Sakata la Bandari na DP World: Serikali yashtakiwa Mahakamani

Sakata la Bandari na DP World: Serikali yashtakiwa Mahakamani

Wamefanya vizuri tatizo wameenda mahakama ya ccm hii ndio shida.Ila Sa100 kwa hili DP world nimemshangaa mno mtu unawezaje kufanya kitu kama hiki. Au hakuwa na mwanasheria ambae na yeye angesema kuna vipengele havipo sawa yeye kaenda kule ni ndio ndio ndio.Ama kweli mtemi Mangungo amerudi tena Tanzania na safari hii karudi kwa jinsia tofauti
 
Mahakama gani? au unaongelea hizi Mahakama za CCM?
Rostam, myamwezi wa Tabora ameshasema Mahakama zetu za Kisutu haziaminiki; zinazoaminika ni zile za South Africa ambako ndege yetu ya Boeing inashikiliwa kwa karibuni mwaka mmoja sasa na inaweza ikapigwa mnada. Serikali ilisha mute kuhusu suala hilo la ndege yetu. Sasa tayari tumeshasaini na bunge kuridhia mkataba wa IGA wa bandari zetu zote kushitakiwa South Africa kama tutavunja hiyo IGA.
 
Wakili Msomi Alphonce Lusako akishirikiana na Wakili msomi Chengula Emmanuel pamoja na wenzao wawili wameiburuza serikali mahakamani kwa kupitisha mkataba wa ubinafsishaji wa bandari zetu bila kuzingatia maslahi ya nchi.

Washtakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi, Waziri wa Ujenzi Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi Gabriel Migire na Katibu wa Bunge Nenelwa Mwihambi.

Wote wanne wanashtakiwa kwa makosa yafuatayo;

1. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini Makataba wa kimataifa na kuupeleka bungeni kwa ajili ya kupitishwa bila kushirikisha umma na kutoa nafasi ya kutosha kwa wananchi kutoa maoni yao, kinyume na sheria ya rasilimali za taifa no.5 ya mwaka 2017 kifungu cha 11 (1) na (2).

2. Washtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kuwaongoza wabunge vibaya, kupiga kura ya ukasuku (ya kupayuka NDIOO) badala ya kura ya Mbunge mmoja mmoja kama sheria inavyotaka (Natural Wealth and Resource Contract Act) no.6 ya mwaka 2017 kifungu cha 5 na 6.

3. Mshtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kushindwa kuliongoza bunge vizuri kufanya kazi yake ya kushauri serikali na kusimamia maslahi ya umma kwenye mikataba ya kimataifa kinyume na ibara ya 63(2) na (3) ya Katiba ya nchi.

4. Mshtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai wenye vipengele vinavyovunja Katiba (ibara ya 28(3) pamoja na sheria mbalimbali za nchi.

5. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba wa "hovyo" unaozigawa rasilimali zetu za kimkakati kwa mamlaka ya nje ya nchi, kinyume na Katiba ibara ya 1, 8 na 28.

6. Kwamba Mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai una vipengele vinavyoweka rehani enzi kuu ya taifa letu (National sovereignty) na kuuza uhuru wetu, kinyume na ibara ya 1, 8 na 28 ya Katiba.

7. Kwamba Mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai haukufuata sheria ya manunuzi ya umma no.64 ya mwaka 2011 na hivyo Mkataba huo kuwa batili tangu mwanzo (null & void ab-initio).

Washtakiwa wote wameitwa Mahakamani tar.3 July 2023 kujibu tuhuma zinazowakabili. Kesi hiyo itasikilizwa na Jaji Dunstun Ndunguru na Jaji Abdi Kagomba.!

View attachment 2670319
Isijekua wanatumika ili ishu hii ije ihalalishwe!
 
Ni vizuri sasa TLS ikajiunga kwenye kesi hii kama interested party ili munyukano huu wa kisheria mahakamani uwe na nguvu kubwa hadi kieleweke. Na uendelee hadi mahakama yetu ya upeo (rufaa) na mahakama ya katiba. Hii itakuwa funzo kwa spika wetu huyu Tulia kuacha kuliburuza bunge letu kwa msimamo ya kisiasa. Spika wa bunge anapaswa kuwa neutral katika mijadala ya bunge na kuruhusu free debate ya pande zote mbili: ile inayounga mjadala wa serikali na ile inayopinga mjadala wa serikali. Huyu spika kajionesha wazi wazi kuwapinga na hata kuwazuia wasiseme wale wote wanaopinga mijadala ya serikali kama akina Mpina. Amepoka demokrasia kwenye bunge letu. Yeye kapoka kazi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG) ya kuitetea kisheria mijadala / misuada ya serikali inayofikishwa bungeni. Huyu spika ndiye amesababisha suala hili la mkataba wa IGA kufikia hatua hizi tunazozishuhudia. Kwa spika mweledi hatungalifika huku.
 
View attachment 2670932
Hatima ya uhalali wa mkataba wa makubaliano ya ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania nay a Dubai sasa kuamuriwa na Mahakama baada ya jopo la mawakili wanne kuiburuza Serikali mahakamani kupinga mkataba huo.

Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na mjadala mkali kuhusu uhalali wa mkataba huo baina ya Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na Dubai kupitia Kampuni ya Dubai Port World kuhusu uboreshaji na uendeshaji wa bandari nchini.

Juni 10, 2023, Bunge la Tanzania lilipitia azimio la kuridhia ushirikiano.

Licha ya Bunge kuridhia, mjadala umeendelea kuhusu ushirikiano huo huku Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwaeleza Watanzania kutokuwa na wasiwasi kwani Serikali haitadharau maoni, ushauri na mapendezo yatakayokuwa yametolewa.

Hata hivyo, wakati mjadala huo ukiendelea kutoka kwa makundi mbalimbali, jopo la mawakili wanne wamechukua hatuza za kisheria kwa kuufikisha mjadala huo mahakamani.

Mawakili hao, Alphonce Lusako, Emmanuel Kalikenya Changula, Raphael Japhet Ngonde na Frank John Nyalusi, wameiburuza mahakamani Serikali, kutokana na kupitisha mkataba huo kwa kile wanachodai hauzingatii maslahi ya nchi.

Kwa mujibu wa nyaraka ambazo Mwananchi limeziona kuthibitishwa na wakili Lusako leo Jumanne, Juni 27, 2023, mawakili hao wamefungua kesi hiyo Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi na Katibu wa Bunge la Tanzania.

Madai dhidi ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi pamoja na Katibu Mkuu wake wanadaiwa kusaini mkataba huo wa kimataifa na kuupeleka bungeni kwa ajili ya kupitishwa bila kushirikisha umma na kutoa nafasi ya kutosha kwa wananchi kutoa maoni yao.

Wanadaiwa kwa kufanya hivyo wamekiuka Sheria ya Rasilimali za Taifa namba.5 ya mwaka 2017, kifungu cha 11 (1) na (2).

Kwa upande wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Katibu wa Bunge madai yanayowakabili katika shauri hilo ni kuwaongoza wabunge vibaya, kupiga kura ya kuitikia kwa ujumla kwa pamoja (yaani kura ya ndio) badala ya kura ya Mbunge mmoja mmoja.

Wadai hao katika shauri hilo wanadai kuwa wadaiwa hao kuwaongoza wabunge kupiga kura ya namna hiyo ni kinyume cha Sheria.

Kwa mujibu wa hati ya wito wa kufika mahakamani, ambayo Mwananchi limeiona nakala yake, shauri hilo limepangwa kuanza kutajwa Julai 3, 2023 saa 3:00 asubuhi na Serikali (wadaiwa) wametakiwa kufika mahakamani siku hiyo bila kukosa.

Shauri hilo la maombi mchanganyiko namba 5 la mwaka 2023, limepangwa kusikilizwa na jopo la majaji watu lianoloongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru, akishirikiana na majaji Mustafa Ismail na Abd Kagomba.
Hakuna kitu hapo ni Wakili anatafuta kiki kwenye CV yake. Hakuna Mahakama onevu na oga kama Mahakama ya Tz. Mahakama inayochukuwa haki ya mbuzi inampa fisi. Ndiyo maana DPW wameistudy Mahakama ya Tz na kugundua ni tarishi na nyapara wa serikali, DPW ikaogopa na kutaka kesi zote za kimkataba ziende Afrika Kusini. Mahakama ya Tz inaendeshwa kwa akili za Pilato, Herode, Herodia na Yuda wa Iskariote.

Wakili Alphonce anapoteza muda. Mbona Wakili Wangwe ameshinda hadi Mahakama ya EAC lakini bado nchi inaendesha chaguzi ndogo za marudio za Madiwani bila kuzingatia uamuzi wa Korti hiyo ya EAC kwenye shauri la Wakili Wangwe aliyepewa haki (ushindi).

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Ni vizuri sasa TLS ikajiunga kwenye kesi hii kama interested party ili munyukano huu wa kisheria mahakamani uwe na nguvu kubwa hadi kieleweke. Na uendelee hadi mahakama yetu ya upeo (rufaa) na mahakama ya katiba. Hii itakuwa funzo kwa spika wetu huyu Tulia kuacha kuliburuza bunge letu kwa msimamo ya kisiasa. Spika wa bunge anapaswa kuwa neutral katika mijadala ya bunge na kuruhusu free debate ya pande zote mbili: ile inayounga mjadala wa serikali na ile inayopinga mjadala wa serikali. Huyu spika kajionesha wazi wazi kuwapinga na hata kuwazuia wasiseme wale wote wanaopinga mijadala ya serikali kama akina Mpina. Amepoka demokrasia kwenye bunge letu. Yeye kapoka kazi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG) ya kuitetea kisheria mijadala / misuada ya serikali inayofikishwa bungeni. Huyu spika ndiye amesababisha suala hili la mkataba wa IGA kufikia hatua hizi tunazozishuhudia. Kwa spika mweledi hatungalifika huku.
AG hana kazi, Spika anafanya kazi ya AG.
Dubai kusaini mikataba pia AG hakwenda, hatujui kama rais alichukuwa ushauri wa AG au alivaa makoti 2 ya rais na AG kama Spika alivyovaa koti 2 za Spika na AG.

Katika hali ya kawaida kabisa, AG alitakiwa hadi sasa ameishajiuzulu ili kutetea usafi na weledi (professionalism) wake.

Sijajuwa hadi sasa VP, PM, CDF wanashiriki kumpoteza mama kwa kumshauri visivyo au labda wamesondwa? Nini mchango wao kwenye abracadabra hii?

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Wakitoka huko baada ya kushindwa kesi ‘fair and square’ unajua sampuli ya aina hii itakachosema, “judge amepokea maagizo kutoka juu”.

Kama mpaka dakika kuna mtu ajaelewa majibu ya serikali huo sio mkataba rasmi wa kibiashara; awezi elewa tena.

Unapata picha kwanini ata inapotokea serious breach ya mtu kutekeleza shamba kwa miaka kadhaa, wazi serikali ipo sahihi kutaifisha; kesi ikienda arbitration wanashindwa na ndege kukamatwa.

Kwa wanasheria hawa awashindi kesi ya biashara nje ya nchi.

It’s time UDSM ianzishe business law; hakuna hao wanasheria Tanzania.

Ifundishe pia module za introduction to contract law, tort law and business law. Kwenye degree za masomo ya biashara. It’s standard mtu anaesoma masomo ya biashara na finance awe na elementary knowledge ya hayo mambo. Uelewa wa jamii kwenye hayo maswala unapwaya to say the least.
Kusoma ni jambo moja, kusaliti elimu yako na uzalendo wako ni jambo jingine.

Taratibu taratibu tutawaelewa Magufuli na Ndugai.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Ambacho hujui ni kwamba hatutegemei kushinda, bali huu ni mchakato mahsusi wa kuamsha nguvu ya UMMA! Be careful
Wafuatao waunge mkono jitihada za Wakili hawa ili tujiridhishe na uhalali wa ufunguaji wa shauri hili:-

1. Viongozi wa Dini (akina Kitima, Kilaini, Kakobe, Niwemugizi, Mwingira, Bagonza, Eliona Kimaro, Hananja, wengine ni Madeganyanga)
2. Wanahabari.
3. Wasomi Vyuo Vikuu.
4. Wapinzani.
5. Wanaharakati.
6. Wamachinga.
7. Trade Unions ambao maelfu ya wanachama wao wanapoteza kazi kwenye bandari 65 (58 za ziwa, 5 za bahari na 2 bandari kavu).

Madai yao:-
1. Mkataba huu na mingine chechefu ipigiwe kura ya maoni (referendum) kuikataa au kuikubali.

2. Wahusika wote wawajibishwe.

3. Mamlaka ya rais yapunguzwe kwa 50% kwa njia ya kuandika Katiba Mpya.

4. Rais avunje Bunge nchi iende kwenye uchaguzi, maana Bunge haliaminiki tena, Serikali haiaminiki tena, Mahakama nayo haiaminiki tena kwa kuwa inaendesha tu mashauri lakini hukumu inaandikiwa na serikali.

5. Mafao ya wafanyakazi wa bandari zote 65 wanaoachishwa ajira na mkataba huu. Vyama vya wafanyakazi DOWUTA, TRAWU, TUCTA vianze jaramba la kudai mafao bora, kikokotoo cha kueleweka kwa kuwa wao ndiyo jasho lao lilichangia asilimia kubwa 39% ya bajeti ya taifa.

6. TAKUKURU ifanyiwe marekebisho upya ya sheria iliyoiunda ili sheria mpya iifanye kuwa taasisi huru kabisaaa 100% ya uchunguzi. Kwa jinsi hii itatenda haki na itatendewa haki pia. Aidha, itakuwa na weledi kitaifa na kimataifa kiasi kwamba itaweza kushinda zabuni za uchunguzi za kimataifa kama zilivyo Scotland Yard, Federal Bureau of Investigation, Central Intelligence Agency, US Intelligence Coy, Federal Security Services, Research Analysis Wing, M16, Secret Intelligence, Canadian Security Intelligence na (SVR, FSB, FSO, GUSP za Urusi zilizochukuwa nafasi ya KGB) na kuliingizia taifa la Tz mapato pia.

NB.
Nina wasiwasi hii kesi ya Wakili Alphonce Lusako na Wakili Chengula Emmanuel ni geresha la dola kuwahadaa na kuwachanganya wananchi. Time and circumstance will prove me correct later.


Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
wangekua wameishitaki serikali nje ya Africa hapo ningewaelewa.

ila hapa hapa Mahakama yenyewe ni ya Serikali halafu unaishtaki Serikali ?

wategemee kupewa kesi za kutolipa kodi nk.

niko hapa nimekaa
 

Attachments

  • C2EE77F4-C290-4C6C-ACEF-962CEC7F4451.jpeg
    C2EE77F4-C290-4C6C-ACEF-962CEC7F4451.jpeg
    17.4 KB · Views: 4
Natamani kujitoa mhanga pale katikati ya bunge.
[emoji23]
nisepe na kijiji cha wajinga
Nasemaje.. Nasemaje...! Wa husika wote yaani na wale wamjengoni Dodoma waongeze ulinzi hadi vijijini kwako... Babu na bibi zao wawe na mabody guard.. Wasije kusema sijawaonya... 😁 😁 😁
 
Wakili Msomi Alphonce Lusako akishirikiana na Wakili msomi Chengula Emmanuel pamoja na wenzao wawili wameiburuza serikali mahakamani kwa kupitisha mkataba wa ubinafsishaji wa bandari zetu bila kuzingatia maslahi ya nchi.

Washtakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi, Waziri wa Ujenzi Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi Gabriel Migire na Katibu wa Bunge Nenelwa Mwihambi.

Wote wanne wanashtakiwa kwa makosa yafuatayo:

1. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini Makataba wa kimataifa na kuupeleka bungeni kwa ajili ya kupitishwa bila kushirikisha umma na kutoa nafasi ya kutosha kwa wananchi kutoa maoni yao, kinyume na sheria ya rasilimali za taifa no.5 ya mwaka 2017 kifungu cha 11 (1) na (2).

2. Washtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kuwaongoza wabunge vibaya, kupiga kura ya ukasuku (ya kupayuka NDIOO) badala ya kura ya Mbunge mmoja mmoja kama sheria inavyotaka (Natural Wealth and Resource Contract Act) no.6 ya mwaka 2017 kifungu cha 5 na 6.

3. Mshtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kushindwa kuliongoza bunge vizuri kufanya kazi yake ya kushauri serikali na kusimamia maslahi ya umma kwenye mikataba ya kimataifa kinyume na ibara ya 63(2) na (3) ya Katiba ya nchi.

4. Mshtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai wenye vipengele vinavyovunja Katiba (ibara ya 28(3) pamoja na sheria mbalimbali za nchi.

5. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba wa "hovyo" unaozigawa rasilimali zetu za kimkakati kwa mamlaka ya nje ya nchi, kinyume na Katiba ibara ya 1, 8 na 28.

6. Kwamba Mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai una vipengele vinavyoweka rehani enzi kuu ya taifa letu (National sovereignty) na kuuza uhuru wetu, kinyume na ibara ya 1, 8 na 28 ya Katiba.

7. Kwamba Mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai haukufuata sheria ya manunuzi ya umma no.64 ya mwaka 2011 na hivyo Mkataba huo kuwa batili tangu mwanzo (null & void ab-initio).

Washtakiwa wote wameitwa Mahakamani tar.3 July 2023 kujibu tuhuma zinazowakabili. Kesi hiyo itasikilizwa na Jaji Dunstun Ndunguru na Jaji Abdi Kagomba.!

View attachment 2670319
Safi sana
 
Fisadi Rostam alisema nendeni mahakamani

Ujue tayari mfumo wa mahakama umejuaanda kuwadhulumu watanganyika na kuwahalalisha waarabu kuuziwa nchi

Hapa ni kula sahani moja na hawa mafisadi
Kazi ipo!!
 
Wakili Msomi Alphonce Lusako akishirikiana na Wakili msomi Chengula Emmanuel pamoja na wenzao wawili wameiburuza serikali mahakamani kwa kupitisha mkataba wa ubinafsishaji wa bandari zetu bila kuzingatia maslahi ya nchi.

Washtakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi, Waziri wa Ujenzi Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi Gabriel Migire na Katibu wa Bunge Nenelwa Mwihambi.

Wote wanne wanashtakiwa kwa makosa yafuatayo:

1. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini Makataba wa kimataifa na kuupeleka bungeni kwa ajili ya kupitishwa bila kushirikisha umma na kutoa nafasi ya kutosha kwa wananchi kutoa maoni yao, kinyume na sheria ya rasilimali za taifa no.5 ya mwaka 2017 kifungu cha 11 (1) na (2).

2. Washtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kuwaongoza wabunge vibaya, kupiga kura ya ukasuku (ya kupayuka NDIOO) badala ya kura ya Mbunge mmoja mmoja kama sheria inavyotaka (Natural Wealth and Resource Contract Act) no.6 ya mwaka 2017 kifungu cha 5 na 6.

3. Mshtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kushindwa kuliongoza bunge vizuri kufanya kazi yake ya kushauri serikali na kusimamia maslahi ya umma kwenye mikataba ya kimataifa kinyume na ibara ya 63(2) na (3) ya Katiba ya nchi.

4. Mshtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai wenye vipengele vinavyovunja Katiba (ibara ya 28(3) pamoja na sheria mbalimbali za nchi.

5. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba wa "hovyo" unaozigawa rasilimali zetu za kimkakati kwa mamlaka ya nje ya nchi, kinyume na Katiba ibara ya 1, 8 na 28.

6. Kwamba Mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai una vipengele vinavyoweka rehani enzi kuu ya taifa letu (National sovereignty) na kuuza uhuru wetu, kinyume na ibara ya 1, 8 na 28 ya Katiba.

7. Kwamba Mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai haukufuata sheria ya manunuzi ya umma no.64 ya mwaka 2011 na hivyo Mkataba huo kuwa batili tangu mwanzo (null & void ab-initio).

Washtakiwa wote wameitwa Mahakamani tar.3 July 2023 kujibu tuhuma zinazowakabili. Kesi hiyo itasikilizwa na Jaji Dunstun Ndunguru na Jaji Abdi Kagomba.!

View attachment 2670319
100%
 
4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Back
Top Bottom