Sakata la Kampuni ya Lugumi: IGP na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani watupiana mpira

Sakata la Kampuni ya Lugumi: IGP na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani watupiana mpira

Hamumjui Ngosha. N
Masikini ngosha wa watu!!!!!
Duuuh panya watakuwa wameula,nchi hii bwana

Usihofu Mkuu. Mh. Tayari ana kila kitu, taarifa zote anazo na mpaka mkataba anao. Mkwere aliwapuuzia jamaa wa nusa nusa kila wakimpelekea taarifa za kiintelejensia. Kumbe alikuwa anafanya hivyo kwa maksudi kwa kuwa yeye ndo alikuwa mpiga ngoma. Kipindi hiki Ngosha anawatumia sana Nusa nusa kwa hiyo anajua kila kitu. Hizo briefings za kila siku kutoka kwenye vyombo vyake anazifanyia kazi. Hatokubali watu 50,000 waumize population ya watu mil 50. Mungu akupe Maisha Marefu Mh. Rais uwapiganie watanzania
 
Kuanzia former prez,mtoto,igp, lugumiz wote majipuu ktk sakata hilo,shida ni moja hakuna ambaye anaweza kulitumbuaaa jipuz hilo.
Sana Sana hayo matume yakatayoundwa na wanasiasa wataishiaaa kupiga makelele tu
 
Mkuu bado unawaamini hawa jamaa? katika miaka 10 ya utawala wa awamu ya nne pamoja na kushamiri sana kwa ufisadi na upokeaji rushwa walifanya nini? Usitegemee jipya kutoka kwa hawa si ajabu bajeti yao imeshakatwa kwa 80% watahangaika na vidagaa tu lakini mapapa wa ufisadi nchini kamwe hawawezi kuwasogelea karibu.
Ndio maana unaona hizi dana dana zote zinaendelea

Watanzania wangejiuliza kwanza kabla ya kujadili huu mpira wanaotupiana

Vifaa vilivyotarajiwa kununuliwa ni vitendea kazi vya Polisi
Mkuu wa jeshi la Polisi alipaswa kujua mradi wa vitendea kazi vyake unakwendaje

Hapa angejiuliza, kama mradi ulikuwa wa vituo zaidi ya 100 nchini, iweje vituo 14 ndivyo vipate huduma tarajiwa kama ilivyoandikwa na gazeti moja?

Angeangalia bajeti na kuwasiliana na wahusika haya yasingefika hapa.
Kwa maneno mengine, mkuu wa jeshi hakuwa na taarifa wala kujua mkataba
Tumefikaje hapa!

Pili, Watanzania wajiulize, kulipokuwa na harufu za ufisadi bandarini timu iliondoka mapema tena wakiwa na nyaraka zote za kuonyesha makontena yaliyopita hadi walinzi.
Vipi kuna kigugumizi kutafuta ukweli wa suala hili?

Tatu, tuliona habari za mita za mafuta zikiibuliwa na wahusika kutakiwa kujieleza.
Vipi hili lina kigugumizi na wale wale waliokuwa wanashangiliwa hawaonekani?

Nne, kashfa kama hii si ndogo. Inahusisha jeshi la Polisi wenye dhamana kubwa katika jamii. Ni wakati serikali itoke na kueleza wananchi nini hasa kimetokea.

Iwe ni uzushi basi ielezwe, iwe ni ukweli ielezwe, tumezoa mikataba ya magumashi
Huu utumbuaji mbona umejikita katika vijipu uchungu, matambazi hayaguswi?

Watu ni wale wale na sera ni zile zile za kulindana. Wanafeli !!

Nyani Ngabu The Boss Mzee Mwanakijiji Mag3
 
Mkuu bado unawaamini hawa jamaa? katika miaka 10 ya utawala wa awamu ya nne pamoja na kushamiri sana kwa ufisadi na upokeaji rushwa walifanya nini? Usitegemee jipya kutoka kwa hawa si ajabu bajeti yao imeshakatwa kwa 80% watahangaika na vidagaa tu lakini mapapa wa ufisadi nchini kamwe hawawezi kuwasogelea karibu.
mkuu natangaza hadharani furaha kubwa sana niliyonayo baada ya kusoma andiko lako humu tena , nilipatwa na mashaka makubwa sana kutokana na kimya chako , BAK is back , Welcome home mkuu , thank you god .

Nakala kwa Chakaza
 
Hawa nao wajinga sana, wamepewa mkataba mnono na kwa zaidi ya miaka mitano wameshindwa kufunga mashine ktk kila wilaya sawa sawa na mkataba wanategemea nini eti!!??

Aisee, acha tu watumbuliwe.......hakuna jinsi nyingine!!
Ukishakuwa mdhulumati huwezi fanya mambo ya halali
 
Mhh! Ngoja tusubiri Jipu uchungu hili
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,Ernest Mangu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya ndani,Jaji Meja Jenerali Projest Rwegasira, wameripotiwa kutupiana mpira kuhusu kuhusu ni nini kimesababisha kutokuwasilishwa kwa mkataba huo kwa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali siku ya jana.

Mangu anasema: "Iliyoagizwa ni wizara kwahiyo siwezi kuzungumza kwa niaba ya wizara na hiyo siku Katibu Mkuu alikuwepo."

Alipoulizwa kwamba,kwa upande wao wamekwishawasilisha mkataba huo wizarani alisema: "Kwani anayesaini mkataba si katibu mkuu,hivyo wasaliana na ofisi ya katibu mkuu au waziri."


Gazeti lilimtafuta Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ambae alisema: "Ninaomba uwasiliane na IGP."

Baada ya kauli hiyo,Tanzania Daima lilimweleza kwamba IGP Mangu amesema atafutwe Katibu Mkuu kwani siku hiyo alikuwapo(siku walipokutana na kamati ya PAC) ambapo Rwegasira alisema: "IGP atoe maelezo siyo Katibu Mkuu,kwani hata siku hiyo tulipokwenda aliyekuwa anajibu maswali ni IGP siyo mimi."

Alipoulizwa ulipo mkataba huo,Katibu Mkuu huyo alisema: "Hata kama ofisi yetu ndiyo inasaini mkataba,lakini suala hilo lilielekezwa moja kwa moja kwa IGP ambae alikuwa anajibu."

"Mimi nategemea aliyeambiwa kupeleka ni IGP,huu ni uelewa wangu na kama alijua hana angeeleza kwamba hana ili kamati ya Bunge itoe maelezo ya jinsi ya kumsaidia kuupata." aliongeza Rwegasira.

Baada ya ufafanuzi huo wa Rwegasira,Tanzania Daima lilimtafuta kwa mara nyingine IGP Mangu ambae hakupatikana kwani simu yake ya kiganjani ilikuwaa ikiita bila kupokelewa.

Chanzo: Tanzania Daima

Bora ya yule mama!
 
Halafu cha kushangaza wakati sakata hili likiendelea Magufuli na Majaliwa wamepiga kimya kama haliwahusu. HAPA KAZI TU! 🙂

Ndio maana unaona hizi dana dana zote zinaendelea

Watanzania wangejiuliza kwanza kabla ya kujadili huu mpira wanaotupiana

Vifaa vilivyotarajiwa kununuliwa ni vitendea kazi vya Polisi
Mkuu wa jeshi la Polisi alipaswa kujua mradi wa vitendea kazi vyake unakwendaje

Hapa angejiuliza, kama mradi ulikuwa wa vituo zaidi ya 100 nchini, iweje vituo 14 ndivyo vipate huduma tarajiwa kama ilivyoandikwa na gazeti moja?

Angeangalia bajeti na kuwasiliana na wahusika haya yasingefika hapa.
Kwa maneno mengine, mkuu wa jeshi hakuwa na taarifa wala kujua mkataba
Tumefikaje hapa!

Pili, Watanzania wajiulize, kulipokuwa na harufu za ufisadi bandarini timu iliondoka mapema tena wakiwa na nyaraka zote za kuonyesha makontena yaliyopita hadi walinzi.
Vipi kuna kigugumizi kutafuta ukweli wa suala hili?

Tatu, tuliona habari za mita za mafuta zikiibuliwa na wahusika kutakiwa kujieleza.
Vipi hili lina kigugumizi na wale wale waliokuwa wanashangiliwa hawaonekani?

Nne, kashfa kama hii si ndogo. Inahusisha jeshi la Polisi wenye dhamana kubwa katika jamii. Ni wakati serikali itoke na kueleza wananchi nini hasa kimetokea.

Iwe ni uzushi basi ielezwe, iwe ni ukweli ielezwe, tumezoa mikataba ya magumashi
Huu utumbuaji mbona umejikita katika vijipu uchungu, matambazi hayaguswi?

Watu ni wale wale na sera ni zile zile za kulindana. Wanafeli !!

Nyani Ngabu The Boss Mzee Mwanakijiji Mag3
 
Ahsante sana Mkuu Erythrocyte kwa kuonyesha furaha yako kubwa sana ya uwepo wangu hapa jamvini, shukrani sana.

mkuu natangaza hadharani furaha kubwa sana niliyonayo baada ya kusoma andiko lako humu tena , nilipatwa na mashaka makubwa sana kutokana na kimya chako , BAK is back , Welcome home mkuu , thank you god .

Nakala kwa Chakaza
 
Ahsante sana Mkuu Erythrocyte kwa kuonyesha furaha yako kubwa sana ya uwepo wangu hapa jamvini, shukrani sana.
Duh, BAK, umetokea wapi tena! Karibu sana, nilianza kuingiwa na wasiwasi kuhusu uwepo wako humu. Naomba nikupe tahadhari moja tu, viwavi vingi vimemwagwa humu na wapo wenzetu wachache wamesalimu amri na kuweka silaha chini kwa ule mtindo wa if you can't fight them, join them.

Taasisi za serikali zilizokuwa mstari wa mbele zikihusishwa na ufisadi bado ziko pale pale...Jeshi la Polisi lipo pale pale, jukumu lao kubwa kwa sasa ni kuwashughulikia wanaokosoa serikali. Badala ya kuwalinda raia wema na mali zao, wamejikita katika kukilinda chuo cha Mafisadi na wahitimu wake!
 
Back
Top Bottom