapa hapa na ukivurunda utahukumiwa hapa hapa. Wengine wanapakutokea
 
Sijaona utetezi wa kijinga kama huu maana hawajajibu hoja. Hapa watuhumiwa ni wawili, Lugumi na Polisi. Halafu Lugumi anatuambia kuwa tulikuabaliana na mtuhumiwa mwenzangu, yeyote asiporidhika na chochote aende kwa Mwanasheria Mkuu! Upuuzi kabisa!

1) Lugumi anatakiwa ajibu tuhuma kuwa hakuwa na sifa wala uwezo wa contract aliyopewa. Athibitishe kama alikuwa na uwezo au hapana. Na kama hakuwa na uwezo, kwa nini alipewa? Ni rushwa au upendeleo wa kifamilia ndiyo uliosaidia?

2) Kazi hakuifanya, lakini kalipwa karibia hela yote kinyume cha utaratibu, kwa nini? Alitoa rushwa au watoa tenda nao walikuwa ni sehemu ya Lugumi?

Hizi ni tuhuma za wizi uliofanywa na Polisi/Mambo ya Ndani na Lugumi, halafu Lugumi anajitetea kuwa walikubaliana na mtuhumiwa mwenzake, halafu anasema amefanya ufafanuzi.

Huu ni ufafanuzi wa kueleza kuwa watuhumiwa hawa walikuwa na makubaliano fulani kwa nia ovu wakiamini wamejiwekea kinga. Hii ni sawa una mtoto umempa hela akateleze jukumu fulani, njiani anaamua kushirikiana na tapeli, wanaposhtakiwa wote, tapeli anasema tulikuwa tumefanya makubaliano na mwenzangu tukutapeli namna gani, halafu kwa kusema hivyo anaamini amejisafisha!


Hii ndiyo taswira ya taifa liliokuwa likijengwa kwa kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya. Ndiyo rangi halisi ya elimu ya kina Kawambwa, mulugo na kushabikiwa na CCM ya awamu ya nne. Sitaki kuamini kama huyu jamaa alikuwa na uchovu wa kufikiri na kuona ni afadhali taifa leot liwe la majuha na ama liongozwe kwa ujuha ili majuha wasifahamike. Sijui ilikuwa ni kwa interest ipi na maslahi ya nani hasa.

Hii ndiyo sura halisi wa watu waliokuwa wakiibuliwa katika awamu wa BRN!.
 
hapa watu tunaambiwa tuzibe midomo yetu na tujenge nchi huku wala nchi ni wengine kabisaa hata buumu hawalijui I mean wameishia std 7 ila tu ujanja ujanja wao unawaweka mjini.then huku kijijin mnatwambia tumuulize mtendaji mapato na matumiz ya serilali yetu ya kijiji. Ebu sasa wao waonyeshe mfano waanze na mapato na matumizi ya hizo bil 37 jinsi zilivyotumika ambapo zingeweza kununua 740 john Deere tractor tena new model mpyaa kabisa ambazo zingesaidia kuinua sekta ya Kilimo nchini
 
Back
Top Bottom