Watu wengi wanafikiria kupiga dili za kujitajirisha huko ! Kwa watu binafsi sio rahisi kupiga dili huko !!SIO BANK tu taasisi nyingi ambazo zinaendeshwa binafsi kwa asilimia kubwa hufanya vizuri, serikali ikashakua tu na hisa nyingi tatizo huanzia hapo
Ndio tujiulize kwa nini mashirika ya kiserikali hayafanyi vizuri?
StupidHuwa nakupuuza. Naona wewe ni mlimbukeni. Hujui chochote.
Yani huu ndo ukweli mtupu.wanapanga kuludisha nchi nyuma .watu wamepambana kukuza bandari wao wanagawana kila kitu..You hit the nail on the head. Yote uliyosema ni kweli tupu. Nakubaliana pia na wengi wa wachangiaji wa uzi huu. Kwa mfano kwenye Uzi #5 Mlaleo anasema 'we are moving backwards'. Kwenye Uzi #8 Vyamavingi anakejehi kwa kusema 'tupate pia mbia wa kuiendesha Serikali'. Kwenye Uzi #11 KeyserSoze anasikitika kwamba 'ufunguaji wa nchi unapitiliza kiasi'.
Tujikumbushe historia. Miaka ya 80 Rais Mwinyi alitamka kwamba kwa kuwa Hoteli ya Kilimanjaro inafanya kazi kwa hasara, tuwape kampuni ya kigeni waiendeshe. Waandishi wa habari wakaenda kumhoji Timothy Kasela, aliyekuwa Mkurugenzi wa shirika la utalii, ambalo hoteli hiyo ilikuwa chini yake, kuhusu kauli hiyo ya Rais. Yeye akasema kufanya biashara kwa hasara kwa Kilimanjaro si kwa sababu ya wafanyakazi wabovu wa Kitanzania. Badala ya kuwapa wageni hoteli waiendeshe, wawape ardhi wajenge hoteli yao ili tuone kama watatengeneza faida. Hiyo ilichukuliwa kama 'insurbodination' kusema kitu kinyume na alivyosema Rais. Kasela alisimamishwa kazi kwa karibu mwaka mzima 'uchunguzi' ukifanywa. Baada ya hapo, akafukuzwa kazi.
Mfano wa vitu ambavyo vilikuwa vikitia hasara Kilimanjaro ni kwamba ufuaji wa nguo wa hoteli ya Africana ulikuwa ukifanyika Kilimanjaro. Hoteli zote mbili zilikuwa zimepewa mwendeshaji mmoja ambapo mwenye mali Africana ilikuwa kampuni ya binafsi ambapo Kilimanjaro ilikuwa ya Serikali. Matumizi yanakwenda Kilimanjaro, mapato yanakwenda Africana. Mwisho Serikali iliamua Kilimanjaro iuzwe kabisa; kwanza kwa Hilton, Sheraton, etc. Kwa hiyo tulikuwa na Kempinski Kilimanjaro Hotel na sasa hoteli inaendeshwa na Hyatt Regency Hotels tangu 2012. Kila mwendeshaji aliyepewa alikuja na mbinu zake za kuiba mpaka miaka mitano ya nafuu ya kodi inapita halafu anaiuza.
Tuliona pia ubia ulioingiwa na ATC na South African Airways jinsi tulivyokuwa tukipigwa. Serikali ikagutuka mkataba ukasitishwa. Tukaingia ubia mwingine wa watatu: ATC, Uganda Airways, na kashirika kadogo ka ndege ka Afrika Kusini. Ubia huu ukadumu kwa kama mwaka mmoja tu. Mapungufu yakagundulika na kuufuta ubia huo.
Tukaingiza TRC ubia na Wahindi waendeshe treni zetu. Haukupita muda tukagundua tunaibiwa. Tukasitisha ubia.
Sasa tunataka ubia wa kuendesha bandari. Mifano niliyoitaja hapo juu inatosha kutukanya kwamba ubia si kwa manufaa yetu. Tujiulize kwanza wapi tunakwama kunakosababisha tusitengeneze faida inayopaswa? Jee, ni ukosefu wa utaalamu, au uwekezaji mdogo, au ni kitu gani hasa? Tukigundua hilo, hapo ndipo tuchukue hatua zipaswazo. Tusikimbilie kuingia ubia. Labda tuanzie kwanza kuingia ubia wa kuendesha Serikali na baadaye ndiyo tufikirie kuingia ubia kwenye kuendesha bandari.
Unawajua watz kwa fitina lkn atapigwa majungu ata kurogwa ili atoke hapa mwarobaini Ni kutafuta mbia tu.Mbia wa nini? kwanini wasitafute CEOs wenye uzoefu mkubwa waliowahi kuendesha bandari kubwa za kueleweka kama Amsterdam, New York etc nina uhakika wapo na wanaweza kunyoosha hiyo bandari kwa mshahara tuu bila ubia
Nchi unaiuza unamuuzia nani? Hii lugha ya "kuuza nchi" ni ya kijinga sijapata kuona.Hujaelewa kwasababu hukubaliani na hoja yangu. Huyo mama kwa hili la kubinafsisha bandari ya Dar asijaribu maanake tutakua tumeuza nchi .
Nipe mfano wa project mojawapo iliyofanikiwa.Huenda walijifunza kutokana na makosa ya kipindi hicho.
Siyo atakuwa ameshapatikana..Hapo tayari atakuwa kashapatikana, wanapima upepo tu
Ten percent ya udalali
ccm bhna mnamatatzEehh kweli kabisa, tukapeleka na Airport ya Kimataifa Chato, sasa wanatua mbayuwayu tu. Tukawaibia na majumba na magari yao matajiri. Tukawatolea bastola kuwatisha mawaziri hadharani waliposema ukweli. Tukafumua utawala wa bandari na kuweka "The" gang ndiyo waiendeshe. Usiyasahau yote hayo.
Lete ushaidi wa uliloandika kama huna chuki binafsi .mwanzo kama nilianza kukuelewa lkn hapa si sawa.changamoto za uendeshaji wa bandari TPA inashindwa kutokana na vitu kadha wa kadhaTumefanya hivyo kipindi Cha mwinyi, tukashindwa, tukafanya hivyo kipindi Cha mkapa tukashindwa, tukafanya kipindi Cha JK tukashindwa.
Kipi kimebadilika sasa tusishindwe? Juzi tu hapa raisi na jopo zima waliingizwa kwenye mkataba wa kinyonyaji hapo bandari na kampuni hewa
Wale jamaa wameshaingiza mabega tayari. Wacha tupigwe na kitu kizitoNimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.
Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?
Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.
Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.
--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.
Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.
Nyie watumishi wa Umma mnaenda Lunch masaa ma 3 mtaweza kujifananisha na private sector tukikamata bandariNadhani hapa kuna harufu ya ufisadi.
Hivi kuna Evaluation and monitoring report ya ufanisi wa TICTS toka awe mbia wa kuendesha bandari.
Ni lipi alifanikiwa ambalo TPA wangeshindwa kulifanya.
Ni imani potofu kwamba kila shirika akipatikana mbia basi litafanyakazi kwa ufanisi.
Hayo yote yamefanywa na ninyi CCM kuanzia baba yako mpaka wewe mwenyeweEehh kweli kabisa, tukapeleka na Airport ya Kimataifa Chato, sasa wanatua mbayuwayu tu. Tukawaibia na majumba na magari yao matajiri. Tukawatolea bastola kuwatisha mawaziri hadharani waliposema ukweli. Tukafumua utawala wa bandari na kuweka "The" gang ndiyo waiendeshe. Usiyasahau yote hayo.
Lete usha
Lete ushaidi wa uliloandika kama huna chuki binafsi .mwanzo kama nilianza kukuelewa lkn hapa si sawa.changamoto za uendeshaji wa bandari TPA inashindwa kutokana na vitu kadha wa kadha
gharama za ukarabati
tekinologia ya kisasa
ushindani uliopo kwenye bandar za Africa n.k
ebu lete nn kifanyike sio kama unaleta chuki binafsi