Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Kuingia kwenye mkumbo itakuwa mbaya sana .Ila zinatakiwa data kwa watu wenye nyeti wazilete tuzidi kuwasha moto . Jamaa hawa ni wajanja na kweli issue serious zinaanza kuzimika bila ya ufumbuzi are we going to be the same wa kulala na kuwaka na issue kwa muda ?
 
Is management African problem? Even the so called supper-power of Africa, management is a problem.. What is happeninng here? It never happened before!

Posted to the web on: 19 January 2007
SA firms look to generators in power crunch
Reuters

SOUTH African companies facing a power crunch are turning to generators as the country gears up to host the Soccer World Cup in 2010.

Blackouts engulfed much of the country on Thursday, crippling business in major cities amid warnings from the state utility Eskom that unexpected cuts could stretch into next week.

Companies fearful of losing more business in future crises are not taking any chances and are launching plans to pour money into their own power generation.

Absa, SA’s biggest retail lender, was forced to close 27 branches and 170 ATM machines during the cuts. "We are taking this very seriously and making contingency plans to buy generators for branches across the country," said Absa spokeswoman Phillipa-Jane Vermoter.

Power woes have raised political temperatures in the past, with critics accusing government of failing to address the energy crunch plaguing the country. Demand shows no sign of letting up as an economic boom pushes mothballed power plants purchased in the 1970s and 80s beyond capacity.

Analysts say it could take up to 10 years to fix the problem, time that SA does not have as it tries to prepare for the World Cup and keep foreign investors happy. Azar Jammine, chief economist at Econometrix Treasury Management, estimates the country will need a new power station every three years at a cost of $6bn.

While industrial giants may have invested in generators, smaller companies remain vulnerable to unpredictable cuts, especially ahead of the peak season in five months. "It is the companies who don’t have the capital to invest in generators that will suffer," said Jammine.

"Companies like ours that depend heavily on computers will face difficulties. When there are power cuts everyone might as well go home." Eskom, which has been under pressure to repair ageing infrastructure, promised to cut as little power as possible on Friday after an unplanned outage of 4 600MW.

Some big companies like Virgin Atlantic Airways anticipated more energy troubles. It purchased a giant four-room generator three years ago. "We just can’t afford to have communications with customers cut off," said general manager Peter Barry.

SA plans to spend billions of dollars to shore up the electricity grid in industrial centre Johannesburg. Eskom will borrow up to €300m from the European Investment Bank (EIB) to help it improve power transmission.

"We feel they are getting their priorities right and that’s why we gave them the financing," said David Ivan White, head of Regional Representation at EIB.

Network advertising company is not so sure after shutting down for half a day on Thursday. It has no generators, but that might change. "This is a serious issue we are looking at. I can’t remember how many times power cuts have hit our business," said Chris Groenewald, of its information technology unit.
 
Hii itawapa kichwa kweli CCM; watasema hata Afrika Kusini kuna matatizo ya umeme. Kwa hiyo ni ya kawaida, acha kabisa, hii ni habari mbaya sana.
 
Mwanasiasa

Sifikirii kuwa hii ni habari mbaya. Cha msingi ni kuwa wazi na matatizo yanayotokea na kutatuliwa kwa ufasaha. Sitegemei south Africa watanunua majenerator kutoka Richmonduli? Hawawezi kufanya yale ambayo Tanzania tumefanya. Watakwenda kwa makampuni yenye uwezo wa kutatua shida yao.

Sisi tulikwenda kuwaneemesha Richmonduli and company - HILO SIO SAHIHI.
 
Dua
mawazo yako ni ya msingi pale ambapo wananchi wake wanaweza kuainisha mambo. Kwa Wadanganyika inatosha mno kwenda na article hiyo kwenye mkutano wa hadhara na kusema si unaona hata huko. Kumbuka jinsi JK alivyotoa pumba zake eti hata Tokyo kuna ujambazi, kwa nini tushangae ujambazi Bongo. Au jinsi Richmonduli alivyorudi kutoka Canada na kudai kuwa hata Canada kuna mgao wa umeme!!
Si utaratibu wa watawala wetu kujifunza mazuri ya watu wengine maana upeo huo hawana au basi ukaidi tu. Lakini ni wepesi mno wa kuchukua mabaya ya watu wengine kuhalalisha kuharibu kwao
 
Mamlaka haina taarifa za mzimu wa Richmond
Na Midraji Ibrahim
KAMATI ya Bunge ya Fedha na Uchumi imeijia juu Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), baada ya kutoa maelezo kwamba haifahamu jinsi utaratibu wa utoaji wa zabuni za Kampuni ya Richmond Development Corporation na Aggreko International ulivyokwenda kwa madai kwamba zilitolewa kabla haijaanza kazi.
Wiki iliyopita kamati hiyo kupitia Makamu Mwenyekiti wake, Adam Malima, iliitaka PPRA kuwasilisha kwenye kamati hiyo taarifa ya kina inavyoonyesha kwa kina namna kampuni za Richmond na Aggreko zilivyoshinda zabuni za kuzalisha umeme wa dharura.
Hatua hiyo inaelezwa kuchukuliwa na kamati hiyo kutokana na wabunge kutilia shaka utaratibu mzima wa utoaji zabuni hizo na hasa jinsi utendaji wa Richmond ulivyosuasua kabla ya kuuza mkataba huo kwa kampuni ya Dowan's.
PPRA ilitakiwa kuwasilisha taarifa hiyo jana, lakini ilitoa taarifa kwenye kamati hiyo iliyodai kwamba haifahamu utaratibu uliofuatwa katika kutoa zabuni hizo kwa sababu ilikuwa haijaanza kazi.
"Hawa watu wanasikitisha na kushangaza sana, iweje waseme hawafahamu utaratibu ulivyokwenda wakati baadhi ya wajumbe wa PPRA wametoka Bodi Kuu ya Zabuni?" alihoji Mbunge mmoja ambaye hakutaka jina lake kutajwa.
Baadhi ya Majukumu ya kisheria ya Mamlaka hiyo iliyoanza kazi rasmi Mei mosi 2005 ni kutoa na kuhifadhi taarifa muhimu kuhusu zabuni zinazoendeshwa nchini, kusuluhisha migogoro na malalamiko ya zabuni pamoja na kutoa nyaraka za zabuni na miongozo mbalimbali ya kuendesha shughuli za zabuni.
Baada ya wajumbe kuonyesha kukerwa na hatua ya PPRA kujivua kuhusika na suala hilo, waliagizwa kuandaa upya taarifa hiyo kisha kuiwasilisha kwa kamati mjini Dodoma katika kikao kijacho cha Bunge kinatarajia kuanza Januari 30.
PPRA ilitakiwa kufanyia marekebisho taarifa yake iliyoiwasilisha kwenye kamati hiyo kutokana na upungufu kadhaa, pia kuwasilisha taarifa zote za ununuzi zilizofanywa na Tanesco kama shirika la umma lenye maslahi makubwa kwa jamii.
Kampuni hizo zilipata zabuni hizo ili kuzalisha umeme wa dharura baada ya ukame kusababisha upungufu wa maji kwenye mabwawa mbalimbali yanayotumika kuzalisha umeme nchini.
PPRA, kulingana na sheria ya ununuzi ya mwaka 2004, kifungu cha 9 ina madaraka ya kuanzisha uchunguzi wa suala linalotiliwa wasiwasi bila kuomba kibali kutoka kwa Waziri wa Fedha isipokuwa katika masuala ya kijeshi na usalama.
Richmond ina mkataba wa kuzalisha megawati 100, lakini imekuwa ikikumbwa na matatizo katika utekelezaji wa mkataba wake hadi ilipouzwa kwa kampuni ya Dowan's. Mradi utagharimu dola za Marekani 172,500,000 (sawa na Sh225 bilioni).

Kwa upande wa Aggreko ilipewa zabuni ya kuzalisha megawati 40 ambazo tayari zimezalishwa na kuingizwa kwenye gridi ya taifa. Mkataba wake ni wa dola za Marekani 61 milioni (sawa na Sh 77.4 bilioni).
Kwa mujibu wa sheria hiyo, Mamlaka inapaswa kuhakikisha kwamba ununuzi unafanywa kwa kuzingatia usawa katika kushiriki kwa uwazi na bila ubaguzi na taratibu hizo ziiwezeshe serikali kupata thamani ya vifaa na huduma inayolingana na pesa zilizotumika.
 
Nafikiria wakati wa kuwadanganya wabongo umekwisha. Wengi wao hivi sasa ni waelewaji wa mambo, kitu ambacho kinakosekana ni ujasiri wa kuamini kwamba wanaweza kubadili mwelekeo wa serikali ambayo wameichagua.

Kila kitu kina mwanzo na mwisho na huko tunakokwenda ishara zote zinaonyesha uongo wa kitoto ambao viongozi wetu wamezoea kuutoa kama ule wa wizi Japan au hata Canada umeme unakatika ni mabo ambayo wabongo wengi wanafahamu fika ni hadithi za pwagu na pwaguzi - ukitaka kutathmini hilo nenda vijijini leo uone jinsi viongozi wanavyosutwa wakati Richimonduli anapotembelea, viongozi wanazomewa. Hata maandamano ya juzi ambapo kuna bango ambalo lilisema Richmonduli afukuzwe au JK aondoke naye siyo kitu kidogo hiki. One year ago hakuna mtu ambaye angetabiri hili lakini limetokea na sasa njia nyeupe, waswahili walisema mwanzo mgumu maandamano mengi zaidi na makubwa yanafuata ambayo yataandaliwa vema na mambo yataanza kubadilika.

Hatuwezi kukaa kimya wakati watu wachache waliopewa dhamana serikalini wanajitajirisha kama vile wenye mali hatujali. Richmonduli inabidi afukuzwe na baada ya hapo wale wote waliotuingiza kwenye mikataba hewa. wabongo wanalijua hili na ni wao pekee ndio wataweza kufanya haya mabadiliko hivyo ni lazima tuwaamini.
 
To: Dua
From: Invisible

Re: Notification

Nadhani huna taarifa juu ya Richmond kuachia ngazi kwenye mkataba husika na kupunguza kelele zilizopigwa sana. Kwa kumbukumbu nilizo nazo (sikumbuki tarehe) waliondoka mwaka jana na kazi hiyo imeuzwa. Nikipata full details nitakupa lakini hii ni taarifa tu kwani umesema: Richmonduli inabidi afukuzwe...

Shukrani...
 
TO: Invisible

Re: NOTIFICATION

Rejea maandiko ya Dua hapo juu...

Napenda kukufahamisha kuwa kuna Richmond na Richmonduli. Richmond ndiyo waliouza mkataba wao kwa Dowans Holding. Richmonduli ni jina la mtu!
 
Wow...!
That's a nice info. I had an inverse meaning then! Umesababisha nicheke japo nipo alone hapa. Nashukuru kwa kunijuza naamini kweli sikuwa updated siku nyingi. Nakuwa occupied sana na tangu December mwaka jana sikuwa online sana sana... Ndo naisoma hii nikachukulia ni Richmond japo pia sikuwa na data za kutosha kwani sikuwa hapa in deep.

Thanks and regards!
 
Warithi wa Richmonds mahakamani
Wabunge kutembelea eneo la mradi leo

Na Waandishi Wetu Uhuru publications

WAFANYAKAZI waliotimuliwa kampuni ya Dowans SA, wameenda katika Mahakama ya Kazi kuwasilisha malalamiko yao kuhusu stahiki zao kikazi, imebainika.
Wakati hayo yakijitokeza leo Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara, inatembelea miradi ya dharura ya uzalishaji wa umeme ili kujionea hali halisi.
Kwa upande wa wafanyakazi, wameichukua hatua hiyo kutokana na kutoridhishwa na 'mafao' waliyopewa na jinsi haki ya ajira yao ilivyochukuliwa na wawekezaji hao, waliotwaa majukumu ya kampuni ya Richmonds Develepment.

"Tumeenda Mahakama ya Kazi na nadhani tutaenda kuchukua barua zetu (ya kuanza shauri)," alisema mfanyakazi mmoja alipozungumza na gazeti hili jana.
Kwa mujibu wa habari ambazo gazeti hili imelipata, waajiriwa hao wa Dowans walienda mahakamani kutafuta haki, baada ya kulipwa sh. 80,000 kila mmoja ikiwa ni baada ya kutoa shinikizo la kudai haki yao.

Mfanyakazi huyo, alisema walichukua hatua ya kwenda mahakamani baada ya mmoja ambaye ni mlinzi kulipwa sh. 60,000 na mwingine ambaye aliongezewa majukumu ya uhudumu, alikuwa analipwa sh. 85,000.
Waajiriwa hao walianza ajira tangu zama za kampuni ya Richmonds, ambapo iliuza shughuli na mali zake kwa Dowans.
Haijajulikana maudhui ya mkataba wa mauzo ya Richmonds kwa Dowans na mkataba mkuu na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) uliowezesha Richmonds kupewa kandarasi.
Pia, mmoja wa wafanyakazi hao kabla ya kuchukua hatua, alisema walimfuata mwajiri wao wa zamani, aliyekuwa Meneja Mradi wa Richmonds, Naem Gire, ambaye aliwapa baraka kwamba wana haki ya kwenda kwenye sheria, iwapo wataona kuna haja ya kufanya hivyo. Gire yupo nchini tangu mwisho wa wiki iliyopita.

Hii ni mara ya pili kwa Gire kutoa kauli ya kuitaka Dowans iwalipe wafanyakazi aliowaajiri Septemba mwaka jana. Mara ya kwanza alifanya hivyo mwezi uliopita akiwa nje ya nchi na uongozi wa Dowans ulitii.
Katika hatua nyingine, Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara, leo inatembelea miradi ya dharura ya uzalishaji wa umeme ili kujionea kama kuna kazi yoyote inayofanyika kwa mujibu wa mkataba.Wakati kamati hiyo imeamua kufanya ziara hiyo, wajumbe wake pia wametaka kuundwa kwa tume kuchunguza kwa nini Richmonds ilipewa kazi ya kuzalisha umeme wa megawati 100 wakati haikuwa na uwezo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dk. Harrison Mwakyembe alisema jana kuwa uamuzi wa kutembelea miradi hiyo unafuatia kikao cha jana baina yake na Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO.


Alisema kamati itafanya ziara hiyo katika eneo la Ubungo, Dar es Salaam ambako kampuni ya Dowans SA inaendeleza miradi hiyo baada ya kampuni ya Richmonds kushindwa.

"Baada ya kujadiliana kwa muda, kamati imeona ni vyema ikaenda kujiridhisha na kazi inayoendelea na hatimaye kupata jibu la uhakika, tofauti na ambavyo imekuwa ikielezwa," alisema.
Richmonds iliingia mkataba na serikali kwa ajili ya kuzalisha umeme wa megawati 100 lakini ilishindwa kufanya hivyo na ilidai kufanikisha kuzalisha megawati 20 tu.
Kampuni hiyo iliuza kazi kwa Dowans ambayo pia imekuwa ikisuasua kutekeleza mradi huo ambao kwa mujibu wa ahadi unatakiwa kukamilika takriban wiki tatu zijazo.
Katika hatua nyingine, wajumbe wa kamati walitaka kuundwa kwa kamati ili kuchunguza sababu zilizofanya Richmonds kupewa kazi ya kuzalisha nishati hiyo wakati wa mgawo mwaka jana.

Habari kutoka ndani ya kamati hiyo, zilieleza kwamba wajumbe hao ambao ni wabunge, walionyesha nia hiyo wakati wa mjadala uliodumu kwa zaidi ya saa nne kati ya kamati na TANESCO.
Wakizungumza kwa masharti ya kutokutajwa majina, wabunge hao walisema katika kikao hicho walichachamaa na kuibana bodi ya TANESCO kujua ni kwa nini ilikubali kuingia mkataba na kampuni hiyo huku ikijua haina uwezo wa kuzalisha hata megawati moja.

Hata hivyo, kwa mujibu wa wajumbe hao, TANESCO ilidai ilifanya hivyo kwa kufuata maagizo kutoka kamati ya majadiliano ya kimataifa ambayo inajumuisha makatibu wakuu wa wizara kadhaa, akiwemo wa Wizara ya Nishati na Madini.
Vile vile, wajumbe wa kamati waliibana TANESCO kueleza kwa nini imeamua kupandisha bei ya umeme ambapo ilijibiwa kuwa ni kutokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji na ununuzi kutoka kwa kampuni zinazozalisha nishati hiyo.
 
Warithi wa Richmonds mahakamani

Wabunge kutembelea eneo la mradi leo

Na Waandishi Wetu

WAFANYAKAZI waliotimuliwa kampuni ya Dowans SA, wameenda katika Mahakama ya Kazi kuwasilisha malalamiko yao kuhusu stahiki zao kikazi, imebainika.

Wakati hayo yakijitokeza leo Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara, inatembelea miradi ya dharura ya uzalishaji wa umeme ili kujionea hali halisi.

Kwa upande wa wafanyakazi, wameichukua hatua hiyo kutokana na kutoridhishwa na 'mafao' waliyopewa na jinsi haki ya ajira yao ilivyochukuliwa na wawekezaji hao, waliotwaa majukumu ya kampuni ya Richmonds Develepment.

"Tumeenda Mahakama ya Kazi na nadhani tutaenda kuchukua barua zetu (ya kuanza shauri)," alisema mfanyakazi mmoja alipozungumza na gazeti hili jana.

Kwa mujibu wa habari ambazo gazeti hili imelipata, waajiriwa hao wa Dowans walienda mahakamani kutafuta haki, baada ya kulipwa sh. 80,000 kila mmoja ikiwa ni baada ya kutoa shinikizo la kudai haki yao.

Mfanyakazi huyo, alisema walichukua hatua ya kwenda mahakamani baada ya mmoja ambaye ni mlinzi kulipwa sh. 60,000 na mwingine ambaye aliongezewa majukumu ya uhudumu, alikuwa analipwa sh. 85,000.

Waajiriwa hao walianza ajira tangu zama za kampuni ya Richmonds, ambapo iliuza shughuli na mali zake kwa Dowans.

Haijajulikana maudhui ya mkataba wa mauzo ya Richmonds kwa Dowans na mkataba mkuu na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) uliowezesha Richmonds kupewa kandarasi.

Pia, mmoja wa wafanyakazi hao kabla ya kuchukua hatua, alisema walimfuata mwajiri wao wa zamani, aliyekuwa Meneja Mradi wa Richmonds, Naem Gire, ambaye aliwapa baraka kwamba wana haki ya kwenda kwenye sheria, iwapo wataona kuna haja ya kufanya hivyo. Gire yupo nchini tangu mwisho wa wiki iliyopita.

Hii ni mara ya pili kwa Gire kutoa kauli ya kuitaka Dowans iwalipe wafanyakazi aliowaajiri Septemba mwaka jana. Mara ya kwanza alifanya hivyo mwezi uliopita akiwa nje ya nchi na uongozi wa Dowans ulitii.

Katika hatua nyingine, Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara, leo inatembelea miradi ya dharura ya uzalishaji wa umeme ili kujionea kama kuna kazi yoyote inayofanyika kwa mujibu wa mkataba.

Wakati kamati hiyo imeamua kufanya ziara hiyo, wajumbe wake pia wametaka kuundwa kwa tume kuchunguza kwa nini Richmonds ilipewa kazi ya kuzalisha umeme wa megawati 100 wakati haikuwa na uwezo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dk. Harrison Mwakyembe alisema jana kuwa uamuzi wa kutembelea miradi hiyo unafuatia kikao cha jana baina yake na Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO.
Alisema kamati itafanya ziara hiyo katika eneo la Ubungo, Dar es Salaam ambako kampuni ya Dowans SA inaendeleza miradi hiyo baada ya kampuni ya Richmonds kushindwa.

"Baada ya kujadiliana kwa muda, kamati imeona ni vyema ikaenda kujiridhisha na kazi inayoendelea na hatimaye kupata jibu la uhakika, tofauti na ambavyo imekuwa ikielezwa," alisema.

Richmonds iliingia mkataba na serikali kwa ajili ya kuzalisha umeme wa megawati 100 lakini ilishindwa kufanya hivyo na ilidai kufanikisha kuzalisha megawati 20 tu.

Kampuni hiyo iliuza kazi kwa Dowans ambayo pia imekuwa ikisuasua kutekeleza mradi huo ambao kwa mujibu wa ahadi unatakiwa kukamilika takriban wiki tatu zijazo.

Katika hatua nyingine, wajumbe wa kamati walitaka kuundwa kwa kamati ili kuchunguza sababu zilizofanya Richmonds kupewa kazi ya kuzalisha nishati hiyo wakati wa mgawo mwaka jana.

Habari kutoka ndani ya kamati hiyo, zilieleza kwamba wajumbe hao ambao ni wabunge, walionyesha nia hiyo wakati wa mjadala uliodumu kwa zaidi ya saa nne kati ya kamati na TANESCO.

Wakizungumza kwa masharti ya kutokutajwa majina, wabunge hao walisema katika kikao hicho walichachamaa na kuibana bodi ya TANESCO kujua ni kwa nini ilikubali kuingia mkataba na kampuni hiyo huku ikijua haina uwezo wa kuzalisha hata megawati moja.

Hata hivyo, kwa mujibu wa wajumbe hao, TANESCO ilidai ilifanya hivyo kwa kufuata maagizo kutoka kamati ya majadiliano ya kimataifa ambayo inajumuisha makatibu wakuu wa wizara kadhaa, akiwemo wa Wizara ya Nishati na Madini.

Vile vile, wajumbe wa kamati waliibana TANESCO kueleza kwa nini imeamua kupandisha bei ya umeme ambapo ilijibiwa kuwa ni kutokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji na ununuzi kutoka kwa kampuni zinazozalisha nishati hiyo.
 
hakuna kitu cha kuchekesha na kinachofurahisha jamii kama mazingaombwe! Wakati watanzania wanalalamika na kuhoji maswali, wakati Richmond bado walikuwa wanatoa ahadi hewa, wakati Rais anatoa ahadi zisizotimizika na kuonekana kituko hii Kamati ilikuwa wapi? Kama kweli hili suala limewagusa kwanini wasubiri mwaka mmoja baadaye. Kwanini Kamati hii ya Bunge letu tukutu haiitishi kama kwa dharura kikao cha kuangalia mkataba wa Richmond. Wahusika wote wapo Tanzania, ripoti ya mwaka 2006 waisubiri mwezi Novemba, lakini ripoti ya Richmond waitafutie majibu yake sasa!!!
 
Mambo yanazidi kuendelea...
Habari hii ni kwa mujibu wa Uhuru.

Wabunge wawatilia shaka 'walioinunua' Richmonds

Umeme bado kuingizwa kwenye gridi
NA WAANDISHI WETU
KAMATI ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara, imesema hairidhishiwi na utendaji wa kampuni ya Dowans Holdings SA Limited iliyopewa kazi ya kuzalisha megawati 100 za umeme wa dharura.
Wabunge hao pia wameitaka kampuni ya Richmonds Development Corporation (iliyoiuzia kazi hiyo Dowans) kusafisha jina la Tanzania, kufuatia kauli yao kuwa gesi ya Tanzania ni chafu ndiyo maana walishindwa kuanza kazi mara moja.
Akizungumza wakati wa majumuisho ya ziara jana, Makamu Mwenyekiti wa kamati, Dk. Harrison Mwakyembe alisema hali ambayo wameiona katika maeneo ya miradi ni ya kukatisha tamaa, hivyo kuonyesha wasiwasi kama itatimiza masharti.
"Utendaji wa kampuni hii hauridhishi hata kidogo. Kama kamati tutaandaa ripoti na kuiwasilisha mbele ya Bunge katika kikao kijacho (kinachoanza Jumanne ijayo). Lengo ni kutaka umma uelewe kinachoendelea," alisema.
Alisema kamati yake itaendelea kufuatilia suala la kampuni hiyo kwa kuwa linagusa maslahi ya taifa, na kwamba kutokufanya hivyo ni kutowatendea haki wananchi.
Katika ziara hiyo ya Kamati ya Bunge, wajumbe walitembelea miradi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na ile ya dharura ambayo inaendeshwa na kampuni binafsi zilizopewa kazi ya kuzalisha umeme.
Baada ya kufika katika eneo la awali la mradi wa kuzalisha megawati 20, wabunge walipatwa na mshangao baada ya kuelezwa kuwa kiwango hicho hakizalishwi kama inavyopaswa. Dowans inazalisha kati ya megawati 18 na 19 tu.
Mbali na kutozalishwa kwa kiasi kinachotakiwa kwa mujibu wa mkataba, umeme huo bado haujaingizwa kwenye gridi ya taifa kwa kuwa mashine bado ziko kwenye majaribio.
Wasiwasi mwingine uliojitokeza katika ziara hiyo ya Wabunge ni ukamilishaji wa awamu ya pili ya mradi unaoendelezwa na Dowans kwa kuwa hakuna dalili za kazi hiyo kukamilika kama ilivyoelezwa kwa mujibu wa mkataba.
Meneja ujenzi wa Dowans, Carlos Gaset, alishindwa kueleza lini mradi huo unaweza kukamilika licha ya kutoa makadirio tu.
Licha ya kukatishwa tamaa na Dowans, Kamati ya Bunge ilisifu kazi inayofanywa na kampuni ya Aggreko ambayo tayari inazalisha umeme wa dharura megawati 40.
Katika hatua nyingine, wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara wameitaka kampuni ya Richmonds kuisafisha Tanzania kutokana na taarifa yake kuwa gesi ya Tanzania ilikuwa chafu.
"Walitoa taarifa kuwa hawakuanza kazi kutokana na gesi kuwa chafu. Sasa tunaomba taarifa ya kina juu ya hili la sivyo tutachukua hatua kwa vile wametuchafua kwa kauli yao hii," alisema Mbunge wa Hai (CCM), Fuya Kimbita.
Kimbita alisema inashangaza kuona kampuni hiyo ilitoa kauli hiyo wakati kampuni zingine zinatumia gesi hiyo hiyo. Meneja Mkuu Uzalishaji wa TANESCO, Stephen Mabada alisema taarifa hiyo haikuwa na ukweli wowote.
Kauli hiyo ya Kimbita pia iliungwa mkono na Mohamed Habib Mnyaa wa Mkanyageni (CUF), Lucy Owenya (Viti Maalum-CHADEMA) na Siraju Kaboyonga wa Tabora Mjini (CCM).
Walisema TANESCO na serikali hawana budi kuichukulia kauli hiyo kwa uzito wa aina yake kwa kuwa inaharibu sifa ya Tanzania juu ya nishati inayozalisha.
 
Inasikitisha kuona kuwa watu waliopishwa kuilinda na kuitetea Katiba wanapiga soga!! CCM siku ya kuanguka kwenu... mtalia kilio cha mbwa koko!! maana mambo mengine hata hayaingii akilini..

Tuliposema Richmond ni kampuni hewa mlisema nini? Tulipouliza hawa Dowans wanatoka Uarabuni au AFrika ya Kusini mlijibu nini? Tuliposhangaa inakuwaje mkataba huu uuzwe kinyemela mliiitisha waandishi wa habari na kutuambia nini!! Waswahili walisema "laana nyingine ni za kujitakia"!! Namalizia makala yangu moja (siyo ile special...).. wanachofanya CCM kitawekwa kwenye maudhui yake!!
 
DOWANS[RICHMONDKIKWEROST]WASHINDWA KUFIKIA MALENGO ,KUANZIA KESHO KUTAKIWA KULIPA 10 MILLION USD/DAY[/B]

kamati ya bunge imeelezwa kuwa leo kuwa kampuni ya rishmond au dowans tayari wameshindwa kutimiza mkataba wa kuleta 100mw kufikia leo so kuanzia kesho na kutokana na mkataba watatakiwa kuilipa tanesco usd 10,000,000/day..mpaka watakapoingiza 100mw kwenye grid.

sasa naomba tuanze kutupa mawe kuhakikisha kweli hawa kina richmondkikwerost watidhinisha kampuninyao ilipe hiyo pesa...tudai ni haki ya watanzania kulipwa hii fidia ..kumbukeni machungu tunayopata kwa kulipa usd almost 7million/month kwenye mikataba ya nishati hata bila kutumia umeme ,,tushikie bango hili ...
 
Mliyoko jikoni tafadhalini sana sana tupeni nyeti kwa uhakika . Maana hapa mauza uza ni mengi . Mwakyembe ni mpambe na mpenda madaraka namkumbuka na statement yake dhidi ya CUF kisa anakwenda kuwa Mbunge EA wakati ule .Kamati hii haina mpinzani hata mmoja kaeni macho .
 
Mzimu wa Richmond kuibuka bungeni

Na Mwandishi Wetu

WABUNGE kadhaa wamepania kuamsha mjadala wa suala la kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond Development

Corporation (sasa Dowans) bungeni katika mkutano unaoanza keshokutwa, lakini kwa kutegemea zaidi kudra za Spika.
Hali hiyo inatokana na ukweli kwamba, hadi sasa kuna makundi mawili makubwa yenye maoni yanayokinzana kuhusu Richmond, moja

likijielekeza kutaka suala hilo liwekwe wazi lakini jingine likitaka lifunikwe kwa staili ya kulindana.

Wabunge hao wanategemea kudra za Spika, Samuel Sitta kutokana na kushindwa kutimiza kanuni za Bunge za kuwasilisha hoja binafsi

Habari kamili:
http://www.mwananchi.co.tz/mwananchisite/Mwananchi/Habari/Habari0.asp
 
Miaka Thelathini!!! Hivi ua ni Selasini au Thelathini!!?

Najua-kwamba -Unajua -kwamba -Ninajua!!

Hivi [Reach mond] Jumulisha na Rada!! Utapata shilingi ngapi zilizo Tapeliwa!!
Ndani Ya rushwa kuna utapeli!!! sasa kama Mkisanikiwa(u Kifani kiwa kufanya ivesheni) kuudhibiti utapeli basi na rushwa ita toko mea!!--Sorry Nafikiri Itakua ni Typing mistakes---au ndioa Nimefanikiwa Kugundua neno fulani la kiswahili...!!!

Hoja yangu Nikamba--Rushwa Ya rada na Richmond Izungumzwe kwa Pamoja!!!

Ina onekana walio kula rushwa ya rada ni watu wanao wajua watu wa rada!!!
Na ulinzi wa anga!!- sorry ni watu wanao wajua matapeli wa rich mond!!!
Kama walifanikawa Kusanikiwa basi kesi moja ita muokoa!! au Kinyume chake...

vingozi wa africa Mmefanya kazi nzuri sana!!lakini mna jua kwamba Dunia hii ime tusaidia sana!!....???
 
2007-01-28 11:37:37
Na Joseph Mwendapole


Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Biashara, imeshindwa kutoa msimamo wake kuhusu uamuzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wa kupandisha bei ya umeme kwa asilimia sita.

Awali, kamati hiyo iliahidi kuwa itatoa tamko kuhusu msimamo na ushauri kwa serikali, lakini hadi tunakwenda mitamboni jana jioni haikuweza kufanya hivyo.

Kwa mujibu wa habari ambazo gazeti hili inazo, uongozi wa TANESCO na kamati hiyo juzi walikutana kwa siku nzima katika ofisi za Bunge, wakijadili masuala mbalimbali yanayohusu shirika hilo, kupanda kwa umeme ikiwa moja ya ajenda.

Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk. Harrison Mwakyembe alipoulizwa jana kuhusu tamko hilo, aliahidi kuzungumza baada ya kufanya ziara TANESCO.

Dk. Mwakyembe alisema kuwa ingawa mamlaka inayosimamia nishati hiyo, EWURA, imeshatoa idhini kwa TANESCO kupandisha bei ya umeme, wao kama wabunge wanao uwezo wa kushawishi isipande.

Alisema kamati yake inaridhishwa na utendaji wa baadhi ya makampuni ya kuzalisha umeme ambayo yanaendelea na kazi kwa sasa.

``Jumapili kamati yetu itakutana Dodoma ili kuangalia namna ya kufuatilia tatizo la umeme kwa maslahi ya umma, `` alisema.

Kumekuwa na malalamiko mengi kuhusu kupanda kwa gharama za umeme, ambapo baadhi ya watu, wakiwemo wabunge wamesema ni mzigo kwa wananchi maskini.

Mbunge wa Kinondoni (CCM), Bw. Idd Azan, alisema hivi karibuni kuwa katika mikutano yake mingi na wananchi, amekuwa akipokea malalamiko ya kupanda kwa bei ya umeme.

``Nimefanya mikutano kama mitatu na wapiga kura wangu, kila sehemu malalamiko ni umeme, kwa hiyo lazima tuiulize serikali tatizo ni nini,`` alisema Bw. Azan.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA), Bi. Lucy Owenya, alisema serikali inapaswa kushusha gharama hizo ili ahadi yake ya kupeleka umeme vijijini kwa ajili ya kupunguza uharibifu wa mazingira itekelezeke.

Alisema bila kufanya hivyo, wananchi wa vijijini watashindwa kumudu gharama hizo, hivyo kuendelea kukata miti kwa ajili ya kupikia.

``Wakati Net Group Solution inaingia mwaka 2002, serikali iliahidi kuwa umeme utashuka, sasa badala yake unapanda, tutauliza kwanini wanawatwisha mzigo walalahoi,`` alisema.

SOURCE: Nipashe
 
Back
Top Bottom