Sakata la Kupotea Rajab Omari Mtana na Hukumu ya Kunyongwa kwa Masheikh 10 Tanga

Sakata la Kupotea Rajab Omari Mtana na Hukumu ya Kunyongwa kwa Masheikh 10 Tanga

Utingo,
Nakuomba uwe na subra.

Anza kuusoma huu uzi toka mwanzo uelewe mkasa wa Madina.

Baada ya hapo unaweza kuja na maswali.
Ok mkuu.....nimesoma tangu mwanzo au umeshawishika kuupa sula ya udini baada ya poor judgement ya mkuu wa mkoa?

But you know majority of these people (RCs) are just poor politicians who lack tools of analysis. To me kilichofanyika ni jinai tu baada ya mnunuzi wa hiliki kukataa kulipa ushuru wa hiliki yote kijiji kimoja. Na alikuwa sahihi. Na waliomfuata mkulima walikosea maana kisheria au utaratibu unaojulikana nchi nzima anayelipia ni mnunuzi, walipaswa wahangaike na mnunuzi tu na si mkulima mwanakijiji mwenzao.

Wao ndiyo walisababisha yote yaliyotokea na damu yote iliyomwagika na itakayomwagika iko juu yao
 
Mama...
Ukisoma makala zangu na ukachangia ni vyema sana kwangu na mimi nakuahidi nitakujibu kistaarabu.

Usikae kimya.

Tatizo ninaloliona kwako ni hasira na kutoa matusi.

Hii inaharibu mjadala.

Mkuu mohamed mimi naona ungeendelea kuelezea ILI sisi tujue unachoandika kinajikita katika udini kama watu wengi wanavyodai au kulikuwa na udhalimu juu ya watu uliowataja.
Embu jaribu kueleza kwa undani kwanini liwepo neno waislamu na si watanzania ungejikita kumaliza hii stori ILI tujue kiongozi
 
Najaribu kuangalia connection ya tukio na neno 'Waislam' hata sioni. Kuna ulazima gani wa kuandika neno waislam kama sio kutafuta public sympathy? Kwa nini hukusema Wadigo au wabondei? Yani muislam akiua asihukumiwe kwa sababu ni muislam? Wew mzee unazeeka vibaya.

Yani unataka waislam wasiguswe kisa wataonekana wanaonewa. Uzuri yote haya yamefanyika ktk ardhi iliyojaa waislam ambapo ukiacha na Rais wa kipindi hicho kuwa muislam, RC alikuwa muislam na possibly migambo wa kijiji na serikali ya kijiji nayo ilikuwa ni ya Waislam. Possibly hata aliyeuawa naye alikuwa muislam.

Wew mzee hizi chuki zako uzuri umekuta nchi ni ya ki demokrasia au ni kwa sababu nchi haijapitia machafuko yoyote ya kidini au kikablia ikaona madhara yake. Wew ulitakiwa uwe ulisha shughulikiwa mapema. Ni vile tu hata hvyo watu wanakupuuza
Kbsa bwana tashwishi.....MZee huyu Ni mvuruga amani na ninashangaha sna jf kuendelea kumpa tuzo mbali mbali na kuendelea kumvuga Happ alitakiwa awe amepigwa ban life ban
 
Najaribu kuangalia connection ya tukio na neno 'Waislam' hata sioni. Kuna ulazima gani wa kuandika neno waislam kama sio kutafuta public sympathy? Kwa nini hukusema Wadigo au wabondei? Yani muislam akiua asihukumiwe kwa sababu ni muislam? Wew mzee unazeeka vibaya.

Yani unataka waislam wasiguswe kisa wataonekana wanaonewa. Uzuri yote haya yamefanyika ktk ardhi iliyojaa waislam ambapo ukiacha na Rais wa kipindi hicho kuwa muislam, RC alikuwa muislam na possibly migambo wa kijiji na serikali ya kijiji nayo ilikuwa ni ya Waislam. Possibly hata aliyeuawa naye alikuwa muislam.

Wew mzee hizi chuki zako uzuri umekuta nchi ni ya ki demokrasia au ni kwa sababu nchi haijapitia machafuko yoyote ya kidini au kikablia ikaona madhara yake. Wew ulitakiwa uwe ulisha shughulikiwa mapema. Ni vile tu hata hvyo watu wanakupuuza
mwandishi mara nyingi kwa uandishi wake amejitanabaisha kuwa ni mwislamu mwenye chuki dhidi ya wasiyo waislamu. Unaposoma makala zake ni kama unasoma makala za al-shabaab. Ni mchochezi aliyepitiliza
 
SAKATA LA KUPOTEA RAJAB OMARI MTANA KIJIJI CHA LULAGO HANDENI 2013

Waislam 10 wamehukumiwa kunyongwa kwa tuhuma za kuua mlinzi mmoja.

Kufikia hukumu hii kuna mengi na chanzo chake kilianzia katika biashara ya hiliki na malipo ya ushuru kijijini Lulago.

Ninaanza leo kueleza kisa hiki kama nilivyotafiti na kuweka kumbukumbu miaka 10 iliyopita.

Rajab Omar Mtana alikuwa mwanakijiji wa kawaida tu akiishi kijijini Lulago, Handeni kama wanavijiji wengine wanavyoishi na alikuwa na biashara yake ya kuuza hiliki kama mkulima wa zao hilo.

Siku moja akaja mnunuzi mfanyabiashara wa hiliki nyumbani kwake kununua hiliki na akamuuzia.

Yule mfanyabiashara alipokuwa anatoka na gari yake akasimama kwenye kizuizi cha kulipia ushuru.

Alipotakiwa kulipa ushuru akasema kuwa si hiliki yote amenunua katika kijiji hicho kwa hiyo hawezi kulipa ushuru wa hiliki yote.

Hapo palitokea ubishi na mfanyabiashara yule akagonga lile geti na akaondoka.

Hii ikapelekea kwa wakusanya ushuru wa hapo kijijini kwenda nyumbani kwa Rajab Omar Mtana kumkamata na kumweka chini ya ulinzi katika ofisi ya serikali ya kijiji hadi hapo atakapolipa ushuru ambao yule mfanyabiashara alitakiwa alipe.

Ndugu zake Rajab Omar Mtana wakaenda pale ofisini kwa nia ya kumtoa ndugu yao na hapo pakatokea vurugu na mapigano.

Katika mapigano hayo, mgambo ambae ndiye aliyekuwa akishughulika na kudai ushuru akauawa.

Kisa hiki cha ushuru wa hiliki ndicho kilichozua balaa kubwa la mauaji na uchomwaji moto nyumba za Waislam wa kijiji cha jirani cha Madina na kuvunjwa kwa misikiti katika vijiji ambavyo vilikuwa na idadi kubwa ya wakazi wake Waislam.

Baada ya haya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa akatoa amri kuwa hapana ruhusa tena ya sehemu hizo kuwa makazi kwa kuwa hizo ni kambi za ugaidi.

Mkuu wa Mkoa alisema mengi ambayo takriban yote yamedhihirika baadae kuwa hayakuwa na ukweli.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa wapo Al Shabab vijijini, kumechimbwa mahandaki ya vita katika vijiji na kuna silaha za kutungulia ndege nk. nk.

Mkuu wa Mkoa alizungumza na Radio Nuur, Tanga inayomilokiwa na Msikiti wa Ibadh.
Nilifunga safari hadi Radio Nuur Tanga kwa nia ya kupata taarifa kamili yalivyorushwa.

Radio Nuur waliogopa kunipa juu wala kuniruhusu kusikiliza kipindi hicho cha Mkuu wa Mkoa ingawa kabla sijahama Tanga nilikuwa mmoja wa Wakurugenzu wa radio hiyo.

Lakini niliwahoji watu waliosikia kipindi hicho.

Katika Waislam waliokamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani Handeni ni huyu kijana Rajab Omari Mtana.

Baada ya kukaa rumande alipata dhamana yeye pamoja na wenzake na akawa nje.
Rajab Omar Mtana alirejea kijijini kwake.

Wakati anakaribia kuingia kijijini alisimamishwa na askari wa kijiji akapekuliwa na akanyang'anywa simu yake na fedha taslimu.

Baada ya mkasa huu walimwachia na yeye akaendelea na safari yake.

Lakini wakati akiwa rumande nyumba yake ilikuwa imevurugwa haifai kuishi mtu kwa hiyo alifikia kwa dada yake.

Akiwa nyumbani kwa dada yake alifatwa na watu wa serikali ya kijiji usiku akatolewa ndani na kuanza kupigwa kwa bakora na kisha kwa mapanga.

Kujitetea kijana huyu alikimbia huku akikimbizwa.
Asubuhi kulipokucha palionekana damu nyingi sana.

Taarifa ilitolewa polisi lakini hakuna kilichofanyika.
Polisi walitoa taarifa (SON/RB346/2014).

Dada yake na mumewe walikamatwa na kushitakiwa katika mahakama ya hapo kijijini na wakapigwa faini ya kila mtu shs. 20.000.

Kosa lao ni kumleta kijiji Rajab Omari Mtana mtu asiyetakiwa.

Miaka 10 imetimia Rajab Omar Mtana hajulikani alipo na inasadikiwa ameuawa na wale waliokuja kumtoa nyumbani kwa dada yake.

Rajab Omar Mtana ametafutwa kote hajapatikana na waliompiga na kumjeruhi wako huru nje hawajaguswa wala kuhojiwa na polisi.

Lakini wale waliotumiwa kwa mauaji ya mlinzi wa kijiji wamehukumiwa kifo.

Hapa kuna mengi sana ya kufikirisha mbali ya yale kuwa kulikuwapo na silaha za kutungua ndege katika vijiji hivi vya Waislam wa Handeni vilivyokuwa na nyumba za nyasi na udongo.

View attachment 2668468
Ungesema Wanakijiji 10 au ukipenda ungesema watu 10 kunyongwa.Ulipotia neno waislam 10 huo ni uchochezi na ujinga ulipitiliza.

Mzee unataka kuvuruga amani ya nchi kupitia mgongo wa dini sijui utakimbilia Sudan au Syria !.
 
Ntamfungia kesi MamaSamia2025 kwa kosa la kufananisha mnyama mwenye nyama pendwa ulimwenguni na lizeee lisilo na staha lizee lisilojitambua!

Nguruwe ana thamani kubwa sana
Kwa niaba yangu binafsi ninaomba radhi kwa kumfananisha mnyama mwenye nyama pendwa duniani na huyu mzee mpuuzi wa kuitwa Mohamed Said. Ninakiri kumkosea heshima Nguruwe.
 
Mama...
Siandiki uchochoezi ni wewe tu hujapenda historia hii.

Ningekuwa naandika uchochezi vitabu vyangu visingechapwa na Oxford University Press, Nairobi na New York, nisingetafutwa kwq mahojiano na vyombo vikubwa vya habari kama BBC, VoA, DW, TBC, AZAM, nisingehojiwa na watu kama Hamza Kassongo nk.

Chunguza ni watu gani wananipinga.
Kisha rejea na jiulize vyombo vikubwa vinafatana nini kwangu?
Acha upumbavu.
 
Id yako na ulichokiandika vimenipa picha halisi juu ya kipi hasa unachokitaka.
 
Acha upumbavu.
Mama...
Nitakupa kisa cha Prof. Haroub Othman, Mwalimu Nyerere na kitabu cha Abdul Sykes.

Mimi ndiyo mapenzi ya Mwenyezi Mungu nimezaliwa 1952 wakati vuguvugu za kudai uhuru wa Tanganyika zinaanza.

Baba yangu ananihadithia anasema huo ndiyo mwaka alimuona Nyerere nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuuu.

Baba yangu anasema pembeni Abdul alimfahamisha kuwa kuna mpango wa kuunda chama cha siasa kudai uhuru na Nyerere atakuwa kiongozi wa harakati hizi.

Kipindi hiki Abdul Sykes alikuwa TAA Secretary na Act. President.

Babu yangu Salum Abdallah alikuwa katika siasa za kupigania uhuru na alikuwa pia kati ya wafadhili wa TAA na TANU Tabora na pia akawa muasisi wa TANU na Tanganyika Railways African Union (TRAU).

Nilipokuja kusoma historia ya TANU nikagundua kuwa wale wote ambao nilikuwa nikiwasikia wakitajwa nyumbani kwetu katika historia ya TANU wote wamefutika.

Anatajwa mtu mmoja tu - Julius Kambarage Nyerere.

Siku moja nikamsikia baba yangu anasema, ''Hawa wanaweza vipi kuandika historia ya TANU wasimtaje Abdul?''

Lakini ndiyo ukweli uliokuwapo.

Historia ya TANU ipo lakini Abdul Sykes hayumo wala babu yangu hayumo na wazalendo wengi sana hawamo na wengi wao Waislam.

Hapa ndipo nikajiuliza kwa nini?

Nikaamua kuandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kueleza harakati za kuunda TANU kupitia maisha ya Abdul Sykes na kwa kutumia Nyaraka za Sykes.

Prof. Haroub Othman alipokisoma kitabu changu alipata mshtuko mkubwa sana.
Akaomba miadi na Mwalimu.

Prof. Haroub akamwambia Mwalimu kuwa kitabu changu kimebadilisha historia yake (Nyerere) na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Prof. Haroub akamwambia kubwa ni kuwa hata ''legacy'' yake imeguswa pakubwa ni lazima Mwalimu na yeye aeleze historia ya maisha yake hadi kufika kuwa kiongozi wa TAA 1953 na kiongozi wa TANU 1954.

Ukipendezewa naweza nikaendelea na kisa hiki.

Kwa sasa tusimame hapa.

Kitabu ni hicho hapo chini:

1687950180783.jpeg

The Life and Times od Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)
The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika
(Minerva Press, London 1998)​
 
Umeingiza udini mahali ambapo hapastahili. Kutokana na maelezo yako mwenyewe Rajab alikamatwa kwa mara ya kwanza kwa sababu mtu aliyemuuzia hiliki alikataa kuzilipia ushuru. Ingawa ulikuwa ni uonezi mkubwa hakukamatwa kwa sababu ni muislamu. Umetuambia kuwa ndugu zake walienda kujaribu kumtoa ndio vurugu zikatokea ambapo mtu mmoja aliuawa. Ingawa bila shaka ndugu zake wengi kama sio wote walikuwa waislamu lakini hawakwenda kituoni kumtoa Rajab kwa sababu ni muislamu bali kwa sababu ni ndugu yao. Mkuu wa Mkoa unayemtaja Chiku alikuwa muislamu na sidhani kama alifanya unayomshutumu kwa sababu ya chuki dhidi ya waislamu.

Kugeuziwa kibao na kesi kugeuzwa kuwa ya ugaidi si kwa sababu ya chuki dhidi ya waislamu bali ilikuwa njia ya kuhakikisha kuwa hawachomoki kirahisi. Hata Freeman Mbowe alifunguliwa kesi ya ugaidi na hamna hata mmoja aliwahi kusema kuwa ilikuwa kwa sababu yeye ni mkristu na Rais muislamu.

Kama unayosimulia yana ukweli wowote ni dhahiri kuwa uonevu mkubwa umefanyika dhidi ya Rajab na ndugu zake. Kuingiza udini hakuwatendei haki maana unageuza suala lao kuwa la maonevu dhidi ya waislamu ( yanayofanywa na wakristu na vibaraka wao) wakati ni mfano mwingine wa watu kutumia nafasi zao kuwaonea na kuwafanyia ukatili binadamu wenzao. Badala ya hili suala kuwa letu wote maana watu wa imani zote wamewahi kufanyiwa ukatili (mfano Mdude Nyangali) nyie mnaligeuza kuni ya kuchochea chuki kati ya waislamu na wakristu. Sio vizuri mnavyofanya.

Amandla....

Utakua mgeni wa Muddy Said wewe. Good luck with that.
 
Duuuh inafikirisha hii..

naamini si haki kudhulumu haki ya mtu yeyote awe islam au budha..

kila penye neno muislamu hapo nadhani ungefaa kuweka mtanzania..
katika hukumu hiyo ..
Hata mm ananishabgaza sana kuweka neno waislam, kwa nn si watanzania ?
 
Mleta maada inaonyesha wazi utafita wako uliegamia upande mmoja..

Pia umeathirika na udini,

so conclusion fanya utafiti upande wa pili.
 
Mama...
Nitakupa kisa cha Prof. Haroub Othman, Mwalimu Nyerere na kitabu cha Abdul Sykes.

Mimi ndiyo mapenzi ya Mwenyezi Mungu nimezaliwa 1952 wakati vuguvugu za kudai uhuru wa Tanganyika zinaanza.

Baba yangu ananihadithia anasema huo ndiyo mwaka alimuona Nyerere nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuuu.

Baba yangu anasema pembeni Abdul alimfahamisha kuwa kuna mpango wa kuunda chama cha siasa kudai uhuru na Nyerere atakuwa kiongozi wa harakati hizi.

Kipindi hiki Abdul Sykes alikuwa TAA Secretary na Act. President.

Babu yangu Salum Abdallah alikuwa katika siasa za kupigania uhuru na alikuwa pia kati ya wafadhili wa TAA na TANU Tabora na pia akawa muasisi wa TANU na Tanganyika Railways African Union (TRAU).

Nilipokuja kusoma historia ya TANU nikagundua kuwa wale wote ambao nilikuwa nikiwasikia wakitajwa nyumbani kwetu katika historia ya TANU wote wamefutika.

Anatajwa mtu mmoja tu - Julius Kambarage Nyerere.

Siku moja nikamsikia baba yangu anasema, ''Hawa wanaweza vipi kuandikia historia ya TANU wasimtaje Abdul?''

Lakini ndiyo ukweli uliokuwapo.

Historia ya TANU ipo lakini Abdul Sykes hayumo wala babu yangu hayumo na wazalendo wengi sana hawamo na wengi wao Waislam.

Hapa ndipo nikajiliza kwa nini?

Nikaamua kuandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kueleza harakati za kuunda TANU kupitia maisha ya Abdul Sykes na kwa kutumia Nyaraka za Sykes.

Prof. Haroub Othman alipokisoma kitabu changu alipata mshtuko mkubwa sana.
Akaomba miadi na Mwalimu.

Prof. Haroub akamwambia Mwalimu kuwa kitabu changu kimebadilisha historia yake (Nyerere) na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Prof. Haroub akamwambia kubwa ni kuwa hata ''legacy'' yake imeguswa pakubwa ni lazima Mwalimu na yeye aeleze historia ya maisha yake hadi kufika kuwa kiongozi wa TAA 1953 na kiongozi wa TANU 1954.

Ukipendezewa naweza nikaendelea na kisa hiki.
Kwa sasa tusimame hapa.

Kitabu ni hicho hapo chini:

View attachment 2671719
The Life and Times od Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)
The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika
(Minerva Press, London 1998)​
Kawasimulie wala nguruwe wenzako pale Kigogo Sambusa
 
Umeingiza udini mahali ambapo hapastahili. Kutokana na maelezo yako mwenyewe Rajab alikamatwa kwa mara ya kwanza kwa sababu mtu aliyemuuzia hiliki alikataa kuzilipia ushuru. Ingawa ulikuwa ni uonezi mkubwa hakukamatwa kwa sababu ni muislamu. Umetuambia kuwa ndugu zake walienda kujaribu kumtoa ndio vurugu zikatokea ambapo mtu mmoja aliuawa. Ingawa bila shaka ndugu zake wengi kama sio wote walikuwa waislamu lakini hawakwenda kituoni kumtoa Rajab kwa sababu ni muislamu bali kwa sababu ni ndugu yao. Mkuu wa Mkoa unayemtaja Chiku alikuwa muislamu na sidhani kama alifanya unayomshutumu kwa sababu ya chuki dhidi ya waislamu.

Kugeuziwa kibao na kesi kugeuzwa kuwa ya ugaidi si kwa sababu ya chuki dhidi ya waislamu bali ilikuwa njia ya kuhakikisha kuwa hawachomoki kirahisi. Hata Freeman Mbowe alifunguliwa kesi ya ugaidi na hamna hata mmoja aliwahi kusema kuwa ilikuwa kwa sababu yeye ni mkristu na Rais muislamu.

Kama unayosimulia yana ukweli wowote ni dhahiri kuwa uonevu mkubwa umefanyika dhidi ya Rajab na ndugu zake. Kuingiza udini hakuwatendei haki maana unageuza suala lao kuwa la maonevu dhidi ya waislamu ( yanayofanywa na wakristu na vibaraka wao) wakati ni mfano mwingine wa watu kutumia nafasi zao kuwaonea na kuwafanyia ukatili binadamu wenzao. Badala ya hili suala kuwa letu wote maana watu wa imani zote wamewahi kufanyiwa ukatili (mfano Mdude Nyangali) nyie mnaligeuza kuni ya kuchochea chuki kati ya waislamu na wakristu. Sio vizuri mnavyofanya.

Amandla....
Genius! 🙌🤛
 
Back
Top Bottom