Sakata la Israel na Palestina anaetafutwa na Marekani ni Saudi Arabia. Gaza wanazuga tu

hkuna

hakuna taifa lina ujasiri wa kuvamia ndani ya Saudi arabia. hakuna vita itapiganwa ndani ya Saudi arabia hadi dunia inaisha
iran ina ujasiri kuivamia saudia, na kuna siku watafanikiwa, hiyo imekuwa ndoto yao kuiteka saudia na maeneo yote matakatifu, huku wakimsubiria mahdi wao kwa mujibu wa imani ya kishia. kama hujui, hilo ndilo lilifanya saudia na iran wamekuwa maadui kwa miaka mingi, na ndio maana iran amekuwa na ujasiri hata kufadhili waasi wa huthi Yemen waliorusha makombora hadi saudia.
 
hujui hata kusoma nyakari. anayetafutwa hapo ni IRAN. marekani hawezi hata siku moja kuifanyia hivyo saudia kwasababu ni mshirika wake mkubwa sana. hapo anatafutwa iran na muda si mrefu kibuyu kitapasuka.
Iran atafutwe wa nini na tayari vikundi vyote vya mapigano vinavoizunguka Israel vinajulikana au vimeanzishwa na Iran au vina full support ya Iran.

Unavijuwa hivyo vikundi?

Iran tayari ipo kwenye mapigano ya muda refu na US, unafahamu maana ya "muqawamma" ya Iran?
 
Yeah, of course.
 
iran anatafutwa kwasababu alishatamka kwamba atalifuta taifa la israel kwenye uso wa dunia, pia anafadhili hamas na hezbollah na vikundi vingine kule westbank. marekani asingefanya chochote kwa saudia wakati israel kabla ya vita na hamas alikuwa kwenye mazungumzo naye ya kuneutralize relations, na walifikia pazuri tu. na kwa upande mwingine, israel na marekani wana mpango wa kuteketeza kabisa vitisho vya makundi ya hamas na hezbollah yasiwepo kabisa, na wanajua wakifanya hivyo iran anaweza kuingilia kati au anaweza kuwa anaendelea kutuma silaha ndio maana wamesogeza silaha karibu ili iran ikifanya chochote, waimalize.

pia, iran inajua kuwa, haiwezi kuishambulia israel na kuishinda kama haitasaidiwa na vikundi vya kigaidi ilivyovitengeneza ambavyo vyenyewe vitapigana bila kufuata sheria za kivita. iran akipigana na israel anawajibika kufuata sheria za vita na kwenye uwanda wa aina hiyo atapigwa asubuhi kabisa, ila kupigana na watu ambao hawafuati sheria za vita (mfano, kutumia raia kama shielf, kuteka raia n.k) ni ngumu sana. ndio maana iran anawatumia hamas na hezb kupunguza makali ya israel. ila unachotakiwa kujua ni kwamba, walichoamua sasaivi hawataki kubaki na tishio lolote around them, hivyo iwe leo au kesho lazima hamas na hezbu waifute kabisa, na wataongeza ukali wa sheria za kuwakalia wapalestina ili vikundi kama hivyo visiwepo karibu yao tena.
 
Faiza kumbe wewe ni bure kabisa; analysis zako zahovyo sana na kwakweli inaonyesha ni kwa kiasi gani haujui kinachoendelea huko Duniani.
Kama kuna Taifa ambalo limeonyesha ukomavu kwa sasa ni Saudia. Kwanza umeisha sikia Saudia kuna mtu ameandaana kwa sababu ya Hamas!? Zero. na kwa taarifa yako Saudia, UAE, na Egypty hawawataki Hamas, kwa sabau ya siasa zao za Muslim Brotherhood.
Ona hii screenshot Mwana wa Mfalme akitak kuwe na suluhisho kwa kuzingatia mipaka ya Palestine na Isarel ya 1967 ambayo kimsingi ndiyo ipaka ambayo UN waliweka 1947 isipokuwa tu kwa mjia wa Jerusalemu ambao UN waliazimia uwe Mji wa Kimataifa. Wapalestina walikataaga
Video clip ni ya Former Intellegence Chief wa Saudia Mr. Turki Al-Faisal amaye anawalaumu Hamas kwa kuhujumu Mpango wa Amani ambao ulikuwa karibuni ufikiwe kati ya Israel na Saudia. Sasa watu kama hao Marekani na Israel watakuwaje na Mpango wa kuwahujumu????!!!!!

Your browser is not able to display this video.
 
Sawa sawa, lakini Iran sio waarabu ila majority ni waislam. Wairan ni kama wahindi/wapakistan vile.Mapashtun aka waajemi aka wapersia. Kitambo ndio walikua marafiki wakubwa wa US chini ya uongozi wa Shah wa Iran kabla ya mapinduzi ya kiislam yakiongozwa na Ayatollah Khomeini.
 
Kuna kaukweli kwa 95%
 
Wewe upo shallow sana.

Jitahidi kuzama ndani kidogo.
 
Changia hoja kistarabu acha kuattack watu kipumbavu hivi
 
Wewe ndio pumba kabisa. Saudia alikubali kuwa kibaraka wa marekani. Na ukishakuwa kibaraka wa marekani hauwezi hata kidogo kuwa upande wa palestina.
Hamas sio wajinga, saudia ilitumika tu kuchelewesha juhudi za palestina kuwa taifa huru

TUONDOLEE UPUMBAVU, ISRAEL HAUKUWAHI NA MPAKA LEO HII HATAKI PALESTINE KUWA TAIFA HURU
 
Acha arabinism
 
Bimkubwa usipokula ugoro uwaga uko jicho la mbali sana
 
Acha arabinism
Saudi Arabia anatafutwa lazima asaini mkataba wa ulinzi na US. Zimtoke.

Unafikiri kama Mashariki ya kati kuna amani na Urusi na Mchina wameshajipenyeza huko, US atapiga wapi pesa ndefu?
 
Wewe ndiyo wale wanaojilipua kwa kuahidiwa bikra 71 mbinguni, yaani mtupu na wala kichwa chako hakitafakari neno lolote zaidi ya kuvaa mabomu tu. ungekuwa na akili ungejiuliza uzi unasema nini? ndiyo ungepata umaana wa jibu langu kwa Faiza.
 
Na bila shaka isipokuwa kweli utakuja na stori nyengine. Ila usisahau asilimia 80% ya bajeti ya kijeshi ya Saudia Arabia inafadhiliwa na Marekani. Usisahau hilo!
 
🇺🇸 amechonganisha nchi hizo za Middle East kwa miaka nenda rudi
Saudia aliambiwa Iran anataka kumvamia wakaamua kumchonganisha na Iraq ile vita ambapo nilikiwa huko
Hapo kumfanya KSA kuwa hasimu mkubwa wa Iran na chuki kubwa na yote hiyo mnafiki anajukikana
Sasa amekuja huyu dogo ingawa nae amechukua nafasi ya baba yake mdogo kibabe na kumuweka kizuizini kwa mda na kujitwalia cheo ambacho kilikuwa sio chake na kumshinikiza baba yake ambaye kajizeekea wala hajui kinachoendelea

Hapo akawaweka jela hotel ndugu zake wote na kuwalazimisha kutoa mabilioni ya fedha ndio atawaachilia
Baada ya hapo akaanza miradi kibao na pia kumtandika Yemen sana na kuwatunukia pilots 100 kila mmoja gari la RR (Rolls Royce) sio Range ok
Akaanza kuwaalika Iran na Israel kimya kimya na mwisho hadharani

Hebu tusubiri maana dogo anajiunga kila sehemu ambapo 🇺🇸 hapendi na inaonekana atakuja kupigwa risasi na ndugu yake tu maana historia hiyo wanayo
 
Mimi sikubaliani na wewe kwanza ulipotaja habari za sept 11.Tukio lile ni la uongo mwingi na la kupangwa.Saudi Arabia hakujua chochote kilichotokea.
Na vile vile huyu MBS ana tabia tu za kujiona na kutaka kutukuzwa kutokana na kutawala taifa tajiri na kitovu cha waislamu.Pamoja na hivyo kwa sasa hakuna anayemlaumu kwa kile kinachoendelea Palestina.Hivyo Marekani hawezi kumgusa akaungwa mkono na waislamu.
Na mwisho Marekani haina tena uwezo wa kupigana.Mambo yamemchanganyikia mno.Kila kwenye ugomvi kaingia na ndani ya nchi yake maandamano ya kuunga mkono Palestina ni makubwa kuliko katika nchi nyingi za kiarabu.Sasa hawezi tena kuendelea kuwachokoza raia zake kwa kuendeleza uhasama ili kuilinda Israel.
 
Wewe ndiyo wale wanaojilipua kwa kuahidiwa bikra 71 mbinguni, yaani mtupu na wala kichwa chako hakitafakari neno lolote zaidi ya kuvaa mabomu tu. ungekuwa na akili ungejiuliza uzi unasema nini? ndiyo ungepata umaana wa jibu langu kwa Faiza.
Kila mtu anamuona mwenzake hana akili🤣🤣
Wewe upo kwenye kukariri tu lakini alichokieleza hapo bi mkuwa kina make sense.

Saudia ndio ilikuwa kete kubwa sana ya marekani kufanya nchi za kiarabu zisiwe na uwelewano. Kama huo uwadui wa iran na saudia marekani ndio alioutengeneza ili apige pesa ya msaudia na kuisaidia Israel kwa kuzifanya nchi za kiarabu kutoelewana.

Sasa hii kitu saudia ilivyochenji kwa kiasi kikubwa, ni jambo la kuwekea question mark. Kwanza hilo la kupatana na irani ni pigo kubwa kwa Israel na marekani, kujiunga na bricks, kujiweka karibu na china na Russia. Haya mambo tunayaangalia kwa uwepeai sana lakini kuna kitu kikubwa sana ktk huku kubadilika kwa saudia
 
Kwenye red ulikuwa ukiwaambia raia kama Shuleni walifundishwa Ujinga! haya rekebisha faster kama usemamvyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…