Tetesi: Sakata la Makonda, Clouds na Nape kutua Bungeni na kupotelea huko

Tetesi: Sakata la Makonda, Clouds na Nape kutua Bungeni na kupotelea huko

Raisi keshatoa tamko hilibswala hakuna haja ya kuhangaika nalo tena coz ameshaonyesha hatoangaika nalo so its better to keep our mouth shut
 
"Inasemekana, 1 bil uwenda ilitumika kuwa ziba mdomo baadhi ya wadhibiti madawa ya kulevya sehemu za bandari, wanafanya kazi wapi hao na waliowaziba midomo wanaojishughulisha na nini !?" taarifa kama hizi zingekuwa zimejaa mitandao, magazeti na TV, tungemrahisishia kazi Kamishna Siang'a na timu yake. Na hapa tungekuwa tunapiga hatua kubwa kuokoa kizazi chetu cha sasa na vinavyokuja.

Watanzania ebu tuungane kutokomeza biashara mbaya kabisa na haramu ya madawa ya kulevya.
 
unaposema hakuna aliyejitokeza kwenda mahakamani hadi sasa ninakuelewa. kwa sababu mkuu ameamua kukaa kimya wakati kuna mambo mengine yaliyokua wazi hakukaa kimya basi inatakiwa watu wakapigie kelele mahakamani. lakini ninaweza kubet daudi anaweza kukataa kwenda mahakamani. hili limeshajithibitisha kwa matukio mawili au matatu yanayoonyesha yeye hayuko tayari wala rafiki yake hayuko tayari huyo mtu kuhojiwa. aliitwa na bunge akakataa (taarifa zinasema aliamrishwa na mkuu kutokwenda), alitafutwa na tume ya nape kuhojiwa akakataa (kwa kuingia mitini), mahakama ilimuita kwa kesi ya mbowe akakataa kwenda na hakuna kilichofanyika. wewe hapo unaonaje? kwa sababu raisi ana mamlaka makubwa kikatiba anaamua mambo kwa kiburi hicho na mambo yanakwisha. anamwambia hakuna kwenda nae haendi waliomuita wanaogopa na kupotezea. kuna mifano mingi ambapo raisi alichukua hatua hata bila kusubiri mtuhumiwa ashikwe na hatia na mahakama. mfano suala la Kabwe yeye alishtakiwa na Daudi bashite kwa rais wakiwa mkutanoni alichofanya raisi aliuliza wananchi ''nitubue nisitumbue?' wananchi wakasema ''tumbua''. raisi akamtumbua Kabwe hapohapo bila kuchelewa. hizi tuhuma dhidi ya Daudi Bashite mbona zimevuka mipaka na raisi asituulize kama atumbue au asitumbue?
Kitwanga picha za video/taarifa za kwenye tv zilionyesha akiwa anajibu maswali akiwa amelewa na he was right away sacked based on that very evidence. huyu Daudi cctv footages zinaonyesha akivamia kituo cha tv akiwa na armed mixed forces hilo ni kosa au sio kosa? raisi hajaziona? mbona hakumtumbua? hivi huyu raisi akimwambia Daudi hakuna kwenda mahakani kama ambavyo imeshatokea kwa mambo mengine tutafanyaje? kwanini tusiamini kuwa hata kuhojiwa na kamati ya nape ni rasi ndiye alimkataza? raisi ana power kubwa ila anachofanya ni kuzijaribu powers zake kuona zinatoaje matokeo na akiyaona matokeo ndio kwanza anazidisha kiburi. alizuia kuitikia wito wa bunge ikawa. alizuia kwenda mahakani ikawa sawa. kiburi kikazidi akazuia kuohojiwa na na kamati ya nape na huyo aliyeitisha mahojiano hayo akafukuziliwa mbali. kwa staili hiyohiyo ipo siku ataamuru kitu ambacho watu hawataamini kabisa.
hiyo ya mahakani unayoisema ndugu uko sahihi lakini na akijitokeza wa kumshitaki daudi mahakamni utaona kituko cha mwaka. hatakwenda mahakani na mahakama ndio itakaa kimya.
Umeandika mambo mengi na nakuelewa, machoni mwa watu ni pure double standard. Wanasiasa wanaagalia maslahi ya kisiasa kabla ya kuamuwa jambo, kama vile uwongozi Chadema walipinga mahesabu kwa Lowassa na vile walivyo mpamba kuwa yeye ni fisadi mkubwa lakini wakajuwa Lowassa atawavusha kwenye uchaguzi kitu ambacho kina maslahi zaidi ya ufisadi wake. Na kwa Makonda ni hivyo hivyo, makonda ni mtu muhimu kwenye kuhamisha mawazo ya watu. Badala ya kufikiria makubwa, watu wako busy na maisha binafsi ya makonda. Ulisema wengine walitumbuliwa papo hapo, lakini kwa Makonda ni kigugumizi. Kwanza lazima uelewe kwamba Dr. Dau kutumbuliwa hadharani yale yalikuwa maigizo ya kisiasa, mtu (tena mweye vyeo vikubwa) kabla hajatumbuliwa anajadiliwa kwa kina na jalada lake linachabuliwa na kujiridhisha kama kweli inabidi aende. Kikwete hakuawa makini, alitumbuwa watu halafu hao watu wanakuja kushitaki mahakani wanashinda kesi na kurudi kazini. Lakini sio kwa JPM, walio tumbuliwa wote wanajuwa wanamakosa na hakuna aliyeshitaki mpaka muda huu. Mimi kwangu siamini kama mtu anauwezo wa kupuuza wito wa mahakama, labda kuna ufundi wa kitaalamu utakuwa umetumika kabla ya mtu kutoonekana mahakani. Utakimbia bunge, utakimbia kamati za uchunguzi, lakini sio mahakama. Kesi ya Mbowe, aliyeshitakiwa ni mkuu wa mkoa sio P. Makonda. Na ofisi ya mwanaseria mkuu inaweza kujibu hizo tuuma za mfanyakazi wa serikali. Kuna watu wanataka kutumia njia rahisi ya kumuhukumu Makonda kwa kutumbuliwa, na ndio hilo ambalo JPM hataki kuwapa mkate wapinzani wake wa kisiasa. Na mimi nikasema, mkipiga kelele ili JPM afanye mnachotaka haita wezekana ila mwenye ushahidi aupeleke mahakani ili ukweli ujulikane. Lakini mpaka sasa hakuna mwenye uwezo huo kutokana na ushahidi sio mzito kisheria.
 
Ndugu wanabodi, pamoja na madhaifu makubwa ya katiba yetu, bado katiba hii ya mwaka 1977 haijanyima haki kwa Wananchi wake. Bunge lina mamlaka kamili lakini aliwezi kutekeleza majukumu yake kikamilifu kutokana na sababu nilizozieleza hapo juu. Mahakama kama chombo chakutoa haki, bado kina fursa ya kutafsiri sheria, kukutanisha pande zote mbili ama kuchukua hatua (kutoa hukumu ama kuachia huru)

Nakubaliana na mawazo yako kuwa kazi ya bunge sio kutoa adhabu kwa wananchi, hivyo bunge limechukua madaraka yasiyo yake ya kutaka kumwita Makonda huko Dodoma. Bunge wanamuita Makonda huko Dododma kama mkuu wa mkoa, mkuu wa mkoa yuko chini ya waziri wa Tamisemi na waziri mkuu hivyo basi bunge lingeweza kupata maelezo ya kina kutoka kwa waziri wa Tamisemi au waziri mkuu kuhusu yale wanayodhani yalisemwa kuwadhihaki!!

Zitto kuandika kuwa Magufuli amemkataza Makonda kwenda bungeni ni uchochezi wa kutaka kuligombanisha bunge na Rais!! Kama mbunge, Zitto alitakiwa kuelewa kuwa lolote linalowahusu watendaji waliochini ya serikali linaweza kujibiwa bungeni na waziri mkuu ambae ndio kiongozi wa shuhuri za serikali huko!!
 
Umeandika mambo mengi na nakuelewa, machoni mwa watu ni pure double standard. Wanasiasa wanaagalia maslahi ya kisiasa kabla ya kuamuwa jambo, kama vile uwongozi Chadema walipinga mahesabu kwa Lowassa na vile walivyo mpamba kuwa yeye ni fisadi mkubwa lakini wakajuwa Lowassa atawavusha kwenye uchaguzi kitu ambacho kina maslahi zaidi ya ufisadi wake. Na kwa Makonda ni hivyo hivyo, makonda ni mtu muhimu kwenye kuhamisha mawazo ya watu. Badala ya kufikiria makubwa, watu wako busy na maisha binafsi ya makonda. Ulisema wengine walitumbuliwa papo hapo, lakini kwa Makonda ni kigugumizi. Kwanza lazima uelewe kwamba Dr. Dau kutumbuliwa hadharani yale yalikuwa maigizo ya kisiasa, mtu (tena mweye vyeo vikubwa) kabla hajatumbuliwa anajadiliwa kwa kina na jalada lake linachabuliwa na kujiridhisha kama kweli inabidi aende. Kikwete hakuawa makini, alitumbuwa watu halafu hao watu wanakuja kushitaki mahakani wanashinda kesi na kurudi kazini. Lakini sio kwa JPM, walio tumbuliwa wote wanajuwa wanamakosa na hakuna aliyeshitaki mpaka muda huu. Mimi kwangu siamini kama mtu anauwezo wa kupuuza wito wa mahakama, labda kuna ufundi wa kitaalamu utakuwa umetumika kabla ya mtu kutoonekana mahakani. Utakimbia bunge, utakimbia kamati za uchunguzi, lakini sio mahakama. Kesi ya Mbowe, aliyeshitakiwa ni mkuu wa mkoa sio P. Makonda. Na ofisi ya mwanaseria mkuu inaweza kujibu hizo tuuma za mfanyakazi wa serikali. Kuna watu wanataka kutumia njia rahisi ya kumuhukumu Makonda kwa kutumbuliwa, na ndio hilo ambalo JPM hataku kuwapa mkate wapinzani wake wa kisiasa. Na mimi nikasema, mkipiga kelele ili JPM afanye mnachotaka haita wezekana ila mweye ushahidi aupeleke mahakani ili ukweli ujulikane. Lakini mpaka sasa hakuna mwenye uwezo huo kutokana na ushahidi sio mzito kisheria.
ushahidi sio mzito kisheria? hebu fafanua. mimi nadhani unaona ushahidi sio mzito kwa sababu hakuna aliyejitokeza kwenda kushitaki na ushahidi huo ukatolewa. lakini ikiwa ushahidi uliopo utatolewa mahakamani ushahidi huo ni mzito kisheria. sijui ni ushahidi wa aina gani nyingine utakua mzito kisheria
 
Clouds wanajua kila ktu sio had uwambie wale clouds wana juana vzr na rafk yao hvo ndugu wakigombana chukua jembe ukalime na wakipatana kuchukua kapu ukavune acha kushakunaku utadhilika...kuhusu nape una ushahidi gan yulr askari kanzu? au ubaropokwa husoyajua? kabla hujandka uzi humu hakikisha na unacho kiandka...askari kanzu yule kwa ushahidi em nipe ushahidi kama yule ni askari kanzu na ni wakituo gani? ww kwa akil yako askari kanzu yupi anayeweza kumfata nape? macho yako yameshindwa hata kugundua kwa muonekane wake na kusoma mengi kutpia yule mtu kujua anatoka kitengo gan?pole sana....kuhusu makonda ndugu zako wangefungua kesi muda sana...jiulze kwann meya jacob kapeleka kuhusu kuvamia clouds na sio vyeti? hakuna mwenye ushahidi timilifu juu ya vyeti na kama wanavo mbona hawend mahakamn? ndugu zko wana akil sio wajinga ndomana wanaishia kuropokwa kwenye media...hv ushamckia mbowe mara ngap akisema kuhusu cheti cha makonda??? mbowe ana akil zake timamu....fungua maskio usikie..funguka akili huelewe...fungua macho yako uone na sio utazame.....hii ndo Tanzania....ni mfano wa ukuta ulopakwa rangi ya purple wewe unaona ukuta wa rang ya purple wenzio wanaojua wanaona zaidi nyuma ya ukuta na kati kati ya ukuta mpaka kilichochangwanywa ndani ya ukuta kufkia kuwa ukuta.....ni rahisi kuchora number 13 lakini sio rahisi huishke kwa mkono.....
 
ushahidi sio mzito kisheria? hebu fafanua. mimi nadhani unaona ushahidi sio mzito kwa sababu hakuna aliyejitokeza kwenda kushitaki na ushahidi huo ukatolewa. lakini ikiwa ushahidi uliopo utatolewa mahakamani ushahidi huo ni mzito kisheria. sijui ni ushahidi wa aina gani nyingine utakua mzito kisheria
Jana nilijadiliana na baadhi ya watu hapa JF, kuhusu hili swala la kwanini Mwakyembe amesema ushahidi ulio mezani hauna nguvu kumchulia makonda hatuwa. Kwa ushahidi wa video ukimpeleka Makonda mahakamani, kama ana wakili mzuri anashinda hiyo kesi kirahisi. Kwasababu video haiko vizuri na imechukuliwa kwenye mwanga mdogo, Makonda anaweza kusema yeye sio huyo mtu kwenye video, inabidi kuwe na mashahidi wa kutosha kuthibitisha kuwa ni yeye. Na yeye Makonda anaweza kuja na lundo la mashahidi kusema yeye alikuwa nyumbani na mkewe na marafiki zake wakati hiyo video inachuliwa. (Hii ni mifano tuu)
Unahitajika ushahidi wenye nguvu zaidi kuliko uliopo hivi sasa.
 
Mahakama patapufunga mjadala, huko zitapigwa kalenda kama kawaida mwisho maelelekezo yatatolewa. Huko si sehem sahihi bora bunge
 
I love people like you with good thinking capacity and objective. Kelele kuhusu mtu mmoja zinaboa sasa. Mahakama ipo kama kweli ni mkosaji waende huko vinginevyo ni kelele za debe tupu.[/quote]
 
Jana nilijadiliana na baadhi ya watu hapa JF, kuhusu hili swala la kwanini Mwakyembe amesema ushahidi ulio mezani hauna nguvu kumchulia makonda hatuwa. Kwa ushahidi wa video ukimpeleka Makonda mahakamani, kama ana wakili mzuri anashinda hiyo kesi kirahisi. Kwasababu video haiko vizuri na imechukuliwa kwenye mwanga mdogo, Makonda anaweza kusema yeye sio huyo mtu kwenye video, inabidi kuwe na mashahidi wa kutosha kuthibitisha kuwa ni yeye. Na yeye Makonda anaweza kuja na lundo la mashahidi kusema yeye alikuwa nyumbani na mkewe na marafiki zake wakati hiyo video inachuliwa. (Hii ni mifano tuu)
Unahitajika ushahidi wenye nguvu zaidi kuliko uliopo hivi sasa.
kumbe tulikua mbalimbali. mimi nimekua niongelea ushahidi wa kashfa yake ya vyeti. ndio huo hasa nilikokua nikiuliza sio mzito kivipi.
lakini hata wa uvamizi wa kituo nao mbona ni ushahidi ulio wazi sana. kama ni hivo usemavyo basi nadhani wangekua wanafungwa watu waliokutwa readyhanded tu na si vinginevyo. huyu mtu alipovamia kulikua na watu pale. kama getini kuna cctv cameras basi hata gari lake lingeweza kuonekana kama sehemu ya ushahidi. camera za ndani studio pia zimuonyeshe yeye. watangazaji wote waliokuwepo wamuone yeye bado yeye anaweza kukataa na kudai alikua nyumbani na yeye akawa na mashahidi wake wa uongo na akashinda kesi. hii inanishawishi nione kwamba itakua vigumu kumfunga yeyote. ukumbuke hata magaidi wanaoshikwa baada ya kutekeleza matukio kwenye nchi za wenzetu ni hizohizo cctv camera ndio huwa zinawakamatisha na kuwa ushahidi mkubwa zikisaidiwa na forensic evidences nyingine kama finger prints nk. haya yote si angejitokeza hata kwenye kamati ya mahojiano akakana kwamba hakua yeye na kwamba yeye alikua nyumbani. hapo na maaskali aliokua nao na wote wakane picha zao. hapo hatujaona footages za ndani ya studio.
 
kumbe tulikua mbalimbali. mimi nimekua niongelea ushahidi wa kashfa yake ya vyeti. ndio huo hasa nilikokua nikiuliza sio mzito kivipi.
lakini hata wa uvamizi wa kituo nao mbona ni ushahidi ulio wazi sana. kama ni hivo usemavyo basi nadhani wangekua wanafungwa watu waliokutwa readyhanded tu na si vinginevyo. huyu mtu alipovamia kulikua na watu pale. kama getini kuna cctv cameras basi hata gari lake lingeweza kuonekana kama sehemu ya ushahidi. camera za ndani studio pia zimuonyeshe yeye. watangazaji wote waliokuwepo wamuone yeye bado yeye anaweza kukataa na kudai alikua nyumbani na yeye akawa na mashahidi wake wa uongo na akashinda kesi. hii inanishawishi nione kwamba itakua vigumu kumfunga yeyote. ukumbuke hata magaidi wanaoshikwa baada ya kutekeleza matukio kwenye nchi za wenzetu ni hizohizo cctv camera ndio huwa zinawakamatisha na kuwa ushahidi mkubwa zikisaidiwa na forensic evidences nyingine kama finger prints nk. haya yote si angejitokeza hata kwenye kamati ya mahojiano akakana kwamba hakua yeye na kwamba yeye alikua nyumbani. hapo na maaskali aliokua nao na wote wakane picha zao. hapo hatujaona footages za ndani ya studio.
Sikujuwa ulikuwa unaongelea vyeti, lakini sio vibaya maana huyo kijana ndio anashikilia maongezi mengi hapa mjini kwa hivi sasa. Ni kweli mtu anaweza kucheza na sheria ili ajikwamuwe katika matatizo yake. Unakumbuka Kenyatta na kesi yake ya ICC, mahakamani na mashahidi walikuwa na uhakika kama alihusika na machafuko, lakini aliweza kutoka kwenye makucha ya sheria baada mashahidi wote kupotea na wengine wanasema hawakumbuki kilicho tokea. Sheria ipo pale ili ijaribiwe. Na watu wataijaribu tuu kama Mh.Mbowe alivyoenda mahakamani kuzuia kuhojiwa na polisi.

Tukirudi kwenye vyeti, hata huko, ushahidi wa Gwajima kuuongea kwenye majumba ya ibada hausaidi kitu. Maana majumba ya ibada sio mahakama wala sio mwajiri wa Makonda. Kama kungekuwa na mwalimu aliyejitokeza akasema yeye yuko tayari kula kiapo na kusema alimfundisha mtu anaitwa Daudi Bashite, hapo tungesema tukienda mahakani kesi ingekuwa na nguvu au hata Rais angekuwa na chakumtumbulia. Hakuna hata kijana aliyesimama na kusema mimi nilisoma na mtu anaitwa Bashite. Kuna uvumi ambao serikali itaufatilia, na mwingine itaupuzia. Kama uvumi hauna madhara kwenye maisha ya watu basi serikali itaupitia na kuona kama kuna haja ya kuchukuwa hatua au la.
 
Bunge likiongozwa na Ndugai sawa lakini nahisi huenda tayari alishaandaliwa safari ya kwenda kucheki afya huyo mwanamke atalizima kama Lugumi
 
Sikujuwa ulikuwa unaongelea vyeti, lakini sio vibaya maana huyo kijana ndio anashikilia maongezi mengi hapa mjini kwa hivi sasa. Ni kweli mtu anaweza kucheza na sheria ili ajikwamuwe katika matatizo yake. Unakumbuka Kenyatta na kesi yake ya ICC, mahakamani na mashahidi walikuwa na uhakika kama alihusika na machafuko, lakini aliweza kutoka kwenye makucha ya sheria baada mashahidi wote kupotea na wengine wanasema hawakumbuki kilicho tokea. Sheria ipo pale ili ijaribiwe. Na watu wataijaribu tuu kama Mh.Mbowe alivyoenda mahakamani kuzuia kuhojiwa na polisi.

Tukirudi kwenye vyeti, hata huko, ushahidi wa Gwajima kuuongea kwenye majumba ya ibada hausaidi kitu. Maana majumba ya ibada sio mahakama wala sio mwajiri wa Makonda. Kama kungekuwa na mwalimu aliyejitokeza akasema yeye yuko tayari kula kiapo na kusema alimfundisha mtu anaitwa Daudi Bashite, hapo tungesema tukienda mahakani kesi ingekuwa na nguvu au hata Rais angekuwa na chakumtumbulia. Hakuna hata kijana aliyesimama na kusema mimi nilisoma na mtu anaitwa Bashite. Kuna uvumi ambao serikali itaufatilia, na mwingine itaupuzia. Kama uvumi hauna madhara kwenye maisha ya watu basi serikali itaupitia na kuona kama kuna haja ya kuchukuwa hatua au la.
haohao mashahidi unaowasema (walimu kuanzia shule ya msingi kolomije, nyanza, pamba sec, nyegezi fisheries, classmates, ndugu) wote wapo. ndio hapo sasa nikasema kama kesi itafika mahakamani ushahidi uliopo usipokua mzito basi sijui ni ushahidi wa aina gani utakua mzito.
 
haohao mashahidi unaowasema (walimu kuanzia shule ya msingi kolomije, nyanza, pamba sec, nyegezi fisheries, classmates, ndugu) wote wapo. ndio hapo sasa nikasema kama kesi itafika mahakamani ushahidi uliopo usipokua mzito basi sijui ni ushahidi wa aina gani utakua mzito.

Sasa kwanini hao uliowataja hawatoki hadharani kuthibitisha, kwanini wasije kula kiapo cha uthibitisho kama wanaushahidi. Matokeo yake Gwajima ana taja majina na kusema fulani yupo, fulani nina mfahamu na yupo. Lakini hadharani hawaonekani, vipi??
 
Sasa kwanini hao uliowataja hawatoki hadharani kuthibitisha, kwanini wasije kula kiapo cha uthibitisho kama wanaushahidi. Matokeo yake Gwajima ana taja majina na kusema fulani yupo, fulani nina mfahamu na yupo. Lakini hadharani hawaonekani, vipi??
hapo ndio sasa tunarudi kulekule kwenye hoja yako kwamba ''hakuna kesi mahakamani''. sasa hao watu watatokeaje tu na kutoa ushahidi bila kutakiwa kufanya hivyo? kuwapo wapo ila inatakiwa kesi kwanza ili mashahidi waitishwe. tena wapo wengi sana. mfano hata gwajima tu anao wengi tu. classmates, walimu nk
 
hapo ndio sasa tunarudi kulekule kwenye hoja yako kwamba ''hakuna kesi mahakamani''. sasa hao watu watatokeaje tu na kutoa ushahidi bila kutakiwa kufanya hivyo? kuwapo wapo ila inatakiwa kesi kwanza ili mashahidi waitishwe. tena wapo wengi sana. mfano hata gwajima tu anao wengi tu. classmates, walimu nk
Hata huyo Gwajima mwenyewe, mbona amebaki kuhuburi makanisani mambo ya Bashite na hayapeleki mbele ya Sheria ili wote tujuwe? Mimi najuwa Gwajima anajipatia umaarufu kwenye hili jambo, mwenzetu yupo kwenye mavuno ya waumini kuliko kupata haki na ukweli.
 
Hata huyo Gwajima mwenyewe, mbona amebaki kuhuburi makanisani mambo ya Bashite na hayapeleki mbele ya Sheria ili wote tujuwe? Mimi najuwa Gwajima anajipatia umaarufu kwenye hili jambo, mwenzetu yupo kwenye mavuno ya waumini kuliko kupata haki na ukweli.
ana ushahidi mwingi sana. ukumbuke kabla ya kukusanyas taarifa zake alikwenda sehemu zote hizo physically. ana mashahidi ambao makonda mwenyewe hawezi kuwakana kwamba hawajui. wapo walezi wake, walimu, classmates nk.
ukiachilia mbali gwajima, hata mange kimambi aliwahi kutoa kafsha hizo kabla ya gwajima na alimtaja na hata kuweka picha ya mwenye cheti original. baadae gwajima alikuja na vitu hivyohivyo. ushahidi wa kuhusu vyeti hata yeye muhusika anajua hawezi kuupinga hata kidogo ni uko wazi sana sababu hakusoma shule ya peke yake kama mwanafunzi. ana classmates, ana walimu, ana majirani aliokua akicheza nao, ana walezi ana ndugu kuna picha zake nk. ndio maana kashfa ilipotoka aliishia kuwa mpole na kubakia kuhaha makanisani na misikitini na kulialia kama mtoto. katika hilo kaka tutaishia kubishana na kupoteza muda wetu bure tu. wewe wasema hivo. lakini yeye hasemi kwamba mwenye ushahidi kwamba cheti sio changu aende mahakamani. kaishia kubadilisha waganga kuwafunga watu midomo. sishangai hata yanayofanywa na raisi juu yake. maana si mambo y kawaida.
 
Pili kuhusu kushurutishwa au kutishiwa ni vitu ambavyo havina uhakika kwani mtu akatazwi kusema wangeweza kusema hata walifanyiwa vitendo vya kikatili nani angekataa so wanaweza kusema chochote hili kuweka mazingira ya hoja yao kuonekana nzito au kutafuta huruma ya watu kuwa wameonewa pia inasemekana walipewa fedha je ni sawa kwa wao kupewa fedha kama ile ni kazi yao na wamechukua hela za watu wangapi kuwachafua watu?
Nafadhaika na kufadhaika kuwa upande mmoja unakubali hoja na upnde wa pili unatia mashaka kwa watu hao hao.
1. Umesema "wanaweza kusema chochote hili kuweka mazingira ya hoja yao kuonekana nzito au kutafuta huruma"
2. Unasema " walipewa fedha je ni sawa kwa wao kupewa fedha kama ile ni kazi yao na wamechukua hela za watu wangapi kuwachafua watu?

Sasa unawezaji kuhoji (1) na kukubali ya (2) kama sio double standard. Umelalia upande sio mwega utatenguka.

"awkward Hours" ni kuanzia saa
"awkward Hours" ni saa zaidi ya ule muda uliowekwa na ofisi ya kuwahudumia wateja, yaani " office hours" na sio " operational hours"
 
Ule niuvamizi kwa utaratibu kama ingelikuwa ni operesheni ya kikazi kuna watu wanatakiwa wawe na taarifa RSO RPC kanda RCO kama hao walikuwa na taarifa haina tabu vinginevyo ni uvamizi kwa kutumia askari inapasa kituo kilichotoa silaha kwa ajili ya shughuli hiyo wanapaswa kuwajibika
 
Back
Top Bottom