Sakata la Jerry Silaa kuvunja majumba ya watu nchi nzima: Johnson Mahululu aidai serikali ya Tanzania bilioni 20

Sakata la Jerry Silaa kuvunja majumba ya watu nchi nzima: Johnson Mahululu aidai serikali ya Tanzania bilioni 20

Huyo na komwe lake mpaka limefunika macho kama kofia aache due legal process ifanye kazi, wizara yake ni mtuhumiwa wa kutoa hati mbili, anatakiwa awe kizimbani, cha ajabu mtuhumiwa ndio anaamua kesi yake.

Kama Wizara yake ilitoa hati mbili, kwa nini isimfidie waliyemuingiza chaka, aachie kiwanja, wampe wanayeona yuko sahihi?
Letters of offer mbili siyo titles mbili
 
Jerry Silaa anashinikiza ifunguliwe kesi ya criminal trespass wakati msimamo wa Mahakama za Tanzania ni kwamba hiyo ni civil case, kama kuna dispute ya umiliki ni lazima kwanza mahakama ya madai ithibitishe nani mmiliki ndipo ujue nani kafanya criminal trespass.

Pengine Mwendesha Mashtaka wa Mkoa kawagomea kupeleka jalada Mahakamani kwa sababu hiyo

Anajua hiyo bili ya bilioni 20 lazima aitolee maelezo Baraza la Mawaziri, au kabla,kwa Waziri Mkuu
Vyeo ni dhamana ,tutafika tu
 
Huyo Johnson Mahururu inaonyesha amekuwa na kesi nyingi za migogoro ya ardhi. Alishawahi kushindwa kesi shidi ya Emmanuel Nchimbi kugombania kiwanja Tegeta. Ukim google utaona. Huyu jamaa ni seasoned litigator.
 
For whatever reason, kawaida kama zimetolewa Letters of Offer mbili na kuna mgogoro, anayepewa hati Wizarani ni yule mwenye latest Letter of Offer, siyo oldest Letter of Offer. Sijui ni mantiki gani inayotumika hapa
 
Naomba nielimishwe, fedha za fidia za namna hii utolewa fungu gani ndani ya Wizara husika? Je zinakuwa allocated ndani ya bajeti ya Mwaka wa Fedha husika?
Hizo fedha hazipo, na wala haziwezi kupangiwa kwenye bajeti labda mpaka washike ndege za ATCL 😂... Unaijua serikali mzee, anajitafutia kufa kwa stress
 
1. I agree with you, that, zipo scenario hizo za watu wenye nguvu kifedha kutumia udhaifu wa sheria kudhulumu watu wengine wanyonge kifedha. Lakini je, hiyo inampa uhalali gani waziri kufanya alichokifanya? Je, unadhani kila mwenye uwezo kifedha na kujipatia mali, basi amedhulumu tu?

2. Katika scenario ya mgogoro huu, na kwa maelezo ya wakili huyu ni kuwa jengo hilo si kwamba lilijengwa ktk eneo lisiloruhusiwa kisheria bali ni mgogoro wa watu wawili (Johnson & Naomi) kila mmoja akidai ni mmiliki halali wa kiwanja kile. Hivi ktk busara ya kawaida na ktk situation kama hii waziri alipaswa kufanya nini? Ni hiki alichokifanya, kubomoa nyumba ya mtu bila hata amri ya mahakama ingalau? Really?

3. Katika mfululizo wa matukio ya mgogoro huu, mtu mwenye kufikiri vizuri anaweza kutambua mara moja kuwa uko msukumo wa rushwa, ufisadi ukihusisha matumizi mabaya ya madaraka upande wa waziri na anaowapambania. Kamwe huu si utendaji wa kazi za kawaida tu za waziri.

Mathalani;

☑Ni kwanini wamkamate wanayedai ni tapeli na kumweka kwenye selo ya polisi kwa siku 6 bila kumfikisha mahakamani?
☑Ni kwanini yeye waziri abomoe nyumba ya mtu bila kibali cha mahakama? Na yeye amepata wapi mamlaka ya kuwa msikilizaji na mwamuzi wa migogoro ya haki za watu badala ya mahakama?

Kwa maoni yangu, Waziri Jerry Silaa amekosea na kama sheria itazingatiwa na kuheshimiwa, basi imekula kwake hiyo!!!
Mkuu argument yako doesnt hold.
Custodian wa official records za Ardhi ni wizara yenyewe, and they undoubtly know who the authentic owner of the parcel of land is.
And you have the audacity to dispute THAT?
Just make a quick buck from your client.
 
Nimemsikiliza wakili mwanzo mwisho ila nimekuwa na hofu kidogo kwa nini huyu mteja wake Kila kiwanja anachonunua kina migogoro? Na ni lazima mahakama ihusike?
Mkuu matapeli wa viwanja huwa wana budget ya around 20 million kuvuruga umiliki wa kiwanja cha mtu.
Hivyo badala ya kukinunua 200million wao wanaweka wanasheria na kuhonga watu wa ardhi na hivyo kupata hati za kughushi kwa bei rahisi.

Kuna jamaa wakishirikiana na maafisa wa Ardhi walitaka kunichezea mchezo huo, wakakuta mimi maji marefu.
Waka give up.
 
Sheria ina utaratibu, kama kashinda mahakamani, aliyeshinda aende mahakamani akabidhiwe alichoshinda, na kama walioshindwa wamesharau mahakama, sheria ina maelekezo, unamkamata wewe Waziri ili iweje?
wewe zungumza hivyo kirahisi rahisi bila ya uzoefu wa mahakama na nchi hii.

Unashinda kesi halafu unaambiwa ati kakamate mali za huyo aliyeshindwa ili mahakama ije itathmini na kukulipa wewe - umewahi kuusikia hiyo? Ilitutokea sisi na kijana mmoja tajiri sana hapa nchini.

We acha tu mahakama ya nchi hii baadhi ya hao majaji (Mungu anisamehe) lakini watakuwa na kesi nyingi za kujibu huko akhera mbele ya Mungu.
 
Watanzan

Huyo wakili amelipwa pesa, anatoa jasho na mishipa, anatetea uovu. Nchi hii imejaa wahuni tupu, ambao wanakutapeli wanaleta mawakili waongo kama huyu. Aende mahakamani sasa.
Umesikiliza "pleadings" zake? kama una elimu ya sheria kidogo, msikilize tena! Kuna hard facts ambazo zitamuingiza matatani! weka uchawa pembeni......
 
Umesikiliza "pleadings" zake? kama una elimu ya sheria kidogo, msikilize tena! Kuna hard facts ambazo zitamuingiza matatani! weka uchawa pembeni......
Hamna chochote hapo. Ukitetea wanyonge Tanzania kelele zinakuwa nyingi sana. Hizo zote ni issue za kutengeneza ili kuwe na ukweli. Sasa, apambane na serikali tone. Dhuluma tupu!!!
 
Suluhu siyo kutumia ubabe wa kiongozi. Mahakama ndiyo chombo cha kutoa haki.
Mahakama ilitoa haki lini tena mahakama hii ya tanzania ?

ndio maana mtu mmoja alisema siendi mahakaman maana najua una nguvu ya pesa na cheo lakini nakuhakikishia kuna mahali mimi nitashinda , na kweli haikupita wiki mtu na mkewe na bint yao wakaliwa kichwa na israeli mtoa roho kwa pamoja
 
Hamna chochote hapo. Ukitetea wanyonge Tanzania kelele zinakuwa nyingi sana. Hizo zote ni issue za kutengeneza ili kuwe na ukweli. Sasa, apambane na serikali tone. Dhuluma tupu!!!
Nakumbuka wakati wa utawala wa BM miaka ya 2000 kuna mtu dhulumati kama huyu alijenga nyumba ya ghorofa pale kwa, nyerere mikocheni. Ghorofa kubwa kweli kweli. Mama Maria alimwomba BM kuhusu dhuluma ya huyo mnyanganyi. BM alimuagiza huyo dhulumati kutoa huo uchafu wake pale kwenye kiwanja cha Mama Nyerere ndani ya 24 hrs. Na kweli ghorofa lilivunjwa.
 
Source: Youtube-wakiliTv, taarifa ya Wakili Dickson Matata

Nilisema kwamba haya mambo ya kujifanya mwendesha mashitaka na hakimu anayofanya Jerry Silaa yasipoangaliwa, ataitia nchi hasara kubwa sana.

Sasa watanzania wataingia hasara ya bilioni 20 ili kumlipa Johnson Mahululu baada ya Jerry Silaa kuvunja ghorofa lake, kumdhalilisha kumuita tapeli wakati hana hukumu ya mahakama iliyompata na hatia ya utapeli, na kumharibia jina na biashara zake.

Niliwahi kuonya humu kwamba wizara kubwa na nzito wasipewe watoto, hawa watoto waanzie wizara ya michezo, utamaduni na kwingine.

Nimefuatilia kule Mwanza, anatangatanga na Polisi kwemye mikutano, na wale ambao hawajaelewa maelezo yake, anatoa amri wakamatwe na Polisi. Kimsingi, analeta chaos kubwa sana.

Ameenda kuonana na RPC na kutoa amri (udikteta ambao samia hataki) kwamba Johnson Mahululu anyimwe dhamana, ana siku tano hajatoka.

Tunajua weekend iliyoisha ilibidi awahi kikao mahali akutane na bosi wake mkubwa., tunaipa angalizo serikali dhidi ya Jerry Silaa.

Kuhusu nyumba kuvunjwa, soma Aliyevamia Kiwanja cha mwingine kwa miaka 20 Mbezi Africana avunjiwa ghorofa

Pia soma Serikali impe angalizo Jerry Silaa, namuona anaiingiza Serikali katika mgogoro mkubwa wa kulipa fidia!
wakati mwingine busara huwa inaitajika unapotoa maamzi. mediation inaweza kutumika .kwani kuna faida gani unapovunja nyumba ya mtu hata kama kiwanja si chake? wewe mwambie kiwanja si chake then akikubari mwambia nunua kiwanja hiki.ziko taasisi zenye kuthaminisha viwanja na majumba .hivyo mhusika au mtuhumiwa ataweza kununua kiwanja hicho au nyumba hiyo kwa thamani halali iliyopangwa na wathaminishaji.unabomoa ghorofa ya mabilioni ili upate faida gani? kwanza serikali inakosa mapato kupitia ubomoaji huo kwa sababu let us say ni nyumba ya kibiashara pale watu walikuwa wanaingiza hela na serikali inapata kodi .sasa nyumba umevunja hapo serikali inapata nini
 
wewe zungumza hivyo kirahisi rahisi bila ya uzoefu wa mahakama na nchi hii.

Unashinda kesi halafu unaambiwa ati kakamate mali za huyo aliyeshindwa ili mahakama ije itathmini na kukulipa wewe - umewahi kuusikia hiyo? Ilitutokea sisi na kijana mmoja tajiri sana hapa nchini.

We acha tu mahakama ya nchi hii baadhi ya hao majaji (Mungu anisamehe) lakini watakuwa na kesi nyingi za kujibu huko akhera mbele ya Mungu.
Bahati mbaya wakati wenzako wanaenda shule, wewe ulikuwa unasubiri uji jikoni, ukapewa kazi ya kuchochea kuni
 
Mkuu argument yako doesnt hold.
Custodian wa official records za Ardhi ni wizara yenyewe, and they undoubtly know who the authentic owner of the parcel of land is.
And you have the audacity to dispute THAT?
Just make a quick buck from your client.
Wewe ni mpumbavu sana. Wapi amebisha lolote kuwa Wizara husika ndiyo mhodhi wa mwisho wa kumbukumbu zote za umiliki wa ardhi? Au umeamua kuturingishia Kiingereza chako cha kuunga unga?
 
Wewe ni mpumbavu sana. Wapi amebisha lolote kuwa Wizara ndiyo mhodhi wa mwisho kumbukumbu zote za umilik wa ardhi?
Soma uelewe argument ya huyo "wakili msomi"

Tatizo lenu ninyi watu wajinga wajinga ni kufikiri kuna kaujanja unaweza kufanya,kumiliki ardhi, halafu nyie vilaza mnaita "kutoboa"!

Hamjui kuwa process ya documentation ya ownership ya ardhi iko zaidi ya ofisi 5 mbali mbali, ambazo kwa ujinga wenu mnafikiri ukiforge document za ofisi moja basi " umetoboa"!
 
Soma uelewe argument ya huyo "wakili msomi"
Tatizo lenu ninyi watu wajinga wajinga ni kufikiri kuna kaujanja unaweza kufanya,kumiliki ardhi, halafu nyie vilaza mnaita "kutoboa"!
Hamjui kuwa process ya documentation ya ownership ya ardhi iko zaidi ya ofisi 5 mbali mbali, ambazo kwa ujinga wenu mnafikiri ukiforge document moja basi " umetoboa"!
Your level of mental retardation behooves me to quit all exchanges with you henceforth. You can impossibly be a sane, rational individual.
 
Source: Youtube-wakiliTv, taarifa ya Wakili Dickson Matata

Nilisema kwamba haya mambo ya kujifanya mwendesha mashitaka na hakimu anayofanya Jerry Silaa yasipoangaliwa,
Sasa wewe unakimbilia kutuandikia mambo ya YouTube? Ili iweje? Hujui kwamba wanasheria wapo kwa ajili ya wapuuzi kama hao? Unaomba bilioni za nini? Yaani alitaka aendelee kucheza na maisha ya wengine yeye akijiona ni star wa Dar?

Halafu wanaojiita wanasheria wajiulize kama wana akili za kusaidia nchi. Tunachotaka ni haki, siyo hukumu ya mahakama, ambayo iko kwenye tano bora kwa rushwa. Sifa za wanasheria imekuwa kutetea waharifu na kushinda, badala ya kupata haki. Yaani hata wanasheria wanashiriki kutoa rushwa kwa mahakimu na majaji ambao wengine ni classmates wao. RUBBISH!!
 
Back
Top Bottom