Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hao mawakili waliofungua kesi wasijekuwa ni maofisa kipenyo ili kuharibuMawakili Alfonce Lusako na Emmanuel Chengula wakishirikiana na wenzao wamefungua Kesi Mahakamani dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakipinga 'makubaliano ya mkataba' ulioingiwa baina ya Serikali hiyo na Serikali ya Dubai kupitia Kampuni ya DP World, makubaliano yanayolenga uendelezaji wa Bandari Nchini
Katika Kesi ya msingi iliyofunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya ambao washtakiwa wake ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Dkt.Eliezer Feleshi, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof.Makame Mbarawa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi) Gabriel Migire na Katibu wa Bunge Nenelwa Mwihambi,
ambapo Mawakili hao wameeleza kuwa Washtakiwa wote wanne wanakabiliwa na makosa yafuatayo:
1.) Washtakiwa namba 2 na namba 3 wanashtakiwa kwa kusaini Mkataba wa Kimataifa na kuupeleka Bungeni kwaajili ya kupitishwa bila kushirikisha Umma na kutoa nafasi ya kutosha kwa Wananchi kutoa maoni yao, kinyume na Sheria ya raslimali za taifa namba 5 ya mwaka 2017 kifungu cha 11 (1) na (2),
2.) Washtakiwa namba 1 na namba 4 wanashtakiwa kwa kuwaongoza Wabunge vibaya kupiga kura ya "NDIO" badala ya kura ya Mbunge mmoja mmoja kama Sheria inavyotaka (Natural Wealth and Reasource contract Act) namba 6 ya mwaka 2017 kifungu cha 5 na 6,
3.) Mshtakiwa namba 1 na 4 wanashtakiwa kwa kushindwa kuliongoza Bunge vizuri kufanya kazi yake ya kuishauri Serikali na kusimamia maslahi ya Umma kwenye mikataba ya kimataifa kinyume na ibara ya 63 (2) na (3) ya Katiba ya Nchi,
4.) Mshtakiwa namba 2 na 3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na 'Emirate' ya Dubai wenye vipengere vinavyovunja Katiba, Ibara ya 28 (3) pamoja na Sheria mbalimbali za Nchi,
5.) Washtakiwa namba 2 na 3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba wa 'hovyo' unaozigawa raslimali za taifa za kimkakati kwa mamlaka ya nje ya Nchi, kinyume na Katiba, Ibara ya 1, 8 na 28,
6.) Kwamba, Mkataba kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na 'Emirate' ya Dubai una vipengere vinavyoweka rehani enzi kuu ya taifa (National Sovereignty) na 'kuuza' uhuru wa Nchi, kinyume na Ibara ya 1, 8 na 28 ya Katiba, Nk
Washtakiwa wote wameitwa Mahakamani July 03.2023
Yule aliingia mitiniHv yule jamaa alifunguaga kesi dhidi ya mitandao ya smu,,, iliishia wapi?
Hapo hapo anasema mahakama haziaminikiFisadi Rostam alisema nendeni mahakamani
Ujue tayari mfumo wa mahakama umejuaanda kuwadhulumu watanganyika na kuwahalalisha waarabu kuuziwa nchi
Hapa ni kula sahani moja na hawa mafisadi
Ngoja tusubiri trh 3 siyo mbali na bahati nzuri ni siku ya kuwapeleka watoto shule kwa hiyo siyo rahisi kusahau.
Jaribu uwai kuzimuNatamani kujitoa mhanga pale katikati ya bunge.
[emoji23]
nisepe na kijiji cha wajinga
Magufuli aliwaaminisha umasikini wenu uliletwa na Matajiri ndio mana mwawachukia sana!Hata matajiri hulka yao ni kuchukia masikini
Kwenye jambo muhimu kama hili, ninapendekeza mawakili wote wanne wanaohusika katika jambo hilo majina yao yatajwe na yapewe uzito stahiki.Wakili Msomi Alphonce Lusako akishirikiana na Wakili msomi Chengula Emmanuel pamoja na wenzao wawili
wewe unasubiri utajiri wako toka kwa Azizi Rostam, au Samia?Magufuli aliwaaminisha umasikini wenu uliletwa na Matajiri ndio mana mwawachukia sana!
Wametumwa na kkanisa hao
Safi sanaWakili Msomi Alphonce Lusako akishirikiana na Wakili msomi Chengula Emmanuel pamoja na wenzao wawili wameiburuza serikali mahakamani kwa kupitisha mkataba wa ubinafsishaji wa bandari zetu bila kuzingatia maslahi ya nchi.
Washtakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi, Waziri wa Ujenzi Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi Gabriel Migire na Katibu wa Bunge Nenelwa Mwihambi.
Wote wanne wanashtakiwa kwa makosa yafuatayo;
1. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini Makataba wa kimataifa na kuupeleka bungeni kwa ajili ya kupitishwa bila kushirikisha umma na kutoa nafasi ya kutosha kwa wananchi kutoa maoni yao, kinyume na sheria ya rasilimali za taifa no.5 ya mwaka 2017 kifungu cha 11 (1) na (2).
2. Washtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kuwaongoza wabunge vibaya, kupiga kura ya ukasuku (ya kupayuka NDIOO) badala ya kura ya Mbunge mmoja mmoja kama sheria inavyotaka (Natural Wealth and Resource Contract Act) no.6 ya mwaka 2017 kifungu cha 5 na 6.
3. Mshtakiwa no.1 na no.4 wanashtakiwa kwa kushindwa kuliongoza bunge vizuri kufanya kazi yake ya kushauri serikali na kusimamia maslahi ya umma kwenye mikataba ya kimataifa kinyume na ibara ya 63(2) na (3) ya Katiba ya nchi.
4. Mshtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai wenye vipengele vinavyovunja Katiba (ibara ya 28(3) pamoja na sheria mbalimbali za nchi.
5. Washtakiwa no.2 na no.3 wanashtakiwa kwa kusaini mkataba wa "hovyo" unaozigawa rasilimali zetu za kimkakati kwa mamlaka ya nje ya nchi, kinyume na Katiba ibara ya 1, 8 na 28.
6. Kwamba Mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai una vipengele vinavyoweka rehani enzi kuu ya taifa letu (National sovereignty) na kuuza uhuru wetu, kinyume na ibara ya 1, 8 na 28 ya Katiba.
7. Kwamba Mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Emirate ya Dubai haukufuata sheria ya manunuzi ya umma no.64 ya mwaka 2011 na hivyo Mkataba huo kuwa batili tangu mwanzo (null & void ab-initio).
Washtakiwa wote wameitwa Mahakamani tar.3 July 2023 kujibu tuhuma zinazowakabili. Kesi hiyo itasikilizwa na Jaji Dunstun Ndunguru na Jaji Abdi Kagomba.!
View attachment 2670319
Mbona serikali imeshashindwa kesi nyingi tu mahakamani?Kwa mfumo uliopo, mhimili mmoja auwezi kutoa hukumu kwa mhimili mwingine zaidi ya hiyo mihimili kuungana. Mwisho wa siku, mashtaka yatatupiliwa mbali.