Sakata la Escrow: AG Werema amvaa Kafulila, Amwita tumbili asiyeweza amua mambo ya msituni

Sakata la Escrow: AG Werema amvaa Kafulila, Amwita tumbili asiyeweza amua mambo ya msituni

werema mpaka leo yale mabilioni ya uswiswi hajaja kutupa taarifa, leo hii tena huo ufisadi anatoa hoja nyepesi anaita ushahidi vipeperushi? kweli watawala wamejisahau katika nchi hii, wanajua nchi ya kwao, na kutusifia kuwa watanzania ni wastaarabu sana. huo ushahidi ukipelekwa kwa pccb ndio walewale. katuni ya kipanya leo kimejieleza.
 
serekali ya ccm wakimbiwa ukweli unawauuma sana ushahidi makinda anao wanataka nn tena werema hamna kitu bora hata mwanasheria wa serikali angekuwa tundu lissu ccm imeshachoka jamani
 
kula mgao ndo umwite mwenzio tumbili dah pesa hizi singa singa kakusikia werema atakuongezea dau
 
Siasa ni ya ajabu sana kafulila huenda anataka mgao nayeye maana haaminiki tokea ajiondoe chadema. Full unafki
 
Sio lugha nzuri kwa binadamu mwenzako. Usishabikie

Ndugu stanley huwezi amini kuwa kuna binadamu tena mtanzania anachekelea kiongozi mkubwa wa serikali kumwita binadamu mwenzake tumbili. Hizi hela za wizi wanazosomeshea watoto wao , kuhonga wanawake zitawatokea puani siku si nyingi
 
Last edited by a moderator:
CCM ni sawa na ukoo wa Panya, baba mwizi, mama mwizi, mtoto mwizi, babu mwizi, bibi mwizi, kaka mwizi,dada mwizi, shemeji mwizi, mkwe mwizi! By Mh.Nassari.
 
Magamba yamezoea vya kunyonga vya kuchinja hayawezi. Yakishikwa pabaya hata kama ni issue Muhimu za kitaifa, huweweseka na kutoa povu ili mradi tu kulinda maslahi yao.Sasa hapo Werema alikuwa na sababu gani ya kutoa kashfa na matusi. Kwanini asijibu kwa hoja bila hasira?
 
Yataka moyo was chuma kusikiliza habari za tz. Hata mambo ya msingi wao wanaingiza siasa
 
Back
Top Bottom