Sakata la DP WORLD: Rais Samia asema Serikali itatafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar, sasa kuchangia robo tatu ya bajeti ya nchi

Sakata la DP WORLD: Rais Samia asema Serikali itatafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar, sasa kuchangia robo tatu ya bajeti ya nchi

Tafuta kampuni zenye uwezo wa kufanya biashara tuache kupeana fake companies ziko kampuni wako serious utaratibu uwe wa vigezo hakuna kampuni ikaja kufanya hasara ujuwe mikataba ilikuwa fake. Unaleta kampuni ina record technical finance wako vizuri ili waboreshe huduma za kisasa hakuna kampuni ikaendeshhwa kiserikali ikafanikiwa hakuna tumeuwa mamia ya kampuni na hii SGR wakijifanya kuwapa hawa Railway basi wape miaka miwili tu kwisha, lete watu waendeshe hii ni business ikiwa takataka tu kuzoa hatuwezi mpaka waje kampuni binafsi ndio tutaweza kuendesha kampuni. TTCL ni mfu toka imezaliwa sababu ya ruzuku wanapiga hasara hawajali mishahara si inatoka serikali kuu shida iko wapi.
Binafsi sijaelewa vizuri, Ila unahisi kwa nini hizo kampuni nzuri hazikuwahi kuja?
 
Sasa hivi wapo wengi hapo bandarini, wezi watupu kila idara, siyo wachache. Ndiyo maana naunga mkono atafutwe mbia bandari iendeshwe kibiashara na si kihasara. Au ifaywe ni banadari ndogo tu ya ndani ya nchi utakapokamilika mji kamili wa bandari, Bagamoyo.
Huyo mbia atafanya nini ikiwa hao watu bado wapo? Si itakua Kama ilivyokua atcl, Tanesco na wengine?
 
Aiseee! Kuna siku tutatafuta mbia wa kuiendesha serikali maana tumeshashindwa kuiendesha bandari.

Ili bandari ifanye vizuri zaidi inatupasa kuachana na siasa kwenye uendeshaji wake Menejimenti ya Bandari iwekewe malengo na wasiingiliwe na serikali.

Kuwe na mkataba baina ya serikali na menejimentj ya TPA, iwapo watashindwa kufikia malengo yaliyowekwa kwa kila robo mwaka basi kibarua kinaota nyasi na iwapo kuna jinai sheria ichukue mkondo wake.

Nadhani tuanzie hapo.

Vv
Ipo siku nchi itapigwa mnada.
( nimekosa mimi nimekosa sana)
 
You hit the nail on the head. Yote uliyosema ni kweli tupu. Nakubaliana pia na wengi wa wachangiaji wa uzi huu. Kwa mfano kwenye Uzi #5 Mlaleo anasema 'we are moving backwards'. Kwenye Uzi #8 Vyamavingi anakejehi kwa kusema 'tupate pia mbia wa kuiendesha Serikali'. Kwenye Uzi #11 KeyserSoze anasikitika kwamba 'ufunguaji wa nchi unapitiliza kiasi'.
Tujikumbushe historia. Miaka ya 80 Rais Mwinyi alitamka kwamba kwa kuwa Hoteli ya Kilimanjaro inafanya kazi kwa hasara, tuwape kampuni ya kigeni waiendeshe. Waandishi wa habari wakaenda kumhoji Timothy Kasela, aliyekuwa Mkurugenzi wa shirika la utalii, ambalo hoteli hiyo ilikuwa chini yake, kuhusu kauli hiyo ya Rais. Yeye akasema kufanya biashara kwa hasara kwa Kilimanjaro si kwa sababu ya wafanyakazi wabovu wa Kitanzania. Badala ya kuwapa wageni hoteli waiendeshe, wawape ardhi wajenge hoteli yao ili tuone kama watatengeneza faida. Hiyo ilichukuliwa kama 'insurbodination' kusema kitu kinyume na alivyosema Rais. Kasela alisimamishwa kazi kwa karibu mwaka mzima 'uchunguzi' ukifanywa. Baada ya hapo, akafukuzwa kazi.
Mfano wa vitu ambavyo vilikuwa vikitia hasara Kilimanjaro ni kwamba ufuaji wa nguo wa hoteli ya Africana ulikuwa ukifanyika Kilimanjaro. Hoteli zote mbili zilikuwa zimepewa mwendeshaji mmoja ambapo mwenye mali Africana ilikuwa kampuni ya binafsi ambapo Kilimanjaro ilikuwa ya Serikali. Matumizi yanakwenda Kilimanjaro, mapato yanakwenda Africana. Mwisho Serikali iliamua Kilimanjaro iuzwe kabisa; kwanza kwa Hilton, Sheraton, etc. Kwa hiyo tulikuwa na Kempinski Kilimanjaro Hotel na sasa hoteli inaendeshwa na Hyatt Regency Hotels tangu 2012. Kila mwendeshaji aliyepewa alikuja na mbinu zake za kuiba mpaka miaka mitano ya nafuu ya kodi inapita halafu anaiuza.
Tuliona pia ubia ulioingiwa na ATC na South African Airways jinsi tulivyokuwa tukipigwa. Serikali ikagutuka mkataba ukasitishwa. Tukaingia ubia mwingine wa watatu: ATC, Uganda Airways, na kashirika kadogo ka ndege ka Afrika Kusini. Ubia huu ukadumu kwa kama mwaka mmoja tu. Mapungufu yakagundulika na kuufuta ubia huo.
Tukaingiza TRC ubia na Wahindi waendeshe treni zetu. Haukupita muda tukagundua tunaibiwa. Tukasitisha ubia.
Sasa tunataka ubia wa kuendesha bandari. Mifano niliyoitaja hapo juu inatosha kutukanya kwamba ubia si kwa manufaa yetu. Tujiulize kwanza wapi tunakwama kunakosababisha tusitengeneze faida inayopaswa? Jee, ni ukosefu wa utaalamu, au uwekezaji mdogo, au ni kitu gani hasa? Tukigundua hilo, hapo ndipo tuchukue hatua zipaswazo. Tusikimbilie kuingia ubia. Labda tuanzie kwanza kuingia ubia wa kuendesha Serikali na baadaye ndiyo tufikirie kuingia ubia kwenye kuendesha bandari.
Umechanganua vizur sana mkuu
 
KWa mtazamo wangu; sheria ya kuchapa viboko wafanyakazi wazembe hasa kwenye sekta nyeti bora INGERUDI; Bandari, TRA, BOT, ATCL nk tukianza na hao watu hakika tutasogea mbele; watu wamesoma hadi mwisho wa vyeti but kusimamia vitu vidog vidogo tu hawawezi, JINGA kabisa
 
Tunahitaji kwenda na wakati, Pale bado sana. Kauli yakutaka ubia sio kwamba Rais kaamua tu kusema, Kuna kazi kubwa sana imefanyika watu wametembelea bandari kubwa wakaona uendeshaji wake wakapima uwezo wetu wakaona hatutaweza kuwafikia bila ubia na wenye uwezo huo.

Kuna tofauti ya uwezo na akili. Uwezo ni ni akili 100% lakini akili sio uwezo asilimia 100%.
Hata ulichoandika pengine wewe mwenyewe hujaelewa.

Kuendesha kwa ufanisi Wala halihitaji mbia, tumewahi kufanya ubia karibu mashirika yote makubwa na tulishindwa, yapo yaliyokufa na yapo yaliyobaki na madeni makubwa
 
Hufahamu yaliyofanyika huko, labda ulikuwa mdogo sana.
Mm niwe mdogo kwenye hayo mashirika? Ikiwa nilikua nafanya kazi sehemu mojawapo?
Ni kipi kilifanyika Tanesco,trl na ATCL tulipokabidhi kwa wabia?
Hii inahitaji uwe na akili kujua kilichofanyika?
 
Nimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.

Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?

Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.

Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.

--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.

Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.

View attachment 2153881
😂, kumbe hata Chamvino tunaweza kuwa na mbia.
 
Binafsi sijaelewa vizuri, Ila unahisi kwa nini hizo kampuni nzuri hazikuwahi kuja?
Mazingira ya uwekezaji Tanzania ni magumu sana hayavutii mpaka kwenye visa za kazi tu ni gharama kubwa na tax ni kubwa sana Tanzania mazingira sio rafiki na kubwa zaidi hatuna mwendelezo wepesi wa kuvunja mikataba kwa pressure tu angalia kama kina Dangote wanapata tabu kufanya biashara Tanzania, makampuni makubwa yatakuja tu kukiwa na sera imara sio unakuta RC tu anamtia pingu mwekezaji bila sheria kufuatwa haya mambo hayakubaliki. Sera za biashara ziwe haziingilani na siasa za ndani biashara kitu kingine na siasa kingine.
 
Mazingira ya uwekezaji Tanzania ni magumu sana hayavutii mpaka kwenye visa za kazi tu ni gharama kubwa na tax ni kubwa sana Tanzania mazingira sio rafiki na kubwa zaidi hatuna mwendelezo wepesi wa kuvunja mikataba kwa pressure tu angalia kama kina Dangote wanapata tabu kufanya biashara Tanzania, makampuni makubwa yatakuja tu kukiwa na sera imara sio unakuta RC tu anamtia pingu mwekezaji bila sheria kufuatwa haya mambo hayakubaliki. Sera za biashara ziwe haziingilani na siasa za ndani biashara kitu kingine na siasa kingine.
Hizi unazoeleza hapa ni theories, kampuni haziji sio sababu ya sera au RC sijui kafanyaje. Haziji kwa kuwa wanashindana kwenye maslahi, ni Hilo tu.
Kuna kampuni kubwa zimewekeza pale congo, pamoja na vita kila siku.
 
Bandari ya Dar kwa sasa wangeacha utaratibu huu huu wa Sasa uendelee ila Serikali ipeleke nguvu ya ubia kwenye bandari ya Dar.

Pia Mradi wa Dart ndio unatakiwa upelekwe kwenye ubia na sekta binafsi..

Mwisho kama ni lazima ishu za ubia na bandari ya Dar iwe ni baadhi ya section zinazoleta failures
 
Mm niwe mdogo kwenye hayo mashirika? Ikiwa nilikua nafanya kazi sehemu mojawapo?
Ni kipi kilifanyika Tanesco,trl na ATCL tulipokabidhi kwa wabia?
Hii inahitaji uwe na akili kujua kilichofanyika?
Inategemea ulikabidhi vitengo gani,mbona banks zinafanya vizuri.
 
Nimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.

Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?

Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.

Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.

--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.

Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.

View attachment 2153881
Hii kitu ni unrealistic kupata mapato robo tatu ya kuendesha bajeti ya serikali. Bajeti ya serikali kama trilioni 38-40.. Je sasa hivi bandari wana mapato kiasi gani?

Kiasi kutamani kwenda hapo?

Watatumia mbinu gani? Wataongeza ghati mpya au hizi za sasa...? Imekuwaje sasa hivi wasipate hayo mapato waje kuyapata baada ya mwekezaji mpya.?

Uzoefu umeonyesha wawekezaji huja kupata faida wao na si vinginevyo.. Kwa hiyo mwekezaji apate faida yake na aiachie au alete mapato kwa serikali kwa 75% ya bajeti.

Ni kauli ya kuvutia sana, lakini haina uhalisia... Ahadi kama hizi zimetolewa kwenye tozo mbalimbali na mpaka sasa , serikali imebidi iende ikakope kujenga mashule ... Hata kwenye mashule hatujajua kama huo uwezo zaidi wa madarasa na wanafunzi wa sekondari na msingi..Tunayo ziada ya kuendesha , hilo ni swala la siku nyingine.

Sasa kwenye bandari , kweli lipo tatizo , meli kuchelewa kuingia bandarini , meli chache kutumia bandari yetu, mizigo kidogo kutumia bandari yetu. Hivyo mapato kuwa madogo. Changamoto kama hizi zinaweza tatuliwa kwa kuongeza sehemu za kupokelea mizigo nje ya bandari , mageti ya kuingiza na kutoa mizigo bandarini, hivyo kuongeza uwezo kupokea na kutoa mizigo na maeneo mengine kama bandari kavu.. Kuimarisha barabara na vivuko mbalimbali vinavyounganisha bandari zetu na nchi jirani..Mifumo ya kikodi na utendaji wa taasisi mbali mbali zinazohusika na mizigo inayoingia Tanzania ikiwemo TRA....

Haya yote yanaweza kufanyika , lakini mapato hayatoongeza kuweza kukidhi robo tatu ya bajeti ya Tanzania... Na haya yanaweza kufanyika kwa uwekezaji wa serikali kuimarisha miundo mbinu mbalimbali.... Kama haya hayafanyiki na unamuleta mwekezaji atakuja kuleta maajabu gani?

Au ndiyo yale yale , huyu anakuja anafanya yake , halafu awamu ya uongozi mwingine inakuja kubadilisha ya awamu iliyopita..

Tuwekeze kwenye miungo mbinu yetu, tuongeze uwezo wa taasisi zetu , wafanyakazi wa Kitanzania .. Hakuna mjomba atakayekuja kuleta maendeleo TANZANIA.
 
Hakuna haja ya mbia ila inatakiwa tuwekeze mzigo wenyewe na faida tule wenyewe sidhani hizo fedha atakakazokuja kuwekeza mbia sisi tutashindwa.
 
Nimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.

Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?

Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.

Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.

--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.

Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.

Tungeanza na Tanesco.
 
Nimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.

Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?

Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.

Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.

--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.

Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.

namkubali sana Dr msukuma kwamba wasomi wameirudi nyuma kwa kiasi kikubwa sana.sasa Ndugai walimlazimisha kujiuzuru kwa nn wkt inaonekana kabisa nchi inaenda kuuzwa kama awali?
 
Back
Top Bottom