mgeni wenu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 3,664
- 1,730
Dar mzee wa watu kapewa ukatibu mkuu juzi tu jamani,si aulizwe Chikawe na Abdul wakil? Poleni sana mambo ya ndani
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ana wasi wasi gani kama atakuwa anajua mkataba hauta patikana,watu wamejisaidia na kufukia kama paka.kama Igp na katibu mkuu wanatupiana mpira....sipati picha uyo lugumwi mwenyewe yupo katika hali gani???
Hivi huyo mangu ni chaguo la ngosha au mkwere? Maana hapo naona kama safari yake ya kurudi ziwa singidani kuvua samaki ndio inawadia na huyo katibu ajiandae kwenda kwao bukoba kuvuna kahawaMkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,Ernest Mangu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya ndani,Jaji Meja Jenerali Projest Rwegasira, wameripotiwa kutupiana mpira kuhusu kuhusu ni nini kimesababisha kutokuwasilishwa kwa mkataba huo kwa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali siku ya jana.
Mangu anasema: "Iliyoagizwa ni wizara kwahiyo siwezi kuzungumza kwa niaba ya wizara na hiyo siku Katibu Mkuu alikuwepo."
Alipoulizwa kwamba,kwa upande wao wamekwishawasilisha mkataba huo wizarani alisema: "Kwani anayesaini mkataba si katibu mkuu,hivyo wasaliana na ofisi ya katibu mkuu au waziri."
Gazeti lilimtafuta Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ambae alisema: "Ninaomba uwasiliane na IGP."
Baada ya kauli hiyo,Tanzania Daima lilimweleza kwamba IGP Mangu amesema atafutwe Katibu Mkuu kwani siku hiyo alikuwapo(siku walipokutana na kamati ya PAC) ambapo Rwegasira alisema: "IGP atoe maelezo siyo Katibu Mkuu,kwani hata siku hiyo tulipokwenda aliyekuwa anajibu maswali ni IGP siyo mimi."
Alipoulizwa ulipo mkataba huo,Katibu Mkuu huyo alisema: "Hata kama ofisi yetu ndiyo inasaini mkataba,lakini suala hilo lilielekezwa moja kwa moja kwa IGP ambae alikuwa anajibu."
"Mimi nategemea aliyeambiwa kupeleka ni IGP,huu ni uelewa wangu na kama alijua hana angeeleza kwamba hana ili kamati ya Bunge itoe maelezo ya jinsi ya kumsaidia kuupata." aliongeza Rwegasira.
Baada ya ufafanuzi huo wa Rwegasira,Tanzania Daima lilimtafuta kwa mara nyingine IGP Mangu ambae hakupatikana kwani simu yake ya kiganjani ilikuwaa ikiita bila kupokelewa.
Chanzo: Tanzania Daima
Bora ya yule mama!
Ndio mwanzo wa kusambaratika huoTutaona nakusikia mengi sana ccm maigizo mengi
Tukiwagusa mafisadi nchi itayumbaYale yale. Sinema imeanza....... Chezeya mwana wa mfalme. Vita vya Mafisadi ni ngumu sana kwa Magufuli. Sidhani huo mkataba utapatikana
Masikini ngosha wa watu!!!!!Na ndo itafifia hivyo.
Keshokutwa watakuja na jipya tena na hili litapita kama ambavyo wamezoea kusema ni upepo tu
Wacha wapapatuwane tuKama IGP alimsimamisha afisa manunuzi wake, mbona la kupeleka documents anasita? Au nae anamjengo mmoja kati ya hizo 40? Kwa katubu mkuu bado mgeni sana kwenye hiyo Wizara. Haelewi historia ya hicho kitu.
Kuja mambo hapo.
Mkuu adui muombee njaasasa hii inaitwa kama mmbwai ni mmbwai tu , kila kitu kitafahamika .
Na hata likiwa live unge tegemea nini wakati wabunge walio wengi ni wa chama tawala na tayari wamesha anza kuonyesha madhaifu yao.Watakomaa Bunge lisiwe live!
Wewe fisi wa lumumba wacha kutokwa na mapovu, naona yamekujaa kwenye migongo ya midomo yako utadhani umebugia uyoga wenye sumu tulia sindano ikuingie vizuriMagu kivipi tena wewe fisi wakati ngoma ipo chini ya kamati ya Bunge? Au mnataka mpewe fursa ya kusema Magu dikteta anaingilia Bunge?
Usijusumbue na huyo mtu. Hao ni walee....wasomao magazeti yao ya uhuru.tupatie iliyo sahihi basi.wewe si umeona hadi wamewanukuu hao wahusika?kama una chuki binafsi na hilo gazeti sema tu.
Teeeeeeh teeeeeeeeh, unataka kijarida cha kufungia vitumbua? TANZANIA DAIMA NDIO GAZETI DUME KWA SASA NCHINI TANZANIATanzania daima? Source ina walakini.
Mkuu huyo wacha kuhangaika naye maana ni mfagiaji pale lumumbaLikishajadiliwa Bungeni mapendekezo/maazimio ya Bunge hupelekwa wapi kwa ajili ya utekelezaji ikiwa ni pamoja na wahusika kuchukuliwa hatua?
Acha kukurupuka kama hujui kaa kimya.
Muda sawa hata miaka kumi au ishirini ni muda pia ila tungesikia basi hata tetesi tu juu ya Escrow inge tupa moyo,haya majipu ni kama yana fanyiwa sorting vile.Itafahamika ni swala la muda tu.!
Teeeeeeh teeeeeeeeh umenikumbusha mzee wa wapigwe cheki alivyo lala chali chezea mkwere weye?Tanzania Daima nanyi wachokozi! Hamjui hilo jipu limekaa pabaya sana - liktumbuliwa ina maana mhusika inabidi awe ameishaandika wosia! Haya ndio yale mzee wa 'wapigwe tu' alikuwa akiyasema 'ukiwagusa nchi itayumba'.
utashangaa akisoma gazeti la udaku analiamini 100%Teeeeeeh teeeeeeeeh, unataka kijarida cha kufungia vitumbua? TANZANIA DAIMA NDIO GAZETI DUME KWA SASA NCHINI TANZANIA