Sio propaganda. Nisawa na kusema wale Jamaa wa mtwara nao wangekamatwa na kufikishwa kizimbani. We ukienda kule ni mapambano hakuna cha msaliamtume.
Kuku....
Mwezi Desemba 2013 vyombo vya habari vilisheheni taarifa ya magaidi waliokuwa katika vijiji vya Handeni.
Taarifa zilifika Tanga kuwa kulikuwa na magaidi wanaishi katika mahandaki na operesheni maalum ilikuwa ikifanyika kuwateketeza.
Ukisikilza taarifa kama hizi ikiwa umejaaliwa akili ya kuweza kufikiri utajiuliza mengi.
Hawa watu wametoka wapi?
Kwa nini wanapigana na serikali?
Wameanza lini kujikusanya kama jeshi?
Nani kiongozi wao?
Propaganda ikaenezwa kuwa walikuwa hawaitambui serikali ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Habari zilivuja Tanga mjini na vitongoji vyake kuwa kuna vijiji vimeteketezwa.
Kwa hakika kuna watu waliletwa Hospitali ya Bombo wakiwa na majeraha ya risasi.
Kwa watu waliofika Hospitali ya Bombo waliwaona vijana waliokuwa wamefungwa pingu wakiwa katika vitanda vyao huku wakilindwa na askari.
Taarifa zikafika vilevile kuwa kuna watoto wadogo wamefikishwa Tanga baada ya kukutwa porini.
Watoto hawa walikuwa wamehifadhiwa katika moja ya shule za hapo mjini.
Katika hali kama hiyo vilevile zikafika taarifa tofauti kwa Waislam wa Tanga kuwa hao walioletwa Hosptali ya Bombo na watoto waliookotwa porini ni Waislam wa vijiji vya Madina, Dibungo na Lwande walioshambuliwa na askari pasi na sababu.
Hapa sasa pakaanza kuulizwa maswali?
Walioshambiuliwa ni wana vijiji Waislam si magaidi waliokuwa na silaha na katika vita dhidi ya serikali?
Juhudi za Umoja wa Taasisi za Kiislam Tanga (SHITA) chini ya Mayor Omari Guledi na Katibu wake Ahmed Mustafa kukutana na Mkuu wa Mkoa Chiku Galawa kupata ukweli zikagonga mwamba.
Hali ikawa tete baada ya Sheikh Rajab Ramadhani Chambuso mmoja katika masheikh vijana mjini Tanga kukamatwa na kuwekwa rumande kisha kuhamishwa Handeni ambako alifunguliwa kesi ya kubambika ya ''kushawishi mauaji.''
Sheikh Rajab Chambuso ni kijana maarufu mjini Tanga na ni mwalimu wa dini shule za sekondari za Tanga na anasomesha watoto wadogo Quran.
Ikavuma kuwa patakuwa na maandamano baada ya sala ya Ijumaa kushinikiza kuachiwa kwa Sheikh Chambuso.
Askari wa FFU walizingira misikiti kadhaa Ijumaa hiyo lakini hapakuwa na maadamano yoyote.
Sheikh Chambuso akaachiwa kwa dhamana.
Alipopata dhamana na kuachiwa Sheikh Chambuso alikuja Tanga na habari za kutisha kuhusu dhulma iliyopita katika vijiji vya Madina, Dibungo na Lwande.
Habari hizi alielezwa na mahabusi wenzake katika hivyo vijiji vilivyoshambuliwa.
Sheikh Chambuso katika hotuba aliyotoa katika moja ya misikiti maarufu Tanga aliwafahamisha Waislam kuhusu misikiti iliyovujwa na kuchomwa moto, Qur'an zillizochomwa moto na nyumba za Waislam zilizoteketezwa kwa kisingizo cha ugaidi.
Binafsi nikajiambia ninaloweza mimi kufanya ni kuhakikisha kuwa haya yote yanahifadhiwa katika maandishi, sauti na picha.
Lakini kubwa niliamua lazima nifike Tanga na Handeni na lazima nizungumze na wale walioshuhudia haya na waathirika wenyewe.
Ndugu yangu Kuku...,
Haya si mambo kama unavyodhania.
Niambie katika hayo uliyosoma hapo juu unapata picha kuwa kulikuwa na magaidi katika mahandaki na silaha za kutungua ndege?
Propaganda hizi nini ilikuwa makusudio yake na nani alikuwa yuko nyuma ya haya yote?
Toka mapema asubuhi nilikuwa kila nikisoma michango yenu nakuombeni mfanye subra kuna mengi.
Bado mkasa huu unaendelea nakuombeni muwe na subra.
Sheikh Rajab Ramadhani Chambuso akigawa Mashafu kwa wanafunzi wa Shule ya St. Christine Tanga alipokuwa akisomesha Uislam kwa kujitolea