Sakata la DP WORLD: Rais Samia asema Serikali itatafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar, sasa kuchangia robo tatu ya bajeti ya nchi

Sakata la DP WORLD: Rais Samia asema Serikali itatafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar, sasa kuchangia robo tatu ya bajeti ya nchi

Nimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.

Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?

Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.

Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.

--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.

Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.

Kwa bandari aambiwe hapana. Kama Waarabu wamempa masharti, aachane nao.
Tuache utani. Maswala ya ubia yakishatuangusha sana.
Nilishasema hapa haya ndio matokeo ya mikopo, misaada na kijipendekeza.
 
Ni Hivi Serikali inakula Chake / Kodi
Muwekezaji anakula Chake Faida
Pesa inatoka kwa mtuamiaji i.e. Mteja

Sasa kama wateja wapo na hawajapungua na tunaongeza mtu kati ili tugawane faida unategemea ni nini kitatokea ? (Mapato kuongezeka bila kuongeza Bei)?

Je ni kwamba kama taifa tumeshindwa kuweka unangalizi na kusimamia pesa na kudhibiti wizi ili tupate faida yote ?, Au tunahitaji uwekezaji mkubwa wa mtaji ? Is this Rocket Science..., Kama tunashindwa hata hiki, Kusimamia mizigo inayoingia ambayo ni lukuki tumezungukwa na land locked countries (je tunaweza nini )?

Kwanini hao wawekezaji tusiwapeleke huko in the middle of nowhere ili waanze kuwekeza from scratch ? Yaani tuwape vitu kwenye silver platter ?
Ni kama tumelaaniwa hivi
 
Ni Hivi Serikali inakula Chake / Kodi
Muwekezaji anakula Chake Faida
Pesa inatoka kwa mtuamiaji i.e. Mteja

Sasa kama wateja wapo na hawajapungua na tunaongeza mtu kati ili tugawane faida unategemea ni nini kitatokea ? (Mapato kuongezeka bila kuongeza Bei)?

Je ni kwamba kama taifa tumeshindwa kuweka unangalizi na kusimamia pesa na kudhibiti wizi ili tupate faida yote ?, Au tunahitaji uwekezaji mkubwa wa mtaji ? Is this Rocket Science..., Kama tunashindwa hata hiki, Kusimamia mizigo inayoingia ambayo ni lukuki tumezungukwa na land locked countries (je tunaweza nini )?

Kwanini hao wawekezaji tusiwapeleke huko in the middle of nowhere ili waanze kuwekeza from scratch ? Yaani tuwape vitu kwenye silver platter ?
Ndio imeshindikana sasa,leta suluhisho.Tzn kwa wizi na uzembe ni shida sana.
 
Kwa bandari aambiwe hapana. Kama Waarabu wamempa masharti, aachane nao.
Tuache utani. Maswala ya ubia yakishatuangusha sana.
Nilishasema hapa haya ndio matokeo ya mikopo, misaada na kijipendekeza.
Rubbish, bandari kote Duniani zenye ufanisi ni private sector run.

Kwanza aambiwe na nani wakati wanaopendekeza haya ni watendaji wa Serikali.
 
Ndio imeshindikana sasa,leta suluhisho.Tzn kwa wizi na uzembe ni shida sana.
Kwahio tuna wizi na uzembe tulete Mbia ili aongeze mapato (achukue faida zaidi) na atulipe kodi ambayo huenda tulikuwa hatupati sababu ya wizi na uzembe...., Kwahio tuna guarantee gani kwamba na hio kodi haitaibiwa kwa wizi au kutofanya lolote sababu ya uzembe ?

Hapa ni kama mtu unawashwa kidole alafu unajikuna kwenye nywele.....
 
Kwahio tuna wizi na uzembe tulete Mbia ili aongeze mapato (achukue faida zaidi) na atulipe kodi ambayo huenda tulikuwa hatupati sababu ya wizi na uzembe...., Kwahio tuna guarantee gani kwamba na hio kodi haitaibiwa kwa wizi au kutofanya lolote sababu ya uzembe ?

Hapa ni kama mtu unawashwa kidole alafu unajikuna kwenye nywele.....
Tutapata ambacho Tulikuwa hatupati Kwa maana ya kupotea kwa wizi na uzembe.

Japo inahitaji proof ya kitafiti kwamba how efficiency will be guaranteed.

Mwisho nadhani kuna aina ya operations ndizo zitakuwa privitazed sio the whole .
 
Rubbish, bandari kote Duniani zenye ufanisi ni private sector run.

Kwanza aambiwe na nani wakati wanaopendekeza haya ni watendaji wa Serikali.
Huu ni uongo mkubwa, eti bandari kote duniani zenye ufanisi ni private sector run. Uongo huu na sijui kwa nini mnapenda kusema uongo

Bandari nyingi zenye ufanisi zipo chini ya serikali.
 
Huu ni uongo mkubwa, eti bandari kote duniani zenye ufanisi ni private sector run. Uongo huu na sijui kwa nini mnapenda kusema uongo

Bandari nyingi zenye ufanisi zipo chini ya serikali.
Thibitisha uongo kwa kuweka ukweli sio kuhemka kama unakimbizwa na kibaka.
 
Tutapata ambacho Tulikuwa hatupati Kwa maana ya kupotea kwa wizi na uzembe.

Japo inahitaji proof ya kitafiti kwamba how efficiency will be guaranteed.

Mwisho nadhani kuna aina ya operations ndizo zitakuwa privitazed sio the whole .
Kuna vitu vinaitwa Commanding Heights of the Country Economy na hivi inabidi vikumbatiwe na State..., Issue ya kuzuia wizi na Uzembe sio kumpa mwingine afanye..., tena kwa kutumia watu ambao wanatoa hio mikataba ambao ni hao hao wezi na walafi...

Issue ni kuhakikisha hizo Institutions zinafanya kazi kwa ufasaha..., (China has done it) Most and Better Performing Companies ni State owned..., Badala ya kuwapa wadau creme de la creme kwanini tusiwape makapi ? or better still kwanini wasifanye na sisi tufanye ?, After all its Free Market..., Tuwape kabandari kabaya huko ambako hakana wateja ili wakatengeneze kawe na potential kubwa sio kuwapa a finished product....
 
Huu ufunguaji wa Nchi inabidi tuufanyie due diligence ya kupata Pro and Cons.

Naona tunatafuta short term gains for long term pains.

Na wale tuliotegemea wasimamie na kuishauri serikali wamegeuka kuwa rubber stampers.

Hawa wanafanya zile Propaganda za awamu iliyopita zianze kuonekana Maybe..., Just Maybe kulikuwa na Ukweli ndani yake.
That was reality sio maybe...Only fools argued for what they never understood.
 
By the way kule Bagamoyo tumefikia wapi ?

Naona kama tunashika shika tu hapa na pale na tunahamia hapa hata kabla hatujaanza kule....
 
Kuna vitu vinaitwa Commanding Heights of the Country Economy na hivi inabidi vikumbatiwe na State..., Issue ya kuzuia wizi na Uzembe sio kumpa mwingine afanye..., tena kwa kutumia watu ambao wanatoa hio mikataba ambao ni hao hao wezi na walafi...

Issue ni kuhakikisha hizo Institutions zinafanya kazi kwa ufasaha..., (China has done it) Most and Better Performing Companies ni State owned..., Badala ya kuwapa wadau creme de la creme kwanini tusiwape makapi ? or better still kwanini wasifanye na sisi tufanye ?, After all its Free Market..., Tuwape kabandari kabaya huko ambako hakana wateja ili wakatengeneze kawe na potential kubwa sio kuwapa a finished product....
State owned but unaweza Kuta management yake ni private kama zilivyo banks nyingi za Serikali..

Hilo unalopendekeza ndio kama limeshindikana kwa sababu linasababishwa na nature ya jamii, hatuwezi kuwa kama China mkuu.
 
Kwa hali ilivyo naunga mkono hili la kuleta mbia, yaani meli zinakaa nje kusubiri nafasi kwa siku 23! Nani ataleta meli zake DSM? Tena tumechelewa sana sana na ni aibu!
Lakini tusikurupuke,maamuzi yenye mashiko kwa manufaa mapana ya taifa letu yanataka maandalizi yaliyo sahihi.
DP World port operator wa bandari za UAE na kwingineko katika nchi mbali mbali alifikaje huko hadi akanunua kampuni kongwe ya P&O?
 
Shida hapa ni uroho ni uroho wa watu tu lakini wazo lenyewe sio baya. ukiiangalia PIRAEUS "the gate way to Europe" imepata ufanisi mkubwa kupitia ubinafsishaji wa baadhi ya sector za bandari na mbia wao mkubwa ni CHINA kupitia COSCO. PIRAEUS ni bandari kubwa Ulaya ipo UGIRIKI ndio njiapanda ya meli myingi zinazotoka Ulaya kuja Afrika, kwenda nchi za ulaya na kwingineko ni bandari inayopokea meli nyingi na kufanya ufaulishaji(TRANSHIPMENT) kwenda kwa dsetination. Ni wazo zuri kabisa ila kwenye implementation ndio sipati picha
 
Back
Top Bottom