Sakata la Bandari na DP World: Serikali yashtakiwa Mahakamani

Sakata la Bandari na DP World: Serikali yashtakiwa Mahakamani

Wakili Msomi Alphonce Lusako akishirikiana na Wakili msomi Chengula Emmanuel pamoja na wenzao wawili wameiburuza serikali mahakamani kwa kupitisha mkataba wa ubinafsishaji wa bandari zetu bila kuzingatia maslahi ya nchi.

Washtakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi, Waziri wa Ujenzi Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi Gabriel Migire na Katibu wa Bunge Nenelwa Mwihambi.

Wote wanne wanashtakiwa kwa makosa yafuatayo;

1. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini Makataba wa kimataifa na kuupeleka bungeni kwa ajili ya kupitishwa bila kushirikisha umma na kutoa nafasi ya kutosha kwa wananchi kutoa maoni yao, kinyume na sheria ya rasilimali za taifa no.5 ya mwaka 2017 kifungu cha 11 (1) na (2).

2. Washtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kuwaongoza wabunge vibaya, kupiga kura ya ukasuku (ya kupayuka NDIOO) badala ya kura ya Mbunge mmoja mmoja kama sheria inavyotaka (Natural Wealth and Resource Contract Act) no.6 ya mwaka 2017 kifungu cha 5 na 6.

3. Mshtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kushindwa kuliongoza bunge vizuri kufanya kazi yake ya kushauri serikali na kusimamia maslahi ya umma kwenye mikataba ya kimataifa kinyume na ibara ya 63(2) na (3) ya Katiba ya nchi.

4. Mshtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai wenye vipengele vinavyovunja Katiba (ibara ya 28(3) pamoja na sheria mbalimbali za nchi.

5. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba wa "hovyo" unaozigawa rasilimali zetu za kimkakati kwa mamlaka ya nje ya nchi, kinyume na Katiba ibara ya 1, 8 na 28.

6. Kwamba Mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai una vipengele vinavyoweka rehani enzi kuu ya taifa letu (National sovereignty) na kuuza uhuru wetu, kinyume na ibara ya 1, 8 na 28 ya Katiba.

7. Kwamba Mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai haukufuata sheria ya manunuzi ya umma no.64 ya mwaka 2011 na hivyo Mkataba huo kuwa batili tangu mwanzo (null & void ab-initio).

Washtakiwa wote wameitwa Mahakamani tar.3 July 2023 kujibu tuhuma zinazowakabili. Kesi hiyo itasikilizwa na Jaji Dunstun Ndunguru na Jaji Abdi Kagomba.!

View attachment 2670319
Kwa mara ya kwanza watanzania tumefunguka! Mungu wa mbinguni tunakushuru saana! Lazima wananchi tuamke tutoke usingizini nchi ikiuzwa hatuna pa kwenda! Watoto na wajukuu zetu watakuwa watumwa. Ongera sana watanzania wazalendo kwa kufungua shauri hili na kuwaburuza kwenda kwenye mkono wa sheria na haki
 
Kwenye jambo muhimu kama hili, ninapendekeza mawakili wote wanne wanaohusika katika jambo hilo majina yao yatajwe na yapewe uzito stahiki.
Hawa ni mashujaa wa nchi, iwe wamefanikiwa au hawakufanikiwa katika juhudi zao za kuipigania Tanzania.
Hakika.
 
wewe unasubiri utajiri wako toka kwa Azizi Rostam, au Samia?

Utasubiri sana!
Wewe endelea tu kuwachukia Matajiri kwa sababu lile shetani lenu la Chato ndo lilivyowaaminisha wakifilisika nyie ndo mtatoka kwenye unyonge aliokuachieni
 
Wewe endelea tu kuwachukia Matajiri kwa sababu lile shetani lenu la Chato ndo lilivyowaaminisha wakifilisika nyie ndo mtatoka kwenye unyonge aliokuachieni
Hakuna anayewachukia matajiri hata siku moja maana katika jamii yoyote ile kama hakuna matajiri basi jamii hiyo imekufa.Utaratibu unaotumika awamu hii wa kugawa Rasilimali zetu kwa wageni huku wakisingizia maendeleo kwa kusaini mikataba mibovu ni uhaini.
 

Attachments

  • IMG-20230627-WA0003.jpg
    IMG-20230627-WA0003.jpg
    94.3 KB · Views: 3
Wewe endelea tu kuwachukia Matajiri kwa sababu lile shetani lenu la Chato ndo lilivyowaaminisha wakifilisika nyie ndo mtatoka kwenye unyonge aliokuachieni
Huu ndio ujinga, kudhani kila mtu anayepinga anapinga kwa sabau ya huyo wa Chato. Unapokuwa na akili ya namna hiyo unajionyesha upungufu mkubwa sana.

Hilo la "kuchukia matajiri" ni lako mwenyewe kwa sababu zako uzijuazo. Tajiri anayepata utajiri kwa juhudi zake mwenyewe, tena kwa haki, utaanzia wapi kumchukia mtu kama huyo?
 
Huu ndio ujinga, kudhani kila mtu anayepinga anapinga kwa sabau ya huyo wa Chato. Unapokuwa na akili ya namna hiyo unajionyesha upungufu mkubwa sana.

Hilo la "kuchukia matajiri" ni lako mwenyewe kwa sababu zako uzijuazo. Tajiri anayepata utajiri kwa juhudi zake mwenyewe, tena kwa haki, utaanzia wapi kumchukia mtu kama huyo?
Hakika.
 
Wakili Msomi Alphonce Lusako akishirikiana na Wakili msomi Chengula Emmanuel pamoja na wenzao wawili wameiburuza serikali mahakamani kwa kupitisha mkataba wa ubinafsishaji wa bandari zetu bila kuzingatia maslahi ya nchi.

Washtakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi, Waziri wa Ujenzi Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi Gabriel Migire na Katibu wa Bunge Nenelwa Mwihambi.

Wote wanne wanashtakiwa kwa makosa yafuatayo;

1. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini Makataba wa kimataifa na kuupeleka bungeni kwa ajili ya kupitishwa bila kushirikisha umma na kutoa nafasi ya kutosha kwa wananchi kutoa maoni yao, kinyume na sheria ya rasilimali za taifa no.5 ya mwaka 2017 kifungu cha 11 (1) na (2).

2. Washtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kuwaongoza wabunge vibaya, kupiga kura ya ukasuku (ya kupayuka NDIOO) badala ya kura ya Mbunge mmoja mmoja kama sheria inavyotaka (Natural Wealth and Resource Contract Act) no.6 ya mwaka 2017 kifungu cha 5 na 6.

3. Mshtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kushindwa kuliongoza bunge vizuri kufanya kazi yake ya kushauri serikali na kusimamia maslahi ya umma kwenye mikataba ya kimataifa kinyume na ibara ya 63(2) na (3) ya Katiba ya nchi.

4. Mshtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai wenye vipengele vinavyovunja Katiba (ibara ya 28(3) pamoja na sheria mbalimbali za nchi.

5. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba wa "hovyo" unaozigawa rasilimali zetu za kimkakati kwa mamlaka ya nje ya nchi, kinyume na Katiba ibara ya 1, 8 na 28.

6. Kwamba Mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai una vipengele vinavyoweka rehani enzi kuu ya taifa letu (National sovereignty) na kuuza uhuru wetu, kinyume na ibara ya 1, 8 na 28 ya Katiba.

7. Kwamba Mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai haukufuata sheria ya manunuzi ya umma no.64 ya mwaka 2011 na hivyo Mkataba huo kuwa batili tangu mwanzo (null & void ab-initio).

Washtakiwa wote wameitwa Mahakamani tar.3 July 2023 kujibu tuhuma zinazowakabili. Kesi hiyo itasikilizwa na Jaji Dunstun Ndunguru na Jaji Abdi Kagomba.!

View attachment 2670319
Wakili Msomi ndugu Lisu, ongezeka kwenye hilo jopo letu la Mawakili tukapambane nao.
 
CCM ni moja na wanaccm tuko pamoja na Samia mbebamaono ya nchi. DP world welcome and Samia hoyeeeee!
Tulia kijana,uzuri huu mziki ni baina ya CCM maslahi na CCM uzalendo,hayupo mpinzani hapo.

Acha waumane wao kwa wao
 
Back
Top Bottom